Thursday, August 17

TEF



Kumekuwa na mjadala wa muda mrefu kuhusu TEF. Licha ya kasoro zake, pengine TEF kwa sasa ndiyo jumuiya ya waandishi wa habari Tanzania yenye umaarufu zaidi kuliko zote. Moja ya tuhuma kubwa dhidi ya TEF ni kuwa jukwaa hili limekuwa linatumika kama "kichaka" ambacho viongozi wa taasisi mbalimbali (hususan za umma) hujificha ili kujikinga na tuhuma za ufisadi.

TEF pia imekuwa inajulikana kwa kutoa matamko ya kufungia au kufungulia watu fulani wasiandikwe na vyombo vya habari nchini. Suala ambalo sisi wengine ambao siyo wanachama wa TEF tumekuwa tunahoji ni kuwa TEF ni jukwaa la wanachama (members only), hivyo basi, wanachama wa TEF wana *haki* ya kualikwa kwenye mikutano ya TEF na semina zinazoandaliwa na TEF na wana *wajibu* wa kupokea na kutekeleza maagizo ya TEF. Kwa muktadha huo huo, wahariri na waandishi ambao sio wanachama wa TEF hawana haki ya kuitwa kwenye vikao vya TEF, na hawana wajibu wa kutekeleza maagizo ya TEF.
Kumekuwa na dhana potofu kuwa maagizo na maamuzi yote ya TEF ni lazima yatekelezwe na waandishi wote wa habari, wahariri na taasisi zote za habari za Tanzania, hata wale wasio wanachama wa TEF bila kuzingatia dhana ya haki na wajibu.
Mara kadhaa tumesikia wahariri au vyombo vya habari vikiitwa wasaliti kwa kutotekeleza maagizo ya TEF bila kujali kama wahariri hao ni wanachama wa TEF au la. Je, ni nani amewapa TEF mamlaka ya kuwa wafanya maamuzi, watoa amri na wasemaji wa waandishi wa habari, wahariri na vyombo vyote vya habari vya Tanzania?

Lazima ieleweke wazi kuwa wenye wajibu wa kutekeleza maamuzi ya TEF ni wahariri ambao ni wanachama wa TEF tu. Wahariri ambao sio wanachama wa TEF hawana wajibu wowote ule wa kupokea maagizo ya TEF. Ni jukumu la TEF kuwashawishi wahariri hao waungane na msimamo wao kwa kujenga hoja.
Ni vyema TEF ikajitathmini na kurekebisha hii taswira mbaya iliyopo. Je, kuandaa semina ambazo wahariri wanalipwa posho na kufungia/kufungulia watu fulani wasiandikwe na vyombo vya habari ndiyo jukumu kubwa la TEF?
Ningependa kuona TEF ikijikita kukabiliana na matatizo ya msingi zaidi yafuatayo kwenye tasnia ya habari ya Tanzania:

1. Tatizo la rushwa kwenye tasnia ya habari ya Tanzania

2. Kuhakikisha kuwa baadhi ya wamiliki wa vyombo vya habari Tanzania wanaacha kutoa maslahi duni kwa waandishi wa habari na kuhakikisha waandishi wa habari wanakuwa katika mazingira mazuri ya kazi

3. Kuondoa tatizo sugu la kuporomoka kwa maadili na weledi kwenye tasnia ya habari ya Tanzania

4. Kukemea na kukabiliana na kuongezeka kwa vitendo vya kuminywa kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania

5. Kutoa dira kuhusu hatma ya vyombo vya habari nchini Tanzania kutokana na mazingira magumu ya biashara hiyo nchini kwa sasa

Pale ambapo TEF itakapojitathmini, naamini kwa dhati kuwa ina fursa kubwa ya kuwa jukwaa lenye nguvu na linaloheshimiwa na kuungwa mkono na waandishi wa habari na wananchi wengi zaidi nchini.

