Saturday, October 14

RAIS DKT MAGUFULI AONGOZA SHEREHE ZA KUZIMA MWENYE, NYERERE DAY NA WIKI YA VIJANA ZANZIBAR LEO

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali haitafuta mbio za Mwenge wa Uhuru kwa kuwa ni alama ya Uhuru na Utaifa wa nchi na kwamba unatoa mchango mkubwa katika kuchochea maendeleo, kuwaunganisha Watanzania na kuimarisha Muungano.

Mhe. Rais Magufuli amesema hayo leo tarehe 14 Oktoba, 2017 katika sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, kumbukumbu ya Baba wa Taifa Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere na Wiki ya Vijana zilizofanyika kitaifa katika uwanja wa Amaan uliopo Mjini Magharibi, Zanzibar.

Pamoja na kauli hiyo Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zitaendeleza mbio za mwenge wa uhuru na kuutetea Muungano kwa nguvu zote. “Kauli mbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka huu inasema Shiriki Kukuza Uchumi wa Viwanda kwa Maendeleo ya Nchi yetu. Nimefarijika zaidi kusikia kuwa katika Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu jumla ya viwanda 148 vimezinduliwa, viwanda hivyo vimejengwa kwa gharama ya Shilingi Bilioni 468.46 na vinatarajiwa kuzalishaji ajira 13,370.

Hii ndio sababu tumekuwa tukihimiza ujenzi wa viwanda na hizi ni baadhi ya faida za Mwenge” amesema Mhe. Rais Magufuli. Kuhusu Kumbukumbu ya Mwl. Nyerere, Mhe. Rais Magufuli amewataka Watanzania wote kuendelea kumuenzi Baba wa Taifa kwa kuwa wazalendo, kuthamini utu na usawa wa binadamu na muhimu zaidi kujitathimini ni kwa kiasi gani wanajiepusha na vitendo vinavyoathiri ustawi wa nchi na watu wake kama vile wizi, rushwa, ubinafsi na kukosa uzalendo.

Ametolea mfano wa Mwl. Nyerere ambaye mwanzoni mwa uongozi wake alipochaguliwa kuwa Rais wa Tanzania aliamua kupunguza mshahara wake na kukataa kuongeza mishahara ya wafanyakazi wengine Serikalini kwa maelezo kuwa hawezi kuongeza mishahara ya wachache wakati wananchi wengi ni masikini na hawapati huduma muhimu za afya, elimu na maji.

“Ninaposema hivyo simaanishi kuwa mishahara isiongezwe. La hasha. Ninachosema ni kwamba kabla ya kudai nyongeza ya mishahara ni lazima kwanza kufahamu uwezo wa Serikali, lakini pia tutambue kuwa kuna Watanzania wenzetu wengi tu wanaohitaji kuboreshewa huduma.

Hata hivyo baada ya kukamilisha zoezi la uhakiki wa watumishi hewa na vyeti feki, Serikali imewapandisha vyeo na kuwarekebishia mishahara watumishi 59,967 ambapo kiasi cha Shilingi Bilioni 159.33 zimetengwa kwenye bajeti ya mwaka huu na mishahara mipya itaanza kulipwa kuanzia mwaka huu. Na kwa upande wa Zanzibar kima cha chini cha mshahara kimeongezwa kutoka Shilingi 150,000/- hadi kufikia Shilingi 300,000/-” Amesema Mhe. Rais Magufuli.

Kuhusu vijana Mhe. Rais Magufuli amewataka kuendelea kujielimisha katika Nyanja mbalimbali, kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewapongeza na kuwakabidhi vyeti wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa walioongozwa na Amour Hamad Amour kwa kukimbiza mwenge huo kwa siku 195 katika mikoa yote 31 na Halmashauri 195, ambapo jumla ya miradi 1,512 yenye thamani ya jumla ya Shilingi Trilioni 1.1 imepitiwa. Na pia ameahidi kuchukua hatua dhidi ya wote waliohusika kusababisha dosari katika miradi 19 ambayo viongozi wa mwenge wamebaini.

