Tuesday, April 10

TUWAKUMBUKE NAKUWASHUKURU MASHUJAA WETU WANGALI HAI - GRACA MACHEL



“Embu jiulize ni namna gani shujaa wa taifa angejisikia pale ambapo amekaa mbele ya watu wa rika tofauti jinsia tofauti wenye mirengo tofauti ya kisiasa wote wakimsifia na kumshukuru kwa werevu wake wakulipigania taifa?”

Maneno ya Mama Graca Machel mwanaharakati wa masuala ya wanawake na watoto wa Afrika akiongea mbele ya umati wa watu kutoka maeneo mbalimbali duniani waliofika kutoa salamu za mwisho wakati wa kuaga mwili wa Marehemu Winnie Mandela aliyefariki tarehe 2 Aprili 2018 nchini afrika kusini.

Winnie Madikizela-Mandela (81) alikuwa mwanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi nchini humo hali iliyopelekea kufungwa mara kadhaa mbali na kuendelea kupokea vitisho lakini aliendea kuwa mwanaharakati mpaka mauti yaliyomfika. 

Winnie Mandela ambaye kwa wengi anafahamika kama mama wa taifa la Afika Kusini pia alikuwa mke wa Nelson Mandela  kwa miaka 38 toka mwaka 1958 mpaka walipoachana mwaka 1996 na kufanikiwa kupata watoto wawili.

Akiongea katika Msiba huo mama Graca Machel ambaye amekuwa akimuita Marehemu Winnie Mandela “dada mkubwa” amesema ni wakati sasa wa kuwaita mashujaa wa taifa na kuwashukuru wangali wakiwa hai kwakuwa hakuna ajuae kama wanasikia na kuona vile wanavyosifiwa wakati wa Misiba yao.

Pia amekemea tabia ya jamii kuwananga na kuwasema watoto wa wapigania uhuru kwakuwa wengi wao wamekosa miongozi na malezi bora ya wazazi kwakuwa wazazi wao walikuwa na ujasiri wa kuacha familia zao na kupigania taifa hivyo si sawa kuwasema na kuwanyooshea vidole badala yake waoneshe upendo zaidi kwao katika kile kilichofanywa na wazazi wao.

Kuhusu rambirambi na ahadi zinazotolewa misibani Mama Graca amewataka wananchi na wanasiasa kuacha maneno ya hadaa kwakuwa mengi yanayoahidiwa hayatekelezwi.

Akitolea mfano wa ahadi zilizotolewa wakati wa wa msiba wa Nelson Mandela miaka mitano iliyopita amesema “ kwasasa ukiangalia Afrika kusini mambo yamekuwa mabaya zaidi ya kipindi Mandela yuhai na hii inaonesha kiasi gani watu hawaishi ahadi zao walizoahidi na ndio jambo hata leo watu wengi wameahidi kuendeleza harakati za Winnie Mandela lakini nani anajua kama zitatekelezwa?”

Badala yake amewataka wanajamii kwa ujumla kuamka na kusaidia kuinua jamii kwakuwa zaidi ya asilimia 50 ya wananchi ni masikini na hakuna juhudi za mmoja mmoja zakulikomboa taifa katika tatizo hilo badala yake kila mtu anaitupia lawama serikali.

Katika hotuba hiyo Graca Machel kwa zaidi ya robo saa aliahidi kutomzungumzia  Winnie Mandela kwakuwa kila mtu amekuwa akifanya hivyo na badala yake kuitaka jamii kubadilika.

Mama Graca Machel ambaye alikuwa mke wa Nelson Mandela tangu mwaka 1998 mpaka mauti yalipomkuta mwaka 2013 alikuwa rafiki wa karibu wa marehemu Winnie Mandela na wamekuwa wakishirikiana katika masuala mbalimbali ya kutetea haki za raia nchini Afrika kusini na afrika kwa ujumla. 

Wanaume waibuka kwa Makonda


Dar es Salaam. Wanaume zaidi ya kumi wameibuka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kulalamika kupokwa watoto, huku mamia ya wanawake wanaodai kutelekezewa watoto wakiendelea kumiminika kwenye ofisi za mkuu huyo wa mkoa.
Wanaume hao ambao wamefika leo Jumanne Machi 10, 2018 wamesema hawashindwi kulea watoto isipokuwa wake zao wamewapoka kwa madai ya umasikini.
Wamesema kama Makonda ameamua kuwasaidia wanawake basi ajue wapo wanaume wanaolia kunyanyaswa na wake zao.
"Mke wangu alinikimbia nilipougua miguu kiasi cha kushindwa kutembea, aliondoka na watoto wangu wote watatu, nimekuwa mtu wa mawazo kiasi cha kupata vidonda vya tumbo naomba awarudishe," amesema Tito Chemba, mkazi wa Kijichi jijini Dar es Salaam.
Tito (35), amesema ujio wake kwa Makonda ni kutaka kurejeshewa wanawe wanaoishi Bukoba kwa ndugu wa mkewe.
Mwanamume mwingine, Edmond Mbisho amesema mkewe aliondoka na mtoto wake tangu akiwa na miaka mitatu na sasa ana miaka sita.
“Ninachoomba ni kupata mwanangu si kingine, kwa sasa mwanamke anaishi na mtu mwingine," amesema.
Mwanamume mwingine, Vedasto Mdesa mkazi wa Iringa amesema watoto wake watatu waliozaliwa kwa pamoja walichukuliwa na ndugu wa mkewe na kupelekwa Urusi.
"Nilipokwa watoto kisa mimi ni masikini, hivi sasa naishi kwa tabu na sababu kubwa ni umasikini na wanasema sijasoma. Huyo mwanamke ana shahada na mimi ni mpiga picha nisiye na elimu," amesema.

