Monday, November 13

ASEAN kuepuka ugomvi kuhusu bahari ya Kusini mwa China

Viongozi kutoka nchi 10 wanachama wa Jumuiya ya mataifa ya Kusini Mashariki mwa Asia ASEAN pamoja na China walijadili mkataba unaohusu shughuli zao

Vietnam chinesicher Präsident Xi Jinping in Hanoi (picture-alliance/AP Photo/Hoang Dinh Nam)
Vietnam na China zimekubaliana kuepuka ugomvi katika eneo linalozozaniwa la bahari ya Kusini mwa China kama njia mpya ya kuwezesha mazungumzo ya viongozi wa nchi zaeneo hilo  ili kupunguza hali ya  wasiwasi.
Nchi hizo mbili jirani na za kikoministi zimekuwa katika mvutano kuhusu bahari ambayo huwezesha biashara ya dola trilioni tano kila mwaka na ambayo inaaminika kuwa na utajiri mkubwa wa gesi.
Katika taarifa ya pamoja, baada ya rais wa China Xi Jinping kuitembelea Vietnam , Vietnam na China zimekubaliana kudumisha Amani katika bahari hiyo.
Mkataba wa kumaliza ugomvi
Katika mkutano uliofanyika mji mkuu wa Ufilipino-Manila na kufunguliwa na rais wa nchi hiyo Rodrigo Duterte, viongozi kutoka nchi 10 wanachama wa Jumuiya ya mataifa ya Kusini Mashariki mwa Asia ASEAN pamoja na China walijadili mkataba unaohusu shughuli zao, ambapo walielezea matumaini kuhusu mustakabali wa mahusiano yao.
Wamekubaliana kusimamia vyema mizozo ya bahari, kutochukua hatua zinazoweza kutatua au mizozo na pia kudumisha Amani katika Bahari ya Mashariki.
Rais Trump ashangaa alipogundua anasalimiana tofauti na jinsi viongozi wa ASEAN husalimiana
Rais Trump ashangaa alipogundua anasalimiana tofauti na jinsi viongozi wa ASEAN husalimiana
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa kutoka upande wa Vietnam kuhusu maafikiano hayo. Viongozi hao pia watasaini mkataba wa kulinda wafanyakazi wahamiaji wanaotoka nchi maskini katika kanda hiyo.
China yadai umiliki wa bahari hiyo
China inadai takriban bahari hiyo yote na hata kukaribia fukwe za nchi jirani. Katika miaka ya hivi karibuni China imeunda kisiwa na kujenga uwanja mdogo wa wa ndege unaoweza kutumiwa kijeshi katika eneo hilo linalozozaniwa ili kuimarisha udhibiti wake, hali ambayo imezusha wasiwasi  miongoni mwa mataifa jirani.
Kumekuwa na mizozano ya kivita mara mbili kati ya China na Vietnam baharini mnamo 1974 na 1988 ambapo wanajeshi kadhaa wa Vietnam waliuawa.
Trump ashiriki mikutano na viongozi wa ASEAN
Mapema wiki hii, rais wa Marekani Donald Trump alikuwa mjini Manila kwa mikutano na viongozi wa ASEAN na nchi nyingine ambapo pia ndicho kituo chake cha mwisho katika ziara yake barani Asia.
Katika wa Jumuiya ya ASEAN, China na Jumuiya hiyo ambamo Vietnam pia ni mwanachama zilitangaza kuwa zimekubaliana kuanzisha mazungumzo kuhusu mkataba wa shughuli zao katika bahari hiyo ya Kusini mwa china.
Kwa mujibu wa kituo cha televisheni kinachomilikiwa na serikali ya China Waziri Mkuu wa China Li Keqiang aliridhia mkataba wa viongozi wa ASEAN. Hata hivyo hakuna muda maalum ambao ulitolewa kuhusu kuwepo kwa mkataba kamili.

Jeshi laonya kuhusu mgogoro ndani ya Zanu-PF Zimbabwe

kamanda mkuu wa jeshi nchini Zimbabwe Jenerali Constantino ChiwengaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionkamanda mkuu wa jeshi nchini Zimbabwe Jenerali Constantino Chiwenga
Kamanda mkuu wa jeshi la Zimbabwe ameonya kuingilia kati iwapo pande pinzani zitaendelea kuzozana ndani ya chama tawala cha Zanu-PF.
Katika taarifa isio ya kawaida , Jenerali Constantino Chiwenga ametaka kusitishwa kwa vita dhidi ya wanachama waliopigania uhuru wa taifa hilo.
Matamshi yake yanajiri baada ya rais Robert Mugabe kumfuta kazi makamu wake wa rais aliyetarajiwa kumrithi Emmerson Mnangagwa.
Kufutwa kwake kunampatia bi Grace Mugabe fursa kumrithi kiongozi huyu mwenye umri wa miaka 93.
Bwana Mnangagwa amelitoroka taifa hilo akihofia maisha yake.
Akizungumza katika makao makuu ya jeshi , jenerali Chiwenga alisema: Mgogoro unaoendelea unaowalenga wanachama wa chama hicho waliopiganai uhuru ni lazima ukome.
''Tunawakumbusha wale wanaofanya hivyo kwamba inapofikia wakati wa kulinda uhuru wetu jeshi halitasita kuingilia kati''.

