Sunday, August 20

Idadi ya watu waliouawa kwenye maporomoko ya ardhi DRC kuongezeka hadi 200

map
Image captionIdadi ya watu waliouawa kwenye maporomo ya ardhi DRC kuongezeka hadi 200
Idadi ya watu ambao wameuawa kufuatia mkasa wa maporomoko ya ardhi kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, huenda ikapanda hadi kufikia watu 200, maafisa wamesema.
Watu ambao walikufa ni kutoka jamii ya wafugaji katika ziwa Albert.
Maafisa wanasema kuwa idadi hiyo ni kutokana na idadi ya familia zilizofukiwa baada ya mvua kubwa kusababisha sehemu za mlima ulio karibu kuporomoka.
Matumaini ya kuwapata manusura yamedidimia wakati waokoaji wakiwa hawana njia za kuondoa mawe makubwa.
"Kuna watu wengine zaidi waliofukiwa ambao hatuna uwezo wa kuwakoa," naibu gavana wa mkoa wa Ituri aliliambia shirika la Reuters.
Milima nayo inasababisha eneo hilo kutofikika kwa urahisi.
Sehemu nyingi za magharibi na kati kati mwa Afrika zinakubwa na maporomoko ya ardhi kwa sababu miti imekatwa sana na jamii zimesongamana kwenye maeneo yaliyo chini ya milima.
Mashariki mwa Congo ni eneo ambalo pia hukumbwa na mitetemeko ya ardhi.
Zaidi ya watu 400 wameuawa huku 600 wakiwa hawajulikani waliko baada ya janga kama hilo kuikumba Sierra Leone.

Grace Mugabe arudi Zimbabwe licha ya kutafutwa na polisi Afrika Kusini

Haijulikani ikiwa serikali ya Afrika Kusini ilimpa Bi Mugabe kinga ya kidiplomasia.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionHaijulikani ikiwa serikali ya Afrika Kusini ilimpa Bi Mugabe kinga ya kidiplomasia.
Vyombo vya habari nchini Zimbabwe zinasema mkewe rais Mugabe, Grace Mugabe amerejea nyumbani kutoka Afrika kusini licha ya kukabiliwa na mashtaka ya kushambulia mwanamitindo Gabriella Engels katika hoteli moja Johannesburg.
Inaeleweka kwamba Grace Mugabe alisafiri pamoja na mumewe leo asubuhi.
Wawili hao walikuwa wanahudhuria mkutano wa kikanda Afrika kusini.
Haijulikani ikiwa serikali ya Afrika Kusini ilimpa Bi Mugabe kinga ya kidiplomasia.
Mwamitindo Gabriella Engels 20, alimshtumu Bi Mugabe kwa kumpiga baada ya kumpata akiwa na watoto wake wawili wavulana ndani ya chumba kimoja cha hoteli huko Sandton, mtaa mmoja wa kifahari kaskazini mwa mji wa Johannesburg
Mwamitindo Gabriella EngelsHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMwamitindo Gabriella Engels
Bi Engels aliambia BBC kwamba alishambuliwa na bi Mugabe aliyeamini kwamba alikuwa akijua kule aliko mwanawe Bellarmine.
Mawakili wa Gabriella Engels mwanamke ambaye analaumu Bi Mugabe kwa kumgonga, wanasema kuwa mteja wao alipewa pesa kuachana na kesi hiyo lakini akakataa.
Bi Engels, alionekana kwenye mkutano wa waandishi waahabari siku ya Alhamisi akiwa na bendeji kubwa kwenye uso wake.
Grace Mugabe alikataa kufika mahakamani baada ya kushtakiwa wiki jana, akisema kwamba ana kinga ya kidiplomasia.
Mamalaka za Afrika kusini zimekanusha madai kwamba Grace Mugabe ana kinga ya kidiplomasia.

Mwanamume mchina alipia sahani 5000 za chakula baada ya kupata pete ya mpenzi wake iliyopotea

Watu wapanga mlolongo kupata chakulaHaki miliki ya pichaTENCENT NEWS
Image captionWatu wapanga mlolongo kupata chakula
Mwanamume mmoja nchini China alilipia sahani 5000 za chakula kwenye mji ulio kusini magharibi mwa nchi wa Chongqing, baada ya pete aliyokuwa ampe mpezi wake na iliyokuwa imepotea kupatikana.
Kulingana na gazeti Chongqing Morning Post, mwanamume huyo kwa jina Wang, alikuwa na nia ya kumshangaza mpenzi wake kwa kumuomba akubali kumuoa, baada ya kuchumbiana kwa mwaka mmoja.
Alikuwa amefanya maandalizi ya mpango huo lakini wakati alipokuwa akipata chakula cha mchana, ghafla aliondoka kwenye kiti chake kwenda kupokea simu.
Aliporudi alipata kuwa mkoba wake uliokuwa na pete ya almasi yenye thamani ya dola 44,900 ulikuwa umetoweka.
Lakini kwa bahati nzuri mfanyakazi mmoja wa mkahawa aliupata mkoba huo na kuukabidhi kwa meneja Yue Xiaohua ambaye baadaye aliurejesha kwa Bwana Wang
Bwana Yue aliambia gazeti la Chingqing Morning Post, kuwa bwana Wang alirudi kwenye mkahawa huo siku iliyofuata na kuuliza kuwa ni sahani ngapi za chakula walikuwa wanauza kwa siku.
Kisha akalipa jumla ya dola 5,200 sawa na sahani 5000 za chakula akisema kila mtu aalikwe ili apate chakula.
Gazeti hilo pia lilisema kuwa bwana Wang aliandika barua ya kushukuru mkahawa huo akisema kuwa mpenzi wake aliikubali pete hiyo.

