Tuesday, October 24

Vyombo vya Habari vya Serikali vimetakiwa kufuata Maadili ya Uandishi wa Habari

Na: Genofeva Matemu –WHUSM
Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza amevitaka vyombo vya habari vya serikali kufuata maadali na miiko ya uandishi wa habari kwa kuzingatia weledi ili umma eweze kupata habari zilizokidhi vigezo vya uandishi wa habari.
Rai hiyo ameitoa jana jijini Dar es Salaam alipofanya ziara katika Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) pamoja na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) na kuzungumza na watendaji wa taasisi hizo.
“Vyombo vya habari vya serikali viwe mfano bora kwa kuwa mstari wa mbele kuhakikisha kuwa watanzania wanapata taarifa sahihi na kwa wakati kwani vyombo hivi ni moja kati ya mhimili mkubwa wa nchi na kama vitatumika vibaya madhara yake ni makubwa sana” amesema Mhe. Shonza  
Aidha Mhe. Shonza amesema kuwa Serikali inathamini na kutambua mchango unaotolewa na vyombo vya habari vikiwemo vyombo vya serikali TBC katika kufikisha taarifa za ukweli na uhakika katika jamii.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Dkt. Ayob Rioba amemhakikishia Mhe. Shonza kuwa TBC itaendelea kuzingatia weledi na maadili katika kuhabarisha umma huku ikiendelea kubuni vipindi mbalimbali vitakavovutia jamii kuangalia televisheni hiyo.
Naye Mkurugenzi Mtendaji Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Dkt. Jim Yonazi amesema kuwa TSN imeendelea kuhakikisha kuwa taifa linahabarishwa kwa hakika kwa kutumia nyenzo mbalimbali na uzoefu tangu ilipoanzishwa miaka 88 iliyopita hivyo kuchangia katika maendeleo ya nchi yetu
“kwa sasa TSN ni zaidi ya magazeti, imejikita zaidi kuwa kampuni inayotoa huduma za habari kwa kutumia nyenzo mbalimbali za kiteknolojia ili kuweza kuendana na kasi ya maendeleo ya sayansi na taknolojia” amesema Dkt. Yonazi.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) Bw. HAB Mkwizu (kulia) akizungumza na Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (katikati) alipofanya ziara katika Kampuni hiyo jana Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji TSN Dkt. Jim Yonazi
 Mkurugenzi Mtendaji TSN Dkt. Jim Yonazi akizungumza wakati wa ziara ya Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) katika Kampuni hiyo jana Jijini Dar es Salaam
 Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kushoto) akizungumza na Menejimenti ya Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) alipofanya ziara katika Kampuni hiyo jana Jijini Dar es Salaam
 Mhariri wa gazeti la Daily News Bw. Leonard Mwakalebela (kushoto) akimwelezea Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kulia) namna habari zinavopitiwa na kupangwa katika gazeti hilo alipofanya ziara katika kampuni ya TSN jana Jijini Dar es Salaam
 Meneja wa uchapishaji wa magazeti ya Serikali Bw. Boniface Mwajombe (kulia) akimuonyesha Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (katikati) mpangilio wa habari unavokuwa kabla ya gazeti kuchapishwa wakati wa ziara ya Naibu Waziri huyo katika kampuni ya TSN jana Jijini Dar es Salaam
 Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza akiangalia mashine ya kuchapishia magazeti ya Serikali inavyofanya kazi alipofanya ziara katika Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) jana Jijini Dar es Salaam
 Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (watano kushoto) katika picha ya pamoja na menejimenti ya Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) alipofanya ziara katika kampuni hiyo na kuangali shughuli zinazofanywa na kampuni hiyo jana Jijini Dar es Salaam
 Mkurugenzi Mkuu Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Dkt. Ayob Rioba (kushoto) akizungumza na Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kulia) alipofanya ziara TBC jana Jijini Dar es Salaam
 Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (katikati) akimsikiliza Mkuu wa TBC Fm Bw. Othuman Iddy (kushoto) alipotembelea studio za TBC Fm wakati wa ziara yake TBC jana Jijini Dar es Salaam
 Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (katikati) akimsikiliza mkuu wa TBC International Bw. Deogratius Salufu (kulia) alipotembela studio za redio hiyo jana wakati wa ziara yake katika Shirika la Utangazani la Taifa (TBC) Jijini Dar es Salaam
 Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (kulia) akiwa katika meza ya kusomea taarifa ya habari ya Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) jana wakati wa ziara yake katika TBC Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) Dkt. Ayob Rioba
Naibu Waziri Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza (watatu kushoto) katika picha ya pamoja na menejimenti ya Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC) jana wakati wa ziara yake TBC Jijini Dar es   Salaam. Watatu kulia ni Mkurugenzi Mkuu TBC Dkt. Ayob Rioba. Picha na: Genofeva Matemu - WHUSM