Sakata la kufungiwa nyimbo laibuka bungeni

Dodoma. Sakata la kufungiwa nyimbo za wasanii limeibuka bungeni na kusababisha kelele za wabunge pande zote.
Hata hivyo Serikali imeendeleza msimamo wake kuwa itaendelea kuzifungia nyimbo hizo ili  kulinda maadili ya nchi huku Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe akiwatuhumu wabunge kushabikia mambo ilihali wabunge wa mataifa mengine hawafanyi hivyo.
Mbunge wa Viti Maalumu Catherine Magige aliibua sakata hilo wakati akiuliza swali la nyongeza ambapo ametaka kujua ni kwa nini Serikali imekuwa ikiwafungia wasanii na kama kamati ya maudhui imeshindwa kazi yake kwanini inasubiri hadi nyimbo zitoke.
Waziri Mwakyembe amesema Serikali haina vita na wasanii bali kinachofanyika ni kulinda utamaduni wa Mtanzania ili taifa lisiwe kokoro la kila mmoja.
Amesema baadhi ya mataifa yanafanya kazi kwa umakini katika kuangalia kazi za wasanii wao na baadhi wanafungiwa.

Dk Mwakyembe ametolea mfano wa wasanii kutoka Nigeria na Marekani pamoja na mkongwe Koffi Olomide ambao hivi karibuni baadhi ya nyimbo zao zilifungiwa.
Nyimbo ambazo zilifungiwa ni pamoja na Pale kati Patamu na Maku Makuz zilizoimbwa na Ney wa Mitego, kibamia wa Roma Mkatoliki,
Wimbo wa Amani Hamisi maarufu kama Manifango wa Hainaga Ushemeji pia umefungiwa, sawa na I am Sorry JK wake Nikki Mbishi.
Nyimbo nyingine ni Tema mate tumchape (Hamad Ali maarufu Madee), Uzuri Wako (Juma Mussa Mpolopoto maarufu Jux), Nampa Papa (Gift Stanford maarufu Gigy Money) na Nampaga (Barnaba Elias maarufu Barnaba).
Nyimbo za Diamond, ambaye jina lake halisi ni Nasib Abdul, zilizofungiwa ni Hallelujah (aliomshirikisha Morgan Heritage ) na Waka Waka (aliomshirikisha Rick Ross).

Mtoto aliyemzuia baba’ke kuuza shamba apokewa kifalme shuleni

Mwanga. Mtoto Anthony Petro (10) wa Wilaya ya Ngara mkoani Kagera aliyemzuia baba yake kuuza shamba, amepokewa kama mfalme wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro baada ya kuwasili katika Shule ya Amani Vumwe kwa ajili ya kuanza masomo.
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Mwanga, Golden Ally Mgonzo alimvisha Anthony mataji ya maua kuonyesha upendo na jinsi wananchi wa wilaya hiyo walivyopendezwa na ujasiri wake kama mkombozi wa familia.
Pia aliimbiwa nyimbo za kumkaribisha akiitwa mtoto shujaa toka wilayani Ngara.
Katika mapokezi hayo wanafunzi wa shule hiyo, viongozi mbalimbali wa halmashauri ya Mwanga na Ngara na wananchi waliotamani kumuona walikuwwepo. Mgonzo alimuombea Anthony amani na upendo pamoja na baraka awe kiongozi bora ndani na nje ya Tanzania
Alisema mtoto huyo amekuwa na ujasiri, utii, heshima, juhudi na kazi ukiwemo ushirikiano katika kupigania haki za familia bila kutumia ubinafsi na uchoyo.
“Tutahakikisha kipaji chake kinalindwa kwa weledi na kuelekeza kile kitakachokuwa matamanio ya maisha kwake,” alisema.
Ofisa elimu msingi wa wilayani Mwanga, Allan Saidi alisema mtoto huyo ameachwa na waliompeleka na atakuwa katika mazingira salama ili aweze kusoma vizuri na kutimiza malengo yake.
Alisema idara yake itakuwa ikiratibu maendeleo ya taaluma na mahitaji yake kama yataweza kupungua halmashauri kupitia idara hiyo itawajibika kusaidia.
Katika hatua nyingine, ofisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya ya Ngara, Mussa Balagondoza alimkabidhi Anthony kwa ofisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Mwanga, Alex Kameo akidai mtoto huyo hana kovu wala jeraha, hivyo atunzwe na kuangaliwa kwa ukaribu.
“Tunashukuru waliomuibua na vyombo vya habari kufuatilia na kuufahamisha umma kuhusu familia ya mtoto huyu, kiujumla anatoka kaya maskini ambayo hata sisi maofisa ustawi tusingejua kama si vyombo vya habari kushiriki,” alisema.
Anthony aliwatoa machozi waliohudhuria hafla ya mapokezi aliposimama na kusimulia kisa cha kutaka kumshtaki polisi baba yake aliyetaka kuuza shamba.
Akizungumzia ujio wa Anthony, meneja wa Shule ya Amani Vumwe, Isihaka Msuya alisema alimjua kupitia mitandao ya kijamii na kuguswa na maisha yake, hatimaye kuandika kuwa atamsomesha hadi mwisho mwa ndoto zake.

