Friday, July 14

MASAUNI AWATAKA MAAFISA UHAMIAJI, POLISI KUONGEZA KASI KUCHUNGUZA NA KUWAKAMATA WAHAMIAJI HARAMU TANGA




Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kulia) akizungumza na Viongozi wa Taasisi zilizopo chini ya Wizara yake, mkoani Tanga wakati kiongozi huyo alipofanya ziara yake kikazi mkoani humo. Katika mazungumzo yao, Masauni aliwahasa viongozi hao kuhakikisha wanafanya kazi kwa kujituma zaidi na kuwahakikishia kero zote walizompa atahakikisha anazifanyia kazi. Kushoto ni Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Benedict Wakulyamba.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (watatu kushoto) akimsikiliza  Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela (katikati) alipokua anatoa taarifa ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa huo, kabla ya kiongozi huyo kuanza ziara yake mkoani humo. Katika mazungumzo yao, Masauni aliwataka Maafisa Uhamiaji pamoja na Polisi kuongeza kasi ya kutafuta mizizi ya wahamiaji haramu mkoani humo. Kushoto ni Kamanda wa Polisi Mkoa huo, Benedict Wakuliamba. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akitoka kulikagua jengo la Ofisi ya Mkuu wa Polisi Wilaya ya Tanga ambalo linahitaji matengenezo ili kulirudisha katika hali yake ya kawaida. Hata hivyo, Masauni alimuagiza Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Benedict Wakulyamba (kulia) kuhakikisha jengo hilo linatengenezwa haraka iwezekavyo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhandisi Hamad Masauni (kushoto) akimfafanulia jambo Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela (katikati) na Katibu Tawala wa Mkoa huo, Zena Saidi, kabla ya kiongozi huyo kuanza ziara yake mkoani humo. Katika mazungumzo yao ambayo yalifanyika ofisini kwa Mkuu wa Mkoa huyo, Masauni aliwataka maafisa uhamiaji pamoja na Polisi kuongeza kasi ya kutafuta mizizi ya wahamiaji haramu mkoani humo. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Ajira 11,000 zazalishwa katika Kipindi cha maonesho ya Kimataifa ya 41


 Waziri wa  Biashara, Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (MB) Mhe. Balozi Amina Salum Ali akifurahia zawadi ya begi lililotengenezwa kwa bidhaa za ngozi ya Tanzania.
 Waziri wa  Biashara, Viwanda na Masoko wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (MB) Mhe. Balozi Amina Salum Ali akifunga maonesho ya Kimataifa ya 41 ya Biashara ya Dar es Salaam leo Katika Viwanja vya JK Nyerere ,Barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda Biashara na Uwekezaji (Biashara na uwekezaji) Prof. Adolf Mkenda akiongea wakati wa hafla yakufunga maonesho ya Kimataifa ya 41 ya Biashara ya Dar es Salaam Leo Katika Viwanja vya JK Nyerere ,Barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa  Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE) Bw. Edwin Rutageruka akitoa maelezo mafupi kuhusu maonesho ya Kimataifa ya 41 ya Biashara ya Dar es Salaam.
 .Kikundi cha kwaya ya TOT kikitumbuiza wakati wa hafla ya kufunga maonesho ya Kimataifa ya 41 ya Biashara ya Dar es Salaam Leo Katika Viwanja vya JK Nyerere ,Barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam.

 Mtaalamu wa ushonaji mavazi Bw. Abdalah Nyangalio ambaye ni mlemavu wa macho akifurahia hafla ya kufunga maonesho ya Kimataifa ya 41 ya Biashara ya Dar es Salaam Leo Katika Viwanja vya JK Nyerere ,Barabara ya Kilwa Jijini Dar es Salaam
Baadhi ya washiriki wa hafla ya ufungaji wa maonesho ya Kimataifa ya 41 ya Biashara ya Dar es Salaam  wakimsikiliza mgeni rasmi (hayupo pichani).

