Thursday, September 28

Madiwani wavutana Dodoma


Dodoma. Mvutano umeibuka katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Manispaa ya Dodoma baada ya baadhi ya madiwani kubishana iwapo kikao ni cha dharura au maalumu.
Mabishano hayo yametokea baada ya sekretarieti kusoma ajenda mbili za kupokea taarifa ya ufungaji wa hesabu za mwaka na kupokewa mali za iliyokuwa Mamlaka ya Ustawishaji wa Makao Makuu ya Mji wa Dodoma (CDA).
Diwani wa Majengo (CCM), Mayaomayao Msinta amesema alipokea barua ya mwaliko kuwa ni kikao maalumu lakini walipofika wameambiwa ni cha dharura.
"Mtuambie ni kikao gani, maalumu au cha dharura? Barua inaeleza kikao maalumu lakini hapa tumesomewa ajenda mbili na kikao cha dharura kina kanuni, huwa na ajenda moja tu," amesema.
Diwani wa Nzuguni (CCM), Alloyce Luhega amesema makabrasha wamepewa leo Alhamisi asubuhi, hivyo itakuwa vigumu kujadili na kutoa mapendekezo kwa manufaa ya watu waliowachagua.
"Mimi nimepata taarifa leo asubuhi ni vigumu kujadili kwa sababu hatujasoma," amesema.
Akijibu hoja hizo, katibu wa baraza ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Dodoma, Godwin Kunambi amesema kikao hicho ni matokeo ya maazimio ya vikao vya mabaraza yaliyopita ambavyo viliamua kuwa baada yakupokewa mali za iliyokuwa CDA wapatiwe taarifa.
"Nawaomba tuendelee na kikao maana hata mkiuliza maswali hamtapata majibu maana sisi tumekabidhiwa. Isipokuwa tumepewa mapendekezo ya namna ya kutoa huduma kwa wananchi bila kukwama," amesema.
Amesema kuna watu walianza kulalamika kuwa manispaa imeanza kufanya kazi za iliyokuwa CDA kabla ya kukabidhi taarifa.
Amesema walilazimika kufanya baadhi ya kazi za iliyokuwa CDA ili kuondoa usumbufu kwa wananchi waliokuwa wakihitaji huduma.
Meya wa Manispaa ya Dodoma, Profesa Davis Mwamfupe amewasihi madiwani kuwa na busara katika kujadili jambo hilo.
Mvutano huo umemalizwa kwa kikao kuendelea baada ya madiwani kupiga kura. Madiwani 43 kati ya 46 wameridhia kikao kiendelee.

Jaji Manento: Nimeamua kukaa kimya kwa sababu ni mstaafu

Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Haki za Binadamu

Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji Amiri Manento 
Dar es Salaam. Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji Amiri Manento amesema asingependa kuwa mzungumzaji katika vyombo vya habari.
Jaji Manento amesema ameamua kukaa kimya kwa sababu yeye ni mstaafu katika nafasi yake.
Kauli hiyo ameitoa siku chache baada ya Rais John Magufuli kuwapiga kijembe wastaafu, akisema kuna baadhi yao wanaowashwa washwa kuzungumza kwenye vyombo vya habari.
"Ujumbe uliotumwa kwangu (kuwa mgeni rasmi) sijui niliuonea aibu... nikakubali lakini nilikuwa nimeamua nisiongee siku hizi sababu mimi ni mstaafu," amesema Jaji Manento leo Alhamisi jijini hapa wakati wa mkutano wa siku ya kimataifa ya kupata taarifa.
Hata hivyo, amewataka watendaji wa Serikali kuhakikisha kanuni za Sheria ya Haki ya Kupata Taarifa ya 2016 zinapatikana mapema ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa kwa wananchi.
"Haki ya kupata taarifa ni haki inayotakiwa kulindwa kwa nguvu zote, ni kiashiria kimojawapo cha Serikali yenye uwazi, kwa hiyo watendaji wa serikali wahakikishe wanashiriki kufanikisha uandaaji wa kanuni za sheria hiyo ili isaidie kuongeza uwazi na uwajibikaji," amesema.

Pingamizi la utetezi lazua mapya kesi ya mmiliki Lucky Vincent


Arusha. Kesi inayomkabili mmiliki wa Shule ya Lucky Vincent, Innocent Moshi na makamu mkuu wa shule hiyo, Longino Mkama imekwama kusikilizwa katika Mahakama ya Wilaya ya Arumeru.
Hatua hiyo imetokana na hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Desdery Kamugisha kuutaka upande wa Jamhuri kurekebisha hati ya mashtaka.
Awali, wakili wa utetezi, Method Kimomogoro aliweka pingamizi katika kosa la kwanza na la tatu yanayomkabili Moshi akidai hayana msingi wa kisheria.
Akisoma hati ya mashtaka mahakamani, Wakili wa Serikali, Alice Mtenga alitaja makosa manne yanayomkabili Moshi la kwanza likiwa ni kuruhusu gari aina ya Toyota Rossa kubeba wanafunzi bila ya kuwa na kibali. Kosa la pili ni kuruhusu gari kutembea barabarani bila kuwa na bima.

