Wednesday, November 22

MWANAFUNZI WA CHUO CHA UHAZILI TABORA AKUTWA AMEJINYONGA KWA KUTUMIA TAI


MWANACHUO mmoja Chuo cha Utumishi wa Umma –Tawi la Tabora kinachojulikana kama Uhazili  Raphael Kadesha (22)  amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia tai ya kuvaa shingoni.

Kwa mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Graifton Mushi tukio hilo limetokea jana saa 4 asubuhi ambapo marehemu alifunga tai juu ya kitanda chake.

Alisema kuwa marehemu alikuwa akisoma kozi cha Cheti cha Awali cha Utawala katika Chuo hicho.

Mushi aliongeza kuwa chanzo cha kifo hicho hakijulikani na Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi kujua nini kilimfanya mwanachuo huyo kuchukua maamuzi hayo yaliyoacha simanzi katika jamii yake na Chuo kwa ujumla.

Alitoa wito kwa wanachuoni kuomba ushauri kwa viongozi wao Chuo au wa kiroho pindi wanapokuwa na matatizo binafisi kwani kujiua sio suluhisho la matatizo bali ni kuwaongezea walezi wao shida na majonzi zaidi.
Mushi alisema kuwa mwili wa marehemu umehifahiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete.

Naye Mkurugenzi wa  Chuo hicho Dkt. Ramadhani Marijani alitoa wito kwa wanachuo kuwa watulivu wakati Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi wa sababu zilizopelekea mwanachuo huyo kuchukua maamuzi yaliyoacha simamazi sio tu kwa familia yake bali hata kwa Jumuiya nzima ya Uhazili.

Alisema kuwa ni vema kama kuna mwanachuo yoyote anakuwa na tatizo au msongo wa mawazo kuwaeleza viongozi wake wawe wa Serikali ya Wanafunzi, Mama Mlenzi, Mshauri wa Wanachuo au Mkurugenzi mwenye ili waweze kusaidia katika ushauri utakaowapa ufumbuzi kuliko kuchukua maamuzi ya haraka.

NCC YATAKIWA KUZINGATIA UBORA WA MIUNDOMBINU NCHINI

Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) limetakiwa kuzingatia ubora katika kutekeleza kazi zake ili kuokoa fedha zinazotolewa kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali nchini.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa alipokuwa akijitambulisha na kuongea kwa mara ya kwanza na Wafanyakazi wa Baraza hilo jana jijini Dar es Salaam.Kwandikwa amesema kuwa Taasisi hiyo ni muhimu na ina manufaa kwa nchi ingawa kuna maeneo ambayo yanahitaji kusukumwa zaidi ili kazi zinazofanywa zizidi kuleta tija zaidi kwa Taifa.

“Baraza hili ni kama jicho katika Wizara kwa sababu majukumu yake yamejikita katika kusimamia Sera, hivyo Wafanyakazi tunatakiwa tujikite zaidi katika kufanya kazi zinazoonyesha ubora wa hali ya juu”, alisema Kwandika. 

Akizungumzia juu ya upunguzaji wa gharama za ujenzi, Naibu Waziri amesema kuwa gharama za ujenzi zinabadilika mara kwa mara, hivyo ni lazima zichunguzwe ili ujenzi ufanyike kwa bei ndogo lakini uwe katika kiwango bora zaidi na fedha zinazobaki zitumike kwa shughuli nyingine.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa NCC, Matiko Mturi amesema ili kutekeleza majukumu yake kikamilifu, kwa mwaka huu wa fedha Baraza limejiwekea malengo mbalimbali yakiwemo kukusanya maoni ya Wadau na kuandaa kuhusu utendaji wake ili kufanya maboresho ya utoaji wa huduma na shughuli zinazotekelezwa na Baraza.

Malengo mengine ni kuandaa na kukamilisha Kanuni za utekelezaji washeria, kuratibu na kutoa mafunzo kwa Wadau, kutoa ushauri wa kiufundi na kutatua migogoro, kufanya ukaguzi wa miradi ya ujenzi inayotumia fedha za Umma pamoja na jitihada za kutunisha Mfuko wa Maendeleo ya Ujenzi.