WAZIRI MWIGULU AFANYA MAZUNGUMZO NA NAIBU BALOZI WA MAREKANI NCHINI TANZANIA




Naibu Balozi wa Marekani nchini, Dk. Inmi Patterson, akizungumza na Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba, alipomtembelea Waziri huyo kujadili Masuala ya Ulinzi na Usalama, jijini Dar es Salaam leo.Kulia ni Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Siasa na Uchumi wa Ubalozi huo,Marilyn Gayton na kushoto ni Katibu wa Waziri,Nelson Kaminyoge. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 
Waziri wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi,Mwigulu Nchemba, akiwa katika picha ya pamoja na Naibu Balozi wa Marekani nchini, Dk. Inmi Patterson(kulia), baada ya kumaliza mazungumzo yaliyohusu Masuala ya Ulinzi na Usalama.Kikao hicho kimefanyika leo jijini Dar es Salaam.Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 

SERIKALI KUPITIA UPYA MIKATABA YA UWANJA WA NDEGE PAMOJA NA KUFUMUA UONGOZI ULIOPO.


Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii

SERIKALI imesema kuwa itapitia mikataba yote katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere pamoja na kufanya mabadiliko ya uongozi huo kutokana na kufanya kazi kwa mazoea.

Hayo ameyasema leo Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa wakati alipotembelea uwanja wa ndege huo baada ya kuwepo kwa taarifa ya wasafiri wakichukua muda mrefu kutoka uwanjani hapo.

Mbarawa amesema kuwa watu wanapoingia kutoka nje ya nchi wanaanza kusoma Tanzania ilivyo ikiwemo na uwanja wan degu kukaa kwa muda mrefu kutokana na mifumo ya watu kushindwa kujipanga.

Amesema kuwa mikataba katika uwanja huo wameingia wale watu waliofanya mikataba hawakuangalia masilahi ya nchi ndio maana mapato yanakuwa kidogo tofauti na ilivyo katika uhalisia.

Aidha amesema kuwa watakaa kikao kimoja kati ya watoa huduma katika uwanja wa mwalimu Julius Nyerere wakiwemo Idara ya Uhamiaji pamoja na benki ambako ndio inafanya watu wakae muda mrefu.

Nae Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Salim Msangi amesema kuwa wanazifanyia kazi changamoto ambazo Wazari amezianisha licha ya kuwa na miundombinu finyu.

Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuangalia utoaji huduma katika uwanja wa Mwalimu Julius Nyerere.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Salim Msangi akizungumza na waandishi wa habari juu Uboreshaji wa Huduma katika Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere leo.
Waziri Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akipata maelezo KaimuMkurugenzi wa Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Josepp Nyahende alipofanya ziara katika uwanja huo leo .
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akipata maelezo Afisa Maidizi wa Ushuru uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere, Hezron Gibe jinsi wanafanya kazi katika uwanja huo.
Waziri wa Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mnyaa Mbarawa akipewa maelezo na watoa huduma Ushuru uwanja wa Ndege wa Mwalimu Julius Nyerere leo .