Sherehe hizo zimehudhuriwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Ali Mohamed Shein, Makama wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Seif Ali Idd, Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Janeth Magufuli, Mke wa Rais wa Zanzibar Mama Mwanamwema Shein na viongozi wengine wa Tanzania Bara na Zanzibar.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea Mwenge wa uhuru wakati wa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo Oktoba 14, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipokea ripoti ya miradi mbalimbali kutoka kwa kiongozi wa mbio za Mwenge wa uhuru wakati wa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo Oktoba 14, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli na Rais wa Zanzibar na Mwnyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Ali Mohamed Shein wakiteta jambo wakati wa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzib
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akihutubia wakati wa sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo Oktoba 14, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akisalimiana na mwakilishi wa familia ya Mwalimu, Mhe. Makongoro Nyerere wakati akiwasili kwenye sherehe za Kilele cha Mbio za Mwenge wa uhuru, Kumbukumbu ya Baba wa Taifa na Wiki ya Vijana katika uwanja wa Amaan mjini Zanzibar leo Oktoba 14, 2017.
Vijana shupavu sita waliokimbiza mwenye wa Uhuru mwaka 2017.

TUMUENZI BABA WA TAIFA KWA KUIGA MAISHA YAKE-MAJALIWA

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewaomba Watanzania waendelee kumuenzi Hayati Baba wa Taifa Mwl. Julius Nyerere kwa kuiga maisha yake na utendaji wake.

Ameyasema hayo leo (Jumamosi, Oktoba 14, 2017) aliposhiriki ibada maalumu ya kumuombea Mwl. Nyerere iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Minara Miwili Zanzibar.

Ibada hiyo ya kumbukumbu ya miaka 18 ya kifo cha Mwl. Nyerere ni sehemu ya maadhimisho ya kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru uliozimwa leo katika mkoa wa Mjini Magharibi visiwani Zanzibar.

Katika Idaba hiyo Waziri Mkuu amewasisitiza wananchi kuhakikisha wanamuenzi Mwl. Nyerere kwa kuendeleza mambo mema yote aliyoyafanya enzi za uhai wake.Awali, Katibu wa Jimbo Katoliki Zanzibar Padri Cosmas Shayo ambaye aliongoza ibada hiyo aliwaomba waamini wamuenzi Mwl. Nyerere kwa kudumisha umoja na mshikamano wa Taifa.

“Hayati Baba wa Taifa Mwl. Nyerere aliwapenda watu wote bila kujali Imani zao wala itikadi zao. Alikuwa mzalendo na alitaka Watanzania waishi maisha bora.”

Padri Shayo aliongeza kuwa tunu za amani na umoja zilikuwa miongoni mwa falsafa kuu ya Mwl. Nyerere, ambapo matokeo yake ni umoja na mshikamano wa Taifa uliopo.

Ibada hiyo ilihudhuriwa na Makamu wa Pili wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Ally Idd, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Bi Jenista Mhagama, Mke wa Waziri Mkuu Mama Mary Majaliwa.

Wengine ni Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto Bi. Mauldine Castico, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira Bw. Anthony Mavunde, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu Walemavu Bi. Stella Alex Ikupa na mwakilishi wa familia ya Mwl. Bw. Makongoro Nyerere.


IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMAMOSI, OKTOBA 14, 2017.         

 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa kwenye ibada maalum ya kumuombea Mwalimu Julius Nyerere, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Minara Miwili Zanzibar (katikati) ni Makamu wa pili wa Rais, Balozi Seif Ali Iddi (kushoto) ni Mke wa Waziri Mkuu mama Marry Majaliwa. Oktoba 14, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na waumini waliyo hudhuria kwenye ibada maalum ya kumuombea Mwalimu Julius Nyerere, iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Minara Miwili Zanzibar, Oktoba 14, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)    

KATIBU MKUU IKULU AONGOZA MATEMBEZI YA KUMUENZI BABA WA TAIFA


Katibu Mkuu Ikulu, Alphayo Kidata akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa Ikulu baada ya matembezi ya kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu J.K Nyerere yaliyoanzia Ikulu mpaka katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es salaam leo ikiwa pia ni siku ya kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru.
Baadhi ya wafanyakazi wa Ikulu wakimsikiliza Katibu Mkuu Alphayo Kidata baada ya matembezi ya kumuenzi Baba wa Taifa Mwalimu J.K Nyerere yaliyoanzia Ikulu mpaka katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es salaam leo ikiwa pia ni siku ya kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru.
Mazoezi ya viungo yakiendelea.

MAADHIMISHO YA KUMBUKUMBU YA NYERERE YAFANA TEMEKE

Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Felix Lyaviva (wa katikati) akiwa sambamba na watumishi wa serikali wa manispaa hiyo na vikundi vya mazoezi ya Jogging katika maadhimisho ya kumbukumbu ya Hayati Mwalim Julius Nyerere leo uwanja wa Taifa  Jijini  Dar es salaam.