“Katika kipindi cha kuanzia Julai hadi Oktoba mwaka huu, tumetoa ushauri mbalimbali ikiwa ni jukumu letu la msingi katika mradi wa ujenzi wa nyumba za kuishi za magomeni, tulitathmini usahihi wa idadi ya nondo katika ujenzi wa jengo la maabara iliyopo katika eneo la Mabibo, pia tulifanya tathmini ya thamani ya pesa katika jengo la dharura lililopo Makumbusho pamoja na tathmini ya kiufundi ya miradi inayotekelezwa kwa kutumia fedha za Mfuko wa Barabara”, alisema Mturi

Baraza la Taifa la Ujenzi lilianza kazi rasmi mwaka 1981 likiwa na lengo kuu la kuboresha shughuli zinazofanywa na Sekta ya ujenzi ambapo jukumu lake kubwa ni kutoa uongozi wa kimkakati wa kuendeleza Sekta ya ujenzi kwa nia ya kuboresha uwezo wa Wataalam na Taasisi za ndani zinazotoa huduma katika Sekta ya ujenzi.
Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Matiko Mturi (kulia) akizungumza na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa mara baada ya kuripoti ofisini hapo jana Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha na kuongea na wafanyakazi wa Baraza hilo.
Mtendaji Mkuu wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC), Matiko Mturi (kulia) akitoa taarifa fupi mbele ya Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa pamoja na wafanyakazi wa baraza hilo alipofika kwa mara ya kwanza ofisini hapo jana Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kujitambulisha na kuongea na wafanyakazi wa Baraza hilo.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, (Sekta ya Ujenzi), Elias Kwandikwa akiongea na wafanyakazi wa Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) jana Jijini Dar es Salaam katika kikao kilichofanyika kwa mara ya kwanza kwa ajili ya kujitambulisha na kuongea na wafanyakazi hao.

MENEJA WA NYANZA CORMERCIAL FARM APIGWA FAINI YA SH MILIONI 534 AU KIFUNGO CHA MIAKA 20 KWA KUKUTWA NA KUCHA 17 ZA SIMBA


Na Karama Kenyunko, blogu ya Jamii.
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu meneja wa Nyanza Commercial Farm, Dilipkumar Pater, kulipa faini ya Sh milioni 53.4 ama kutumikia kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya kukutwa na kucha 17 za simba kinyume na sheria.

Hukumu hiyo imetolewa leo Novemba 22 na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Cyprian Mkeha, 

Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Mkeha alisema ameridhika na ushahidi wa mashahidi wanne uliotolewa upande wa mashtaka na vielelezo vitatu kuwa mshtakiwa kweli alitenda kosa hilo Katika kesi hiyo, mshtakiwa Pater alijitetea mwenyewe.

Hakimu Mkeha amesema mahakama imemuona mshtakiwa Pater ana hatia baada ya upande wa mashtaka kuthibitisha kesi yao pasipo kuacha shaka.

Katika ushahidi, upande wa utetezi waliwasilisha, vielelezo vitatu ambavyo ni kucha za simba, hati ya ukamataji na cheti cha kutathmini kucha hizo.
Kabla ya kusomwa hukumu hiyo, Hakimu Mkeha alimuuliza Wakili wa serikali kama alikuwa na lolote la kusema ndipo, wakili Elia Atanas kwa kushirikiana na wakili Batlida Mushi aliiomba mahakama Kutoa adhabu kali ili iwe fundisho kwa watu wengine.

Akijitetea kabla ya kusomewa hukumu hiyo Pater alidai a yeye ni mgonjwa na anategemewa na familia. "Kutokana na ushahidi uliotolewa unaonyesha mshtakiwa alibeba kucha hizo huku akijua ni kosa na akajaribu kuzisafirisha kwenda nchini India kupitia Dubai" amesema Mkeha.

Katika kesi hiyo mshtakiwa huyo anadaiwa kuwa Novemba 19, mwaka 2016, katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Pater alikutwa na kucha 17 za Simba zenye thamani ya Sh 53,483,500 bila ya kuwa na kibali kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyamapori.

RC MAKONDA ATINGA OFISI ZA CLOUDS MEDIA GROUP KUWAPA POLE



 Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar,ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mh Paul Makonda wamefika mjengoni Clouds Media Group kutoa pole  na kujionea athari zilizosababishwa na moto uliozuka jana asubuhi katika ofisi hizo zilizopo Mikocheni jijini Dar.Pichani wa pili kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hiyo Bwa.Joseph Kusaga.
  Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar,ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mh Paul Makonda wakipata maelezo mafupi mara baada ya kufika katika jengo la Clouds Media Group kutoa pole  na kujionea athari zilizosababishwa na moto uliozuka jana asubuhi katika ofisi hizo zilizopo Mikocheni jijini Dar.
Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Mh Paul Makonda akisalimiana na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni  ya Clouds Media Group Bwa.Joseph Kusaga mara baada ya kuwasili katika ofisi hizo kutoa pole  na kujionea athari zilizosababishwa na moto uliozuka jana asubuhi katika ofisi hizo zilizopo Mikocheni jijini Dar.Pichani kati ni Mmoja wa Maafisa Uhusiano wa Kampuni hiyo Simon  Simalenga

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII, MHE. JAPHET HASUNGA AAGIZA KUUNDWA KWA CHOMBO CHA KUDHIBITI UBORA WA MAZAO YA MISITU NCHINI


Na Hamza Temba – WMU
..........................................................
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga ameuagiza uongozi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kubuni utaratibu mpya ikiwemo kuanzishwa kwa chombo kitakachosimamia upangaji wa madaraja ya ubora wa mbao zinazozalishwa hapa nchini ziweze kukidhi viwango vya mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

Ametoa agizo hilo jana kwenye kikao cha majumuisho na watumishi wa Shamba la Miti la Serikali la Kiwira ambalo linasimamiwa na wakala huyo wakati anahitimisha ziara yake ya kikazi ya siku moja katika Wilaya ya Rungwe Mkoani Mbeya.

