Sunday, June 11

Vifo vya wanafamilia watatu vyazua hofu Tarime

Watu watatu wa familia moja wakazi wa Kijiji cha Nyantira wilayani hapa mkoani Mara wanadaiwa kufariki katika mazingira ya kutatanisha huku wanannchi wakihusisha vifo hivyo na ulaji wa asali.
Kaimu Kamanda wa Mkoa wa Polisi Tarime, Rorya, Sweetbert Njewike akizungumza kwa simu akiwa Shirati wilayani Rorya, amesema hana taarifa hiyo ofisini kwake.
Mwenyekiti wa kijiji cha Nyantira, James Chacha amesema tukio hilo lilitokea kati ya Juni 7, 8 na 9 na kuzua taharuki kijijini hapo kutokana na aina ya vifo vya wanafamilia hao watatu kufariki kwa kufuatana.
Amewataja waliofariki kuwa ni Kerato Nyangerela (70), Regina Kerato (50) na Samwel Kerato (12) ambaye ni mwanafunzi wa darasa la tatu Shule ya Msingi Nyantira.
Chacha amesema, "Juni 7 tulizika mzee baada ya kumkimbiza Kituo cha Afya, Muriba, baada ya saa 12 akafariki, tukamleta nyumbani kuzika, tulipomaliza maziko mtoto naye akawa kwenye hali mbaya, tukamkimbiza kituoni, akafa siku tunazika akaanza mama naye akafa pia," alisema.
Ameongeza kuwa kufariki kwa watu hao kwa mfuatano kijiji kumeibua hali ya wasiwasi na huzuni hasa kwa kuwa wameacha watoto wadogo.
Akizungumzia vifo hivyo, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Tarime, Mkumbo  Odari alisema,"asali kama asali haina madhara kwenye mwili wa binadamu isipokuwa pale inapokuwa imechanganyika na sumu ndipo inapoweza kuleta madhara, na ndiyo maana asali inatumiwa kama dawa, kwenye chakula na kupaka kwenye mikate," alibainisha Odari.
Naye Diwani wa Kata ya Nyansicha, Sunday Magacha alisema hadi sasa chanzo cha vifo vya wanafamilia hao hakijajulikana na uchunguzi bado unaendelea ili kufahamu chanzo licha ya kuwa uchunguzi wa awali uliofanywa na kituo cha afya Muriba ulionyesha kuwa walikuwa wamekula sumu.
Alisema tukio hilo lilikuwa la kwanza na la aina yake ambalo limewaacha wananchi wakiwa wameathirika kisaikolojia.

GOR MAHIA MABINGWA WA SPORTPESA SUPER CUP 2017, WAWATANDIKA FC LEOPARDS BAO 3-0


 Mabingwa ma Mashindabo ya SportPesa Super Cup 2017, Timu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya wakishangilia ushindi wao na Kombe la Ubingwa huo, baada ya kuwatandika wapinzani wao FC Leopards Mabao 3-0 katika mchezo uliomalizika hivi punde katika Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam.
 Mabingwa ma Mashindabo ya SportPesa Super Cup 2017, Timu ya Gor Mahia kutoka nchini Kenya wakishuhudia Nahodha wao akipokea mfano wa hundi yenye thamani ya Dola elfu 30, baada ya kutwaa Ubingwa wa Mashindano hayo kwa kuwatandika wapinzani wao FC Leopards Mabao 3-0 katika mchezo uliomalizika hivi punde katika Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam. 

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

Timu ya Gor Mahia ya Kenya imetwaa ubingwa wa kwanza wa mashindano ya SportPesa Super Cup baada ya kuwasambaratisha wapinzani wao, AFC Leopards kwa mabao 3-0 kwenye uwanja wa Uhuru.

Kwa ushindi huo, Gor Mahia imepata nafasi ya kupambana na timu maarufu ya Ligi Kuu ya Uingereza, Everton FC  Julai 13 kwenye uwanja wa Taifa jijini.

Kwa ushindi huo, Gor Mahia ilizawadiwa Sh milioni 62 za Tanzania huku AFC Leopards ikiambulia Shilingi Milioni 22 kwa kushika nafasi ya pili.