Rais Buhari awasili nyumbani baada ya miezi mitatu London

Rais Buhari awasili nyumbani baada ya miezi mitatu LondonHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais Buhari awasili nyumbani baada ya miezi mitatu London
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari, amewasili nyumbani katika mji mkuu Abuja, baada ya likizo ya matibabu ya miezi mitatu mjini London.
Buhari amekuwa akiugua ugonjwa usiojulikana.
Wafuasi waliimba na kucheza densi walijipanga kwenye barabara za mji, ambapo maafisa wa ngazi za juu serikalini walikusanyika kumkaribisha Buhari.
Haijulikani ikiwa Buhari atarejea shughuli zke kamili kama rais.
Amefanya safari ya kupata matibabu London mara tatu tangu mwezi Juni mwaka uliopita.
Anatarajiwa kuhutubia taifa siku ya Jumatatu asubuhi. Kumekuwa na maandamano ya kumtaka Buhari arudi nyumbani au ajiuzulu.

Teknolojia huchangia wanaume kuwafanyia ukatili wanawake


Umeshawahi kurudi nyumbani ghafla watoto wakashtuka na kuzima simu, iPad au runinga na kila mmoja kwenda na njia yake.
Ukikutana na hali hiyo fuatilia kwa karibu kufahamu huwa wanatizama nini, mbali na hiyo kuwa makini pia na katuni, kwa sababu zipo zisizofaa.
Inawezekana walikuwa wanaangalia picha za ngono. Usiache kufuatilia kwa sababu wana umri wa miaka mitano, tafiti mbalimbali zinaonyesha wapo watoto wenye umri usiozidi miaka sita na tayari wametizama picha hizo mara kadhaa.
Wataalamu wa Chuo Kikuu cha Nebraska-Lincoln nchini Marekani, wametafiti tabia ya watoto hususani wa kiume wanaotizama picha hizo wanapokuwa wakubwa.
Utafiti umeangalia uhusiano kati ya kuangalia picha katika umri mdogo na matendo ya uhusiano wa mapenzi baadaye.
Umebaini vijana wa kiume wanaoangalia wakiwa wadogo huwa hawana utaratibu mzuri katika mapenzi na huwachukulia wanawake kama chombo cha kutimiza matakwa yao.
Utafiti huo pia ulibaini vijana hao huwa na tabia ya kutaka kushiriki tendo la ndoa kwa kutumia nguvu na aina mbalimbali za mitindo.
Wamepata uhusiano wa kati ya umri ambapo mvulana anayetizama picha hizo chafu huwa na mtizamo wa ubaguzi wa kijinsia baadaye hususani wa kingono.
“Hujiona wanafahamu kila kitu kuhusu mapenzi, ikiwamo kuwa na asilimia kubwa ya tabia za kupenda kutumia nguvu na namna za kuudhi na kukera wakiwa faragha, ” anasema Dk Bischmann.
Akiuzungumzia utafiti huo mpya uliochapishwa Agosti 3 mwaka huu kwenye tovuti ya Dailymail, Dk Alyssa Bischmann mhadhiri wa chuo kikuu hicho alisema lengo la utafiti lilikuwa ni kufahamu madhara ya awali anayopata kijana anayetizama picha za ngono akiwa na umri mdogo.
Anasema walilenga zaidi kanuni mbili za kufanya ngono ambazo ni kupenda sana tendo hilo au kuwatumia wanawake kwa nguvu anaposhiriki tendo hilo na kutamani wafanye zaidi ya wanachokifanya.
Bischmann na wenzake waliwafanyia utafiti wanaume 330 wenye umri kati ya miaka 18 na 54 katika Chuo Kikuu cha Mid Western, ambacho pia huwa na wataalamu wa afya.
Anasema kila mtu aliulizwa juu ya kujihusisha kwake kwa mara ya kwanza kuangalia picha hizo alikuwa na umri gani na ilikuwa ni kwa makusudi, bahati mbaya au kwa kulazimishwa.
Washiriki waliulizwa mfululizo wa maswali 46 ili kupima uelewa wao na utendaji katika kanuni mbili za kujamiiana na matendo yao ya ukatili dhidi ya wanawake kingono.
Anaeleza asilimia 43.5 walisema waliona picha hizo kama ajali, asilimia 33.4 walisema walitizama kwa hiyari yao na asilimia 17.2 walisema walilazimishwa huku asilimia sita wakikosa jibu.
“Tumegundua vijana wengi walioanza kuona picha hizo mapema wamekuwa na tabia za kutumia nguvu katika mapenzi na kutaka kuona aina na mitindo tofauti, ukilinganisha na walioangalia picha hizo ukubwani, ” anasema Dk.
Dk anafafanua kuwa jibu hilo wamelipata kwa kufuata mtiririko wa mahojiano ya vijana wadogo wa miaka mitano na wakubwa wa miaka 26, ambao kwa pamoja majibu yao yalifanana.
Anataja miongoni mwa majibu yao ni kutotaka kukutana kimwili na wanawake kawaida bila kuonyesha kuwa wao wanaweza.
“Nataka hadi alie, abadilike rangi, avimbe na ikiwezekana siku ya kwanza anichukie kabisa, ” alisema mmoja wa vijana waliohojiwa.
Anasema utafiti huo pia ulibaini mwanaume mtu mzima akitizama picha za ngono kwa mara ya kwanza hutamani kufanya mapenzi na wanawake wengi na kurudi katika umri mdogo.
Mwandishi mwenza wa utafiti huo Chrissy Richardson, anasema hawakutegemea kupata matokeo hayo.
Anasema walichobaini hawakukitegemea kwa sababu walidhani kutizama picha hizo hakutakuwa na athari hasa kwa watoto wadogo, lakini imekuwa kinyume ambapo wamekuwa na athari kuliko wanaume wakubwa.
Anasema hawakudhani kama kuangalia picha hizo kungekuwa na athari katika ushiriki wa ngono halisia.
Watalaamu wanena
Mtaalamu wa saikolojia Dk Theopista Rutayunga anasema kuwa kisaikolojia wanaume wamezaliwa viongozi, hivyo kadri wanavyokuwa wanataka utawala hususani kwa wenza wao.
Anasema hata akiwa na hekima kiasi gani, mpole na msikivu hali ya kuwa mtawala haiondoki, tofauti itakuwa ni jinsi anavyowasilisha utawala wake.
“Kuhusu kuangalia picha za ngono sijafanya utafiti na kupinga au kukubaliana na hao waliofanya, lakini nakubaliana nao kuwa wanaume wanapenda kuwa watawala hususani wanapokuwa na wenzi wao, ” anasema Dk Rutayunga.
Dk Rutayunga anasema watoto ni rahisi kunakili kichwani kitu wanachokiona au kukisikia, ndiyo maana wazazi wanashauri kuwa makini hata katika mazungumzo ya kawaida.
“Kisaikolojia watoto hawana vitu vingi kichwani, hivyo kila kinachopita karibu yao kinaingia kichwani moja kwa moja, mara nyingi akili hupenda kile kinachokatazwa badala ya kinachohimizwa, hivyo inawezekana utafiti wao una ukweli kwa maantiki hiyo.
Naye mtaalamu wa saikolojia Modester Kamongi anasema siyo tu watoto wa kiume, mtoto yoyote akiona jambo katika umri mdogo linamkaa kichwani na kuamini kuwa hayo ndiyo maisha.
Anasema kwa wanaume kutaka kutawala jambo lolote wanalofanya na wenza wao hayo ni maumbile na taratibu zilizopo.
“Unajua saikolojia za wanaume wengi zimeathiriwa na mila na tamaduni, watoto wa kiume wamekuwa wakichukuliwa kama ndiyo ngao kwenye familia, kuanzia urithi, kufanya maamuzi, kusoma na wanapooa pia husisitiziwa jambo hilo, ” anasema Kamongi.
Kamongi anaeleza sababu zote hizo na nyingine nyingi tayari zinampa mwanaume nafasi kubwa kuwa mtawala wa mwenza wake.
“Siwezi kusema sana kuhusu huo utafiti, lakini ninachofahamu mwanaume hawezi kukubali mwanamke amshinde hata kama jambo haliwezi atajitutumua na akishindwa atalipiga vita, ndiyo saikolojia yao ilivyo, ” anasema.

