Saturday, September 23

IMARISHENI TAKWIMU ZA UJENZI NCHINI: PROF. MBARAWA


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akihutubia wakati wa ufunguzi wa warsha ya wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), jijini Dar es Salaam.


Wadau wa sekta ya ujenzi wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani), katika warsha ya sekta hiyo kuhusu uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akizungumza jambo na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Ujenzi), Mhandisi Joseph Nyamhanga (kulia), katika warsha ya wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Prof. Mayunga Nkunya (kulia), akifafanua jambo na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto), jijini Dar es Salaam.
Afisa Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Dkt. Samson Mturi akitoa taarifa kwa mgeni rasmi Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani), katika warsha ya wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza hilo, jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (kushoto), akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Huduma za Biashara Bw. Milton Lupa (aliyesimama), kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), wakati alipokagua mradi wa ujenzi wa nyumba za magomeni, jijini Dar es Salaam.
Mkadiriaji Majenzi na Msanifu Majengo Neema Kifua (wa pili kulia), akitoa taarifa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa kuhusu maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za magomeni, alipotembelea mradi huo leo, jijini Dar es Salaam.



Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amewataka wadau wa sekta ya ujenzi kuanza kuweka twakwimu takwimu zinazohusu masuala ya ujenzi hapa nchini.

Akifungua warsha ya wadau wa sekta ya ujenzi kuhusu uboreshaji wa utendaji kazi wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Prof. Mbarawa, amesisitiza umuhimu wa sekta hiyo kuimarisha taarifa za aina, vifaa, viwango vinavyohitajika kimataifa na gharama katika shughuli za ujenzi wa barabara, viwanja vya ndege, nyumba na miundombinu mingine.

“Sekta ya Ujenzi ina mchango mkubwa katika ujenzi wa miundombinu ya kiuchumi na kijamii hivyo uwepo wa taarifa mbalimbali unahitajika ili kurahisisha uelewa wa wananchi wa kawaida katika masuala ya ujenzi na gharama zake”, amesema Prof. Mbarawa.

Aidha, Waziri Prof. Mbarawa amewahakikishia wadau wa sekta ya ujenzi kuwa Serikali itaendelea kuweka mazingira wezeshi ili kuhakikisha sekta hiyo inakidhi matarajio ya watanzania wengi kwa lengo la kuwajengea miundombinu iliyo bora na imara.

Ameongeza kuwa mapendekezo yatakayotolewa na wadau hao yatarahisisha utekelezaji wa miundombiu mbalimbali ambayo italeta chachu kwa sekta nyingine zikiwemo za kilimo, nishati, utalii, viwanda, madini na uendelezaji wa biashara na nchi nyingine za kikanda.

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo (Sekta ya Ujenzi) Mhandisi Joseph Nyamhanga amesema ongezeko la miradi ya ujenzi imechangia Serikali kutafuta wataaalm waliofanya tafiti kwa ajili ya uboreshaji wa baraza hilo wataongeza tija na ufanisi wa sekta hii muhimu ya ujenzi kwa wadau, wananchi na Serikali.

Naye, Mwenyekiti wa Baraza la NCC  Prof. Mayunga Nkunya amemuhakikishia Waziri Prof. Mbarawa kuwa baraza lake litasimamia michango yote itakayotolewa na wadau hao na kuahidi kushughulikia changamoto zinazoikabili NCC ikiwemo za takwimu ili kuhakikisha sekta hiyo inaendelea kukua kwa kuwa ni sekta mtambuko.

