Saturday, October 21

Raia wa DRC adaiwa kuiba watoto watatu


Mwanza. Jeshi la Polisi mkoani Mwanza linamshikilia raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), Ashia Ismail kwa tuhuma za wizi wa watoto watatu Jijini Mwanza.
Kamanda wa polisi mkoani Mwanza, Ahmed Msangi alisema kwamba mtuhumiwa huyo alikamatwa Oktoba 18, akiwa katika harakati za kuondoka na watoto hao wanaoishi Mtaa wa Shede, eneo la Mkuyuni.
“Wakati wa tukio, watoto hao walikuwa wakicheza nje ya nyumba yao,” alisema kamanda Msangi
Alifafanua kwamba baada ya kuwafikia watoto hao, mtuhumiwa alimchukua na kumbeba mgongoni mtoto mdogo huku akiwashikilia mikono wengine wawili na kuanza kuondoka nao kabla ya wakazi wa eneo hilo kumtilia shaka na kutoa taarifa kwa wazazi.
Akizungumzia tukio hilo, mzazi wa mmoja wa watoto hao, Elizabeth Marco alisema kwamba familia yake imeingiwa hofu kuhusu usalama wa watoto wao.
Tukio la kuibwa kwa watoto hao limetokea huku Watanzania wakiwa bado wana kumbukumbu ya matukio ya kusikitisha ya wizi wa watoto yaliyolikumba jiji la Arusha.

Kwa nini wanawake wamekuwa wakitumia #MeToo kwenye Twitter

Alyssa MilanoHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMui Alyssa Milano
Wanaume na wanawake kutoka maeneo mbalimbali duniani ambao wamenyanyaswa kijinsia wamekuwa wakisambaza habari zao katika mitandao ya kijamii wakitumia alama ya #Metoo kuonyesha viwango vya unyanyasaji wa kinjinsia ulivyokithiri.
Hatua hiyo inafuatia madai ya unyanyasaji dhidi ya mtayarishaji wa filamu katika Hollywood Harvey Weinstein.
Zaidi ya wanawake 20 akiwemo nyota wa filamu Angelina Jolie, Gwyneth Patltrow na Rose McGowan wametoa malalamishi dhidi yake ikiwemo ubakaji na nunyasaji wa kingono.
Wienstein amesisitiza kuwa uhusiano wa kingono aliokuwa nao ulikuwa umeruhusiwa na pande zote.
Tangu madai hayo kufichuliwa watu wengi maarufu wametumia mitandao ya kijamii kuliangazia swala la unyanyasaji wa kingono huku wengine wakielezea unyanyasaji waliopitia.
Wito huo unaotolewa chini ya #MeToo umetumiwa zaidi ya mara 200,000 tangu Jumapili usiku.
Neno hilo lilipata nguvu baada ya nyota wa filamu Alyssa Milano kuwataka waathiriwa wa unyanyasaji wa kingono kuwataka waathiriwa wa unyanyasaji wa kingono kujitokeza ili kuonyesha umoja.
Watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii walisambaza habari zao kuhusu vile walivyonyanyaswa.
Mtumiaji mmoja wa mtandao wa Twitter ambaye hakutaka kujulikana alichapisha: Nilikuwa na miaka 19.
Wanaume na watu waliobadili jinsia pia waliunga mkono wito huo akiwemo nyota wa filamu Javier Munoz huku wengine wakisambaza maelezo kuhusu waliyopitia.
Rajini VaidyanathaHaki miliki ya pichaRAJINI VAIDYANATHA
Image captionRajini Vaidyanatha
Rajini Vaidyanatha
Wito wa #MeToo umesambazwa sana duniani , ikiwemo Uingereza, Marekani , India na Pakistan huku wito mwengine kama huo ukiendelea kusambazwa katika maeneo mengi.
Nchini Ufaransa , watumiaji wa Twitter wanatumia #balancetonporc ama ''rat on dirty old man'' ili kuwashinikiza wanawake kutaja na kuwaibisha washambuliaji wao ,huku #womenwhoroar ni neno jingine linalotumika kuwashinikiza waathiriwa wa unyanyasaji huo kujitokeza na kuongea

