Thursday, November 30

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU WABUNGE WA CUF WALIOVULIWA UBUNGE



TANZANIA NA CHINA KUSHIRIKIANA KUUKABILI UHALIFU WA KIMATAIFA

Tanzania na China wamekubaliana kuimarisha ushirikiano katika maeneo mbalimbali kama njia mojawapo ya kupambana na uhalifu wa kimataifa ambao umekuwa ukiisumbua dunia. Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya kufanyika mazungumzo kati ya Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi na mgeni wake Naibu Waziri wa China mhe. Zhao Dacheng ambae yuko nchini kwa ziara ya siku nne nchini.

Akizungumza baada ya kukamilika kwa mazungumzo hayo, Prof.Kabudi ameyataja makosa ya kimataifa ambayo wamekubaliana kuwa ni makosa ya kimtandao,utakatishaji fedha, usafirishaji binadamu na mengineyo ambayo yamekuwa yakiikabili dunia kwa wakati huu.

Prof.Kabudi pia amesema kwamba wamekubaliana kuimarisha ushirikiano kayika eneo la msaada wa kisheria kwa watu wenye uhitaji ambapo China pia watajifunza kutoka kwa Tanzania katika eneo hilo ambalo Inataka kuwa na sheria yake kama ilivyofanya Tanzania.

Viongozi hao pia wamekubaliana kushirikiana katika eneo la mafunzo ili kuwaongea ujuzi na uwezo watendaji wao kupitia semina za kimataifa au mafunzo maalum ili kubadilidhsna uwezo na uzoefu katika eneo la usimamizi wa sheria nchini. Tanzania na China pia wamekubaliana kushirikiana katika eneo la Mahakama ikiwa ni pamoja na usimamizi na uendeshaji wa Magereza nchini.

Awali akizungumza katika kikao hicho Naibu Waziri wa China Mhe. Dacheng alisema Tanzania ni moja ya nchi marafiki wa dhati wa China urafiki ambao uliasisiwa na viongozi waandamizi wa nchi hizo. Alisema ziara yao nchini inafungua milango mipya ya ushirikiano baina ya China na Tanzania na kuongeza kuwa itazidi kuimarisha uhusiano baina ya nchi hizo.

Amesema anaamini kuwa Wizara yake imedhamiria kuisaidia Tanzania katika sekta ya Sheria ili isonge mbele kama ilivyofanikiwa China na kuongeza kuwa wao pia wataitumia nafasi hiyo kujifunzakatima maeneo ambayo Tanzania imepiga hatua kama eneo la msaada wa sheria kwa watu wake.

Naibu Waziri huyo wa Sheria wa China yuko nchini kwa mwaliko wa Waziri wa Katiba na Sheria wa Tanzania Prof. Kabudi, anatarajiwa kutembelea Shule Kuu ya Sheria ya Chio Kikuu chabDar es salaam na Chama cha Wanasheria Tanganyika na Desemba Mosi ataelekea visiwani Zanzibar ambako atakutana na Jaji Mkuu wa Tanzania na viongozi wengine wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Waziri wa Katiba na Sheria Prof.Palamagamba Kabudi wa pili kushoto akizungumza na ugeni wa Naibu Waziri wa Sheria wa China mhe. Zhao Dacheng katika ukumbi wa mikutano jijini Dar es salaam.
Naibu Waziri wa Sheria wa China mhe. Zhao Dacheng watatu toka kulia na ujumbe wake wakiwa katika ukumbi wa mikutano jijini Dar es salaam.
Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Kabudi aliekaa katikati akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Waziri wa Sheria wa China mhe. Zhao Dacheng wa pili kushoto wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mazungumzo yao jijini Dar es salaam.

Mwaziri wa Uganda watebelea mgodi Tanzania


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa pili kushoto) na Waziri wa Nchi anayeshughulikia Madini wa Uganda, Lokeris Peter (kushoto) wakitembelea mgodi wa Dhahabu wa Blue Reef uliopo Rwamgasa. Wa pili kutoka kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Lughumbi na kulia ni mmiliki wa mgodi huo, Christopher Kadeo.

