Friday, December 7

Familia ya Sharo yaibua mazito

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Teule Muheza, Dk Julius Mjema aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Sharo Milionea alisema sababu ya kifo chake ni kichwa kupondeka.

“Mimi ndiye niliyefanyia ‘postmoterm’ (uchunguzi), mwili wa Sharo Milionea, ni kwamba kichwa kilikuwa kimepondeka huku mifupa ya kichwa ikiwa imepondeka pia,” alisema Dk Mjema.
FAMILIA ya msanii Hussein Ramadhani Mkiety (Sharo Milionea) aliyekufa katika ajali wilayani Muheza wiki iliyopita imedai kuwa haiamini kwamba kifo cha mtoto huyo kilitokana na ajali, hivyo kulitaka Jeshi la Polisi kufanya uchunguzi wa kina kubaini ukweli.
Mjomba wa marehemu , Mohamed Msenga alisema jana kwamba familia imekuwa na shaka juu ya mazingira ya kifo hicho baada ya kurejeshewa nguo za msanii huyo zilizokuwa zimeibwa baada ya ajali lakini hazikuwa na damu.

Msenga alisema muda mfupi baada ya mama mzazi wa Marehemu Zaina Mwaimu Mkiety (54), kuitwa polisi na kukabidhiwa  vitu mbalimbali zikiwamo nguo ambazo marehemu alikuwa amevaa siku ya ajali hawakuona hata alama ya damu jambo ambalo liliwashangaza.
Alisema shaka hiyo ilianzia katika eneo ambalo ajali hiyo ilitokea akisema walipofika na kuonyeshwa mahala alipokuwa ameangukia, hawakuona damu jambo ambalo liliwatia shaka.
Alisema begi la nguo za msanii huyo lilikuwa na udongo mwingi likionyesha kwamba walioiba walikuwa wamelifukia kabla ya kusalimisha lakini hakuna damu zilizoonekana.

Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Teule Muheza, Dk Julius Mjema aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Sharo Milionea alisema sababu ya kifo chake ni kichwa kupondeka.
“Mimi ndiye niliyefanyia ‘postmoterm’ (uchunguzi), mwili wa Sharo Milionea, ni kwamba kichwa kilikuwa kimepondeka huku mifupa ya kichwa ikiwa imepondeka pia,” alisema Dk Mjema.

Kuhusu madai ya nguo kutokuwa na damu, alisema marehemu alipata mpasuko wa ndani kwa ndani na siyo wa  nje, ndiyo maana alipofikishwa chumba cha maiti damu zilionekana zikiwa zimeganda masikioni.

Hata hivyo, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Constantine Massawe alipoulizwa kuhusu madai hayo ya familia  alisema: “Hiyo ni taarifa ambayo jeshi la polisi litaifanyia kazi kwa kuingia kwa kina katika kuchunguza ili kuridhisha pande zote.”

Mama yake alia kukosa mjukuu
Katika hatua nyingine, mama mzazi wa msanii huyo amesema kutoachiwa mjukuu na tarehe za mwisho wa mwezi ni alama ambazo zitasababisha awe akimkumbuka mwanaye huyo milele. Akizungumza nyumbani kwake, katika Kitongoji cha Jibandeni Kijiji cha Lusanga wilayani hapa alisema kila ulipokuwa ukifikia mwisho wa mwezi ulikuwa ni muda wake wa neema kwani Sharo Milionea alimtumia fedha za matumizi yake binafsi pamoja na familia nzima nyumbani hapo.

“Pamoja na kwamba kila mara alikuwa akinitumia fedha za kutatua shida zangu mbalimbali nilizokuwa nikimweleza lakini kila mwisho wa mwezi alikuwa akihakikisha anatuma fungu la matumizi yangu na ndugu zake hapa nyumbani,” alisema mama huyo. Alisema mwisho wa mwezi itakuwa ni alama ya kudumu ya kumbukumbu ya mwanawe kwa sababu ni wakati ambao alikuwa akimtumia fedha za matumizi yake pamoja na familia nzima.


Kuhusu mjukuu alisema: “Sharo ni mwanangu wa pekee wa kiume, amekufa bila kuniachia mjukuu.. hii inaniuma sana lakini namshukuru Mungu kwani amechukua kiumbe chake na ndiye ajuaye siri iliyofichika mbele yangu,” alisema.