MAKAMU WA RAIS AKUTANA NA RAIS MSTAAFU WA IRELAND NA BI. GRACA MACHEL


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Rais wa Mstaafu wa Ireland, Mary Robinson ambaye pia ni Mjumbe wa Taasisi inayoshughulika na Amani,Haki za Binadamu na Huduma za Afya, Rais huyo Mstaafu aliongozana na Mjumbe mwingine wa Taasisi hiyo Bi. Graca Machel . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Rais wa Mstaafu wa Ireland, Mary Robinson ambaye pia ni Mjumbe wa Taasisi inayoshughulika na Amani,Haki za Binadamu na Huduma za Afya, Rais huyo Mstaafu aliongozana na Mjumbe mwingine wa Taasisi hiyo Bi. Graca Machel . (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na  Rais wa Mstaafu wa Ireland, Mary Robinson pamoja na Bi. Graca Machel ambao ni Wajumbe wa Taasisi inayoshughulika na Amani,Haki za Binadamu na Huduma za Afya, wengine pichani ni Ujumbe ulioongozana na Viongozi hao pamoja na Wasaidizi wa Makamu wa Rais. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akimsikiliza Mjumbe wa Taasisi inayoshughulika na Amani,Haki za Binadamu na Huduma za Afya, Bi. Graca Machel ambaye aliongozana na  Rais wa Mstaafu wa Ireland, Mary Robinson kumtembelea Makamu wa Rais ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Rais wa Mstaafu wa Ireland, Mary Robinson (kulia) ambaye pia ni Mjumbe wa Taasisi inayoshughulika na Amani,Haki za Binadamu na Huduma za Afya, kushoto ni Mjumbe wa Taasisi hiyo Bi. Graca Machel mara baada ya kumaliza mazungumzo kwenye ofisi za Makamu wa Rais, Ikulu jijini Dar es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).

ZANTEL YASHIRIKI KATIKA MKUTANO WA MOBILE 360 AFRICA JIJINI DAR ES SALAAM



Meneja wa Kitengo cha chapa na Mawasiliano Zantel, Rukia Mtingwa (kushoto) akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wakuu wa vitengo vya mawasiliano kutoka kampuni mbalimbali Afrika Mashariki wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kukuza matumizi ya teknolojia ya simu ili kufikia maendeleo endelevu ulioandaliwa GSMA Mobile 360 Africa kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jana jijini Dar es salaam. Katikati ni Meneja wa Mawasiliano wa Tigo Tanzania Woinde Sishael na Kulia ni Meneja Ushirikiano wa Masoko wa Africa-GSMA, Adreni Mhuhura.
Meneja wa Kitengo cha chapa na Mawasiliano Zantel, Rukia Mtingwa (kulia) akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wakuu wa vitengo vya mawasiliano kutoka kampuni mbalimbali Afrika Mashariki wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kukuza matumizi ya teknolojia ya simu ili kufikia maendeleo endelevu ulioandaliwa GSMA Mobile 360 Africa kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jana jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mwakilishi kutoka Idara ya Mambo ya nje na biashara Australia Dan Woods. 
Meneja wa Kitengo cha chapa na Mawasiliano Zantel, Rukia Mtingwa (katikati) akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wakuu wa vitengo vya mawasiliano kutoka kampuni mbalimbali Afrika Mashariki wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kukuza matumizi ya teknolojia ya simu ili kufikia maendeleo endelevu ulioandaliwa GSMA Mobile 360 Africa kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jana jijini Dar es salaam. Kushoto ni Mwakilishi kutoka Idara ya Mambo ya nje na biashara Australia Dan Woods na Kulia ni Meneja Mawasiliano wa Safaricom Eunice Mumma.
Mwakilishi kutoka Idara ya Mambo ya nje na biashara Australia Dan Woods akizungumza katika mkutano uliowakutanisha wakuu wa vitengo vya mawasiliano kutoka kampuni mbalimbali Afrika Mashariki wakati wa ufunguzi wa mkutano wa kukuza matumizi ya teknolojia ya simu ili kufikia maendeleo endelevu ulioandaliwa GSMA Mobile 360 Africa kwenye ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere jana jijini Dar es salaam Pamoja nae ni Meneja wa Kitengo cha chapa na Mawasiliano Zantel, Rukia Mtingwa. 

WAZIRI MKUU AUPONGEZA UONGOZI WA NHC KWA UTENDAJI



Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,akikata utepe wakati alipofungua Zahanati katika kijiji cha Mnolela, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne (kutoka kushoto) ni Mbunge wa Jimbo la Mtama Nape Mnauye, Diwani Kata ya Mnolela Omar Liveta, Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba (NHC) kutoka kulia ni Meneja NHC Lindi Gibson Mwaigomole, Meneja NHC Mtwara Nehemia Msigwa, Mkuu wa Mkoa Lindi Godrey Zambi Julai 13, 2017. 


