Wednesday, July 12

William Ngeleja kurudisha fedha za ESCROW, Sheria ya TZ inasemaje?


Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alitangaza hivi karibuni kurudisha Tsh. mil 40.4 alizopewa na mfanyabiashara James Rugemarila ambaye anahusishwa na tuhuma za ESCROW na kuibua mijadala katika jamii.
Hatua ya Ngeleja kurudisha fedha hizo imeibua mijadala mbalimbali katika jamii ambapo watu mbalimbali waikiwemo Wanasheria wamekuwa wakiizungumzia issue hiyo ambayo tayari baadhi ya wahusika wamefikishwa Mahakamani akiwemo Rugemarila na kusomewa mashtaka.
Miongoni mwa wanasheria hao ni Hashimu Mziray ambaye anasema alichokifanya Ngeleja ni udhaifu na anatakiwa kuomba radhi, kwani fedha hizo alizichukua muda mrefu na huenda alizifanyia uzalishaji ambapo kisheria halijakaa sawa
.

Hatma ya IPTL Ipo Mikononi Mwa JPM....Zimebaki Siku Mbili

ZIKIWA zimebaki siku mbili kufika Julai 15 ambao ndio ukomo wa leseni ya Kampuni ya kufua umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL), imeelezwa kuwa hatima yake sasa ipo mikononi mwa Ikulu.

Wakati Ikulu ikisubiriwa kuijibu wizara husika, endapo Julai 15 itapita bila IPTL kuongezwa muda wa leseni yake, haitaweza kuendelea tena na uzalishaji wa nishati hiyo.

Juni 11, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, alimsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Felix Ngamlagosi, ikiwa ni siku chache tangu mamlaka hiyo itoe taarifa kwa umma ya kuanza kukusanya maoni baada ya ombi la IPTL la kuongezewa leseni ya uzalishaji umeme kwa miezi 55.

Mara baada ya taarifa ya kusimamishwa kazi kwa Ngamlagosi iliyohusishwa na hatua ya Ewura kutoa tangazo kwa umma kuutarifu juu ya kutoa maoni yao kufuatia ombi la IPTL kuongezewa muda wa leseni yao ya uzalishaji umeme, mamlaka hiyo ilitoa taarifa nyingine kwa umma ikitaarufu kusimamisha ukusanyaji huo wa maoni.

“Taarifa inatolewa kwa umma kwamba kufuatia maombi ya kampuni ya uzalishaji umeme ya Independent Power Tanzania Limited (IPTL) (“Mwombaji”)
kuomba kuongezewa muda wa leseni yake ya kuzalisha umeme kwa kipindi cha miezi 55 kutokea tarehe 15 Julai 2017.

“Ewura zaidi ya hatua nyingine za kiudhibiti, iliwasiliana na Wizara ya Nishati na Madini ili kupata maoni yake kwa mujibu wa kifungu cha 7 (3) cha Sheria ya Ewura, sura ya 414 ya sheria za Tanzania.

“Wizara ya Nishati na Madini imetoa mapendekezo ya kuwapo na mashauriano zaidi kati ya Wizara, Ewura na wadau mbalimbali wa sekta ndogo ya umeme kabla ya kuendelea na mchakato wa maombi ya mwombaji.

“Kutokana na maoni hayo, Ewura inasitisha mchakato wa kushughulikia maombi ya leseni ya mwombaji ikiwa ni pamoja na upokeaji wa maoni/mapingamizi dhidi ya maombi hayo mpaka hapo yatakapotolewa maelekezo mengine,” ilisema taarifa hiyo.

Jana Meneja Mawasiliano na Uhusiano wa Ewura, Titus Kaguo, alipotafutwa na gazeti hili ili kuzungumzia hatima ya IPTL, alisema mashauriano na Serikali bado yanaendelea na ikifika Julai 15 ataweza kuwa na jambo la kusema.
“Kwenye tangazo letu tulisema mashauriano na Serikali yanaendelea na wadau wengine yanaendelea, kwa hiyo kwa sasa siwezi kusema kitu ila subiri hiyo Julai 15 nitakuwa na cha kusema,” alisema Kaguo.

MTANZANIA pia ilimtafuta Kamishina wa Nishati, Innocent Luoga, ili kujua mazungumzo ya suala hilo yalipofikia.
“Natamani kama ningeweza kukujibu, lakini suala hili msemaji wake ni Katibu Mkuu ambaye hayupo, lakini tu nikwambie ukweli kwamba kwa sasa lipo kwa Katibu Mkuu Kiongozi, kwa hiyo siwezi kusema chochote,” alisema Luoga.
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu, Gerson Msigwa, alipotafutwa ili kuthibitisha kama kweli suala hilo limefika mezani kwa Katibu Mkuu Kiongozi, alisema: “Hili suala ni la Wizara ya Nishati, kama wamewaambia kuwa wamelipeleka kwa Katibu Mkuu Kiongozi, basi watakachojibiwa watawaeleza.”

Kwa upande wao, Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) walipoulizwa baada ya leseni ya IPTL inayozalisha umeme megawati 110 (MW) kwa kutumia mafuata mazito itakapofika kikomo Julai 15 ni hatua gani itafuata, walisema hawawezi kusema lolote kwa sasa.

“Kwa sasa siwezi kuzungumza chochote juu ya suala hilo,” alisema msemaji wa shirika hilo, Leila Muhaji.
Makubaliano ya kuuziana umeme (Purchase Agreement-PPA) kati ya IPTL na Tanesco, yalisainiwa mwaka 1995 kwa miaka 20, huku leseni ya sasa ya IPTL ikiwa imetolewa na Wizara ya Nishati na Madini mwaka 1996 kwa kipindi cha miaka 21.