Mtenga alisoma kosa la tatu dhidi ya Moshi kuwa ni kushindwa kuwa na mkataba wa kazi akidaiwa Juni Mosi akiwa mmiliki wa gari hilo, alishindwa kumpatia mkataba wa kazi dereva Dismas Gasper na kosa la nne ni kuzidisha abiria 13 kwenye gari lililowabeba wanafunzi wa Shule ya Lucky Vincent.
Upande wa mashtaka ulimsomea Mkama shtaka la kuruhusu gari kubeba abiria kinyume cha sheriaakiwa msimamizi  wa shule hiyo.
Wakili Kimomogoro amesema kosa la kwanza dhidi ya Moshi halina msingi wa kisheria kwa kuwa hati ya mashtaka haijafafanua kwa kina endapo biashara hiyo ilikuwa ni ya kukodi au ujira. Kwa kosa la tatu amedai hati ya mashtaka haikutaja kifungu cha kanuni ya adhabu ambacho kimekiukwa.
Baada ya pingamizi, hakimu Kamugisha alitoa nafasi kwa upande wa Jamhuri kuzungumzia pingamizi hilo, ndipo Wakili wa Serikali Khalili Nuda aliposimama na kukiri katika kosa la kwanza hawakuainisha maneno kukodi au ujira lakini hilo halizuii hati ya mashtaka kutopokewa
Nuda amedai katika kosa la tatu kuwa, kesi ndiyo inaanza kusikilizwa mahakamani, hivyo upande wa Jamhuri bado unaweza kupewa muda wa kurekebisha hati ya mashtaka. Ameiomba Mahakama iwapatie muda kwa kuwa walikosea.
Hakimu Kamugisha ametoa uamuzi akikubaliana na hoja za pingamizi zilizotolewa na upande wa utetezi.
Ametoa amri kwa Jamhuri kwenda kufanya marekebisho katika hati ya mashtaka. Ameahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 6.

Gari la Mbowe lazua utata Nairobi

Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (KUB),

Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (KUB), Freeman Mbowe 
Dar es Salaam. Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema kimesikitishwa na hatua ya uongozi wa Bunge la Tanzania ya kulichukua gari la Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni (KUB), Freeman Mbowe alilokuwa akilitumika kwa shughuli za matibabu ya Tundu Lissu jijini Nairobi .
Chadema imesema Mbowe ambaye ni Mbunge wa Hai, aliamuru gari hilo lipelekwe Nairobi kwa ajili ya kusaidia matibabu ya Lissu ambaye ni mwanasheria mkuu wa chama hicho
Lissu ambaye pia Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), alishambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi Septemba 7 akiwa nyumbani kwake Area D mjini Dodoma na yuko Nairobi kwa matibabu.
Mkuu wa Idara ya Uenezi  Chadema, Hemed Ali  ameeleza hayo leo Alhamisi wakati akizungumza na Mwananchi kwa njia ya simu na kwamba hawana wasiwasi na hatua hiyo kwa kuwa wana marafiki wengi wakiwamo Watanzania waishio nchini humo na Wakenya wenyewe ambao kwa namna moja au nyingine watashirikiana nao.
Akizungumzia suala hilo Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah amedai kuwa hana na taarifa hizo, ndiyo kwanza anazisikia kutoka kwa mwandishi na alimtaka mwandishi amuulize huyo aliyetoa taarifa kama kweli ametumwa na Mbowe.
“Naomba uumulize aliyesema taarifa hizi je ametumwa na Mbowe? Kwa sababu napata shida Mbowe ni kiongozi pale bungeni na ana wasaidizi wake na haya mambo ni ya ndani ndiyo maana nataka kujua huyu aliyetoa taarifa amezungumza kama nani? Alihoji Dk Kashililah.
“Haya mambo yana taratibu zake za kiofisi naomba niishie hapa. Maana tukiendelea nitakuuliza maswali ambayo utashindwa kuyajibu. Pia na utatakakujua mengi ikiwamo hata posho ya dereva wa Mbowe,” amesema.

