Saturday, October 7

Polisi wawalaumu panya kwa mihadarati iliotoweka India

Panya wamelaumiwa kwa kutoweka kwa mihadarati iliohifadhiwa katika ghala la serikali India
Image captionPanya wamelaumiwa kwa kutoweka kwa mihadarati iliohifadhiwa katika ghala la serikali India
Police katika mji wa Mumbai nchini India wanawalaumu panya kwa kutoweka kwa kilo 34 za dawa za kulevya kwa jina Ketamine.
Wanasema wanawatuhumu panya hao kwamba ndio wa kulaumiwa baada ya kupata mabagi hayo yalitobolewa kwa chini.
Uchunguzi wa miaka mitatu umekamilika kwamba iwapo ingekuwa binadamu wangechukua mabagi yote.
Dawa hizo zilizohifadhiwa katika ghala moja la serikali zilikuwa miongoni mwa kilo 200 za mihadarati zilizopatikana na walanguzi wa mihadarati 2011.
Hii sio mara ya kwanza kwa maafisa wa polisi nchini India kuwalaumu panya kwa kutoweka kwa mihadarati iliokamatwa.

TAIFA STARS ZAFUNGANA SARE YA 1-1 NA TIMU YA MALAWI,MECHI BADO INAENDELEA UWANJA WA UHURU


Nahodha wa timu ya Taifa, Mbwana Samatta akiondoka na mpira mbele ya Mabeki wa Malawi.

Mmoja wa Wachezaji wa timu ya Tanzania (Taifa Stars) akimchomoko mchezaji wa timu ya Taifa ya Zambia,ambapo mpaka sasa kipindi cha pili timu hizo zimefungana sare ya 1-1 na mpira unaendelea katika uwanja wa Uhuru,jijini Dar.
 Kikosi cha timu ya Taifa Stars
 Waziri wa Habari,Utamaduni ,sanaa na Michezo Dkt Harrison Mwakyembe akiikagua timu ya Taifa Stars kabla ya mchezo wa kirafiki wa Kimataifa dhidi ya timu ya Malawi kuanza jioni ya leo katika uwanja wa Uhuru,jijini Dar
 Wimbo wa Taifa Ukipigwa

Kikosi cha timu ya Malawi.

JERRY MURO AMKALIA KOONI GODBLESS LEMA, AJIBU TUHUMA ZILIZOTOLEWA NA CHADEMA



Mbowe amshukuru Magufuli kwa kutenganisha Wizara ya Nishati na Madini


Babati. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amepongeza kitendo cha Rais John Magufuli kuitenganisha Wizara ya Nishati na Madini kwa kuwa kwa zaidi ya miaka saba kambi hiyo ilikuwa inaishauri Serikali kufanya hivyo.
Mbowe amesema hayo leo Jumamosi kwenye mazishi ya marehemu Philip Gekul, baba mzazi wa Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul yaliyofanyika kata ya Dareda.
Amesema kwa mujibu wa kumbukumbu za Bunge zinaonyesha kuwa kambi rasmi ya upinzani ilikuwa inashauri wizara hiyo itenganishwe lakini ushauri wao haukufanyiwa kazi.
"Wizara ya Nishati na Madini ni wizara nyeti mno na mara nyingi tumekuwa tukiishauri Serikali iitenganishe wizara hiyo kwani ni kubwa na nyeti ila sasa wameona ushauri wetu unafaa na kuzitenganisha," amesema Mbowe.

Amesema suala siyo nani anafaa kuwa waziri na nani hafai kuwa waziri au ukubwa wa wizara ila suala ni kuona namna gani ya kuendesha Serikali ya Awamu ya Tano.
"Magufuli ajitafakari namna anavyoendesha Serikali kwani matakwa ya viongozi ndiyo yanakuwa maelekezo ya kuendesha nchi na hata mawaziri wanafanya kazi kwa matakwa ya mtu," amesema Mbowe.