CHIMBUKO LA IPTL

Chimbuko la IPTL ni uhaba wa umeme mwaka 1994, ilipoonekana kuna uhitaji wa kuwa na umeme wa dharura.

Agosti 19, 2014, Mkurugenzi wa Kampuni ya Mechmar, iliyokuwa ikimiliki asilimia 70 ya hisa za IPTL, Datuk Baharuden Majid, aliongoza ujumbe kutoka Malaysia kuja kuzungumza na Serikali ya Tanzania.

Septemba 1994, Mkataba wa Maelewano (MOU) ulifikiwa, licha ya tahadhari kutoka kwa washauri wa Tanesco ambao ni kampuni za Acres (Canada) na Hunton and Williams (Uingereza), kwamba uwekezaji huo ulikuwa ni janga kwa sekta ya umeme na kwa uchumi wa taifa.

Kampuni hiyo ambayo wamiliki wake ni Mechmar ya Malaysia mwenye asilimia 70 na VIP ya Tanzania yenye asilimia 30 ilisaini mkataba wa miaka 20 (1995-2015) na Serikali ya Tanzania.

7.92 kwa mwezi kama ada ya huduma za mtambo. Mwaka 2002 IPTL ikaanza kuiuzia umeme Tanesco, lakini ilipofika 2004 ikabainika kuwa ilidanganya kuhusu mtaji.

Awali IPTL ilisema asilimia 30 ya mtaji ilikuwa nao sawa na Dola milioni 36 na kwamba asilimia 70 ilikopa.
Baada ya ukaguzi ikabainika IPTL haikuweka dola milioni 36 kama mtaji, bali iliweka dola 50 ambazo kwa wakati huo zilikuwa sawa na Sh 50,000.

Kutokana na kasoro hiyo, Tanesco ikataka gharama ya umeme ishuke.
Mabishano yakaendelea hadi mwaka 2006, ikaamuliwa kufunguliwa kwa akaunti maalumu (Tegeta Escrow) ili Tanesco iwe inaweka huko fedha hadi pale mwafaka utakapopatikana.

Mwaka 2008, IPTL ilishindwa kujiendesha, hivyo ikawekwa chini ya usimamizi wa Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini (RITA).
Hukumu ya Mahakama Kuu iliyotoka Septemba 2013 chini ya Jaji John Utamwa, iliamua IPTL iondolewe chini ya usimamizi wa Rita na mali zake zote ipewe Kampuni ya Pan Africa Power Solutions Ltd (PAP) ya Harbinder Singh Sethi.

Hukumu hiyo ilitoka huku mmiliki wa asilimia 70 ya IPTL (Mechmar) akiwa mufilisi nchini Malaysia na zaidi ICSID kukiwa na kesi inayohusu mgogoro wa IPTL na Serikali uliofunguliwa na Standard Chartered Bank, ambayo ilinunua deni la kampuni hiyo mwaka 2005 na ikaruhusiwa kuishtaki Serikali ya Tanzania kwenye baraza hilo lenye mamlaka ya mwisho.

Februari 2014, ICSID ilifanya uamuzi wa awali kwamba ni kweli IPTL inaitoza zaidi Tanesco na kuelekeza pande mbili zikafanye hesabu upya ndani ya siku 90 zilizoisha Mei 2014 kwa lengo la kujua ni kwa kiasi gani kampuni hiyo imelipunja shirika hilo katika bei tangu 2002 hadi 2013.

Hata hivyo, Tanesco na Serikali hawakutoa ushirikiano ndani ya siku hizo 90 kutekeleza uamuzi huo.
Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusu ukaguzi wa Akaunti ya Tegeta Escrow na umiliki wa Kampuni ya IPTL iliyowasilishwa bungeni Novemba 2014, ilionyesha kuwa fedha zilizokuwa kwenye akaunti hiyo ni Sh bilioni 306 na zilitakiwa kurudishwa Tanesco.

Kutokuwapo kwa umakini kwa Serikali kulisababisha Kampuni ya PAP kujimilikisha fedha za IPTL kwa asilimia 70 bila kuwa na ushahidi wowote kwamba iliinunua IPTL ikiwamo malipo ya kodi kama ilivyofanya kwa VIP yenye asilimia 30 za hisa.


IPTL INAVYOINYONYA TANESCO

Moja ya taarifa za Ewura kuhusu kampuni zinazoiuzia Tanesco umeme, zinaonyesha kuwa IPTL inaiuzia kila uniti kwa Dola za Marekani senti 23.1 na kila mwezi inalipwa Capacity Charge ya Dola za Marekani 2,655,786.
Ukikokotoa kiasi hicho kwa wastani wa kila Dola moja kwa Sh 2,238, inafanya kila mwezi IPTL kulipwa Sh bilioni Sh bilioni 5.943 ambayo kwa mwaka inakuwa wastani wa Sh bilioni 71.316.

SHULE YA HAZINA INTERNATIONAL SCHOOL

HAZINA INTERNATIONAL SHOOL ipo Magomeni Makuti Mtaa wa Mpwapwa, Shule ni ya Nursery na Primary pia ni Day na Boarding Mazingira ya shule ni mazuri sana, Shule ilianzishwa mwaka 2005 na tangu hapo Shule imefanya vizuri sana katika matokeo ya Darasa la 7.

Hivi ndivyo Shule ya HAZINA ilivyofanya vizri katika matokeo ya Darasa la 7 kwa miaka 3 mfululizo.

Matokeo ya Taifa ya darasa la  7 shule ya Hazina international school:

Mwaka 2014 Darasa la 7 ya 1 kiwilaya ya 1 kimkoa ya 12 kitaifa.