Mawaziri Wanne kutoka Uganda wakiongozwa na mwenyeji wao Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo Agosti 29, 2017 walitembelea migodi ya dhahabu ya Mkoani Geita inayomilikiwa na Watanzania. Miongoni mwa migodi iliyotembelewa ni Mgodi wa Dhahabu wa Blue Reef uliopo Rwamgasa, Mgodi wa Dhahabu wa Busolwa Gold Mine Project uliopo Nyarugusu na Kituo cha Mfano cha Uchimbaji Madini ya Dhahabu cha Tan Discovery kilichopo Rwamgasa.

Mawaziri hao waliwasili nchini Tanzania Agosti 27, 2017 kwa ajili ya zira ya siku mbili ya kujifunza juu ya Usimamizi wa Sekta ya Madini hususan suala la Uendelezaji wa Uchimbaji Mdogo wa Madini. Kwa mujibu wa Naibu Waziri Nyongo, Mawaziri hao wametembelea migodi hiyo ili kuona namna gani migodi hiyo inaendesha shughuli zake na namna ambavyo serikali imekuwa ikiwasaidia kuhakikisha wanakuwa na uchimbaji madini wenye tija. “Wamekuja kujifunza, kuangalia Sera zetu, Sheria zetu na mchango wa Serikali katika kuwasaidia wachimbaji wadogo,” alisema.

Alisema walipendekeza kutembelea migodi inayomilikiwa na Watanzania ili kujionea namna ambavyo wazawa wanavyoendesha shughuli za uchimbaji madini ikiwa na pamoja na kuzungumza nao ili kupata uzoefu wa uendeshaji wa shughuli husika na kubaini ushirikiano uliopo baina yao na Serikali.

Akizungumza kwa niaba ya Mawaziri wa Uganda, Waziri wa Nchi anayeshughulikia Madini wa Uganda, Lokeris Peter alisema Tanzania ni miongoni mwa nchi Barani Afrika zilizopiga hatua kwenye usimamizi wa Sekta ya Madini hususan eneo la Uchimbaji Mdogo wa Madini ikilinganishwa na nchi zingine walizotembelea.

"Uamuzi wa kufanya ziara nchini humu unafuatia uzoefu wa muda mrefu wa Tanzania kwenye masuala ya uchimbaji wa madini hususan namna ambavyo Tanzania imeweza kurasimisha suala la uchimbaji mdogo," alisema Waziri Peter.

Awali kabla ya kuwasili Mkoani Geita, ujumbe huo wa Mawaziri kutoka Uganda; Agosti 28, 2017 ulikutana na Waziri wa Madini, Angellah Kairuki ambapo ulielezwa masuala mbalimbali yanayohusu sekta husika ikiwemo Sera, Sheria na Kanuni za Madini pamoja na masuala yanayohusu Wachimbaji Wadogo wa madini.

Mawaziri kutoka Uganda waliofanya ziara hiyo ni Waziri wa Nchi- Madini, Lokeris Peter, Waziri wa Nchi- Mambo ya Ndani, Obiga Kania, Waziri wa Nchi- Mamlaka ya Mji Mkuu wa Kampala,  Namugwanya Bugembe na Waziri wa Nchi- Masuala ya Uchumi, Dkt. Kasirivu Atwooki.
Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (kulia) akiongozana na Waziri wa Nchi anayeshughulikia masuala ya Madini nchini Uganda, Lokeris Peter (kulia kwake) mara baada ya kuwasili kwenye Mgodi wa Dhahabu wa Busolwa Gold Mine Project uliopo Nyarugusu.
Mawaziri kutoka Uganda wakiwa pamoja na mwenyeji wao, Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo walipotembelea mgodi wa Dhahabu wa Blue Reef uliopo Rwamgasa ili kujionea shughuli zinavyoendeshwa mgodini hapo.
Mawaziri kutoka Uganda wakimsikiliza mmiliki wa Mgodi wa Dhahabu wa Blue Reef, Christopher Kadeo (hayupo pichani) baada ya kutembelea eneo (shimo) linalochimbwa Dhahabu. Kutoka kushoto ni Waziri wa Nchi- Mambo ya Ndani, Obiga Kania, Waziri wa Nchi- Masuala ya Uchumi, Dkt. Kasirivu Atwooki, Waziri wa Nchi- Madini, Lokeris Peter na Waziri wa Nchi- Mamlaka ya Mji Mkuu wa Kampala, Namugwanya Bugembe.


