Saturday, July 29

ZIMAMOTO WAKUTANA NA WADAU WA VIFAA VYA USALAMA DHIDI YA MAJANGA YA MOTO (TAFEDA) JIJINI DAR ES SALAAM.

 Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye (Katikati), akizungumza na Wadau wa Vifaa vya Usalama dhidi ya majanga ya moto (TAFEDA), walipokutana na kufanya kikao katika ukumbi wa Mikutano Makao Makuu ya Jeshi hilo, leo jijini Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Wadau wa Vifaa vya Usalama dhidi ya majanga ya moto (TAFEDA), Mohamed Kaumbwa akitoa utambulisho wa wajumbe aliombatana nao, walipokutana na kufanya kikao katika ukumbi wa Mikutano Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, leo jijini Dar es Salaam.
Kamishna Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Thobias Andengenye, akiwa kwenye picha ya pamoja na Wadau wa Vifaa vya Usalama dhidi ya majanga ya moto, leo jijini Dar es Salaam. (Picha na Jeshi la Zimamoto Na Uokoaji)

IMEANDALIWA NA KITENGO CHA HABARI NA ELIMU KWA UMMA-JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI

Chanjo ya Homa ya Ini Kupungua Bei Nchini

Na Agness Moshi – MAELEZO.

Bohari Kuu ya Dawa (MSD) imepunguza gharama ya chanjo ya ugonjwa wa homa ya ini kutoka shilingi 22,000 kufikia shilingi 5,300 ili kusaidia upatikanaji wa chanjo hiyo katika vituo vingi vya tiba hapa nchini hususani vituo vya Umma.

Hayo yamesemwa leo  Jijini Dar es Salaam  na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee  na Watoto Ummy Mwalimu  katika maadhimisho ya siku ya homa ini Duniani  yanayoadhimishwa kila mwaka Julai 28 kama ilivyopendekezwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) Kwa lengo la kuelimisha jamii  na kutambua athari za ugonjwa huo.
Ummy amesema kuwa Serikali imeamua kununua dawa ya chanjo ya ugonjwa huo moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji ili kuwawezesha Wananchi kuipata kwa gharama nafuu zaidi  kwa lengo la kuunga mkono kauli mbiu ya maadhimisho ya ugonjwa huo kwa mwaka huu ambayo inasema “Tokomeza Homa ya Ini (Eliminate Hepatitis)”.

“Matibabu ya homa ya ini yana gharama kubwa, ambapo kwa mgonjwa aliyepata maambukizi ya virusi C anaweza kutibiwa kwa millioni tatu hadi tano kulingana na muda wa tiba ndio maana tunasema bora kinga kuliko tiba,” alisema Ummy.

Aliongeza kuwa  chanjo inayotolewa nchini  kwa sasa ni  ya  virusi B inayojulikana kama Hepatitis B  japo chanjo ya virusi A ipo na inatolewa nchi nyingine  kutokana na Tanzania kukabiliwa  na  aina mbili tu virusi ambavyo  ni virusi B na C. 

“Kwa sasa hakuna ushahidi wa mlipuko wa homa ya Ini nchini, hata hivyo wananchi wa Tanzania na Afrika Mashariki wapo katika hatari ya kupata ugonjwa huu kutokana na njia za maambukizi kufanana kwa kiasi na zile za maambukizi ya virusi vya ukimwi,” aliongeza Ummy.

Waziri huyo  alisema kuwa chanjo hiyo ilianza kutolewa bure nchini kwa watoto waliozaliwa kuanzia mwaka 2003 na kuendelea. Aidha mwaka 2015 zaidi ya dozi 650,000 ilitolewa kwa watumishi wa afya ili kuwakinga na hatari ya  maambukizi  ya ugonjwa huo wakati wakitekeleza majukumu yao ya utoaji huduma kwa waathirika wa ugonjwa huo.