Mabao ya Timotho Otieno katika dakika ya 60, OliverMaloba katika dakika ya 76 na John Ndirangu katika muda wa nyongeza yalitosha kuinyamazisha AFC Leopards kwenye fainali hiyo iliyokuwa ya kusisimua.

Dalili za ushindi kwa Gor Mahia zilionekana tokea mwanzoni  mwa mchezo huo ambapo mshambuliaji wake hatari, Medie Kagere alikosa baola wazi baada ya pasi nzuri ya GeorgeOdhiambo.

Baada ya kosa kosa hiyo, AFC Leopards ilikuja juu na kukosa nafasi tatu za kufunga kupitia kwa Gilbert Fiamenyo, Allan Katerega na Mangoli Benard. Mshambuliaji hatari wa Gor Mahia,Medie Kagere aliibuka  kuwa mfungaji bora wa mashindano hayo kwa kufunga mabao manne.



WAZIRI MHAGAMA AZINDUA MRADI WA PROGAMU YA KITAIFA YA KUKUZA UJUZI WA NGUVU KAZI, MKOANI IRINGA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu(sera, bunge, kazi, vijana, na watu wenye ulemavu), Mhe Jenista Mhagama, akiwa na Naibu Waziri Mhe Anthony Mavunde wakikagua karakana na baadhi ya kazi zinazofanywa na Taasisi ya Don Bosco wanaotekeleza mradi wa Programu ya kitaifa ya kukuza ujuzi wa nguvu kazi wa stadi za maisha ya Taifa kwa vijana, Mkoani Iringa mpango ambao utawanufaisha vijana elfu tatu mianne 3,400 mpango unaogharamiwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu(sera, bunge, kazi, vijana, na watu wenye ulemavu), Mhe Jenista Mhagama amezindua Programu ya kitaifa ya kukuza ujuzi wa nguvu kazi wa stadi za maisha ya Taifa kwa vijana, Mkoani Iringa mpango ambao utawanufaisha vijana elfu tatu mianne 3,400 mpango  unaogharamiwa na Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Mhe, Dkt. John Pombe Magufuli.

Mhe Mhagama amesema mpango huu ni sehemu ya kuwaandaa vijana ambao watashiriki katika mapinduzi ya viwanda nchi Tanzania na utasaidia kutoa fursa kwa vijana kujiajiri na kuajiriwa kupitia mafunzo ya Uanagenzi, katika nyanja za ujenzi, tehama, ufundi magari, na ushonaji nguo katika mikoa yote nchini Tanzania.

Katika awamu hii ya kwanza, mpango huu unaendeshwa kwa pamoja baina ya Serikali ya Tanzania na taasisi ya Wasalesiani wa Don Bosco Tanzania.

Uzinduzi huo umeshuhudiwa na Naibu waziri Mhe Anthony Mavunde, Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe Amina Masenza, Wabunge kutoka mkoa wa Iringa, na Njombe na Mkuu wa Shirika la Wasalesiani wa Don Bosco Africa Mashariki Fr. Simon Asira.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu(sera, bunge, kazi, vijana, na watu wenye ulemavu), Mhe Jenista Mhagama akiangalia baadhi ya bidhaa katika moja ya mabanda baada ya kuzindua Programu ya kitaifa ya kukuza ujuzi wa nguvu kazi wa stadi za maisha ya Taifa kwa vijana, Mkoani Iringa. Kulia ni Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Mhe. Anthony Mavunde.
Picha ya Pamoja.

Amani Kabuku wa Dar es Salaam aibuka kidedea Milioni 20 za Biko


DROO ya 13 ya Biko waendeshaji wa mchezo wa kubahatisha Tanzania maarufu kama ‘Ijue Nguvu ya Buku’, imefanyika leo asubuhi, huku mkazi wa Mbezi jijini Dar es Salaa, Amani Kabuku, mwenye miaka 23, akifanikiwa kuibuka na ushindi mnono wa Sh milioni 20.

Mshindi huyo ameibuka katika droo iliyochezeshwa jana jijini Dar es Salaam na Balozi wa Biko, Kajala Masanja, kwa kushirikiana na mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Abdallah Hemed.