Sekta ya Ujenzi ni mojawapo ya sekta zinazokua kwa kasi hapa nchini na ina mchango mkubwa kwa Pato la Taifa ambapo mwaka 2016 sekta hiyo ilichangia asilimia 14 ya Pato la Taifa.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano

DOKTA MPANGO AAGIZA WATUMISHI WA TRA BANDARINI DAR ES SALAAM WAFUMULIWE


Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (wa pili kulia) akiwa katika kikao na Maafisa Waandamizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) alipofanya ziara ya kukagua utendaji ambapo aliwataka kuchukua hatua dhidi ya watumishi wasiowaaminifu wanaolikosesha Taifa mapato stahiki.
Meneja wa Idara ya Forodha, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bandari ya dar es Salaam, Bw. John Micah (kulia) na Meneja anaye husika na suala la Mafuta Bw. Stephen Malekano (kushoto) wakimsikiliza Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (hayupo pichani) alipofanya ziara Idara ya Forodha, Bandarini, Jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Forodha Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), bandaro ya dar es Salaam, Bw. John Micah, akifafanua jambo kwa Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb)(hayupo pichani), alipofanya ziara ya kushitukiza bandarini, Jijini Dar es Salaam. 
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), (wa pili kushoto) akitoa maelekezo kwa Maafisa waandamizi wa Mamlaka ya mapato Tanzania-TRA, alipofanya ziara ya kushitukiza bandari ya Dar es Salaam na kuagiza kitengo cha ukaguzi na upimaji wa mizigo bandarini kifumuliwe baada ya watumishi wake kutofanyakazi ya kukusanya mapato ya Serikali ipasavyo
Afisa Kitengo cha Bandari Majahazi, Bw. Mahmood Makame, akifafanua jambo mbele ya Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kushoto) kuhusu changamoto ya elimu kuhusu masuala ya kodi kwa wateja wanaotumia Bandari ya Dar es Salaam, alipofanya ziara ya kushitukiza katika ofisi hiyo.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Wizara ya Fedha na Mipango)

Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam

WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika Kituo cha Forodha Bandarini, kilichoko katika Bandari ya Dar es Salaam na kuiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA, kufanya mabadiliko makubwa ya watumishi walioko katika idara ya upimaji na ukaguzi wa mizigo baada ya kubainika kuwa baadhi yao wanajihusisha kwa namna moja au nyingine na upotevu wa mapato ya Serikali.

Dokta Mpango ametoa muda wa siku saba kwa TRA kumpa taarifa kamili ya utekelezaji wa maagizo hayo, ikiwemo kuwahamisha watumishi wote waliokaa muda mrefu kwenye eneo hilo la upimaji na ukaguzi wa mizigo ili kuongeza ufanisi wa ukusanyaji mapato ya Serikali katika Bandari hiyo.

Ameshangazwa na kitendo cha Mapato katika Bandari ya Dar es Salaam kutoongezeka licha ya juhudi kubwa zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano, kuboresha Bandari hiyo kutokana na baadhi ya watumishi wasio waaminifu kushirikiana na wafanyabiashara wasio waaminifu kukwepa kodi ya serikali.

“Pamoja na kuwepo kwa mitambo ya kukagua mizigo (Scanners), baadhi ya bidhaa zinakadiriwa kodi ndogo ikilinganishwa na thamani ya mizigo huku mizigo mingine ikiwa si ile iliyotajwa kuwemo kwenye makontena na hupitishwa na watumishi wasio waaminifu” alisisitiza Dokta Mpango.

Aidha, Waziri huyo wa Fedha na Mipango ameuagiza ungozi wa TRA kuhakikisha kuwa wanaongeza mapato katika bandari ya majahazi kutoka wastani wa mapato ya shilingi bilioni 3.5 kwa mwezi hadi shilingi bilioni 5, kulingana na malengo yaliyowekwa baada ya kubainika kuwa kuna ukwepaji mkubwa wa mapato ya Serikali katika eneo hilo.

Dokta Mpango ameuambia uongozi huo wa Mamlaka ya Mapato nchini TRA kuhakikisha kuwa Bandari ya Majahazi ianze mara moja kutumia mfumo wa kukusanya mapato ujulikanao kama TANSIS ili kudhibiti mianya ya ukwepaji kodi.

Aidha, ameviagiza vyombo vya dola kuwachunguza watumishi wote wakiwemo wa ngazi za juu katika idara ya forodha bandarini na kuwachukulia hatua kali wale wote watakao bainika kujihusisha na vitendo vyovyote vinavyoikosesha Serikali mapato yake.

