Tuesday, September 26

JIJI LA MWANZA KUBADILI MFUMO WA ARDHI KUTOKA ANALOJIA KUWA DIGITALI


Na Agness Francis, Blogu ya jamii
 SSERIKALI ya Tanzania wakishirikiana na serikali ya Korea Kusini  wamezindua utekeleza mradi utakaosaidia kuboresha  upatiikanaji wa  huduma bora  za ardhi  katika mkoa  wa Mwanza  na mradi huo  utanzia Manispaa ya Ilemela na Nyamagana.

Ambapo  hafla hiyo ya mradi huo umezinduliwa leo na Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,  Dkt Angeline Mabula  katika ukumbi wa  Hyatt Regency hoteli Jijini  Dar es Salaam.   

Katika ushirikiano huo wa kuimarisha utawala wa ardhi nchini ambapo makubaliano rasmi  ya ushirikiano huo yalianza mwaka 2015, ikiwa ni msada wa vifaa vya upimaji na mafunzo yanayohusu  matumizi ya vifaa vya kisasa vya upimaji, nayo yalianza mwaka 2016.

Naibu waziri Angeline Mabula ametamabaisha kuwa kuleta teknolojia hiyo mpya na nafuu  itarahisishia serikali  upimaji ardhi kwa kupanga na kupima kila kipande, pamoja na kusaidia wananchi kupata kumbukumbu na taarifa za ardhi kwa urahisi.

Mbali na hayo Dkt Angeline Mabula  ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya Korea Kusini kwa kuona umuhimu wa utekelezaji wa mradi  huo ambao utaleta mapinduzi makubwa  katika sekta ya ardhi hapa nchini.
 Balozi wa Korea Kusini Tanzania, Song Geum-Young  akizungumza na mkurugenzi halmashauri ya Manispaa Ilemela pamoja na wakuu wa idara na taasisi wizara ya ardhi kuhusu ushirikiano uliopo kati ya Serikali ya Tanzania na Korea Kusini kuimarisha mfumo bora wa upimaji ardhi kwa urahisi.leo katika uzinduzi uliofanyika kwenye ukumbi Hayyat Regency Hotel Jijini Dar es Salaam.
 Mkurugenzi wa biashara  wa Kampuni ya LX, Cho Man-Seung akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu kuwa mradi huo unatarajia kuanza kutekeleza  hivi karibuni na  utakuwa ni wa kisasa zaidi hapa Nchini.
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,Dkt Angeline Mabula akizungumza na waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa maradi wa uboreshaji wa huduma za ardhi leo  uliofanyika kwenye ukumbi wa Hayyat Regency Hotel Jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wageni waalikwa pamoja na wakuu wa idara na taasisi wizara ya ardhi waliohudhuria uzinduzi huo leo katika ukumbi Hayyat Regency Hotel Jijini Dar es Salaam. (Picha na Agness Francis, Blogu ya Jamii)

BASI LA TASHRIFF LILILOKUWA LIKITOKA TANGA - DAR LAUNGUA KWA MOTO PONGWE - TANGA


Basi la Tashriff lililokuwa likitokea Tanga - Dar es Salaam limewaka moto majira ya saa 8 mchana eneo la Pongwe, Tanga. Kwa mujibu wa taarifa za awali chanzo cha moto huo hakijafahamika japo hakuna mtu aliyezurika japo mizigo yote imeungua.
Kikosi cha Zima Moto na Uokoaji Mkoani Tanga wakiendelea na zoezi la uokoaji na kuzima moto kwenye basi hilo. 