Katika kuadhimisha siku ya kumbumbuku ya hayati Baba wa Taifa Mwl; Julius Kambarage Nyerere, Wilaya ya Temeke yafanya michezo mbalimbali ambayo ilijumuisha watumishi wote wa Wilaya hiyo na vilabu vyote vya michezo vya Mkoa wa Dar.

Mgeni rasmi wa tamasha hilo ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Temeke Felix Lyaniva alifurahishwa na kazi nzuri ya maandalizi ya Tamasha hilo, jinsi watumishi na vilabu vya michezo walivyojitokeza kwa wingi katika kuadhimisha siku hiyo ya kifo cha baba wa taifa.

Lyaniva alisisitiza kuyaishi maisha ya Mwl Nyerere  kwa kuwa wazalendo wa taifa letu na kuikataa rushwa ambayo ni adui wa maendeleo na adui wa haki. 

Alisema "Mwalimu Nyerere alikua mpenzi wa michezo ndio maana leo tunamuenzi". Mwl Nyerere ndiye alikua muanzilishi wa michezo mbalimbali. 

Alisisitiza katika vilabu vyote vya michezo kuwa na shughuli mbalimbali za kijasiliamali ili kujikwamua kiuchumi.

Alisema hayo alipowakumbusha wanamichezo kuwa pamoja na kwamba michezo ni afya lakini pia ikitumiwa vizuri itakuinua kiuchumi.
Mkuu wa Wilaya ya Temeke Felix Lyaviva na watumishi wa serikali wa manispaa hiyo pamoja na vikundi vya mazoezi wakifanya mazoezi ya pamoja.
Wakishiriki michezo mbalimbali ikiwemo kukimbia ndani ya magunia.
Watumishi wa manispaa ya Temeke wakifurahi kwa pamoja.

RAIS WA ZANZIBAR DK. SHEIN AKUTANA NA UJUMBE WA SHIRIKA LA UNAIDS


 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji  wa Shirika la UNAIDS na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw.Michel Sidibe alipofika Ikulu Mjini Zanzibar na Ujumbe wake.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji  wa Shirika la UNAIDS na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw.Michel Sidibe alipofika Ikulu Mjini Zanzibar na Ujumbe wake.
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji  wa Shirika la UNAIDS na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw.Michel Sidibe alipofika Ikulu Mjini Zanzibar na Ujumbe wake(hawapo pichani)
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji  wa Shirika la UNAIDS na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw.Michel Sidibe (wa pili kulia) alipofika Ikulu Mjini Zanzibar na Ujumbe wake (Picha na Ikulu) 

KITUO CHA POLISI MOROMBO KUPUNGUZA MSONGAMANO “CENTRAL” ARUSHA


Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo akiongoza askari kuhamisha udongo "Kifusi" toka kwenye msingi wa ujenzi wa nyumba za Polisi na kupeleka kwenye mtaro.

Na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha

Ujenzi wa kituo kidogo cha Polisi cha Morombo kilichopo kata ya Murieti halmashauri ya Jiji la Arusha  huenda ukawa mkombozi mkubwa kwa wakazi wa eneo hilo ambalo linakuwa kwa kasi kibiashara na ongezeko la  idadi ya watu.

 Uwepo wa kituo hicho utawezesha kusogeza huduma ya kiusalama kwa wakazi hao kwa ukaribu zaidi lakini pia kesi zao zitaripotiwa hapo hapo badala ya Kituo kidogo cha Sombetini au kituo Kikuu ambavyo vipo umbali mrefu toka eneo hilo.

Akizungumza katika eneo la kituo hicho, Kamanda wa Polisi mkoa wa Arusha Naibu Kamishna (DCP) Charles Mkumbo alisema kwamba ufunguzi wa kituo hicho ambacho kipo kwenye hatua za umaliziaji unatarajia kwenda sambamba na wa nyumba za askari watakaofanya kazi kituoni hapo na hiyo itasaidia askari kutoa huduma kwa haraka na ukaribu kwa kuwa watakuwa wanaishi eneo hilo.

Kamanda Mkumbo alisema kwamba, yeye pamoja na askari wapatao 200 wa vikosi mbalimbali jana waliamua kushiriki katika kuchimba msingi na kubeba udongo “Vifusi” kutoka eneo la ujenzi na kwenda kuumwaga kwenye mtaro.

Alisema pamoja na majukumu walionayo ya kuhakikisha jiji la Arusha pamoja na wilaya nyingine za mkoa huu zinakuwa salama lakini pia wameamua kufanya hivyo kwa nia ya kupunguza gharama na watakuwa tayari kushiriki katika kusogeza matofali kwa mafundi na hata kukoroga zege pindi nguvu kazi itakapohitajika. 