Grace Mugabe akosa kuhudhuria mkutano wa SADC Afrika Kusini

Rais Mugabe na mkuwe GraceHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionRais Mugabe na mkuwe Grace
Mke wa rais wa Zimbabwe Robert Mugabe, amakosa kuhudhudia mkutano wa kanda nchini Afrika Kusini.
Grace Mugabe, 52, anataka kupewa kinga ya kidiplomasia baada ya kulaumiwa kumshambulia mwanamitindo nchini Afrika Kusini wiki iliyopita.
Alikuwa ahudhuria mkutano na wake wa marais kwenye mkutano huo wa SADC
Mamlaka zinasema kuwa anasalia nchini Afrika Kusini wakati ombi lake la kutaka apewe kinga ya kidiplomasia likiendelea kushughulikiwa.
Polisi wanataka kumhoji kuhusu madai hayo.
Polisi wameweka ulinzi mkali kwenye mipaka ya taifa hilo kuhakikisha kwamba Bi. Mugabe hatatoroka.
Image captionGabriella Engels
Mwamitindo Gabriella Engels 20, alimshtumu Bi Mugabe kwa kumpiga baada ya kumpata akiwa na watoto wake wawili wavulana ndani ya chumba kimoja cha hoteli huko Sandton, mtaa mmoja wa kifahari kaskazini mwa mji wa Johannesburg
Bi Engels aliambia BBC kwamba alishambuliwa na bi Mugabe aliyeamini kwamba alikuwa akijua kule aliko mwanawe Bellarmine.
''Tuliendelea kumwambia hatujui aliko...hatujamuona usiku wote...alinikamata na kuanza kunipiga.Nakumbuka nikianguka katika sakafu na damu nyingi katika uso na shingo yangu.Alitupiga akiwa na chuki nyingi'', alisema msichana huyo.