DK. MPOKI AFUNGUA MAFUNZO YA KUTATHIMINI KWA ULINGANIFU UFANISI , UBORA NA USALAMA WA DAWA KATIKA UKANDA WA AFRIKA MASHARIKI


Na Chalila Kibuda, Globu ya jamii.
CHUO  Kikuu cha Tiba na Sayansi  Shirikishi  Muhimbili  kupitia Shule ya Famasi  kwa kushirikiana  kwa Kituo cha cha Mafunzo ya kutathimini Dawa cha Afrika Mashariki wameendesha mafunzo ya kutathimini kwa ulinganifu ufanisi. Ubora na usalama wa  dawa katika ukanda wa Afrika Mashariki ambapo Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA), Shirika la Afya Duniani (WHO) na Sekeretarieti ya Jumuiya ya Afrika Mashariki wameshiriki katika uratibu wa mafunzo hayo na kutoa misaada ya hali na mali.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Mgeni Rasmi,  Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Ulisubisya Mpoki amesema mfumo wa kutathimini dawa za Afrika Mashariki ni muhimu katika kuhakikisha kuwa wananchi wa ukanda huo wanapata dawa bora, salama na zenye ufanisi mkubwa.

Dk. Mpoki amesema mafunzo hayo ya nadharia na vitendo kwa wataalam wa dawa wa nchi za ukanda wa Afrika Mashariki yanalenga  kuhakikisha kuwa dawa zote zilizokidhi vigezo zinasajiliwa kwa mfumo wa ulinganifu unaotumika  baada wataalam hao kujiridhisha kisayansi.

Nae Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Bw. Hiiti Sillo amesema kuwa kumekuwa na ushirikiano wa karibu na wananchi katika utoaji wa taarifa pale wanapoona kuna dawa zenye mashaka ziko mtaani, hivyo kusaidia katika dhima ya kulinda afya ya jamii.

Amesema kuwa kuanzishwa kituo cha kutathimini Dawa cha Afrika Mashariki kitakuwa ni msaada mkubwa katika kuhakikisha kuwa kila dawa zilizo katika nchi za Afrika Mashariki ni zile zilizosajiliwa na usajili huo ni kwa matumizi ya wananchi wote wa ukanda husika.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Ulisubisya Mpoki akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya kutathimini kwa ulinganifu ufanisi , Ubora na usalama wa dawa katika ukanda wa Afrika Mashariki yalifanyika jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa TFDA, Hiiti Sillo, Kulia ni Mkurugenzi wa Shahada za awali wa MUHAS, Profesa Mainen Moshi.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Hiiti Sillo akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo ya kutathimini kwa ulinganifu ufanisi, Ubora na usalama wa dawa katika ukanda wa Afrika Mashariki yalifanyika jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Ulisubisya Mpoki akiwa katika pamoja na Maprofesa wa Chuo cha Kikuu cha Tiba na Sayansi Shirikishi pamoja na Watalaam jijini Dar es Salaam.

VIJANA NA WATEJA WA VODACOM TANZANIA WALETEWA MKOMBOZI WA MAWASILIANO

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Ian Ferrao (katikati) na wafanyakazi wa kampuni hiyo wakionyesha mabango yanayoelekeza jinsi yakupata vifurushi vya bando la”Pinduapindua” kwa ajili ya wateja wao hususani vijana wakati wa uzinduzi wa bando hilo ambapo mteja anatakiwa kupiga namba *149*01# kisha kuchagua kifurushi cha siku, cha wiki au cha mwezi,Kutoka kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, Jaquiline Materu, Mkuu wa Kitengo cha Masoko, Nandi Mwiyombela ,Mkurugenzi wa Masoko, Hisham Hendi na Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa na Huduma kwa Wateja, Linda Riwa.

Vijana wakitanzania na wateja wote kwa ujumla wa Vodacom Tanzania PLC,wameletewa Uhuru na wepesi zaidi wa kutumia bando jipya la”Pinduapindua” lililozinduliwa jana na kampuni hiyo likiwa mahususi kwaajili ya wateja wa mtandao huo.

Akiongea wakati wa Uzinduzi wa huduma hiyo,Mkurugenzi wa biashara na Masoko wa Vodacom Tanzania PLC, Bw. Hisham Hendi alisema huduma ya bando hili jipya la “Pinduapindua” ni ya kwanza na yakihistoria katika kampuni zote za mawasiliano nchini,Hii ni moja ya mikakati ya kampuni yetu kutaka kuleta mabadiliko kwenye jamii hususani vijana kwa kuwarahisishia maisha yao ikiwemo kuongeza vipato na dhamira kubwa yakuwapeleka watanzania katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia.