Mwaka 2015 Darasa la 7 ya 1 ya kiwilaya ya 1 kimkoa ya 11 kitaifa.

Mwaka 2016 Darasa la 7 ya 1 kiwilaya ya 1 kimkoa ya  5 kitaifa.

Shule ya HAZINA inafanya vizuri kwa sababu ina walimu wazuri sana na mazingira ya kufundishia ni mazuri sana Mlete mwanao aje kusoma shule ya HAZINA INTERNATIONAL SHOOL..

PIGA SIMU NAMBA 0713295712 / 0716999822 / 0716999800 kwa maelezo zaidi..


WHO WE ARE

Hazina International School follows the current Tanzania National curriculum with English as a medium of instruction. The curriculum also offers computer studies designed to fit the pupils’ needs as well as equipping them with the technological know – how. There are also extra curriculum activities geared to develop the health of the pupils and their physical fitness. As an English proverb goes – All work without play makes Jack a dull boy.

School Mission

To provide quality education and enable students of different cultures to live together and build lifelong friendships hence a united nation.

School Vision

To provide disciplined, educated and suitably qualified candidates for tomorrow’s job market and industrialists.



Picha za Taswira ya Shule ya HAZINA INTERNATIONAL SHOOL









Waziri wa Fedha akifungia kituo cha mafuta


Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika eneo la Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam na kuamuru kituo cha Mafuta cha GBP kifungwe hadi hapo kitakapo funga mashine maalumu za kutolea risiti baada ya kubainika hakitumii ipasanyo mashine za kieletroniki za kukusanyia kodi (EFD)

Dkt. Mpango amechukua hatua hiyo baada ya kujionea kituo hicho kikiwa na pampu nne za mafuta lakini kuna mashine moja pekee ya mkononi ya kutolea risiti jambo linasababisha wateja wao wengi kutopewa risiti na hivyo kuikosesha Serikali mapato yake na ni kinyume cha sheria za nchi.

“Sasa nawachukulia hatua ili liwe fundisho kwa wengine wote wanaouza mafuta nchini bila kufuata taratibu, na nitaanza na wewe, biashara yako isimame mpaka mashine zifungwe kwenye kituo chote na utekeleze mara moja,” alisema Dkt. Mpango

Katika ukaguzi wa Kituo cha Mafuta cha Puma, Dkt. Mpango amesifu utaratibu mzuri uliowekwa na kituo hicho kwa kufunga mashine maalumu za kutolea risiti zilizounganishwa na kila pampu za mafuta kitu ambacho ndicho Serikali inavitaka vituo vyote vya mafuta vitumie mfumo huo

“Kituo hiki kimezingatia sheria sheria kwa kufunga mashine kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali na hapa tunauhakika wa kupata fedha za kuwatumikia wananchi, kinyume kabisa na kituo cha mafuta nilichokifungia, hapa ndio ningeomba Watanzania wanunue mafuta” aliongeza Dkt. Mpango.

Ameiagiza Mamlaka ya mapato Tanzania-TRA kufanya ukaguzi nchi nzima ili kubaini wamiliki wa vituo vya mafuta wanaokiuka maagizo ya Serikali yaliyowataka wafunge mashine hizo maalumu tangu mwaka uliopita.

Waziri wa Fedha na Mipango amewageukia wenye vyombo vya moto wanaonunua mafuta kwenye vituo vya mafuta kote nchini kudai risiti wanapopata huduma ya kuwekewa mafuta kwenye vituo hivyo ili kuokoa fedha za Serikali zinazoishia mikononi mwa wajanja wachache wanaokwepa kodi kwa makusudi na kuikosesha Serikali mapato yake.

Baadhi ya wananchi wamepongeza uamuzi wa Serikali kupitia Waziri wa Fedha na Mipango wa kufanya ziara za kushitukiza kwenye vituo vya mafuta na kutaka hatua hiyo iwe endelevu kwa maafisa wengine wa Serikali ili kukomesha vitendo vya wenye vituo vya mafuta kukwepa kodi ya Serikali.

Katika siku yake ya kwanza ya ziara za namna hiyo, Julai 10 mwaka huu, Dkt. Mpango alikifungia kituo cha Mafuta cha Mawenzi kilichoko Kigamboni, Jijini Dar es Salaam baada ya kubaini kuwa kituo hicho kimefunga mashine maalumu za kutolea risiti za kielektroniki lakini hazitumiki na kuamuru kituo hicho kifungwe hadi kitakapo rekebisha kasoro hiyo na kuvionya vituo vya mafuta vya OilCom kufunga mashine za aina hiyo mara moja.

NAMNA WAZIRI WA FEDHA ALIVYOSHTUKIZA VITUO VYA MAFUTA KIGAMBONI



Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango, ameamuru kufungwa kwa kituo cha Mafuta cha Mawenzi kilichoko Kigamboni hadi mmiliki wake atakaporekebisha kasoro baada ya kubaini kuwa mashine maalumu za Kieletroniki zilizofungwa kwenye pampu za mafuta kwa ajili ya kutolea risiti hazitumiki jambo ambalo ni kinyume cha sheria.