Mshambuliaji aliyewachoma watu kisu Finland aliwalenga wanawake

Vigil in TurkuHaki miliki ya pichaEPA
Image captionMshambuliaji aliyewachoma kisu watu Finland aliwalenga wanawake
Polisi nchini Finland wanasema wanachunguza shambulio la visu lilofanywa jana, katika mji wa Turku kusini mashariki mwa nchi na wanachukulia tukio hilo kuwa la kigaidi.
Watu wawili waliuawa, na wanane wengine kujeruhiwa watatu wakiwa mahututi.
Polisi wamemtambua mshukiwa kuwa kijana wa miaka 18 kutoka Morocco.
Candles are lit at the scene of the stabbings in TurkuHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMshambuliaji aliyewachoma kisu watu Finland aliwalenga wanawake
Plisi wanasema, inaonyesha aliwalenga hasa wanawake, na wanaume aliowashambulia ni wale waliojaribu kumzuia.
Watu wengine wane wamekamatwa, kuhusu shambulio hilo, na amri imetolewa kimataifa, ya kumsaka mtu mwengine wa tano.
Wote wanasemekana kuwa na asili ya Morocco.
A map showing the market square and Puutori in relation to Turku
Image captionMshambuliaji aliyewachoma kisu watu Finland aliwalenga wanawake

Mwanao anautumia muda kiasi gani kwenye vifaa vya kielektroniki?


Tunapozungumzia malezi ya mtoto tunaangazia hatua zote za ukuaji wa mtoto tangu mimba inapotungwa hadi kipindi cha utoto kuisha. Kipindi cha utoto hutofautiana kutoka nchi na nchi; kwa hapa kwetu Tanzania, ni yule aliye chini ya umri wa miaka 18. Kila hatua ya ukuaji ina mahitaji yake na uangalizi maalumu toka kwa mzazi au mlezi.
Kutokana na mabadiliko ya kiteknolojia yanayoendelea kukua kwa kasi, imekuwa ni changamoto kwa wazazi kutimiza majukumu yao ya malezi ipasavyo. Mabadiliko haya yameleta tofauti kubwa katika maisha ya watoto katika hatua zote za ukuaji, hasa katika mazingira na vifaa ambavyo watoto wamekuwa wakitumia kuchezea. Wasiwasi umetanda kwa wazazi juu ya matatizo ya afya ya mwili kwa watoto yatokanayo na vyakula vya kisasa, madhara ya afya ya akili yatokanayo na matumizi ya vifaa vya kielektroniki, midoli na utazamaji wa vikaragosi pamoja na video zenye jumbe hatarishi kwa makuzi ya watoto.
Kabla ya teknolojia kuleta mabadiliko hasa ya mtandao, watoto wengi walikuwa wana muda wa kutosha kucheza nje ya nyumba na kujifunza mengi juu ya asili na halisi ya dunia inayowazunguka. Walicheza michezo ya kuwajenga kiafya na kuchangamsha akili kama kukimbia, kuruka na kucheza mpira na ile ya kuwajenga kiakili na kiubunifu kama vile kutengeneza vifaa mbalimbali kwa kutumia udongo, matope, miti, vitambaa vya nguo, kamba, mifuko, karatasi, sponji na vingine kadha wa kadha vilivyokuwa vikiwazunguka katika mazingira yao.
Kutokana na hali hii, wazazi hasa wa mijini, wamekuwa wakipata changamoto ya namna gani watafanikisha uwiano kati athari za kiteknolojia na malezi bora kwa watoto.
Kuna baadhi wanafikiri kumpatia mtoto vifaa vya kielektroniki vya kuchezea au kuwaacha waangalie televisheni muda wote wanaotaka ni jambo la kawaida na ni kutimiza wajibu. Kwakuwa mara nyingi watoto hufurahia sana vitu hivi kiasi cha kuwafanya watulie na hata waache kulia, kuuliza maswali na kuzunguka nyumba nzima, wazazi hutumia fursa hii kama namna ya kuwatuliza na kuendelea na shughuli zao.
Tafiti iliyofanywa hivi karibuni na madaktari wa watoto nchini Marekani inaonesha kuwa, watoto wa chini ya umri wa miezi 18 hawapaswi kutumia vifaa vyovyote vya kielektroniki; watoto wa chini ya miezi 18 hadi 24 wanapaswa kutumia vifaa hivyo kwa kutizama video au michezo yenye dhima za kuelimisha na dhima hizo zipitiwe na wazazi pia. Miaka 2 hadi 5 wanatakiwa kutumia muda wa saa moja tu kwa siku kutizama luninga au vifaa vingine. Miaka 6 inabidi wasimamiwe na waongozwe kwa ukaribu zaidi juu ya muda wanaoutumia kwenye vifaa vya kielektroniki.
Wazazi wanatakiwa kuwa makini kuhakikisha matumizi ya vifaa vya kielektroniki visiingilie na kuvuruga ratiba ya watoto ya kulala, kupumzika, kucheza, kuhusiana na marafiki, familia pamoja na kujisomea. Kama wazazi, tusibebwe na hisia za mabadiliko ya kiteknolojia tukidhani kuwapatia watoto vifaa vya kielektroniki ndio mapenzi kwa watoto wetu. Ukweli ni kwamba hata watu maarufu duniani tunaowaona wakitumia mtandao, wana taratibu za kudhibiti matumizi ya mtandao yaliyopitiliza kwa watoto wao. Jarida la US Magazine linatutaarifu kuwa familia za watu maarufu kama ya mtoto wa mfalme wa ulaya Prince William, Kourtney Kardashian, Jennifer Lopez na wengine wengi huwapa watoto wao dakika 30 tu za kuangalia video na michezo kwenye vifaa vya kielektroniki katika siku za wiki na dakika 60 tu katika siku za mwisho wa wiki huku wakitumia muda mwingi kucheza, kufurahi na marafiki, wazazi na familia pamoja na kujisomea.