Naomba kuwasilisha.
Fumbuka Ng'wanakilala, 

Serikali imetoa siku 60 kwa mkandarasi wa Kampuni ya Hari Singh & Sons kumaliza ujenzi

Serikali imetoa siku 60 kwa mkandarasi wa Kampuni ya Hari Singh & Sons kumaliza ujenzi wa kipande cha barabara cha kilomita 1.5 kilichobaki kwa kiwango cha lami katika barabara ya Kimara Baruti-Msewe-Chuo Kikuu yenye jumla ya urefu wa kilomita 2.6.
Akitoa agizo hilo jijini Dar es salaam, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, amemtaka mkandarasi huyo kuhakikisha kuwa anamaliza mradi huo haraka na kwa viwango vilivyo kwenye mkataba ili idumu kwa muda mrefu.
"Ikifika mwezi Oktoba nataka unikabidhi barabara hii ikiwa imekamilika kwa kiwango cha lami na vigezo vinavyokubalika, amesisitiza Eng. Ngonyani.

Aidha, Naibu Waziri Ngonyani amefafanua kuwa mkandarasi huyo hatoruhusiwa kutekeleza mradi mwingine wa barabara nchini endapo atashindwa kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo kwa wakati.
Kwa upande wake Mhandisi Mradi kutoka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Ngusa Julius, amesema kuwa TANROADS tayari imeshatoa notisi kwa mkandarasi huyo kuwa kama hatakamilisha kazi ya ujenzi ndani ya muda wa mkataba hatua za kudai fidia kulingana na mkataba zitafuata na baadae kukatisha mkataba.
Ameongeza kuwa mradi wa ujenzi wa barabara hiyo unasimamiwa na TANROADS kupitia kitengo chake cha wahadisi washauri wazalendo (TECU) na unagharimu shilingi Bilioni 5.7 ikiwa ni fedha za Serikali kwa asilimia mia moja.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Eng. Ngonyani amekagua daraja la Mlalakuwa lenye urefu wa mita 15 kila upande, lililopo barabara ya Mwai Kibaki jijini Dar es salaam na kusisitiza kwa mkandarasi Milembe & Kika JV kuhakikisha anamaliza ujenzi wa daraja hilo kwa wakati.
Ujenzi wa Daraja la Mlalakuwa unagharimu shilingi Bilioni 4.8 na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba mwakani.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, akitoa maelekezo kwa mkandarasi wa kampuni ya Hari Singh & Sons, Jaspal Singh (kushoto), wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Kimara Baruti – Msewe – Chuo Kikuu yenye urefu wa KM 2.6 kwa kiwango cha lami, jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa kampuni ya Hari Singh & Sons, Jaspal Signh, akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Kimara Baruti – Msewe – Chuo Kikuu yenye urefu wa KM 2.6 kwa kiwango cha lami, jijini Dar es Salaam.
 Muonekano wa sehemu ya barabara ya Kimara Baruti – Msewe – Chuo Kikuu yenye urefu wa KM 2.6 inayojengwa kwa kiwango cha lami, ambapo ujenzi wake umefika asilimia 57.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, akitoa maelekezo kwa Mkandarasi wa Kampuni ya Milembe & Kika JV anayejenga Daraja la Mlalakuwa lenye urefu wa mita 15 kila upande, lililoko barabara ya Mwai Kibaki, wakati akikagua ujenzi wake, jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa sehemu ya chini ya ujenzi wa Daraja la Mlalakuwa lenye urefu wa mita 15 kila upande, lililoko barabara ya Mwai Kibaki, jijini Dar es Salaam. Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano,

Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS)

WAZIRI MKUU AKUTANA NA BALOZI WA TANZANIA NCHINI MALAWI MHE BENEDICT MASHIBA


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mheshimiwa Balozi Benedict Mashiba, ambapo amemtaka kuimarisha mahusiano baina ya nchi zote mbili. 