ECOBANK YAINGIA MAKUBALIANO NA TICTS





Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Raphael Benedict (kulia) akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es salaam kuhusu ushirikiano wa Benki hiyo na TICTS ambapo wateja wa kampuni hiyo wataweza kufanya malipo yao kwa haraka na ufanisi zaidi kupitia tawi lolote la Ecobank hapa nchini ambapo katika kufanikisha jambo hilo benki imefungua Tawi lake katika jengo la PSPF linalopakana na geti la ofisi za TICTS, huku muda wa huduma ukiongezwa kuanzia saa 8:00 asubuhi hadi saa 4:00 usiku kwa siku za kazi, na saa 3:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni kwa siku ya Jumamosi. Katikati ni Mkurugenzi Mkuu wa TICTS Jared H. Zerbe na kushoto ni Katibu Mkuu wa Tanzania Freight Forwarders Association (TAFFA), Tony Swai. 
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Raphael Benedict (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa TICTS Jared H. Zerbe wakisaini mkataba wa makubaliano wa kushirikiana katika kuhakikisha wateja wa TICTS wanafanya malipo yao kwa haraka na ufanisi zaidi kupitia tawi lolote la Ecobank hapa nchini. Mkataba huo ulisainiwa jana katika tawi la Ecobank lililopo PSPF Towers jijini Dar es salaam. Anayeshuhudia kushoto ni Katibu Mkuu wa Tanzania Freight Forwarders Association (TAFFA), Tony Swai.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Raphael Benedict (wa pili kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa TICTS Jared H. Zerbe (katikati) wakipeana mkono baada ya kutia saini ya mkataba wa makubaliano wa kushirikiana katika kuhakikisha wateja wa TICTS wanafanya malipo yao kwa haraka na ufanisi zaidi kupitia tawi lolote la Ecobank hapa nchini. Mkataba huo ulisainiwa jana katika tawi la Ecobank lililopo PSPF Towers jijini Dar es salaam. Wanaoshuhudia (kulia) ni Mkurugenzi wa Usimamizi wa fedha wa Ecobank Africa, Isaac Kamuta, Katibu Mkuu wa Tanzania Freight Forwarders Association (TAFFA), Tony Swai (wa pili kushoto), na Mkurugenzi wa Maendeleo wa Kampuni ya TICTS, Donald Talawa (kushoto). 
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Ecobank Tanzania, Raphael Benedict (kulia) na Mkurugenzi Mkuu wa TICTS Jared H. Zerbe (katikati) wakibadilisha mikataba ya makubaliano ya kushirikiana katika kuhakikisha wateja wa TICTS wanafanya malipo yao kwa haraka na ufanisi zaidi kupitia tawi lolote la Ecobank hapa nchini. Mikataba hiyo ilisainiwa jana katika tawi la Ecobank lililopo PSPF Towers jijini Dar es salaam. Anayeshuhudia kushoto ni Katibu Mkuu wa Tanzania Freight Forwarders Association (TAFFA), Tony Swai. 





Benki ya Ecobank Tanzania leo imeingia katika ushirikiano rasmi na TICTS, ambapo wateja wa kampuni hiyo wataweza kufanya malipo yao kwa haraka na ufanisi zaidi kupitia tawi lolote la Ecobank. 

Benki hii imeanzisha mfumo ambao utawawezesha wateja wa TICTS kufanya malipo yao papo kwa hapo kupititia mfumo huu rahisi. Huduma hiyo itakuwa inapatikana kwa wateja wa Ecobank na wasio wateja wa benki hii. 

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaaam leo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ecobank, Raphael Benedict alisema benki hiyo inataka kuhakikisha huduma ya uagizaji na utoaji mizigo bandarini katika Bandari ya Dar es Salaam inakuwa rahisi zaidi na ya haraka zaidi kwa wateja wa TICTS. 

Benedict aliongeza kuwa ili kuwezesha jambo hilo, Ecobank Tawi la PSPF ambalo linapatikana karibu na geti la ofisi za TICTS, limeogeza muda wa huduma zake na sasa litakuwa likifunguliwa saa 8:00 asubuhi hadi saa 4:00 usiku kwa siku za kazi, na saa 3:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni kwa siku ya Jumamosi. 

Hata hivyo mipango ya benki hiyo ni kupanua zaidi huduma zake hadi siku ya Jumapili. Kwa maana hiyo, muda ulioongezwa utawawezesha wateja kuwa na wigo mpana zaidi wa kufanya shughuli zao na kukamilisha shughuli za upakuaji wa makontena. 

Alisema kupitia mfumo mpya wa benki wa kidijitali, Eckobank Tanzania imekuwa katika mchakato wa kukamilisha hatua za utoaji huduma kwa saa 24 za malipo kwa wateja wa TICTS. 

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Tanzania International Container Services (TICTS), Jared Zerbe alisema kampuni hiyo imekuwa ikijitahidi katika kuboresha huduma zake ili kuendana na mahitaji ya wateja wake. 

“Tunafuraha sana kuingia ushirikiana huu na Ecobank ambao utatusaidia kuboresha huduma zetu za kila siku. Kwa kuboresha huduma zetu, tumefungua akaunti yetu Ecobank ambapo wateja wataweza kufanya malipo yote ya huduma za TICTS. Pia Benki imefungua tawi jipya jirani na ofisi zetu za TICTS ghorofa za jengo la PSPF pembezoni mwa Barabara ya Sokoine Drive ili kurahisisha utoaji huduma kwa wateja,” alisema. 

“Wateja wetu wanashauriwa kutumia matawi matano ya Ecobank yaliyopo jijini Dar es Salaam kwa huduma za malipo ya huduma mbalimbali za TICTS.” 

TICTS na Ecobank watatambulisha njia mpya ya malipo kupitia mtandao wa simu ya mkononi na vituo vya mauzo kwa pamoja kwa mtindo mwingine wa malipo kupitia Ecobank. Taarifa itatolewa mara mpango huo utakapokamilika. Pia wateja watajulishwa kuhusu sehemu na tarehe ya kuhudhuria semina kwa wateja ili kukuza uelewa kuhusu malipo kwa mtandao na kupunguza usumbufu jinsi ya kutumia huduma za kibenki kwa mtandao.