Nyalandu asikitishwa na Waziri Kigwangala



Dar es Salaam. Aliyekuwa Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu  amesema inasikitisha kuona Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamis Kigwangalla  akitumia muda  ndani ya Bunge kumchafua, kudhihaki na kusema uzushi na  uongo dhidi yake.
Nyalandu amejibu mapigo hayo leo Jumatatu ikiwa imepita saa kadhaa kwa Dk Kigwangalla kumtuhumu mbunge huyo wa zamani kwamba alitumia madaraka yake vibaya wakati akiwa Wazari wa Maliasili na Utalii katika Serikali iliyopita.
Amesema, "hizi ni njama za makusudi zilizopangwa  kunichafua mara baada ya mimi kukihama Chama Cha Mapinduzi (CCM). Hatua hii imepangwa kwa lengo la kuhakikisha kuwa hakuna kiongozi yeyote wa CCM atakayethubutu ama kudiriki tena kuhama CCM,” amesema Nyalandu.
Nyalandu amedai kuwa Dk Kigwangalla anatumika vibaya kwa kauli za uongo dhidi yake mara baada ya kuteuliwa kushika wadhifa huo hivi karibuni.
Katika kujibu mapigo hayo Nyalandu ametoa hoja sita kuonyesha Dk Kigwangalla ana chuki dhidi yake na amelidanga Bunge kwa tuhuma dhidi yake.
Amesema Dk Kigwangalla amekejeli kuwa Nyalandu alitumia fedha za Serikali kusafiri  nchini Marekani na msanii wa bongo movie Aunt Ezekiel.
“Habari ilikuwa ya kuzushwa  na ilichunguzwa na vyombo vya dola mwaka  2014 na kuthibitika ilitungwa na katika mkutano huo wa Washington DC nilialikwa na  Balozi wa Tanzania, Marekani na nikapewa ruhusa ya maandishi na Serikali kuhutubia mkutano huo kwa siku moja. Wasanii wote walioalikwa, akiwamo Aunt Ezekiel hawakuwa na mwaliko wa wizara ama Serikali, bali waandaji wa kongamano. Na Serikali haikulipa gharama zozote kwao."
Amesema Dk Kigwangalla amelidanganya Bunge kuwa Nyalandu ametumia  helikopta kugombea urais
“Habari hii ni ya uzushi na  waziri atakuwa aidha hana busara ambayo angepaswa kujiridhisha na taarifa kabla ya kuisoma bungeni ama waliomtuma wamemwambia asome  hivyo hivyo. Ukweli ni kuwa  Nyalandu alipokuwa CCM niligombea katika kinyang’anyiro cha urais  na kuomba kuteuliwa ndani ya CCM na alitumia aidha usafiri wa magari au ndege za kawaida kwa kulipa nauli (fixed wings pale ilipobidi), hadi mchakato ulipoisha kama uilivyoisha."
“Miaka yote nikiwa Mbunge wa Singida Kaskazini, nimekuwa nikifanya kampeni za kumalizia kwa njia ya helikopta. Inawezekana Waziri Kigwangalla hajawahi kupanda helikopta katika maisha yake, nimjulishe tu kuwa kwangu huo ni usafiri wa kawaida sana na umesaidia ilipobidi kusaidia kufika baadhi ya maeneo jimboni kwangu wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu 2000, 2005, 2010, na 2015.
Amesema Dk Kigwangalla amezusha kuwa  Nyalandu alitumia vibaya madaraka yake. Amezungumzia suala la Waziri Nyalandu kutotia sahihi tozo mpya zilizopendekezwa na Tanapa
“Jambo ambalo Dk Kigwangalla angepaswa kulijua kabla ya kutoa kauli isiyo sahihi bungeni ni kuwa sakata la tozo za  Tanapa lilijadiliwa bungeni  na Spika Anne Makinda, likiwa limeletwa na Kamati ya Lembeli na kwa kupitia wizara na nililitolea ufafanuzi na likamalizika na GN ilitolewa.”
Akizungumzia vitalu Nyalandu amesema, "inasikitisha sana na inatia aibu kwamba Dk Kigwangalla atalihadaa Bunge kuwa Nyalandu amehusika na kuuza au kugawa  vitalu  na mbaya zaidi kwa njia ya rushwa."
Amesema Sheria ya Wanyamapori inatamka wazi kuwa vitalu vitagawiwa kwa wawindaji kila baada ya miaka mitano  na mara ya mwisho vitalu vilitolewa Januari, 2017 ambapo Nyalandu hakuwa waziri.
"Pia kabla ya hapo vitalu viligawiwa mwaka  2013. Nyalandu hakuwa Waziri."
“Hii ni aibu sana natumaini kwa Dk  Kigwangalla na wanaomtuma wangetamani sana miaka ibadilike ili isomeke Waziri Nyalandu,” amesema.
Nyalandu amesema Dk  Kigwangalla amedai kuwa yeye (Nyalandu) alikuwa anafanyia kazi katika chumba maalumu katika hoteli ya Serena.
“Naomba athibitishe ni chumba namba ngapi na wahusika wa hoteli pia wathibitishe kama waziri, nilifanya kazi katika ofisi yangu iliyopo Wizara ya Maliasili na Utalii. Kigwangalla pia akumbuke mimi nilikuwa mteule wa Rais ambaye alikuwa na vyombo vya kumsaidia kusimamia mawaziri."
Mwisho Nyalandu amesema  mbwembwe hizi na kusingiziwa kunakofanywa kwa makusudi baada ya  yeye kuhama CCM  ni aibu kwa Taifa  na ni matumizi mabaya ya madaraka.