“Utafiti wetu unaonyesha kwamba vijana ni moja ya kiungo kikubwa sana kwa mapinduzi yakiuchumi nchini pia ni tabaka linalokuwa kwa kasi ya kuridhisha na wana mahitaji maalum yakipekee yakiteknolojia tunapenda vijana watambue kwamba Vodacom Tanzania PLC imesikia kilio chao ndiyo maana leo hii tumewaletea Pinduapindua ”, alisema Hendi.

Pinduapindua ni kifurushi huru na chakipekee zaidi kuliko vifurushi vingine vinavyowapangia wateja wa kampuni zingine za mawasiliano nchini,Bando hili litawapatia vijana na wateja uhuru wao wa kuchagua kiasi cha kupangia kwenye data, kupiga simu (voice) au ujumbe mfupi (SMS) kulingana na mahitaji ya wakati huo. “Pinduapindua” pia itamwezesha mteja kutumia Facebook (ikiwa pamoja na picha), Whatsapp (maandishi na picha) na SMS hadi 200 bure.

Mkurugenzi huyo alifafanua zaidi kwamba kampuni inaelewa kwamba mahitaji ya wateja wao ya utumiaji hubadilika siku hadi siku kuna siku unaweza kuhitaji matumizi ya mtandao (data) zaidi ya muda wa maongezi, kwa hiyo unakuwa huru kupangilia matumizi ya kifurushi chako kuendana na mahitaji yako na jinsi yakupata vifurushi vya bando

hili ni rahisi mteja atahitaji kupiga namba *149*01# kisha kuchagua kifurushi cha siku, cha wiki au cha mwezi. Vifurushi hivi vinaweza kulipiwa kupitia muda wa maongezi au Mpesa na mara baada ya kununua, mteja atapatiwa kifurushi chake, Facebook BURE, Whatsapp BURE na SMS, vyote ambavyo vitatumika kwa muda wote wa kifurushi alichochagua” alisema Hendi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania Ian Ferrao (katikati) akicheza na wafanyakazi wa kampuni hiyo wakati wa uzinduzi wa bando jipya la Pinduapindua kwa ajili ya wateja haswa vijana,Jinsi yakupata vifurushi vya bando hili mteja anatakiwa kupiga namba *149*01# kisha kuchagua kifurushi cha siku, cha wiki au cha mwezi.
Wacheza shoo wa promosheni ya bando la Pinduapindua la Kampuni ya Vodacom Tanzania wakicheza wakati wa uzinduzi wa huduma hiyo, Dar es Salaam jana. Jinsi yakupata vifurushi vya bando hili mteja anatakiwa kupiga namba *149*01# kisha kuchagua kifurushi cha siku, cha wiki au cha mwezi.

Diamond akiri kuwa na mtoto nje ya ndoa

Msanii wa Tanzania Diamond PlatinumzHaki miliki ya pichaFACEBOOK/DIAMOND
Image captionMsanii wa Tanzania Diamond Platinumz
Msanii wa Tanzania Diamond Platnumz ameomba radhi baada ya kupata mtoto nje ya ndoa na mwana mitindo wa taifa hilo Hamisa Mobetto ambaye alishiriki katika kanda yake ya muziki.
Katika mahojiano na idhaa moja nchini humo nyota huyo alifumbua fumbo la muda mrefu lililokuwa likiwakera mashabiki wake wengi kuhusu uvumi uliokuwa ukisambaa kuhusu uhusiano wake na Hamisa.
Diamond ameomba radhi kwa mkewe mfanyibiashara wa Uganda Zari Hassan na familia yake.
''Ningependa kuomba radhi kwa mke wangu na watoto kwa makosa hayo'', alisema katika mahojiano.
Bi Mobetto alishiriki katika video ya wimbo wa Diamond Salome ambao umegonga vichwa vya habari na kupendwa na mashabiki wengi wa muziki katika eneo la Afrika mashariki.
Katika mahojiano hayo Diamond alisema kuwa alimjua kipusa huyo kwa miaka saba na kwamba walikuwa na uhusiano ambao haukuendelea kati ya mwaka 2009-10 kabla ya kukutana na Wema Sepetu na mkewe Zari Hassan.
Anasema baadaye walikutana tena na kuanza uhusiano wakati ambapo Diamond tayari alikuwa amefunga ndoa na mfanyibiashara wa Uganda Zari Hassan.
''Tuliendelea na uhusiano wetu na ndiposa akawa mjamzito, lakini nilimwambia kwamba niko tayari kumuangalia mtoto lakini ajue kwamba mimi tayari nina familia kwa hivyo iwe siri yetu mimi na yeye, alisema Diamond.
Diamond anasema kwamba kulianza kuzuka uvumi katika mitandao ya kijamii kuhusu ujauzito aliokua nao na alipoulizwa iwapo alikuwa akitoa siri hiyo alikataa katakata.
Msanii huyo anasema kuwa amekuwa akimpatia bi Hamisa shilingi 70,000 za Kitanzania kila siku mbali na kumnunulia gari jipya aina ya RAV 4 ili kumuangalia mtoto.