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,akisalimiana na Mkurugenzi wa Shirika la Nyumba (NHC),wakati alipofungua Zahanati katika kijiji cha Mnolela, akiwa  njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne (katikati) ni Mbunge wa Jimbo la Mtama Nape Mnauye Julai 13, 2017. 


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,akikagua wakati kifaa katika Zahanati ya Mnolela, baada ya kuifungua, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne Julai 13, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,akizungumza na wananchi wa Mnolela mara baada ya kuifungua Zahanati hiyo iliyopo katika Kijiji cha Mnolela, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne Julai 13, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 


Mbunge wa Jimbo la Ndanda Cecil Mwambi akiwa na Mbunge wa Masasi Rashid Chuwachuwa (Kushoto) na Diwani wa Kata ya Ndanda Costancia Bernad, wakimsikiliza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakati alipo simama katika kijiji cha Nanganga, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne Julai 13, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nanganga, wakati alipo simama, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne Julai 13, 2017.
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amkabidhi Mbunge wa Jimbo la Ndanda Cecil Mwambi mipira, wakati alipo simama katika kijiji cha Nanganga, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne Julai 13, 2017.

Wananchi wa kijiji cha Nanganga wakimsikiliza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, wakati alipo simama katika kijiji hicho, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne Julai 13, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Wananchi wa kijiji cha Mtama wakishangilia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,  wakati alipo simama kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Polisi kijijini hapo, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne Julai 13, 2017.

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,akiteta jambo na Mbunge wa jimbo la Mtama,Nape Mnauye alipo simama kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Polisi kijijini hapo, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne Julai 13, 2017. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa,akizungumza na wananchi wa kijiji cha Mtama, wakati alipo simama kuweka jiwe la msingi katika kituo cha Polisi kijijini hapo, akiwa njiani kuelekea Lindi, Waziri Mkuu yupo Mkoani Lindi kwa ziara ya kikazi ya siku nne Julai 13, 2017.

…………………………………………………………………

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ameupongeza uongozi wa Shirika la Nyumba (NHC) kwa kukamilisha ujenzi wa zahanati ya kijiji cha Mnolela mkoani Lindi kwa muda mfupi.

Amesema ujenzi wa zahanati hiyo ya kisasa mwezi Machi, 2017 na sasa tayari kimekamilika, jambo ambalo litarahisisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi wa eneo hilo na wa jirani.

Waziri Mkuu alitoa pongezi hizo jana jioni (Alhamisi, Julai 13, 2017) alipozungumza na wananchi wa kijiji cha Mnolela baada ya kuzindua zahanati hiyo iliyosimamiwa na NHC.

Alisema ujenzi wa zahanati hiyo ni muendelezo wa mkakati wa Serikali ya awamu ya tano wa kuboresha huduma za afya kwa kusogeza huduma karibu kwa wananchi wake.

“Rais wetu Dkt. John Magufuli amedhamiria kuwaondolea wananchi changamoto za mbalimbali zikiwemo za huduma za afya, hivyo tuendelee kumuunga mkono.”

Kwa upande wake Mkurugenzi wa NHC, Bw. Nehemia Mchechu alisema mradi wa ujenzi wa zahanati hiyo ulisimamiwa na NHC na umegharimu sh. milioni 65.5.

“Shilingi milioni 15 zilitolewa na Rais. Dkt. Magufuli, sh. milioni 10 zilitolewa na Mheshimiwa Mbunge wa jimbo la Mtama, Nape Nnauye, NHC ilitoa sh. milioni 10 na kiasi kilichosalia ni mchango wa halmashauri.”

Awali Mbunge wa jimbo la Mtama, Mheshimiwa Nape alimshukuru Rais Dkt. Magufuli kwa mchango mkubwa alioutoa katika mradi wa ujenzi wa zahanati hiyo.