Jinamizi la talaka linavyotafuna ndoa za Watanzania


Ndoto za wanandoa wengi wanapooana huwa ni kuishi pamoja hadi kifo kinapowatenganisha. Vivyo hivyo, wazazi wao, ndugu na jamaa hupenda kushuhudia wanandoa hao wakifanikiwa katika safari ya maisha yao ikiwamo kuwa na familia imara yenye watoto wenye afya bora.
Hata hivyo, siyo wanandoa wote hutimiza ndoto hizo. Kasi ya wanandoa nchini kupeana talaka imeongezeka mara mbili ndani ya miaka sita ya hivi karibuni, jambo linalotishia mustakabali wa ‘taasisi’ hiyo muhimu kwa maisha ya binadamu.
Utafiti wa kufuatilia kaya Tanzania (National Panel Survey) wa mwaka 2014/15 uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) unaonyesha kuwa kiwango cha talaka kimeongezeka kutoka asilimia 1.1 mwaka 2008/09 hadi asilimia 2.1 mwaka 2014/15.
Hii ina maana kuwa kwa sasa kila watu 100 wenye umri wa kuoa au kuolewa waliopo nchini, wawili wametalakiwa kutoka mmoja mwaka 2008/09. Ikumbukwe kuwa utafiti huo unabainisha kuwa watu takriban 40 kwa kila 100 wanaopaswa kuoa au kuolewa bado hawajaingia kwenye ndoa.
Mbali na talaka, kuna wanandoa takriban wanne kwa kila 100 ambao wametengana, jambo linaloashiria huenda nao wakatalikiana siku zijazo iwapo hawatapata suluhu ya kudumu ya tofauti zao.
Kuvunjika kwa ndoa hizo kunawaweka watoto katika maisha magumu ya kukosa mapenzi ya wazazi wote wawili na hata baadhi yao kujikuta wakiingia mitaani kuwa ombaomba kutokana na kukosa huduma stahiki za malezi.
Wataalamu wa masuala ya saikolojia, takwimu na walimu wa dini wanaonya kuwa mwenendo huu ni hatari kwa mustakabali wa Taifa ikizingatia kuwa ndoa ni moja ya taasisi muhimu za kujenga upendo, amani na mshikamano.
Takwimu zinavyoeleza
Matokeo ya utafiti huo uliochapishwa mwaka huu yanakwenda sanjari na yale ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 yaliyobainisha kuwa watu 715,447 walikuwa wametalikiwa (sawa na watu watatu kwa kila 100) wenye umri wa kuoa au kuolewa.
Mikoa ya Kusini Unguja, Mtwara, Mjini Magharibi, Lindi na Kaskazini Unguja inaongoza kwa kiwango cha talaka huku kiwango kikiwa zaidi ya asilimia nne ambacho ni juu ya wastani wa kitaifa wa asilimia tatu kwa takwimu za Sensa mwaka 2012.
Siyo wote wanaotalakiana mahakamani hupeleka matamko ya talaka kwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita) baada ya takwimu za wakala huo kuonyesha idadi ndogo ya talaka, lakini mwenendo wake unapaa kwa kasi.
Pamoja na kuwa talaka zilizosajiliwa ni chache, Rita inabainisha kuwa zinaongezeka mwaka hadi mwaka kwa kuwa Dar es Salaam pekee zimeongezeka kutoka 106 mwaka 2014 hadi 149 mwaka jana jambo linalosadifu hali halisi iliyotolewa na NBS.
Rita, WLAC zinasemaje?
“Inawezekana kabisa talaka ni nyingi kuliko takwimu zetu kwa kuwa wengi hawaji kusajili matamko ya talaka kutoka mahakamani ili tuwapatie vyeti,” anasema Meneja wa Masoko, Habari na Elimu kwa Umma wa Rita, Josephat Kimaro.
“Tumeanza mchakato wa kuwasiliana na mahakama ili baada ya kutoa tu matamko ya talaka watuletee takwimu zote ili tupate picha kamili.”
Taarifa za Rita zinaonyesha kuwa baadhi ya ndoa zimedumu muda mfupi chini ya mwaka mmoja ikiwamo iliyochukua miezi minane iliyojumuisha kipindi cha mashauriano, kuendesha kesi mahakamani hadi kusajili tamko la talaka Rita. Sheria ya Ndoa ya mwaka 1971 inaeleza kuwa tamko la kutengana au talaka hutakiwa kutolewa na mahakama pekee baada ya kujiridhisha na sababu za wanandoa kufanya hivyo.
Kifungu cha 100 cha sheria hiyo kinaeleza kuwa mahakama haiwezi kusikiliza shauri la talaka kwa ndoa zenye umri chini ya miaka miwili na ili isikilize ni lazima ijiridhishe kuwa kuna mmoja wa wanandoa anateseka kupindukia.
Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) kinaeleza katika kijitabu cha ufafanuzi kuhusu sheria ya ndoa kuwa, “mazoea ya wanandoa kupeana talaka mitaani aidha kwa maandishi au kwa mdomo, hizo si talaka kwa mujibu wa sheria ya ndoa.”
“Ni lazima talaka itolewe na mahakama ili kila haki ya mwanandoa itamkwe bayana,” inaeleza sehemu ya kitabu hicho ya WLAC kilichotolewa mwaka 2013.
Kauli za mwathirika
Mwananchi limebaini kuwa ukosefu wa uaminifu na kubadilika tabia baina ya wanandoa ni miongoni mwa sababu kuu zinazofanya wanandoa kutalikiana.
Esther (siyo jina lake halisi) alitalikiana na mumewe mwaka jana baada ya kubaini kuwa alikuwa amebadilika tabia ikilinganishwa na wakati wa uchumba.
“Zamani alikuwa ananishirikisha kwa kila jambo, msikivu, mpole na mfanyakazi aliyeonekana kuwa baba bora wa familia. Lakini baada ya kuoana alianza kuwa mkali hata kwa vitu vidogo licha ya kumwambia kwa upole,” anasema Esther.
Esther (37) anaeleza kuwa kabla ya kuachana na mumewe waliyeoana baada ya kufahamiana kwa miezi tisa, aliwashirikisha wazee wa karibu, familia zao hadi viongozi wa dini lakini bado mwanaume huyo ‘hakuambilika’ jambo lililosababisha waachane.