Wanawake 61 Dar wadai kuzaa na viongozi wa dini, wabunge


Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kati ya wanawake 480 waliozungumza na wanasheria jana Jumatatu Aprili 9, 2018, 61 wamezalishwa na kutelekezwa na wabunge pamoja na viongozi wa dini.
Makonda ametoa kauli hiyo leo Aprili 10, 2018 wakati akitoa salamu zake kwa Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan wakati wa uzinduzi wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 unaofanyika leo katika viwanja vya Zakeem Mbagala.
Amesema wanawake 47 wanadai wabunge ndio wamewatelekeza na 14 wamesema kuwa wamezalishwa na kutelekezwa na viongozi wa dini.
"Katika Mkoa wangu wa Dar es Salaam, mwaka 2017 wanawake waliojifungua walikuwa 129,347 na kati ya hao asilimia 60 walitelekezwa na watoto 274 waliokotwa maeneo mbalimbali ndiyo maana tumeona tuje na mkakati huu kuhakikisha tunapambana na wale wanaume wote wanaotelekeza watoto," amesema Makonda.

Samia atia neno wanawake ‘waliotelekezwa’


Dar es Salaam. Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kwa kuibuka na kampeni ya kuwasaidia wanawake wenye watoto ‘waliotelekezwa’.
Mbali na kumpongeza mkuu huyo wa mkoa, amewataka wanaume waliowazalisha wanawake hao iwe kwa kupenda au bahati mbaya kuchukua jukumu la malezi ya watoto wao.
Makamu wa Rais ametoa kauli hiyo leo Jumanne Aprili 10, 2018 wakati akizindua chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wasichana wenye umri wa miaka 14 uliofanyika leo katika viwanja vya Mbagala Zakeem jijini.
Samia ametoa kauli hiyo baada ya awali Makonda kumueleza kuhusu kampeni hiyo sambamba na idadi ya watu waliotajwa kuzaa na wanawake hao na kuwatelekeza, wakiwemo wabunge na viongozi wa dini.
Makamu wa Rais ameyataka mashirika yasiyo ya kiserikali kumuunga mkono kiongozi huyo katika jitihada alizozianza kuokoa kinamama na watoto.
Aidha aliwataja wahusika wakiwemo wanasheria na vituo mbalimbali vinavyohusika na masuala ya ustawi wa jamii kupitisha suala hilo katika njia sahihi kisheria, huku akiwataka Watanzania kuunga mkono na si kukosoa juhudi hizo.
"Mkuu wa mkoa nakupongeza, hatua hii itatupa takwimu zitakazosaidia kufanya utafiti, pengine na mikoa mingine itafanya, naomba baada ya hatua hii wakina mama hawa waelekezwe njia za kufanya," amesema.
"Taasisi nyingine nazo zitoe ushirikiano, tukikosoa hatua hizi za awali tutakuwa hatusaidii jamii, maofisa maendeleo jamii wapo pale baada ya hatua hii wayabebe yatakayokusanywa, watakaokubaliana yaishe wayamalize lakini yale yatakayopelekwa mahakamani yapelekwe."

Mke, mume wakutana kwa Makonda


Dar es Salaam. Mapya yameendelea kuibuka katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda baada ya wazazi wawili kukutana ana kwa ana katika ofisi hizo.
Kuanzia jana asubuhi, wanawake waliotelekezwa na wenza wao walifurika katika ofisi ya RC Makonda kama alivyoagiza ili kuwasaidia kisheria.
Katika tukio la leo, Aprili 10, mwanamke, Sylvia Felisiano alitinga katika viwanja vya ofisi ya RC Makonda, baada ya kusikia mume wake amekwenda kulalamika kuwa amemkimbia na watoto wao watatu.
Awali, mwanaume, Tito Chembs, alifika kwa mkuu wa mkoa akilalamika kuwa mke wake amempokonya watoto na kwenda nao Bukoba.
Saa chache baadaye, Sylvia alipata taarifa hizo kupitia mitandao ya kijamii na kutinga katika ofisi hizo.
Maofisa ustawi wa jamii waliokuwa wakisikiliza mashauri hayo, waliwachukua wenza hao na kuingia nao ndani, huku Sylvia akionekana mwenye hasira na kuahidi ataongea kwa kina na wanahabari.
MCL Digital itaendelea kukujuza kwa kina yanayojiri kutoka katika viwanja vya ofisi ya mkuu wa mkoa.

Serikali yamjibu Nape

Dodoma. Serikali imemjibu Mbunge wa Mtama (CCM) Nape Nnauye na kumueleza kuwa si kweli kuwa imetelekeza miradi ya uzalishaji wa umeme kwa njia ya gesi.
Hayo yameelezwa leo Aprili 10, bungeni na Waziri wa Nishati, Medard Kalemani wakati akichangia bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu katika mwaka wa fedha 2018/19.
 Dk Kalemani amesema si kweli kwamba ilani ya uchaguzi haijataja kabisa mradi wa uzalishaji wa umeme.
“Katika kifungu cha 43 (a) ilani hiyo imeeleza juu ya uzalishaji wa umeme kwa gharama nafuu ikiwa ni pamoja na kutumia gesi na maji lakini haikutaja aina ya mradi,”amesema.
Nape aliibua hoja hiyo jana wakati akichangia hotuba ya ofisi ya Waziri Mkuu na alihoji kuwa ilani ya uchaguzi ya CCM haijazungumzia kuhusu mradi wa Stieglers Gauge na kwamba miradi ya gesi haien