Iran yafanyia majaribio kombora lake

Iran inasema kuwa imefanyia majaribio kombora la Khorram-shahr.
Image captionIran inasema kuwa imefanyia majaribio kombora la Khorram-shahr.
Iran inasema kuwa imefanyia majaribio kombora la Khorram-shahr.
Kombora hilo lilionyeshwa hadharani katika maonyesha ya kijeshi jana Ijumaa.
Iran imesema kuwa kombora hilo linaweza kusafiri mwendo wa kilomita 2,000.
Kituo cha runinga cha taifa hilo kilionyesha picha za sherehe hizo.
Kombora la kwanza la Khorram-Shahr lilirushwa angani Januari lakini likalipuka katikati ya mwendo.
Rais Donald Trump na rais Rouhani wa Iran
Image captionRais Donald Trump na rais Rouhani wa Iran
Jaribio hilo lilifanywa siku chache baada ya Rais Trump wa Marekani kushambulia Iran katika hotuba yake katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Rais wa Iran, Hassan Rouhani, ametetea hatua ya taifa lake kuimarisha zana zake kwa lengo la kujitetea.

Tetemeko la ardhi lasikika Korea Kaskazini, Je ni jaribio la kombora?

Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 3.4 katika vipimo vya Ritcher limesikika nchini Korea Kaskazini.
Image captionTetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 3.4 katika vipimo vya Ritcher limesikika nchini Korea Kaskazini.
Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 3.4 katika vipimo vya Ritcher limesikika nchini Korea Kaskazini.
Tetemeko hilo lilitokea kilomita 50 kutoka kituo cha majaribio ya makombora ya kinyuklia .
Mitetemeko mengine ya ardhi imetokea wakati wa majaribio ya makombora.
Wataalam wa mitetemeko nchini China wamesema kuwa wanatuhumu ulikuwa mlipuko.
Lakini Korea Kusini inasema kuwa huenda ni tetemeko la kawaida ambalo halikusababishwa na jaribio la kombora la kinyuklia.
Korea Kaskazini ilifanya majaribio makubwa ya kombora lake la kinyuklia mnamo Septemba 3 ambalo limeshutumiwa pakubwa katika mkutano wa umoja wa mataifa.
Kiwango cha tetemeko la siku ya Jumamosi ni kidogo ikilinganishwa na wakati taifa la Korea Kaskazini linapofanyia majaribio makombora yake.

China yaiwekea vikwazo Korea Kaskazini

China yaiwekea vikwazo Korea KaskaziniHaki miliki ya pichaALAMY
Image captionMagari ya kubeba mafuta kotoka China Kueleka Korea Kaskazini
Uchina imeimarisha vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini, ambapo imetangaza usitishaji wa ununuzi wa nguo kutoka Korea kaskazini mbali na uuzaji wa mafuta kwa taifa hilo kuanzia leo na baada ya muda fulani.
Hatua hiyo inaambatana na maagizo ya vikwazo yaliyowekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa siku 11 zilizopita.
Wachanganuzi wanasema kuwa vikwazo hivyo vitaathiri sana raia wa Korea Kaskazini iwapo vitatekelezwa kwenye mpaka kati ya mataifa hayo ambao hauna doria ya kutosha.
Rais Kim Jong Un wa KOrea kaskazini amesema kuwa rais Trump atalipia kauli zake katika mutano wa umoja wa mataifaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais Kim Jong Un wa KOrea kaskazini amesema kuwa rais Trump atalipia kauli zake katika mutano wa umoja wa mataifa
Utengenezaji wa nguo ni huduma muhimu ya pili inayoletea Korea Kaskazini fedha za kigeni na sehemu nne kwa tano ya nguo hizo hupelekwa Uchina.
Inakisiwa kuwa zaidi ya watu 100,000 wanafanya kazi katika sekta hiyo nchini Korea Kaskazini.