APANDISHWA KIZIMBANI KWA KUKUTWA AKIMILIKI MALI ZISIZOENDANA NA KIPATO CHAKE HALALI


 Afisa forodha msaidizi wa TRA, akitoka katika mahaka ya hakimu mkazi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo mara baada ya kusomewa mashtaka yanayomkabiri ya kimiliki mali nyingi kuliko kipato chake.
Na Karama Kenyunko, Glogu ya Jamii.

Afisa Forodha msaidizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Jennifer Mushi leo October 24, 2017 amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka mawili likiwamo la kukutwa akimiliki mali isiyolingana na kipato chake halali ambapo ni magari 19 ya aina tofauti.

Mshtakiwa huyo ameshtakiwa chini ya kifungu cha 27, (1) (a) na (b) cha sheria ya kuzuia na kupambana na rushwa namba 11 ya mwaka 2007. Jennifer amesomewa hati ya mashtaka na Wakili wa Serikali Mkuu, Vitalis Peter  mbele ya Hakimu Mkazi Huruma Shaidi wa mahakama hiyo.

Wakili Peter akisoma hati ya mashtaka amedai, kati ya Machi 21 na Juni 30 mwaka jana, jijini Dar es Salaam mshtakiwa Jennifer akiwa  ameajiriwa na TRA kama Afisa Forodha Msaidizi alikutwa akimili magari 19 ya aina mbali mbali

Magari hayo yalitajwa kuwa ni, Toyota RAV4, Toyota Dyna Truck, Toyota Viz, Suzuki Carry, Toyota Ipsum, Toyota Wish, Toyota Mark II, Toyota RAV4, Toyota Wish na  Toyota Mark X.

Mengine ni Toyota Regiusage, Toyota Estimated, Toyota Alex, Toyota Noah, Toyota Crown,  Toyota Hiace, Toyota Estima, Toyota Passo na Suzuki Carry ambapo yote yanathamani ya Sh 197, 601, 207/- Mali ambayo hailingani na kipato chake halali.

Katika shtaka la pili imedaiwa, kati ya Machi  21 ,2012 na  Machi 30, mwaka jana jijini Dar es Salaam, Jennifer alikutwa akiishi maisha ya kifahari  yenye thamani ya Sh 333,255,556.24/- fedha ambayo hailingani na Kipato chake halali.

Mshtakiwa amekana mashtaka hayo na yuko nje kwa dhamana baada ya kutimiza masharti ya dhamana ambayo yalimtaka kuwa na mdhamini mmoja atakayeweka bondi ya milioni 20.

Kwa mujibu wa upande wa mashtaka upelelezi wa kesi hiyo umekamilika. Imeahirishwa hadi Novemba 7 kwa ajili ya kusikilizwa maelezo ya awali.

FastJet yasababisha abiria kufanya vurugu Mwanza


Mwanza. Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia(FFU) leo wamelazimika kuingilia kati kutuliza vurugu zilizoazishwa na abiria 75 waliokosa usafiri wa ndege ya kampuni ya FastJet kutoka Mwanza kwenda Dar es Salaam kutokana na hitilafu za kiufundi.
Abiria hao waliokaa uwanjani hapo kwa zaidi ya saa nne kuanzia saa 3:00 asubuhi walipotakiwa kusafiri hadi saa 7:00 mchana, walianzisha vurugu kushinikiza kupatiwa usafiri.
Wakizungumza na Mwananchi uwanjani hapo kwa nyakati tofauti, abiria Rukia Mohamed, Juma Kisombi na Mamad Mohamed wamesema walilazimika kuushinikiza uongozi wa kampuni hiyo kuwapa maelezo ya kutosha baada ya ahadi ya kutakiwa kusubiri kidogo kutotekelezwa kwa zaidi ya saa tatu waliyosubiri uwanjani hapo.
“Nimefika Jumapili iliyopita na leo, nilitakiwa kurejea jijini Dar es Salaam na nilifika uwanjani kwa muda uliotakiwa lakini hadi sasa hakuna ndege na uongozi hautoi maelezo ya kueleweka,” alilalamika Rukia.
Akizungumzia kadhia hiyo, Meneja wa FastJet Mkoa wa Mwanza, Ezekiel Manyiga amesema ndege iliyotakiwa kusafirisha abiria hao haikufika kutoka jijini Dar es Salaam kutokana na kupata hitilafu ya kiufundi.
“Hata abiria waliotakiwa kusafiri kutoka Dar es Salaam kuja Mwanza hawajafika hadi sasa; tunafanya kila lililo ndani ya uwezo wetu kutatua tatizo hili,” amesema Manyiga
Ilipofika saa 7:00 mchana jana, uongozi wa kampuni hiyo ulifikia uamuzi wa kuwarejeshea nauli abiria waliokuwa tayari kupokea fedha zao ili kutafuta usafiri mwingine pamoja na Sh30, 000 ya kujikimu kwa kila abiria aliyekosa usafiri.
“Watakaokuwa tayari kusubiri ndege yetu watalazimika kusafiri kesho (Jumatano)  kwa sababu ndege tayari imejaa,” amesema Manyiga