Viongozi wa upinzani Kenya wazuiwa kwenye uwanja wa ndege Nairobi

Raila OdingaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRaila Odinga
Kiongozi wa Muungano wa Upinzani nchini Kenya (Nasa) Raila Odinga, ameilaumu Ikulu ya Nairobi ya State House, kwa kuwazuia vigogo wa muungano huo, Kalonzo Musyoka na Moses Wetangula kusafiri kwenda nchini Uganda.
Bw. Odinga amesema kuwa viongozi hao wawili walizuiwa kwenye uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta walipokuwa wakiondoka kwenda nchini Uganda ambapo Bw. Musyoka angekuwa ahutubie mkutano wa sherehe za kufuzu.
Musyoka alikuwa akielekea kwenye chuo cha Uganda Technology and Management ambapo yeye ni chansela.
Licha ya wawili hao kuruhusiwa kuondoka, Bw. Odinga alisema kuwa hiyo isharaya kuzoroteka kwa haraka kwa hali ya kisiasa nchini na mikakati ya kujaribu kuzua hofu nchini.
Kupitia taarifa Bw. Odinga alisema kuwa polisi waliwaambia wawili hao kuwa viongozi wote wa upinzani watahitaji ruhusa kutoka Ikulu ya Nairobi kabla ya kuondoka ndani ya nchi.
"Nasa inalaani jihada za hivi punde ya kuingilia uhuru na kuwahangaisha viongozi wake wakuu," taarifa hiyo ilisema.
Alisema kuwa upinzani utapuuza agizo lolote kwa kuwa viongozi wake hawahitaji ruhusa yoyote ya kusafiri nje ya nchi.
"Upinzani nchini Kenya ni lazima uwe huru kama sehemu ya siasa za Kenya na ni lazima uruhusiwe kuendelea na mikakati yake kama serikali mbadala na sauti ya watu kwa mujibu wa katiba, kwa mujibu wa katiba." Odinga alisema.

Utafiti: Idadi ya watu wazima wanaoambukizwa virusi vya HIV yaongezeka Ulaya

Bernie McDade, 67, living with HIV since 2014Haki miliki ya pichaTERRENCE HIGGINS TRUST
Image captionBernie McDade, 67, ameishi na HIV tangu 2014
Idadi ya watu wazima ambao wanagunduliwa kuwa na virusi vya HIV kote barani Ulaya inazidi kuongezeka, kwa mujibu wa utafiti.
Watafiti kutoka kituo cha kukabiliana na magonjwa cha Ulaya waliangalia matokeo ya vipimo kutoka nchi 31 kati ya mwaka 2004 na 2015.
Waligundua kuwa mwaka 2015, karibu kisa kimoja kati ya visa vipya sita vilikuwa miongoni mwa watu walio na zaidi ya maika 50, ikilinganishwa na kisa kimoja kati ya visa 10 miaka kumi iliyopita.
Uchunguzi huo unazitaja nchi 16 zikiwemo Uingereza na Ujerumani kuwa zile zinazoshuhudia kuongezeka kwa visa vya watu walio na zaidi ya 50 wanaoambukizwa ugonjwa wa HIV.
Utafiti huo uliochapishwa kwenye jarida la Lancet pia uligundua kuwa watu wazima, wana uwezekano wa kupatikana na ugonjwa wa HIV, ambao umefika viwango vya juu ulio vigumu kutibu.
Hata hivyo uchunguzi huo hakuangalia kuhusu ni kwa nini watu wazima wanambukizwa sana na ugonjwa huo. Lakini uligundua kuwa maambukizi ni kupitia mapenzi ya watu wa jinsia moja na kuwa wanaume zaidi wanaambukizwa ugonjwa huo kuliko wanawake.
Uchunguzi huo ulitaka kuwepo hamazisho zaidi na watu kupimwa hasa wale walio na zaidi ya miaka 50.
Vijana bado ndio wengi wanaopata maambukizi mapya ya ugonjwa wa HIV huku zaidi ya watu 300,000 walio kati ya miaka 15 na 49 wakipatikana na ugonjuwa wa hiu kote ulaya katika kipindi cha miaka 12 ya utafiti huo ikilinganishwa watu 54,000 wazee.

Obama atokwa na machozi alipomfikisha mwanawe chuo kikuu cha Harvard

Rais Obama na mwanawe Malia ObamaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionRais Obama na mwanawe Malia Obama
Rais wa zamani wa Marekani Barack Obama amesema kuwa hakuweza kuzuia machozi yake alipomfikisha mwanawe mkubwa Malia katika chuo kikuu.
Ilikuwa kama ''upasuaiji uliofanyika hadharani'', rais huyo wa zamani alizungumzia kuhusu wakati alipomfikisha Malia katika chuo kikuu cha Harvard.
''Nilifurahi kwamba sikububujikwa na machozi mbele yake'', alisema bwana Obama.
''Lakini nilipokuwa nikirudi, maafisa wa jinai hawakuwepo nikaangalia mbele nikijifanya kwamba hawanisikii nikinungunika na kufuta pua yangu.Ilikuwa vigumu''.
Bwana Obama alielezea wakati huo siku ya Jumatatu wakati wa hafla ya wakfu wa Beau Biden. Shirika hilo la kusaidia jamii lilianzisha kwa heshima ya mwana{marehemu} wa aliyekuwa makamu wa rais Joe Biden
''Mwisho wa maisha yetu chochote kile ambacho utakuwa umefanikiwa, ambayo tutayakumbuka ni maisha mazuri ya wana wetu na baadaye kile kitakacholetwa na wajukuu zetu'', alisema Obama.
Malia mwenye umri wa miaka 19 aliamua kujiunga na chuo kikuu cha Harvard baada ya kupumzika kwa mwaka mmoja baada ya kukamilisha elimu ya shule za upili.
Bwana Obama mara kwa mara amekuwa akizungumza kuhusu umuhimu wa kuwa baba kwa wanawe.
''Katika mambo yote ambayo nimefanya nafurahia kuwa baba yenu'',aliwaambia wanawe wakati wa hutuba yake ya miwisho akiwa rais.

