Monday, July 17

Wanafunzi 10 waliofanya vizuri zaidi kitaifa katika matokeo ya kidato cha nne 2016/2017.


Baraza la Mitihani nchini (NECTA) limetangaza matokeo ya kidato cha nne ambapo ufaulu umeongezeka kutoka asilimia 67.91 mwaka 2015, hadi kufikia asilia 70.35 mwaka 2016 huku shule 6 za Dar es Salaam zikifanya vibaya.
Wanafunzi 10 waliofanya vizuri kitaifa.

TABORA..Muuguzi Amchoma Binti Sindano ya Usingizi na Kumbaka.....

MUUGUZI anayefanya kazi Kituo cha Afya Kata ya Igurubi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Damian Mgaya (26) anashikiliwa na Polisi kwa tuhuma ya kumbaka binti wa miaka 18 mkazi wa Kitongoji cha Mwagala B, Kijiji cha Mwagala.

Mtendaji wa Kata ya Igurubi, Ntemi James alisema uhalifu huo umefanyika Julai 14, mwaka huu saa 8 hadi alfajiri wakati binti huyo akimuuguza mama yake, Tatu Simbi ambaye amelazwa katika kituo hicho cha afya baada ya kushambuliwa kwa kipigo na mume wake. James alidai mtuhumiwa alimpokea mama wa binti huyo akiwa hoi na ndipo alimpatia matibabu kisha kumlaza katika kituo hicho cha afya huku akimchoma sindano ya usingizi ambayo ilisababisha mama huyo kupitiwa na usingizi.

Mtendaji huyo alidai kuwa muuguzi Damian alipoona mama wa binti huyo amelala, alimwambia waende wote chumba kingine ili akachukue dawa ya mama yake; lakini hata hivyo hakumpa dawa na badala yake alimwambia amchome sindano ili asipate maradhi kwa kuwa mazingira ya hospitali sio mazuri. Baada ya kuambiwa hivyo, binti huyo alikubali kuchomwa sindano mbili na alipochomwa sindano ya kwanza aliishiwa nguvu na alipochomwa sindano ya pili alianguka na kupitiwa na usingizi hadi asubuhi.

Alisema baada ya kuona amelala pasipokuwa na fahamu, muuguzi huyo alianza kumbaka hadi alfajiri alipoamshwa na mama yake huku yeye akiwa hajitambui kutokana na maumivu aliyokuwa akiyasikia sehemu zake za siri na mwili wote. Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya ya Igunga, Bonaventura Kalumbete alithibitisha kubakwa kwa binti huyo na muuguzi huyo na kueleza kuwa baada ya kupata taarifa hiyo, alituma timu ya wataalamu ambayo ilibaini binti huyo kubakwa na amelazwa kwenye kituo hicho na hali yake ni mbaya kwani hawezi kutembea.

Aidha, Dk Kalumbete alisema uchunguzi wa awali unaonesha binti huyo alichomwa sindano wakati alikuwa hata haumwi na hizo dawa nazo zimechangia kumsababishia kushindwa kutembea huku akiahidi kuwa baada ya uchunguzi, muuguzi huyo atachukuliwa hatua kali za kisheria.

Mkuu wa Wilaya ya Igunga ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya, John Mwaipopo alikiri kukamatwa kwa muuguzi baada ya kupokea taarifa ya kubakwa kwa binti huyo, alimwagiza Mkuu wa Polisi Igunga kumkamata muuguzi huyo Damian Mgaya ili afikishwe kwenye vyombo vya sheria.

Hamad Rashid Awaponda Tena Chadema na CUF, Adai Wanaweweseka tu Hakuna ‘Ukawa Wala Upawa’


Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi wa Zanzibar Hamad Rashid ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) ameirudia kauli yake aliyoitoa kipindi cha Bunge la Katiba mwaka 2014 kuwa Hakuna “UKAWA wala UPAWA”


Akizungumza Jumapili hii Jijini Dar Salaam Katika kuelekea kuadhimisha miaka mitano ya chama hicho AgostI 22 mwaka huu, Waziri Hamad Rashidi ameeleza kuwa kipindi cha Bunge la Katiba aliposema kuwa Hakuna UKAWA wala UPAWA baadhi ya watu walimcheka lakini kwasasa matokeo yake yanaonekana kwa kile kinachoendelea ndani ya vyama vya siasa ikiwemo mgogoro wa CUF ambao imefikia hatua unaingiliwa na chama kingine cha upinzani ikiwemo CHADEMA.

Waziri Hamad Rashidi amefafanua kuwa “Jambo lolote ambalo halipo katika misingi ya kikatiba na kisheria haliwezi kupiga hatua” jambo ambalo limetokea kwa UKAWA kwasababu haikuwa kikatiba wala kisheria jambo lililopelekea migogoro katika uchaguzi wa mwaka 2015 ambapo baadhi ya maeneo walishundwa kuelewana na kusimamisha wagombea wao kwa kila chama kinyume na matakwa ya kuungana kwao.