UKISTAAJABU YA GAGA, NJOO UYAONE YA KIZOTA


Ehhh!! Haya! Na leo naandika tena? Mazoea mengine bana!!  

Ndio, nimeona niandike ujinga wangu ila safari hi naandika kuhusu suala jepesi la wachezaji kuhama timu kubwa moja kwenda timu kubwa nyingine. Hapa nazungumzia Simba na Yanga, aka mapacha Kulwa na Dotto.

Kiuhalisia hili jambo halikuanza leo,limeanza miaka Dahal. Na ukienda katika historia, zamani lilikuwa linakera zaid pengine kupita zama zetu, sababu miaka ya nyuma kabisa, wachezaji walikuwa wakihama upande mmoja kwenda mwingine sababu za kishabiki zaid kuliko sasa, ambapo sababu za kimaslahi zmechukua nafasi kubwa.

Kihistoria mchezaji wa kwanza maarufu kuhama katika  timu hizi ni wajina wangu Haji Omari....Huyu alikuwa sentahafu mahiri sana wa Yanga, lakini akaja kuhamia Sunderland (Simba). Inaarifiwa kwa kitendo chake cha kuhama jinsi kilivyowakera wanayanga,wakaamua kuhakikisha hachezi Simba. Haji akaishia kuuza soda pale Ilala Stadium (Karume).

Baada ya hapo kulikuwa na mtikisiko mkubwa katika  medani ya kabumbu nchini, baada ya anaetajwa kuwa kiungo bora nchini kuwahi kutokea miaka ya 19960  na mwanzoni mwa 1970 ,Gilbert Mahinya kuihama klabu ya Simba na kujiunga na Yanga. Kiungo huyo inatajwa kuwa alinyan'ganywa hadi fenicha alizonunuliwa na Simba,hali iliopelekea kuacha gumzo kubwa nchini. Gilbert anatajwa na mchezaji wa zamani wa Yanga, Pan, Pamba na timu ya Taifa,Mohamed Rishard Adoph, kuwa ndie half back six bora kuwahi kumuona nchini.

Miaka ya 70 suala la kuhama halikuziacha salama klabu hizi. Kwanza kwa kiungo Adam Juma akihama kutoka Simba kwenda Yanga. Huyu alidhihakiwa kuwa alihama Simba kufuata safari ya Yanga iliolikwa kwenda Romania, ingawa baadae nayo Simba ilikwenda nchini Poland kupitia Italy miaka hyo.

Miaka hii pia ilishuhudia kipa bora kupita wote nchini kuwah kutokea Athumani Mambosasa nae akienda Yanga kwa kipindi kifupi, sambamba na namba ten ya Afrika Maulid Dilunga "Eusebio" nae akihamia Simba toka Yanga - ingwa hawa hawakudumu sana na klabu zao mpya.

Mtikisiko kwa miaka hyo ni kwa Ezekiel Greyson "Jujuman",mzaramo wa Kisarawe na baba wa muigizaji mahiri wa filamu Aunt Ezikiel, huyu alihama Yanga kuja Simba. Kiungo huyo aliye mbele ya haki kwa sasa,alichezea Yanga wakati ikipokea kipigo cha kihistoria cha goli Sita kwa bila mwaka 1977. Jujuman alikuwa akicheza kiungo wa ushambuliaji.

Miaka ya themanini haikuwa na vbweka hivyo sana. Zaidi ya Omary Hussein "Kevin Keegan wa Yanga,kama walivyokuwa wakimwita washabiki wao,kuja kucheza Simba mwishoni mwa miaka hiyo. Simba wakambatiza jina la One Ten - aina ya gari zilizokuwa kwenye chati miaka hiyo.

Ila kwa faida ya wasomaji, mwanzoni mwa miaka hyo almanusura katibu mkuu wa sasa wa Yanga,Charles Boniface Mkwasa kujiunga na Simba. Mkwasa au Master kama alivyokuwa akiitwa na wafuasi wake,alishasajili Simba, ila mwenyekiti wa FAT (TFF )wakati huo Mzee Said El-Maamry akampa fursa ya kuchagua timu gani anayotaka kuichezea. Ndipo kiungo huyo mtaratibu akaichagua timu yake anayoishabikia ya Yanga.

Pia full back kutoka Pamba Yusuf Bana nae aliingia katika  mtego kama huo, wakati akihama huko kuja Dar, Bana alijisajili timu zote mbili, ila FAT ikamuidhinisha kuchezea Yanga, hali iliyopelekea kubadilisha jina kwa kuongeza jina Ismail. Akaitwa Yusuf Ismail Bana.

Vurugu hasa zilianza miaka ya 90. Kwanza zikianzishwa na marehemu Syllesaid Mziray kocha msaidizi wa Simba,ambae alijiunga na Yanga katikati ya msimu wa 1990. Tena mara baada ya mechi kali ya mwezi May,ambapo Simba iliibwaga Yanga kwa goli moja kwa sifuri, kwa shuti la yadi 45,toka kwa beki Mavumbi Omari.
Mziray alikuwa kocha wa kwanza rasmi kuhama toka kwa watani hao wa jadi,ambao baadhi ya wasiojua huwaita mahasimu,

Mziray akiwa kocha aliifunga Simba alivyotaka, huku ikichagizwa na mfadhili bepari Abbas Gulamali, ambapo waliifunga Simba mara tano mfululizo, ikianzia kipigo cha 3-1 mwaka huo, kabla ya kuwafunga mara nne tena katika  msimu wa 1991, hadi pale Simba walipoifunga Yanga kule Zanzibar kwenye fainali ya Ubingwa wa Afrika mashariki na kati katika michuano ambayo leo ni Kagame Cup.