Akizungumza katika droo hiyo leo asubuhi, Meneja wa Huduma kwa Wateja wa Biko, Grace Kaijage, alisema ni wakati wa kutajirika kwa kupitia mchezo wao wa Biko uliozidi kujizolea umaarufu katika kipindi kifupi tangu kuanzishwa kwake nchini Tanzania.

Alisema anaamini washindi wao wanaoendelea kujipatia fedha mbalimbali kupitia mchezo wao, huku akiwataka Watanzania waendelee kucheza kwa kufanya miamala ya fedha kwenye simu zao za Tigo Pesa, M-Pesa na Airtel Money kwa kuanzia Sh 1,000, ambapo namna ya kucheza ni kuweka namba ya kampuni ambayo ni 505050 na ile ya kumbukumbu 2456.

“Wanachotakiwa kufanya ni kucheza mara nyingi zaidi ili wajiwekee mazingira mazuri yaushindi wa zawadi mbalimbali kuanzia Sh 5,000, 10,000, 20,000, 50,000, 100,000, 500,000 na Sh Milioni moja, huku zikilipwa moja kwa moja kupitia simu zao za mikononi walizotumia kuchezea Biko,” Alisema Grace.

Naye Balozi wa Biko Kajala Masanja aliwataka Watanzania kujitokeza kwa wingi kucheza Biko ili wajipatie chanzo kipya cha uchumi ili wajiendeshe kiuchumi.

“Huu si muda wa kuachia wengine wajipatie fedha huku wengine tukikaa tu, badala yake wote tuamke ili kuchangamkia fursa ya kiuchumi kwa ajili ya kupata mtaji kwa ajili ya kujiendesha kimaisha kwa namna moja ama nyingine,” Alisema.

Akizungumzia ushindi wake, mshindi huyo kutoka Mbezi, Amani aliwashukuru Biko kwa kumtangaza mshindi utakaompatia jumla ya Sh Milioni 20 ambazo zitamsaidia kwa kiasi kikubwa katika vitu vitakavyomuwezesha kiuchumi.

“Nashukuru kwa kutangazwa mshindi wa Biko wa droo ya 13 ambayo kama nikipata fedha hizo Sh Milioni 20 hakika nitazitumia vizuri katika kuinua kipato change, ukizingatia kuwa nilicheza Biko kwa malengo ya kushinda kwa kumuomba Mungu,” Alisema Amani.

Kwa kutangazwa mshindi huyo, Biko wanatarajia kumpatia zawadi yake mapema wiki hii kwa ajili ya kuhakikisha kwamba anaziweka katika matumizi yake ya kuinua uchumi wake, huku mamilioni mengine yakiendelea kutoka kwa ushindi wa papo kwa hapo pamoja na Sh Milioni 20 kwa droo ya Jumatano hii.




Balozi wa Biko Tanzania, Kajala Masanja kulia akiwa kwenye majukumu ya kumtafuta mshindi wa droo ya 13 ya Biko ambapo kijana mwenye miaka 23 mkazi wa Mbezi Makonde, jijini Dar es Salaam, Amani Kabuku, alifanikiwa kuibuka na zawadi nono ya Sh Milioni 20. Kushoto ni mwakilishi wa Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Abdallah Hemed.