Kichwa cha mwandishi aliyetoweka chapatikana baharini Sweden

Mwandishi Kim Wall kuliaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionMwandishi Kim Wall kulia
Kichwa cha mwandishi wa Sweden Kim Wall kimepatikana , miezi miwili baada ya kupotea katika ziara na raia mmoja wa Denmark.
Waogeleaji walipata mifuko iliokuwa na kichwa chake, miguu na nguo katika eneo la Koge Bay kusini mwa mji wa Copennhagen kulingana na inspekta mkuu wa polisi wa eneo hilo Jens Moller Jensen.
Vilipatikana karibu na pale mwili wa Wall ulipokuwa siku chache tu baada ya kupanda katika manuwari tarehe 10 Agosti.
Bwana Marsden mwenye umri wa miaka 46 amekana kumuua bi Moller Jensen akisema mabegi hayo yaliopatikana yalikuwa yamechanganywa na kupimwa uzani na vipande vya vyuma.
''Jana alfajiri tulipata begi ambalo lilikuwa na nguo za Kim, suruali ya ndani na viatu.katika begi hilo hilo kulikuwa na kisu na kulikuwa na mabomba ya magari'' .
Matokeo ya uchunguzi yamebaini kwamba kichwa hicho ni cha bi Wall na kwamba hakina ishara za kwamba fuvu lake la kichwa liliumizwa ama hata kupigwa.
Matokeo hayo yanaenda kinyume na taarifa za Marseden kwamba alifariki baada ya kugonga kichwa chake katika mlango.
Bi Wall ,30, alionekana mara ya mwisho akiwa hai jioni ya Agosti 10 wakati alipokuwa akiondoka na bwana Marsden katika manowari aliotengeza mwenyewe kuhusu habari aliokuwa akiandika kuhusu safari hatari aliotaka kufanya.
Mpenziwe alipiga kamsa siku ya pili baada ya kutorudi kutoka kwa safari yake.
Awali bwana Marsden alisema kuwa alimsafirisha na kumwacha akiwa salama mjini Copenhagen , lakini baadaye akabadilisha taarifa yake na kusema kwamba alimzika baharini baada ya ajali mbaya na alikuwa amepanga kujiuwa kwa kuizamisha manowari yake.

Walaani unyama Cameroon, wakemea mapepo Uganda


Yaounde, Cameroon. Watumishi wa Mungu, baada ya kuona yanayoendelea Cameroon na Uganda, wamejitokeza na kupaza sauti zao kukemea pepo anayeelekea kuchafua hali ya hewa ya siasa na amani.
Kutoka Yaounde, maaskofu wa Kikatoliki wamelaani “unyama” na “matumizi yasiyo ya lazima” ya nguvu dhidi ya waandamanaji katika eneo la wanaozungumza Kiingereza wiki iliyopita yaliyosababisha kuuawa watu 19.
Mapambano hayo yalitokea wakati viongozi wa eneo hilo walipoashiria kujitangazia uhuru wakidai kwamba Wanaozungumza Kiingereza kwa miongo mingi wamekuwa wakikosa usawa kiuchumi na kukosa haki za kijamii mbele ya wenzao walio wengi wanaozungumza Kifaransa.
"Tunalaani kwa nguvu zetu zote unyama na matumizi ya silaha za moto yasiyo ya lazima dhidi ya raia ambao wala hawakuwa na silaha yaliyofanywa na vikosi vya sheria na usalama hata kama walichokozwa,” ilisema taarifa ya Baraza la Maaskofu jimbo la Bamenda.
Watu 14 waliuawa katika mapambano na vikosi vya usalama wiki iliyopita, na wafungwa watano walipigwa risasi na walinzi walipojaribu kuvunja gereza la Kumbo.
Baadhi ya waombaji walipigwa mabomu ya kutoa machozi walipokuwa wakiondoka katika misa wakati wengine “walikamatwa, kujeruhiwa na baadhi (wakiwemo vijana wasio na silaha na wazee) walipigwa risasi kutoka kwenye helikopta.”
Lakini serikali imejitetea kwa kusema askari wake walilazimika kujihami baada ya kuweka amri ya kutotemba katika eneo hilo. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres na shirika la kutetea haki za binadamu la and Amnesty International wametoa wito ufanyike uchunguzi.
Kutoka Kampala Uganda, waumini wapatao 100 wakiongozwa na mchungaji Julius Oyet, walikwenda bungeni ambako walifanya ibada, wakalitakasa Bunge kwa damu ya Jesu kisha wakamwekea mikono kichwani Spika wa Bunge Rebecca Kadaga.
Watumishi hao wa Mungu waliombea utakaso ili Bunge lirejea katika hali yake ya kawaida baada ya wiki iliyopita kukumbwa na vurugu zilizosababisha wabunge kadhaa kujeruhiwa na wengine wa upinzani kukamatwa na polisi.
Wabunge 24 wa upinzani walisimamishwa Septemba 27 baada ya vurugu kuibuka huku wakimtuhumu Waziri wa Maji Ronald Kibuule kuingia na bunduki. Mgawanyiko mkubwa ulijitokeza wakati wa mjadala wa ukomo wa umri wa rais.
“Tunaomba hekima na mwongozo wenye mwelekeo. Tunatangaza kwamba hakuna silaha itakayofanya kazi dhidi yake na wala hatakufa mapema,” alisema Oyet akiwa amemwekea mikono Spika.
Katika sala zake, Mchungaji Tony Okot kutoka Kaskazini mwa Uganda alisema: “Tunaombea amani katika bunge hili na mzunguko wa viongozi wakati tukiomba utulivu wa wabunge wanapojadili muswada na kunyamazisha mapepo mengine yasifike hapa. Tunaomba kuwa chochote wanachofanya wafanye kwa hofu, amani, upendo, umoja na kuheshimiana.”

