Monday, August 7

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA


Simu: 255 22 2460735/2460706
FAKSI: 255 22 2460735/2460700 S.L.P. 3056
Barua pepe: met@meteo.go.tz DAR ES SALAAM
Tovuti: www.meteo.go.tz
Unapojibu tafadhali nakili:
Kumb. Na.: TMA/1622 07 Agosti, 2017
Taarifa kwa Umma:

TUKIO LA KUPATWA KWA MWEZI LEO JIONI YA TAREHE 7 AGOSTI, 2017

Kupatwa kwa mwezi ni tukio linaweza kutokea mara kadhaa kwa mwaka na halina athari yoyote kwa hali ya hewa.
Tukio hili hutokea pale Dunia, katika mizunguko yake, inapokuwa kati ya Jua na Mwezi; hali hii husababisha Dunia kuikinga miali ya Jua ielekeayo katika mwezi na hivyo kivuli cha Dunia kuonekana katika Mwezi. Ikiwa kivuli cha Dunia kitaonekana katika upande mmoja wa Mwezi basi hali hii huitwa kupatwa kiasi kwa Mwezi (yaani partial lunar eclipse). Kwa upande mwingine, ikiwa kivuli chote cha Dunia kitaonekana katika uso wa Mwezi basi hii huitwa kupatwa kamili kwa Mwezi (yaani total lunar eclipse).
Kwa ujumla kupatwa kwa Mwezi huwa hakuna athari kubwa katika hali ya hewa. Hata hivyo, kutokana na Mwezi, Dunia na Jua kukaa katika mstari mmoja, nguvu za uvutano huongezeka na hivyo kuweza kusababisha maji ya bahari kupwa na kujaa kwa kiasi kikubwa kuliko ilivyo kawaida.
Jioni ya leo tarehe 7 Ogasti 2017, kati ya saa 2:22 hadi saa 4:18 usiku, Mwezi unatarajiwa kupatwa kiasi (yaani partial lunar eclipse) ambapo kilele chake kinatarajiwa kuwa saa 3:20. Hali hii inatarajiwa kuonekana kutoka katika maeneo mengi ya Dunia ikiwemo yote ya Tanzania.
Kama ilivyoainishwa hapo awali, kwa ujumla hali hii huwa haina athari kwa hali ya hewa ila tu uwezekano wa maji ya bahari kupwa na kujaa kwa kiasi kikubwa kuliko ilivyo kawaida.
Imetolewana
Mamlakaya Hali yaHewa Tanzania.

MTANZANIA ALPHONCE SIMBU ASHIKA NAFASI YA TATU MBIO ZA DUNIA JIJINI LONDON



MTANZANIA Alphonce Felix Simbu amefanikiwa kunyakua medali ya Shaba baada ya kushika nafasi ya tatu katika mbio za dunia za IAAF zinazoendelea kufanyika nchini Uingereza katika Jiji la London.
Simbu ameshika nafasi ya tatu nyuma ya Mkenya aliyeshika nafasi ya kwanza akifuatiwa na Muethiopia aliyeshika nafasi ya pili.
Akitumia masaa 2 na dakika 10 Simbu aliweza kushika nafasi ya tatu baada ya kumpita Mkenya mwingine aliyekuja kushika nafasi ya tano.
Hii inakuwa ni kwa mara ya kwanza kwa Simbu kushika nafasi ya tatu baaada ya mwaka jana katika mbio ndefu za  London Marathonaliweza kushika nafasi ya tano.

USAJILI WANACHI VITAMBULISHO VYA TAIFA WAPAMBA MOTO VIWANJA VYA NGONGO MKOANI LINDI


 Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Bw. Deodatus Alexander akimkabidhi kitambulisho chake Bw. Abrahman Mohamed Mussa, akiwa miongoni mwa wananchi waliokamilisha taratibu za Usajili na kukabidhiwa Vitambulisho vyao wakati wa maonyesho ya Nanenane yanayoendelea kwenye viwanja vya Ngongo Lindi.
 Baadhi ya wananchi wakikamilisha taratibu za Usajili kwa kuchukuliwa alama za vidole, picha na saini ya Kielektroniki wakati wa maonyesho yanayoendelea Viwanja vya Ngongo Lindi.
 Wananchi wa Manispaa ya Lindi wakipata maelezo ya taratibu za Usajili toka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bi.Rose Mdami wakati maonyesho ya Nanenane yakiendelea mkoani Lindi.
 Wananchi wakiendelea kusubiria kupata huduma ya Usajili kwenye banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) mkoani Lindi.