“Kwa sasa tunaangalia ni namna gani tunaweza kuifikia jamii iliyobaki ili tuweze kuwapatia chanjo, Serikali imeshafanya mchanganuo rasmi ambao umeonyesha kiasi cha gharama ya chanjo, vitendanishi vya vipimo vya awali, kutunza chanjo, kusambaza chanjo na shughuli yenyewe ya uchanjaji,” alifafanua Ummy.

Aidha amesema kuwa kwa sasa chanjo hiyo inatolewa kwa malipo ya shillingi 50,000 mpaka 70,000 kwa dozi moja  katika baadhi ya vituo binafsi vya Afya  ikiwa  ni pamoja na Premier Care Clinic, IST Na Hindu Mandal kwa mkoa wa Dar es Salaam. 

Ummy amewataka wananchi kujiepusha na maambukizi ya ugonjwa huo kwa kuachana na matumizi ya dawa kiholela, vilevi kupita kiasi, madawa ya kulevya, matumizi ya sindano zisizo salama na vihatarishi vyote vya maambukizi ya ukimwi kwani wagonjwa wa ukimwi wapo kwenye hatari kubwa ya kupata maambukizi kuliko wazima.

Mwenyekiti wa Kijiji Jela Miaka Mitatu kwa Rushwa ya Sh.20,000


Mwenyekiti wa Kitongoji cha German, Kijiji Machochwe wilayani hapa Mkoa wa Mara, Ibrahim Magere amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh500,000 kwa kosa la kuomba rushwa ya Sh20,000.

Akitoa hukumu hiyo Hakimu wa Wilaya ya Serengeti, Amalia Mushi alisema mshtakiwa ametiwa hatiani katika kesi ya jinai namba 37/2017 kufuatia ushahidi uliotolewa upande wa Takukuru kutoacha shaka.

Kabla ya hukumu hiyo, Wakili wa Takukuru, Eric Kiwia alidai kuwa mshtakiwa aliomba Sh20,000 kutoka kwa Joseph Rhobi mkazi wa kijiji hicho aliyekamatwa kwa madai kuwa alikuwa akitafutwa na polisi.

Aliendelea kuwa Rhobi mwaka 2012 alikamatwa na askari wa Kituo kidogo cha Polisi Machochwe, lakini alitoroka akiwa amefungwa pingu ambazo baadaye alizisalimisha kwa mtendaji wa kijiji.

Mwanzoni mwa mwaka huu, Rhobi alihitaji barua ya utambulisho kutoka ofisi ya kijiji, hivyo mwenyekiti huyo alitoa taarifa polisi na mtuhumiwa alikamatwa.

Hata hivyo, Rhobi aliachiwa kwa dhamana hivyo Mwenyekiti wa Kitongoji alimdhamini huku akimdai Sh20,000 kumaliza suala hilo hali iliyosababisha kutoa taarifa Takukuru na kufanikisha kukamatwa.

Mshtakiwa alipelekewa magereza baada ya kushindwa kulipa faini ya Sh500,000.

RAIS AAGIZA KUSIMAMISHWA KAZI KWA NAIBU KAMISHNA WA UHAMIAJI


 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiongea wakati wa kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Projest Rwegasira na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala 