Serikali yasema Mbowe anapotosha


Dodoma. Serikali imemjia juu Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kutokana na kauli yake kuwa Rais John Magufuli amekuwa akipendelea baadhi ya kanda katika uteuzi wake.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Ajira na Watu wenye Ulemavu, Jenister Mhagama leo Jumatatu jioni amesema Mbowe anapotosha na kumtaka aache kuingilia madaraka ya Rais.
Wakati akichangia Mpango wa Taifa wa Maendeleo wa 2018/2019, Ijumaa iliyopita Mbowe alienda mbali na kudai anaweza kuleta uthibitisho kama Bunge litamkata kufanya hivyo.
“Mumwambie bwana mkubwa unapoamua mambo mengine tenda haki pande zote. Lakini unapokuwa haki hiyo unaipeleka mahali fulani na unakandamiza upande mmoja unawanyima haki”
Mbowe alitolea mfano wa teuzi mbalimbali alizozifanya Rais Magufuli tangu aingie madarakani mwaka 2015, akisema hazikugawanywa kwa usawa wa mikoa kama utamaduni uliokuwepo awamu zilizopita.
Hata hivyo, leo Jumatatu jioni Jenister amesema Ibara ya 36 (1) (2)(3)(4) imempa Rais madaraka ya kuanzisha na kufuta ya nafasi za mbalimbali kwa utumishi na haijasema atazingatiwa usawa wa kanda.
“Ibara hiyo haisemi kuwa Rais wakati atakapokuwa anafanya uteuzi eti aangalie ukanda. Haisemi hivyo Ibara hiyo haisemi anavyoandaa uteuzi aaangalie makabila mbalimbali,”amesema Mhagama.
“Unasimamaje ndani ya Bunge kuhoji madaraka ambayo Rais amepewa kwa mujibu wa Katiba? Alihoji Mhagama na kutoa mifano ya teuzi tatu zilizofanywa na Rais kutoka mikoa ya Kaskazini. 
“Ameteuliwa Aggrey Mwandry kutoka Siha kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora na anafanya kazi vizuri sana. Ameteuliwa Alexander Mnyeti kuwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara,”amesema na kuongeza
“Ameteuliwa Anna Kilango kutoka Same. Nina orodha ndefu lakini uteuzi huo unafuata madaraka ya kikatiba. Niwaombe sana wabunge tusiingile madaraka ya Rais aliyopewa kwa mujibu wa Katiba.”
Amesema Rais amekuwa akifanya teuzi mbalimbali kwa utashi wa hali ya juu na anateua watu wa kubeba dhamana ya kumsaidia kuongoza kwa niaba yake pasipo upendeleo.

Wanadiplomasia Saudia wadadisi vita vya ufisadi

Picha zinazo waonyesha Mfalme wa Saudi Arabia Salman bin Abdulaziz Al Saud na Mrithi wa Ufalme Mohammed bin Salman, huko Riyadh, Saudi Arabia, Nov. 9, 2017.
Wiki moja baada ya zoezi la kukamatwa kwa baadhi ya wana wa mfalme wa Saudi Arabia ambao ni matajiri wakubwa na wafanyabiashara ni kitendo ambacho hakijawahi kutokea katika historia ya nchi hiyo.
Serikali mbalimbali duniani na wawekezaji bado wanajaribu kujibu maswali ya msingi juu ya zoezi hilo la kamatakamata ambalo serikali ya Saudi Arabia inaeleza kuwa ni vita dhidi ya ufisadi inayoendeshwa na aliyeteuliwa kuwa mrithi wa mfalme wa nchi hiyo.

Swali liliopo hivi sasa ni iwapo Mohammad bin Salman mwenye umri wa miaka 32 ameanza kujiandaa kuchukua madaraka ili kuhakikisha kuwa urithi wake hautokabiliwa na matatizo wakati baba yake ambaye ni mgonjwa atakapokufa?
Au yeye ni kama vile anavyojielezea, ni mwanamabadiliko aliyedhamiria kuibadilisha falme hiyo kutokana na misimamo mikali ya kiutawala ambayo ilikuwa inashinikizwa na vitengo mbalimbali vya familia hiyo pana ya kifalme.
Habari zilizoenea ambazo hazikuthibitishwa katika mji mkuu wa Saudia zinaeleza kuwa kamatakamata hiyo haijamalizika na huenda kukawa na watu zaidi watakao kamatwa kama ilivyotabiriwa na wanadiplomasia wakigeni walioko nchini Saudi. Wanadiplomasia hao wameshtushwa na ukamataji huo.
Hata hivyo vijana wa kipato cha kati Saudia, ambao wamekatishwa tamaa na kuwepo rushwa na mtizamo finyu ya utawala huo wa kifalme, wanashangilia kitendo cha mrithi wa ufalme kuendesha operesheni hiyo.
Kwa upande wao wawekezaji wanachukua tahadhari , wakihofia kuwa Mohammad bin Salman ameuma kile ambacho hawezi kukitafuna.
Kwa muda mrefu ikiangaliwa kama ni sehemu yenye utulivu kufanya biashara, hatua za kutumia nguvu zilizojitokeza zimeshuhudia takriban watu 500 wakikamatwa, akiwemo mtu tajiri kuliko wote nchini humo, Mwana wa mfalme Waleed bin Talal.
Talal ni bilionea mfanyabiashara ambaye ni mshirika wa umiliki wa hoteli za Four Sessions na hivi karibuni alikuwa mwekezaji mkuu wa himaya ya vyombo vya habari ulimwenguni ya Rupert Murdoch. Alikamatwa akiwa katika kambi yake ya kifahari iliyoko jangwani.

Viongozi wa kijeshi maarufu pia walikumbwa na wimbi hilo la ukamataji, akiwemo mwana wa mfalme Miteb bin Abdullah, waziri wa jeshi maalum la askari 100,000 ambaye ni mtoto wa marehemu Mfalme Abdullah, ambaye kifo chake miaka miwili iliyopita kilipelekea Mohammed bin Salman kuchaguliwa kuwa mrithi wa mfalme na mtawala wa hivi sasa mwenye umri wa miaka 81.

Chama cha Wamiliki wa Mabasi Yaendayo Mikoani (TABOA)


Chama cha Wamiliki wa Mabasi Yaendayo Mikoani (TABOA) na Umoja wa Wasafirishaji Abiria Jijini Dar es Salaam (UWADAR) wamekanusha taarifa inayosambazwa kwenye mitandao kuwa Novemba 14 mwaka huu watakuwa na mgomo wa kusitisha huduma za usafirishaji.