Mama wa mtoto wa Kichina afunguka


Dar es Salaam. Safina Mohamed mkazi wa Mbagala jijini Dar es Salaam amedai kusikitishwa na picha ya mwanawe mwenye asili ya China inayosambaa kwenye mitandao kinyume cha haki za watoto.
Akizungumza na MCL Digital leo Aprili 10, Safina amesema lengo lake lilikuwa si kumdhalilisha mtoto ila kuhitaji matunzo.
"Nasikitishwa kuona mwanangu anasambazwa kwenye mitandao, anazo haki na ni mtoto kama watoto wengine," amesema.
Safina amesema mumewe Zhou Quin aliondoka nchini baada ya kibali chake cha kufanya kazi nchini kuisha mwaka mmoja uliopita, hakuna mawasiliano.
Amesema mtoto wake amekuwa akisumbuliwa na magonjwa ikiwamo macho hivyo hana mtu wa kumsaidia malezi.
"Huyu mwanaume anaishi Jiangsu huko China, binafsi sina kazi wala chochote nimekuja kuomba msaada, nisaidiwe mwanangu apewe matumizi," amesema Safina.

Mwanasheria Mkuu Uganda apinga Mkuu wa Jeshi, Spika kuhojiwa

Wabunge wa Uganda wakipigana makonde Bungeni September 26, 2017.
Waliowasalisha kesi hiyo pia wanapinga hatua ya Bunge hilo kuongeza muda wa rais na wabunge kutumikia wadhifa huo kutoka miaka 5 hadi 7.
Jopo la majaji watano wakiongozwa na Jaji Mkuu Alphonse Owiny Dollo inasikiliza ombi la kupinga hatua ya Bunge la Uganda kuifanyia mabadiliko ibara ya 102(b) ya Katiba ya nchi hiyo, kuhusu umri wa wagombea urais.
Kesi hiyo inasikilizwa katika mji wa Mbale, kilomita 200 mashariki mwa mji wa Kampala.
Kikao cha leo kimekuwa cha kutoa mwelekeo jinsi kesi hiyo itakavyoendeswa na wale watakaoshirikishwa.
Masuala 13 kusikilizwa
Kati ya masuala 13 yanayosikilizwa ni pamoja na hatua ya kuwasilishwa kwa muswada uliopelekea katiba kufanyiwa marekebisho, iwapo ulifanyika kwa mujibu wa sheria.
Kwa sababu kuna madai kwamba wakati wa kuwasilishwa kwake, kiongozi wa upinzani hakuwepo bungeni na wabunge wa upinzani walifukuzwa na spika.
Mahakama ya katiba pia inatakiwa kuamua iwapo hatua ya wanajeshi kuingia bungeni na kuwacharaza wabunge viboko na kuwapiga ngumi wakati wa kuwasilishwa muswada wa mabadiliko hayo ya sheria haukuwa kinyume cha sheria.
Je mchakato ulifuata sheria?
Pande husika pia zitaangalia mchakato mzima uliofuatwa katika kuifanyia Katiba hiyo marekebisho, ikiwemo kuandikwa kwa muswada huo, kutafuta maoni ya raia, kujadili na kupitishwa kwake.
Wanaowasilisha kesi hiyo wanadai kwamba chama kinachotawala cha National Resistance Movement (NRM), hakikuwashirikisha raia katika kufanya mabadiliko hayo na kwamba mchakato mzima uligubikwa na fujo.
Mahakama pia inatakiwa kueleza iwapo Bunge lilitii sheria kwa kuifanyia katiba marekebisho kuhusu utawala wa nchi badala ya kuruhusu raia kufanya uamuzi kupitia kwa kura ya maoni.
Mawakili wanataka mahakama kumwamrisha Mkuu wa Jeshi la Uganda Jenerali David Muhoozi na Spika wa Bunge Rebecca Kadaaga kufika mahakamani ili kuhojiwa.
Lakini Mwanasheria Mkuu Mwesigwa Rukutana, amepinga ombi hilo akisema kwamba maafisa wote wa ngazi ya juu serikalini wanakingwa na sheria na hawawezi kufika mahakamani kuhojiwa.
Muungano wa mawakili
Walalamikaji, wakiongozwa na muungano wa mawakili nchini Uganda na wabunge sita wa upinzani, wanasisitiza kwamba ni ukiukwaji wa katiba kwa wabunge kujiongezea muda wao katika nafasi za ubunge kutoka miaka 5 hadi 7.
Mnamo tarehe 20 mwezi Disemba 2017, Bunge la Uganda lilifanya marekebisho ya katiba ya nchi hiyo na kuondoa kikomo cha umri kwa wagombea urais, pamoja na kuongeza mda wa sasa wa rais na wabunge ofisini kutoka miaka 5 hadi 7.
Wachambuzi wa siasa wanasema kwamba hatua hiyo inamnufaisha rais wa sasa Yoweri Museveni ambaye katiba ilikuwa inamzuia kugombea tena urais baada ya kuitawala nchi hiyo kwa kipindi cha miaka 35.
Majaji wana muda wa siku 7 kusikiliza kesi hiyo kabla ya kufanya maamuzi.