MTOTO WA MIAKA 12 AIBUKA KIDEDEA MASHINDANO YA KUHIFADHI QURAN



  Waziri Mkuu, Kasssim Majaliwa akizungumza katika kilele cha Mashindano  ya 11 ya Afrika ya Kuhifadhi Qur-an Tukufu yaliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Juni 11, 2017. 
Waziri Mkuu, Kasssim Majaliwa akizungumza katika kilele cha Mashindano ya 11 ya Afrika ya Kuhifadhi Qur-an Tukufu yaliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Juni 11, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimkabidhi , Mohammed Abdullah Aden (12) wa Somalia hundi ya shilingi milioni 15, 750,000/= mshindi wa kwaza wa mashindano ya 18 ya Afrika ya Kuhifadhi Qur-an Tukufu yaliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Juni 11, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akimkabidhi , Mohammed Abdullah Aden (12) wa Somalia hundi ya shilingi milioni 15, 750,000/= mshindi wa kwaza wa mashindano ya 18 ya Afrika ya Kuhifadhi Qur-an Tukufu yaliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Juni 11, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Paul Makonda akizungumza katika mashindano hayo yaliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam leo. 
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili na Mlezi wa Taasisi ya Al- Hikma Foundation, Alhaj Ali Hassan Mwinyi akizungumza katika kilele cha Mashindano ya 18 ya Kuhifadhi Qur-an Tukufu yaliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Juni 11, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally (kulia) na Sheikh Sharif Abduqadir Mohamed Ahmed Al Ahdar ambaye ni Rais wa Taasisi ya Al – Hikima Foundation na Mlezi Mwenza wa Taasisi hiyo , katika Mashindano ya 18 ya Afrika ya Kuhifadhi Qur-an Tukufu yaliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Juni 11, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiteta na Mufti na Sheikh Sharif Abduqadir Mohamed Ahmed Al Ahdar ambaye ni Rais wa Taasisi ya Al – Hikma Foundation na Mlezi Mwenza wa Taasisi hiyo, katika Mashindano ya 18 ya Afrika ya Kuhifadhi Qur-an Tukufu yaliyofanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam Juni 11, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

…………………………………………………………

MTOTO wa miaka 12 kutoka Somalia, Mohammed Abdullahi Aden ameibuka kidedea na kitita cha dola za Marekani 7,000 (sawa na sh. milioni 15.75) katika mashindano ya 18 ya Afrika ya kuhifadhi Quran kwenye kundi la washiriki wa juzuu 30.

Mohammed ambaye ni miongoni mwa washiriki wadogo zaidi wawili kuliko wote (mwenzake anatoka Burundi), amejishindia pia IPAD, cheti, kompyuta iliyotolewa na Balozi wa Kuwait, ahadi ya sh. milioni moja kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam na ahadi ya kwenda nchi yoyote aitakayo kutoka kwa kampuni ya Sky Bus Travel Agency ya jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na maelfu ya waumini na Watanzania waliofurika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam leo mchana (Jumapili, Juni 11, 2017), Waziri Mkuu Kassim Majaliwa waandaaji wa mashindano hayo ambayo ni Taasisi ya Al-Hikma waangalie uwezekano wa kuboresha zawadi kwa kutoa scholarships (udhamini) kwa washindi au washiriki, hususan kwa washiriki wa Tanzania.

“Ongeeni na nchi marafiki kama Saudi Arabia, waone uwezekano wa kutoa zawadi za ufadhili kwenye masomo ya sekta za kimkakati kama vile mafuta na gesi, ili kuongeza hamasa na chachu ya vijana walioko kwenye sekondari zetu nao waone fursa hii na kuichangamkia, badala ya mashindano kujikita kwenye madrasa peke yake,” amesema.

Waziri Mkuu amewataka wazazi wafuatilie nyendo za vijana wao ili wasijiingize kwenye matumizi ya dawa za kulevya na vitendo vingine viovu vinavyoweza kuhatarisha maisha yao na ustawi wa nchi yetu lakini akasisitiza pia waisaidie Serikali katika mapambano yake dhidi ya rushwa na ufisadi.

“Endeleeni kushirikiana na Serikali katika mapambano yake dhidi ya rushwa na ufisadi na kuwafichua wakwepa kodi. Kila mmoja wetu ahakikishe analipa kodi stahiki kwa mujibu wa sheria. Hii itasaidia Serikali kuboresha huduma kwa wananchi ili waweze kufanya ibada zao vizuri zaidi,” amesema.

Washindi wengine kwenye kundi hilo na umri wao kwenye mabano ni Abdulkarim Ahmed Farhina (22) wa Sudan ambaye ameshinda dola za Marekani 5,000, cheti, IPAD, kompyuta iliyotolewa na Balozi wa Kuwait, ahadi ya sh. milioni moja kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Wa tatu ni Mahamoud Ali Chamfi wa Comoro (18) na Seif Ramadhani Zombe (18) kutoka Taasisi za Tanzania ambao wote wamepata dola za marekani 3,000, cheti, IPAD, kompyuta iliyotolewa na Balozi wa Kuwait, ahadi ya sh. milioni moja kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam.