Hayo yamesemwa leo Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa UWADAR, Kismat Dhalla wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kwa ajili ya kukanusha suala hilo.

Dhalla amesema kuwa taarifa hiyo iliandaliwa na vyama hivyo lakini ilishatolewa katika vyombo vya habari siku nyingi zilizopita hivyo kuna baadhi ya watu wameamua kuisambaza upya bila ridhaa ya wahusika.

“Ni kweli ile taarifa ni ya kwetu lakini tulishaitoa siku nyingi na mgomo huo haukufanyika kwa kuwa tuliahidiwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (SUMATRA) kuwa itayafanyia kazi madai yetu”, alisema Dhalla.

Dhalla ameongeza kuwa tayari SUMATRA imeandaa mkutano na wadau ambao utafanyika mnamo Novemba 15 mwaka huu kwa ajili ya kujadili kuhusiana na baadhi ya Kanuni zilizotungwa katika Sheria hiyo ya SUMATRA.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Huduma za Sheria wa SUMATRA, Tumaini Silaa amesema kuwa lengo la SUMATRA ni kuhakikisha kuwa usafiri unapatikana muda wote na unamfaidisha msafiri na msafirishaji ndio maana mamlaka hiyo inajitahidi kuyamaliza malalamiko ya TABOA na UWADAR pindi yanapojitokeza.

“Sisi kama SUMATRA tunaona kuwa hakuna mgogoro kati yetu na wadau wa usafiri isipokuwa ni kutoelewa Kanuni ambazo zimepitishwa na Mhe. Waziri mwenye dhamana hivyo tutakapokutana katika mkutano huo tutaeleweshana kwani tunaamini kuwa kanuni zilizoandaliwa ziko vizuri”, alisema Bw.Silaa.

Amefafanua kuwa baadhi ya watu bado wanachanganya Kanuni za mwaka 2007 ambazo zimefutwa na kanuni hizi mpya lakini wanatakiwa kufahamu kuwa kanuni mpya zimeweka usawa kwa upande wa msafirishaji, abiria, dereva na kondakta.

Pia, kanuni hizo mpya bado hazijaanza kutumika mpaka pale SUMATRA itakapotoa elimu ili kila mmoja awe na uelewa na Sheria na Kanuni zake.



MCHANGO WA ASASI ZA KIRAIA KWENYE RASILIMALI MADINI, MAFUTA NA GESI


                    Mkurugenzi wa Taasisi ya Demokrasia na Utawala Bora Vijijini ADLG iliyopo Jijini Mwanza, Jimmy Luhende akichangia mada kwenye Mkutano wa Sekta ya Uziduaji 2017 uliofanyika Mjini Dodoma.

Novemba 02-03, 2017 ulifanyika Mkutano wa Sekta ya Uziduaji (Madini, Mafuta na Gesi) Mjini Dodoma ambapo miongoni mwa maazimio kwenye mkutano huo ni Asasi za Kiraia kushiriki ipasavyo katika kuhakikisha Taifa linanufaika na Rasilimali zake.

Ungana na BMG kujua yaliyojiri kwenye mkutano huo ulioandaliwa na muungano wa Asasi za Kiraia zinazoangazia masuala ya Utawala Bora kwenye sekta ya Uziduaji nchini HakiRasilimali. Tazama HAPA ufunguzi wa mkutano huo. Tazama HAPA hafla ya usiku baada ya mkutano huo.Mwanasheria Veronica Zano (kushoto) kutoka Zimbabwe akichangia mada kwenye mkutano huo. Kulia ni Mkurugenzi wa Taasisi ya Demokrasia na Utawala Bora Vijijini ADLG iliyopo Jijini Mwanza.

MAKUMBUSHO YA TAIFA YAANDAA ONESHO LA PICHA ZILIZOPIGWA MIAKA ILIYOPITA

Makumbusho ya Taifa kwa kushirikiana na Raia wa Denmark, Jesper Kirkanes wameandaa onesho la picha mbalimbali za maisha ya Watanzania zilizopigwa miaka 50 iliyopita.

Akizungumza na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam, Profesa Audax Mabula amesema onesho hilo ni muhimu kwa watanzania kujikumbusha maisha ya miaka 50 iliyopita.

Amesema kuwa onesho hilo litafanyika Novemba 16 katika viwanja vya makumbusho ya Taifa ambalo litafunguliwa na Balozi wa Denmark nchini, Einar Jensen.Profesa Mabula amesema kuwa katika siku ya onesho hilo hakutakuwa na kiingilio katika kuangalia picha hizo pamoja na picha zingine zilizomo katika makumbusho ya taifa.

Aidha amesema kuwa onesho la picha hizo ni pamoja maisha na kazi zilizokuwa zinafanywa watanzania ambapo kwa sasa watanzania wanatakiwa kujua historia ya maisha ya miaka 50 iliyopita.

Amesema wakati uliopo wa sera ya viwanda ni funzo kutoka kwa watanzania ambao waliishi kwa kuweza kuendesha maisha yao kwa kujitengenezea vitu ambavyo walikuwa wakihitaji.Profesa Mabula amesema kuwa picha hizo zilipigwa mwanzoni mwa mwaka 1968 mpaka mwaka 1977 na zilipigwa na Raia wa Denmark, Jesper Kirkanes ambaye alikuja nchini kwa kazi hiyo.
Mkurugenzi Mkuu wa Makumbusho ya Taifa , Audax Mabula akizungumza na waandishi habari juu ya onesho la picha zilizopigwa miaka 50 iliyopita litakalofanyika Novemba 16 mwaka huu katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa.
Raia wa Denmark, Jesper Kirkanes ambaye alipiga picha za maisha ya watanzania miaka 50 iliypita akizungumza na waandishi habari juu ya maana picha hizo leo jijini Dar es Salaam.