Mwanaume apeleka malalamiko ya kunyanyaswa na mke

Dar es Salaam. Mkazi wa Kitunda, Mohammed Juma ametinga katika ofisi za Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akidai kunyanyaswa na mke wake.
Akizungumza na MCL Digital leo Aprili 10, Juma amesema amefukuzwa na mke wake katika nyumba ya urithi, kisha mwanamke huyo kuwafukuza wazazi wake na watoto wa Juma.
“Wanaume tuna matatizo mengi lakini hatuyasemi, hatuyazungumzi bayana, imefikia wakati tupate nafasi tutoe manung’uniko yetu,” amesema.
Amesema wanawake wana umoja ndiyo maana wanaweza kusema matatizo yao, lakini wanaume nao wanafanyiwa mambo ya ajabu lakini wanavumilia kwa kuwa hawana pa kusemea.
“Nimejenga nyumba kwa fedha zangu, kwa sababu nafanya kazi kwa Wahindi, lakini mwanamke amenidhulumu na akafikia hatua ya kuwafukuza wazazi wangu na watoto wake wa kufikia,” amesema.
Wake kwa waume wamefurika katika ofisi ya Makonda leo baada ya mkuu huyo wa mkoa kuagiza wenza waliotelekezwa na kuachiwa watoto, wafike ili wapewe msaada wa kisheria.

Charlie nani? Mwendesha baiskeli mwanafunzi ashinda dhahabu Madola

Si hata mashabiki wa mbio za baiskeli waliwahi kumsikia Charlie Tanfield mwaka mmoja uliopita, lakini sasa Mwingereza huyo kijana ni bingwa wa michezo ya Jumuiya ya Madola, akiweka rekodi ya muda mrefu.

Australien 2018 Commonwealth Games 2018 | Charlie Tanfield (Reuters/P. Childs)
Charlie Tanfield akisherehekea baada ya ushindi katika mbio za mwendeshaji mmoja mmoja za mita 4000 huko Anna Meares velodrome - Gold Coast, Australia, Aprili 6, 2018.
Kimsingi mwanafunzi huyo anaesomea uhandisi wa umekanika, ambaye bado ni mwanagenzi, kwa namna fulani alikwepa nadhari ya wakuu wa chama cha waendesha baiskeli cha Uingereza hadi hivi karibuni -- lakini hawezi kupuuzwa tena.
Tanfield alipata ushindi katika fainali ya mbio za mita 4,000 katika uwanja wa Anna Meares Veladrome mjini Brisbane siku ya Ijumaa, na kuongeza medali ya dhahabu juu ya ile ya fedha alioipta saa 24 kabla ya hapo.
Wakati akija katika michezo hiyo, Tanfield alisema kwa ujasiri kwamba alikuwa anafukuzia rekodi ya dunia ya saa 4:10.534 iliowekwa na raia wa Australia Jack Bobridge mwaka 2011.
Australien 2018 Commonwealth Games 2018 | Charlie Tanfield (Reuters/P. Childs)
Charlie Tanfield akipeperusha bendera ya taifa lake baada ya ushindi wa kushangaza.
Hakufanikiwa kuivunja rekodi hiyo, lakini bado aliweza kushinda katika moja ya muda mfupi zaidi katika historia ya michezo ya Jumuiya ya Madola, kwa muda wake wa  saa 4:11.455. Hakubahatisha.
Mwanzo wake
Tanfield alijitambulisha kwa hadhira kubwa zaidi wiki chache tu zilizopita wakati aliposhirikia kwa mara ya kwanza katika mashindano ya bingwa wa dunia ya UCI mjini Apeldoorn, Uholanzi.
Alikuwa sehemu ya timu iliyoshinda na alikosa kidogo kupata nafasi ya kupanda jukwaa la washindi kwa kuibuka wa nne katika mashindano ya mtu mmoja mmoja.
Tanfield alieanza kushiriki mchezo huo kikamilifu miezi miwili iliopita, kwa kusimamisha masomo yake ya chuo kikuu, anasema anafurahia "mambo yasio ya kawaida" katika mchezo huo kutokana na historia yake ya uhandisi wa umekanika. Lakini itakuwa kuongeza chumvi kusema kwamba daima alitegemewa kushinda medali.
Akiwa kijana, alipoteza hamasa ya mchezo huo, kabla ya kurejesha mapenzi yake kwake, lakini ulikuwa uundwaji wa timu yake ya KGF uliosadia kumfikisha alipo sasa hivi.
Australien 2018 Commonwealth Games 2018 | Charlie Tanfield (Reuters/P. Childs)
Charlie Tanfield (katikati) akionyesha medali yake ya dhabau alioshinda. Wengine ni mshindi wa medali ya fedha John Archibald wa Scotland, na wa tatu ni Dylan Kenneth wa New zealand alieshinda medali ya shaba.
Mafanikio ya kushangaza ya KGF -- ambao hawana ufadhili mkubwa ikilinganishwa na timu kubwa katika programu ya baiskeli ya Uingereza -- yalikuwa moja ya simulizi za mbio za baiskeli mwaka 2017 na ulivuta nadhari ya wakubwa katika mchezo huo nchini Uingereza.     
Baada ya kufanya mazoezi kwa muda wa miezi miwili, timu hiyo ya wanagenzi isiyo na fedha nyingi ilifanya vizuri katika mashindano ya ubingwa ya Uingereza mwaka huo.
Walibeba mafanikio hayo mjini Minski Januari mwaka huu, wakati Tanfield aliposhinda dhahabu ya kombe la dunia kwa mtu mmoja mmoja, na pia walishinda medali ya dhahabu kwa ngazi ya timu.
Mashujaa wao sasa wanatengezea filamu. "Matokeo yanazidi kuja na ni vizuri kuzidi kujidhihirisha mwenyewe katika jukwaa la kimataifa," alisema Tanfield.

Kambi ya jeshi la Syria yashambuliwa

Mashambulizi ya makombora yamepiga katika kambi ya jeshi la Syria leo (09.04.2018) lakini Marekani na Ufaransa zinakanusha kuhusika kama hatua ya kujibu shambulizi la gesi ya sumu lililofanywa Jumamosi mjini Douma.

Syrien Raketenangriff (picture-alliance/Photoshot)
Shirika la habari la serikali ya Syria SANA limeripoti mapema leo alfajiri kwamba makombora kadhaa yamevurumishwa katika kambi ya jeshi ya Tiyas katika mkoa wa kati wa Homs. Shirika hilo limesema mifumo ya ulinzi wa anga imeanza kutumika na awali liliripoti kuhusu shambulizi linaloshukiwa kufanywa na Marekani, lakini baadaye likafuta kabisa kuitaja Marekani.
Shirika linalofuatilia masuala ya haki za binadamu la Syria limesema wapiganaji 14 wameuawa, wakiwemo wanajeshi wa Iran wanaouunga mkono utawala wa rais wa Syria, Bashar al Assad.
Msemaji wa wizara ya ulinzi ya Marekani, Pentagon, amekanusha madai ya Marekani kuhusika na shambulizi hilo, lakini akasema wanaendelea kuifuatilia kwa karibu hali nchini Syria na itaendelea kusaidia juhudi za kidiplomasia zinazofanywa kuwawajibisha waliohusika na shambulizi la sumu katika mji uliozingirwa wa Douma huko Ghouta Mashariki, siku ya Jumamosi ambapo watu 40 waliuawa.
Shambulizi lakosolewa vikali
Rais wa Marekani, Donald Trump, na mwenzake wa Ufaransa, Emmanuel Macron, hapo jana walilaani vikali shambulizi hilo la sumu na kuapa kuchukua hatua za pamoja kujibu shambulizi hilo ambalo limeibua wasiwasi kote ulimwenguni na kukosolewa vikali. Trump alisema rais wa Urusi, Vladimir Putin, Urusi na Iran wanahusika aktika kumuunga mkono mnyama Bashar al Assad na akaonya watalipa kwa gharama kubwa.
Kiongozi wa kanisa Katoliki duniani Papa Francis amesema hakuna kinachoweza kulihalalisha shambulizi la sumu nchini Syria wakati alipokuwa akiifunga misa jana Jumapili. Alizungumzia taarifa za kutisha za watu kuuliwa katika mashambulizi ya mabomu yanayosababisha majeruhi wengi, miongoni mwao watoto na wanawake.
Vatikan Papst hält Ostermesse (picture-alliance/dpa/AP Photo/A. Medichini)
Papa Francis
"Tuwaombee waliokufa, majeruhi na familia za wahanga ambazo zinateseka. Hakuna vita vizuri wala vibaya, na hakuna kinachoweza kuhalalisha nyenzo za maangamizi ya namna hii zinazowaua watu wasioweza kujilinda. Tuwaombee wanasiasa na viongozi wa kijeshi wachague njia nyingine ya mazungumzo, ambayo pekee inaweza kuleta amani badala ya kifo na maangamizi."
Rais wa Uturuki Recep Tayaip Erdogan amelilaani vikali shambulizi hilo la sumu huko Douma akizituhumu nchi za Magharibi kwa kuupuzilia mbali siasa chafu za kinyama zinazoendeshwa na utawala wa Syria. Akizunguza mjini Siirt, Erdogan alisema umma wa Uturuki haukubaliani kabisa na mwenendo huo.
"Tunapinga kwa nguvu zote undumakuwili huu na siasa hizi za kinyama. Nchi za Magharibi! Ni lini mtakapogeuka na kuwatazama watoto hawa, wanawake hawa wanaouliwa Ghouta Mashariki ili tuseme mnatenda haki?"
Kikao cha baraza la usalama kufanyika
Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kukutana leo kuijadili hali nchini Syria huku Umoja wa Ulaya ukisema ushahidi wote wa shambulizi la sumu unaashiria limefanywa na utawala wa Syria. Iran kwa upande wake imesema shambulizi hilo linatumiwa kama kisingio cha kufanya harakati ya kijeshi Syria.
China imesema leo inaunga mkono uchunguzi kuhusiana na shambulizi linaloshukiwa kuwa la sumu mjini Douma huku ikitoa wito kwa baraza la usalama na shirika la kimataifa la kudhibiti silaha za sumu OPCW kuendelea na jukumu lao kama wadau wakuu wa kulishughulikia tatizo hilo.

Trump akasirishwa na FBI kuzipekua ofisi za Cohen

Maafisa wa Shirika la Upelelezi la Marekani, FBI wamezipekua ofisi za wakili binafsi wa Rais wa Marekani Donald Trump, Michael Cohen. Trump amekasirishwa na hatua hiyo na kulikosoa vikali shirika hilo.