 Bi Khadija Khalid mtaalamu wa mifumo ya Komputa mkoani ofisi ya NIDA Lindi, akitoa elimu kuhusu mfumo wa Utambuzi na Usajili wa Taifa kwa wananchi waliofika kujifunza kwenye Banda la NIDA.
 Baadhi ya wananchi wakisubiri kupata huduma kwenye banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa wakati wa maonyesho ya Kilimo Nanenane yanayoadhimishwa kitaifa mkoani Lindi.
 Maafisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakiendelea kutoa huduma kwa wananchi waliofika kutembelea Banda la Mamlaka hiyo viwanja vya Ngongo Lindi.
Hawa ni baadhi tu ya wananchi wakihakikiwa na Afisa wa Idara ya Uhamiaji Bw.Kudrack Kuvagwa kabla ya kuchukuliwa alama za Kibaiolojia, picha na Saini ya Kielektroniki.

USAJILI WANACHI VITAMBULISHO VYA TAIFA WAPAMBA MOTO VIWANJA VYA NGONGO MKOANI LINDI


 
Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa Bw. Deodatus Alexander akimkabidhi kitambulisho chake Bw. Abrahman Mohamed Mussa, akiwa miongoni mwa wananchi waliokamilisha taratibu za Usajili na kukabidhiwa Vitambulisho vyao wakati wa maonyesho ya Nanenane yanayoendelea kwenye viwanja vya Ngongo Lindi.


 
Baadhi ya wananchi wakikamilisha taratibu za Usajili kwa kuchukuliwa alama za vidole, picha na saini ya Kielektroniki wakati wa maonyesho yanayoendelea Viwanja vya Ngongo Lindi.


 
Wananchi wa Manispaa ya Lindi wakipata maelezo ya taratibu za Usajili toka kwa Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Bi.Rose Mdami wakati maonyesho ya Nanenane yakiendelea mkoani Lindi.



 
Wananchi wakiendelea kusubiria kupata huduma ya Usajili kwenye banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) mkoani Lindi.




 Bi Khadija Khalid mtaalamu wa mifumo ya Komputa mkoani ofisi ya NIDA Lindi, akitoa elimu kuhusu mfumo wa Utambuzi na Usajili wa Taifa kwa wananchi waliofika kujifunza kwenye Banda la NIDA.



 Baadhi ya wananchi wakisubiri kupata huduma kwenye banda la Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa wakati wa maonyesho ya Kilimo Nanenane yanayoadhimishwa kitaifa mkoani Lindi.


 
Maafisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wakiendelea kutoa huduma kwa wananchi waliofika kutembelea Banda la Mamlaka hiyo viwanja vya Ngongo Lindi.



Hawa ni baadhi tu ya wananchi wakihakikiwa na Afisa wa Idara ya Uhamiaji Bw.Kudrack Kuvagwa kabla ya kuchukuliwa alama za Kibaiolojia, picha na Saini ya Kielektroniki.

VETA YAGUNDUA KIFAA CHA KULAZIMISHA MADEREVA WA PIKIPIKI KUVAA KOFIA NGUMU



Mkuu wa wilaya ya Newala, Aziza Mangosongo, akitembelea banda la VETA katika maonesho ya Kilimo 2017 yanayoendelea mkoani Lindi katika viwanja vya Ngongo ambapo alipongeza VETA kwa kuweka fursa nyingi za mafunzo ya ujuzi kwa makundi mbalimbali ya wananchi. Aliahidi kushirikiana na VETA ilikuwa wezesha wananchi wilaya ni kwake kunufaika pia na fursa mbalimbali za mafunzo ya ufundi stadi. 



Wanafunzi wa shule ya sekondari Medi ya mkoani Mtwara wakipata maelekezo juu ya aina ya mafunzo yanayotolewa katika vyuo vya ufundi Stadi walipotembelea banda la VETA katika Maonyesho ya kilimo ya Nanenane yanayofanyika kitaifa katika viwanja vya Ngongo Mkoani Lindi.



Mwalimu wa Elektroniki wa Veta Kipawa, Aneth Mganga akiwapa maelezo wananchi waliotembelea banda la VETA Pikipiki inayoendeshwa ni lazima dereva awe amevaa kofiangumu.



Wananchi wakipata maelezo ya jiko la mafuta ya taa ambalo limebuniwa kwa kutotumia mafuta mengi na halina moshi.