Seneta wa Republican ampinga Trump kuhusu Obamacare

Bima ya wagonjwa iliyoanzishwa na Rais Barack Obama ijulikanayo kama ObamaCare inawahudumia Wamerakani wa kipato cha chini.Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionBima ya wagonjwa iliyoanzishwa na Rais Barack Obama ijulikanayo kama ObamaCare inawahudumia Wamerakani wa kipato cha chini.
Seneta wa chama cha Republican aliyekuwa wakati mmoja mgombeaji wa Urais, John McCain, amesema kuwa atapiga kura kupinga mpango wa chama chake wa kufutilia mbali bima ya wagonjwa iliyoanzishwa na Rais Barack Obama ijulikanayo kama ObamaCare.
Alisema kuwa moyo wake haumruhusu kuunga mkoto upigaji marufuku wa bima hiyo inayowasaidia watu wa mapato ya chini bila kuwa na takwimu za kuonyesha watakaonufaika na watakaoathirika.
Mbali na Bwana McCain, seneta mwingine mmoja wa Republican amesema kuwa anapinga ufutiliaji mbali wa bima hiyo.
Tayari wengine wawili wametangaza kuwa wanapinga mswada huo wa chama cha Republican.
Seneta John McCain wa Republican
Image captionSeneta John McCain wa Republican
Kwa kuwa vyama vikuu viwili katika bunge la Seneti linashindiana wanachama wachache sana ni dhahiri kuwa mswada huo hautapita.
Rais Trump ametumia mtandao wa Twitter kumkosoa yeyote anayepinga kuangamizwa kwa bima ya ObamaCare.
Hata hivyo wafadhili wa mswada huo wanasema wataendelea kuusukuma siku zijazo hadi wafaulu.

Trump na Kim Jong-Un waitana ''wenda wazimu''

Rais Kim Jong Un na mwenzake wa Donald TrumpHaki miliki ya pichaEPA
Image captionRais Kim Jong Un na mwenzake wa Donald Trump
Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amesema kuwa matamshi ya rais wa Marekani Donald Trump aliyemtaja kuwa ''na matatizo ya kiakili'' yamempatia motisha zaidi ya kuendelea kutengeza makombora ya taifa lake.
Katika taarifa ya kibinafsi isio ya kawaida, bwana Kim amesema kuwa rais Trump ''atalipia kauli'' zake za hotuba ya baraza la Umoja wa mataifa ambapo alionya kuiangamiza Korea Kaskazini iwapo Marekani italazimika kujilinda.
Bwana Trump naye alijibu akisema kuwa ''mwenda wazimu'' hajawahi kufanyiwa atakachofanyiwa akijaribu.
Mataifa hayo mawili wamejibizana kwa kurushiana maneneo makali katika siku za hivi karibuni.
Rais Kim alimaliza taarifa yake kwa kusema kwamba atamnyamazisha kiongozi huyo ''aliye na akili punguani'' kwa vita.
China ilijibu vita hivyo vya maneno ikionya kuwa hali ni mbaya.
''Pande zote zinafaa kujikaza badala ya kuchokozana'' , alisema msemaji wa waziri wa maswala ya kigeni Lu Kang.Urusi pia ilitoa wito wa kuvumiliana .
Msemaji wa ikulu rais Dmitry Peskov alisema kuwa Moscow ina wasiwasi kuhusu kiwango cha wasiwasi kinachozidi kuongezeka.
Korea Kaskazini imekuwa ikifanyia majaribio makombora yake katika kiwango kisicho cha kawaida na kufanya jaribio lake la sita la kinyuklia licha ya shutuma za kimataifa.
Waziri wa maswala ya kigeni nchini Korea Kaskazini Ri Yong -ho ambaye awali alikuwa ameifananisha hotuba ya rais Trump kama ile ya ''mbwa anayebweka'' ameonya kuwa Pyongyang italifanyia jaribio bomu lake la H-Bomb katika bahari ya pacific kujibu tishio la rais Trump.
''Bomu hilo litakuwa bomu lenye uwezo mkubwa kuwahi kurushwa katika bahari hiyo ya pacific'' , Bwana Ri alisema akinukuliwa na shirika la habari nchini Korea Ksakzini Yonhap.
Hatahivyo, aliongezea: Hatujui ni hatua gani zitachukuliwa na rais Kim jong-un

Mungu aliumba watu wanaojulikana, hawa wasiojulikana wametoka wapi?