“Sikupenda tutalikiane kwa kuwa tuna mtoto mmoja, lakini vitimbi vyake vilifanya maisha yawe ya mateso wakati wote. Angalau kwa sasa napumua na nasikia ameshaoa mke mwingine huenda huyo ndiye aliyekuwa akimsumbua,” anasema.
Viongozi wa dini
Viongozi wa dini ambao hufungisha ndoa na kutatua matatizo yanayowakuta wanandoa wanasema haishangazi kuona talaka zikiongezeka kutokana na kushuka kwa maadili miongoni mwa wanandoa ikiwamo uwapo wa muda mfupi wa wachumba kufahamiana vyema. Mwenyekiti wa Halmashauri ya Baraza Kuu la Kiislamu Tanzania (Bakwata), Sheikh Khamis Mataka anasema kuongezeka kwa talaka ni matokeo ya udhaifu katika taasisi ya ndoa ambayo wahusika wake wanatakiwa wadumu kwa upendo na umoja hadi kifo kinapowatenganisha.
“Kabla ya ndoa unatakiwa uone uliyempata kuwa ana vigezo vinavyotakiwa ikiwamo kujiridhisha tabia na familia yake, uwezo wa kijamii na kama anaweza kuwa mwanajamii,” anasema.
“Bahati mbaya ndoa nyingi kwa sasa ni matokeo ya kukurupuka. Unakuta mwanandoa hajui hata historia ya mwenzie kitu wanachoangalia ni ana mali kiasi gani au anafanya kazi shirika gani.”
Kuingia kwenye ndoa wakati wanandoa wakiwa ‘vipofu’ wa historia ya kila mmoja, kwa mujibu wa Sheikh Mataka kunafanya ndoa ianze kuyumba mara tabia halisi zitakapoanza kujitokeza na kusababisha watalikiane.
Mbali na kutojua historia, Padri wa Kanisa Katoliki, Festo Liheta wa Parokia ya Mtakatifu Kamili ya Kiwalani jijini Dar es Salaam anaongeza kuwa kuongezeka kwa uelewa wa haki za wanawake, kukua kwa kipato miongoni mwa wanandoa na matatizo ya unyumba yanachangia ongezeko la talaka.
Padri Liheta anasema kiutamaduni wanaume wanapenda kutawala, lakini kwa sasa wanawake wengi wanazijua haki zao na hawataki zivunjwe kinyume na wenza wao ambao hawajafikia katika uelewa huo. “Mambo ya kiuchumi yanachangia sana ndoa kuvunjika. Mtu anavyokuwa na uwezo wa kifedha hawezi kukubali kunyanyasika kwa kuwa anaweza kujitegemea tofauti na zamani ambapo akina mama walivumilia kutokana na kipato duni,” anasema Padre Liheta ambaye alifanya utafiti kuhusu kuvunjika kwa ndoa wakati akihitimu Shahada ya Uzamili.
Mbali na masuala ya kipato, padri huyo anasema matatizo ya tendo la ndoa nayo yanachochea ukosefu wa uaminifu hasa pale mmoja anaposhindwa kumridhisha mwenzake.
“Zamani tendo la ndoa lilikuwa kwa ajili ya kuzaa tu, lakini kwa sasa ni pleasure (starehe) hivyo mtu asiporidhika anaenda kutafuta nje. Hapa wanaume wanabidi wajitahidi kuwaridhisha wake zao ili kumaliza mifarakano inayotokana na unyumba,” anasema.
Akifafanua jambo hilo, Sheikh Mataka ambaye ni mwalimu wa dini ya Kiislamu anaeleza kisa cha hivi karibuni alichosuluhisha kilichomhusisha kijana mmoja aliyemkuta mkewe akifanya mawasiliano ya mara kwa mara na mwanaume aliyekuwa na uhusiano naye miaka ya nyuma.
“Pamoja na kumuonya hakusikia. Yule mwanaume anayewasiliana naye alimwambia kuwa ni mwanamke aliyekuwa anamfuata na siyo yeye,” anasimulia Sheikh Mataka akitafsiri kesi hiyo kama mfano wa wanandoa kukosa uaminifu.
NBS yatia neno
Talaka zinazoongezeka kwa kasi haziathiri tu wanandoa husika, bali familia nzima ikiwamo zile zilizozalisha wanandoa.
“Kuongezeka kwa talaka kunahatarisha kuongezeka kwa familia za mzazi mmoja,” anasema Mtakwimu Mwandamizi wa NBS, Abbasy Mlemba . “Watoto wanakosa haki ya kuishi na wazazi wote wawili na hili litaongeza umaskini kwa watoto na kuwafanya wawe ombaomba mitaani, watumikishwe kazi na kuongeza uhalifu na mimba za utotoni.”
Mwarobaini wa talaka
Ili kupunguza tatizo la mifarakano ya awali, Padri Liheta anawasihi wachumba kupeana muda wa kufahamiana vyema kabla ya ndoa ikiwamo kujua asili ya wenza hao, eneo anapotoka kila mmoja, ukoo na wazazi kufahamiana.
Sheikh Mataka anasema uchumi hauwezi kuwa sababu ya wanandoa kutalikiana hivyo watu wanaotaka kuoa au kuolewa wanatakiwa kujitathmini vyema na kuwa na upendo na dhamira ya kweli ya kuingia kwenye ndoa ikiwamo kuwa tayari kuhimili changamoto.
Serikali inasema kuwa inafahamu suala hilo na imeshaanza kutekeleza mikakati ya kulipunguza ili kutengeneza ustawi bora wa familia na Taifa.
Msemaji wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto upande wa maendeleo ya jamii, Erasto Ching’oro anasema wamebaini kuwa mbali na madhara kwa familia, pia ukosefu wa utulivu baina ya wanandoa unapunguza uzalishaji na kurudisha nyuma jitihada za kuelekea nchi ya uchumi wa kati.
“Serikali inataka watoto walelewe na wazazi wote wawili ili kuongeza usalama wao katika kila nyanja ya maisha yao. Hivyo kwenye mpango kazi miaka mitano tumepanga kupunguza kiwango cha talaka kwa asilimia 50 ifikapo mwaka 2021,” anasema Ching’oro.
Katika mpango huo ulioanza kutekelezwa Julai mwaka huu hadi mwaka 2021, Ching’oro anasema wanawashirikisha viongozi wa dini na kimila, asasi za kiraia na maofisa ustawi na maendeleo ya jamii katika utoaji elimu ya uhusiano na ndoa ili kupunguza talaka na ukatili wa wanawake na watoto.