Baadhi ya wananchi waliofika kutembelea banda la VETA ili kuweza kupata taarifa mbalimbali kuhusianana VETA pamoja na kuaangalia teknolojia mbalimbali.


Na Chalila Kibuda,GlobuyaLindi 

Katika kukabiliana na changamoto za madhara ya ajali za pikipiki yanayosababishwa na madereva kutovaa kofiangumu (helmet), Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) imebuni teknolojia ya kukabiliana na hilo. 

Mwalimu wa fani ya elektroniki kutoka VETA Kipawa, AnethMganga, amebuni mfumo wa kielektroniki unaozuia pikipiki kuwa kampaka dereva awe amevaa kofiangumu (helmet). 

Akizungumza na katika viwanja vya maonesho ya Nanenane Ngongo, mkoani Lindi, mwalimu Aneth amesema mfumo huo ukianza kutumika na madereva wa pikipiki utapunguza madhara endapo kunatokea ajali kwa kuwa bila ya kuvaa kofiangumu pikipiki haiwaki na hata ukiwa katika mwendo ikitokea ukavua kofiangumu pikipiki itazimika. 

Aidha, katika usalama barabarani inasaidia kuzuia wizi wa pikipiki kwani mwizi hatoweza kuiwasha bila kofiangumu ambayo imeunganishwa kieletroniki. 

Aneth amesema anaendelea kufanya utafiti nakuboresha zaidi ubunifu huo, lakini ameomba serikali na wadau mbalimbali kuunga mkono ili uweze kuenea, kukubalikana kutumika na waendesha pikipiki katika maeneo mbalimbali nchini.

WAKANDARASI NCHINI WAKABILIWA NA CHANGAMOTO MBALIMBALI



Picha ikimuonesha Mkandarasi kutoka Kampuni ya Caberisa Co.Ltd Bernad Mgohamwende, ambaye anajenga barabara kwa kiwango cha changarawe yenye urefu  wa kilomita 36, eneo la barabara ya mbauda ,Osunyai Mkoani Arusha iko katika hatua za mwisho kukabidhi (Picha na Pamela Mollel)

Wakandarasi nchini bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upitaji wamagari makubwa bila ya kuwa na vipimo maalum ambapo hali hiyo imekuwa ikiharibu miundombinu ya barabara ambapo wamekuwa wakitumia gharama kubwa ya kufanya marekebisho mbalimbali ya kabla ya kukabidhi barabara hizo kwa Serikali.

Hayo yameelezwa leo na mmoja wakandarasi kutoka Kampuni ya Caberisa Co.Ltd Bernad Mgohamwende am,bae anajenga barabara kwa kiwango cha changalawe yenye ukubwa wa kilomita 36 eneo la barabara ya mbauda ,Osunyai iko katika kiwango cha changarawe ambapo yuko katika hatua za mwisho kukabidhi ambapo iko katika wilaya ya Arusha,Mkoa wa Arusha.

ALiongeza kuwa katika kutekelezaji wa kujenga barabara hizo ,Serikali itaweka utaratibu wa kupima magari hayo itawasaidia kuweza kutunza barabara hizo na kuweza kutotumia gharama kubwa kwa wakandarasi .

Kwani Serikali italazimika kutoa pesa za mara kwa mara kuwalipa wakandarasi kwa ajili ya kufanya marekebisho ambapo hali hiyo inawatia hasara Serikali na kuwa na matumizi mabaya ya pesa hizo.

Hata hivyo ameitaka Serikali kuweza kutenga maeneomaalumu ya kuweza kupatikana kwa madini ya udongo na mchanga ili kuwezwsha wkandarsi kupata madini hayo kwa urahisi kwani hivi sasa wanapata changamoto kubwa katika udongo huo..

Aliongeza kuwa hivi sasa wananunua udongo huo kwa wananchi ambapo wamekuwa wakiwauzia kwa gharama kubwa hali ambayo imekuwa ikiwagharimu pesa nyingi ukilinganisha na hali halisi..

Kwa upande wake meneja wa Tanroad Mkoa wa Arusha Mhandisi John Edward Kalupale alisema kuwa kuhusu suala hilo la upitaji wa magari makubwa katika barabara inayijengwa ya Mbauda Osunyai ambapo alisema kuwa kisheria hawaruhusiwi kuweka mizani kutokana na kuwa na barabara hiyo kutokuwa na lami. ambayo hivi sasa iko kiwango cha changalawe.