SHEKH NURDEEN KISHK AISOGEZA JAMII KARIBU KWA KUFUNGUA KISHK TV ONLINE


Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Mkurugenzi wa taasisi ya AL Hikma Nurdeen Kishki amesema kuwa kwa sasa waumini wake pamoja na jamii inayozungumza  wanaweza kupata mawaida yake, hadhara, hotuba  na hadithi mbalimbali kupitia akaunti zake za mitandao ya kijamii.

Shekh Kishk ameweka wazi akaunti zake za mitandao ya kijamii facebook, twitter , instagram sambamba na kufungua TV ya Online itakayokwenda kwa jina la Kishki Online Tv.

 Akizungumza wakati wa utambulisho wa akaunti hizo, Shekh Kishk amesema kuwa jamii iliyokuwa inamfuatilia kwa kipindi kirefu walikuwa wanalalamika kwa  kukosa mawaidha yake ambapo kwa kiasi kikubwa kinazidi kuwasogeza karibu nae.

“ Jamii inayonifuatilia ilikuwa inalalamika kila wakati wakisema kwanin Shekh haufungui mitandao ya kijamii na wengine walitaka kunifungulia ila sikuwa tayati, ila kuna baadhi ya watu walikuwa wanatumia mgongo wangu kufungua akaunti za facebook kwa kutumia jina langu na wakifanikiwa kwani walipata watu wengi kwa kipindi kifupi,”amesema Shekh Kishk.

Shekh Kishk amesema kuwa,  katika akaunti hizo watu wataweza kupata darasa mbalimbali za hadithi, mawaidha, hotuba, hadithi na kutakuwa na usomaji wa Quran katika sauti saba, mbali na hilo kutakuwa na video za mawaidha na hotuba ambazo anazitoa wakati  akiwa katika ziara za mikoani na hata nje ya nchi kwani amekuwa anatembea na watu wa habari kila mahala.

Amewatoa hofu watu kuwa matumizi ya mitandao ya kijamii ndiyo inaweza kusababisha kufanya maovu ila ukiamua kuitumia vizuri inaweza kukuletea faida.

Kwa upande wa katibu wake anayejulikana kwa jina la Masawe, alisema kuwa kwa kipindi kirefu alikuwa anasumbuliwa na watu mbalimbali kwa nini Shekh Kishk hafungui akaunti za kijamii  ila baad aya kukaa naye na kushauriana tukaamua kufungua na katika muda wa saa 24 ameweza kupata marafiki 5000 na kuamua kuwa na page ya facebook.
 Shekhe Nurdeen Kishk akiwaonyesha waandishi wa habari jina analotumia katika mtandao wa kijamiiya facebook, twitter na instagram sambamba na Kishk Online Tv leo Jijini Dar es salaam.
 Shekh Nurdeen Kishk akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake baada ya kufungua akaunti za mitandao ya kijamii facebook, twitter na instagram sambamba na Kishk Online Tv zilizotambulishwa rasmi leo.
Katibu wa Shekh Nurdeen Kishk akizungumza na waandishi kuhusu namna jamii ilivyokuwa inatamani kuona Shekh anakuwa na akaunti katika mitandao ya kijamii.

Wafanyakazi HESLB waaswa kuwa wabunifu

 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe akiongea na menejimenti ya Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi za HESLB jijini Dar es Salaam leo (Jumatatu, Nov 13, 2017). Keshoto ni Mkurugenzi wa Elimu ya Juu kutoka Wizara ya Elimu Prof. Sylvia Temu na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru. (Picha na HESLB) 
 Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe (katikati) akimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul-Razaq Badru wakati wa ziara yake ya kikazi katika Ofisi za HESLB jijini Dar es Salaam leo (Jumatatu, Nov 13, 2017). Keshoto ni Mkurugenzi wa Elimu ya Juu kutoka Wizara ya Elimu Prof. Sylvia Temu. (Picha na HESLB) 
Baadhi ya wajumbe wa menejimenti ya Bodi ya Mikopo katika mkutano na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe ambaye amefanya ziara yake ya kikazi katika Ofisi za HESLB jijini Dar es Salaam leo (Jumatatu, Nov 13, 2017). (Picha na HESLB) 

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe amewataka wafanyakazi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kuongeza ubunifu ili kuondokana na changamoto wanazokutana nazo.

Prof. Mdoe amesema hayo leo (Jumatatu, Novemba 13, 2017) alipokua akiongea na Menejimenti ya HESLB katika ziara aliyoifanya katika makao makuu ya HESLB jijini Dar es Salaam.

“Pamoja na mafanikio mnayoyapata hasa katika ukusanyaji wa mikopo lakini bado kuna changamoto…zikiwemo za malalamiko ya vigezo vya utoaji mikopo ambavyo mnahitaji kuwa wabunifu kwa kuwashirikisha wadau,” amesema kiongozi huyo katika ziara yake ya kikazi.

Kwa mujibu wa Prof. Mdoe, nia ya Serikali ni kuona malalamiko yote ya wadau yanatafutiwa ufumbuzi kwa haraka, na ili hilo litimizwe ni muhimu kwa wafayakazi wa taasisi za umma kuwa wabunifu zaidi.

Awali akimkaribisha Naibu Katibu Mkuu huyo katika mkutano huo, Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Bw. Abdul- Razaq Badru alisema taasisi yake imejipanga kuhakikisha huduma inazotoa zinaakisi matarajio ya Serikali na kwamba mkazo umewekwa kwenye kuongeza kasi ya ukusanyaji mikopo na kushirikisha wadau katika kuboresha vigezo vya utoaji mikopo kwa miaka ijayo.