Pengo: Kauli ya Askofu Niwemugizi siyo msimamo wa Katoliki


Dar es Salaam. Mwadhama Kadinali, Polycarp Pengo amesema kwamba kauli iliyotolewa hivi karibuni naAskofu wa Jimbo la Rulenge mkoani Kagera, Severine Niwemugizi kwamba Katiba mpya ndiyo kipaumbele cha wananchi ni maoni binafsi siyo msimamo wa Kanisa Katoliki nchini.
Pengo alisisitiza hilo wakati akitoa ufafanuzi juu ya sintofahamu iliyojitokeza miongoni mwa Watanzania na waumini wa kanisa hilo kutokana na kauli ya Askofu Niwemugizi.
“Napenda kutamka moja kwa moja kwamba huo siyo msimamo wa kanisa na hauwezi kuwa msimao wa kanisa kwa sababu sisi tuna taratibu zetu za kuishauri Serikali au kuzungumzia masuala ya jamii,” alisema.
Alifafanua zaidi kwamba  kutokana na nafasi ya Uaskofu aliyonayo Askofu Niwemugizi, kauli yake inaweza kutafsiriwa kuwa ndio msimamo wa Kanisa Katoliki au wa Jimbo la Rulenge, Ngara lakini kimsingi kauli ile imekosa vigezo vya kuichukulia kama msimamo wa kanisa au jimbo anakotoka.
Kadinali Pengo alisema yeye binafsi kipaumbele chake ni kuona huduma za jamii kama zile elimu na afya zinaendelea kuboreshwa kwa kasi kama ambavyo Serikali ilivyoanza kufanya.
“Mtu akiniambia priority (kipaumbele) ya Tanzania ni Katiba mpya inabidi anithibitishie huo ukipaumbele maana siwezi kuona mtoto anakufa kwa njaa au kwa kukosa dawa eti kwa sababu ya Katiba mpya. Kwangu mimi Katiba ni kitu ambacho kije baadaye, si cha haraka.
“Wanasiasa wasiache watoto wetu wafe kwa njaa kisa malumbano ya Katiba. Wasiache watoto wakose shule kwa sababu hela zote zimeishia kwenye malumbano juu ya Katiba,” alisisitiza Kadinali Pengo.
Kwa upande wake Balozi wa Vatican nchini Tanzania, Askofu Marek Solczynski hakutofautiana na kauli ya Kadinali Pengo kwa kusema  pamoja na kwamba Askofu Niwemugizi ana haki ya kutoa maoni yake lakini tatizo linakuja pale watu wakaposhindwa kung’amua kuwa ni maoni binafsi au ni ya kanisa.
Amesisitiza kwamba kanisa lina taratibu zake za kutoa maoni kwa masuala ya kijamii na kwa Serikali. “Hayo ni maoni yake binafsi na wala yasihusishwe na kanisa katoliki,” alisema Balozi Askofu Merek.
Hivi karibuni Askofu Niwemugizi alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kipaumbeke cha kwanza cha Watanzania ni Katiba mpya na kuongeza yeye binafsi ni miongini mwa watu walioipinga Katiba Inayopendekezwa.
Hata hivyo, wachambuzi wa mambo walisema, pamoja na mjadala mkubwa ulioibuka na baadhi ya wanasiasa kususia mchakato wa kukamilisha Katiba mpya, wataalamu wa sheria wanasema Katiba inayopendekezwa ilikuwa ni bora kuliko ya sasa ikiwemo kuruhusu wagombea kuhoji mahakamani matokeo mbalimbali ikiwemo ya urais.
“Hata mimi ukiniuliza leo tuache kufanya mageuzi ya msingi katika jamii ili kuwa na uchumi imara au tuanze kushughulika na Katiba mpya, nitakwambia tuachane na Katiba.
“Nakumbuka ile Katiba Inayopendekezwa ilikuwa na masuala makubwa yenye maslahi kwa nchi ikiwemo kipengele cha kupinga matokeo ya urais lakini kwa kuwa kuna watu walikuwa na maslahi yao binafsi, wakatoka nje ya Bunge na kukwamisha mchakato ule sioni uharaka wa leo tuache mengine yote turejee kwenye mchakato huu,” alisema Wakili wa Mahakama Kuu, James Nandonde.