Mziray aliweka historia kubwa sana kipindi hicho,ingawa kwa maneno yake mwenyew kwangu miaka ya baadae aliwahi kunitamkia kuwa yeye ni mnazi wa Simba, na kwamba pale alikuwa kazini tu. Super coach Mziray mtaalam wa soka ya matumizi ya nguvu, baadae alirejea kufundisha klabu yake aliokuwa anaishabikia.

Hapa nimtaje Mkuu wa mkoa wa Manyara, kocha Joel Bendera ambae naye aliwahi kuzifundisha timu hizi mbili, lakini yeye akifundisha zaid pale zilipokuwa zikiwakilisha nchi katika mashindano mbalimbali yanayoandaliwa na CAF.


Hapa niwajuze Kocha Bendera akisaidiana na marehemu Ayoub Mohamed,waliiwezesha Simba kuweka rekodi pekee duniani,ya kushinda goli tano bila ugenini,baada ya kufungwa nyumbani goli nne kwa bila,dhidi ya klabu ya Mufurila Wonderes ya Zambia, Kiukweli hii ni rekodi ya dunia. Ingawa sijui kwa nini haijawekwa katika  vitabu vya Guinnes book. Mechi hii ilikuwa ni ya klabu bingwa barani Afrika, na ilichezwa mbele ya Rais wa Zambia wakati huo Dokta Kenneth kaunda aka KK.

Tukiachana na makocha hao,mwaka huo beki mwenye umbile dogo lakini mahiri Deo Njohole au OCD,alivaa jezi ya Yanga huku akiwa mchezaji wa Simba. Deo alivaa jezi hyo siku Yanga ikicheza na Kikwajuni ya Zbar, na alifungiwa kucheza soka baada ya kusajiliwa na timu zote hizo mapacha.

Kivumbi na jasho kilikuwa mwaka uliofata,1991. Simba ilipoteza nyota wake watatu kwa mpigo. Narudia 'NYOTA', Zamoyoni Mogella, Method Mogella, na Hamis Thobias Gaga. Hawa walianza kuichezea Yanga kule Zanzibar kwenye klabu bingwa Afrika mashariki na kati 1992, na katika hali ya kawaida ungedhani Simba ingeyumba. Lakini ajabu haikuwa hvyo. Ikiwatumia nyota wapya kama Hussein Marsha,George Masatu,Mohamed Mwameja, Kasongo Athmani, Fikiri magoso, Damian kimti, Michael Paul, George Lucas, Mnyama aliweza kumfunga Yanga kule Visiwani na kuchukua kombe hilo tena,ambalo walilitwaa mwaka 1991.

Na hapa ndio ule msemo wa watu wa Soka....klabu ni kubwa kuliko mchezaji unapotimia.

Yanga pia ilishawahi kutimua timu nzima mwaka 1976, wakiwemo wazee wangu, Kitwana na Sunday Manara, Maulid Dilunga, Kilambo,Chitete na wengine wengi. Ingawa uamuzi ule uliacha doa na historia mbaya kwao,kwani ndipo walikula 6-0 na kuifanya Simba ichukue ubingwa kwa miaka mitano mfululizo.

Kikosi cha kina Masha na Masatu ndio kilifika fainali ya Caf, medali pekee kubwa katika soka nchini kuwahi kuvaliwa. Wachezaji hao wanaungana na Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu kuwahi kuvaa medali zinazotolewa na Shirikisho la soka Afrika, CAF. Kina Samata wao walivaa medali za ubingwa wakiwa na TP Mazembe ya Congo DRC.

Sina hakika msomaji hadithi yangu kama unajua kukosa huruma ya Rais mstaafu wa awamu ya pili, Alhaji Ally Hassan Mwinyi, wachezaji Kenneth Mkapa wa Yanga, Mwameja na Michael Paul almanusura wafungiwe baada ya kujisajili timu zote mbili!! Hiyo ilikuwa 1993. Lakini mzee Ruksa aliwaombea msamaha kwa waziri wa michezo wakati huo Profesa Philemon Sarungi,ambae aliwaagiza FAT  wawafungulie nyota hao wakubwa kwa kipindi hcho.

Godwin Aswile na Thomas Kipese nao walihama Yanga kuja Simba msimu huo,na walivaa medali hzo za CAF,ambazo ziliwawezesha kujipatia magari aina ya Toyota Corolla toka kwa mfadhili wa Simba wakati huo,Azim Dewji. Simba ni timu pekee nchini kuwahi kuwapa wachezaji wake wote magari kwa mpigo,,jambo ambalo halijawahi kufanywa na klabu yoyote nchini kwa miaka 56 ya uhai wa Taifa hili liliojaa wapiga domo.

Ninazo pia kumbukumbu za kiungo mnyumbufu Athaman China ambae alikuwa nyota wa Yanga,lakini baadae akajiunga na Simba 1994,akitokea Ughaibuni alipokuwa akicheza soka ,

Sololist Dally Kimoko ndio jina la utani alilokuwa akitumia Mwanamtwa Kihwelo, ambae nae kuhama hakukumuacha salama. Yeye alihama msimu wa 1994, Mtwa ni ndugu wa beki mahiri wa zamani wa Simba Mussa kihwelo, na pia Julio au Jamhuri kihwelo, Muhesa na Muhehe ambao nao walikuwa wachezaji walioacha alama nchini. Dally Kimoko yeye alihama Yanga kuja Simba.