Naibu Waziri wa Madini, Stanslaus Nyongo (wa nne kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri kutoka Uganda mara baada ya kuwasili kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

WAZIRI MBARAWA ATAKA BODI YA TPA KUFANYA MAAMUZI KWA WAKATI


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa wajumbe wa Bodi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA), na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo Mhandisi Deusdedit Kakoko, kukamilisha Skana mpya (haipo pichani), ambayo inajengwa kwa ajili ya ukaguzi wa mizigo inayoingia Bandarini hapo ambayo haijakamilika hadi sasa.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, amesema anasikitishwa na utendaji wa Bodi na Menejimenti ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), kutofanya maamuzi kwa wakati hali ambayo inachangia malalamiko kuongezeka Bandarini hapo. Aidha, Mbarawa amesema Serikali inapeleka Naibu Mtendaji Mkuu mpya wa shughuli za Uendeshaji Bandarini hapo kutokana na aliyekuwepo kushindwa kusimamia majukumu yake ipasavyo.

Profesa Mbarawa amesema hayo leo wakati wa ziara ya kushtukiza aliyoifanya bandarini ikiwa ni siku chache baada ya Rais John Magufuli, na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kufanya ziara ya kustukiza na kubaini madudu bandarini hapo.   Ziara ya Waziri Mbarawa ni mwendelezo wa ziara mbalimbali bandarini hapo kubaini uendeshaji na utendaji wa shughuli zinazotolewa na Mamlaka hiyo.
Muonekano wa Skana mpya ambayo inajengwa kwa ajili ya ukaguzi wa mizigo inayoingia Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), ambayo haijakamilika hadi sasa.

“Nimelazimika leo kuwaita Watendaji na Bodi ya TPA ili kuwaeleza kasoro zenu ambapo inaonesha wazi kuwa asilimia kubwa ya mambo yanayotokea humu ni kuwa mnakuwa wazito katika kutoa maamuzi”, amesema Profesa Mbarawa.   Amesema katika bandari hiyo ipo mizigo ya kahawa ambayo imefika bandarini tangu mwaka 2014 huku kukiwa hakuna sababu za kueleweka za wenye mali kutochukuwa mizigo yao.  

Profesa Mbarawa amesema hahitaji wasaidizi ambao wanakaa katika vikao na kulipana posho ila wanapaswa kufanya kazi ya kuangalia shughuli zote za bandari.   “Kama hamtabadilika nitaendelea kuja katika bandari hii ili kuchukua hatua pale ambapo inaonekana kwani haipendezi kila kukicha malalamiko kutokea,” amesisitiza Waziri Mbarawa.  
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akitoa maelekezo kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Profesa Ignatus Rubaratuka (Wakwanza kushoto), wakati akikagua shehena ya kahawa iliyohifadhiwa Bandarini hapo kwa muda mrefu.

Aidha, Waziri Mbarawa ameitka bodi na menejimenti kuhakikisha kuwa inatatua changamoto iliyopo katika bandari ya kushusha na kupakia mizigo kutoka Zanzibar na kuingia Tanzania Bara ambapo wafanyabiashara wanalalamikia utaratibu unaotumika kuwahudumia.   Amesema haingii akilini kuona mizigo inayotoka au kwenda Zanzibar kutozwa kodi baada ya masaa huku inayotoka nje ya Tanzania ikitozwa baada ya siku saba.   

Kuhusu ujio wa Naibu mtendaji Mkuu mpya Mbarawa aliitaka Bodi na menejimenti kumpa ushirikiano ili aweze kutoa matokeo chanya kwenye bandari.   “Tunaleta Naibu Mtendaji Mkuu mpya ambaye atasimamia operesheni, naomba apewe ushirikiano ili kusaidia Serikali huyu ambaye anakaimu tunamuondoa ameshindwa kwenda na kasi yetu,” amefafanua Profesa Mbarawa.  
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, akikagua shehena ya kahawa iliyohifadhiwa tangu mwaka 2014 hadi sasa katika ghala iliyopo katika Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Dar es Salaam. Pembeni yake ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka hiyo, Profesa Ignatus Rubaratuka akishuhudia ukaguzi huo.