Amekutana na Balozi Mashiba leo (Jumatano, Agosti 16, 2017) katika makazi ya Waziri Mkuu, Oysterbay jijini Dar es Salaam, ambapo amemtaka balozi huyo kuhakikisha anaboresha shughuli za Kidiplomasia kati ya Tanzania na Malawi. 
Pia Waziri Mkuu amemtaka Balozi huyo kuhakikisha anatangaza vivutio vya utalii vilivyopo nchini, ukiwemo mlima Kilimanjaro, mbuga za wanyama pamoja na fursa za uwekezaji zilizopo nchini hususan katika sekta ya viwanda. 
Waziri Mkuu amesema licha ya kutangaza fursa za uwekezaji na vivutio vya utalii pia amemtaka kuboresha biashara baina ya Tanzania na Malawi kwa kutumia meli mbili za mizigo za Mv. Ruvuma na Mv. Njombe alizozizindua hivi karibuni. 
Hata hivyo, Waziri Mkuu amemtaka Balozi Mashiba kukutana na kufanya mazungumzo na Watanzania waishio nchini Malawi na kuwasisiza kuishi kwa kuzingatia sheria za nchi husika. Pia kuwaunganisha pamoja na kuwashauri waje kuwekeza nchini. 
Kwa upande wake Balozi Mashiba amesema atahakikisha anayafanyia kazi maelekezo yote aliyopewa ikiwa ni pamoja na kuimarisha ulinzi na usalama pamoja na kuboresha ushirikiano baina ya Tanzania na Malawi.

Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa akisalimiana na Balozi wa Tanzania nchini Malawi, Mheshimiwa Balozi Benedict Mashiba wakati alipokutana naye Ofisini kwake Magogoni jijini Dar es salaam leo

BARABARA YA KIMARA BARUTI-CHUO KIKUU JIJINI DAR ES SALAAM YATAKIWA KUKAMILIKA NDANI YA SIKU 60

Serikali imetoa siku 60 kwa mkandarasi wa Kampuni ya Hari Singh & Sons kumaliza ujenzi wa kipande cha barabara cha kilomita 1.5 kilichobaki kwa kiwango cha lami katika barabara ya Kimara Baruti-Msewe-Chuo Kikuu yenye jumla ya urefu wa kilomita 2.6.
Akitoa agizo hilo jijini Dar es salaam, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, amemtaka mkandarasi huyo kuhakikisha kuwa anamaliza mradi huo haraka na kwa viwango vilivyo kwenye mkataba ili idumu kwa muda mrefu.
"Ikifika mwezi Oktoba nataka unikabidhi barabara hii ikiwa imekamilika kwa kiwango cha lami na vigezo vinavyokubalika, amesisitiza Eng. Ngonyani.

Aidha, Naibu Waziri Ngonyani amefafanua kuwa mkandarasi huyo hatoruhusiwa kutekeleza mradi mwingine wa barabara nchini endapo atashindwa kukamilisha ujenzi wa barabara hiyo kwa wakati.
Kwa upande wake Mhandisi Mradi kutoka Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Eng. Ngusa Julius, amesema kuwa TANROADS tayari imeshatoa notisi kwa mkandarasi huyo kuwa kama hatakamilisha kazi ya ujenzi ndani ya muda wa mkataba hatua za kudai fidia kulingana na mkataba zitafuata na baadae kukatisha mkataba.
Ameongeza kuwa mradi wa ujenzi wa barabara hiyo unasimamiwa na TANROADS kupitia kitengo chake cha wahadisi washauri wazalendo (TECU) na unagharimu shilingi Bilioni 5.7 ikiwa ni fedha za Serikali kwa asilimia mia moja.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri Eng. Ngonyani amekagua daraja la Mlalakuwa lenye urefu wa mita 15 kila upande, lililopo barabara ya Mwai Kibaki jijini Dar es salaam na kusisitiza kwa mkandarasi Milembe & Kika JV kuhakikisha anamaliza ujenzi wa daraja hilo kwa wakati.
Ujenzi wa Daraja la Mlalakuwa unagharimu shilingi Bilioni 4.8 na unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba mwakani.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, akitoa maelekezo kwa mkandarasi wa kampuni ya Hari Singh & Sons, Jaspal Singh (kushoto), wakati akikagua maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Kimara Baruti – Msewe – Chuo Kikuu yenye urefu wa KM 2.6 kwa kiwango cha lami, jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa kampuni ya Hari Singh & Sons, Jaspal Signh, akitoa ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, kuhusu maendeleo ya ujenzi wa barabara ya Kimara Baruti – Msewe – Chuo Kikuu yenye urefu wa KM 2.6 kwa kiwango cha lami, jijini Dar es Salaam.
 Muonekano wa sehemu ya barabara ya Kimara Baruti – Msewe – Chuo Kikuu yenye urefu wa KM 2.6 inayojengwa kwa kiwango cha lami, ambapo ujenzi wake umefika asilimia 57.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, akitoa maelekezo kwa Mkandarasi wa Kampuni ya Milembe & Kika JV anayejenga Daraja la Mlalakuwa lenye urefu wa mita 15 kila upande, lililoko barabara ya Mwai Kibaki, wakati akikagua ujenzi wake, jijini Dar es Salaam.
Muonekano wa sehemu ya chini ya ujenzi wa Daraja la Mlalakuwa lenye urefu wa mita 15 kila upande, lililoko barabara ya Mwai Kibaki, jijini Dar es Salaam. Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano,

Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS)

WAZIRI MWAKYEMBE AHIMIZA MASHIRIKIANO KATI YA WIZARA NA UNESCO KATIKA KUHIFADHI HISTORIA YA NCHI



Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akipokea moja ya kitabu chenye kumbukumbu ya historia ya Afrika ikiwemo Tanzania kutoka kwa Mwakilishi Mkazi wa UNESCO nchini Tanzania Bibi. Zulmira Rodrigues wakati wa kikao na watendaji wa Wizara pamoja na UNESCO kujadili mashirikiano yaliyopo katika kuhifadhi historia ya nchi leo Jijini Dar es Salaam .

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) akizungumza na Mwakilishi Mkazi wa UNESCO nchini Tanzania Bibi. Zulmira Rodrigues wakati wa kikao na watendaji wa Wizara pamoja na UNESCO kujadili mashirikiano yaliyopo katika kuhifadhi historia ya nchi leo Jijini Dar es Salaam 
Mwakilishi Mkazi wa UNESCO nchini Tanzania Bibi. Zulmira Rodrigues (wapili kushoto) akizungumza wakati wa kikao na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (kushoto) pamoja na watendaji wa Wizara kujadili mashirikiano yaliyopo katika kuhifadhi historia ya nchi leo Jijini Dar es Salaam 
Mkurugenzi Msaidizi Tathmini na Ufuatiliaji kutoka Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Bw. Benard Lubogo (katikati) akichangia mada wakati wa kikao na watendaji kutoka UNESCO kujadili mashirikiano yaliyopo katika kuhifadhi historia ya nchi leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Bibi. Martha Swai  



Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe (katikati waliokaa) katika picha ya pamoja na watendaji wa Wizara yake na watendaji kutoka UNESCO baada ya kikao na watendaji hao kujadili mashirikiano yaliyopo katika kuhifadhi historia ya nchi leo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa UNESCO nchini Tanzania Bibi. Zulmira Rodrigues na kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mkuu Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Bibi. Martha Swai 

Picha na: Genofeva Matemu -WHUSM

KWA NINI NASITA KUJIUNGA NA TEF - FUMBUKA NG'WANAKILALA




Kumekuwa na mjadala wa muda mrefu kuhusu TEF. Licha ya kasoro zake, pengine TEF kwa sasa ndiyo jumuiya ya waandishi wa habari Tanzania yenye umaarufu zaidi kuliko zote. Moja ya tuhuma kubwa dhidi ya TEF ni kuwa jukwaa hili limekuwa linatumika kama "kichaka" ambacho viongozi wa taasisi mbalimbali (hususan za umma) hujificha ili kujikinga na tuhuma za ufisadi.
TEF pia imekuwa inajulikana kwa kutoa matamko ya kufungia au kufungulia watu fulani wasiandikwe na vyombo vya habari nchini. Suala ambalo sisi wengine ambao siyo wanachama wa TEF tumekuwa tunahoji ni kuwa TEF ni jukwaa la wanachama (members only), hivyo basi, wanachama wa TEF wana *haki* ya kualikwa kwenye mikutano ya TEF na semina zinazoandaliwa na TEF na wana *wajibu* wa kupokea na kutekeleza maagizo ya TEF. Kwa muktadha huo huo, wahariri na waandishi ambao sio wanachama wa TEF hawana haki ya kuitwa kwenye vikao vya TEF, na hawana wajibu wa kutekeleza maagizo ya TEF.
Kumekuwa na dhana potofu kuwa maagizo na maamuzi yote ya TEF ni lazima yatekelezwe na waandishi wote wa habari, wahariri na taasisi zote za habari za Tanzania, hata wale wasio wanachama wa TEF bila kuzingatia dhana ya haki na wajibu.
Mara kadhaa tumesikia wahariri au vyombo vya habari vikiitwa wasaliti kwa kutotekeleza maagizo ya TEF bila kujali kama wahariri hao ni wanachama wa TEF au la. Je, ni nani amewapa TEF mamlaka ya kuwa wafanya maamuzi, watoa amri na wasemaji wa waandishi wa habari, wahariri na vyombo vyote vya habari vya Tanzania?