Mudavadi: Upinzani hauna nia ya kuzua vurugu Kenya


Zimebaki wiki nne kwa raia wa Kenya kurejea tena kwenye uchaguzi. Wakati uchaguzi ukisubiriwa Muungano wa vyama vya upinzani Nasa, umepanga maandamano makubwa hapo Jumanne kushinikiza kuondolewa kwa Afisa Mkuu Mtendaji wa tume ya uchaguzi, Ezra Chiloba na wengine kwa madai ya kuvuruga uchaguzi wa Agosti 8.
Mahakama ya juu kabisa ilifutilia mbali uchaguzi huo kutokana na kugundulika kuwepo na kasoro.
Zuhura Yunus alizungumza na mmoja wa viongozi waandamizi wa NASA Bwana Musalia Mudavadi aliye ziarani London- kwanza akitaka kujua hisia zake baada ya Jubilee kudai kuwa alihusika na udukuzi wakati wa uchaguzi uliopita.

Korea Kaskazini yadai Marekani imetangaza vita

This picture taken on September 23, 2017 and released from North Korea's official Korean Central News Agency (KCNA) on September 24 shows an anti-US rally in Kim Il-Sung Square in Pyongyang.Haki miliki ya pichaKCNA
Image captionKorea Kaskazini yailaumu Marekani kwa kutangaza vita
Waziri wa mambo ya nje wa Korea Kaskazini amedai kwamba rais wa Marekani Donald Trump ametangaza vita dhidi ya taifa hilo.
Ri Yong-ho aliwaambia waandishi wa habari kuwa Korea Kaskazini ina haki ya kudungua ndege za vita za Marekani.
Hi ni hata kwa zile ndege zenye hazipo katika anga ya Korea Kaskazini, aliongeza waziri huyo.
Uwezo wa Makombora ya Korea Kaskazini
Image captionUwezo wa Makombora ya Korea Kaskazini
"Dunia ni lazima ikumbuke kuwa Marekani ndiyo ilikuwa ya kwanza kutangaza vita," Bwana Ri alisema.
Pande hizo mbili zimekuwa zikitupiana maneno makali.
Licha ya majuma kadhaa ya misukusuko, wataalamu wanasema kuwa hakuna uwezekano wa makabiliano ya moja kwa moja kati ya Marekani na Korea Kaskazini.
Baada ya Bw Ri kuhutubia Umoja wa Mataifa siku ya Jumamosi, Rais Trump alijibu kupitia mtandao wa twitter, akisema kuwa Bw. Ri na kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un hawatakuwepo kwa muda ikiwa wataendelea na maneno yao.
Jibu la Bwana Ri lilikuja wakati akiondoka New York baada mkutano wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa.
Makombora ya Hwasong yakiwa katika maonyeshoHaki miliki ya pichaAFP
Image captionMakombora ya Hwasong yakiwa katika maonyesho
Korea Kaskazini imeendelea na majaribioya makombora ya nyuklia na ya masafa marefu siku za hivi karibuni licha ya vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
Viongozi wa nchi hiyo wanasema kuwa uwezo wake wa zana za nyulia ndiyo njia pekee dhidi ya mataifa yanayotishia kuiharibu.
Baada ya jaribio la hivi majuzi na kubwa zaidi la nyulia mapema mwiezi huu, baraza la usalama la Umoja wa Mataifa, liliidhinisha vikwazo vipya dhidi ya nchi hiyo.