“Kuna changamoto kubwa kwenye soko la mbao, kwa kiwango kikubwa mbao zetu nyingi tunaziuza hapa nchini, Lazima tufike mahali hizi mbao tuwe tunaziexport (uza nje) kwa kiwango kikubwa. Lakini ili tufikie malengo hayo mbao zetu lazima ziwe kwenye kiwango kinachokubaliwa.

“Mbao zinazokuwepo kwenye soko letu la ndani huwezi kuzitenganisha kwamba hizi ni za TFS au za mwananchi wa kawaida, nyingine zina ubora nyingine hazina, agizo langu kwenu kaeni chini kama watendaji tuje na utaratibu utakaotuwezesha kuzipanga kwenye madaraja, daraja la kwanza, la pili, la tatu au la nne ili mnunuzi ajue ananunua mbao ya ubora wa aina gani,” alisema Hasunga.

Alisema amepata taarifa kuwa baadhi ya wananchi wanavuna miti ambayo haijakomaa jambo ambalo linaathiri ubora wa mbao kwenye soko kwa kutokidhi mahitaji ya wateja, hivyo akaagiza Wakala huyo kubuni mbinu mpya za kuwalinda wateja ikiwemo kuanzishwa kwa chombo maalum cha udhibiti wa ubora wake.

"Kwa maeneo mengine tuna TBS, kwenye chakuka tuna TFDA, kwenye mbao je? Nani anaregulate?(dhibiti), ni lazima tufike mahali tuwe na mdhibiti atakayetusaidia kuhakikisha kwamba ubora unakuwepo,” alisema Hasunga.

Aidha alitoa wito kwa taasisi hiyo kuendelea kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kuvuna miti ikiwa imeshakomaa ikiwa ni pamoja na kuongeza uzalishaji wa miche ya miti na kuhamasisha wananchi wapande miti zaidi kwa faida yao na taifa kwa ujumla.

Akizungumzia nidhamu kwenye Utumishi wa Umma, Naibu Waziri Hasunga alisema Serikali ya awamu ya tano haitomvumilia mtumishi yeyote atakayejihusisha na vitendo vya rushwa, uzembe au uvivu kwenye kutekeleza majukumu ya Serikali kwa kua sifa hizo ni chanzo kimojawapo kikubwa cha umasikini nchini.

Kwa upande wa kampeni ya upandaji miti kitaifa, alisema Serikali itafuatilia nchi nzima kuona utekelezaji wa agizo hilo ambalo linaitaka kila Wilaya kupanda miti milioni moja na laki tano kwa mwaka ikiwa ni pamoja na kuweka mikakati ya pamoja ya kuhakikisha miti mingi zaidi inapandwa kwa kuwashirikisha zaidi wananchi.

Kwa upande wake, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Zawadi Mbwambo alisema taasisi hiyo imewahi kupokea malalamiko juu ya ubora hafifu wa baadhi ya mbao zinazopatikana kwenye soko ambazo baadhi ya wananchi hutumia jina la Shamba la Miti Sao Hill kuziuza na hivyo kuharibu sifa ya shamba hilo.

Alisema maagizo yote aliyoyatoa Naibu Waziri Hasunga yatafanyiwa kazi kupitia vikao halali vya kiutendaji vya taasisi hiyo ikiwemo vile vya kuandaa mikakati ya utekelezaji wa majukumu yake ya uhifadhi.

Awali Meneja wa Shamba la Miti Kiwira, William Dafa akiwasilisha taarifa yake kwa Naibu Waziri Hasunga, alisema shamba hilo ambalo lilianzishwa mwaka 1964 likiwa na hekta 2,713 limekuwa na maendeleo mazuri ambapo mwaka 2016/2017 lilivuka malengo ya makusanyo ya mapato ya Serikali kutoka bilioni 1.3 hadi bilioni 1.7.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kushoto) akizungumza na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mbeya, Mariam Mtunguja (wa pili kushoto) alipofika ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo akiongozana na Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Mhe. Juliana Shonza (wa pili kulia) kwa ajili ya kujitambulisha wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi mkoani humo.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akimsikiliza Meneja wa Shamba la Miti Kiwira, William Dafa wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi katika shamba hilo jana katika Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akimsikiliza Meneja wa Shamba la Miti Kiwira, William Dafa wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi katika shamba hilo jana katika Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya. 
 Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga (kulia) akizungumza na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Zawadi Mbwambo (kushoto) wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi kwenye Shamba la Miti Kiwira lililopo Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya jana.