Lazima ieleweke wazi kuwa wenye wajibu wa kutekeleza maamuzi ya TEF ni wahariri ambao ni wanachama wa TEF tu. Wahariri ambao sio wanachama wa TEF hawana wajibu wowote ule wa kupokea maagizo ya TEF. Ni jukumu la TEF kuwashawishi wahariri hao waungane na msimamo wao kwa kujenga hoja.
Ni vyema TEF ikajitathmini na kurekebisha hii taswira mbaya iliyopo. Je, kuandaa semina ambazo wahariri wanalipwa posho na kufungia/kufungulia watu fulani wasiandikwe na vyombo vya habari ndiyo jukumu kubwa la TEF?
Ningependa kuona TEF ikijikita kukabiliana na matatizo ya msingi zaidi yafuatayo kwenye tasnia ya habari ya Tanzania:

1. Tatizo la rushwa kwenye tasnia ya habari ya Tanzania

2. Kuhakikisha kuwa baadhi ya wamiliki wa vyombo vya habari Tanzania wanaacha kutoa maslahi duni kwa waandishi wa habari na kuhakikisha waandishi wa habari wanakuwa katika mazingira mazuri ya kazi

3. Kuondoa tatizo sugu la kuporomoka kwa maadili na weledi kwenye tasnia ya habari ya Tanzania

4. Kukemea na kukabiliana na kuongezeka kwa vitendo vya kuminywa kwa uhuru wa vyombo vya habari nchini Tanzania

5. Kutoa dira kuhusu hatma ya vyombo vya habari nchini Tanzania kutokana na mazingira magumu ya biashara hiyo nchini kwa sasa

Pale ambapo TEF itakapojitathmini, naamini kwa dhati kuwa ina fursa kubwa ya kuwa jukwaa lenye nguvu na linaloheshimiwa na kuungwa mkono na waandishi wa habari na wananchi wengi zaidi nchini.

Naomba kuwasilisha.
Fumbuka Ng'wanakilala, 

VIGOGO 6 JIJINI MBEYA KORTINI KUJIBU MASHTAKA YA KUTAFUNA BILIONI 5 ZA SOKO LA KIMATAIFA



Na Mbeya Yetu
Vigogo 6 kati ya 12 wanaotuhumiwa kuhusika kwenye kashifa ya ufisadi wa soko la Kimataifa la Mwanjelwa jijini Mbeya wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Mbeya na kusomewa mashtaka matatu ya uhujumu uchumi.
Waliopandishwa kizimbani Mahakamani hapo ni aliyekuwa Meya wa jiji hilo, Athanas Kapunga (70)  aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji hilo, Elizabeth Munuo (65) na aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Jiji hilo Dk. Samwel Lazaro ambaye kwa sasa ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe. 
Wengine ni aliyekuwa Mtunza Hazina wa Jiji hilo, James Jorojik (62), aliyekuwa Mwasibu wa jiji hilo, Tumaini Msigwa (47) na Mhandisi wa jiji hilo, Emily Maganga (42). 
Mwendesha mashtaka wa serikali, Shadrack Martin, akisaidiwa na Hebel Kihaka pamoja na Baraka Mgaya wakati akiwasomea mashtaka yanayowakabili vigogo hao alisema wote kwa pamoja walitenda makosa ya uhujumi uchumi kati ya mwaka 2008 na 2013 hivyo kuisababishia serikali hasara kubwa.
Katika Shtaka la kwanza mwendesha mashtaka huyo alisema linawahusu watuhumiwa waili ambao ni Athanas Kapunga ambaye alikuwa Meya wa Jiji la Mbeya na Elizabeth Munuo ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Jiji ambao wanadaiwa kuisababishia halmashauri hiyo hasara ya Shilingi Bilioni 3.3, ambapo wanadaiwa kusaini mkopo wa kiasi hicho cha fedha kutoka katika Benki ya CRDB ambao ulianza kulipiwa riba kabla ya kuanza kujengwa kwa Soko hilo la Mwanjelwa kinyume cha vifungu vya sheria namba 57 (1) na 60 (1)  na (2)  vya Sheria za uhujumu uchumi Sura ya 200 ya mwaka 2002.