Jaji mkuu wa Kenya David Maraga akaribishwa kwa shangwe Dar es Salaam

Jaji mku wa Kenya David MaragaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionJaji mku wa Kenya David Maraga
Jaji mkuu nchini Kenya David Maraga, ambaye alipata umaarufu kote duniani baada kufanya uamuzi wa kihistoria wa kufuta matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwezi Agosti nchini Kenya, amekaribishwa kwa shangwe kwenye mkutano wa kikanda kwa mujibu wa gazeti ya Citizen nchini Tanzania.
Gazeti hilo linaripoti kuwa Maraga alishangiliwa na washiriki wakati wa mkutano wa majaji ya mahakimu ambao unafanyika mjini Dar es Salam nchini Tanzania.
Bw. Maraga ambaye alisifiwa na wakati huo huo kulaumiwa kutokana na uamuzi wa kufuta matokeo ya kura, amewaambia wale wanaomkosoa kuwa yuko tayari kulipia gharama ya kutetea sheria.
Jaji mkuu nchini Tanzania Prof Ibrahim Juma, alimpongeza Bw. Maraga kwa kutetea uhuru wa mahakama nchini Kenya.

Washauri wa Trump wadaiwa kutumia barua pepe binafsi

TrumpHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionBinti wa Rais Trump, Ivanka ni miongoni mwa washauri wa karibu wa Trump
Gazeti moja la Marekani limeandika kuwa, washauri sita wa karibu wa rais Trump wamekuwa wakitumia barua pepe binafsi kuzungumzia masuala yahusuyo Ikulu ya Marekani tangu rais Trump kuingia madarakani.
Gazeti la New York times limeyataja majina ya washauri hao na mtoto wake Ivanka ni miongoni mwao.
Huku jalada la "Newsweek"lenyewe limeandika kuwa barua pepe alizokuwa anazitumia Ivanka alikuwa anatafuta ushirikiano na makampuni ya kibiashara na aliwatumia nakala wakuu wawili wa ofisi.
Wakati wa kampeni za uchaguzi, rais Trump alitishia kuwafunga wapinzani wake pale ambapo Hillary Clinton alipotumia barua pepe yake ya binafsi wakati alipokuwa katibu wa serikali ya Marekani.
Na siku ya jumapili, mume wa Ivanka, Jared Kushner alitajwa pia kutumia barua pepe yake binafsi kuwasilisha shughuli za serikali.
Gazeti moja la Marekani limeandika kuwa, washauri sita wa karibu wa rais Trump wamekuwa wakitumia barua pepe za binafsi kuzungumzia masuala yahusuyo Ikulu ya Marekani tangu rais Trump kuingia madarakani.

Merkel asema ataendelea kuwa na msimamo


Kansela wa Ujerumani ,Angela MerkelHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKansela wa Ujerumani ,Angela Merkel
Kansela wa Ujerumani ,Angela Merkel amesema kuwa chama chake hakitaegemea sera za mrengo wa kulia kujaribu kuwashawishi wapiga kura ambao walimuacha wakati alipokuwa anapambana na chama kinachopinga sera za uhamiaji cha AfD wakati wa uchaguzi wa jumapili.
Lakini Merkel amesema atajaribu awezavyo kurejesha Imani ya idadi kubwa ya watu ambayo walijisikia kutengwa.
Mafanikio ya chama cha mrengo wa kushoto cha AfD
Kimekiacha chama chake Merkel,CDC bila kuwa na na mshirika wa wazi kuunda serikali.
Merkel amesema alitaka kuunda serikali imara ambapo amezungumza na chama cha Liberals na Greens pamoja na So Social Democrats ambao walijitoa kuungana kwa mara nyingine na Christian Democrats.

Mada zinazohusiana