“Pamoja na sisi kujitoa kufanya kazi hizi lakini pia wananchi wanaozunguka eneo hilo wanapaswa kujitolea kubeba vifusi kwa kuwa kituo hicho ni cha kwao”. Alitoa wito huo Kamanda Mkumbo.

Kwa upande wake mkazi wa eneo hilo aliyejulikana kwa jina la mzee Isihaka Kivuyo alisema kwamba, kituo hicho  kitasaidia kuiweka jamii karibu na jeshi hilo jambo ambalo litasaidia kupunguza uhalifu. 

Alisema kwamba wananchi wanatakiwa wafurahie ujenzi wa kituo hicho hivyo na kuwataka wajitolee katika shughuli ndogondogo za ujenzi wa nyumba hizo za askari badala ya kazi hizo kufanywa na askari Polisi pekee ambao wana majukumu mengine ikiwemo kuhakikisha usalama wa wananchi na mali zao unakuwepo.

Ujenzi wa kituo hicho chenye hadhi ya daraja B ambao umefadhiliwa na Kampuni ya Lodhia Group ulianza toka mwaka 2016 mwezi Mei, lakini pia ujenzi wa nyumba saba za askari kwa sasa upo kwenye hatua za uchimbaji wa msingi na unatarajiwa kwenda kwa kasi ili uende sambamba na ufunguzi wa kituo.
Baadhi ya askari wakichimba na kubeba udongo toka eneo la ujenzi wa nyumba saba za askari kwa ajili ya kuweka mazingira mazuri ya ujenzi.
Kituo kipya cha Polisi Mrombo kilichopo kata ya Murieti halmashauri ya jiji la Arusha ambacho kina hadhi ya daraja "B" kipo katika hatua za mwisho za umaliziaji.

WAZIRI DKT DKT. MWAKYEMBE ALALAMA NA UNYONYAJI WA KAZI ZA SANAA


Na Agness Francis ,Blogu ya jamii
Waziri wa habari,utamaduni, sanaa na michezo, Dkt Harrison Mwakyembe amehudhudhuria  mkutano   wa  wasanii wa shirikisho la sanaa za ufundi  hapa nchini kusikiliza maendeleo na changamoto zinazowakabili wasanii hao na kuwataka kuchangamkia fursa kazi za mikono yao.

Katika mkutano huo uliofanyika leo jijini Dar es Salaam, Shirikisho hilo la sanaa za ufundi  hapa nchini ambalo lilianza rasmi mwaka 2009 na kupata usajili wake mwaka 2010 ambapo wasanii hao walimepata mafanikio  kwa kushirikiana na (BASATA)pamoja na ubalozi wa China katika mradi ambao ulijulikana kwa jina la Tingatinga Art Biennale na walipatikana washindi wawili ambao walizawadiwa tiketi ya kwenda nchini China.

Vile vile shirikisho limeeleza changamoto zinazowakabili wasanii hao kuwa Elimu ya sanaa za ufundi haifundishwi  mashuleni, hakuna kituo maalumu  cha Taifa cha kuonesha kazi za wasanii na masoko ya sanaa kuwa hafifu kutokana na ugumu wa usafirishaji wa vinyago kwenda  nje ya nchi kupitia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere.

Aidha Waziri Mwakyembe amekanusha dhana potofu isemwayo  kuwa wasanii wa sanaa za ufundi wengi wao  hawajaenda shule na amesema kuwa wizara yake itaunga mkono na kushirikiana bega kwa bega  na juhudi za  sanaa hiyo ili kuepukana na wanyonyaji wa  kazi ya wasanii hao.

Nae naibu waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo Juliana Shonza amemalizia kwa kutoa wito kwa Baraza la sanaa la Taifa (BASATA) kuendelea kuinua vipaji  kwa kuweza kuwafikia hasa  wasanii wa mikoani  na wilayani ambao wamesahaulika kwa muda mrefu katika kuiendeleza tasni hiyo.
 Waziri wa habari, utamaduni, sanaa na michezo, Dkt Harrison Mwakyembe akizungumza na waandishi wa habari pamoja na wasanii wa shirikisho la sanaa za ufundi Tanzania pamoja kuwapongeza kwa kazi za mikoni wanazozifanya wasanii hao leo katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam.
 Naibu waziri wa habari,utamaduni,sanaa na michezo Juliana Shonza, akizungumza na wandishi wa habari pamoja na wasanii wa shirikisho la sanaa za ufundi Tanzania na kuwataka( BASATA) kuendelea kuinua vipaji vya wasanii hapa nchini hasa kwa wale walioko wa mikoani.
Wageni waalikwa waliojitokeza kwa wingi katika kuhudhuria mkutano uliofanyika leo katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam.
Wasanii wa maigizo ya maonyesho ya  jukwaani wakifanya igizo linalohusu kampeni ya kuzuia rushwa  leo katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa Jijini Dar es Salaam.