Ndiyo ukweli wenyewe, usiokuwa na chembe yoyote ya shaka ulivyo. Kwamba, Mwenyezi Mungu kwa huruma, mapenzi, utashi na mamlaka aliyonayo aliumba watu. Watu ambao kwa mujibu wa maandiko, Mungu aliwaumba kwa mfano wake mwenyewe, kwa vyovyote vile ni watu wanaojulika.
Sasa kuna wimbi la watu ‘wasiojulikana’. Pengine swali la kujiuliza ni je, hawa waliumbwa na nani?
Haipingiki na ndivyo ilivyo. Kwa sasa Tanzania imekuwa ni nchi ya kwanza tangu kuumbwa kuwamo watu wanaodaiwa hawajulikani.
Hii ni kwa mujibu wa taarifa za mara kwa mara, zinazodai kwamba wanaotenda uhalifu fulani, unyama fulani, ujambazi fulani ni watu wasiojulikana.
Watu ambao Serikali pamoja na dola yake, mara zote wamekuwa wakipata si kuwatambua tu, bali hata kuwakamata na kuwachukulia hatua za kisheria kwa matukio wanayoyafanya kila uchao.
Watu ambao kwa kiwango kikubwa wamekuwa wakiteteresha na kuififisha amani iliyokuwapo kwa miaka mingi.
Tanzania sasa inaelekea kuwa si kisiwa tena cha amani kama ilivyojulikana hapo awali; sifa yake inaanza kumong’onyolewa kwa maana ya ndani na nje ya mipaka ya nchi yetu, jaribu kuchunguza na kutafiti utajua tu!
Na wala si kimbilio tena, la wenye kuitafuta amani waliyoikosa kule walikotokea; kama ilivyodhaniwa na mataifa mbalimbali huko nyuma. Hii ni kutokana na kuwapo kwa watu ‘wasiojulikana’.
Hakika hawa watu ‘Wasiojulikana’ idadi, ni nani na mahali walipo, wametuathiri kwa kiwango kikubwa na kupausha sifa ya Taifa lililokuwa mfano wa kuigwa na wengine.
Kama kiini macho hivi, watu hawa ‘wasiojulikana’ hivi sasa wamejipatia umaarufu mkubwa kuzidi hata watu wengi maarufu.
Ajabu yake, watu hawa wamepoka na kujitwalia umaarufu, eti wao sasa wanacho kibali walichokipata kusikojulikana cha kuteka, kuua, kuiba, kufungia kwenye viroba, kuteketeza na kufanya uhalifu wote kwa jinsi wanavyojisikia. Kisha hutoweka bila kujulikana bila Serikali yenye mkono mrefu wala vyombo vyake vya dola kuwaona na kuwatia nguvuni.
Wanafanya lolote wanalojisikia kwa wakati wowote, kana kwamba Serikali na dola yake imesafiri kwenda kusikojulikana. Hili ni la ajabu kwelikweli.
Mpaka ninavyoandika makala haya, kijana Mtanzania, Ben Saanane hajulikani alipo na wala hakuna tetesi tu za kujua ikiwa yu hai au la, hakuna ajuaye asilani. Liwe Jeshi la Polisi, Serikali, ndugu, jamaa na hata marafiki; wote hawajui wala kuwa na tetesi za mahali alipo.
Licha ya ndugu zake, wananchi pamoja na wabunge kupaza sauti zao wakitaka dola ichukue hatua kuhakikisha anapatikana akiwa hai au akiwa amekufa, mara zote jitihada hizo zimekuwa ni za bure.
Hata polisi wameshindwa kutoa jibu mujarabu, la wapi alipo au inapodhaniwa aweza kuwa. Imani kubwa ni kwamba, watu ‘wasiojulikana’ peke yao ndiyo pekee wanaoweza kufahamu mpaka sasa ni wapi alipo kijana huyu.
Hilo ni tukio mojawapo lililofanywa na watu ‘wasiojulikana’, linalowashangaza na kuwastaajabisha mamilioni ya wananchi na watu wengine kutoka nchi majirani zetu, wasioamini kama kweli jeshi limeshindwa kufanya kazi yake kikamilifu.
Lakini yapo matukio mengine mbali na hili la Saanane, ambalo sasa limegeuka na kuwa sawa na kutafuta upepo; ambayo hayajapatiwa ufumbuzi wa kina na yamefanywa na watu hao wasiojulikana na Serikali imeshindwa kuwakamata na kuwaleta mbele ya mkono wa sheria.
Miongoni mwa hayo ni tukio la miaka michache iliyopita linalomhusu, Mhariri wa New habari 2006, Absalom Kibanda ambaye alipigwa na kuteswa mateso makali na watu wasiojulikana.
Na mpaka leo, hao watu ‘wasiojulikana’ hawajaweza kupatikana kujibu tuhuma za matendo waliyoyafanya. Hata kama wasingiziwa basi wajitetea kwa tuhuma zinazowakabili.
Kabla ya tukio lililompata Kibanda, kulikuwa na jingine la kumtekaji Dk Steven Ulimboka, Kiongozi wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT). Huyu bada ya kutekwa na kuteswa kadri watesaji walivyotaka alitupwa nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam kwenye eneo la pori la Mabwepande ambako aliokotwa na wasamaria akipigania roho yake.