NSSF ARUSHA KUWASHTAKI WAAJIRI 126 KWA KOSA LA KUTOWASILISHA MICHANGO YA WAAJIRIWA INAYOFIKIA SHILINGI BILIONI

NA: ANDREA NGOBOLE, PMT

Jumla ya Kampuni 126 zinazodaiwa kiasi cha shilingi bilioni moja pointi tano zinatarajiwa kufikishwa mahakamani wiki ijayo na shirika la Taifa la hifadhi ya jamii NSSF mkoani Arusha kwa kosa la kutowasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa kipindi cha miezi sita iliyopita.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mapema jana meneja kiongozi wa NSSF mkoani Arusha Dr. Frank Maduga amesema kuwa makampuni hayo yamegawanyika kati ya waajiri wakubwa 14 wanaolipia kiasi cha shilingi milioni 50 na kuendelea, wajiri wa kati 69 wanaolipia milioni 5 hadi 49.9 na wale waajiri wadogo 53 wanaolipia kiasi cha shilingi elfu ishirini hadi milioni 4.9 kwa mwezi ambapo jumla ya michango yao inafikia Zaidi ya bilioni moja nukta tano mpaka sasa.

“Waajiri wakubwa wote wamekwisha pelekewa onyo la Mwisho na sasa taratibu za kimahakama zinaendelea hivyo kuanzia jumatatu ya tarehe 2 october 2017 mtawajua ni waajiri gani wameshindwa kutekeleza wajibu wao na kwa kiasi gani wanadaiwa kila mmoja wao” alisema dokta Maduga

Amesema kuwa Mashitaka yatakayokuwa yakiwakabali waajiri hao ni kutowasilisha michango ya wafanyakazi wao kwa wakati na kwa muda unaozidi miezi sita, kitendo hicho kimekuwa na madhara makubwa kwa wafanyakazi na wategemezi wao kwa kukosa huduma za matibabu , fao la uzazi na pia kuna baadhi ya wanachama taarifa zao za kumbukumbu hazioneshi fedha yoyote katika muda ule ambao michango haijawasilishwa na kusababisha taharuki na msongo wa mawazo kwa wafanyakazi husika.

Mwanachama ana haki ya kulipwa michango yake yote akiacha kazi au kampuni ikifa na kuacha kuendesha biashara hulazimika kulipa fedha zote za michango ya wanachama na wao kama taasisi inayosimamia haki za waajiriwa huhakikisha malipo yote yanalipwa na kutolea mfano kampuni za snowcrest na mukidoma zilizositisha shughuli zake na kutangaza kufilisika walihakikisha kuwa kila mfanyakazi anapata mafao yake bila wasiwasi wowote.

Amesisitiza kuwa mwanachama akishaacha kazi atasubiri kwa kipindi cha miezi sita ndiyo aweze kupewa fao la kustaafu na kipindi hiki huwekwa ili kumpa nafasi mwanachama kuweza kutafuta kazi na ama kuajiriwa na kampuni nyingine na changamoto inayowakabili ni kuwa baadhi ya wanachama hufoji barua za kuacha kazi ili waweze kupewa mafao yao huku bado wanafantya kazi jambo ambalo halikubaliki kwa mwanachama kulipwa fao lake huku anafanya kazi.

Naye Straton Simon Afisa msimamizi wa fao la matibabu NSSF kanda ya kaskazini inayowakilisha mikoa ya ARUSHA,KILIMANJARO, TANGA na MANYARA amesema kuwa fao la matibabu hutolewa bure na mfuko huo kwa kila mwanachama anayekuwa amewekewa michango yake kwa miezi mitatu na kuendelea na fao hili halihusiani na kukatwa akiba yako siku utakayostafu kazi au kampuni yako kusimama kufanya kazi hivyo amewataka wanachama wasiwe waoga kutumia fao hili kwani lina faida kwa mwanachama na wategemezi wake wane ambao ni mke au mume na watoto wane.

Amesema kwa Arusha pekee NSSF ina mkataba wa matibabu kwa wanchama wake na hospitali 34 zinazotibu wanachama wote wa hiari na wale waajiriwa ambao mpaka sasa wanafikia 18,400 na kwa kanda nzima ya kaskazini wanafikia wanachama 34000 wanaopata fao hilo la matibabu na kuwasihi wanachama wengine wote wahakikishe wanajaza fomu na kuchagua moja ya hospital ambayo ungependa kutibiwa kati ya hizo hospitali 34 ili wanufaike na fao hilo muhimu kwa maisha ya mwanachama.