Siku za Tillerson zinahesabika


Washington, Marekani. Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Rex Tillerson, mkurugenzi wa zamani wa kampuni ya mafuta ambaye aliteuliwa na Rais Donald Trump kusimamia masuala ya kimataifa anatajwa na maofisa wa utawala kuwa anaelekea kuondoka.
Sababu za Tillerson kutajwa kuwa siku zake katika nafasi hiyo zinahesabika zimechochewa wiki hii na ripoti mpya kali baina ya watu hao, ambapo inadaiwa Tillerson alihoji uwezo wa kufikiri wa Trump alipozungumza na maofisa wengine.
Kisa hicho kimemkera rais huyo na alichukizwa kuona kwamba mtu aliyedhaniwa ni mdogo kicheo alikuwa akimtusi kwa marafiki zake. Habari zinasema hali hiyo imezidisha taswira ya Tillerson kama mshirika asiyekubali sera za Trump kuhusu ajenda ya sera ya mambo ya nje, maeneo ambayo watu wawili hao wameshindwa kukubaliana hadharani.
Vyanzo zaidi ya dazani kutoka ndani ya utawala na nyanja za kidiplomasia vinasema kuwa uhusiano kati ya Tillerson na Trump uko chini sana. Watu wawili hao wameshindwa kukuza uhusiano wa karibu ambao Trump anaufurahia kutoka kwa mawaziri wengine.
Tofauti za kihaiba kati ya Tillerson na Trump zimewaingiza katika msuguano na dharau.
Habari zinasema Tillerson amewaambia marafiki zake kwamba anakusudia kushikilia nafasi hiyo kwa angalau mwaka mmoja, mstari aliojichorea kisaikolojia kwamba utamwezesha, kwa hiari yake moyoni, kuondoka kwa heshima.
Lakini kukirihika kwa bosi wake kukichanganywa na kukerwa kwake kumesababisha wakati fulani kuyumba. Tillerson alionyesha ishara wiki hii kwamba ataendelea na kazi zake walau kwa sasa, ikiwa ni pamoja na kuonekana hadharani kumuunga mkono Trump.
Chanzo kinachofahamu vizuri mzozo unaomzingira Tillerson kinasema “hakuna dalili” kuwa kibarua chake kiko hatarini walau siyo kwa sasa.

Hizi ndizo sura mpya baraza la mawaziri

Dar es Salaam. Mabadiliko yaliyofanywa na Rais John Magufuli katika baraza la mawaziri yamekuja na sura mpya ambazo hazina umaarufu kwenye siasa za Tanzania.
Katika baraza hilo jipya Rais Magufuli ameonekana kuwateua wabunge wengi ambao wameingia bungeni kwa mara ya kwanza.
Ikiwa ni mara yake ya kwanza kuingia bungeni kuwatumikia wananchi wa Pangani, Jumaa Awesu ameteuliwa kwenye baraza la mawaziri kutumia nafasi ya naibu waziri wa maji.
Mbunge wa Viti maalum anayewakilisha kundi la walemavu, Stella Ikupa anaweka historia ya kuwa mwanamke wa kwanza kutoka kwenye kundi hilo kuingia ndani ya baraza kuitumikia nafasi ya naibu waziri anayeshughulikia masuala ya walemavu.
Mwanasiasa machachari na Mbunge wa Mwibara, Kangi Lugola naye amechomoza kwenye baraza hilo kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano  na Mazingira).
Mbunge wa Maswa Mashariki, Haroon Nyongo anaingia kwenye baraza la mawaziri kusaidiana na Angela Kairuki kuiongoza wizara ya madini.
Ukiacha huyo pia Mbunge wa Vwawa, Japhet Hasunga ameingia kwenye baraza hilo kutumikia nafasi ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii.
Pia Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Pwani, Subira Mgalu naye ameingia kwenye baraza hilo kutumikia Wizara ya Nishati kama naibu waziri.
Wizara hii inatajwa kuwa na changamoto lukuki ikiwemo kukosekana kwa umeme wa uhakika hasa katika kipindi hiki ambacho serikali ya awamu ya tano inalenga kuifanya Tanzania nchi ya viwanda.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Mbeya, Dk Mary Mwanjelwa naye kwa mara ya kwanza ameingia kwenye baraza la mawaziri kuwa Naibu Waziri wa Kilimo.
Bahati imeendelea kuwa njema kwa Mkoa wa Pwani kwani Mbunge wa Mkuranga, Abdala Ulega ameingia kwenye baraza hilo kutumika kama naibu waziri katika wizara mpya ya mifugo na uvuvi.
Juliana Shonza aliyejipatia umaarufu baada ya kunusurika kupigwa na wabunge wa Chadema, naye ameingia kwenye baraza hilo kama Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Mbunge wa Muhambwe, Atashasta Nditiye anaingia kwenye baraza hilo kama Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi akishughulikia masuala ya Ujenzi na Uchukuzi.
Elias Kwandikwa ameingia kwenye wizara hiyo kama naibu waziri anayeshughulikia masuala ya mawasiliano.
Mbunge wa Kigamboni, Dk Faustine Ndugulile anaingia kwenye baraza jipya kama Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.
Josephat Kandege na Joseph George Kakunda wameingia kwenye baraza hilo kama manaibu Waziri Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi).