Mti huu wa kumbukumbu ulipandwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1965 katika shamba la miti la Serikali  la Kiwira katika Wilaya ya Rugwe Mkoani Mbeya.
 Mti alipanda Mwalimu Nyerere mwaka 1965 katika shamba la miti Kiwira.
  Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Japhet Hasunga akizungumza na watumishi wa Shamba la Miti Kiwira  wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za uhifadhi kwenye Shamba hilo katika Wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya jana.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania, Zawadi Mbwambo akizungumza katika kikao hicho.
Baadhi ya watumishi wa shamba la miti Kiwira.

Applying Nuclear Medicine in Tanzania to Tackle Serious Diseases


According to estimates of Dar es Salaam’s Ocean Road Cancer Institute (ORCI), Tanzania registers about 50,000 new cancer patients every year. However, ORCI, which is the largest cancer referral institution in the country, is only able to attend to 5,000 or 10% of the patients.

In Tanzania, there are few cancer treatment centers to serve the entire population of 55 million people. Unfortunately, not many can afford to cover long distances from all over the country to receive treatment, which can take weeks or months. And it’s not always easy to get cancer patients to keep coming back following initial on-the-scene diagnosis of oncology. Many don’t have the money to get to the hospital or stay for treatment.

With few medical facilities patients need to wait long time to clear out their diagnosis and receive timely treatment.For many of the patients who manage to receive treatment, their cancers have already metastasized to the point that administering palliative care becomes the only remaining option.

Such a tragic state of affairs can be considerably leveled down by increasing services of nuclear medicine and development of special centers of isotope production for local hospitals. Isotopes, nuclear particles, are used in scanning and treatment as they are able to detect and cure tumors at early stage. Globally more than 40 million procedures with nuclear isotopes are performed annually. Nuclear medicine proved to be very efficient in treating oncology and other serious diseases.

Today, using nuclear technologies, Tanzanian doctors can deliver more precise radiation treatment for cancer patients. Specialist at ORCI are now able to employ 3D scanning of tumors, which according to Mark Mseti, oncologist at the institute, is a very important technique to treat successfully a tumor.In modern nuclear medicine the radiation is used only to focus on affected area avoiding any harm to healthy tissue.

Tanzania is set to develop a cancer registry as part of a new health policy to manage the non-communicable disease.Tanzanian own experience in the nuclear medicine will help to prevent the majority of cancer cases, as early scanning and tumor detection can save thousands of lives.

In future Tanzania can follow the example of Zambia, which decided to build its own center of nuclear science and technologies to give an impetus to its own nuclear medicine, because the center will provide a ground to conduct comprehensive research in the sphere.
As mentioned Viktor Polikarpov, Rosatom Vice-President for Sub-Saharan Africa, Nuclear research center will make it possible for Zambia to become one of the industry leaders in Central and Eastern Africa. Research reactors have potential to adjust nuclear technologies for social development. For instance production of medical isotopes to treat cancer and other diseases could not be possible without research reactors.

The broad range of applications of nuclear technologies in medicine is impressive. For instance, nuclear technologies in medicine can be used to examine diverse conditions such as; blood flow to brain, functioning of liver, lungs, heart or kidneys, to determine primary oncological disease and assess presence of metastases, and etc. Diagnostic procedures using radioisotopes have become common practice around the world.

STANDARD CHARTERED BANK MWENYEJI WA ‘ONE BELT- ONE ROAD’ (OBOR) AFRICA-CHINA ROADSHOW

   Mgeni Rasmi Waziri wa viwanda, biashara na uwekezaji, Mh. Charles Mwijage akihutubia waalikwa mbalimbali kuhusu fursa zinazopatikana katika uwekezaji. (OBOR Initiative) katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na Stanchart bank jana,
    Sanjay Rughani akizungumza na wageni waalikwa katika hafla fupi ya chakula cha jioni ambayo Standard Chartered Bank iliwaandalia wateja wake ambao ni wenyeji kutoka China.
   Bw. Sun Chengfeng, Mkuu wa kitengo cha uchumi na biashara ambaye ni mwakilishi wa China nchini Tanzania akizungumza na waalikwa katika hafla ya chakula cha jioni iliyofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es salaam 
   Mgeni rasmi Mh. Charles Mwijage Waziri wa viwanda,biashara na uwekezaji akibadilishana mawazo na Bw, Chengfeng , Mkuu wa kitengo cha uchumi na biashara ambaye ni mwakilishi wa China nchini Tanzania katika hafla ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na standard charterd bank
  Wawakilishi kutoka standard chartered bank china, pamoja na afisa mtendaji mkuu wa standard chartered bank Tanzania wakimsikiliza kwa makini Mh. Waziri Mwijage.
     Wakifuatilia kwa makini hotuba ya mgeni rasmi,Bw Sanjay Rughani, Bw.Sun Chengfeng na wawakilishi mbalimbali katika kitengo cha uchumi na biashara wanaoiwakilisha China nchini Tanzania