 Meneja kiongozi wa NSSF mkoa wa Arusha katikati Dr. Frank Maduga akizungumza na waandishi wa habari juu ya kuwapeleka waajiri 126 mahakamani kwa kosa la kutowasilisha michango ya waajiriwa inayofikia kiasi cha shilingi bilioni moja nukta tano kwa kipindi cha miezi sita sasa. 

MARUFUKU SHULE MKOANI SINGIDA KUNUNUA CHAKI NJE YA MKOA-RC NCHIMBI

Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi amepiga marufuku Shule zote Mkoani Singida kuagiza chaki nje ya Mkoa kwakuwa kuna viwanda vinavyozalisha chaki bora mkoani hapa.

Dkt Nchimbi ametoa katazo hilo mara baara ya kufanya ziara katika viwanda viwili vinavyozalisha chaki katika halmashauri ya Itigi na kushuhudia chaki yenye ubora ikiwa imezalishwa kwa wingi na ikiwa haijapata soko.

“Hawa wenye viwanda wamejitahidi kuzalisha chaki bora haina vumbi na inauzwa kwa bei sahihi lakini shule zetu badala ya kuja kununua hapa ambapo ni karibu wanaagiza Dar es salaam na mikoa mingine”, amesema na kuongeza kuwa,

“Yani mnasubiri chaki hii hii iende Dar es Salaam halafu mnainunulia kutoka huko, hii haikubaliki, kuanzia leo shule zote zinunue chaki hapa hapa ili tupunguze gharama pamoja na kuinua viwanda vyetu”.Dkt Nchimbi ameongeza kuwa Mikoa ya Jirani itakayonunua chaki katika Viwanda vya Singida, vitasafirishiwa chaki hiyo bure kama motisha kwa kuunga mkono viwanda hivyo.

Amezitaka halmashauri kushirikiana katika kuboresha mazingira ya utendaji wa viwanda hivyo hasa kwa kuangalia namna ya kuboresha barabara zinazoenda katika machimbo ya jasi yanayotumika kutengeneza chaki kwakuwa wenye viwanda wamekuwa wakilalamikia ubovu wa barabara hizo.

Aidha Dkt Nchimbi ametoa wito kwa wenye viwanda wote nchini ambao wanatumia madini ya jasi (gypsum) katika shughuli zao wasihangaike kutafuta madini hayo bali waje singida kuna viwanda vinatengeneza madini hayo kwa ubora mzuri na bei nzuri.

Amesema viwanda vya kutengeneza jasi Singida vimekuwa vikizalisha madini hayo kwa wingi hivyo wenye uhitaji wa madini hayo kutengenezea chaki, gypusum board POP, wanakaribishwa kununua madini hayo mkoani hapa.

Dkt Nchimbi amewapongeza wenye viwanda hivyo kwa kutumia rasilimali kama madini ya jasi iliyopo Singida kwa kuanzisha viwanda mabavyo vinatengeneza ajira na kukuza uchumi kwa kuwa wao wamekuwa walipa kodi wazuri.

Naye Meneja wa kiwanda cha chaki cha Dober Color kilichopo Itigi Abdul Mahamoud amemshukuru Mkuu wa Mkoa kwa hatua yake ya kukataza kuagizwa chaki nje ya Singida kwakuwa kutaongeza soko ambalo litasaidia viwanda hivyo kukua.

“Mkuu wa Mkoa tunashukuru kwa katazo hilo kwakuwa litafanya viwanda vyetu vikue na kuongeza uzalishaji, lakini pia itafanya viwanda hivi viongeze ajira na hata kodi tunayolipa itaongezeka hivyo kukuza uchumi wa Singida”, amesema Mahamoud.

Ameongeza kuwa kwa sasa kiwanda hicho kinazalisha tani hamsini kwa siku lakini kutokana na katazo hilo matarajio ni kuongezeka uzalisha hadi kufikia tani 200 za chaki kwa siku.



Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akishiriki zoezi la kutengeneza chaki katika kiwanda cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.



Mkuu wa Wilaya ya Manyoni Miraji Jumanne Mtaturu akiwa amebeba ili kuzianika chaki alizotengeneza Mkoa Singida Dkt Rehema Nchimbi katika kiwanda cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.



Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt Rehema Nchimbi akikagua kiwanda cha kutengeneza jasi cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi.



Wafanyakazi wa kiwanda cha Dober Color wakifungasha chaki, Meneja wa Kiwanda hicho amesema sehemu ya kufungasha chaki hiyo inafanywa na wanawake kwakuwa wako makini na haraka.