RAIS Dkt. John Magufuli amemuagiza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kumsimamisha kazi Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Bi. Grace Hokororo asimamishwe kazi kwa tuhuma za kuingiza nchini raia 50 wa Somalia na kuwapa vibali vya kuishi kinyume cha taratibu.
Kauli hiyo imetolewa leo (Ijumaa, Julai 28, 2017), na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kumaliza kikao na Makamishna wa uhamiaji. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.
Pia Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba kuunda tume ya uchunguzi kuhusu utoaji wa vibali uraia nchini.
Amesema haiwezekani raia wa kigeni wanaingizwa nchini na wanapewa vibali vya kuishi bila ya kufanyiwa uchunguzi wa kina. “Idara ya Uhamiaji tunaitegemea kusimamia mipaka yetu na kuziba mianya ya watu kuingia bila ya kufuata taratibu lakini kwa mapenzi yake Ofisa huyu ameruhusu Wasomali kuingia bila kufuata taratibu.”
Waziri Mkuu amesema ni lazima uchunguzi ufanyike ili kubaini jambo hilo kwa kina: “Tulidhani ni kitu gani kilimsukuma kutoa vibali kwa Wasomali hao ambao hawakuwepo nchini wameingia na kupewa vibali moja kwa moja kwa mapenzi yake tu...Sasa hii ni dosari hatuwezi kuivumilia.”
Amesema Serikali inaitegemea Idara ya Uhamiaji kwa kuzuia mianya ya uingiaji raia mbalimbali kutoka nje ya nchi bila ya kufuata taratibu, hivyo Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ameagiza Ofisa huyo asimamishwe kazi na uchunguzi ufanyike ili kubaini malengo yake.
"Hawa Wasomali aliowapa vibali vya kuishi wala hawakuwa wanaishi nchini wameingia tu na kupewa vibali. Hivyo Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli ameagiza ofisa huyo akae pembeni na achunguzwe ni kujua ni kitu gani kilimsukuma kutoa vibali kwa raia hao."
Pia Waziri Mkuu ameiagiza idara ya Uhamiaji wadhibiti kitengo cha utoaji hati za kusafiria za Kibalozi na kwa wanaomaliza muda wasipewe tena. " Lazima hati hizo zikaguliwe katika mipaka yote na maeneo yote ya usafiri ili kujua kama huyo anayeitumia bado anahadhi hiyo na msiporidhika ichukuweni kwani kuna watu wanazitumia vibaya."
Hata hivyo Waziri Mkuu ameagiza uchunguzi wa kina ufanyike kwa watu wote walioomba hati za kusafiria pamoja na vibali vya makazi kama wanakidhi matakwa ya kisheria kabla ya kuwakabidhi.
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiongea wakati wa kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akitoa maagizo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt.  Anna Peter Makakala baada ya kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.


 
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiendela kutoa maagizo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Projest Rwegasira, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala na Makamishna wa Idara hiyo baada ya kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Projest Rwegasira, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala na Makamishna wa Idara hiyo baada ya kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiteta jambo na  Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala. Picha na habari na Ofisi ya Waziri Mkuu

WAKILI WA LISSU, FATMA KARUME AMBURUZA KORTINI ASKARI POLISI ALIYEMSHIKA MKONO MAHAKAMANI


Wakili wa Mwanasheria Mkuu wa Chadema na Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika, Fatma Karume amefungua kesi ya madai Mahakama Kuu ya Tanzania dhdi ya Inspekta wa Polisi Eugene Mwampondela wa Kituo Kikuu cha Polisi Dar es salaam.

Fatma amesema kuwa Inspekta Mwampondela alimshika mkono na kumvuta kwa nguvu hali iliyomsababishia maumivu makali, hivyo anadai alipwe kiasi cha shilingi bilioni moja kwa kosa la kumwingilia mwilini mwake na kumbughudhi kwa kumzuia kufanya kazi yake.

“Aliniambia kuwa ameagizwa na wakubwa kutoka juu, hivyo namfikisha mahakamani ili amweleze jaji ni nani aliyemtuma, na mimi sitaki kushikwa shikwa mwili wangu kwa hiyo naomba anilipe shilingi bilioni moja ili liwe fundisho kwa wengine,”amesema Fatma.

Fatma ambaye ni mmoja wa mawakili wa Mbunge wa Singida Mashariki alikumbana na kadhia hiyo wakati akiwa katika harakati za kumtetea mteja wake ili aweze kupata dhamana.

Waziri Mkuu wa Israil akifunga kituo cha tv cha Al-Jazeera


Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu aamuru ofisi za kituo cha habari cha al Jazeera kufungwa mjini Jerusalemu

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu ametoa amri ya kufungwa kwa  ofisi za kituo cha habari cha kimataifa cha al Jazeera mjini  Jerusalem.