Steven Casmir Nemes na Said Mwamba Kizota nao katika msimu wa 1995 wakajiunga na Simba kutokea Yanga. Nimewah kuwapenda nyota wengi kiuchezaji nchini,,ila Kizota na Gaga niliwazimia sana. Miguu yao ilikuwa ni kuliko almasi. Wakati fulani hivi nilikuwa naamini Kizota alikuwa anacheza huku anaweka nta miguuni,ukizingatia anatokea mkoa wenye kuzalisha Asali kwa wingi.

Siku moja miaka ya nyuma kdogo nilikuwa naongea na Charles Boniface Mkwasa kuhusu masuala mbalimbali ya mpira, akaniambia wachanganye Gaga na Kizota, basi hawajamfikia baba yako Sunday hata nusu. Hapo niliogopa kdogo,,lakini majuzi tu Waziri Mwakyembe alimuita Messi wa zama hizo. Nasikitika macho yangu hayakujaaliwa kumuona mzee wangu katika  ubora wake uwanjani. Nilikuwa mdogo mno, ingawa ni mpekepeke wa kuuliza historia na kusoma majarida ya zamani.

Hebu turejee katika  mada kuu. Jina la kocha Nzoyisaba Tauzani walikumbuka? Mrundi huyu nae anaingia kwenye historia ya kuhama, ingawa yeye hakutokea Yanga moja kwa moja kuja Simba, lakini nae hakuachwa salama katika  mkumbo huu maarufu kama iba uibiwe.

Unadhani ntawasahau Edibiy Jonas Lunyamila na Mohamed Hussein Mmachinga? La, Hasha! Hawa nao mwanzoni mwanzoni mwa karne hii nao waliasi toka Yanga kuja Simba. Eddy kwa vigezo vyovyote vile ndio winga bora niliowahi kumuona nchini kwa macho yangu...achana na hao niliohadithiwa, sijui kina Leonard Chitete na Willy Mwaijibe. Lunya kwa macho yangu nimeshuhudia akiwakalisha chini kwa chenga kali mabeki wafuatao,David Mwakalebela, Kassongo, Aziz Nyoni, Said korongo, Deo mkuki, Mohd Mtono na ukitaka hilo nenda kamuulize nahodha wa zamani wa timu ya taifa ya Uganda, Paul Hassule jinsi alivyompindua pindua kama chapati pale Nakivubo Stadium 1993,wakati Yanga ilipotwaa ubingwa wa Kagame cup (ndio linavyoitwa kwa sasa).

Ikumbukwe Yanga walikabidhiwa na mfadhili wao Seti ya TV inch 18, toka kwa marehemu Gulamali, mwaka ambao Simba ilikabidhiwa ndinga mpya toka Toyota.

Ohhh kichwa kimechoka nini? Akida Makunda nae hakubaki salama na iba uibiwe. Huyu bwana alihama Simba kwenda Yanga pia.

Mwaka 1998,Yanga ilipata fursa ya kucheza fainali za ligi ya mabingwa, ikawaazima nyota watatu kutoka Simba, Beki bora wa kushoto nchini Alphonce Modest,  kando ya Mohamed Kajole,Mohamed Chuma, Ahmed Amasha na Kenneth Mkapa, Kiungo mtundu Shaban Ramadhan na mshambulizi aliyecheza miaka mingi zaid ligi ya Tanzania kando ya Kitwana Manara na Madaraka Selemani, Monja liseki.

Kitendo hiki kilichofanywa na Simba ni uungwana bora michezoni kupita kitendo chochote kufanywa katika  historia ya mapacha hao watukutu. Mimi nnaloamini mwakani wakati Simba ikirudi kwenye caf.com, Yanga itawaazima wachezaji Simba, nikiamini Simba itafuzu kwa hatua za makundi, huku wenzetu kama kawaida yao.

Nikimrejea Lunyamila nae ana historia kubwa ya pengine mchezaji pekee nchini kucheza hatua za makundi mara mbili za ligi ya Mabingwa Afrika, akianzia na Yanga 1998, kisha Simba 2003.

Jembe Ulaya na Yusuf Macho iba uibiwe nao haikuwacha,ingawa uhamaji wao ni tofauti kdogo. Huku wote wakija Simba baada ya kutokea nje walikoenda kujaribu kucheza soka la kulipwa,awali walikuwa wakiitumikia Yanga.

Jina kamili la Jembe Ulaya ni Bakari Malima, ambaye ni mpwa wa sentahaf wa kimataifa wa zamani nchini na klabu za Simba na Cosmopolittan Mohammed Bakari Tall. Timu ya pili kuchukua ubingwa baada ya Sunderland (Simba) Cosmo walichukua ubingwa 1967,huku Simba ikiitangulia mwaka 1966.

Kipa bora nchini kwa wakati wake Tanzania one Juma Kaseja au Juma K Juma unamuachaje katika mkumbo huu wa kuwatumikia mafahari hawa wawili nchini,  tena yeye alitoka unyamani kwenda bondeni , au Kiggi Makassi na Amiri Maftah unadhani walibaki salama? au Ephrahim Makoye? hawa nao iba uibiwe iliwakumba. Wote hao walikuwa Yanga baadae wakaja Unyamani.

Au mkumbo huo wa iba uibiwe utawaacha vipi, watu kama, kipa Yaw Berko , Rashid Gumbo, Nurdin Bakar, ambao kwa nyakati tofauti walitoka timu moja kwenda upande wa pili kwa mapacha hawa wawili nchini - Simba na Yanga

Loooh masikini  Athman Iddi 'Chuji' ni kweli anastahili kutokuwemo kwenye ligi kuu nchini kwa sasa? Hebu zifikirie zile pasi zake kama rula zinazogawa uwanja!! ahh yote maisha, ila nae alihama Simba kwenda Yanga na kuna kipindi alirudi Simba kabla ya kurudi alipopapenda zaid,Yanga. Doyi Moki,nae aliwah kuhama Yanga kwenda kudakia Simba.