Akizungumza baada ya ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya TPA Ignas Rugaratuka, amesema wamejipanga kikamilifu kuhakikisha kuwa wanaitendea haki nafasi waliyopewa kwa kusimamia mabadiliko ndani ya bandari.   Amesema tangu waingie wamekuwa wakipambana kuhakikisha kuwa mapungufu ya TPA yanaisha ambapo wamefanikiwa kurekebisha kwenye utawala kwa kutoa mafunzo kwa watumishi na kuzuia wizi ambao ulikuwa umekithiri.   

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Mhandisi Deusdedit Kakoko, amesema kuwa tangu aingie katika mamlaka hiyo wamekuwa wakifanya jitihada za kurekebisha mapungufu na kumuahidi waziri kuwa ataongeza jitihada zaidi.

  “Kama ni mabadiliko tumefanya makubwa sana hasa katika utawala na uongozi ila kila anayehusika katika sekta hiyo anapaswa kutoa msaada,” amesema Mkurugenzi Mkuu.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania(TPA), Mhandisi Deusdedit Kakoko, akifafanua jambo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, alipofika Bandarini hapo leo wakati wa ziara ya kushtukiza kuangalia uendeshaji wa huduma Bandarini hapo.

CHINA YAAHIDI KUFADHILI UJENZI WA RELI KWA KIWANGO CHA KIMATAIFA (SGR)

BALOZI wa China hapa nchini, Wang Ke amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango na kuahidi kuwa nchi yake iko tayari kushawishi taasisi za fedha ikiwemo Benki ya EXIM ya nchini humo kushiriki ujenzi wa reli ya kati kwa kiwango cha kimataifa baada ya kufanyika kwa upembuzi yakinifu wa mradi huo.

Alisema kuwa kutokana na ukubwa wa mradi huo, unaokadiriwa utagharimu Dola za Marekani bilioni 7.6 hadi kukamilika kwake, utahitaji kufanyiwa upembuzi yakinifu ili kukidhi masharti ya kupata mkopo kupitia Benki ya Exim na taasisi nyingine zitakazotaka kujenga mradi huo muhimu. 

“Mradi huu ni muhimu na wa kihistoria kwa nchi hizi mbili, China ingependa kuona mradi huo unaboreshwa ili uweze kutoa huduma ya kusafirisha mizigo na abiria na kwamba kuimarika kwake kutaokoa miundombinu ya barabara kwa kuwa shehena kubwa ya mizigo itasafirishwa kupitia reli hiyo.

Aidha, Balozi Ke alisema kuwa nchi yake inasubiri pia kukamilika kwa taratibu za ndani kati yake na Tanzania ili mradi wa reli ya TAZARA uanze  ili kuboresha usafiri na usafirishaji wa mizigo na abiria kati ya Tanzania na Zambia pamoja na nchi za maziwa makuu.

Balozi Ke alitumia fursa hiyo kupongeza kazi nzuri inayofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano kwa kukusanya kodi, kusimamia matumizi adili ya fedha za umma, kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na kupambana na rushwa.

Akizungumza mara baada ya mazungumzo na mgeni wake, Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango alisema kuwa Serikali imeridhia uamuzi wa China wa kufanya upembuzi yakinifu wa mradi huo wa Reli ya Kati kwa kiwango cha Kimataifa (SGR) ili China kupitia taasisi zake iweze kujenga sehemu ya mradi huo.

“Tayari mradi umeanza kujengwa kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma, kwahiyo kujitokeza kwa China kutaka kufadhili ujenzi wa mradi huo kutasaidia kukamilisha mradi huo muhimu kwa haraka na kwa wakati” Alisema Dkt. Mpango.

Alisema pia kuwa China imeonesha nia ya kusaidia kuujenga na kuupanga mji wa Dodoma kutokana na nchi hiyo kuwa na uzoefu wa kupanga miji ambapo nchi hiyo imeonesha nia ya  kujenga miundombinu ya elimu, barabara, uwanja wa ndege wa kimataifa-Msalato, kujenga mfumo wa maji safi na maji taka pamoja na majengo ya kisasa.

Kuhusu biashara, Dkt. Mpango alisema wamekubaliana kuwa China itaisaidia Tanzania kukuza kiwango cha biashara ambapo takwimu zilizoko zinaonesha kuwa urari wa biashara kati ya nchi hizo unaonesha kuwa Tanzania imekuwa ikinunua bidhaa nyingi kutoka nchini humo kuliko inavyo uza bidhaa na huduma zake.