Wa nne ni Khalil Mussa Hussein (17) kutoka Tanzania Bara ambaye amepata dola za marekani 1,500, cheti, IPAD, na ahadi ya sh. milioni moja kutoka kwa  Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam. Wa tano ni Ismail Issa Qasim (17) kutoka Tanzania Visiwani ambaye dola za marekani 1,000, cheti, IPAD, na ahadi ya sh. milioni moja kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,

Washiriki wengine kwenye kundi la juzuu 30 walitoka nchi za Nigeria, Kenya, Uganda, Djibouti, Afrika Kusini, Rwanda, Ghana, Ethiopia, Congo DRC, Burundi na Msumbiji. Umro wao ulikuwa ni kati ya miaka 12 na 26.

Washiriki wengine waliopewa zawadi ni wale walioweza kuhifadhi Juzuu tatu (washindi watano), Juzuu tano (washindi watatu); Juzuu 10 (washindi watatu) na Juzuu 20 (washindi watatu).

Viongozi wengine waliohudhuria kilele hicho ni Rais Mstaafu wa awamu ya pili, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, Makamu wa Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dk. Mohammed Gharib Billal, Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na Balozi wa Saudi Arabia nchini Tanzania, Mhe. Mohamed Bin Mansour Al Malek. Wengine ni wawakilishi wanne wa Imam Mkuu wa Mskiti Mtakatifu wa Makkah, Sheikh Abdul Rahman Ibn Abdul Aziz as-Sudais; Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir bin Ally na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad Mussa.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amemuagiza Meya wa Temeke, Bw. Abdallah Chaurembo kesho (Jumatatu, Juni 12, 2017) afuatane na Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Bw. Nassib Mmbaga hadi kwenye kiwanja kilichopo eneo la Matumbi na kukagua kama kuna uwezekano wa kuliongeza kwa taasisi ya Al-Hikma na wampe majibu Jumanne kwani limekaa wazi kwa muda mrefu licha ya kuwa walishaliomba na hawakupata majibu.

“Mstahiki Meya wa Temeke na Mkurugenzi wako, kesho Jumatatu nendeni mkaangalie eneo husika kama linafaa kuongezwa na mfanye maamuzi. Eneo hilo limekaa wazi kwa muda mrefu, na hawa wanataka wanataka kujenga zahanati. Jumanne asubuhi nipate taarifa ya maamuzi yenu,” alisema Waziri Mkuu na kushangiliwa na maelfu ya waumini waliokuwepo kwenye hafla hiyo.

Abiria 75 wanusurika kifo basi likiteketea kwa moto


Butiama. Basi la kampuni ya Batco lililokuwa likitokea Sirari kuelekea Mwanza muda mfupi baada ya kuvuka Mto Mara lilianza kufuka Moshi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara, Jaffari Mohamed akizungumzia tukio hilo amesema wanafuatilia kubaini chanzo cha ajili hiyo iliyosababisha mali za abiria kuteketea kwa moto, huku abiria 75 waliokuwamo wakinusurika kifo.
Basi hilo lilianza kuteketea moto leo (Jumamosi) saa saba mchana eneo la Kirumi, Kata ya Bukabwa wilayani Butiama.
Chanzo cha kuteketea basi hilo hakijajulikana, huku zaidi ya abiria 75 waliokuwa ndani wakinusurika. 
Mmoja wa abiria hao, mwalimu Malakwa Asenga amesema basi lilianza kuonyesha kuwa na hitilafu walipokuwa wakitoka mjini Tarime.
Amesema dereva aliendelea na safari na walipofika eneo la Mto Mara alisimama kwa muda akiwa ameegemea usukani na baadaye aliondoka.
Asenga amesema hawakufika mbali dereva alisimama tena, ndipo walipoona moshi ukitoka kwenye injini.
Abiria huyo anasema alimwambia mwenzake washuke kwa kuwa gari linaungua.
“Nikisema hayo tayari abiria wengine walikuwa wameanza kushuka kwa haraka wakiwa na mizigo yao ili kuokoa maisha lakini moto ulikuwa umeanza kuongezeka hivyo ni mizigo michache tu ndiyo iliyookolewa, yangu imeteketea,” amesema Asenga.

TFF YATOA UFAFANUZI KUHUSU SERENGETI BOYS


Kuna taarifa zimekuwa zikienea na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii, zikidai kuwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limewatelekeza wachezaji wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17.