Wasso Ramadhani, Mrundi aliyekuwa namba tatu mahiri wa Simba nae alihamia Yanga pia, ingawa tunajua ni mnazi mkubwa wa unyamani. Deogratius Munishi Dida, Ally Mustafa Barthez, Kevin Yondan na Kessi nao wote kwa vipindi tofauti waliwah kukipiga na Simba na kwa sasa wapo Yanga.

Kuna na yule Diego wa kiganda, mwe mwe mweh!! Hamis Kiiza!! nae alikuja kucheza Simba akitokea Yanga, ingawa ni dhambi ya kuhitaji utubu kwake kutumia jina hili la Aramando, Sambamba na mwanasoka bora wa kigeni kuwah kucheza nchini Emmanue Okwi. Hawa wote washawahi kuvaa jezi za mapacha hawa, na hapa nimpe heko Okwi aliondoka kwa heshma Simba na anarejea kwa heshma ile ile.

Niliwasahau hata hao??......

Na safari hii Ibrahim Ajibu ambae sijawah kukosa kuamini kuwa ana kipaji halisi cha soka nae kajiunga na Yanga. Ndio binafsi imeniuma kwa kuwa naamini angepata fursa zaidi akiwa Simba, ila mwisho wa siku uamuzi wa maisha ya mtu hufanya yeye mwenyewe, na kwa kuwa Ibra ni mtoto wa mjini sijui kama msomaji umemsikia kasema lolote baya au zuri kuhusu Simba. Hii inampa fursa ya kutochukiwa na wanazi wetu, tofauti na vjana wengine wanaohama huku midomo ikiwa wazi, wanaoshindwa kuweka akiba ya maneno, wakisahau vilabu hivi ni vikubwa na vina rasilimali watu kila pembe ya nchi.

Rai yangu kwa wachezaji ni kuwa binadam kuhama huzuiwi ila uweke akiba. Yasije kukuta kama marehemu Haji Omari. mcheza mpira hupaswi kuwa msemaji, zaidimpira uwe miguuni mwako na sio kinywani. Kazi ya usemaji mtuachie wenyewe, hii ni taaluma kama zilivyo taaluma zenu.

Mwisho
Niwaombe wanazi wenzangu, nimejaribu kuwapa historia hii fupi ili mjue suala la mchezaji kuhama ni jambo la kawaida,limeanza miaka Dahal nyuma,na halitaisha kamwe. Muhimu sisi washabiki tuwe na uvumilivu...Ikitokea kwa Yanga kama ilivyokuwa kwa Simba mvumilie tu, ndio *IBA UIBIWE HYO*,

Bolassie wachangamsha ‘eapoti’



Dar es Salaam. Wakongomani wanaoishi Tanzania, leo wametoa mpya baada ya kuingia Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere wakiwa na vingoma wakiimba nyimbo mbalimbali kwa kile walichosema kumlaki mchezaji wao anayecheza nafasi ya wingi, Yannick Bolasie.
Mashabiki hao walifika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, JNIA wakiwa na basi aina ya Coaster mbili zikiwa zimefunga bendera kubwa ya DR Congo huku wakiimba na kucheza.
Walianza kucheza kwenye lango kuu la kutokea VIP kabla ya kuhamia kwenye kizuizi cha kutokea uwanjani hapo na kuanza kucheza huku wakipiga ngoma na kuimba.
Mmoja wa mashabiki hao aliyejitambulisha kwa jina la Francesca Bazuku alisema kuwa wameamua kumshangilia Bolasie kwa kuwa wanampenda kutokana na soka yake.
“Sisi ni bapenzi ba Ligi Kuu na tunaipendaga Everton kwa kuwa iko na mchezaji wetu anacheza huko, tunampenda Bolasie na Ligi Kuu ya England na hii tunampa heshima kubwa ajue tunamheshimia,” alisema kwa Kiswahili cha Kikongo.

Kumbe mashabiki walijipanga kwa selfie na Rooney


Baadhi ya mashabiki waliofika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere walikuwa wakiwaza kupiga picha za selfie na mshambuliaji wa zamani wa Manchester United, Wayne Rooney.

Mashabiki waliofika JNIA walikuwa wakiuliza kama Rooney yumo kwenye msafara na waliposikia atakuwepo wakaanza kujipanga kwa ajili ya picha.
“Mimi nataka Rooney akitoka nimuombe nipige naye picha yaani hiki ndicho kilichonileta hapa,” alisema shabiki moja akiwa na simu yake ya smart.
Shabiki mwingine alilazimika kumfuata mwandishi wa habari wa Mwananchi na kumuuliza kama kuna uwezekano wa kupiga picha na wachezaji wa Everton, lakini hakukuwa na nafasi hiyo.
Baada ya wachezaji kuwasili, hata waandishi wa habari hawakuwa na nafasi ya kuzungumza na wachezaji zaidi ya kuwekewa mpaka wa kufanya kazi na zaidi ilikuwa kwa wapigapicha waliokuwa wakiwavuta kwa lenzi kwani hawakupewa hata nafasi ya kuwasogelea.
Wakati basi lililokuwa na wachezaji lilipokuwa linatoka, simu zaidi ya 100 zilikuwa juu kurekodi ujio wa wachezaji hao wakitoka uwanjani. Mashabiki lukuki walikuwa nje la lango japo kushuhudia tu ujio huo.