Mheshimiwa Nape alisema zahanati hiyo ni mkombozi kwa wakati wa kijiji cha Mnolela na wananchi wengine wanaoishi kwenye maeneo yaliyo jirani na kijiji hicho.

Rooney, Everton Wafurahia Ukarimu wa Watanzania


Timu ya Soka ya Everton inayoshiriki ligi kuu nchini Uiungereza imemaliza ziara yake ya siku mbili nchini Tanzania na kuelezwa kufurahishwa na namna Watanzania walivyoipokea timu hiyo.

Timu ya Everton iliwasili Tanzania siku ya Jumatano wiki hii ambapo jana ilicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Gor Mahia kutoka Kenya.

“Imekuwa ni uzoefu mpya kwangu kuja hapa (Tanzania) na nina tumaini sasa Makamu wa Rais atakuwa akiishabikia Everton”, alieleza Wayne Rooney kupitia tovuti ya timu hiyo.

Pia katika akaunti yake ya mtandao wa tweeter, Rooney aliwashukuru washabikji wa Tanzania kwa kuiunga mkono Everton katika mchezo wao wa kirafiki dhidi ya timu ya Gor Mahia kutoka Kenya.

“Great start to the pre-season. Special thanks to the fans supporting us in Tanzania”, aliandika Rooney akitoa shukrani za pekee kwa washabiki wa Tanzania.

Kwa upande wa Kocha wa timu hiyo, Ronald Koeman alielezea kufarahia ziara ya kuja Tanzania na zaidi ni kutokana na hali ya urafiki iliyooneshwa na washabiki wa soka nchini.

Rooney pia aliungana na wachezaji wengine kama Morgan Schneiderlin, Jonjoe Kenny na Kevin Mirallas wa timu hiyo walipata fursa ya kujifunza tamaduni za kimsai, kujifunza kupika chakula cha asili, kutembelea shule yenye wanafunzi wenye mahutaji maalum na pia kufanya mazoezi na timu ya vijana wenye ulemavu wa ngozi (Albino United).

Timu ya soka ya Everton ilifanya ziara nchni Tanzania ambapo ilicheza mchezo wa kirafiki dhidi ya Gor Mahia ya Kenya katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na viongozi mbali mbali akiwemo Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan ambaye alikuwa Mgeni Rasmi, Marais wastaafu, Ali Hassan Mwinyi na Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na wageni mbalimbali kutoka ndani na nche ya nchi. 







Wayne Rooney (wa tatu kushoto) kushoto akiwa na wachezaji wenzake walipokuwa Jijini Dar es Salaam ambapo timu ya Everton ilicheza na timu ya Gor Mahia katika mchezo wa kirafiki ulichezwa katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam. 

TANAPA YATOA TUZO YA HESHIMA YA UTUNZAJI WA SOKWE KWA DKT. JANE GOODALL


Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii. Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Shirika la Hifadhi za Tanzania TANAPA, limempatia tuzo nne za Heshima, mwanasayansi na mtafiti wa kimataifa Dkt. Jane Goodall. Dkt. Jane amekabidhiwa tuzo mapema leo na Waziri wa Maliasili na Utalii Prof. Jumanne Magembe ambazo ni kinyago cha Sokwe, Kitenge, cheti cha heshima na ngao. 

Tuzo hiyo ya heshima imetolewa maalumu kwa kutambua mchango wake katika masuala ya utafiti na uhifadhi wa Sokwe kwenye hifadhi ya taifa ya Gombe ambao ameufanya kwa zaidi ya miaka 60. Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji tuzo hizo, Waziri wa Magembe amesema, Tanzania ni nchi ya kwanza ya uhifadhi katika bara Africa. 