Wadai kwamba eti hawakulipwa posho na kushutumu viongozi wa juu wa shirikisho kuhusu jambo hilo. Hizi taarifa si za kweli.

Aidha, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), linapenda kuwajulisha wazazi na umma kwa ujumla kwamba vijana wetu walilipwa posho zao zote wakiwa kambini Morocco na Cameroon na zile za mashindano ya AFCON nchini Gabon.

Vilevile, Shirikisho linafanya taratibu za kupeleka maombi kwenye Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (Football Development Fund FDF) ili kuweza kuwalipa vijana na benchi la ufundi sehemu ya posho zilizokuwa bado hazijakamilishwa wakati wa michuano ya kufuzu kwa AFCON 2017.

Tumeshtushwa na taarifa hizo ambazo tafsiri yake ni kuharibu uhusiano mwema kati ya shirikisho, wazazi na wachezaji ambao wanatarajiwa  kuitumikia timu ya Taifa ya Vijana wenye umri wa chini ya miaka  20 maarufu kama Ngorongoro Heroes.

Shirikisho linaendelea kuwatambua vijana wa Serengeti Boys kwani bado ni sehemu ya kikosi cha Ngorongoro Heroes na hivyo ukifika wakati wataitwa kambini kwa ajili ya michezo ya kimataifa ya U-20.

TFF inazidi kuushukuru umma ambao umeendelea kuchangia Mfuko wa FDF ambao kimsingi kazi yake ni kutafuta rasilimali kwa ajili ya maendeleo ya mpira.

Tunaomba michango iendelee kwani bado tuna changamoto za mashindano mbalimbali kwa timu za wanawake na vijana ikiwemo fainali za wanawake Afrika zitakazofanyika Ghana hapo mwakani kwa timu ya Twiga Stars na AFCON 2019 kwa Serengeti Boys ambayo itakuwa mwenyeji.

Mfuko wa Maendeleo ya Mpira - FDF ulianzishwa kwa lengo la kutafuta rasilimali za maendeleo ya mpira wa miguu hasa kwa wanawake na vijana pamoja na miundombinu ya mchezo huo.

Mfuko huo uko chini ya Mwenyekiti Bw. Tido Mhando anayeongoza Bodi na Mtendaji Mkuu (CEO) ni Bw. Dereck Murusuri anayesimamia sekretarieti

MASHINDANO YA QUR'AN YA AISHA SURURU FOUNDATION 2017



IMG-20170610-WA0108
IMG-20170610-WA0071
IMG-20170610-WA0107
IMG-20170610-WA0110
IMG-20170610-WA0105
IMG-20170610-WA0106
IMG-20170610-WA0036
Pichani za juu, Masheikh na Viongozi mbalimbali wa dini ya Kiislam waliohudhuria katika mashindano ya Qur'an yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0046
Mufti wa Tanzania, Sheikh Abubakar Zubeir akiwapa nasaha waumini wa dini ya Kiislam waliohudhuria katika mashindano ya Qur'an yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0112
Sheikh Nurdin Kishki akiwapa nasaha waumini wa dini ya Kiislam waliohudhuria katika mashindano ya Qur'an yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0100
Baadhi ya waumini wa Kiislam na washindani wa mashindano ya Qur'an waliohudhuria kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0104
Baadhi ya waumini wa Kiislam waliohudhuria kwenye mashindano ya Qur'an kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0111
Baadhi ya waumini wa Kiislam waliohudhuria kwenye mashindano ya Qur'an kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0103
Baadhi ya waumini wa Kiislam waliohudhuria kwenye mashindano ya Qur'an kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0116
Masheikh wa dini ya Kiislam na viongozi wakubwa akiwamo Sheikh Basaleh na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Sheikh Alhad, kwenye mashindano ya Qur'an yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0101
IMG-20170610-WA0049
Maskauti wakimsindikiza kwenye jukwaa mlemavu wa macho aliyehifadhi Qur'an.
IMG-20170610-WA0114
Mgeni wa heshma, Mke wa Makamu wa Rais Mstaafu, Mama Gharib Bilal, akitoa nasaha kwa waumini wa dini ya Kiislam waliohudhuria katika mashindano ya Qur'an yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0115
Mwanaharakati wa kijamii, Mwenyekiti na Mlezi wa Mashindano ya Qur'an ya Aisha Sururu Foundation, Bi Aisha Sururu, akitoa nasaha kwa waumini wa dini ya Kiislam waliohudhuria katika mashindano ya Qur'an yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja, jijini Dar es Salaam, leo.
IMG-20170610-WA0041
IMG-20170610-WA0117
IMG-20170610-WA0118
Baadhi ya zawadi zilizozawadiwa kwa washindi wa mashindano ya Qur'an yaliyoandaliwa na taasisi ya Aisha Sururu Foundation. Wabillahi tawfeeq.

Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson awajulia hali watoto wanawaosubiri kufanyiwa upasuaji wa Moyo katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)


 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akimpokea  Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Tulia Ackson alipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuwajulia hali watoto  wanawaosubiri kufanyiwa upasuaji.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Prof. Mohamed Janabi akieleza jinsi wanavyotoa  huduma za matibabu ya magonjwa ya Moyo kwa Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. Tulia Ackson alipotembelea Taasisi hiyo leo kwa ajili ya kuwajulia hali watoto wanawaosubiri kufanyiwa upasuaji.
 Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akimjulia hali  mtoto Doreen Sostenes (3) ambaye  Tulia Trust Fund imemlipia gharama za matibabu ya upasuaji wa Moyo ambao utafanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI). Kulia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kwa watoto Naiz Majani.
 Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akiwa amembeba   mtoto Doreen Sosthenes (3) ambaye  Tulia Trust Fund imemlipia gharama za matibabu ya upasuaji wa Moyo ambao utafanyika katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI).
 Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akimtazama mtoto Johnson Raphael (6) akichora picha ya mtu wakati alipotembelea  Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) leo  ili kuwajulia hali  watoto wanaosubiri kufanyiwa upasuaji. Kulia ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kwa watoto Naiz Majani.
 Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akiwa amembeba mtoto Zuwena Said (4) aliyelazwa katika   Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kusubiri upasuaji wa Moyo. Kushoto ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kwa watoto Naiz Majani.
 Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akimjulia hali mtoto Abdukarim Mahilo (2)  aliyelazwa katika   Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa ajili ya kusubiri kufanyiwa upasuaji wa Moyo huku Mama wa mtoto Fatuma Bakari akiangalia.
  Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akiongea na Maria Gervas  ambaye ni mama wa Doreen Sosthenes (3) anayelipiwa gharama za upasuaji wa  Moyo na Tulia Trust Fund. Mhe. Dkt. Tulia alitembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)  leo kwa ajili ya kuwajulia hali watoto wanaosubiri kufanyiwa upasuaji.

 Daktari Bingwa wa Moyo kwa watoto na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo kwa Watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Sulende Kubhoja akimuelezea   Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson magonjwa mbalimbali ya moyo yanayowasumbua watoto. Mhe. Dkt. Tulia alitembelea  Taasisi hiyo  leo kwa ajili ya kuwajulia hali watoto wanaosubiri kufanyiwa upasuaji.
  Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akimbembeleza mtoto Venance  Christopher (14) aliyelazwa katika Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwaajili ya kusubiri upasuaji wa  Moyo. Mhe. Dkt. Tulia alitembelea Taasisi hiyo   leo kwa ajili ya kuwajulia hali watoto wanaosubiri kufanyiwa upasuaji.
 Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akiongea jambo wakati akimjulia hali mtoto Rashid Kombo aliyelazwa katika  chumba cha uangalizi maalum (ICU) baada ya kufanyiwa upasuaji wa Moyo. Kushoto ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naiz Majani akifuatiwa na  Daktari Bingwa wa Moyo kwa watoto na Mkuu wa Idara ya Magonjwa ya Moyo kwa Watoto Dkt. Sulende Kubhoja. 
Mhe. Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akimsikiliza Daktari Bingwa wa upasuaji wa Moyo kwa Watoto na Mkuu wa Idara ya Upasuaji wa Moyo kwa Watoto Godwin Sharau alipotembelea leo chumba cha upasuaji wa Moyo kilichopo Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwetwe (JKCI). Picha na  Anna Nkinda wa JKCI