Aliongeza kuwa wasafirishaji ni waharibifu lakini wapende nchi yao na kuwa makini katika kutumia barabara zinzoboreshwa kwa viwango vyote kuanzia changarawe mpaka lami kwani maendeleo yoyote yale yanaletwa na uboreshaji wa miundo mbinu ya barabara zote.

Ambapo katika barabara hiyo ya osunyai mbauda wamekuwa yakipita magari makubwa ambayo yanajaza michanga na udongo kupita kiasi na pia wanachanganya watu na michanga hhiyo hali ambayo imekuwa ikiharibu barabara hiyo badala yake amewataka madereva wawe wazalendo katika kutumia barabara hizo ili kuweza kuleta manufaa zaidi kwa watumiaji wote ili kuweza kuzitunza na kuepusha serikjali kuweza kutumia pesa nyingi katika kujenga barabara hizo.

Mhandisi John alisema kuwa arusha bado kunakabiliwa na changamoto kubwa ya ardhi lakini wanafata taratibu za kuwezesha kupatikana kwa ardhi ilikuweza kuepuka kupata madini udongo pindi wakandarasi hao wanapohitaji kupata malighafi ya kutekeleza miradi wanyopewa na serikali.

Katika kuweza kupata ufumbuzi wakudumu wapo katika hatua za awali ambapo upembuzio yakinifu wa kina unaendelea katika mhandisi mshauri unaendelea.

Ambapo wanatarajia kuweka lami kilomita 400 kuanzia barabara ya Arusha,osunyai .olkesimate mpaka dosidosi Kongwa ili kuweza kumaliza changamoto mbalimbali zilizoko .
Kwa upande wake dereva wa daladala kutoka mbauda mpaka Olkesimati Erasto Msuya alisema kuwa marekebisho hayo ya barabara yasmewarahisishia sana katika kupeleka abiria hao katika maeneo hayo kwa kabla ya marekebisho hayo walikuwa wanapata tabu na changamoto kubwa sana katika kuweza kutumia na kupelekja abiria eneo hilo.

Anapongeza sana Serikali ya awamu ya tano katika kujenga miundombinu ya barabara na kuboresha maeneo ya barabara mbalimbali nchini.

WAZIRI WA KILIMO, MIFUGO NA UVUVI MHE. DK.CHARLES TIZEBA ASISITIZA MATUMIZI YA TAARIFA ZA HALI YA HEWA KWA MANUFAA YA KILIMO NCHINI



 Mhe. Dkt. Tizeba akisisitiza umuhimu wa taarifa za hali ya hewa kwa wakulima alipotembelea banda la Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), anayezungumza nae ni Mkurugenzi wa utafiti na matumizi ya taarifa za hali ya hewa Dkt. Ladislaus Chang'a



 Mkurugenzi wa utafiti na matumizi ya taarifa za hali ya hewa Dkt. Ladislaus Chang'a akitoa maelezo ya umuhimu wa matumizi sahihi ya taarifa za hali ya hewa kwa waziri wa kilimo, mifugo na uvuvi



  Baadhi ya wageni mbalimbali wanaoendelea kutembelea banda ili upata elimu juu ya umuhimu wa taarifa za hali ya hewa na jinsi ya kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa



Mhe. Dkt Tizeba akiteta jambo na Mkurugenzi wa utafiti na matumizi ya taarifa za hali ya hewa Dkt. Ladislaus Chang'a na Meneja wa Kanda ya Kusini  wa TMA Bw. Amas Daudi