Ukandamizwaji wa waandishi wa habari na vyombo vya habari na jeshi la Israel mjini Jerusalem umeathiri kituo cha habari la al Jazeera.

Waziri mkuu wa Israel  katika kurasa zake katika mitandao ya kijamii amesema kuwa ameamuru kufungwa kwa ofisi za kituo cha al Jazeera kwa kuwa kinashawishi ghasia katika mskiti wa al Aqsa.

Wanahabari wanoajaribu kunasa picha za matukio  ya ghasia al Aqsa hushambuliwa na kubugudhwa na jeshi la Israel.

Serikali Haitavumila Kuona Taasisi Zinajiendesha kwa Hasara

 Msajili wa Hazina Dkt. Oswaid J. Mashindano akifafanua jambo katika kikao kazi cha uhamasishaji wa sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu mbele ya Wenyeviti wa Bodi, Watendaji Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara  leo Jijini Dar es Salaam.Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Kimenejimenti kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina Bw. Mihale Mwakabinga na Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Umma wa OMH, Bw. Maftah Bunini.
 Mkurugenzi wa Huduma za Kimenejimenti wa Ofisi ya Msajili wa Hazina Bw. Mihale Mwakabinga akiwasilisha mada kuhusu majukumu ya Msajili wa Hazina, Bodi na Wizara Mama katika usimamzi wa Mashirika na Taasisi za Umma katika kikao kazi kikao kazi cha uhamasishaji wa sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu kilichowakutanisha na Wenyeviti wa Bodi za Wakurugenzi,Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara leo Jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa Uwekezaji wa Umma kutoka Ofisi ya Msajili wa Hazina akielezea jambo wakati akiwasilisha mada kuhusu maana ya Mashirika ya Umma katika kikao kazi kikao kazi cha uhamasishaji wa sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu kilichowakutanisha Wenyeviti wa Bodi za Wakurugenzi, Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara leo Jijini Dar es Salaam. Kutoka kulia ni Msajili wa Hazina Dkt. Oswaid J. Mashindano na Mkurugenzi wa Huduma za Kimenejimenti wa Ofisi ya Msajili wa Hazina Bw. Mihale Mwakabinga.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), Samwel Mwita Nyantahe akichangia hoja wakati wa kikao kazi baina ya Ofisi ya Msajili wa Hazina na Wenyeviti wa Bodi za Wakurugenzi, Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara leo Jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kimefanyika kwa lengo la kuhamasisha sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu yao.
 Mkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT)  akichangia mada wakati wa kikao kazi baina ya Ofisi ya Msajili wa Hazina na Wenyeviti wa Bodi za Wakurugenzi, Watendaji Wakuu wa Mashirika na Taasisi za Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara leo Jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kimefanyika kwa lengo la kuhamasisha sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu yao.
 Baadhi ya washiriki wa kikao kazi cha uhamasishaji wa sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu mbele ya Wenyeviti wa Bodi, Watendaji Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara  leo Jijini Dar es Salaam.
Msajili wa Hazina Dkt. Oswald J. Mashindano akifurahia jambo na Kaimu Mkurugenzi wa Bima ya Maisha na Mafao kutoka Shirika la Taifa la Bima (NIC) Bw. Michael Mowo walipokutana katika kikao kazi cha uhamasishaji wa sheria mbalimbali za Ofisi ya Msajili wa Hazina, wajibu na majukumu kilichowakutanisha Wenyeviti wa Bodi za Wakurugenzi, Watendaji Wakuu wa Taasisi na Mashirika ya Umma pamoja na Makatibu Wakuu wa Wizara  leo Jijini Dar es Salaam.