“Katika mwaka 2016/2017 pekee, tulikusanya zaidi ya Tshs 116 bilioni na wastani wa makusanyo yetu kwa mwezi kwa sasa ni Tsh 12 bilioni. Tunataka kufikisha Tsh 15 bilioni kwa mwezi ifikapo mwakani,” amesema Bw. Badru katika mkutano huo uliohidhuriwa pia na Mkurugenzi wa Elimu ya Juu kutoka Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Sylvia Temu.

Wakati huohuo, HESLB imewakumbusha wanafunzi wote ambao hawajaridhika na mikopo waliyopangiwa au kukosa, kuhakikisha kuwa watatemebelea mtandao wa Bodi (olas.heslb.go.tz) wanakata rufaa na kuwasilisha kwa maafisa mikopo waliopo kwenye vyuo vyao kabla ya tarehe 19 Novemba mwaka huu.

Ufafanuzi huo unafuatia baadhi ya wanafunzi walikosa mikopo au kutoridhika na mikopo waliyopangiwa kufika katika ofisi za HESLB jijini Dar es Salaam na zile za kanda zilizopo Dodoma, Arusha, Mwanza na Zanzibar.

Mwishoni mwa wiki, HESLB ilitangaza kufungua dirisha la rufaa ambalo litafungwa Novemba 19, 2017 ili kuwapa fursa waombaji wote ambao hawajaridhika na upangaji wa mikopo kuwasilisha rufaa kupitia vyuo walivyopata udahili. Kwa muibu wa HESLB, lengo ni kutoa orodha ya waombaji waliofanikiwa katika rufaa zao ifikapo Novemba 30, 2017.

Maelezo ya kina kuhusu utaratibu wa kuwasilisha rufaa yatatolewa kupitia tovuti ya Bodi (www.heslb.go.tz). 

TUME YA UCHAGUZI YAKUTANA NA VYAMA VYA SIASA KUELEKEA UCHAGUZI MDOGO

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Semistocles Kaijage akizungumza na viongozi wa vyama vya siasa kwenye mkutano wa Tume na vyama hivyo ikiwa ni maandalizi ya uchaguzi mdogo wa Novemba 26, 2017. Mkutano huo umeliofanyika leo jijini Dar es Salaam leo.Kushoto ni Makamu Mwenyekiti Jaji  Mst. Hamid Mahmoud Hamid na kulia ni Mkurugenzi wa Uchaguzi Kailima Ramadhani.
Mkurugenzi wa Uchaguzi, Kailima Ramadhani akitoa mada kwa viongozi wa vyama vya siasa wakati Tume ilipokutana na vyama vya siasa jijini Dar es Salaam leo. 
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Semistocles Kaijage (wa tatu kulia) akiwa meza kuu na Makamu Mwenyekiti Jaji Mst. Hamid Mahmoud Hamid( wa tatu kushoto), Mkurugenzi wa Uchaguzi Kailima Ramadhani )wa pili kulia), Makamishna wa NEC Jaji Mst. Marry Longway na Asina Omari na kulia ni Mwakilishi wa Mkuuu wa Jeshi la Polisi (IGP), kwenye mkutano wa Tume na vyama vya siasa uliofanyika Dar es Salaam jijini leo.
Baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wakifuatilia hotuba ya Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Semistocles Kaijage kwenye mkutano wa Tume na vyama vya siasa uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Kaimu Mwenyekiti wa Chama cha ACT-Wazalendo Yeremia Maganja akichangia mada kwenye mkutano wa Tume na vyama vya siasa uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
Mkurugenzi wa Uchaguzi Kailima Ramadhani akizungumza na waandishi wa Habari baada ya ufunguzi wa mkutano wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na vyama vya siasa uliofanyika jijini Dar es Salaam leo.
 Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Semistocles Kaijage   (kushoto) akisalimiana na Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Kanda ya Pwani Casimir mabina.Katikati ni Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha UDP Saumu Rashid. 
Picha na Hussein Makame-NEC

Hussein Makame-NEC
Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Semistolces Kaijage amevitaka vyama vya siasa kufanya kampeni kwa kuzingatia maadili ya Uchaguzi.

Jaji Kaijage ameyasema hayo wakati akifungua mkutano wa NEC na vyama vya siasa uliofanyika jijini Dar es Salaam leo kuelekea Uchaguzi mdogo wa madiniwa.

Alisema iwapo ukiukwaji au uvunjaji wa Maadili  hayo utatokea, Chama au Mgombea awasilishe malalamiko hayo mbele ya Kamati husika ili ishughulikiwe kisheria.

Aliwakumbusha kuwa kwa mujibu wa kifungu cha 53 cha Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292 Tume inayo mamlaka ya kuruhusu kuwepo kwa Kampeni za Uchaguzi katika maeneo ya Uchaguzi na siyo Mikutano ya Vyama vya Siasa. 

Hivyo, kampeni hizo zifanyike kwenye Kata husika na inategemewa kuwa Mikutano ya Kampeni italenga kuwashawishi, kwa namna ya kistaarabu, wananchi wa Kata husika ili wamchague Mgombea anayefanyiwa kampeni. 

” Kwa mujibu wa kipengele cha 2.1. (c) cha Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015 tunategemea kila Chama cha Siasa kiendelee kufanya Kampeni kwa mujibu wa ratiba. Kampeni zote zinatakiwa kuanza saa 2:00 asubuhi hadi saa 12:00 jioni” alisema Jaji Kaijage. 

Aliongez kuwa kwa kuzingatia Maadili ya Uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ya mwaka 2015, Tume imekwisha kutoa ushauri kwa Viongozi wa Mikoa na Wilaya ili katika kipindi hiki cha Uchaguzi wahakikishe wanazingatia wajibu wao na ukomo wa madaraka yao katika shughuli za Uchaguzi kuanzia kipindi cha Kampeni hadi kutangazwa kwa Matokeo. 