Hili ni miongoni mwa matukio yenye kuleta simanzi na majonzi makubwa, yanapokumbukwa na kusimuliwa kama hivi.
Tukio la karibuni, nalo kama yalivyo mengine yaliyo na sura ya sintofahamu ni lile la kummiminia mvua ya risasi mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu wakati akitokea kwenye majukumu yake ya kibunge mkoani Dodoma. Alikuwa akirejea kwa mapumziko ya mchana katika eneo la makazi ambalo ni maalumu kwa ajili ya wanasiasa, wakiwamo viongozi wa Serikali na Bunge.
Tofauti kidogo na matukio mengine, hili lilifanywa mchana kweupe, naamini lilishuhudiwa na watu lukuki. Ila kwa woga waliopata watu wengi, hakuna aliyejitokeza kusimulia, labda mpaka baadaye sana.
Inasemekana Lissu alipigwa risasi zaidi ya 28 na kati yake zilimvunja mguu wa kushoto zaidi ya mara tano.
Risasi hizo hazikuishia kumvunja mguu huo tu, ila zilifululiza na kumjeruhi tumboni na kwenye bega, zikimsababishia maumivu makali na matatizo makubwa.
Kutokana na majeraha hayo, kurejea katika hali yake ya awali kunategemea kudra na majaliwa ya Mwenyezi Mungu na juhudi kubwa na madaktari wanaomhudumia.
Bado taarifa za Jeshi la Polisi zinadai kuwa wanaendelea kuwasaka watu wasiojulikana waliomshambulia na kuhakikisha wanawatia nguvuni haraka iwezekanavyo.
Hivi sasa, watu hao wasiojulikana wamezusha tafrani miongoni mwa jamii, kwenye miji na majiji kila mmoja akiwa hamuamini anayeongea naye pasipo kumfahamu kiundani.
Utamaduni ambao kwa Taifa letu umekuwa ni mgeni na haukuwahi kushuhudiwa kwa siku zilizopita; na hasa kutokana na umaarufu iliojijenga nchi yetu, ikijulikana ni kisiwa cha amani atakaye na aje. Ila kwa sasa hali haiko hivyo wasiwasi umetanda kila kona.
Kwa muktadha huo, ndiyo maana nikaanza na kichwa cha habari kama kilivyojinadi hapo juu, nikitaka kila mtu kuona tatizo na kuanza kubadili hali hii.
Swali: Mungu aliwaumba watu kwa mapenzi mema sana na wakawa wanaojulikana.....hawa ‘wasiojulikana’ ambao kila mara jeshi linahaha na kuhangaika kuwatafuta, na mara zote hizo wakiishia kutowapata na kushindwa kuwaleta mbele ya sheria; waliumbwa/wameumbwa na nani?
‘Wasiojuliakana’, wanawezaje kuishi kwenye nchi na kujichanganya na watu wanaojulikana, pasipo kushtukiwa au kutambuliwa na watu wanaojulikana hata wafanikiwe kila mara kufanya unyama na uhalifu wote huo?
Wanathubutuje kuuingilia uhuru na maisha kiujumla ya wanaojulikana, bila kujulikana na au kushakiwa kwa wakati wote huo?
Kila mmoja ajiulize tena, hivi kweli hawa ni watu wasiojulikana au ni watu wanaojulikana isipokuwa tu wameamua kujibadilisha na kuwa watu wasiojulikana?
Je, katika mafunzo askari wetu na kwa muda wanaosomea huko vyuoni, ina maana hawafundishwi kuwabaini na kuwatambua watu wasiojulikana na kuwakamata?
Kama wao wameshindwa kuwabaini na kuwakamata, nani sasa anayeweza kuwabaini na kuwakamata watu wasiojulikana?
Kama yote haya yamekosa majibu. Naungana na wananchi wenye nia njema, wanaotoa ushauri na maoni kwa jeshi letu la polisi, kama lina nia ya kuwajua na kuwakamata watu wasiojulikana liombe msaada kwa vikosi vyenye wataalamu kutoka nje ya nchi; kwa lengo la kusaidia kuwabaini na kuwakamata ili hatimaye wafikishwe mbele ya vyombo vya sheria.
Nchi imepata kigugumizi cha ukubwani. Watu hawawezi tena kutoa mawazo na maoni yao kwa Serikali, kwa mujibu wa Katiba, inayompa kila mtu uhuru na haki ya kutoa maoni yake bila kupuuzwa.
Hofu imetanda, wakiwaza na kuhofia kuchukuliwa na kusombwa na watu wasiojulikana kwenda huko kusikojulikana.
Maana tulipofikia, hakuna anayejua watu wasiojulikana wanataka nini na wanachukia nini. Tukishindwa yote hayo, tutamshtakia Mungu.
0713/0765 937 378.
amwambapa7@gmail.com