Katika hifadhi zetu za taifa za wanyama mbali mbali ambazo ziko 16, ziko pia, hifadhi za taifa mbili, Gombe na Mahale ambazo wanyama wanaohifadhiwa humo kwa sehemu kubwa ni Sokwe ambapo hata katika dunia hizo mbili ndio hifadhi nzuri kupita zote. Amesema, Kazi kubwa iliyofanywa na mtafiti huyo imeiwezesha jamii kugundua kuwa, Sokwe, wanajitambua na kushirikiana. Wao kama wanyama, wana hisia zao kama viumbe na kama binadamu. 


Amesema, kabla ya utafiti huo wa Sokwe, na katika ulimwengu wa sayansi binadamu ndio waliokuwa wa wanahisiwa kuwa ndio wenye hisia na kushirikiana kama viumbe wenye akili sana kumbe hata Sokwe kwani wao pia wanatumia nyenzo katika maisha yao. 

Ameongeza kuwa tafiti anazofanya zimekusanya takwimu zenye maana kubwa sana katika uhifadhi wa Sokwe na pia katika uhifadhi wa wanyama pori. "Kwa mchango wake huu alioutoa, kidunia, kimataifa lakini kwa Tanzania kutoa mchango huu, tumeamua kumtunukia tuzo katika uhifadhi wa wanyamapori na zaidi Sokwe" amesema Waziri Maghembe. 

Ameongeza, uharibifu wa mazingira unatokana na ukosefu mkubwa wa elimu, kabla ya Sokwe kufanyiwa utafiti huu uliofanywa, tulikuwa tunajua sisi binadamu ni tofauti na Sokwe,kumbe katika vinasaba vyetu kama binadamu asilimia 99 ni sawa sawa na Sokwe, tofauti ni moja asilimia moja tu, ya ubongo wetu na uwezo wetu ndio mkubwa kuliko wao, mambo mingine yote tuko sawa sawa", amesema Magembe. 

Aidha Waziri amesisitiza kuwa, msimamo wa Serikali katika utafiti huu mgumu uliofanywa na Dkt. Jane ni kuendeleza kazi hizo, kupanua taasisi ya utafiti ya wanyama hao kama binadamu na kuileta iwe na ushirikiano na mashirika ya wanyama pori nchini kama Tanapa, Ngororo na mengineyo na kuhakikisha kazi ya utafiti inaendelea na kutufanya tuzidi kuwa viongozi duniani katika sekta hiyo. 

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Tanapa, Allan Kikazi amesema, Tanapa ina kila sababua ya kumpa tuzo ya Heshima, Dkt, Jane kwani amekuwa akitumia muda wake mwingi sana kufanya utafiti na kuwapatia taarifa za kutosha zinazowawezesha kujua mienendo na tabia za wanyama aina ya Sokwe ambao unaweza kuwapata kwenye hifadhi ya Gombe iloyopo Kigoma na kwenye Milima ya Mahale pekee. 

Amesema taarifa hizo zinaisaidia Tanapa kuweka mikakati sahihi juu ya namna ya kusimamia hifadhi ya Gombe na kuwasimamia Sokwe ambao wako katika hatari ya kutoweka, kwani bila taarifa hizi, kungekuwa na uwezekano wa idadi ya wanyama hao kuwa ndogo kuliko sasa ambao wanakadiriwa kuwa zaidi ya 80.