Wanawake walioshtakiwa kumuua Kim Jong-nam warudishwa uwanja wa ndege

Vietnamese Doan Thi Huong, who is on trial for the killing of Kim Jong Nam, the estranged half-brother of North Korea"s leader, is escorted as she revisits the Kuala Lumpur International Airport 2 in Sepang, Malaysia 24 October 2017.Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionPolisi wakimsindikiza Doan Thu Huong (kati kati)
Wanawake wawili wanaokabiliwa na mashtaka ya kumuua Kim Jong-nam ambaye ni ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea Kaskazini wamepelekwa eneo la mkasa nchini Malaysia.
Siti Aisyah raia wa Indonesia na Doan Thi Huong raia wa Vietnam walipelekwa uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur leo Jumanne.
Wawili hao wanalaumiwa kwa kumwekea kemikali hatari ya VX Bw. Kim usoni wakati alikuwa anasubiri kuabiri ndege.
Wamekana mashtaka hayo ya mauaji wakisema kuwa walidanganywa kuwa kilikuwa ni kipindi cha runinga na majenti wa Korea Kaskazini.
Korea Kaskazini imekana kuhusika kwenye mauaji hayo ya tarehe 13 Februari, lakini wanaume wanne wanoaminiwa kuwa raia wa Korea Kaskazini walioikimbia nchi siku ya mauaji nao wameshtakiwa.
Uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur ulifurika waandishi wa habari leo Jumamanne.
Haki miliki ya pichaEPA
Baadaye wanawake hao wakafikishwa uwanja wa ndege wakiwa wamevalishwa mavazi yasiyopenya risasi.
Haki miliki ya pichaEPA
Image captionSiti Aisyah (kati kati )
Walisindikizwa na polisi wengi waliokuwa wamevaa mavazi yasiyopenya risasi
Haki miliki ya pichaEPA
Image captionWalisindikizwa na polisi wengi waliokuwa wamevaa mavazi yasiyopenya risasi
Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWalisindikizwa na polisi wengi waliokuwa wamevaa mavazi yasiyopenya risasi
Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionSiti Aisyah akisindikizwa
Haki miliki ya pichaEPA
Image captionWaandishi wa habari walifurika uwanja wa ndege
Malaysia's Special Task Force On Organised Crime (STAFOC) arrive to provide security at the low-cost carrier Kuala Lumpur International Airport 2 (KLIA2) during a visit to the scene of the murder as part of the Shah Alam High Court trial for Indonesian defendant Siti Aisyah and Vietnamese defendant Doan Thi Huong on 24 October 2017.Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionpolisi
Ikiwa watapatikana na hatia wanawake hao wanakabiliwa na hukumu ya kifo. Mawakili wao watajaribu kuwatetea kuwa wahusika wakuu ni maajenti wa Korea Kaskazini ambao waliondoka Malaysia.