MCHAPALO WA MIAKA 50 YA BENKI YA NBC WAFANA JIJINI MWANZA

Image result for mwanza


Jana Julai 28,2017 usiku wa kuamkia leo jumamosi, mchapalo (sherehe) wa kusherehekea miaka 50 tangu kuanzishwa kwa benki inayolitumikia Taifa la Wachapakazi, NBC umefana Jijini Mwanza ambapo benki hiyo imekutana na wadau wake wakiwemo wafanyabiashara.

Kaimu Mkurugenzi wa benki ya NBC, Theobald Sabi alisema maadhimisho hayo yamefanyika Jijini Mwanza ikizingatiwa kwamba Jiji hilo ni la pili kwa ukubwa nchini na kwamba inao wateja wa muda mrefu wanaohudumiwa kwenye matawi yake matatu hivyo ni jambo jema kujumuika nao pamoja.

"Hakika NBC ina historia ndefu katika kujenga uchumi wa nchini yetu, ni jambo lisilopingika kwamba NBC ni mama wa benki za kibiashara hapa Tanzania". Alidokeza Sabi huku akiwashukuru wafanyakazi wa benki hiyo waliojawa uzalendo, umakini na ubunifu katika kazi.

Mkurugenzi wa Bodi ya NBC, Dr.Kassim Hussein alisema moja ya hatua za benki hiyo ni kuwa kitovu cha malipo yote nchini (National Payment System) mfumo ambao hadi sasa unategemewa nchini. Alidokeza kwamba miaka ya 70 mbali ya kutoa huduma nchini nzima, vile vile benki hiyo ilikuwa ikitoa huduma kwa njia ya mawakala, ikawa mwanzishi wa mobile banking pamoja na huduma za bima.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Merry Tesha aliipongeza benki ya NBC kutokana na mapinduzi yake kwenye sekta ya kifedha nchini na kuiomba kuwekeza moja kwa moja ama kwa ubia katika utekelezaji wa azima ya serikali ya ujenzi wa viwanda nchini ikiwemo kutoa mikopo kwa wawekezaji wa ndani.

WADAU WA MAENDELEO WAIMWAGIA TANZANIA MSAADA WA BILIONI 101 KUJENGA BARABARA YA KIDATU HADI IFAKARA KWA KIWANGO CHA LAMI


Wizara ya Fedha na Mipango imetiliana saini na Kampuni ya ujenzi wa barabara ya Reynolds kandarasi ya ujenzi wa barabara ya kutoka Kidatu hadi Ifakara mkoani Morogoro, yenye urefu wa kilometa 67 kwa kiwango cha lami utakaojengwa kwa shilingi bilioni 101, kupitia ufadhili wa Umoja wa Ulaya, Marekani na Uingereza.

Mkataba huo umesainiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bi. Amina Shaaban kwa niaba ya Serikali ya Tanzania na Bw. Dan Yzhak Shahn, Bw. Benjamin Arbit ambaye ni Mkandarasi kutoka Kampuni ya Ujenzi ya Reynolds.
Kiasi hicho cha fedha ni sawa na Euro milioni 40.4 ambapo  Euro milioni  29.6 zimetolewa kwa ushirikiano wa Umoja wa Ulaya na Shirika la Misaada la Uingereza-UK-AID, huku  kiasi kinachobaki cha Euro milioni 10.8 kikitolewa na Shirika la Misaada la watu wa Marekani- USAID.
Akizungumza mara baada ya kutiwa saini kwa kandarasi hiyo, Bi. Amina Khamis Shaaban, amesema ujenzi wa barabara hiyo utakaohusisha pia ujenzi wa daraja katika Mto Ruaha Mkuu, utasaidia wakulima wadogo kupitia Program ya Uendelezaji Kilimo katika Ukanda wa Kusini mwa Tanzania-SAGCOT, walioko katika Bonde la Mto Kilombero, kuyafikia masoko ya uhakika ya mazao yao.