Kikwete atimiza miaka 67 leo Jumamosi


Dar es Salaam.Tarehe na mwezi kama wa leo miaka 67 iliyopita alizaliwa Rais mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete.
Leo Jumamosi akiwa anaadhimisha siku yake ya kuzaliwa salamu mbalimbali zimetolewa kumtakia heri na maisha marefu.
Watumiaji wa mitandao ya kijamii hasa wanasiasa na wasanii hawakuwa nyuma kumtumia salam za heri, kiongozi huyo aliyesifika kuwa karibu mno na wasanii wakati wa uongozi wake.
Julius Mtatiro ni miongoni mwa walimtakia heri, ujumbe wake ulisomeka, “Happy birthday Mr President. Ulitufundisha huko nyuma kuwa siasa si uadui. Ulifanya makosa mengi kwenye uongozi wako, ulifanya mazuri mengi pia. Kwa sasa tunachoweza ni kukutakia umri mrefu,”
Muigizaji Jacob Stephen (JB) amendika, “Wasanii wa fani mbalimbali wanakupenda mno kwa sababu ulionyesha upendo wa dhati… na hilo lilisababisha watu wote kuwaheshimu wasanii..Mungu akubariki, akupe haja ya moyo wako Rais mstaafu Jakaya Kikwete,”
Jackline Wolper ameandika, “Dady kabisa wa Taifa leo kazaliwa… happy birthday mshua tunakuzimia na kukukumbuka juu,”

Tume yaridhia masharti ya Nasa


Nairobi, Kenya. Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC), Wafula Chebukati ametangaza timu ya maofisa watakaosimamia shughuli za uchaguzi wa marudio Oktoba 26 huku jina la ofisa mtendaji mkuu, Ezra Chiloba likikosekana.
Chebukati, wakati anatangaza majukumu ya maofisa hao Ijumaa alisema Chiloba, ambaye muungano wa National Super Alliance (Nasa) unataka aondolewe, hatakuwa na mkono katika uchaguzi huo. Mbali ya Chiloba, pia maofisa wengine saba hawamo.
Hatua hiyo imekuja muda mfupi baada ya maandamano makubwa kufanywa na wafuasi wa Nasa mjini Kisumu, Nairobi na Homabay wakishinikiza kuondolewa na Chiloba na wenzake 10.
Vilevile, mabadiliko hayo yamefanyika wakati Nasa wakitangaza kuongeza siku ya Jumatano katika siku za maandamano. Katika barua yao waliyopeleka polisi sasa Nasa watakuwa wakiandamana kila Jumatatu, Jumatano na Ijumaa kushinikiza maofisa 11 waondolewe, na zifutwe zabuni kwa kampuni ya kuchapisha makaratasi ya kupigia kura na inayosambaza vifaa vya utambuzi wa mpigakura na kutuma matokeo kwa njia ya kielektroniki.
Baada ya shinikizo kali la maandamano ya ghasia, Chubukati ameonekana akikubali yaishe kwa upande wake akianza kwa kuondoa majina ya Chiloba na maofisa wengine saba.
Mabadiliko haya yanafanana na yale yaliyotangazwa siku chache baada ya Mahakama ya Juu kubatilisha matokeo yaliyompa ushindi Rais Uhuru Kenyatta, lakini Tume ilikanusha.
Gazeti la The Nation limefahamishwa kwamba Chebukati alifanikiwa kuwashawishi makamishna wote na wakaridhia timu mpya ambayo itawajibika katika maandalizi na kujibu maswali yote yanayohusu uchaguzi wa marudio.
Timu mpya ni ya Marjan Hussein atakayekuwa msimamizi wa timu; David Towett atahusika na operesheni, Albert Gogo atasimamia teknolojia ya uchaguzi, Dk Sidney Namulungu atasimamia vituo vya kujumlishia kura, Tabitha Mutemi atasimamia mawasiliano, Agatha Wahome atahusika na fedha, manunuzi na utawala, na Salome Oyugi atahusika na masuala ya sheria.