Mkuu wa Mkoa Singida Dkt Rehema Nchimbi akikagua ubora wa chaki inayozalishwa katika kiwanda cha Dober Color Kilichopo Halmashauri ya Wilaya ya Itigi, kushoto kwake ni Meneja wa Kiwanda hicho Abdul Razak Mahamoud.

SOKO LA BUNJU A LAIBUA MTAFARUKU,DC HAPI ATOA MAAGIZO KWA MKURUGENZI NA MMILIKI KUWASILISHA NYARAKA ZAO UMILIKI


 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Ally Hapi akizungumza na baadhi ya wakazi wa Bunju A mapema leo asubuhi,waliokuwa Wakimsubiri Kumueleza Changamoto zao Mbalimbali zinazowakabili ikiwemo changamoto ya soko la wa Wafanyabishara wa soko la Bunju A ambalo inaelezwa kuwa limechukuliwa na Muwekezaji.

DC Hapi akitoa ufafanuzi wa changamoto mbalimbali zilizowasilishwa na Wananchi hao,ikiwemo changamoto ya eneo la Soko Bunju A,Mh Hapi amesema ametoa siku kumi 14  kwa ofisi ya Mkurugenzi kumletea nyaraka za soko la Bunju A ili ajiridhishe na kutoa maamuzi ya umiliki wa soko hilo kwa wananchi, huku kwa mmiliki anayetajwa kuhodhi eneo hilo  amepewa siku  tatu kuwasilisha nyaraka zake za umiliki.



 DC Hapi akitoa ufafanuzi wa changamoto mbalimbali,ambapo pia ametoa siku kumi 14  kwa ofisi ya Mkurugenzi kumletea nyaraka za soko la Bunju A ili ajiridhishe na kutoa maamuzi ya umiliki wa soko hilo kwa wananchi huku kwa mmiliki anayetajwa kuhodhi eneo hilo  ametoa siku  tatu ampelekee nyaraka zake za umiliki



Baadhi ya Wakazi wa Bunju A wakimsikiliza DC Hapi alipokuwa akizungumza nao mapema leo na kusikiliza matatizo ya wananchi hao ikiwemo pia kuyapatia majibu.



 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe Ally Hapi akisoma baadhi ya mabango yaliyokuwa yamebebwa na wakazi hao wa Bunju A mapema leo asubuhi,yakiwa na jumbe za changamoto zao wakihitaji kutatuliwa



MUHIMBILI YAZINDUA MWONGOZO WA KUWAHUDUMIA WATOTO WACHANGA

 Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) leo imezindua muongozo utakaosaidia kuwahudumia watoto wachanga ( Neonatal Guideline) wenye umri kuanzia siku 0 hadi siku 28 ili kuhakikisha wanapata huduma inayostahiki.

Muongozo huo umeandaliwa na madaktari wa MNH na kupitiwa na wadau mbalimbali wakiwemo wataalam kutoka Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) pamoja na Chuo Kikuu cha Kwazulu Natal kilichopo Afrika Kusini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Profesa Lawrence Museru amesema muongozo huo si tu unamanufaa kwa MNH bali pia una manufaa kwa hospitali zingine kwani utawezesha mtoto kupata tiba inayotakiwa hata sehemu ambazo hakuna watalaam.

Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Watoto Edna Majaliwa ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Watoto Wachanga wa hospitali hiyo amesema kuwepo kwa muongozo huo kutasaidia kupunguza vifo vya watoto wachanga sanjari na kupunguza rufaa za watoto hao kuletwa Muhimbili .



 Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru akizungumza katika uzinduzi wa kitabu chenye mwongozo jinsi ya kutoa huduma ya afya kwa watoto wachanga wenye umri sufuri hadi siku 28. Uzinduzi huo umefanyika leo katika hospitali hiyo.



 Madaktari na wauguzi wakiwa kwenye mkutano wa kuzindua kitabu kinachoelezea jinsi ya kuwahudumia watoto wachanga baada ya kuzaliwa.



  Daktari wa watoto wa hospitali hiyo, Dk. Judith Cosmas ambaye ameshiriki kuaanda kitabu hicho akizungumza kwenye mkutano huo.



 Baadhi ya wataalamu wa afya wakiwa kwenye mkutano huo leo.



 Mkuu wa Idara ya Watoto, Dk. Merry Charles akisisitiza jambo huku akionesha kitabu hicho ambacho kitakuwa kikitumika wakati wa kuwahudumia watoto hao.

ENSOL YACHAGIZA KAULI MBIU YA SERA YA VIWANDA KWA WANANCHI WA KIJIJI CHA MPALE WILAYANI KOROGWE


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,Dkt Juliana Pallangyo akizundua mradi huo 



Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,Dkt Juliana Pallangyo kushoto akipata maelezo ya mradi huo mara baada ya kutembelea kwenye eneo la mtambo huo kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga,Mhandisi,Robert Gabriel.



Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,Dkt Juliana Pallangyo akishiriki kucheza ngoma ya wananchi wa Kijiji hicho mara baada ya kuzinduaa mradi huo 



NI ukweli usiopingika utekelezaji wa sekta ya viwanda inahitaji
nishati ya umeme katika shughuli zake mbalimbali ikiwemo za uzalishaji mali ili kuweza kupata mafaniko yanayoweza kusaidia kuinua uchumi wao.

Kwani bila kuwepo kwa nishati hiyo kwa baadhi ya maeneo hasa vijijini kuna pelekea kushindwa kufikia malengo yao kwa kuongeza uzalishaji wa bidhaa mbalimbali kwa kuhofia iwapo zitakaa muda mrefu zitaharibika.Licha ya hivyo lakini pia kukosekana kwa nishati hiyo kuna sababisha watanzania wenye nia ya kuanzisha viwanda vidogo vidogo kukwama kufikia malengo yao waliojiwekea kwa kuvianzisha.

Kufuatia kuwepo kwa changamoto hiyo, Shirika la Umoja wa Mataifa la Mfuko wa Mitaji na Maendeleo (The United Nations Capital Development Fund –UNCDF) kwa kushirikiana na kampuni ya Ensol Tanzania Limited waliamua kuanzisha mradi wa umeme wa jua (sola) kwenye kijiji cha Mpale Kata ya Mpale wilayani Korogwe Mkoani Tanga.

Mradi huo ambao umekuwa mkombozi mkubwa kwa wananchi wa Kijiji hicho umefadhiliwa na Shirika hilo ambao umelenga kuwasaidia kuondokana na changamoto ambazo zilikuwa zikiwakabili ikiwemo kutumia vibatari wakati wakienda kujifungua kwenye zahanati ya Kata hiyo.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mradi huo,Diwani wa Kata ya Mpale Tarafa ya Bungu wilayani Korogwe Mkoani Tanga,Shemakao Miraji anasema mradi huo ni faraja kubwa kwa wakazi wa Kijiji hicho na maeneo jirani ikiwemo kufungua fursa za kiuchumi lakini kuendana sanjari na kauli mbiu ya serikali ya viwanda.

Anasema awali walikuwa wakilabiliwa na changamoto kubwa ya wakina mama wajawazito kwenda kujifungulia kwenye zahanati hiyo kwa kutumia vibatari jambo ambalo lilikuwa ni hatari kwa maisha.

Diwani huyo anasema faida kubwa za mradi huo utasaidia kuboresha huduma za afya kwa wakina mama ambao walikuwa wakienda kwenye vituo vya afya kwa kutumia vibatari lakini baada ya kufika umeme huo utawasaidia kuondokana na kadhia hiyo ambayo ilikuwa ni hatari kwa maisha yao ambao ni nguvu kazi kuelekea uchumi wa viwanda.

"Kilio kikubwa cha wananchi wetu hapa ni maembe yanayoanguka na kuoza ha hatuwezi kupata namna nyengine ya kuweza kutuepusha na adha ya kuondokana nayo na hii itatusaidia kuondokana na dhamana hiyo lakini pia umeme huu utatusaidia kuingia kwen ye uchumi wa kati kwa kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya chai na kukuza zao hilo"Anasema.

Naye kwa upande wake,Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini,Dkt Juliana Pallangyo anawapongeza kampuni hiyo na washirika wa kiufundi TTA kwa juhudi walizofanya kuchagua kijiji hicho kufanya utafiti,kubuni mradi huo kwa kutafuta fedha na kutafuta taratibu zote katika kutekeleza mradi huo huku akiwataka wananchi kuanzisha viwada vidogo vidogo.

“Katika kutafuta fedha nafahamu Ensol ilifanikiwa baada ya kushindwa nishwa na makampuni mengine kwani taasisi hizi zilizotajwa zinatoa fedha kwa mtindo wa ushindani na wanapokea maombi mengi ya ufadhili kutoka maeneo mbalimbali ya dunia na Afrika “Anasema

“Lakini pia nimefurahishwa na zaidi na huduma kadhaa zilizotolewa na mradi kwa jamii hii hapa kwanza kuwawezesha wananchi kuunganishwa na umeme ikiwemo kufanyiwa wayaringi kwa mkopo “Anasema.

Anasema ni kweli katika maeneo ya vijijini huduma ya umeme imefika lakini wananchi wengi wanashindwa kuunganishwa na umeme kwa sababu gharama ya kutandaza nyaya kwenye nyumba zao.

“Tunawashukuru sana Ensol kwa kufikiria kutatua changamoto hii na pia tunawashukuru Power Africa kwa kuunga mkono jambo hili kwa kutoa fedha na naamini wananchi wa hapa mpale watatumia fursa ya umeme ambayo sio rahisi kupatikana kuunganishwa nayo “Anasema.