“Mwaka 2016 Tanzania iliuza China bidhaa na huduma zenye thamani ya Dola za marekani milioni 460 wakati China iliuza hapa nchini bidhaa zenye thamani ya Dola za Marekani bilioni 1.2, kiwango ambacho ni kikubwa karibu mara 5 ya kile tulichowauzia” Alisema Dkt. Mpango.

Ili kuvutia Sekta ya utalii, Tanzania imeiomba China kuanzisha safari ya ndege wa moja kwa moja kutoka China hadi Tanzania ili kuvutia watalii wengi kutoka nchini humo na kwamba utaratibu utafanyika ili Mamlaka ya usafiri wa anga iweze iratibu na kusaini makubaliano ya ushirikiano na hivyo kufanikisha jambo hilo.

“China imeandaa maonesho makubwa ya uwekezaji na biashara ya bidhaa na huduma mbalimbali mwezi Novemba, 2018, hivyo wafanyabiashara wa Tanzania pamoja na  Bodi ya Utalii nchini wahakikishe wanashiriki kikamilifu kwenye maonesho hayo ili kutumia nafasi hiyo kujitangaza” Alisistiza Dkt. Mpango.

Aidha, Dkt. Mpango alieleza kuwa Balozi Wang Ke, amesema kuwa Nchi yake itashiriki katika ujenzi wa miradi ya bandari ili kukuza masuala ya usafiri kwa kuboresha bandari za Tanga, Bagamoyo, Kigoma, Bagamoyo, Dar es Salaam, Mtwara na katika Ziwa Victoria na Ziwa Tanganyika.

Waziri huyo wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango alitoa wito kwa wawekezaji kutoka China na nchi nyingine kuja kuwekeza nchini katika kipindi hiki ambacho Tanzania inaipeleka nchi katika uchumi wa viwanda.

Miradi mikubwa ambayo China imewekeza na kufadhili hadi sasa hapa nchini ni Reli ya TAZARA, Kiwanda cha Urafiki, ujenzi wa barabara, majengo, ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi dar es Salaam, Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dare Salaam, Ujenzi wa Mabweni ya wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na miradi mingine kadha wa kadha.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (katikati),  Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke (wa pili kulia), Mwakilishi wa masuala ya Uchumi na Biashara wa Ubalozi wa China Bw. Lin Zhiyong (wa pili kushoto) pamoja na maafisa waandamizi kutoka Wizara ya Fedha na Mipango  wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa Mkutano kati ya pande hizo kuhusu Biashara, uwekezaji na ushirikiano, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango (Kulia) na mgeni wake Bi. Wang Ke, wakitoka nje ya Jengo la Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam baada ya kumalizika kwa mkutano kati yao uliohusu masuala mtambuka ya ushirikiano kati ya Tanzania na China.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) na Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke,  wakiagana   baada ya kumalizika kwa Mkutano kati yao ambapo balozi huyo aliahidi kuendeleza ushirikiano wa kiuchumi, kijamii na kiutamaduni kati nchi hizo mbili, katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam. 
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb) (kulia) akiagana na Mwakilishi wa masuala ya Uchumi na Biashara wa Ubalozi wa China  nchini Tanzania Bw. Lin Zhiyong baada ya kumalizika kwa Mkutano kati ya Waziri huyo na Balozi wa nchi hiyo Bi. Wang Ke (hayupo pichani), katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Kamishina wa Fedha za Nje Bw. John Rubuga (kushoto) na Afisa anayeshughulikia masuala ya nje katika dawati la China Bw. Alfonce Mayala kutoka Wizara ya Fedha na Mipango wakifuatilia kwa makini majadiliano kati ya Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke,  na Waziri wa Fedha na Mipango (hawapo pichani), katika ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), wa pili kulia akieleza kuhusu fursa zilizopo katika Sekta ya Utalii wakati wa  Mkutano kati yake na Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke, (hayupo pichani), Jijini Dar es Salaam, kulia ni Kamishna wa Fedha za Nje wa Wizara ya Fedha na Mipango, Bw. John Rubuga.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), wa tatu kulia akiwa katika mkutano na  Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke (wa pili kushoto) ambapo walikubaliana kuendeleza ushirikiano katika Biashara na uwekezaji kwa manufaa ya pande hizo mbili, mkutano uliofanyika katika Ukumbi wa Wizara ya Fedha na Mipango Jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Isdor Mpango (Mb), akieleza kuhusu kuwa na uwiano wa kibiashara kati ya Tanzania na China kwa manufaa ya pande hizo mbili wakati wa mkutano kati yake na Balozi wa China nchini Tanzania Bi. Wang Ke, (hayupo pichani), Jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa China hapa Nchini Bi. Wang Ke, (katikati) akiongoza maafisa wake wa ubalozi wa nchi hiyo hapa nchini wakati wa mkutano kati yake na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), Jijini Dar es Salaam.
Balozi wa China hapa nchini, Bi. Wang Ke, akisisitiza jambo alipokutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), Jijini Dar es Salaam.(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha na Mipango)