Katika hatua nyingine ADC ameviomba vyama vya siasa vyenye migogoro kuiga mfano wa chama hicho kwa kutatua migogoro yao kwa amani na kuwataka wafuate misingi ya Mwenyezi Mungu ambaye ameamrisha kusamehana pindi inapotokea tofauti miongoni mwa watu.

“Namshangaa binadamu ambaye anakataa suluhu maana hata siku ya mwisho mlango wa TOBA ndiyo utakao kuwa wa mwisho kufungwa hivyo kiushi bila kusamehana ni kumkosea Mwenyezi Mungu” Alisema Waziri Hamad Rashid

Katika hatua nyingine Waziri Hamad Rashid ameeleza kuwa ADC imeendelea kufanya kazi kwa ukaribu na jamii kwa kuanzisha vikundi mbalimbali vya VICOBA bila riba na kutoa mafunzo mbalimbali ambayo yamewasaidia watanzania wengi ambao walikuwa wamepoteza matumaini.

Ni nini kipya CCM imefanya tangia 2015 ? Ndo yale Mw. Nyerere alisema, msiposimama na kuwa wamoja na kutakaa upuuzi, tutatawaliwa na Madikteta. Sisi tunakubaliana na kauli ya Mw Nyerere na tunasema Chadema na UKAWA 2020 !


Wapendwa Niwasalimu wote kwa jina la Bwana;

Na kwa wana Chadema na Ukawa- People’s Power !
Nina maoni machache tu kutokana na yanayondelea sasa:

Tuko pamoja kama watanzania kuhakikisha haki inapatikana kwa viongozi wetu wote wa Chadema na Ukawa. Isiwapeni tabu kwa maana Bwana Yupo pamoja nasi.

Mungu hapimi kwa mambo ya nje, au yale yanayofanyika nje, anapima mioyo yetu. Na yote anayashuhudia ya kwamba Chadema inafanya mema na tutatunikiwa zawadi yetu.

Sihitaji kutoa mifano mingi maana najua tayari mifano mingi mnaijua; viongozi wengi duniani hata kwenye Biblia walikamatwa na watu waovu kwa kusimamia ukweli tu nay ale wanayoamini. Na tukaona mwisho wa siku Baraka na mavuno makubwa ya ushindi waliopata. Hivo kazeni buti, ushindi ni wa kwetu 2020.

Kuhusu hao madiwani wa Chadema wanafiki, waacheni maana CCM hawawezi kuwanunua wananchi wapiga kura. Wananchi watakula pesa zao nab ado kupigia Chadema. Kwanza imekuwa vizuri wamejiondoa mapema ili tujua mapema nani ni msaliti na asiuze siri cha chama.

Kama mnakumbuka Nigeria, kwenye uchaguzi wa 2015, Chama kilichokuwa madarakani kilihonga mabilioni ya pesa kwa wanasiasa na vyama vya upinzani. Zote zikaliwa na alishinda alikuwa ni Buhari wa Upinzani.

Kwa hiyo kuhonga kwa sisi wakisto haijalishi, tena hasa ni mbaya maana ni machukizo kwa Mungu. Hivo CCM wanazidi kujipalia makaa ya moto kama kweli wanawanunua hawa Madiwani wa Chadema kwa pesa zetu sisi watanzania.

Ni Dhahiri kwamba hao madiwani wa Chadema waliokuwa wasaliti hawajitambui na hawatumii akili na nitawaambia kwa namna zipi:

· Watawezaje kuunga mkono Raisi kwa kuacha kazi waliotumwa na Wananchi.

· Watawezaje kuunga mkono chama ambacho kimewadhalilisha na kuwaonea miaka yote hii.

· Watawezaze kuunga mkono Raisi anayevunja sheria za nchi na kutofata katiba.

· Wanawezaje kuunga mkono uovu wote unaofanywa na CCM, na wanaona kila siku Chadema ndio wanaoibua uozo wa CCM bungeni.

· Wanawezaje kuunga mkono chama cha CCM kinacho abuse power kama Bashite na Raisi hafanyi kitu.
Wanawezaje kuunga mkono CCM ambayo imewadhalilisha CUF Zanzibar, kutumia nguvu kupiga na hata kuuwa watu kukaa tu madarakani.

· Wanawezaje kuunga mkono chama ambacho kinashuhudia utekaji wa wana Chadema wenzao wakina Ben Sanane mpaka leo hatujui walipo, leo wanaunga mkono hicho chama.

· Wanawezaje kuunga mkono CCM inayokamata viongozi wa chadema kama Lowassa, Halima, na Wakina Lissu, na kuwaharibia mashamba wakina Mbowe.

Kibiti imewashinda, kuna mauaji kila siku, wako busy na wapinzani. Ndo sasa unapata kuona namna gani uongozi uliopo madarakani Tanzania haupo serious na kuwalinda wananchi, bali kuwalinda mafisadi wakina Tibaijuka na Chenge. Halafu wanaleta geresha za kurudisha milion 50 wakati mapapa wakubwa wanawalinda.

Na bado mtu mzima mwenye akili zake timamu anaunga mkono haya?

Ni nini kipya mabacho Magufuli kafanya tangia kaingia madarakani? Zaidi tu ya kuzidi kuvunja sheria na kuzidi watu kuonewa, kutekwa na kunyamazishwa?