Pia Dkt. Jane amesaidia kutoa mafunzo na kuwawezesha wafanyakazi wa Tanapa kihakikisha Sokwe wanasimamiwa inavyopaswa. "Idadi ya wanyama walioko ndani ya hifadhi inaonekana inaongezeka lakini pia kama wanyama wanaoonelana kuwa wanaishi kwenye mazingira yao ya asilo wao huwa hawatambui mpaka iliyopo, wamekuwa na tabia ya kutoka na maeneo yaliyopo nje ya hifadhi mengi yameharibiwa na wamekuwa wakiuwawa kwa mambo mbali mbali, lakini tunafanya jitihada kuhakikisha tunaweka mifumo sahihi hata wakiwa nje ya hifadhi', amesema Kikazi. Kwa upande wake Dkt. Jane ameishukuru sana Serikali ya Tanzania na Tanapa kwa kutambua mchango wake.  Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe (kulia), akimkabidhi Tuzo ya Uhifadhi Wanyama aina ya Sokwe, Dkt. Jane Goodall, aliyekuwa akifanya utafiti wa Wanyama hao kwa miaka 60 katika hifadhi mbalimbali na baadaye kujikita katika Hifadhi ya Gombe. Picha zote na Kajunason Blog/Cathbert Kajuna.  Dkt. Jane Goodall akionyesha cheti chake cha kutambua mchango wake katika Uhifadhi Wanyama aina ya Sokwe.  Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe, akimkabidhi Tuzo ya Uhifadhi Wanyama aina ya Sokwe, Dkt. Jane Goodall, aliyekuwa akifanya utafiti wa Wanyama hao kwa miaka 60 katika hifadhi mbalimbali na baadaye kujikita katika Hifadhi ya Gombe. Kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Tanapa, George Waitara na Bi. Gertude Mongella.  Waziri wa Maliasili na Utalii, Prof. Jumanne Maghembe Profesa Maghembe akizungumza wakati wa hafla ugawaji wa tuzo kwa Dk. Jane Goodall ambaye ametoa mchango mkubwa kwenye sekta ya uhifadhi na kubainisha tabia za sokwe ambazo watu wengi hawazijui. Profesa Maghembe aliongeza kuwa mtafiti huyo ambaye ni raia wa Uingereza amebainisha katika tafiti zake kwamba sokwe wana fikiri na wana hisia kama walivyo binadamu. Picha zote na Kajunason Blog/Cathbert Kajuna.  Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Alan Kijazi akitoa machache wakati wa hafla ya ugawaji wa tuzo kwa Dk. Jane Goodall ambaye ni muhifadhi Wanyama aina ya Sokwe aliyekuwa akifanya utafiti wa Wanyama hao kwa miaka 60.  Dkt. Jane Goodall, ambaye aliyekuwa akifanya utafiti wa Wanyama aina ya Sokwe kwa miaka 60 akitoa shukrani za pekee.    Wageni waalikwa waliofika kuhudhuria hafla hiyo. 

WATUMISHI WA MAHAKAMA WAASWA KUSHUGHULIKIA VITENDO VYA RUSHWA.


WAZIRI wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi amewaasa watumishi wa mahakama kushughulikia vitendo vya rushwa kwani vinaipatia mahakama taswira hasi na kuzitaka tume za  mahakama na maadili kuchunguza vitendo vya ukiukwaji wa maadili na kuchukua hatua stahiki.

Waziri Kabudi, amesema hayo leo jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na watumishi wa Mahakama Kuu na Mahakama ya Rufani juu ya mustakabali wa taasisi hiyo, ikiwa ni mara yake ya  kwanza kufanya ziara tangu alipoteuliwa kuwa Waziri.

Amesema, majaji na mahakimu mara nyingi, wamekuwa wakihusishwa na vitendo vya rushwa hivyo, na kuchangia kuwepo kwa kutokuwa na imani kwa wananchi wanaokuwa na shida ,mbali mbali katika taasisi hizo, hasa wale wenye kesi.

 ‘’Pamoja na mabadiliko makubwa katika mahakama bado kumekuwa na changamoto ya uadilifu hususan vitendo vya rushwa na uwajibikaji ambavyo vimeleta taswira hasi kwa wananchi wanaotafuta haki na kusababisha ushiriki mdogo,’’alisema Profesa Kabudi.

Ameongeza, watendaji wanapaswa kubuni mbinu mbali mbali za kuweza kubadili taswira hiyo kwa kuwachukulia hatua za kinidhamu wanaokiuka maadili na kusogeza huduma kwa wananchi.Kwa mujibu wa Profesa Kabudi, mahakama inanafasi kubwa ya kuchangia maendeleo ya nchi na kwamba jambo wanalopaswa kufanya ni kuimarisha utendaji kazi na kutokomeza rushwa.