  Waalikwa mbalimbali wakimsikiliza bi. Maggie Li alipokuwa akizungumza katika hafla ya chakula cha jioni ambayo standard chartered iliwaandalia wateja wake wenyeji kutoka nchini China
 Afisa mtendaji mkuu wa benki ya Standard Chartered Tanzania Bw. Sanjay Rughani akizungumza na waandishi wa habari kuhusu OBOR initiative katika mkutano uliofanyika katika hoteli ya Hyatt Regency
  Afisa mtendaji mkuu wa Standard Chartered Bank Tanzania Bw. Sanjay Rughani (kushoto), Bi. Maggie Li Mkuu wa kitengo cha biashara na mauzo katika benki ya Standard chartered China(katikati), pamoja na Bw. Cleophas Ruhumbika ambae ni mwakilishi wa katibu mkuu wa viwanda na uwekezaji (kulia). Wakizungumza na wanahabari katika mkutano uliofanyika jana.


  Vijana kutoka kundi la Tanzania House of Talent (THT) wakitoa burudani kwa wageni na waalikwa wa standard chartered bank katika hafla iliyoandaliwa katika hoteli ya Hyatt Regency.
  Burudani kutoka kundi la THT ikiendelea

Rais Angola awafukuza mkuu wa polisi, usalama jeshini


Lourenço amemfuta kazi Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi Ambrósio de Lemos na nafasi yake imechukuliwa na Alfredo Mingas. Pia alimwondoa António José Maria katika nafasi ya mkuu wa usalama wa taifa jeshi na nafasi yake imechukuliwa na Apolinário José Pereira.
Makamanda walioondolewa waliteuliwa na mtangulizi wake José Eduardo dos Santos na walikuwa wakionekana kuwa ni watiifu kwa kiongozi huyo.
Lourenco aliyechukua nafasi ya kiongozi wa muda mrefu dos Santos, amekuwa akichukua hatua ambazo wadadisi wa siasa wanasema anadhihirisha mamlaka makubwa aliyonayo katika koloni hilo la zamani la Ureno.
Hivi karibuni alifunga chombo cha habari kilichoanzishwa na dos Santos. Grecima kwa kiasi kikubwa kilitajwa kuwa taasisi ya propaganda iliyoanzishwa na dos Santos. Shughuli zake zilirejeshwa kwenye kitengo cha mawasiliano ya ikulu.
Hatua kubwa zaidi ilikuwa ya kumwondoa mkuu wa shirika la taifa la mafuta la Sonangol, Isabel dos Santos, binti wa dos Santos na mwanamke tajiri zaidi barani Afrika.