 Naye Mkurugenzi wa Uchaguzi kailima Ramadhani aliaviomba Vyama vya Siasa kuwahimiza wanachama na wapenzi wao walioandikishwa kuwa Wapiga Kura wajitokeze  Siku ya Uchaguzi kwenda Kupiga Kura zao bila hofu yoyote  kuhusu usalama wao.

“Ni imani ya Tume kuwa Viongozi wa Vyama vya Siasa mtakuwa chachu ya kuwaongoza na kuwaelekeza wanachama, wafuasi na mashabiki wenu katika kushiriki uchaguzi kwa amani na utulivu’ alisema Kailima.

Uchaguzi Mdogo wa madiwani katika kata 43 za Tanzania Bara, unatarajiwa kufanyika tarehe 26 Novemba, 2017 ambapo wapiga kura 333,309 wanategemewa kupiga kura siku ya uchaguzi huo.

SERIKALI YAREJESHA UMILIKI HALALI WA KIWANJA KILICHOUZWA KWA HATI ZA KUGHUSHI



Frank Mvungi- Maelezo, Dodoma

Serikali imerejesha hati ya  Kiwanja Namba 9331 kilichopo kitalu namba 91 Msalato Dodoma kwa mmiliki wake halisi Bw. Sagaf Omari na Bi Madina Hassan ambao ni wamiliki halali wa kiwanja hicho kilichouzwa kwa Bw. Lucas Mlay  wa Jijini Dar es Salaam kwa shilingi milioni 35  kwa njia zisizo halali.


Akizungumza wakati akimkabidhi hati hiyo Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi amesema kuwa kiwanja hicho  chenye ukubwa wa takribani hekta mbili na nusu kiliuzwa bila mmiliki halali wa kiwanja hicho kuwa na taarifa kupitia kwa wanasheria wasio waaminifu waliosaidia kutaka kufanikisha wizi wa kiwanja hicho.



“Niwatahadharishe Mawakili wote na wanasheria ambao wanashirikiana na watu wasio waaminifu kutaka kudhulumu viwanja vya wananchi kuwa Serikali ya Awamu ya Tano itawachukuliwa hatua kali za kisheria na kwa kuanza tutaanza na hawa mawakili waliofanikisha mchezo huu wakumdhulumu mama huyu na mume wake kiwanja chao wanachomiliki kihalali” Alisisitiza Lukuvi



Akifafanua Waziri Lukuvi amesema kuwa Wizara yake imejiridhisha kuwa nyaraka zilizowasilishwa ili kubadilisha umiliki wa kiwanja hicho ni za kughushi na  wamiliki halali wa kiwanja hawakuwa na taarifa kuhusu kuuzwa kwa kiwanja chao hadi walipopata taarifa kwa majirani na kuamua kuchukua hatua kwa kuwasilisha malalamiko yao katika Ofisi yake.



“Nimechukua hatua na tayari yule mwanasheria aliyehusika katika kughushi nyaraka za kiwanja hiki na kukiuza ameshakabidhiwa kwa vyombo vya dola kwa hatua zaidi hivyo ni vyema watu wote wenye nia yakudhulumu viwanja vya wananchi masikini wakaacha tabia hiyo mara moja kwani Serikali ya Awamu ya Tano itawachukulia hatua kali mara moja ili kukomesha tabia hii ”Alisisitiza Mhe. Lukuvi



Kwa upande wake  Bi. Madina Hassan akipokea hati ya Kiwanja hicho amemshukuru  Waziri Lukuvi kwa hatua anazochukua katika kuhakikisha wanyonge wanapata haki hasa pale panapojitokeza watu wanaojaribu kudhulumu viwanja vya wananchi masikini .



“Kwa kweli naishukuru Serikali ya Awamu ya Tano jinsi inavyotusaidia wanyonge ili tupate haki zetu hasa katika sekta hii ya ardhi nawaombea kwa Mungu ili awalinde Viongozi hawa” alisisitiza bi Madina.



Kwa upande wake mnunuzi wa Kiwanja hicho Bw. Lucas  Mlay amesema kuwa hakuwa na uelewa wa kutosha kuhusu masuala ya sheria na hakutambua kuwa hati za kiwanja hicho zilikuwa zimeghushiwa na kuongeza kuwa angetambua hilo asingelipa zaidi milioni 35 ili kununua kiwanja hicho.



Naye Msajili wa  Hati wa Wizara hiyo Bw. Geofrey William amesema kuwa ni vyema wananchi hasa katika Mkoa wa Dodoma wakachukua hatua kujiepusha na utapeli wa viwanja unaoendeshwa na baadhi ya watu hasa kwa viwanja ambavyo havijaendelezwa kwa muda mrefu.



Aliongeza kuwa kumekuwa na wimbi la watu kuwasilisha maombi ya kupotelewa na hati ili kufanya mchakato wa kubadili umiliki wa viwanja ikiwa ni sehemu ya mbinu zinazotumiwa na matapeli.






Tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani imekuwa ikichukua hatua mbalimbali kukomesha vitendo vya kuwazulumu wananchi masikini viwanja, mashamba  na maeneo ya umma ikiwa ni moja ya mikakati yake kuhakikisha kuwa wanachi wote wanapata haki sawa bila kujali hali ya kipato au wadhifa.