Martini alisema shtaka la pili linawahusu Dk.Samwel Lazaro, James Jorojik, tumain Msigwa na Emily Maganga ambao kwa pamoja wanadaiwa kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa kuidhinisha malipo ya shilingi milioni 304,470,500 kwa Mkandarasi aliyekuwa anajenga soko hilo, Nandhra Engineering and Constaction ltd wakati kazi hiyo ilikuwa tayari imefanywa na Kampuni ya Tanzania Building Works ltd.

Aidha  Washtakiwa wa Shataka namba mbili pia wanashtakiwa kwa kosa la tatu la kuisababishia Halmashauri ya Jiji hasara ya shilingi 1,140,228,750 kwa kuidhinisha malipo ya fedha hizo kwa wakandarasi Tanzania Building Works na Nadhra Engineering kwa ajili ya ujenzi wa Soko hilo wakati kazi iliyotajwa haikuwemo kwenye Mkataba.

Washtakiwa hao kwa pamoja walikuwa wakitetewa na Mawakili watatu wakiongozwa na James Kyando, Baraka Mbwilo na Secilia Luhanga ambao waliiomba Mahakama hiyo kutoa maelezo kuhusu uwezekano wa wateja wao kupata dhamana. Hata hivyo Mwendesha Mashtaka wa serikali alisema upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika hivyo akaiomba mahakama kupanga siku nyingine kwa ajili ya kutajwa tena.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mbeya, Michael Mteite alisema Mahakama haina uwezo wa kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi hivyo washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu hadi Agosti 29, Mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Kufikishwa Mahakamani kwa vigogo hao kunatokana na agizo la Waziri mkuu alilotoa Julai 31 mwaka huu wakati wa ziara ya kikazi jijini hapa alipozungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya na Jiji na kuwataja wahusika 13 waliotajwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG) na kupendekeza wachukuliwe hatua.

WAZIRI MKUU MAJALIWA ZIARANI NCHINI CUBA


 WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameondoka nchini leo (Jumatano, Agosti 16, 2017) kuelekea nchini Cuba kwa ajili ya ziara ya kikazi yenye lengo la kudumisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Akiwa nchini Cuba Waziri Mkuu anatarajiwa kufanya mazungumzo na viongozi waandamizi wa Cuba kwa lengo la kukuza ushirikiano katika sekta za afya, elimu utalii na Kilimo.

Aidha, nchi ya Cuba ni mojawapo ya nchi zenye ushirikano wa muda mrefu na Tanzania Kisiasa, Kijamii na Kiuchumi.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMATANO, AGOSTI 16, 2017.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiagana na Mkuu wa Wilaya ya Temeke ,Felex Jackson katika Uwanja wa Ndege wa Julias Nyerere Dar es salaam leo August,16/2017 akiwa anaelekea Nchini Cuba Kwa ziara ya kikazi.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