Ziara ya JPM yapunguza machungu Kagera


Ziara ya karibuni ya Rais John Magufuli mkoani Kagera, imemalizika kwa kuziba sehemu ya maumivu yaliyoachwa kwa wananchi wakati wa ziara yake ya mwanzoni mwa mwaka huu.
Katika ziara iliyotangulia Rais Magufuli alitumia nafasi hiyo kuwaeleza wananchi ukweli mchungu ambao walitakiwa kuupokea bila ganzi.
Kilikuwa kipindi ambacho wananchi walikuwa wanalia na msaada baada ya kupata maafa ya tetemeko la ardhi la Septemba 2016, lakini yeye akawaeleza ukweli kuwa Serikali haiwezi kumjengea nyumba kila mmoja na kwamba sehemu ya michango iliyotolewa na wasamaria ingesaidia ujenzi wa miundombinu ya jumla kama barabara, madaraja, hospitali na shule.
Ni ukweli uliotakiwa kupokewa kama ulivyo kwamba badala yake wananchi wafanye kazi na wasibweteke kusubiri chakula cha msaada kwa kuwa tetemeko halikusomba migomba.
Lakini katika ziara ya hivi karibuni, Rais Magufuli alikuwa katika sura tofauti na kutoa maamuzi ambayo yalisahaulisha waathirika hata makali ya janga la tetemeko.
Hata hivyo, pamoja na hali hiyo, Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini, Wilfred Lwakatare alimweleza Rais Magufuli kuwa wapo waathirika wa tetemeko ambao bado wanalala nje kwa kukosa uwezo wa kurejesha makazi.
Kauli ya mbunge huyo ilitegemewa kuungwa mkono kwa makofi na vifijo na wananchi waliohudhuria uzinduzi wa kiwanja cha ndege cha Bukoba uliofanywa na Rais Magufuli, mbunge huyo alijikuta peke yake badala yake akiombwa amalize salamu zake mapema na kuwapa nafasi wengine.
Hata Rais Magufuli alipozungumza na wananchi hakujishughulisha kujibu ombi la Lwakatare.
Pengine hata Rais alijua kuwa shauku ya wananchi haikuwa kusikiliza tena habari za misaada ya tetemeko la ardhi, bali kujua ziara yake mpya itakuja na jipya gani.
Rais alitoa ufumbuzi wa kero zinazowakabili wananchi akiwa palepale jukwaani, hatua iliyoshangiliwa na kuonekana kama faraja inayofuta machungu yaliyopita.
Mambo mapya
Ziara hiyo ilitawaliwa na mambo mapya yaliyowahusu wananchi wa Kagera moja kwa moja na mengine kubeba mijadala ya kitaifa.
Aliruhusu wananchi wanaosubiri malipo ya kupisha ujenzi wa kiwanja cha ndege cha Omukajunguti waendelee na kilimo kwakuwa suala hilo halitakuwepo tena.
Alisema badala yake Sh9 bilioni ambazo zingetumika kulipa fidia kwa wananchi hao wa Missenyi zitumike kuboresha zaidi kiwanja cha Bukoba.
Wakati wa ziara hiyo baadhi ya watendaji wa Serikali walipoteza nafasi zao baada ya kushindwa kujibu maswali mbele ya wananchi, hali iliyotafsiriwa kuwa ni kushindwa kumudu majukumu waliyopewa.
Ulikuwa ni wakati mwingine mgumu kwa watumishi wa halmashauri za Bukoba, Missenyi na Karagwe kwa kuwa hawakuwa na uhakika wa usafi kwenye maeneo yao endapo Rais angehitaji maelezo.
Kama si mvua kunyesha wakati Rais akiwahutubia wananchi wa Karagwe katika eneo la Kayanga, pengine kuna jambo kubwa lingetokea kama ilivyokuwa katika maeneo mengine alikopita.
Wakurugenzi kutimuliwa
Kabla ya kutenguliwa kwa kushindwa kutaja fungu la fedha la mfuko wa barabara, rungu lilimshukia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Bukoba, Mwantumu Dau pale Rais Magufuli alipofika eneo la Kemondo na kusikiliza kero za wananchi.
Rais Magufuli alitoa maelekezo ya wananchi kutoendelea kutozwa ushuru katika soko, kwa kuwa Serikali ilipunguza mzigo huo kwa wananchi.
Alimuonya mkurugenzi kuwa suala la kukusanya ushuru lisijitokeze na halmashauri itafute vyanzo vingine vya mapato ambavyo havimuumizi mwananchi wa daraja la chini.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Bukoba, Erasto Mfugale kama ilivyokuwa kwa jirani yake, naye alijikuta matatani baada ya uteuzi wake kutenguliwa kwa kushindwa kutoa maelezo ya zilipo fedha za mfuko wa barabara.
Mkurugenzi huyu alirithi nafasi ya Kelvin Makonda ambaye mwaka mmoja uliopita uteuzi wake ulitenguliwa baada ya kutuhumiwa kufungua akaunti isiyo rasmi kwa ajili ya kukusanya fedha za waathirika wa tetemeko la ardhi.
Siku chache kabla ya uteuzi wake kutenguliwa, habari za ndani zinasema walikuwa na vikao na wakuu wa idara wakijipanga kwa ajili ya ziara ya Rais na kufanya mazoezi kwa njia ya kuulizana maswali.