Mawakili wa Uingereza wamtaka Magufuli kuanzisha uchunguzi kuhusu Lissu

Rais John Pombe Magufuli
Image captionRais John Pombe Magufuli
Chama cha mawakili na watetezi wa haki za kibinaadamu nchini Uingereza wamemuandikia rais John Pombe Magufuli kikimtaka kuanzisha uchunguzi ulio huru mara moja kuhusu jaribio la mauaji lililotekelezwa dhidi ya mbunge wa Singida mashariki Tundu Lissu.
Wakili huyo ambaye pia ni rais wa chama cha mawakili nchini Tanzania TLS mnamo tarehe 7 mwezi Septemba alipigwa risasi tumboni na miguuni na watu wasiojulikana katika makaazi yake ya Dodoma.
''Ufyatulianaji huo wa risasi na maswala mengine ambaye yemetokeo yanayowahusisha mawakili yanatia wasiwasi''.
Ni muhimu mkubwa kwamba chama cha mawakili kinaheshimiwa kwa kuwa ni kitengo muhimu katika kuhakikisha kuwa sheria zinafuatwa kikamilifu, ilisema barua hiyo.
Hali ya mbunge Tundu Lissu baada ya kushambuliwa kwa risasi Dodoma wiki iliyopita
Barua hiyo ilisainiwa siku ya Jumatano na rais wa chama cha mawakili Joe Egan ,mwenyekiti wa baraza hilo Andrew Langdon na Mmwenyekiti wake Kirsty Brimelow.
Mawakili hao wamemwambia rais Magufuli pia kuanzisha uchunguzi kuhusu visa vyengine vya uhalifu vinavyotekelezwa dhidi ya mawakili.
Visa hivyo ni pamoja na mlipuko katika afisi ya mawakili ya IMMMA chini ya mwezi mmoja na tisho la waziri wa maswala ya kikatiba na sheria Harrison Mwakyembe la kutaka kufutilia mbali chama cha mawakili nchini Tanzania katika kipindi cha miezi saba iliopita.