“Kuimarika kwa kipande hiki cha barabara kutaongeza uzalishaji wa nafaka na bidhaa nyingine hatimaye kupunguza gharama za chakula na umasikini wa wananchi” aliongeza Bi. Shaaban

Bi Shaaban amewashukuru wadau hao wa maendeleo kwa msaada huo utakao fungua milango ya kiuchumi kwa Watanzania kupitia Program hiyo ya kuendeleza Kilimo katika Ukanda huo wa Kusini-SAGCOT, unaohusisha pia kuboresha masuala ya nishati ya umeme.

 “Ujenzi wa miundombinu unalengo la kuchochea maendeleo ya kilimo cha kibiashara kwa kuwa itasaidia kuwakutanisha pamoja wafanyabiashara na wakulima”. Aliongeza Bi Shaaban.

Aidha amesema uboreshwaji wa miundombinu utachochea uwekezaji ambao ndio chachu ya maendeleo ya biashara za watu wa chini, hivyo kuinua kiwango cha maisha yao.

“Barabara ya Kidatu hadi Ifakara ndiyo inayounganisha Wilaya za Kilombero na Ulanga na ni barabara kuu itokayo Bandari ya Dar es Salaam kwenda Zambia, Malawi na nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) hivyo kuwa na tija katika kuharakisha maendeleo ya kiuchumi jambo ambalo ndio lengo kubwa la Wahisani hao”. alifafanua Bi Shaaban.

Kwa upande wake Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU) hapa nchini, Roeland van de Geer ameahidi kuwa EU, UKAID na USAID, zitaendelea kushirikiana kwa kiwango cha juu na Serikali ya Tanzania katika kuboresha Sekta ya ujenzi na miundombinu kwa ujumla lakini pia atahakikisha wanachangia katika kupata soko la uhakika la mazao ya kilimo.
Sekta ya kilimo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi wa Tanzania mbapo zaidi asilimia 70 ya wakazi wake hutegemea kilimo na kuna uwezekano mkubwa wa kuongeza uzalishaji, kipato na kukuza ajira, hususan kwa wanawake na vijana ikiwa miundombinu inayochangia ukuaji wa Sekta hiyo itazidi kuimarika.

SHEIKH SHARIFF AFANYA DUA MAALUMU TEMEKE MWEMBE YANGA


Sheikh Shariff Majini kutoka kituo cha Dua na Maombi Mabibo Jijini Dar es salaam Ijumaa amefanya Dua maalum kwa wakaazi wa Temeke na maeneo ya jirani katika uwanja wa Mwembe Yanga.
 Dua hiyo  ambayo imefunguliwa na Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhad Musa itakuwa kwa siku tatu kuanzia Ijumaa tarehe 28-07-2017 mpaka Jumapili tarehe 30-07-2017 ambapo itafungwa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mheshimiwa Paul Makonda. 
 Dua ya Sheikh Shariff  pamoja na kuliombea Taifa letu pamoja viongozi wake makini lakini pia ni maalum kwa wakazi wa Temeke ambao mara nyingi wamekuwa wakimpigia simu Sheikh mara kwa mara ili aende kufanya mkutano wa Dua kwa ajili ya utatuzi wa matatizo yao mbalimbali yakiwemo Majini na wachawi mbalimbali wanaowasumbua. 
 Dua za Sheikh huwa zinaanza mchana saa nane na kumalizika saa kumi na mbili jioni.
Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhad Mussa akizungumza kwenye Dua hiyo iliyoendeshwa na Sheikh Shariff Majini kutoka kituo cha Dua na Maombi Mabibo Jijini Dar es salaam
Sheikh Shariff Majini kutoka kituo cha Dua na Maombi Mabibo Jijini Dar es salaam akiongea
Sheikh Shariff Majini kutoka kituo cha Dua na Maombi Mabibo Jijini Dar es salaam akimshukuru Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Sheikh Alhad Mussa
Sehemu ya umati wa kinamama wa Temeke na maeneo ya jirani waliohudhuria dua hiyo