TANZANIA Africa’s Best Safari Country 2017



Tanzania Best Safari Country 2017
THE NETHERLANDS – SafariBookings.com has conducted an in-depth analysis of reviews from safari tourists and acclaimed Africa experts to determine the continent’s best country for safaris. And the winner? Tanzania came out on top – the country is the clear winner and has been awarded our best safari country for 2017.
More than 2,500 reviews were used in this comprehensive research. Contributions came from safari-goers all over the world. And 22 reputable guidebook authors – working for Lonely Planet, Rough Guides, Frommer’s, Bradt and Footprint, who make-up the SafariBookings expert panel – also contributed reviews.

Tanzania is rated the best safari country of 2017

Tanzania with its teeming wildlife and astounding natural beauty on average had the highest scores. The country won only by a slim margin though from Zambia. Interestingly, when the results are broken down, members of the expert panel rated Tanzania the highest while safari tourists had a preference for Zambia.

Ratings for the 8 major safari countries

  • 1.Tanzania
    4.83/5(Experts: 4.77/5 – Users: 4.89/5)
  • 2.Zambia
    4.79/5(Experts: 4.67/5 – Users: 4.92/5)
  • 3.Botswana
    4.75/5(Experts: 4.71/5 – Users: 4.79/5)
  • 4.Kenya
    4.64/5(Experts: 4.47/5 – Users: 4.82/5)
  • 5.South Africa
    4.58/5(Experts: 4.31/5 – Users: 4.86/5)
  • 6.Namibia
    4.44/5(Experts: 4.29/5 – Users: 4.59/5)
  • 7.Uganda
    4.30/5(Experts: 3.89/5 – Users: 4.71/5)
  • 8.Zimbabwe
    4.29/5(Experts: 4.00/5 – Users: 4.57/5)

Tanzania again overall the best safari country in Africa

In 2013 SafariBookings conducted its first-ever review analysis to determine the best country for safaris in Africa. Tanzania won that contest clearly. However, because things change so rapidly in Africa we conducted another analysis in 2017, using new reviews from safari tourists and from the guidebook authors on our expert panel. One thing that hasn’t changed is Tanzania’s popularity, once again voted the best safari country in Africa.
Best country for wildlife
Our analysis also determined that Tanzania was the best country in Africa for spotting wildlife. Given the exceptional wildlife-viewing opportunities in parks such as the superlative Serengeti and the wildlife-rich Ngorogoro Conservation area, this was unsurprising.

What the experts say about Tanzania

  • Tim Bewer From United StatesUS – Author of 10 Lonely Planet guidebooks to Africa, incl. Tanzania
     
    Rating:
    5/5 stars
     
    “Tanzania is home to Serengeti National Park and Ngorongoro Crater; and this fact alone makes a solid case for declaring it Africa’s best safari country.” Full review
  • Kim Wildman From AustraliaAU – Author of 15 guidebooks, incl. Bradt’s Tanzania guides.
     
    Rating:
    5/5 stars
     
    “Tanzania is a wildlife photographer’s dream come true… with one of the world’s largest and wildest animal populations, the country offers some of the best safari opportunities on the continent” Full review
Want to do a safari in Tanzania?