USA Rechtsanwalt Michael Cohen in Washington (Reuters/J. Ernst)
Michael Cohen, wakili wa Trump
Maafisa wa Shirika la Upelelezi la Marekani, FBI wamezipekua ofisi za wakili binafsi wa Rais wa Marekani Donald Trump, Michael Cohen. Trump amekasirishwa na hatua hiyo na kulikosoa vikali shirika hilo.
Stephen Ryan, ambaye ni wakili wa Cohen, amesema kuwa upekuzi huo uliofanyika jana ni sehemu ya maelekezo kutoka kwa Robert Mueller, mwanasheria anayeoongoza uchunguzi kuhusu ushirikiano kati ya timu ya kampeni ya Rais Trump pamoja na Urusi wakati wa uchaguzi wa urais uliofanyika Marekani mwaka 2016.
Hata hivyo, gazeti la The New York Times limeripoti kuwa uvamizi huo hauhusiani na maelezo ya Mueller. Ryan ametoa taarifa inayoeleza kuwa mteja wake tayari alishirikiana na maafisa kwa kuwasilisha maelfu ya nyaraka kwa wachunguzi wa bunge, ambao pia wanachunguza kuhusu madai ya Urusi kuingilia uchaguzi wa Marekani.
Robert Mueller (Reuters/J. Roberts)
Robert Mueller
Aidha, Ryan amekosa uvamizi huo wa FBI akisema kuwa matumizi ya vibali vya kufanya uchunguzi hayakuwa sawa na hayakufaa kabisa. Amesema katika upekuzi huo maafisa wa FBI wamechukua taarifa kuhusu matukio mbalimbali ikiwemo nyaraka za malipo ya Dola 130,000 yaliyotolewa kwa mcheza filamu za ngono, Stormy Daniels.
Cohen na Mueller wote hawajazungumza lolote kuhusu sakata hilo. Akizungumza na waandishi habari, Trump amelaani vikali uvamizi huo na kusema kwamba uchunguzi unaofanywa na Mueller ni shambulizi dhidi ya Marekani.
''Nimesikia kwamba wamevamia ofisi ya mmoja wa mawakili wangu binafsi, mtu mzuri. Hali hii ni ya aibu. Ni shambulizi dhidi ya nchi yetu, kwa maana halisi. Ni shambulizi katika kile ambacho sisi wote tunakisimamia,'' alisema Trump.
Katika wiki za hivi karibuni, Cohen ametawala katika vyombo vya habari tangu ilipogundulika kuwa alimlipa Dola 130,000 Stormy Daniels kabla ya uchaguzi wa urais mwaka 2016. Daniels alisema fedha hizo zilikuwa ni malipo ya kumnyamazisha na asizungumze chochote kuhusu madai kwamba alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na Trump.
USA | Trump kündigt militärischen Rückzug aus Syrien an (Getty Images/J. Swensen)
Rais Donald Trump
Hata hivyo, Ikulu ya Marekani imeyakanusha madai ya Daniels na Rais Trump amesema hajui lolote kuhusu malipo hayo yaliyotolewa na Cohen. Uvamizi huo ni mtihani mwingine kwa Trump wakati ambapo yeye na mawakili wake wanaangalia iwapo wakubaliane kuhusu kuhojiwa na timu ya Mueller, ambayo inachunguza madai ya uhusiano kati ya Urusi na Marekani.
Kulingana na masharti na kanuni za wizara ya sheria ya Marekani, Mueller anapaswa kushauriana na Naibu Mwanasheria Mkuu Rod Rosenstein, iwapo wachunguzi wake watabaini ushahidi mpya ambao unaweza kuangukia nje ya mamlaka yake ya awali. Baada ya hapo Rosenstein ataamua kama amruhusu Mueller kuendelea au kumpa jukumu hilo mwanasheria mwingine wa Marekani au mtu mwingine ambaye ni sehemu ya wizara ya sheria.
Kwa mujibu wa The New York Times, timu hiyo maalum ya Mueller inachunguza pia malipo ya Dola 150,000 yaliyotolewa wakati wa kampeni za uchaguzi wa urais wa Marekani kwa bilionea wa Ukraine, Viktor Pinchuk. Fedha hizo zililipwa na mfuko wa Trump wa mradi wa mali zisizohamishika ili uweze kupewa muda wa dakaki 20 kuhutubia kwa njia ya video kupitia mfumo maalum wa kuwaunganisha watu kutoka maeneo mbalimbali.

Mkuu wa zamani wa majeshi Sudan Kusini aunda vugu vugu jipya la waasi

Raia wa Sudan ya KusiniHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRaia wa Sudan ya kusini
Aliyekuwa Mkuu Majeshi Sudan Kusini ameunda vugu vugu jipya la kundi la waasi.
Paul Malong ambaye alitimuliwa katika wadhifa wake na Rais Salva Kiir mwaka, amechukua hatua hiyo wakati nchi yake ikianza tena mazungumzoa ya amani mjini Addis Abba Ethiopia.
Mazungumzo hayo pia, yana lenga kufikia makubaliano ya kuachiliwa kwa Makamu Rais Riek Machar ambaye kwa sasa yuko katika kizuizi cha nyumbani nchini Afrika Kusini.
Malong amekuwa akiishutumu serikali kwa rushwa na makosa ya kuifilisi nchi, anasema kuwa kundi lake la waasi litakuwa na jukumu kubwa la kuiondoa Sudan Kusini kwenye sintofahamu na kuielekeza katika demokrasia na maendeleo.
Wapiganaji Sudan Kusini, na silaha hatariHaki miliki ya pichaREUTERS
Kufuatia kuundwa kwa kundi jipya la waasi, serikali ya Suda Kusin haijasema neno lolote, ambayo inapigana na vikundi kadhaa vya waasi nchini mwake .
Inaarifiwa kuwa wakati Malong alipokuwa ana wadhifa wa mkuu wa majeshi alikuwa akituhumiwa na Umoja wa mataifa kwa kuratibu mashambulizi ya kikabila dhidi ya raia.
Wakati hayo yakijiri inaarifiwa kuwa mapigano yanaendelea nchini Sudan Kusini baina ya vikosi vya serikali na vikundi vya waasi licha ya mpango wa amani uliosainiwa mwaka 2015.

