Friday, March 7

DAR ES SALAAM HAINA MASTER PLAN!!??


Kumbe jiji la Dar-es-salaam halina mpango unaoeleweka wa ujenzi, 
hali inayopelekea jiji kuendelea kukua bila mpangilio maalum, ambao unaendena
na mahitaji ya watu kwa maana ya Idadi pamoja na uwezo wa Miundombinu yake..


Na kweli mitaa yetu angalia hapa parking barabarani watu wanapita humo humo yaani kila kitu kipo kipo tuu


Kariakoo nako hakufai vurugu mechi hujui wapi pa kupita waendao kwa miguu wapi pa magari wapi pa biashara wote wamo humo humo 


Na hii ndio upanga 


Hapa sijui huu ni mtaa wa biashara au ila wamo humo humo


Sehemu zenye nafasi mimi nadhani ni kama hizi tuu keepleft au sijui round about ila majina hayo kwa kiswahili usiniulize 


Cheki jinsi majengo yalivyoumana 




Na umeme umo humo humo well usifikirie hizi nyaya zikianguka juu ya umati huo w watu itakuwaje


Vichochoroni nako tumo tumo tuu biashara madampo kama kawa


Ila ukichoka sehemu za kupumzika ndio kama hizi humo humo zipo


Foleni unatamani gari lingekuwa na mabawa upae humo barabarani ni cheni mtindo mmoja


Wale wa kigamboni wao hubanana humo humo kwenye pantoni




Sijui hata hewa ya oxigen inapita ila tumo humo humo wengi ila hatuna jinsi


Mtaa wa kisutu napo wanajenga humo humo na fikiria sasa zamani zileeee kulikuwa na stendi ya mabasi ya mikoani hapo hapo


Biashara hapo hapo kwa kitaa


Ndio masoko yetu tena humo humo


Wateja hawaji kiivyo ila ndio kutafuta tena masoko


Ila wakija wanatukuta humo humo tunawauzia tuu


Hata Obama alipopitia alitukuta humo humo twajeuka kumpungia halafu tunaendelea na yetu


Mungu awalaze mahala pema wale wote waliotutoka maana na lile lililoanguka lilikuwa humo humo kwa kitaa

Hii ndi Dar Es Salaam