RAIS DKT. MAGUFULI AMTEUA BI. STELLA CHAGI KUWA MSAJILI WA MABARAZA YA ARDHI NA NYUMBA WA WILAYA

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MWANZA AKANUSHA TAARIFA ILIYOPO KATIKA GAZETI LA MWANANCHI LA TAREHE 30/11/2017

LEO TAREHE 30.11.2017 KAMANDA WA POLISI MKOA WA MWANZA NAIBU KAMISHINA WA POLISI AHMED MSANGI (PICHANI), AMEKANUSHA TAARIFA ILIYOPO KATIKA GAZETI LA MWANANCHI LA TAREHE 30/11/2017, TOLEO NAMBA 6334, UKURASA WA TATU, INAYOSEMA KUWA AMETHIBITISHA JUU YA KUWEPO HEWA YA SUMU NDANI YA UKUMBI WA CITY MALL AMBAPO KULIKUWA KUKIFANYIKA MKUTANO MKUU WA UCHAGUZI WA VIJANA WA CCM (UVCCM) MKOA WA MWANZA.


AIDHA KAMANDA MSANGI ANASEMA, UKWELI NI KUWA ALIPIGIWA SIMU NA MWANDISHI WA GAZETI HILO TAREHE 29/11/2017 MAJIRA YA SAA 15:00 MCHANA ALIYETAKA KUTHIBITISHIWA TAARIFA YA KUWEPO HEWA YA SUMU NDANI YA UKUMBI WA CITY MALL  AMBAPO KULIKUWA KUKIFANYIKA MKUTANO TAJWA HAPO JUU. 


KAMANDA ALIMJIBU KUWA HANA TAARIFA NA HAWEZI KUTHIBITISHA KWANI HAJAPATA TAARIFA YEYOTE KUHISIANA NA YALIYOTOKEA KATIKA MKUTANO HUO, NA YEYE YUPO KWENYE KIKAO CHA KAMATI YA ULINZI NA USALAMA OFISI YA MKUU WA MKOA.

PIA KAMANDA HAKUFIKA ENEO TAJWA KAMA TAARIFA HIYO  INAVYOSEMA, HIVYO INAONEKANA MWANDISHI WA TAARIFA HIYO ALIAMUA KUANDIKA MANENO HAYO KWA MANUFAA YAKE BINAFSI HIVYO JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINAOMBA GAZETI HUSIKA KUREKEBISHA. PIA ANAOMBA WAELEWE KUWA MATUKIO YA AINA KAMA HIYO YANAHITAJI YAWE NA MAJIBU YA KITAALAMU TOKA KWA WANASAYANSI PINDI YANAPOTOKEA. 

AIDHA JESHI LA POLISI MKOA WA MWANZA LINANAEDELE KUOMBA USHIRIKIANO TOKA KWA WAANDISHI WA HABARI KWA KUFANYA KAZI KWA PAMOJA ILI KUWEZA KUENDELEA KUDUMISHA USALAMA NA ULINZI KATIKA MKOA WETU. PIA JESHI LINAWAOMBA WAANDISHI WA HABARI KUFANYA KAZI KWA KUFUATA TAALUMA YA UANDISHI WA HABARI, UWELEDI NA MAADILI YA UANDISHI WA HABARI ILI KUEPUSHA HABARI ZA AINA KAMA HII AMBAZO ZINALETA PICHA MBAYA KWA JESHI NA MKANGANYIKO KWA JAMII.