VIGOGO 6 JIJINI MBEYA KORTINI KUJIBU MASHTAKA YA KUTAFUNA BILIONI 5 ZA SOKO LA KIMATAIFA



Na Mbeya Yetu
Vigogo 6 kati ya 12 wanaotuhumiwa kuhusika kwenye kashifa ya ufisadi wa soko la Kimataifa la Mwanjelwa jijini Mbeya wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoani Mbeya na kusomewa mashtaka matatu ya uhujumu uchumi.
Waliopandishwa kizimbani Mahakamani hapo ni aliyekuwa Meya wa jiji hilo, Athanas Kapunga (70)  aliyekuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji hilo, Elizabeth Munuo (65) na aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi wa Jiji hilo Dk. Samwel Lazaro ambaye kwa sasa ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Songwe. 
Wengine ni aliyekuwa Mtunza Hazina wa Jiji hilo, James Jorojik (62), aliyekuwa Mwasibu wa jiji hilo, Tumaini Msigwa (47) na Mhandisi wa jiji hilo, Emily Maganga (42). 
Mwendesha mashtaka wa serikali, Shadrack Martin, akisaidiwa na Hebel Kihaka pamoja na Baraka Mgaya wakati akiwasomea mashtaka yanayowakabili vigogo hao alisema wote kwa pamoja walitenda makosa ya uhujumi uchumi kati ya mwaka 2008 na 2013 hivyo kuisababishia serikali hasara kubwa.
Katika Shtaka la kwanza mwendesha mashtaka huyo alisema linawahusu watuhumiwa waili ambao ni Athanas Kapunga ambaye alikuwa Meya wa Jiji la Mbeya na Elizabeth Munuo ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Jiji ambao wanadaiwa kuisababishia halmashauri hiyo hasara ya Shilingi Bilioni 3.3, ambapo wanadaiwa kusaini mkopo wa kiasi hicho cha fedha kutoka katika Benki ya CRDB ambao ulianza kulipiwa riba kabla ya kuanza kujengwa kwa Soko hilo la Mwanjelwa kinyume cha vifungu vya sheria namba 57 (1) na 60 (1)  na (2)  vya Sheria za uhujumu uchumi Sura ya 200 ya mwaka 2002.

Martini alisema shtaka la pili linawahusu Dk.Samwel Lazaro, James Jorojik, tumain Msigwa na Emily Maganga ambao kwa pamoja wanadaiwa kushindwa kutekeleza majukumu yao kwa kuidhinisha malipo ya shilingi milioni 304,470,500 kwa Mkandarasi aliyekuwa anajenga soko hilo, Nandhra Engineering and Constaction ltd wakati kazi hiyo ilikuwa tayari imefanywa na Kampuni ya Tanzania Building Works ltd.

Aidha  Washtakiwa wa Shataka namba mbili pia wanashtakiwa kwa kosa la tatu la kuisababishia Halmashauri ya Jiji hasara ya shilingi 1,140,228,750 kwa kuidhinisha malipo ya fedha hizo kwa wakandarasi Tanzania Building Works na Nadhra Engineering kwa ajili ya ujenzi wa Soko hilo wakati kazi iliyotajwa haikuwemo kwenye Mkataba.

Washtakiwa hao kwa pamoja walikuwa wakitetewa na Mawakili watatu wakiongozwa na James Kyando, Baraka Mbwilo na Secilia Luhanga ambao waliiomba Mahakama hiyo kutoa maelezo kuhusu uwezekano wa wateja wao kupata dhamana. Hata hivyo Mwendesha Mashtaka wa serikali alisema upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika hivyo akaiomba mahakama kupanga siku nyingine kwa ajili ya kutajwa tena.

Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mbeya, Michael Mteite alisema Mahakama haina uwezo wa kusikiliza kesi ya uhujumu uchumi hivyo washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu hadi Agosti 29, Mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Kufikishwa Mahakamani kwa vigogo hao kunatokana na agizo la Waziri mkuu alilotoa Julai 31 mwaka huu wakati wa ziara ya kikazi jijini hapa alipozungumza na Watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbeya na Jiji na kuwataja wahusika 13 waliotajwa kwenye Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali  (CAG) na kupendekeza wachukuliwe hatua.