Roadtrip paradise Namibia, the best country for scenic value

Namibia, with its swirling desert sands, pink-granite mountains and famous dune-meets-ocean landscape was overall considered the best country for scenic value. The experts in particular rated Namibia’s remote and rocky scenery highly, although safari-goers thought South Africa was better.
“Namibia is road-trip paradise and – with its otherworldly,
lunar-like landscapes – has jaw-dropping scenery”
The top 3 countries with the best scenic views
OverallWildlifeScenic BeautyBush VibeBirding
Namibia4,444,514,804,233,68
Tanzania4,834,964,794,464,12
South Africa4,584,694,673,913,94
  • Lizzie Williams From South AfricaZA – Author of 4 Footprint guidebooks to Africa, incl. Namibia.
     
    Rating:
    5/5 stars
     
    “A hauntingly beautiful country that stretches along the west coast of southern Africa, with wide open spaces and some of the earth’s most mystical and vivid sunsets, any visitor is blown away by the way Namibia ‘looks’.” Full review
  • Christopher Clark From United StatesGB – Travel writer who contributed to various Fodor’s guidebooks.
     
    Rating:
    5/5 stars
     
    “Most of Namibia is comprised of harsh and inhospitable desert, yet I’m not sure there’s anywhere in the world that I consider more beautiful.” Full review
Want to do a safari in Namibia?

Zambia, favorite among safari-goers, has the best bush vibe

Zambia with its huge, wild parks and extensive wildlife rated highly in our analysis. It was number one with safari-goers for best country and best destination for birdlife; and everyone’s favorite for its bush landscapes;
Its beautiful, thick foliage and dreamy landscapes ensured Zambia come out on top in the bush vibe category. Both experts and safari-goers were in agreement about the exceptional beauty of bush parks such as South Luangwa and the Lower Zambezi.
“Zambia is a walk on the wild side – its untamed landscapes and
unfenced camps a favorite among safari tourists”
The top 3 countries for the best bush vibe
OverallWildlifeScenic BeautyBush VibeBirding
Zambia4,794,834,504,794,10
Botswana4,754,734,394,514,17
Tanzania4,834,964,794,464,12
  • Stephen Cunliffe From South AfricaZA – International photojournalist specializing in wildlife conservation.
     
    Rating:
    5/5 stars
     
    “I am one of Zambia’s biggest fans and I think this country deserves its reputation as one of Africa’s foremost safari destinations.” Full review
  • Alan Murphy From AustraliaAU – Author of over 20 Lonely Planet guidebooks to Africa, incl. Zambia.
     
    Rating:
    5/5 stars
     
    “Watching Zambia’s prolific wildlife in classic safari country with stunning landscape, churning rivers and wide horizons may just be a life-changing experience.” Full review
Want to do a safari in Zambia?

Kenya best rated safari country for birding

Kenya with its highland, arid and well-watered regions that create many-a-varied habitat for birdlife was rated as the best country overall for bird-watching. Safari-goers, however, preferred Zambia.
The top 3 countries for the best bush vibe
OverallWildlifeScenic BeautyBush VibeBirding
Kenya4,644,934,644,154,49
Uganda4,304,184,374,224,36
Botswana4,754,734,394,514,17
  • Mike Unwin From United KingdomGB – Award winning author of the Bradt Guide to Southern African Wildlife.
     
    Rating:
    5/5 stars
     
    “The birder will be happy: Kenya holds the world record for the most bird species recorded in a single day.” Full review
  • Philip Briggs From South AfricaZA – Author of 7 Bradt guidebooks to Africa, incl. Kenya.
     
    Rating:
    5/5 stars
     
    “Kenya’s biodiversity is such that its national bird checklist of 1,136 species is the second highest for any African country.” Full review
Want to do a safari in Kenya?

Demographics of the reviewers (interactive charts)

User reviews: 1,721
Expert reviews: 969
Nationalities: 79
Percentage of reviews by country
All user reviews. Move your cursor over a country to get the number
Requested map does not exist.×
Age and gender (Percentage)
All people who wrote user reviews. Move your cursor over the chart for more details
35-501/436.9%27.6%27.1%
AgeReviewers
35-501,528
20-351,124
50-651,145
65+282
Under 2064
MaleFemale30%70%
GenderReviewers
Male2,895
Female1,242
Safari Experience Level (Percentage)
All people who wrote user reviews. Move your cursor over the chart for more details
First safari2-5 safarisOver 5 safaris01020304050
YearPercentage
First safari41
2-5 safaris31
Over 5 safaris28



Note from the author
We saw some different results between safari-goers and the expert panel, but they are easily explained. Guidebook authors tend to spend less time in parks and wildlife areas, however they may visit multiple times over several years, and also visit a large number of countries. They are therefore in a good position to make comparisons. Safari-goers on the other hand tend to spend longer in a park and visit less countries overall. Both groups contributed very useful and insightful reviews, which form the basis of our 2017 analysis.

Have a question about this article?

  • Jeroen Beekwilder
  • Contributed by  From Netherlands NL
    Jeroen is co-owner of SafariBookings.com. His desire to feel connected powers his love of travel. He has traveled all over the world with his wife and two children. But he will always remember his first African safari with his family in Tanzania. The thundering hooves of the wildebeest migration over the endless plains helped to develop a passion for Africa which never left.
  •