RAIS AAGIZA KUSIMAMISHWA KAZI KWA NAIBU KAMISHNA WA UHAMIAJI



RAIS Dkt. John Magufuli amemuagiza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kumsimamisha kazi Naibu Kamishna wa Uhamiaji, Bi. Grace Hokororo asimamishwe kazi kwa tuhuma za kuingiza nchini raia 50 wa Somalia na kuwapa vibali vya kuishi kinyume cha taratibu.
Kauli hiyo imetolewa leo (Ijumaa, Julai 28, 2017), na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa mara baada ya kumaliza kikao na Makamishna wa uhamiaji. Kikao hicho kilifanyika Makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.
Pia Waziri Mkuu amemuagiza Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Mwigulu Nchemba kuunda tume ya uchunguzi kuhusu utoaji wa vibali uraia nchini.
Amesema haiwezekani raia wa kigeni wanaingizwa nchini na wanapewa vibali vya kuishi bila ya kufanyiwa uchunguzi wa kina. “Idara ya Uhamiaji tunaitegemea kusimamia mipaka yetu na kuziba mianya ya watu kuingia bila ya kufuata taratibu lakini kwa mapenzi yake Ofisa huyu ameruhusu Wasomali kuingia bila kufuata taratibu.”
Waziri Mkuu amesema ni lazima uchunguzi ufanyike ili kubaini jambo hilo kwa kina: “Tulidhani ni kitu gani kilimsukuma kutoa vibali kwa Wasomali hao ambao hawakuwepo nchini wameingia na kupewa vibali moja kwa moja kwa mapenzi yake tu...Sasa hii ni dosari hatuwezi kuivumilia.”
Amesema Serikali inaitegemea Idara ya Uhamiaji kwa kuzuia mianya ya uingiaji raia mbalimbali kutoka nje ya nchi bila ya kufuata taratibu, hivyo Mheshimiwa Rais Dkt. Magufuli ameagiza Ofisa huyo asimamishwe kazi na uchunguzi ufanyike ili kubaini malengo yake.
"Hawa Wasomali aliowapa vibali vya kuishi wala hawakuwa wanaishi nchini wameingia tu na kupewa vibali. Hivyo Mheshimiwa Rais Dkt. John Magufuli ameagiza ofisa huyo akae pembeni na achunguzwe ni kujua ni kitu gani kilimsukuma kutoa vibali kwa raia hao."
Pia Waziri Mkuu ameiagiza idara ya Uhamiaji wadhibiti kitengo cha utoaji hati za kusafiria za Kibalozi na kwa wanaomaliza muda wasipewe tena. " Lazima hati hizo zikaguliwe katika mipaka yote na maeneo yote ya usafiri ili kujua kama huyo anayeitumia bado anahadhi hiyo na msiporidhika ichukuweni kwani kuna watu wanazitumia vibaya."
Hata hivyo Waziri Mkuu ameagiza uchunguzi wa kina ufanyike kwa watu wote walioomba hati za kusafiria pamoja na vibali vya makazi kama wanakidhi matakwa ya kisheria kabla ya kuwakabidhi.
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiwasili Makao Makuu ya Uhamiaji eneo la Kurasini jijini Dar es Salaam.



 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiongea wakati wa kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam. Kikao hicho kilihudhuriwa pia na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Projest Rwegasira na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala 
 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiongea wakati wa kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akitoa maagizo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt.  Anna Peter Makakala baada ya kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.


 




Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiendela kutoa maagizo kwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Projest Rwegasira, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala na Makamishna wa Idara hiyo baada ya kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.


 Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani Mhe. Mwigulu Nchemba, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Meja Jenerali Projest Rwegasira, Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala na Makamishna wa Idara hiyo baada ya kikao chake na Makamishna wa uhamiaji makao Makuu ya Uhamiaji jijini Dar es Salaam.






Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa akiteta jambo na 
Kamishna Jenerali wa Uhamiaji Dkt. Anna Peter Makakala.
Picha na habari na Ofisi ya Waziri Mkuu