Pacha walioungana wafariki dunia


Dar es Salaam. Pacha walioungana ambao walikuwa wakitumia pamoja baadhi ya viungo vya ndani, wamefariki dunia juzi jioni katika Hospitali ya Taifa Muhimbili wakiwa na umri wa siku 26.
Daktari bingwa wa upasuaji wa watoto wa hospitali hiyo, Zaituni Bokhari alisema jana kuwa watoto hao wamefariki dunia baada ya kupata maambukizi ya kifua kwa muda mfupi.
Alisema kutokana na hali waliyokuwa nayo ilikuwa ni rahisi kwao kupata maambukizi mbalimbali hasa kwenye mapafu na katika baadhi ya viungo vyao.
“Walikuwa wanaendelea vizuri sana ila (juzi) jana ndiyo walibadilika ghafla, wakaanza kuonekana wanapata tatizo la kupumua, hata hivyo, mmoja alizaliwa na tatizo la kupumua,” alisema Dk Bokhari.
Watoto hao walizaliwa katika Hospitali ya Misheni ya Berega, Morogoro, Julai 21.
Kutokana na hali zao, Julai 24 walifikishwa Muhimbili ambako walichukuliwa vipimo mbalimbali vya kuchunguza afya zao na kuangalia uwezekano wa kuwatenganisha.
Baada ya kufanyiwa vipimo vya kimaabara kwa takribani wiki nzima, iligundulika kuwa wanatumia pamoja baadhi ya viungo vya ndani ikiwamo moyo na ini.
Majibu hayo yalikuja baada ya vipimo vya radiolojia vikiwamo CT Scan, MRI, X Ray, moyo (ECO) pamoja na vipimo vyote vya damu.
Mbali ya kugundulika kuwa wanatumia pamoja baadhi ya viungo vya ndani ikiwamo moyo na ini, Dk Bokhari alisema watoto hao wameungana sehemu ya kifua na tumbo na baada ya vipimo vya CT Scan, ikaonekana pia kwamba kuna baadhi ya ogani zimeshikana.
Pia alisema majibu hayo ya CT Scan ya tumbo na kifua yalionyesha kuwa kuna chemba nyingi za milango ambazo walikuwa wakishirikiana.
Pamoja na hali hiyo, Dk Bokhari alisema jopo la madaktari lilikuwa limejiandaa kuwatenganisha watoto hao na kwamba kazi hiyo ilikuwa ifanyike katika miezi sita ijayo.

Saruji ya Dangote yaadimika sokoni




Dar es Salaam. Wafanyabiashara wa vifaa vya ujenzi jijini hapa wamelalamika kukosekana kwa uhakika wa upatikanaji wa saruji ya Dangote, hivyo kuwasababishia usumbufu.
Wakizungumza jana kwenye mkutano wao na Mkurugenzi wa mauzo na ufundi wa Kampuni ya Dangote group, Johnson Olaniyi waliitaka kampuni hivyo kudhibiti changamoto zinazosababisha hali hiyo.
Mkurugenzi wa G&E investmenta, Goodluk Lyatuu alisema huwa wanasubiri hata wiki mbili bila kupata saruji hali inayosababisha usumbufu kwa wateja, ikiwamo kuzuia mtaji kuongezeka.
Alisema pia bei imekuwa ikibadilika mara kadhaa, hali inayoyumbisha soko na aliuomba uongozi uchukue hatua ili kuwajengea mazingira mazuri ya biashara hiyo.
Saruji hiyo hadi jana kwa bei ya jumla ya mfuko wa kilo 50 uliuzwa kati ya Sh10,700 na 11,200 na bei ya rejareja ilikuwa kati ya Sh12,000 hadi 12,500.
Akizungumza kwenye mkutano huo, Olaniyi alisema wanatambua kuna changamoto zinazowakabili hasa kwenye uzalishaji lakini watajitahidi kukabiliana nazo.
“ Ndiyo maana tupo hapa tunazungumza hii ni miongoni wa hatua za kutatua changamoto hizo nimetoka Nigeria hadi chini hapa ili kushughilikia mambo hayo,” alisema.
Mkuu wa mauzo wa Dangote, Felista Masambo alisema changamoto hizo kwa upande mwingine zinatokana na teknolojia mpya ya uzalishaji wanayotumia.