IMETOLEWA NA;
DCP: AHMED MSANGI
KAMANDA WA POLISI (M) MWANZA.

MWAMUZI MTANZANIA KUCHEZESHA KOMBE LA DUNIA KWA WANAWAKE 2018 NCHINI URENO

\\\
Mtanzania Jonesia Rukyaa Kabakama ameteuliwa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA), kuchezesha fainali zijazo za Kombe la Dunia kwa wanawake (Algarve Cup) zitakazofanyika nchini Ureno, mwezi Februari, mwakani.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka TFF, Jonesia, ambaye ni mwanamke, ameteuliwa kupuliza filimbi katika fainali hizo ambazo hukutanisha timu mahiri zilizofanya vema katika michuano ya kila Bara.
Lakini kabla ya kwenda Ureno, Jonesia anatarajiwa kushiriki semina maalumu iliyoandaliwa na FIFA. Semina hiyo itafanyika Doha, Qatar kuanzia Februari 12- 16, mwakani.
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania limempongeza Mwamuzi Jonesia kwa kuteuliwa na FIFA kuchezesha fainali za Kombe la Dunia na kuhudhuria semina hiyo muhimu kwa maendeleo ya mpira wa miguu.
Waamuzi wengine walioteliwa kutoka Afrika Lidya Abebe wa Ethiopia, Glady Lengwe wa Zambia na Salima Mukansanga wa Rwanda.

WCF YAPATA HATI SAFI KATIKA UKAGUZI WA TAARIFA YA FEDHA ULIOFANYWA NA CAG

 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, akifafanua baadhi ya mambo wakati viongozi wa Mfuko walipokuwa wakiwasilisha taarifa za utendaji wake kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Mwaka wa Wadu kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, AICC, jijini Arusha leo Novemba 30, 2017.



MFUKO wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF) umepata hati safi katika taarifa ya hesabu zake za fedha katika kipinmdi cha mwaka 2015-2016 ikiwa ni mwaka mmoja tu tangu kuanzishwa kwake.

Katika taarifa hiyo mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2016 (mwaka wa kwanza tangu kuaza kufanya kazi zake), thamani ya Mfuko ilifikia shilingi bilioni 65.68 na mfanikio haya yaliweza kufikiwa kutokana na ubunifu na ushirikiano mkubwa kati ya Mtendaji Mkuu wa Mfuko na Bodi ya Udhamini, Mkurugenzi wa Fedha na Mipango wa Mfuko huo, Bw.Bezil Kwala, aliwaambia wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Kwanza wa Wadau wa Mfuko huo unaoingia siku yake ya pili nay a mwisho kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa, AICC jijini Arusha, wakati akiwasilisha taarifa hiyo ya fedha leo Novemba 30, 2017.