RAIS DKT MAGUFULI ATEMBELEA VIWANDA JIJINI TANGA, ATOA MAAGIZO MAZITO KWA WAZIRI MWIJAGE


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na wafanyakazi alipowasili  kufungua rasmi  kiwanda cha Saruji cha Kilimanjaro maeneo ya Maweni jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akifunua kitambaa  kufungua rasmi  kiwanda cha Saruji cha Kilimanjaro maeneo ya Maweni jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe kufungua rasmi  kiwanda cha Saruji cha Kilimanjaro maeneo ya Maweni jijini Tanga leo Agosti 6, 2017 
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipatiwa maelezo ya uzalishaji baada ya kufungua rasmi  kiwanda cha Saruji cha Kilimanjaro maeneo ya Maweni jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na uongozi wa kiwanda baada ya kufungua rasmi  kiwanda cha Saruji cha Kilimanjaro maeneo ya Maweni jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea risala toka kwa uongozi wa kiwanda kwenye sherehe za kuweka  jiwe la msingi upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017 
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Mwijage wakifunua kitambaa kama ishara ya kuweka jiwe la msingi upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea na mwandishi wa habari wa TBC Bi. Vumilia Mwasha baada ya kuweka jiwe la msingi upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitembezwa maeneo mbalimbali baada ya kuweka  jiwe la msingi la upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akitembelea kibanda cha maziwa bada ya  kuweka jiwe la msingi upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akigawa maziwa na mtindi kwa wanahabari  katika  kibanda cha maziwa baada ya  kuweka jiwe la msingi upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akigawa maziwa na mtindi kwa wanahabari  katika  kibanda cha maziwa baada ya  kuweka jiwe la msingi upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimgawaia maziwa na mtindi Mstahiki Meya wa Jiji la Tanga Alhaji Mustapha Selebosi   katika  kibanda cha maziwa baada ya  kuweka jiwe la msingi upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akigawa maziwa na mtindi kwa watoto katika  kibanda cha maziwa baada ya  kuweka jiwe la msingi upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungia wanannchi baada ya kugawa maziwa na mtindi kwa watoto katika  kibanda cha maziwa baada ya  kuweka jiwe la msingi upanuzi wa kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh  maeneo ya Kange jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na mkewe Mama Janeth Magufuli wakicheza ngoma ya Baikoko wakati wa sherehe za uwekaji wa jiwe la msingi wa matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungia wananchi na wafanyakazi kwenye sherehe za uzinduzi wa matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipungia wananchi na wafanyakazi kwenye sherehe za uzinduzi wa matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea risala kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji wa  GBP Bw. Badar Sood kwenye sherehe za uzinduzi wa matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na  Mkurugenzi Mtendaji wa  GBP Bw. Badar Sood kwenye sherehe za uzinduzi wa matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine wakikata utepe kwenye sherehe za  uzinduzi wa wa matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine akifunua kitambaa kwenye sherehe za  uzinduzi wa  matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Mama Janeth Magufuli na Waziri wa Afya Mhe Ummy Mwalimu wakifurahia jambo kwenye sherehe za  uzinduzi wa  matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga  ngoma ya Baikoko wakati wa sherehe za uzinduzi wa matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga  ngoma ya Baikoko wakati wa sherehe za uzinduzi wa matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipiga  ngoma ya Baikoko wakati wa sherehe za uzinduzi wa matanki ya kuhifadhia mafuta ya kampuni ya GBP yenye ujazo wa lita 300,000 eneo la Raskazone jijini Tanga leo Agosti 6, 2017. Picha na IKULU

MASAUNI APOKEA VIFAA VYA TAMASHA LA USALAMA BARABARANI LITAKALOFAYIKA AGOSTI 12, MWAKA HUU UWANJA WA TAIFA



Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani, Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akipokea moja ya tisheti zitakazovaliwa Siku ya Tamasha la Usalama Barabarani kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Wateja Binafsi na Mauzo wa Benki ya NMB, Omari Mtiga (kushoto), wakati wa makabidhiano yaliyofanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam. Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi



Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani, Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akipokea moja ya tisheti zitakazovaliwa Siku ya Tamasha la Usalama Barabarani kutoka kwa Meneja Masoko wa Kampuni ya Bakhresa, Omary Kuwe (kushoto) wakati wa makabidhiano yaliyofanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam. Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli



Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani, Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni, akipokea moja ya tisheti zitakazovaliwa Siku ya Tamasha la Usalama Barabarani kutoka kwa Mwakilishi wa Kampuni ya Bin Slum, wakati wa makabidhiano yaliyofanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam. Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli



Mwenyekiti wa Taifa wa Baraza la Usalama Barabarani, Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia), akizungumza na Vyombo vya Habari baada ya kupokea vifaa kutoka Kampuni mbalimbali zilizojitokeza kudhamini Siku ya Tamasha la Usalama Barabarani litakalofanyika Agosti 12 katika Uwanja wa Taifa, ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dkt. John Magufuli. Kulia ni Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Fortunatus Musilimu. Makabidhiano hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam.



Meneja Masoko wa Kampuni ya Bakhresa, Omary Kuwe (kushoto) akizungumza na Vyombo vya Habari baada ya kukabidhi vifaa kwa ajili ya udhamini wa Siku ya Tamasha la Usalama Barabarani litakalofanyika Agosti 12 katika Uwanja wa Taifa, ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli. Makabidhiano hayo yamefanyika katika Ukumbi wa Wizara hiyo, jijini Dar es Salaam.