Tuesday, October 24

Wanawake walioshtakiwa kumuua Kim Jong-nam warudishwa uwanja wa ndege

Vietnamese Doan Thi Huong, who is on trial for the killing of Kim Jong Nam, the estranged half-brother of North Korea"s leader, is escorted as she revisits the Kuala Lumpur International Airport 2 in Sepang, Malaysia 24 October 2017.Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionPolisi wakimsindikiza Doan Thu Huong (kati kati)
Wanawake wawili wanaokabiliwa na mashtaka ya kumuua Kim Jong-nam ambaye ni ndugu wa kambo wa kiongozi wa Korea Kaskazini wamepelekwa eneo la mkasa nchini Malaysia.
Siti Aisyah raia wa Indonesia na Doan Thi Huong raia wa Vietnam walipelekwa uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur leo Jumanne.
Wawili hao wanalaumiwa kwa kumwekea kemikali hatari ya VX Bw. Kim usoni wakati alikuwa anasubiri kuabiri ndege.
Wamekana mashtaka hayo ya mauaji wakisema kuwa walidanganywa kuwa kilikuwa ni kipindi cha runinga na majenti wa Korea Kaskazini.
Korea Kaskazini imekana kuhusika kwenye mauaji hayo ya tarehe 13 Februari, lakini wanaume wanne wanoaminiwa kuwa raia wa Korea Kaskazini walioikimbia nchi siku ya mauaji nao wameshtakiwa.
Uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur ulifurika waandishi wa habari leo Jumamanne.
Haki miliki ya pichaEPA
Baadaye wanawake hao wakafikishwa uwanja wa ndege wakiwa wamevalishwa mavazi yasiyopenya risasi.
Haki miliki ya pichaEPA
Image captionSiti Aisyah (kati kati )
Walisindikizwa na polisi wengi waliokuwa wamevaa mavazi yasiyopenya risasi
Haki miliki ya pichaEPA
Image captionWalisindikizwa na polisi wengi waliokuwa wamevaa mavazi yasiyopenya risasi
Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionWalisindikizwa na polisi wengi waliokuwa wamevaa mavazi yasiyopenya risasi
Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionSiti Aisyah akisindikizwa
Haki miliki ya pichaEPA
Image captionWaandishi wa habari walifurika uwanja wa ndege
Malaysia's Special Task Force On Organised Crime (STAFOC) arrive to provide security at the low-cost carrier Kuala Lumpur International Airport 2 (KLIA2) during a visit to the scene of the murder as part of the Shah Alam High Court trial for Indonesian defendant Siti Aisyah and Vietnamese defendant Doan Thi Huong on 24 October 2017.Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionpolisi
Ikiwa watapatikana na hatia wanawake hao wanakabiliwa na hukumu ya kifo. Mawakili wao watajaribu kuwatetea kuwa wahusika wakuu ni maajenti wa Korea Kaskazini ambao waliondoka Malaysia.

No comments:

Post a Comment