Alisema hadi alipofariki hakuwahi kumdokeza juu ya kuwa na mtoto wala kumpa mimba msichana yeyote... “Unajua Sharo Milionea alizaliwa pacha na mwenzake Hassan lakini mwenzake alifariki dunia siku tano baada ya kuzaliwa kwa hiyo katika kizazi changu mwanangu pekee wa kiume alikuwa Sharo Milionea ambaye nilitumaini kwamba angeniletea wajukuu,” alisema Zaina.

Alisema Sharo Milionea amekufa kabla hajatekeleza ndoto yake ya kumjengea nyumba ya kisasa pamoja na kuweka miradi ya kuboresha maisha yake azma ambayo aliiweka mwezi mmoja kabla ya kupata ajali iliyotoa uhai wake.

Atoa ya moyoni kwa walioshiriki msiba
Zaina alitoa shukrani za pekee kwa Rais Jakaya Kikwete na mkewe, Salma kwa kutuma ujumbe maalumu pamoja na rambirambi kutokana na msiba wa mwanaye huyo. Pia alimshukuru Mkuu wa Wilaya ya Muheza, Subira Mgalu, wasanii, waandishi wa habari na kampuni mbalimbali zilizoshiriki pamoja na kutuma salamu za rambirambi.



Jaji Mark Bomani awashukia polisi

ASEMA WANATUMIA ZAIDINGUVU KULIKO MAARIFA
KUJIRUDIA kwa matukio ya polisi kutumia silaha za moto dhidi ya raia, kumepokewa kwa hisia tofauti, huku Mwanasheria Mkuu wa Kwanza wa Serikali, Jaji Mark Bomani akilitaka jeshi hilo kuacha kutumia nguvu wanapokuwa katika operesheni zao.Wakizungumza jana kwa nyakati tofauti kuhusu tukio la hivi karibuni la kupigwa risasi mwandishi wa habari wa gazeti la Tanzania Daima, watu wa kada mbalimbali walisema, kitendo cha polisi kutumia nguvu sio busara.
Jaji Bomani kitendo cha polisi kutumia nguvu badala ya busara katika operesheni zao kinaweza kuleta uhasama kati ya wananchi na jeshi hilo.
“Kwa ujumla matumizi ya nguvu kwa polisi si mazuri  na nadhani tunatakiwa kubadilika katika hilo.” alisema Jaji Bomani. 
Bomani alieleza kuwa  kwa ujumla polisi wanatumia vibaya silaha zao ingawa bado hajapata uhakika wa jinsi  tukio la kujeruhiwa kwa Matutu lilivyokuwa .
Alisema tukio la Mwangosi lilikuwa baya zaidi lakini picha anayoiona na kuihusisha na tukio la juzi, ni kuwa kuna matumizi mabaya ya mashambulizi ya polisi kwa raia.
Hata hivyo wakati Jaji Bomani akieleza hayo Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji mstaafu Amiri Ramadhan Manento  alisema kila tukio linalofanywa na polisi linatakiwa kufanyiwa uchunguzi kabla ya kuanza kulizungumzia.
Jaji Manento alisema akiwa ni mwanasheria hawezi kutoa hitimisho ya tukio la kujeruhiwa kwa Matutu kabla ya uchunguzi wa kisheria kufanyika.
“Tunahitaji kujua mambo mengi, ya michakato ya makosa ya jinai, (criminal procedure) kwa mfano polisi walipoingia walifanya nini, walipotoka, ni maneno gani walimuuliza mtu wa kwanza waliyekutana naye.
Tunahitaji kujua iwapo walitumia kizuizi cha usalama(safe cage) katika silaha zao au la” alisema Jaji Manento
Alisema kulingana na taarifa zilizopo katika magazeti bado unahitajika uchunguzi wa kujua  ni namna gani polisi waliingia ndani ya nyumba hiyo.
Aidha Jaji huyo mstaafu alisema hawezi kuwahukumu polisi moja kwa moja kwani hakuna ushahidi kuwa walikuwa wakimwinda mwandishi, bali inawezekana waligundua kuwa ni mwandishi baada ya kumjeruhi.
Alisema hili ni tukio la tofauti na lile la kuuwa kwa Mwangosi kwani Mwangosi alikuwa kashika vifaa vyake vya kazi lakini hapa Matutu hakuwa na kitambulisho chochote kuwa ni Mwandishi.
“Unajua polisi wanafuata amri na sheria na wapo kwa ajili ya kulinda raia wake, hivyo hatuwezi kusema kuwa walikuwa wakimwinda mwandishi, kwa sababu hata polisi naye amejeruhiwa kwa panga katika tukio hilo,” alisema Jaji Manento
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam Dk Kitila Mkumbo alisema kuwa jeshi la Polisi limekuwa halifanyi kazi zake kwa kufuata weledi hali inayosababisha kuongezeka kwa matukio ya raia kupigwa risasi na Taasisi ya serikali yenye dhamana ya kuimarisha usalama wa raia hao.
“Matukio haya yanaweza kuathiri amani ya nchi kwa sababu wananchi wakikosa imani na serikali yao wanaweza kufanya jambo lolote bila kufuata sharia, matokeo yake amani inatoweka” alisema Dk Mkumbo.
Dk Mkumbo aliongeza kuwa ni vema IGP Saidi Mwema akatilia mkazo juu ya kufanya kazi kwa weledi ili kuimarisha utendaji kazi wa jeshi la polisi na kulipa taswira mpya katika jamii.
Mkuu wa Idara ya Fedha waskuli ya Biashara chuoni hapoDk Esther Ishengoma alisema kuwa jeshi la Polisi linadhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao, litaendelea kubeba dhamana hiyo, jambo la msingi ni kudhibiti nidhanu ya askari wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao.