Mbunge mteule Janeth Masaburi azungumzia uteuzi wake



Mbunge mteule, Janeth Masaburi
Mbunge mteule, Janeth Masaburi 
Dar es Salaam. Mbunge mteule, Janeth Masaburi amezungumzia uteuzi wake akisema anamshukuru Mungu kwa hatua hiyo.
Rais John Magufuli, Oktoba 21,2017 alimteua Janeth kushika wadhifa huo.
Mteule huyo leo Jumanne Oktoba 24,2017  amezungumza na Mwananchi akisema, “Namshukuru Mungu kwa kuwa imempendekeza na amemtumia mtu wake kumkumbuka mjane na kada wa CCM.”
“Ameamua kuniteua kwenda kuongeza nguvu, kikubwa nitakwenda kuwawakilisha vyema wanawake na tufikie azma ile ya uchumi wa viwanda,” amesema.
Janeth ni mke wa marehemu Dk Didas Masaburi aliyewahi kuwa Meya wa Jiji la Dar es Salaam.
Katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Dk Masaburi aligombea ubunge wa Ubungo na kushindwa na Saed Kubenea wa Chadema.
Uteuzi wa Janeth umefanywa na Rais Magufuli kwa mujibu wa Ibara ya 66 (1)(e) ya Katiba ya Tanzania inayompa mamlaka ya kuteua wabunge 10 na ulihitimisha nafasi hizo.
Wateule hao ambao ni mawaziri ni; Dk Philip Mpango (Fedha na Mipango), Profesa Palamagamba Kabudi (Katiba na Sheria), Profesa Joyce Ndalichako (Elimu, Sayansi na Teknolojia), Profesa Makame Mbarawa (Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano) na Dk. Augustine Mahiga (Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa).
Wengine walioteuliwa na Rais Magufuli ni Dk Tulia Ackson ambaye ni Naibu Spika wa Bunge, Salima Kikwete, Anne Kilango na Abdallah Bulembo.

WADAU WA MAENDELEO NA MAAFISA WA SERIKALI KUTEMBELEA WALENGWA WA TASAF

Moja wa maafisa wa Benki ya Dunia,ambaye pia huratibu shughuli za TASAF (TTL) katika benki hiyo , bw. Muderis Mohamed (aliyesimama) akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa maendeleo na serikali mjini Dar es salaam.
 Mtaalamu wa Habari na Mawasiliano wa TASAF ,Bi. Zuhura Mdungi (aliyesimama) akitoa maelezo ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini- PSSN- kwenye mkutano wa wadau na serikali kwenye ukumbi wa mikutano wa TASAF ,mjini Dar es salaam.

 Baadhi ya washiriki wa mkutano wa wadau wa maendeleo, serikali na watumishi wa TASAF –wakiwa katika ukumbi wa mikutano wa taasisi hiyo kupata maelezo ya hatua zilizofikiwa katika utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya masikini kabla ya kuanza ziara ya kikazi katika maeneo mbalimbali nchini kukutana na walengwa na viongozi.


Na Estom Sanga-TASAF
Baadhi ya watendaji wa Serikali na Wadau wa Maendeleo wanaanza ziara katika maeneo mbalimbali ya Utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini unaoratibiwa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii –TASAF- kukutana na walengwa wa Mpango huo na kuona mafanikio na changamoto za utekelezaji wake.

Akitoa maelezo kabla ya kuanza kwa ziara hizo zitakazofanyika katika mikoa ya Ruvuma, Njombe, Kigoma, Tabora, Singida, Kilimanjaro ,Morogoro na Zanzibar ,Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF ,Bw. Ladislaus Mwamanga ameishukuru serikali na wadau wa maendeleo kwa mchango mkubwa wa kufanikisha shughuli za Mpango huo unaohudumia zaidi ya kaya masikini MILIONI MOJA na Laki MOJA nchini kote.

Hata hivyo Bwana Mwamanga amesema licha ya kuweko kwa mafanikio makubwa ya utekelezaji wa Mpango, bado kuna asilimia 30 ya vijiji nchini ambavyo havijafikiwa na huduma za Mpango jambo linaloendelea kulalamikiwa na wananchi ambao hawajafikiwa na Mpango huo na hivyo amesema serikali kupitia TASAF inalifanyia kazi kwa karibu suala hilo.

Aidha katika maelezo ya utekelezaji wa Mpango huo yaliyowasilishwa na Mtaalamu wa Habari na Mawasiliano wa TASAF,Bi. Zuhura Mdungi imeonyeshwa kumekuwa na mafanikio katika kubadili fikra na za kaya za walengwa katika kupambana na umasikini kwa kutumia huduma za Mpango huo mkubwa kupata kutekelezwa nchini .

Shughuli za ziara na majadiliano kati ya serikali,wadau wa maendeleo na maafisa wa TASAF hufanyika kila baada ya miezi sita kuona namna utekelezaji wa Mpango wa kunusuru kaya masikini unavyoendelea kwa kukutana na walengwa ,viongozi,wataalam na kuwasikiliza namna huduma za Mpango huo zinavyosaidia jitihada za serikali za kupunguza adha ya umaskini kwa wananchi.

HOTUBA KAMILI YA RAIS MAGUFULI BAADA YA KUKABIDHI VYETI KWA WAJUMBE WA KAMATI ZA UCHUNGUZI WA MADINI



PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO OKTOBA 24,2017