“Lakini pia ni kwamba nishati hii ya umeme itapatikana kwa saa 24 kwa siku 7 za wiki bila kukatika hii ni habari njema kwa watumiaji wa umeme kwani iwapo huduma hiyo itakosekana bado ni changamoto hata maeneo ya mijini “Anasema.Anasema ni jambo jema kusikia kuwa hapa kwenu masuala ya mgawo wa umeme kukatika itakuwa ni suala la kusikia kwa wengine na huo ndio uzuri wa kutumia teknolojia ya umeme wa Jua.

“Pamoja na hayo lakini niwahamasishe wananchi wa hapa mpale kutumia vizuri uwepo wa nishati hiyo kwa kuanzisha shughuli za uzalishaji mali ikiwemo kuanzisha viwanda vidogo vidogo na miradi itakayoweza kuwaingizia fedha ili kujikwamua kiuchumi”Anasema.

“Msiishie kupata mwanga tu bali tumieni pia fursa hii kuanzisha 
biashara na miradi itakayowaingizia fedha kwani umeme huu unatosha kuanzisha viwanda vidogo vidogo kama vinu vya kusagia nafaka ,mashine za useremala na kutengeneza samani “Anasema.

Anasema kwa kufanya hivyo wananchi wa kijiji hicho watakuwa wameendana sambamba na mwamko mpya wa Tanzania ya Viwanda ambao utafungua fursa kubwa za kiuchumi kwao.

Naibu Katibu huyo anasema kupitia huduma hiyo ni matumaini yake huduma za afya zitaboreka zaidi kijijini hapo kwani wananchi wengi wa maeneo ya jirani watakwenda kupata matibabu kwao kutokana na uwepo wa uhakika wa kutibiwa muda wote kunakosababishwa na nishati ya umeme.

“Nawaombeni halmashauri pamoja na serikali ya kijiji kujipanga 
kuhakikisha umeme unaotumika unalipiwa kadri inavyotakiwa kila mwezi kwani haipendezi kuona nishati hiyo ipo lakini zahanati inakosa huduma hiyo kwa kushindwa kilipia “Anasema.

“Lakini pia nikuombe Mkurugenzi wa Halmashauri ya Korogwe pamoja na uongozi wa kijiji mjipange hata kwa kutumia fedha mtakazookoa kutoka kwenye manunuzi ya mafuta ya taa na gesi kwa ajili ya jokofu la madawa muweze kulipia umeme “Anasema.

“Serikali sasa kupitia wakala wa Nishati imezindua rasmi mpango wa tatu wa kusambaza umeme maeneo ya vijijini na tumeweka lengo la kufikia vijiji vyote ifikapo mwaka 2022.

Naye, Msimamizi Mkuu wa Mradi huo,Prosper Magali anasema shughuli za mradi huo zilianza rasmi Machi mwaka 2014 baada ya kutembelea kijiji hicho pamoja na vyengine vilivyopo wilayani Korogwe.

Anasema licha ya kutembelea wilaya hiyo lakini pia walitembelea maeneo mengine Tanzania kutafuta vijiji na maeneo yanayofaa kwa miradi ya uzalishaji mdogo wa umeme kwa kutumia teknologia ya umeme wa Jua.

Aidha anaeleza waliamua kuanza mradi wa mfano katika kijiji hicho baada ya kuwa kijiji bora kwa vigezo walivyoweka vya kiuchumi, kijamii na kimakjazi ukilinganisha na vyengine walivyotembelea.

“Shughuli ya mradi zilifuatiwa na zoezi la kufanya upembuzi yakinifu, Mpango wa kibiashara (Bussines Plan) pamoja na makadirio ya kiufundi mambo ambayo yalitusaidia kuandaa nyaraka za kuwasilisha kwa wafadhili na wawekezaji mbalimbali “Anasema.

“Baada ya hapo mmwaka 2014 mwishoni, Taasisi ya Energy and Environment Partnership (EEP) Program yenye makao yake makuu huko Pretoria nchini Afrika kusini inayopata ufadhili wa Serikali za Finland, Uingereza na Austria kupitia mpango wake wa kutoa ufadhili wa miradi ya nishati endelevu kwa nchi za kusini na mashariki ya Africa kwa mtindo wa
ushindani “Anasema

“June 10 mwaka 2015 tuliweza kusaini makubaliano rasmi ya EEP ya ufadhili wa miaka miwili wa mradi huu uliokuwa na thamani ya Euro 263,000 ikiwa ni asilimia 63 ya gharama za mradi “Anasema.

Anaongeza kuwa bado wanaendelea na zoezi la kutafuta fedha zaidi za kutekeleza mradi huo lakini kwa bahati nzuri baada ya mazungumzo ya muda mfupi, Taasisi ya Umoja wa Mataifa ya Maendeleo ya Mitaji (United Nations Capital Development Fund ya UNCDF).

Anaeleza kufuatia mazungumzo hayo taasisi hiyo ilikubali kutoa asilimia 22 ya gharama za mradi USD 124,000 na walitiliana saini ya makubaliano ya ufadhili wa fedha hizo Novemba mwaka 2015.


Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha.