Tuesday, September 19

Waliooana kwa miaka 75 wafariki siku moja

Jean and George Spear met the Duchess of Cambridge in 2011 when she visited OttawaHaki miliki ya pichaWAYNE CUDDINGTON / COURTESY OF OTTAWA CITIZEN
Image captionJean na George Spear walikutana na Duchess of Cambridge mwaka 2011
Wanandoa walio oana kwa miaka 75 wamefriki siku moja wakiachana kwa saa tano tu, ikiwa ni mwezi mmoja tangu washerekee ndoo yao wa miaka 75.
George mwanajeshi wa zamani na Jean Spear walikutana mwaka 1941 karibu na London wakati George akitoa huduma zake nchini Uingereza wakati wa vita vya pili vya dunia.
Wawili hao walifariki kwenye hospitali ya Ottawa siku ya Ijumaa baafa ya Bi Spear 94 kulazwa hospitalini.
Alipewa tuzo la juu zaidi la Uingeza mnamo mwaka 2006.
Bi Spear na mumewa wa miaka 95 walikutana na Duke na Duches wa Cambridge wakati waliitembelea familia ya kifalme mwaka 2011.
Image captionJean na George Spear mwaka 1942
Bw. Spear alilazwa katika hospitali ya Queensway Carleton siku ya Jumatano, siku moja baada ya mke wake kulwzwa, na kulala usingizi mkubwa.
Wahudumu wa hospitali walijaribu kumhamisha Bw Spear kwenda chumba alichokuwa mkewe, lakini Bi Spear akafariki alipokuwa akilala siku ya Ijumaa mwendo wa 04:30 kabla ya hilo kufanyika.
Bwana Spear naye alifarki muda mfupi baadaye mwindo wa saa 09:45.
Wameacha watoto wawili wakubwa Heather na Ian.

Mwandishi kutoka Nigeria ashinda tuzo ya Komla Dumor

Amina Yuguda
Image captionAmina Yuguda ni mtangazaji katika kituo runinga cha eneo hilo cha Gotel
Mwandishi wa habari kutoka kaskazini mashariki mwa Nigeria ameshinda tuzo ya BBC la Komla Dumor.
Amina Yuguda ni mtangazaji katika kituo runinga cha eneo hilo cha Gotel, ambapo ameripoti kuhusu masuala kadha makuu ikiwemo kuhusu kundi la Boko Haram.
Yuguda atasafiri kwenda London kwa mafunzo ya miezi matatu mwezi Septemba.
Tuzo hili lilibuniwa kwa heshima ya Komla Dumor, mtangazaji wa runinga ya BBC ambaye alifariki ghafla akiwa na miaka 41 mwaka 2014.
Bi Yuguda amesema kuwa ushindi wake ni heshima kubwa.
Amina Yuguda
Image captionAmina Yuguda aliwavutia majaji kwa ripoti zake zinazohusu ushawishi wa radio nyumbani kwake.
Aliwavutia majaji kwa ripoti zake zinazohusu ushawishi wa radio nyumbani kwake.
"Kwa kisomo kidogo au kutokuwa na kisomo kabisa, wananchi wenzangu wanaelewa masula kadha ikiwemo uongozi wa Trump nchini Marekani, Korea Kaskania, Urusi chini ya Vladimir Putin na mengine mengi". Anasema Amina.
Mkurugenzi wa BBC World Service Group Francesca Unsworth, alisema Bi Yuguda alistahili ushindi huo.
Washindi wa awali wa tuzo la Kumla Dumor ni pamoja na mtangazaji raia wa Uganda Nancy Kacungira na mwandishi wa masuala ya biashara kutoka Nigeria Did Akinyelure

Suu Kyi: Myanmar haiogopi kuchunguzwa kutokana na mzozo wa Rohingya

Myanmar's State Counsellor Aung San Suu Kyi speaks during a joint a press conference with Sweden's Prime minister at the Rosenbad government office on 12 June 2017 in Stockholm, Sweden.Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionMs Suu Kyi, a Nobel Peace Prize laureate, has been criticised for inaction
Kiongozi wa Myanmar Aung San Suu Kyi amesema kuwa serikali yake haina hofu ya kuchunguzwa kuhusu njia inashughulikia suala la watu wa Rohingya.
Ilikuwa hotuba yake ya kwanza kwa nchi kuhusu ghasia katika jimbo la Rakhine ambazo zimesababisha zaidi ya watu 400,000 wa jamii ya Rohingya kuvuka mpaka na kuingia nchini Bangladesh.
Bi Suu Kyi amelaumiwa vikali kuhusu jinsi alishughulikia suala hilo.
Rohingya refugees walk to a Border Guard Bangladesh (BGB) post after crossing the Bangladesh-Myanmar border by boat through the Bay of Bengal in Shah Porir Dwip, Bangladesh, 10 September 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionA new wave of Rohingya Muslims has been pouring into Bangladesh since 25 August
Lakini amesema kuwa waisilamu wengi hawajakimbia jimbo hilo na kwamba hali imetumia
Kwenye hotuba yake kwa bunge la Mynammar, Aung San Suu Kyi alisema amuhusuniswa na kuendelea kutaabika kwa watu wote katika mzozo huo na kwamba Myanma imejitolea kutatua suala hilo kwa jamii zote nchini humo.
A small village in the distance, over a verdant green field, burns fiercely under a column of thick black smoke
Image captionBBC reporters witnessed burning Muslim villages in Myanmar
Bi Suu Kyi ambaye ameamua kutohudhuria mkutano wa baraza la Umoja wa Mataifa mjini News York badaye wiki hii, alisema kuwa alikuwa anataka jamii ya kimataifa kufahamu kile kilichokuwa kikifanywa na serikali yake.

Suu Kyi: Myanmar haiogopi kuchunguzwa kutokana na mzozo wa Rohingya

Myanmar's State Counsellor Aung San Suu Kyi speaks during a joint a press conference with Sweden's Prime minister at the Rosenbad government office on 12 June 2017 in Stockholm, Sweden.Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionMs Suu Kyi, a Nobel Peace Prize laureate, has been criticised for inaction
Kiongozi wa Myanmar Aung San Suu Kyi amesema kuwa serikali yake haina hofu ya kuchunguzwa kuhusu njia inashughulikia suala la watu wa Rohingya.
Ilikuwa hotuba yake ya kwanza kwa nchi kuhusu ghasia katika jimbo la Rakhine ambazo zimesababisha zaidi ya watu 400,000 wa jamii ya Rohingya kuvuka mpaka na kuingia nchini Bangladesh.
Bi Suu Kyi amelaumiwa vikali kuhusu jinsi alishughulikia suala hilo.
Rohingya refugees walk to a Border Guard Bangladesh (BGB) post after crossing the Bangladesh-Myanmar border by boat through the Bay of Bengal in Shah Porir Dwip, Bangladesh, 10 September 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionA new wave of Rohingya Muslims has been pouring into Bangladesh since 25 August
Lakini amesema kuwa waisilamu wengi hawajakimbia jimbo hilo na kwamba hali imetumia
Kwenye hotuba yake kwa bunge la Mynammar, Aung San Suu Kyi alisema amuhusuniswa na kuendelea kutaabika kwa watu wote katika mzozo huo na kwamba Myanma imejitolea kutatua suala hilo kwa jamii zote nchini humo.
A small village in the distance, over a verdant green field, burns fiercely under a column of thick black smoke
Image captionBBC reporters witnessed burning Muslim villages in Myanmar
Bi Suu Kyi ambaye ameamua kutohudhuria mkutano wa baraza la Umoja wa Mataifa mjini News York badaye wiki hii, alisema kuwa alikuwa anataka jamii ya kimataifa kufahamu kile kilichokuwa kikifanywa na serikali yake.

Trump ataka kumbana zaidi Rais Maduro

Rais Nicolas Maduro, anayelalamikiwa na MarekaniHaki miliki ya pichaEPA
Image captionRais Nicolas Maduro, anayelalamikiwa na Marekani
Rais wa Marekani Donald Trump amesisitizia wito wa kurejesha katika hali ya kawaida uhuru wa kisiasa na demokrasia nchini Venezuela.
Akizungumza na viongozi wa Amerika ya kusini mjini New York, Rais Trump amesema atachukua hatua zaidi, dhidi ya kile alichokiita utawala wa kidikteta wa Rais Nocolas Maduro.
Amesema watu wa Venezuela wamekuwa wakikosa chakula na nchi yao kizidi kuharibika, licha ya awali kuwa ni nchi tajiri.
Mwezi uliopita serikali ya Marekani iliiwekea Venezuela vikwazo vipya vya kifedha.
Aidha ilimuwekea pia vikwazo Rais Maduro na baadhi ya wasaidizi wake wa karibu, kwa kile ilichokiita kuwa ni diktekta.

Wafuasi wa Kenyatta wailaumu mahakama kuwaibia ushindi

Maandamano ya wafuasi wa uhuru kenyattaHaki miliki ya pichaDAILY NATION TWEETER
Image captionMaandamano ya wafuasi wa Uhuru Kenyatta wakiwa nje ya mahakama kuu mjini Nairobi
Wafuasi wa rais wa Kenya Uhuru Kenyatta wanaandamana nje ya mahakama kuu mjini Nairobi, wakiitaka tume ya kitaifa inayoajiri na kufuatilia mienendo ya majaji iwachunguze.
Kwa mujibu wa ukurasa wa Twitter wa gazeti la kibinafsi la Daily Nation, Wafuasi wa Kenyatta wamekusanyika wakiwashutumu majaji wa mahakama kuu kwa kuwaibia "ushindi wao ".
Majaji wa mahakama hiyo walitoa uamuzi wa kubatilishwa kwa matokeo ya uchaguzi wa urais wa tarehe 8 Agosti yaliyompatia ushindi Bwana Kenyatta baada ya kusema kuwa mchakato wake ulitawaliwa na "ukiukaji wa sheria na makosa"
Maandamano hayo yamefanyika wakati gazeti la The Standard kuchapisha taarifa ya madai kwamba majaji wawili wa Mahakama kuu , Philemona Mwilu na Isaac Lenaola, ambao walipigia kura kubatilishwa kwa uchaguzi, walikutana na mawakili wa kiongozi wa upinzani, Raila Odinga, wakati wa kusikilizwa kwa kesi ya kupinga ushindi wa Bwana Uhuru Kenyatta.
Taarifa hiyo iliyotawala mazungumzo ya raia wa Kenya kwenye mtandao wa Twitter,pia inasema kuwa kuna mazungumzo ya simu yaliyo rekodiwa kuthibitisha kwamba kulikuwa na mawasiliano baina ya majaji na mawakili wa upinzani waketi kesi hiyo ikiendelea.
mwandishi wa habari nchini humo ameripoti kuwa waandamanaji wamekwisha wasilisha madai yao kwa tume ya huduma za mahakama inayowaajiri na kuchunguza mienendo ya majaji nchini Kenya.

Serikali ya Tanzania yaendelea kuzuia almasi ya kampuni ya Petra

Mamlaka zilikamata bahasha iliyokuwa na almasi ambayo hadi sasa haijaachiliwa.Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMamlaka zilikamata bahasha iliyokuwa na almasi ambayo hadi sasa haijaachiliwa
Shughuli zimeanza tena katika mgodi mkubwa zaidi wa madini ya almasi nchini Tanzania, licha ya mzozo na serikali ya Tanzania, ambayo ilikamata bahasha iliyokuwa na almasi kwenye uwanja wa ndege.
Shughuli katika mgodi wa Williamson zimerejeshwa baada ya kusimamishwa kwa siku nne.
Wiki moja iliyopita hisa kwenye kampuni ya Uingereza ya Petra zilishuka kwa asilimia 7, baada ya almasi zake kuzuiwa kusafirishwa kutoka nchi Tanzania, ambapo pia wafanyakazi wake kadha walihojiwa na mamlaka za nchi hiyo.
Mamlaka zilikamata bahasha iliyokuwa na almasi ambayo hadi sasa haijaachiliwa.
Mazungumzo ya kampuni na serikali kuhusu suala hilo yanaendelea, kwa kujibu wa kampuni ya Petra.
Kampuni hiyo kubwa zaidi ya kuchimba almasi nchi Tanzania inalaumiwa kwa kuzusha thamani ya almasi zake.
Serikali inasema kuwa Petro iliandika mzigo huo kuwa wa thamani ya dola milioni 14.6 wakati thahamia yake halisi ilikuwa dola milioni 29.5.
Petro ilikana madai hayo, ikisema kuwa serikali ndiyo inahusika kwa kuthibitisha thamani kama hiyo.
Mgodi wa Williamson ulio kaskazini magharibi mwa Tanzania unamilikiwa na Perto kwa asilimia 25 huku serikali ya Tanzania ikimiliki asilimia 25.

Kimbunga chenye nguvu Maria chapiga kisiwa cha Dominica

Image shows Hurricane Maria in the Atlantic oceanHaki miliki ya pichaNASA
Image captionMaria is moving roughly along the same path as Irma, which devastated the Caribbean this month
Kimbunga Maria kilichopata nguvu na kufikia kiwango cha tano kimepiga kisiwa cha Caribbean cha Dominica kikiwa na upepo wa kasi ya kilomita 260 kwa saa.
Waziri mkuu Roosevelt Skerrit aliandika katika mtandao wa Facebook kuwa paa la nyumba yake limeng'olewa.
Alisema nyumba yake ilifurika maji na baadaye kusema kuwa alikuwa ameokolea.
Uwanja wa ndege wa Dominica na bandari vimefungwa.
Maria kinapitia njia ambayo kimbunga kama hicho wa jina Irma kilisababisha uharibifu wakati kikipitia eneo hilo mwezi huu.
Kisiwa kilicho karibu cha Martinique kiliwekwa katika tahadhari huku kingine cha Ufaransa cha Guadeloupe kiliwaamrisha watu kuondoka.
Image shows US soldiers waiting to be evacuated on a beach in the US Virgin Islands on 17 September 2017Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWanajeshi wa Marekani waliondolewa kutioka visiwa vya Marekani siku ya Jumapili
Baaadhi ya sehemu hizo bado zinarejea hali ya kawaida baada ya kupigwa na kimbunga Irma , ambacho ni kimbunga cha kiwango cha tano kilichosababisha vifo vya watu 37 na kusababisha hasara ya mabiliono ya dola.
Visiwa vinavyokumbwa na kimbunga Maria ni pamoja na visiwa vya Leeward vikiwemo Antigua na Barbuda.
ituo cha vimbunga cha Marekani (NHC) kiliongeza nguvu ya kimbunga hicho siku ya Jumatatu kutoka kiwango cha pili hadi kiwango cha nne na kisha kiwango cha tano ambacho ni kiwango cha juu zaidi.
Watabiri wa hali ya hewa walionya kuwa mvua kubwa inayosababishwa na kimbunga hicho inaweza kusababisha mafuriko na maporomoko ya udongo ya kutishia maisha.
Graphic shows Maria's predicted path across the eastern Caribbean
Image captionVisiwa vya Leeward n pamoja na Antigua na Barbuda

Jaji Maraga: Hatuogopi chochote

Jaji mkuu David Maraga wa Kenya amemshutumu inspekta jenerali wa polisi Joseph Boinet Chief kwa kukataa wito wa kuimarisha usalama wa majaji na mahakama
Image captionJaji mkuu David Maraga wa Kenya amemshutumu inspekta jenerali wa polisi Joseph Boinet Chief kwa kukataa wito wa kuimarisha usalama wa majaji na mahakama
Jaji mkuu David Maraga wa Kenya amemshutumu inspekta jenerali wa polisi Joseph Boinet nchini humo kwa kukataa wito wa kuimarisha usalama wa majaji na mahakama na hivybasi kuwahatarisha.
Katika taarifa baada ya mkutano wa muda mrefu na wanachama wa tume ya huduma za mahakama, JSC, jaji mkuu Maraga amesema kuwa idara ya mahakama na majaji hatahivyo itaendelea kutoa huduma zake.
Amesema kuwa wako tayari kukabiliana na lolote lile kutetea katiba na sheria ya Kenya.
JSC imebaini kwamba inspekta jenerali wa plisi ambaye anafaa kutoa usalama kwa idara zote za serikali amekaidi wito ya kuchukua hatua , hivyobasi kuhatarisha maisha ya maafisa waidara ya mahakama, mali na walalamishi kwa hatari, alisema.
Jaji mkuu alisistiza kuwa idara ya mahakama ni kitengo huru cha serikali sawa na uongoza wa taifa na bunge.
Na iwapo viongozi wamechoka kuwa na idara ya mahakama iliyo thabiti na huru, alisema waitishe kura ya maamuzi na kufutilia mbali.
Amesema kuwa inauma kwamba idara ya mahakama na majaji hususana wale wa mahakama ya juu wamekuwa wakishambuliwa mara kwa mara na kusababisha maandamano, yaliofanyika nje ya mahakama ya juu mjini Nairobi, Nyeri, Nakuru na Eldoret
Jaji maraga amesema kuwa maandamano yalikuwa na ghasia na yalilenga kuishinikiza idara ya mahakama na majaji fulani.
"Idara ya mahakama haijawahi kuziagiza idara nyengine za serikali kuhusu majukumu yao waliopewa na raia wa Kenya pamoja na katiba .Tunataka kusema kwamba sheria lazima ifuatwe kila mara.