Trump aapa ''kutumia nguvu'' kujibu shambulio ''la kemikali'' Syria

Rais wa Marekani Donald Trump
Image captionRais Donald Trump amesema Marekani inapata ''msaada mzuri" juu ya nani aliyehusika na shambulio la Douma Jumamosi.
Rais wa Marekani Donald Trump ameahidi " kutumia nguvu " kujibu madai ya shambulio la kemikali nchini Syria, huku mataifa ya magharibi yakitafakari hatua watakayoichukua.
"Tuna njia nyingi za kijeshi,"aliwambia waandishi wa habari.
Aliongeza kuwa hatua ya kujibu shambulio hilo itaamuliwa katika kipindi cha "muda mfupi".
Bwana Trump alisema kuwa Marekani inapata ''msaada mzuri" juu ya nani aliyehusika na shambulio la Douma Jumamosi.
Duru za kitabibu zinasema makumi kadhaa ya watu waliawa katika shambulio hilo, lakini idadi kamili haijathibitishwa.
Bw Trump pia alijadili tukio hilo la rais wa Ufaransa Emmanuel Macron Jumatatu jioni, na viongozi wote walielezea utashi wao wa "kujibu kikamilifu".
Nikki Haley mjumbe wa Marekani katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
Image captionMjumbe wa Marekani Nikki Haley alisema kuwa-wanaounga mkono jeshi la Syrian - wana "damu ya watoto wa Syria " mikononi mwao
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amesema kuwa "analaani vikali" kitendo cha "ukatili" kinachodaiwa kuwa ni shambulio la kemikali na akatoa wito kwa wanaomuunga mkono rais Bashar al-Assad kuwajibishwa.
Kauli za viongozi wa kimagharibi za kulaani shambulio hilo zimefuatia kikao cha malumbano katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambapo Marekani na Urusi walitupia na maneno makali kuhusiana na tukio la Douma.
Muwakilishi wa Urusi kwenye baraza hilo Vassily Nebenzia alisema shambulio linalodaiwa lilipangwa na akaonya kwamba hatua za kijeshi za Marekani zinazolenga kujibu tukio hilo "litakuwa na athari mbaya".
Mjumbe wa Marekani Nikki Haley alisema kuwa-wanaounga mkono jeshi la Syrian - wana "damu ya watoto wa Syria " mikononi mwao na akambandika jina rais Assad kama "zimwi ".
Muwakilishi wa Urusi kwenye baraza hilo Vassily Nebenzia
Image captionMuwakilishi wa Urusi kwenye baraza hilo Vassily Nebenzia alisema linalodaiwa kuwa la kemikali dhidi ya Douma lilipangwa
Bi Haley alitoa wito wa kupigwa kura juu ya muswada wa maazimio ya kubuniwa kwa tume ya uchunguzi juu ya matumizi ya silaha za kemiikali nchini Syria siku ya Jumanne.
Lakini Urusi inasema haiwezi kuunga mkono pendekezo hilo kwasababu lina "vipengele visivyokubalika''.

Ni kipi kilichotokea Jumamosi?.

Shirika la matibabu la Marekani na Syria linasema kuwa watu zaidi ya 500 waliletwa kwenye kituo cha matibabu katika mji wa Douma, uliopo katika jimbo la mashariki la Ghouta , karibu na mji mkuu Damascus, wakiwa na dalili "zinazoonesha kuwa walishambuliwa na kemikali".
Shirika hilo linasema dalili walizaokuwa nazo ni pamoja na ugumu wa kupumua, ngozi ya samawati , kutokwa na povu mdomoni , kuungua kwa mboni na "walikuwa na harufu kama ya kemikali ya chlorine".
Idadi kamili ya vifo ya na ni nini hasa kilichotokea haviwezi kuthibitishwa kwasababu eneo hilo halina mawasiliano.
Makadirio ya idadi ya watu waliouawa katika shambulio linaloshukiwa kuwa la kemikali ni kuanzia watu 42 hadi zaidi 60, lakini makundi ya kitabibu yanasema idadi hiyo inaweza kuongezeka baada ya wahudumu wa uokoaji kuweza kufika kwenye sehemu za chini za majengo ambako mamia ya familia walikuwa wamekimbilia kuepuka mashambulio ya mabomu.
Muwakilishi wa Ufaransa katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa amesema gesi ya sumu ilitumiwa kwa makusudi kwasababu inaweza kusambaa hadi sehemu za chini za majengo hadi.
Marekani ,ufaransa na Uingereza wameongoza kampeni ya kimataifa ya kulaani shambulio hilo linalodaiwa kuwa la kemikali, huku serikali ya Syria na waungaji mkono wao Urusi wakikana kuwajibika kwao kokote na tukio hilo.