Kwa nini viboko wamekuwa al-Kiboko kwa raia Sabaki, Kenya

Viboko wageuka magaidi kwa wakazi pwani ya Kenya
Wakazi wa eneo la Sabaki kaunti ya Kilifi pwani ya Kenya wamelalamika vikali kuhusu viboko ambao wanawavamia mpaka nje ya nyumba zao, na kuharibu mashamba pamoja na kuingilia mifugo yao.
Kwa kawaidia viboko hao huwavamia usiku kwani wakati huo macho yao huona zaidi ya vile yanavyoona mchana.
Kulingana na mzee wa kijiji, Safari Kadenge Karisa, idadi ya viboko imeongezeka na kuwa zaidi ya mia nne, hivyo basi wengi wao ikifika usiku huvamia wenyeji kwenye makaazi yao.
"Tumechoka na uvamizi huu wa viboko,'' asema Karisa.
"La kusikitisha ni kwamba kila mara tunapopiga ripoti kwa watu wa shirika la huduma la wanyama pori wanachelewa sana kuwasili kutuhudumia tunapovamiwa. Tumeamua endapo KWS hawatatusaidia tutavichinja viboko tupate chakula.''
Spika wa wodi ya Sabaki, Stembo Kaviha anasema: "Tangu lini wanyama wakatawala maisha ya binadamu? Ni binadamu ambaye anatawala lakini sasa wakaazi wa Sabaki tumekuwa watumwa wa viboko. Kufikia saa kumi na mbili za jioni sote tuko ndani ya nyumba na hamna kutoka nje maanake viboko wanazunguka kwenye nyumba zetu. Tumeamua sasa ni vita vya binadamu na wanyama. Na KWS wasiingilie.
Spika wa wodi ya Sabaki Stembo Kaviha anasema viboko wamekua na magaudi hatari zaidi kwao.
Image captionKaviha anasema viboko wamekuwa na magaidi hatari zaidi kwao
"Hapa Kenya tuna janga la Al Shabaab lakini sasa imekua ni Al Kiboko!, wale wengine ni magaidi wa kimataifa lakini hawa viboko ni magaidi wa hapa nyumbani.
"Kuna haja gani watu wa KWS wawe huko Marine Park, kilomita kama kumi na tano kutoka Sabaki. Mbona wasije hapa karibu na viboko wao badala ya kutuachia sisi tuwafanyie kazi yao. Ofisi zao ziko mbali sana.''
Kwa hivi sasa wakaazi wa Sabaki wanaomboleza kifo cha mmoja wao, Kennedy Kenga Charo, aliyeuawa na kiboko kwake nyumbani. Tukio hili limewaudhi zaidi, na wanasisitiza watachukua sheria mkononi mwao kwa kuwaua viboko hao.
Mjane wa marehemu Kennedy Charo Kenga, Sidi Mzungu kwake kijiji cha Sabaki. Mumewe aliuawa na kiboko nje ya nyumba yake.
Image captionMjane wa marehemu Kennedy Charo Kenga, Sidi Mzungu kwake kijiji cha Sabaki.
Mzee Kenga amemuacha mjane, Sidi Mzungu, na watoto wanane. Mama huyo anawaza na kuwazua jinsi atawalea watoto hao wote, wengine wakiwa bado wako shule ya chekechea.
Mama Mzungu anatueleza jinsi mumewe alivamiwa kwake nyumbani na kiboko.
"Bwanangu alitoka nje aliposikia ng'ombe anapiga kelele, kumbe ni kiboko alimvamia.Kiboko huyo alipomuona bwanangu akamvamia na kumuangusha chini, akamuuma paja na meno yake marefu ya mbele. Alitoa damu nyingi sana hadi akafa.
Mimi nadai malipo ya kiwango cha juu cha kuniwezesha kulea hawa watoto wangu maanake sina mtu mwingine wa kunisaidia.''
Mtoto wake mkubwa, Emmanuel Kenga, anasema huenda ikambidi aache shule (yuke sekondari sasa) amsaidie mamake.
"Tumeachwa na mzigo mzito sana, na kufikia sasa hawa KWS hawajasema lolote vile watatusaidia. Tuko njia panda hatujui tuanzie wapi. Yote haya ni kwa sababu wa viboko.''
Kahindi Safari ni mmoja ya waathiriwa waliovamiwa na viboko lakini kwa bahati nzuri hakumalizwa kabisa.
Safari anatusimulia zaidi: "Mimi nilikua navuka mto Sabaki sehemu ambayo haina maji mengi nikilisha mifugo yangu, ndio nikavamiwa na viboko wawili. Niliamua kujikinga kwa kuingia ndani ya maji, wakanifuata na kunikanyaga kabisa. Naumia sana kwa maumivu ya tumbo, figo, mgongo, shingo na kichwa. Sijapata matibabu ya kutosha. Hata usiku silali kwa sababu ya maumivu."
Mkuu wa shirika la huduma la wanyama pori kaunti ya Kilifi, Jane Gitau, anasema wanajaribu wawezavyo kuwafidia waathiriwa waliovamia na viboko huko Sabaki.
"Kwanza twatoa rambi rambi zetu kwa familia ya mzee Kenga aliyeuliwa na kiboko wetu. Sote tumesikitika mno na tayari tumeanza kushugulikia malipo yake. Tukifuata sheria tutamlipa shillingi milioni tano za Kenya.
"Ni kiwango kidogo kweli lakini hizo ndizo pesa twatoa kuwapa pole waliouliwa na viboko. Hatahivyo twaweza kumsaidia zaidi kulingana na uwezo wetu. Serikali ya kaunti nayo pia itashugulikia familia ya marehemu.''
Hata hivyo baadhi ya waathiriwa wanasema hawajafidiwa na serikali tangu wavamiwe na viboko hao, wakilaumu shirika la huduma la wanyama pori kwa kutilia maanani maslahi ya viboko zaidi ya binadamu.
Wakazi wa Sabaki
Jane Gitau amekanusha madai ya wakazi wa Sabaki kwamba wamezembea kwa kuwahudumia ipasavyo.
"Sio kweli tumezembea sisi kama KWS. Tunaelewa shida inayowakabili watu wa Sabaki, na ndio kwa maana kila siku tuko huko. Tatizo ni uchache wa watu wetu wa kazi lakini tutawadumia kikamilifu wakaazi hao.''
Mkuu huyo anasema wanafikiria suluhu ya kudumu kama vile kujenga ua ambalo litawazuia viboko kutoka nje na kuvamia watu kwenye makaazi yao.
Kiboko mkubwa kwa kawaida huwa ana uzani wa kati ya kilogramu 1000 hadi 1,600.
Meno yake mawili ya mbele ni makali sana na ndiyo wanayatumia kung'ata wakaazi wa Sabaki.
Kiboko ni miongoni mwa wanyama hatari zaidi duniani.