WANANCHI WA DODOMA KUNUFAIKA NA HUDUMA ZA BENKI YA EXIM


 Mr Fredrick Kanga, Head of Human Resources at Exim Bank Tanzania addressing guests, customers and media during the official launch of Exim Bank Dodoma Branch located inside the University of Dodoma, at Chiwaga area yesterday. Others are Mr Stanley Kafu, Head of Marketing at Exim Bank Tanzania (left) and the guest of honour District Commissioner Christina Mndeme.
 Dodoma District Commissioner Christina Mndeme, addressing the guests, customers and media during the official launch of Exim Dodoma Branch located inside the University of Dodoma, at Chiwaga area yesterday. Others are Mr Fredrick Kanga, Head of Human Resources at Exim Bank Tanzania (left) and Mr Stanely Kafu, Head of Marketing at Exim Bank Tanzania (left).
 Dodoma District Commissioner Christina Mndeme on behalf of the Regional Commissioner Jordan Rugimbana, officially launches Exim Bank Dodoma Branch earlier yesterday during the official ceremony. The branch which is located inside the University of Dar es Salaam Dodoma will serve the captive clients of the University of Dodoma, which consists of over 25,000 students, 2000 employees and over 8 Government Ministries who have moved there. It will also serve the Dodoma City clients, as the branch is only 5 to 7 minutes drive from the city centre. To her right is Mr Fredrick Kanga, head of Human Resources at Exim Bank Tanzania.
 Exim Bank Dodoma Branch staff interacting with the guest of honour Dodoma District Commissioner, Christina Mndeme during the official launch of the branch located inside the Universty University of Dodoma, at Chiwaga area yesterday.
 

BENKI ya Exim Tanzania imethibitisha  kujitolea  kuimarisha ushirikishwaji wa wa nanchi kwenye mfumo rasmi wa kifedha nchini kwa kuzindua tawi jipya katika mkoa wa Dodoma,Tanzania. UtanuzihuuutaongezauwepowaBenkiya Exim kuwanajumlayamatawi 33nchinikote.
Akizungumza katika uzinduzi rasmi Fredrick Kanga, Mkuu wa kitengo cha Rasilimali Watu katika Benki ya Exim Tanzania, alisema, "Utanuzi wa benki ni sehemu ya mkakati wetu wakukuza huduma zetu katika maeneo ambayo yanatuleta karibu na wateja wetu. Tawi litatoa huduma kamili za kibenki kama vile kuhifadhi pesa, huduma za uwekezaji, na suluhisho za malipo ya kampuni."
Tawi la Dodoma, lililopo ndani ya Chuo Kikuu cha Dodoma, litawahudumia wateja wa Chuo Kikuu hiko, ambacho kina wanafunzi zaidi ya 25,000, wafanyakazi2000 na Wizara za Serikali zaidi ya 8 ambazo zimehamia huko. 
Tawi litawatumikia wateja wa Jiji la Dodoma, kwa kuwa tawili na umbali wadakika 5 hadi 7 kwa mwendo wa gari kutoka katikati ya jiji.
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana alipongeza Benki ya Exim Tanzania kwa kujitolea kwake "Tunafurahi kuwa na uwepo wa Benki ya Exim katika mji mkuuwa Tanzania, ili kuimarisha ushirikishwaji wa wananchi kwenye mfumo rasmi wa kifedha  unao wawezesha kupata huduma, bidhaa za kifedha,na mitaji kwa jamii na watu binafsi wa Dodoma. "
Benkiya Exim  imeongezeka kwa ujasiri ilikukuza msingi wa mali na kufanikiwa kutanua uwezo  kwa wateja Shughuli za Benki zinapatikana katika mikoa ya Dar es Salaam, Zanzibar, Tanga, Morogoro, Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Mwanza, Shinyanga, Kigoma, Iringa, Mbeya na Mtwara ndani ya Tanzania na kampuni tanzu nje ya nchi katika Visiwa vya Anjouan, MohelinaMoroni vya Union of Comoros ,kwenye Jamhuri ya Djibouti na Uganda – uwepo wa benki ya Exim.