“Ukiangalia matukio yanayotokea utaona kuna baadhi ya askari polisi wanaolichafua jeshi kwa kufanya mambo kinyume cha sheria, ni vema suala la nidhamu likaimarishwa ili kuongeza ufanisi,” alisema Dk Ishengoma.
Mkazi wa Mbagala Mtongani Solomon Isaiah alisema matendo yanayofanywa na polisi ya kujeruhi na kuua raia  ndani ya kipindi kifupi ni dalili za kutokuwepo utawala bora nchini na usimamizi mzuri wa ngazi za juu ndani ya Polisi.
“Hawa polisi hawajitakii kufanya hivyo bali wanatekeleza amri za viongozi wao wa ngazi za juu, hivyo basi lawama, hatua za kisheria  na mabadiliko yafanyike kwenye ngazi hizo za juu za polisi ndipo wahamie kwa polisi wenyewe” alisema Isaiah.
Matukio ya kuua na kujeruhi raia yanayotekelezwa na jeshi la polisi yamezidi kuongezeka siku hadi siku nchini licha ya wadau na wananchi kupigia kelele matendo hayo hali ambayo imezidi kugharimu maisha ya Watanzania wengi wasio na hatia kwa kuchukua sheria mkononi.
Hivi karibuni Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) kiliazimia kuishtaki Serikali kwa Mahakama ya Kimataifa ya masuala yaUhalifu(ICC) ili ichukue hatua zaidi juu ya mfululizo wa matukio ya kutisha yanayofanywa na jeshi la polisi kwa Wananchi baada ya Serikali kushindwa kuchukua hatua stahiki.
Kauli hizo imekuja siku moja baada ya polisi kulizungumzia tukio hilo kwamba lilitokea wakati wakiwa wanajihami.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni Charles Kenyela akizungumzia tukio la mwandishi huyo kupigwa risasi alisema alijeruhiwa baada ya kuanza kumshambulia askari kwa Panga.
Hata hivyo ufafanuzi wa kamanda huyo unatofautiana na ule wa Matutu na mashuhuda wa tukio hilo, ambao walisema kuwa polisi walivamia nyumba ya mwandishi huyo iliyopo maeneo ya Kunduchi huku wakimtaka mwanamke mmoja waliyemtaja kwa jina la mama J.
Katika maelezo yake Matutu alisema polisi hao walifika nyumbani kwake wakimtaka mkewe baada ya kumfananisha na mtu mwingine, kwamba wakati akiwa katika harakati za kumtenganisha mke polisi hao baada ya kuhisi  huenda wakawa majambazi ndipo polisi hao wakampiga risasi ya b