Wakati mkurugenzi huyo aliposhindwa kutoa ufafanuzi wa fedha za mfuko wa barabara, mmoja wa wakuu wa idara alinyanyuka kwenda kuokoa jahazi baada ya Rais Magufuli kusema anayefahamu ajitokeze.
Hata hivyo, hakutimiza azma hiyo na badala yake ufafanuzi wa kuridhisha ulitolewa na Meya wa Manispaa hiyo, Chief Karumuna.
Mabango yayeyuka
Kumekuwa na utamaduni mpya wa wananchi kuonyesha mabango yenye ujumbe wa kero zao katika mikutano ya Rais John Magufuli, ambao umewavutia wengi.
Hata hivyo, mabango hayo hayakuonekana sana kwenye mikutano Kagera ikilinganishwa na mikoa mingine aliyopita hivi karibuni.
Hii ilitokana na baadhi ya mabango kuzuiwa wakati wa kuingia kwenye eneo la ufunguzi wa kiwanja cha ndege cha Bukoba, ingawa wachache walifanikiwa kupenyeza mabango yao kwa siri.
Hata hivyo, kulikuwapo na woga wa kunyanyua mabango hayo kutokana na baadhi yao kudhibitiwa na kuondolewa eneo la mkutano.
Hata mabango machache yaliyonyanyuliwa baada ya Rais kuwasili hayakuleta msisimko, ingawa mwanamke mmoja alipewa nafasi ya kuwasilisha kero zake.
Baadhi ya wananchi waliokosa nafasi ya kuwasilisha kero zao wakati Rais Magufuli akiwa Bukoba, walifunga safari na kumfuata kwenye mkutano wa Karagwe ambapo hata hivyo mvua iliyonyesha ilipunguza wingi wa matukio.
Miongoni mwa mabango hayo yalieleza kero ya Manispaa ya Bukoba kufyeka mazao ya wananchi kando ya mto Kanoni bila kuwapa muda wa kusubiri yakomae na kuvunwa.
Katika mkutano huo, Rais Magufuli aliwaeleza wananchi kama wapo wenye mabango yanayotaja kuondolewa kwenye vyanzo vya maji wajiondokee mapema kwa kuwa iliyofanyika ni kazi nzuri ya kulinda mazingira.
Hata hivyo, kauli hiyo ya Rais ilizua mjadala kutokana na mkanganyiko wake, kwani akiwa Kyaka njiani kwenda Karagwe aliruhusu wananchi kufanya shughuli za kilimo cha mazao ya muda kando ya mito.
Katika eneo hilo, alielezwa jinsi mahindi yanavyofyekwa na maofisa wa mazingira wa Wilaya ya Missenyi wakati yeye anasisitiza wananchi wafanye kazi na hapo wananchi wakataka ufafanuzi.
Rais Magufuli alieleza kuguswa na hali hiyo na kuamua kumchangia Sh300,000 mwananchi aliyeibua kero hiyo na kuagiza waendelee na shughuli za kilimo bila kuondolewa.
Akiwa katika mkutano wa kuzindua barabara ya Kyaka-Bugene Rais Magufuli alisisitiza agizo lake alilolitoa akiwa Kyaka kuwa wananchi waachwe kuendelea na shughuli za kilimo kando ya mto maadamu shughuli hizo hazifanyiki kwenye vyanzo.
Vibali vya sukari
Katika ziara hiyo ilizuka hoja ya wananchi wa Missenyi kununua sukari kwa bei kubwa ikilinganishwa na walaji walio mbali na eneo hilo lenye Kiwanda cha sukari cha Kagera.
Akiwa eneo la Bunazi wananchi walilalamika kununua sukari kwa Sh2,800 tofauti na maeneo mengine inaponunuliwa kwa Sh2,500.
Walisema sukari ya kiwanda hicho kabla ya kuwafikia walaji wa Missenyi lazima kwanza isafirishwe hadi Mjini Bukoba (umbali wa kilometa 61) na baadaye kurudishwa ikiwa imepanda bei ili kufidia gharama za usafiri.
Kutokana na madai hayo, Rais Magufuli aliacha amemsimika wakala wa bidhaa hiyo kutoka kiwandani ili wananchi wa Missenyi wapate sukari kwa bei nafuu. Pia, Rais Magufuli aliagiza wawekezaji wa viwanda vya sukari wakutane na kujadili jinsi ya kuongeza uzalishaji wa bidhaa hiyo ili kuziba pengo la upungufu wa tani 130,000 unaojitokeza kila mwaka.
Alisema kama watakutana na jambo hilo kuwezekana, atapiga marufuku moja kwa moja uagizaji wa sukari kutoka nje ya nchi.
Magufuli na Museveni
Ziara ilihitimishwa kwa kukutana na Rais wa Uganda, Yoweri Museveni katika mpaka wa Mutukula ambapo walizindua kituo cha pamoja cha forodha ili shughuli zote za forodha zifanyike eneo moja.
Rais Magufuli alisema hatua hiyo pamoja na kuokoa muda kwa wasafirishaji wa bidhaa mbalimbali mpakani pia itaongeza makusanyo ya kodi kwa nchi zote mbili na kukuza uchumi.
Rais Museveni alisema hatua hiyo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi wa nchi hizo na kuwataka wafanyabiashara kutumia fursa zinazopatikana katika nchi hizo kwa kuwa wanapunguziwa vikwazo vilivyokuwepo.  