JUKWAA LA AFYA LA DICOTA LAFANA, GREENBELT, MARYLAND


Meza kuu kutoka kushoto ni Balozi Liberata Mulamula, Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Canada Mhe. Wilson Masilingi, Naibu Waziri wa afya Zanzibar, Mhe. Harusi Said Suleiman,Mkuu wa kitengo cha Diaspora Wizara ya mambo ya nje na ushirikiano Afrika Mashariki, Balozi Anisa  Mbega, Bi.Adila Hilal Vuai mkurugenzi wa Idara ya ushirikiano wa kimataifa na uratibu wa wazanzibari wanaoishi nje ya nchi (Diaspora) !, Bwn. Assenga kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani na Dr. Ali Salum Ali Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar. wakifuatilia jukwaa la afya lililoandaliwa na DICOTA katika kuwakutanisha wadau wote nje na ndani ya Marekani sekta ya afya kuwatambua na kuthamini mchango mkubwa wanaotoa katika sekta hiyo nchini Tanzania. Jukwaa la afya lilifanyika siku ya Jumamosi Novemba 11, 2017 Martins Crosswind Greenbelt, Maryland nchini Marekani. Picha naVijimambo Blog na Kwanza Production
Bwn. Lunda Asmani akiwakaribisha wadau wote na kufungua jukwaa la afya.
Balozi wa Tanzania nchini Marekani na Mexico akisoma hotuba yake kwenye kongamano la Afya lililofanyika siku ya Jumamosi Nov 11, 2017 Greenbelt, Maryaland nchini Marekani. Katika hotuba hiyo aliwashukuru DICOTA kwa kuandaa jukwaa hilo la wadau wa afya kwa kuthamini kazi kubwa inayofanywa na wadau hao na jitihada binafsi zinazofanywa kwa kusaidia ndungu zao nyumbani Tanzania pia alisema Rais Dkt John Pombe Magufuli anatambua na kuthamini mchango mkubwa unaofanywa na Diaspora kwa nchi yao.
Balozi wa African Union nchini Marekani, Mhe.Arikana Chihombori Quao akichangia kwenye jukwaa hilo na kueleza changamoto nyingi nchi za Afrika inazopata katika sekta hiyo kutokana na miundo mbinu kuwa duni na sababu kubwa inachangiwa na wakoloni walivyoligawa bara la Afrika na kuwa nchi mbalimbali kwa kuogopa nguvu ya Afrika na utajiri wake usije ukaongoza Dunia.
Naibu Waziri wa Afya Zanzibar, Mhe. Harusi Said Suleiman akiwashukuru Diaspora kwa mchango mkubwa kwa sekta ya afya Zanzibar na baadae kutoa salamu za Rais wa Zanzibar Mhe. Dr Ali Mohamed Shein kwa kutoa shukurani zake na kuthamini mchango mkubwa wa Diaspora hasa katika sekta ya Afya.
Balozi Anisa Mbega mkuu wa idara ya Diaspora Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akishiriki jukwaa la Afya kwa kuwapongeza DICOTA kwa kuandaa jukwaa hilo na kuwakutanisha wadau wa afya na Serikali inathamini na kutambua mchango mkubwa unaofanywa na Diaspora.
Balozi Liberata Mulamula akitoa shukurani zake kwa DICOTA kwa kuandaa jukwaa la afya na baadae kutoa mfano wa mtu akiwekewa fedha na afya bora yeye atakimbilia kwenye fedha kwa sababu hatambui umuhimu wa afya njema ni zaidi ya fedha kwa maana kwamba binadamu wengi hawaelewi umuhimu wa afya lazima tutambue hilo huku akitolea mfano mwingine wa nyani unapo mwekea fedha na ndizi yeye atachangau ndizi kwa sababu anajua bila ndizi maisha yake yapo hatarini. 
Dr. Mary Banda kutoka Jambo Tanzania akielezea jinsi alivyotumia elimu yake kwa kuelekeza nguvu yake kusaidia sekta ya afya mkoa wa Kagera.

Bi. Christine Lasway kutoka MyAfyaPal akielezea umuhimu wa afya na jinsi anavyoelekeza nguvu zake katika kusaidia sekta ya afya nchini Tanzania.
Kwa picha zaidi bofya soma zaidi


Bi.Tausi Suedi kutoka Childbirth Survival Tanzania akielezea jinsi alivyojikita katika kusaidia kuokoa maisha ya mtoto hasa wakati wa uzazi Tanzania kwa kutoa elimu kwa wakunga na wazazi kabla na baada ya kujifungua ikiwemo kwapelekea mahitaji muhimu kabla ya kujifungua.
Dr. Secelela Malecela kutoka Janet Weir Children's Hospital akieleza anavyoguswa katika kuelekeza nguvu zake katika sekta hiyo Dodoma.

Bi. Adila Hilal Vuai mkurugenzi wa Idara ya ushirikiano wa kimataifa na uratibu wa wazanzibari wanaoishi nje ya nchi (Diaspora) akitoa shukurani kwa niaba ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa jitihada za Diaspora katika sekta ya afya Zanzibar na kuwapongeza DICOTA kwa kuandaa jukwaa la Afya na kuwaasa kutumia lugha ya Kiswahili katika kuendeleza na kuthamini utamaduni wetu.

Dr. Frank Mimja akielezea umuhimu wa kusaidia sekta ya afya Tanzania na jitihada anazofanya kwa kupeleka madaktari Tanzania na kuwaelekeza wadau waliohudhuria jukwaa la Afya njia iliyosahihi kupitia katika kutimiza ndoto na azma yako ya kusaidia ndugu zetu Tanzania.

Kutoka kushoto ni Bwn. Lunda Asmani DICOTA, Bi. Adila Hilal Vuai kutoka Ofisi ya Rais Zanzibar na Dr. Ali Salum Ali Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar.

Juu na chini ni wadau wa jukwaa la afya wakifuatilia jukwaa hilo wakati likiendelea.
Picha juu na chini ni wadau wa afya wakizungumzia na kubadilishana mawazo katika kuweka nguvu ya pamoja katika kusaidia sekta ya afya Tanzania.
Juu na chini ni picha za pamoja na wageni waheshimiwa,
Juu na chini ni mazungumuzo na wageni waheshimiwa.

Mahojiano yaliyofanywa na kwanza Production.