Hata yale ambayo wanafikiri Magufuli kafanya au anafanya, mtu yeyote mwenye akili akiangalia ataona ni yale yale ambayo Chadema imekuwa ikiyapigia kelele kwa miaka yote. Ni aliye na uwelewa mdogo sana ataunga mkono CCM kwa sasa, maana hata CCM pia wameamka na ndani yao wanaona tofauti zao.

Hata hiyo ya watoto wanaopata mimba, in fact iko kinyume hata na ilani ya CCM. Sasa sieliwi hao wanaounga mkono CCM wanaunga mkono kitu gani ?

Lakini hii ndio inatufanya tuelewe ya kwamba ile ripoti ya TWAWEZA ilisema ukweli, ya kwamba watu wanaounga mkono CCM hawajielewi. Maana haiwezekani CCM inafanya uovu wote huo juu niioeleza na mwengine mwingi amabo Lissu aliuongea kuhusu rushwa, nab ado watu wanaunga mkono.

Chadema na Ukawa peke yao ndo wameibua kila uozo wa CCM, kila siku inasikia scandal za CCM kupitia Chadema na UKAWA halafu leo hii tunashangaa eti CCM wanapambwa na maua. Yaani kweli ni rushwa tupu maana mtu mwenye akili anaweza kabisa ona wazi CCM wamekwisha.

Basi niishie hapo:
Endeleeni na mapambano, kijiji hadi kijiji, endeleeni kuvuna wanachama, mkiendelea kusimamia haki na kweli. Na Bwana Yupo nasi kuhakikisha CHADEMA na UKAWA inaingia madarakani 2020. Hao CCM Waendelee kuhonga tu, wananchi watakula hela na mwisho wa siku watachagua Chadema manake watu wanaakili siku hizi na Mungu ndiye mwamuzi wa mwisho wala sio NEC.

Msikubali Hongo ya namna yoyote ile kama alisevosema mwenyekiti Mbowe. Msikubali hongo, mtende haki, na kusimama katika kweli maana hayo ndo mapendezo ya Bwana yanayowapeleka madarakani 2020. God has the final say!

Endeleeni kwa kasi kujiimarisha kila kona, mikoa, vijiji na kuwapa elimu wanawake. 

God sees your good work; your reward is coming in 2020.
People Power 2020!

May God Bless you, May God Bless the United Republic of Tanzania.

Kampuni 100 kushiriki maonyesho ya utalii Arusha



Arusha. Zaidi ya kampuni 100 jijini Arusha na mikoa ya jirani zinatarajiwa kushiriki maonyesho ya utalii na viwanda yatakayofanyika kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha AICC jijini hapa kwa mara ya kwanza.
Mkurugenzi Mkuu wa AICC, Elishilia Kaaya, amesema maonyesho hayo yanalenga kukuza sekta ya utalii na viwanda ili kufikia azma ya serikali ya awamu ya tano ya uchumi wa viwanda. 
Akizungumza leo Jumatatu, Julai 17, Kaaya amesema kuwa, ukumbi huo umegharimu Sh 3.2 bilioni, fedha ambazo ni mkopo kutoka Benki ya NBC.
Kaaya ameongeza kuwa, ukumbi huo wa maonyesho na   mikutano utazinduliwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Augustino Mahiga, Julai 20 mwaka huu .
"Ukumbi huo mpya ambao una uwezo wa kuchukua waonyeshaji wa biashara wa kimataifa 2000 umejengwa kutokana na hitaji la Arusha la kutokuwa na ukumbi wowote maalumu wa maonyesho ya biashara, utaondoa kabisa tatizo la ukosefu wa eneo maalumu la kufanyia shughuli za biashara ya kitaifa na kimataifa mkoani Arusha. "amesema Kaaya. 
Akizungumzia maonyesho hayo Kaaya amesema  yatasaidia kukuza sekta ya viwanda na biashara kwa kuwawezesha wafanyabiashara hao kuonyesha bidhaa zao bure bila gharama yoyote. 
Kaaya, alisema ujenzi wa ukumbi huo ambao umepewa jina la Lake Nyasa, ulianza Aprili 2016 na kukamilika Juni 2017, umejengwa na Kampuni ya Hainan International ya China ambayo ilishinda zabuni.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Miradi na Nyumba wa AICC, Victor Kamagenge, amesema ukumbi huo umejengwa kwa kuzingatia mahitaji ya wananchi wakiwamo walemavu ambapo kuna miundo mbinu maalumu kwa ajili yao.
Alisema kuwa, kuwepo kwa ukumbi huo kutasaidia kuondoa adha ya wafanyabiashara kushindwa kutangaza bidhaa zao ili waweze kupata masoko kutoka ndani na nje ya nchi. 

FORM SIX RESULTS


NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

ACSEE 2017 EXAMINATION RESULTS ENQUIRIES



CLICK ANY LETTER BELOW TO FILTER CENTRES BY ALPHABET


A

B

C

D

E

F

G

H

I

J

K

L

M

N

O

P

Q

R

S

T

U

V

W

X

Y

Z