Kwa hili, nakupa tano Spika Ndugai


Nimefarijika sana nilipomsikia Spika wa Bunge, Job Ndugai akiwataka wabunge wa CCM watimize wajibu wao wa kikatiba wa kuwasemea wananchi badala ya kupongeza hata pasipostahili kupongeza.
Ibara ya 63(2) ya Katiba ya Tanzania iko wazi kuwa Bunge ndicho chombo kikuu ambacho kitakuwa na madaraka kwa niaba ya wananchi, kuisimamia na kuishauri Serikali na vyombo vyake.
Kauli hii ya Spika, naamini imewapa faraja Watanzania walio wengi, ambao wanaona kama uchangiaji wa baadhi ya wabunge hauna tija kwa sababu unatawaliwa na dhihaka na vijembe.
Ni dhahiri Spika aliona mwelekeo usioridhisha wa baadhi ya wabunge, hawa wa chama hicho tawala ambayo haikulenga kuboresha mpango huo bali kupongeza na kujikita kwenye majimbo yao.
Lakini, bahati mbaya sana wako wabunge wanaoomba kuchangia na kutumia karibu muda wote kujibu hoja za wabunge wa upinzani, ilihali wapo mawaziri ndani ya Bunge ambao wana wajibu huo.
Labda kabla sijaingia kwa undani katika mada hii, ni vyema nikawakumbusha kile ambacho alikisema Spika, ambacho naamini kinapaswa kiende hadi kwenye Bunge la Bajeti na wakati wa kujadili miswada mbalimbali.
Ndio maana Spika akasema, “Katiba iliweka utaratibu kwamba mipango ya nchi itapita hapa (bungeni) kwanza nyinyi muijadili. Halikuwekwa hivyo kwa bahati mbaya. Liliwekwa hivyo ili nyinyi mseme kwa niaba ya wananchi.
Akaongeza, “katika mambo ya msingi kama haya fungukeni. Msijifunge funge hapo ooh mimi CCM. CCM haitaki mipango mibovu. Ni wakati wenu wa kusema tumsaidie Waziri na tuisaidie Serikali ili tusonge mbele.”
Baada ya hali hiyo, Spika akasema “Na unapoomba nafasi ya kusema hapa uwe umejiandaa. Sio ile tu naunga mkono nafanya hivi unakaa chini”.
Kwa mtizamo wangu na kwa wosia huu wa Spika Ndugai, nafikiri sasa huu ni wakati muafaka kwa wabunge bila kujali wa CCM au wa upinzani, kuisimamia Serikali pasipo hofu ya kuhojiwa katika vikao vya chama.
Wapo wabunge ambao wameusoma ujumbe wa Spika na kuuelewa na kweli “wamefunguka” kama ambavyo Spika alitarajia wote wafanye hivyo.
Lakini mimi ningependa kwa moyo huo huo, wabunge hao waisimamie Serikali ili iendeshe nchi kwa utawala bora unaoheshimu utawala wa sheria.
Sote tunafahamu tuna mihimili mitatu ambayo ni Serikali, Bunge na Mahakama ambayo inaoongozwa kwa kanuni kuu moja ambayo ni kutoingiliana katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku.
Bunge kazi yake ni kutunga sheria na kupitisha bajeti, Serikali ni kusimamia utekelezaji wa sheria na shughuli za kila siku za Serikali na mahakama ni kutafsiri sheria na kutoa haki.
Ukiona mhimili mmoja unajiona ni bora na kudharau mwingine kama ilivyotokea katika suala la bomoabomoa, ujue uko mgogoro wa kukosekana kwa utawala bora unaoheshimu utawala wa sheria.
Sote ni mashahidi kwamba zipo nyumba zimebomolewa kibabe licha ya kuwapo amri za mahakama, haya ni mambo ambayo Bunge linapaswa kuisimamia Serikali ili iheshimu utawala wa sheria.
Ni lazima tujitafakari kama taifa ni mbegu ya aina gani tunaipandikiza katika taifa linalojipambanua kuheshimu misingi ya utawala bora inayoheshimu utawala wa sheria na kuheshimu Katiba.
Ibara ya 3(1) ya Katiba yetu ya mwaka 1977 imeeleza wazi kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi ya kidemokrasia na kijamaa, yenye kufuata msukumo wa vyama vingi vya siasa ulioanza 1992.
Takwa hilo la kikatiba likaongezewa nguvu na Kanuni za Maadili vya vyama vya siasa za mwaka 2007, kama zilivyotangazwa katika gazeti la Serikali namba 2015 ya Oktoba 12 mwaka 2007.
Kifungu cha 4(1) (c), kimetaja kazi nyingine ni kujadili na kushindanisha sera zake na zile za chama kingine kikiwamo chama tawala kwa lengo la kutaka kukubalika kwa wananchi.
Leo vyama vya siasa vimezuiwa kufanya mikutano ya hadhara kwa tamko la Rais ambalo kwa ujumla wake linalalamikiwa kukiuka katiba, lakini wabunge wamekaa kimya. Hili la Ndugai liende na kuhoji hili.