Kwa upande wake, Kaimu Jaji Mkuu, Profesa Ibrahim Juma alisema kuwa wataendelea kutumia sheria kwa ajili ya kuwainua wananchi wengi kwa lengo la kukuza uchumi.

Profesa Juma alisema majaji na mahakimu ni sehemu ya jamii ambao wanapaswa kushiriki kustawisha wanaqnchi ili kutokomeza umasikini.
Akiwasilisha ripoti kuhusu mahakama, Mtendaji Mkuu wa mahakama, Hussein Katanga alisema kuwa idadi ya majaji imeshuka kutoka 100 hadi 80 huku uhitaji wake ukiwa ni kati ya 100 hadi 120.

Katanga alisema majaji 20 wameacha kazi kwa sababu mbalimbali ikiwemo kustaafu na kwamba uhitaji huo unachangia kasi ya kuongezeka kwa ufunguaji mashauri. 

Hali ya Sethi yabadilika, augua tumbo

Dar es Salaam. Wakili wa kujitegemea, Alex Balomi ameifahamisha Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Harbinder Singh Sethi anaumwa, hali yake imeendelea kubadilika na hii  ni wiki ya nne sasa  hawezi kupata usingizi.
Balomi aliyaeleza hayo leo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi mara baada ya Mwendesha Mashtaka Mwandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Leonard Swai kuieleza mahakama kuwa kesi ilikuja kwa ajili ya kutajwa na upelelezi wake bado haujakamilika.
Baada ya kutolewa maelezo hayo na Swai, Wakili Balomi ameiambia mahakama hiyo kuwa Sethi anasumbuliwa na uvimbe tumboni ambao unahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari.
“Kutokana na hali yake kuwa mbaya hii ni wiki ya nne sasa hawezi kupata usingizi hivyo anahitaji  ungalizi wa karibu wa madaktari  na kwamba wamebahatika kupata nyaraka kadhaa kutoka kwa daktari,” Balomi  aliifahamisha mahakama.  
Balomi aliongeza kuwa hata siku aliyokamatwa alikuwa akienda kwenye matibabu Afrika Kusini.
Swai  amesema  nyaraka ambazo Wakili Balomi anataka kuziwasilisha mahakamani hapo kuhusiana na Sethi hazijakidhi vigezo vya kisheria  na kwamba alitegemea daktari ambaye anamtibu angefika mahakamani kueleza hali  halisi ya ugonjwa husika.
Kutokana na hoja hizo, Hakimu Shaidi amesema suala la ugonjwa si la kufumbiwa macho, linapaswa kuchukuliwa kwa uzito na kuelekeza magereza kufanya kila linalowezekana kuhakikisha hali ya mshtakiwa huyo inabaki katika hali nzuri na inapobidi wawasiliane na wataalam wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
Kesi imeahirishwa hadi Julai 28, 2017 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.
Katika kesi hiyo, Sethi na James Rugemalira wanakabiliwa na mashtaka 12 ya uhujumu uchumi kwa kula njama, kujihusisha na mtandao wa uhalifu, kughushi, kutoa nyaraka za kughushi, kujipatia fedha kwa njia za udanganyifu, kutakatisha fedha na kusababisha hasara ya Dola 22, 198,544.60 sawa na Sh 309,461,300,158.27.

Vituo vya mafuta kuendelea kufungwa


Dar es Salaam. Vituo kadhaa vya kuuza  dizeli, petroli na mafuta ya taa vimefungwa jijini hapa kutokana na kutokuwa na mashine za kielektroniki za kutoa risiti (EFDs).
Hatua hiyo inayotekelezwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), imeelezwa kuwaathiri si tu wenye vituo bali hata watumiaji.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi wa TRARichard Kayombo amesema leo  Julai 14 na kuongeza kwamba  wanaendelea na kazi hiyo nchi nzima ili kuhakikisha sheria inatekelezwa.