CUF kushiriki uchaguzi wa madiwani kivyake


Dar es Salaam. Chama cha Wananchi(CUF), upande wa Profesa  Ibrahim Lipumba kimesema kitashiriki kikamilifu katika uchaguzi wa madiwani uliopangwa kufanyika Novemba 26 lakini kimesisitiza kutoshirikiana na Ukawa.
Hii ni mara ya kwanza kwa chama hicho kuweka msimamo wake katika uchaguzi tangu kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 ambapo CUF ilikuwa miongoni mwa vyama viliunda umoja huo kwa kuweka wagombea waliokubaliana.
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CUF, Abdul Kambaya amesema leo Jumamosi jijini kuwa chama hicho hakioni sababu yoyote ya kushirikiana na vyama vingine kwenye uchaguzi huo ambao unahusisha halmashauri 34.
“CUF tunashiriki kwenye uchaguzi huu lakini hatututegemei kushirikiana na umoja wowote ule, sisi hatuitambui Ukawa lakini tunajua kuna chama kama Chadema, CUF na vyama vingine,” amesema Kambaya wakati alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi za chama hicho zilizopo Buguruni.
Amesema chama hicho kimejipanga vilivyo kuelekea kwenye uchaguzi huo na kwamba ili kuwaletea maendeleo wananchi wa maeneo hayo kunahitajika kuwa na viongozi wenye utulivu wa akili.
“Sisi tuko tayari kuelekea kwenye uchaguzi huo bila kuhusishwa na chama kingine chochote tunaamini tutafanya vizuri,” amesema.
Awali, mkurugenzi wa uchaguzi wa chama hicho, Jafari Mneko aliwataka wana CUF kujitokeza kwa wingi katika kinyang’anyiro hicho. Amesema chama chake kimepokea taarifa kutoka ofisi ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi ikiwaarifu kuhusu uchaguzi huo.
“Tumepata barua kutoka tume ambayo imetueleza kuhusu tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi huo na sisi tumeanza kujiandaa na ndiyo maana tunawaomba wanachama wetu wanaohisi wana uwezo wajitokeze kuomba nafasi na baadaye viongozi wa chama watachuja majina yao,” amesema.
Katika hatua nyingine mkurugenzi huyo alionya kile alichokiita mali ya chama kutumika kinyume na sheria na akawataka wanachama kutetea maslahi ya chama chao.
“Kuanzia sasa hatutapenda kuona mali ya chama kama mihuri, bendera ikiendelea kuchezewa ovyo, tunawataka wanachama kuzingatia katiba ya chama ibara ya 12 ambayo inamtaka kila mwanachama kulinda katiba na imani ya chama,” amesema.

WAZIRI AKIMBIA KIBANO MSHAHARA MPYA Z’BAR

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), imeahirisha mkutano na Jumuiya ya Wawekezaji wa Sekta ya Utalii Zanzibar (ZATI) uliokuwa ufanyike Septemba 29, mwaka huu kuzungumzia pamoja na mambo mengine masuala ya viwango vipya vya wastani wa mishahara ya kima cha chini visiwani humo.