Amesema Mfuko umekuwa ukiaandaa hesabu zake kwa kuzingatia viwango vya kimataifa vya uaandaji wa hesabu za fedha na kwa mujibu wa sheria CAG ndiye mwenye mamlaka ya kufanya ukaguzi na Hati Safi ni uthibitisho wa taarifa ya fedha za Mfuko kuonyesha hali halisi na kutokuwa na dosari ya aina yoyote.
Amesema katika ukaguzi huo, CAG alishirikiana na kampuni ya PricewaterhouseCoopers (PwC). Mwakilishi wa kutoka Ofisi ya CAG, Bw…….. amethibitishia wajumbe usahihi wa taarifa hiyo ya fedha ya WCF.
Mkutanmo huo ambao umeanza Novemba 29, 2017 na kubeba kauli mbiu isemayo, "Mafao ya Fidia: Haki ya Mfanyakazi na chachu katika kukuza uchumi wa viwanda”, pia ulipokea taarifa ya mipango ya uwekezaji ambapo Bw. Kwala aliwaambia wajumbe kuwa, katika kipindi kati ya mwaka 2017/18 – 2021/22, Mfuko umepanga kuwekeza kwenye miradi mbalimbali itakayoleta faida kwa mujibu wa tathmimi za kitaalamu zitakazofanyika.
“Maeneo tuliyoyaanisha katika uwekezaji kwenye sekta ya viwanda ni pamoja na kiwanda cha Grape Processing Factory kwa ushirikiano kati ya  GEPF na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino, kiwanda cha Madawa mkoani Simiyu kwa kushirikiana na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) na Kiwanda cha Morogoro Canvas Mills kwa kushirikiana na mifuko ya WCF, NSSF, PSPF, GEPF, na LAPF”. Alifafanua.
Akifafanua zaidi kuhusu umuhimu wa Mfuko kuwekeza, Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw.Masha Mshomba alisema, fedha zitokanazo na michango ya Wanachama ni kidogo ukilinganisha na mahitaji halisi ya ulipaji Mafao ya fidia na kwa hali hiyo, ni muhimu Mfuko kuwekeza ili kupanua wigo wa kuongeza mapato na hivyo kuendelea kutoa Mafao ya Fidia bila ya shaka yoyote.
 Baadhi ya Wakurugenzi na Wakuu wa Idara wa WCF wakiwa kwenye mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba, akizungumza
 Mkurugenzi wa Fedha WA WCF, Bw.Bezil Kwala, akiwasilisha ripoti ya fedha ya Mfuko kwa mwaka wa 2015-2016.
 Msaidizi wa Mkaguzi Mkuu wa Ofisi ya Mdhibiti wa Hesabu za Serikali (CAG), Bw. Johanes Joel Kisiri, akisikiliza uwasilishaji wa taarifa hiyo ya fedha.
 Mkuu wa Kitengo cha Sheria cha WCF, Bw.Abraham Siyovelwa, akitoa mada kuhusu Sheria juu ya kuanzishwa kwa Mfuko na jinsi unavyofanya kazi zake. Pamoja na mambo mengine Bw. Siyovelwa aliwaambia wajumbe kuwa,   Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi (WCF) ni taasisi ya hifadhi ya jamii iliyoazishwa kwa mujibu wa kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi Sura Na. 263 (Marejeo ya 2015) na kuanza kazi rasmi tarehe 1 Julai 2015. Lengo la kuazishwa kwa Mfuko ni kushughulikia masuala ya fidia kwa wafanyakazi waliopo katika sekta rasmi (Binafsi na Umma) Tanzania bara ambao wataumia, kuugua ama kufariki kutokana na kazi
 Mkurugenzi wa Uendeshaji wa WCF, Bw. Anslem Peter, akiwasilisha taarifa ya uendeshaji ya Mfuko katika kipindi cha uahai wake, ambapo alisema Mfuko umekuwa ukifanya vizuri ikiwa ni pamoja na usajili wa wanachama " katika kipindi cha kuanzia mwaka 2015-2017 jumla ya Waajiri 5,178 walisajiliwa ikiwa ni asilimia 71.92 ya lengo la kusajili waajiri 7,200


 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Dkt.Irene Isaka.
 Kiongozi wa chama cha Waajiri nchini (ATE), Bw. Aggrey Mlimuka, akizungumza kwenye mkutano huo.
 Bw. Hiroshi Yamabana kutoka Shirika mla Kazi Duniani, (ILO), akiuliza masuala mbalimbali kuhusu upembuzi juu ya usalama mahala pa kazi
 Tommie Dounball, kutoka kampuni ya Argen ya Afrika Kusini, akizungumzia uzoefu wa masuala ya Mfuko wa Fidia kutoka nchini kwake


 Bw. Mshomba (kushoto), akizungumza jambo wakati wa mkutano huo. Kulia ni Bw.Tommie Dounball, kutoka kampuni ya Argen ya Afrika Kusini,


 Mbunge wa jimbo la Mlalo Mkoani Tanga, Mhe. Rashiud Shangazi, (kushoto), akimsikiliza Meneja Uhusiano wa PPF, Bi. Lulu Mengele. Wote hao ni miongoni mwa wadau walioalikwa kushiriki mkutano huo.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wdhamini ya WCF, Bw. Emmanuel Humba, (kulia), akibadilishana mawazo na Mkurugenzi Mkuu wa Taifa wa Bima ya Afya, (MHIF), Bw. Afya, Bw. Bernard Konga.

Mkurugenzi wa Matekelezo na Uandikishaji wa Mamlaka ya Usimamizi na Udhibiti wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Bi. Lightness Mauki