Thursday, August 17

WAZIRI MKUU MAJALIWA ZIARANI NCHINI CUBA


 WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa ameondoka nchini leo (Jumatano, Agosti 16, 2017) kuelekea nchini Cuba kwa ajili ya ziara ya kikazi yenye lengo la kudumisha ushirikiano kati ya nchi hizo mbili.

Akiwa nchini Cuba Waziri Mkuu anatarajiwa kufanya mazungumzo na viongozi waandamizi wa Cuba kwa lengo la kukuza ushirikiano katika sekta za afya, elimu utalii na Kilimo.

Aidha, nchi ya Cuba ni mojawapo ya nchi zenye ushirikano wa muda mrefu na Tanzania Kisiasa, Kijamii na Kiuchumi.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU, 
JUMATANO, AGOSTI 16, 2017.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiagana na Mkuu wa Wilaya ya Temeke ,Felex Jackson katika Uwanja wa Ndege wa Julias Nyerere Dar es salaam leo August,16/2017 akiwa anaelekea Nchini Cuba Kwa ziara ya kikazi.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

No comments:

Post a Comment