Kwa mujibu wa barua kutoka kwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto, Ameir A. Ameir kwenda kwa Mwenyekiti wa ZATI, Seif Masoud Miskiry, mkutano huo hautaweza kufanyika kwa vile suala hilo halikuwa miongoni mwa ajenda zilizojadiliwa na kikao cha Baraza la Mawaziri la SMZ.
Mkutano huo uliOkuwa ufanyike chini ya Waziri wa Kazi, Uwezeshaji Wazee, Vijana, Wanawake na Watoto, Maudline Castico, umezua malalamiko kutoka kwa wawekezaji na wafanyakazi wa sekta binafsi ambao hadi sasa hawajui hatima yao.
Mkutano huo ungetoa fursa kwake kushughulikia masuala yaliyowasilishwa na ZATI serikalini katika kikao cha siku mbili Julai 26-27 kutafuta ushauri na mwongozo wa kumwezesha ilikuweza kupata ufumbuzi masuala hayo.
“Ningependa kukufahamisha kwamba suala letu halikuwepo katika ajenda za kikao cha Baraza la Mawaziri na hivyo halikujadiliwa katika tarehe ile. Kutokana na hali hiyo, Mheshimiwa waziri anaahirisha mkutano hadi itakapotangazwa tena baadaye,”   alieleza Ameir katika barua yake
Kutokana na uamuzi huo Ameir alisema kwamba anasikitishwa kufutwa kwa mkutano huo, anatarajia utapangwa tena wakati mwafaka.
Mapema wiki hii MTANZANIA ilimtafuta Waziri Castico ili kupata kauli ya Serikali ambapo mwandishi  alipopiga simu yake na kujitambulisha kwa waziri huyo kuwa anahitaji kupata ufafanuzi wa suala hilo alikata simu bila kujibu lolote.
Waziri Castico ambaye alipigiwa kwa simu yake ya kiganjani namba 0652…348 ambapo baada ya kuulizwa swali kuhusu madai hayo ya wawekezaji hao alikataa simu na baada ya kutumiwa ujumbe kwa njia ya simu aliizima kabisa.
Pamoja na hali hiyo MTANZANIA ilimtumia ujumbe mfupi kwa njia simu uliosomeka “Habari mheshimiwa Waziri ….ni mwandishi wa gazeti la MTANZANIA nahitaji kupata kauli ya Serikali juu ya malalamiko yaliyotolewa na Jumuiya ya Wawekezaji wa Sekta ya Utalii Zanzibar (ZATI),” ulisema ujumbe huo waliotumiwa Waziri Castico ambao ulionesha ameusoma na lakini na alipogiwa simu iliita na kuizima hadi tunakwenda mitamboni.
Kutokana na hali hiyo gazeti hili lilimtafuta Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, Mohamed Abood, ambapo naye alisema kuwa kwa sasa hana mamlaka ya kuzungumzia suala hilo zaidi ya Waziri husika.
Hivi karibuni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wawekezaji wa Sekta ya Utalii Zanzibar (ZATI), Seif Masoud Miskry, alisema wanashangazwa kupewa lawama za wao kukwamisha kutolipwa mishahara mipya kwani wao waliwasiliana na Waziri mwenye dhamana (Castico) na kuwaambia waendelee kulipa mishahara ya zamani.
Alisema licha ya Waziri Castico kutangaza kima kipya cha mhshara kwa wafanyakazi wa sekta binafsi hakuna sehemu yoyote wao kama wadau waliposhirikishwa zaidi ya uamuzi binafsiwa kiongozi huyo.
Naye Mlezi wa ZATI ambaye pia ni Mwakilishi wa Tunguu, Simai Mohamed Said (CCM), alimwomba Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein aingilie kati sakata hilo kuokoa sekta ya utalii nchini.
Kutokana  na hali hiyo alisema wageni hao Zanzibar hushindana na nchi kama Thailand, Tunisia, Morocco, Spain, Visiwa vya Ugiriki kama Crete, Mexico, Cuba, St. Lucia pamoja visiwa vyengine.
Alisema wanaouza nafasi za hoteli kwa Zanzibar kwa nchi za Ulaya tayari tayari wanaanza kuona Zanzibar ni bei ghali hasa ikiwa mishahara itapanda kupindukia na wao itawafanya wapandishe bei ina maana katika mapumziko ya mwaka 2018 wataiondoa Zanzibar katika mabango ya kuitangaza hasa kwenye mitandao ya kununua likizo hizo.
Mabadiliko hayo yamefanyika kwa mujibu chini ya kifungu cha 97 (1) cha sheria ya Ajira nambari 11 ya mwaka 2005 ambapo kima cha chini kwa wafanyakazi  kimeongezeka kutoka Sh 145,000 hadi 180,000 huku kwa wenye mikataba ikingezwa kutoka kiwango cha sasa cha Sh 145,000 hadi 300,000.
Huku kwa vibarua wa kutwa wenye ujuzi, kimeongezwa kutoka Sh 10,000  hadi 30,000  kwa siku na kwa vibarua wa kutwa wasio na ujuzi, kimeongezwa kutoka Sh 7000  na kufikia 25,000.

Chadema chakosoa hali ya uchunguzi wa Tundu Lissu

Mbunge wa Singida mashariki aliyepigwa risasi Tundu Lissu
Image captionMbunge wa Singida mashariki aliyepigwa risasi Tundu Lissu
Chama cha upinzani nchini Tanzania Chadema kimeuliza maswali mengi kuhusu hatua zilizopigwa katika uchunguzi wa Mbunge wa Singida mashariki Tundu Lissu ambaye mwezi uliopita alipigwa risasi mjini Dodoma na sasa amelazwa katika hospitali ya Nairobi kwa matibabu.
Akizungumza katika mkutano na vyombo vya habari , Mkurugenzi mshirikishi na usajili wa chama hicho Benson Kigailia amesema kuwa kufikia sasa hakuna mtu aliyetiwa mbaroni ili kusaidia katika uchaguzi huo.
Kulinaga na gazet la The Citizen Tanzania ,alisema kwamba katika eneo la Kibiti, ambapo mashambulizi na mauaji yamefanyika hatua kadhaa zilichukuliwa ili kuhakikisha kuwa washukiwa wanakamatwa.
Akielezea zaidi , alisema kuwa ni rahisi kwa maafisa wa usalama kuchunguza , kuwatafuta na kuwakamata watu wanaomkosoa rais katika mitandao ya kijamii badala ya kuchunguza na kuwakamata washukiwa wanaotaka kuwaua wengine mchana kutwa.
Gazeti hilo limenukuu akisema kuwa mbali na kuyakamata magari 10 kuhusiana na jaribio hilo la mauaji, la kushangaza ni kwamba hakuna hata mlinzi mmoja aliykuwa kazini katika eneo la Area D mjini Dodoma amekamatwa'', alisema.

Vijana wajadili uchaguzi Kenya



Wakati Kenya ikijiandaa na kinyang'anyiro kingine kikali cha uchaguzi kati ya mafahari wawili - Rais Uhuru Kenyatta na hasimu wake mkuu wa kisiasa Raila Odinga, Eric Ponda anawauliza vijana wa Mombasa wamejiandaa vipi kuhakikisha sauti yao inasikika na kuheshimiwa. Ni kipidi cha Vijana Tugutuke kutoka Pwani ya Kenya.

 
Sikiliza sauti09:45

Mapigano mapya yaripotiwa Mashariki mwa Congo

Ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo umetuma majeshi yake mashariki mwa nchi hiyo kufuatia mapigano mapya yaliyotokea huko.

Beni Demokratische Republik Kongo Blauhelmsoldaten 23.10.2014 (Alain Wandimoyi/AFP/Getty Images)
Umoja huo wa Mataifa haukufafanua ni wanajeshi wangapi waliopelekwa Kivu Kusini, Mashariki mwa Congo kwa sababu ya wasiwasi wa kimkakati. Kutokana na kupunguzwa kwa bajeti, tume ya kulinda amani ya Umoja wa Mataifa, Monusco walilazimika kufunga baadhi ya maeneo yake Mashariki mwa Congo mapema mwaka huu.
Hata hivyo msemaji wa jeshi la Congo amesema kwa siku kadhaa sasa, wanajeshi wamekuwa wakipambana na wanamgambo karibu na mji wa Uvira mpakani na Burundi. Kapteni Dieudonne Kasereka hakutoa maelezo mengine yoyote juu ya majeruhi. Makundi mengi ya wanamgambo yanafanya kazi zake Mashariki mwa Congo wakipigania maeneo yaliyotajiri kwa rasilimali ya madini. 
Huku hayo yakiarifiwa jeshi la wanamaji lilipambana na wanamgambo katika ziwa Tanganyika. Mapigano hayo kati ya wanamgambo wa Mai Mai Yakutumba na vikosi vya serikali ya Congo yalianza mapema wiki hii nje kidogo ya mji wa Uvira karibu na mpaka wa Burundi. Hali ya wasiwasi imezidi kuongezeka tangu Rais Joseph Kabila alipokataa kuondoka madarakani baada ya muda wake kumalizika Desemba mwaka uliopita.
"Tangu saa kumi na moja asubuhi kumekuwepo na makabiliano ya risasi kati ya jeshi na wanamgambo wa Mai Mai mjini Uvira," alisema Lubungula Dem's M'Sato, mwanachama wa kundi la kutetea amani mjini Uvira, mji wa pili kwa ukubwa katika mkoa wa Kivu Kusini.
Jeshi lawarudisha nyuma wapiganaji
Kwa upande wake msemaji wa jeshi Louis-Claude Tshimwanga amesema jeshi la Congo pia limefanikiwa kuwasogeza nyuma wanamgambo hao waliokuwa katika maboti ziwani Tanganyika, huku akitoa hakikisho kwamba vikosi vya serikali bado vinadhibiti eneo la Uvira. Ziwa Tanganyika lina urefu mkubwa na kupakana na Burundi, Tanzania na Zambia.
Kongo Lusenda MONUSCO Flüchtlingslager burundische Flüchtlinge (MONUSCO/Abel Kavanagh)
Kambi ya wakimbizi ya Warundi ya Lusenda, Kivu Kusini, katika fukwe za ziwa Tanganyika
"Wanamgambo walijaribu kuushambulia mji wa Uvira kupitia ziwa Tanganyika, walikuwa na maboti yaliyokuwa yanakwenda kwa kasi," alisema mtu mmoja aliyeshuhudia kisa hicho ambaye hakutaka jina lake litajwe, akiongeza kuwa aliona maboti sita ya wanambambo hao. Amesema jeshi la wanamaji lilifanikiwa kukamata boti moja kati ya hayo sita. Aidha Mai-Mai Yakutumba, waliundwa mwaka 2007 na mwanamgambo mmoja aliyenyimwa nafasi ya kujishirikisha katika jeshi la kitaifa la Congo. Kundi hilo pia limeanzisha kundi kubwa la wafanyibiashara haramu wa madini ya dhahabu karibu na Ziwa Tanganyika.
Wiki hii katika taarifa iliyowekwa katika mitandao ya kijamii kiongozi wa kundi hilo la wanamgambo  William Yakutumba amesema vikosi vyake vinapinga kile walichokiita matumizi mabaya auusimamizi mbaya wa rasilimali asilia za nchi na kushindwa kuachia madaraka baada ya kipindi chake kikatiba kumalizika.  Maeneo yaliyotajiri kwa madini Mashariki ya Congo yamekuwa yakikumbwa na vita vya kikabila na kwa zaidi ya miongo miwili Congo imekubwa na machafuko yaliyosambaa nje ya nchi.  Eneo hilo la Mashariki mwa Congo ni mzalishaji mkubwa wa ,madini ya Cobalt inayotumiwa katika simu na vifaa vyengine vya elektroniki.