Wednesday, July 26

KAZI KUBWA KWA MAGUFULI


BAADA ya serikali kupitisha miswada mitatu bungeni inayohusu ulinzi wa rasilimali za Taifa wiki iliyopita, Rais John Magufuli ametakiwa kujiandaa kwa mapambano makali zaidi katika siku zijazo.

Katika mapitio ya nyaraka mbalimbali na mahojiano na watafiti na sekta ya uziduaji yaliyofanywa na gazeti hili baada ya kupitishwa kwa miswada hiyo mitatu muhimu; imefahamika kwamba bado kuna kazi kubwa ya kufanywa katika kuhakikisha dhamira ya serikali kuwa Taifa linafaidika na utajiri wake inafikiwa.
Miswada ambayo ilipitishwa wiki iliyopita ni ile ya Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba ya Maliasili za Nchi wa Mwaka 2017; Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Maliasili wa Mwaka 2017 na ule wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali wa Mwaka 2017.
Mmoja wa wanasheria na watafiti maarufu katika fani ya uziduaji, Dk. Rugemeleza Nshalla, ameliambia gazeti hili kwamba sheria hizo mpya haziwezi kuleta mabadiliko makubwa kama serikali haijaangalia pia mikataba ya pande mbili na pande tatu iliyoingia na nchi na jumuiya mbalimbali duniani.
Anapozungumzia pande mbili, Dk. Nshalla anazungumzia mikataba ile ambayo Tanzania imeingia na nchi moja moja (bilateral) na pande tatu ni ile ambayo imeingia na nchi zaidi ya moja (multilateral).
Alisema wakati sheria mbili mpya zilizopitishwa bungeni zinazungumzia migogoro ya kisheria kuamuliwa na mahakama za ndani, ipo mikataba ya pande mbili na pande tatu ambayo inasema wazi kwamba migogoro itaamuliwa na Mahakama za Kimataifa.
“ Ndiyo maana nasema sheria hizi zilizopitishwa zinanyimwa nguvu na mikataba ya pande mbili na pande tatu ambayo Tanzania iliingia huko nyuma na baadhi ya nchi na jumuiya za kibiashara.
“ Katika hilo hakuna la kufanya zaidi ya kuingia kwenye majadiliano upya na nchi hizo tulizoingia nazo mikataba ili tufanye marekebisho na huko pia. Bila hivyo, kazi yote hii iliyofanywa na serikali haitakuwa na maana inayotarajiwa,” alisema Nshalla ambaye amesomea shahada yake ya uzamivu (PhD) katika Chuo Kikuu maarufu cha MIT nchini Marekani.
Uchunguzi uliofanywa na gazeti hili katika baadhi ya mikataba ya pande mbili umeona vipengele mahususi vilivyowekwa vinavyosema wazi kwamba migogoro yote itapelekwa kwenye Mahakama za Kimataifa.
Kwa mfano, kwenye mkataba wa pande mbili kati ya Tanzania na Canada, kifungu cha 24 kinatamka bayana kwamba migogoro itapelekwa katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID).
“ Pande hizi mbili zimekubaliana kwamba kama kutatokea mgogoro wowote unaohitaji usuluhishi, basi mgogoro utatatuliwa kwa kupitia sura ya pili ya mkataba wa ICSID au ibara ya pili ya mkataba wa New York, inasema ibara hiyo ya mkataba wa pande mbili kati ya Tanzania na Canada.
Canada ndiko makao makuu ya kampuni ya Barrick inayomiliki kampuni ya Acacia; ambayo imeingia katika sintofahamu na serikali ya Rais Magufuli katika mgogoro wa usafirishaji wa makinikia ya madini.
Kwa mujibu wa tovuti inayoeleza kuhusu mkataba huo kati ya Tanzania na Canadahttp://international.gc.ca/trade-commerce/trade-agreements-accords-commerciaux, mkataba wa pande mbili baina ya Tanzania na Canada, yaani A bilateral Foreign Investment Promotion and Protection Agreement (FIPA) uliingiwa rasmi Desemba, 2013.
Katika mazungumzo yake na Raia Mwema, Dk. Nshalla alisisitiza kwamba mikataba mingi ya pande mbili au tatu huingiwa kwa dhana potofu kwamba pande mbili zinazokubaliana zina uwezo sawa kiuchumi – jambo lisilo la kweli.
“ Utakuta Tanzania inaingia mkataba na Uingereza kuambiana kwamba yenyewe itapata fursa za kuwekeza kule na iachie huku fursa hizo kwa Waingereza. Lakini hata Mwalimu Nyerere aliwahi kuhoji huko nyuma, hivi Stamico au NDC zetu zinaweza kushindana na Waingereza kwenye mitaji huko kwao?”, alisema Nshalla.
Kwa upande wake, Mbunge wa Kigoma Mjini, ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema sheria hizo mpya zinapaswa kupongezwa kwa uzalendo wake lakini akasema kuna mambo yanatakiwa kusemwa lakini serikali haiyasemi.
Alisema dalili zimeanza kujionyesha kwamba mgogoro wa sasa unaweza kupunguza mitaji ya uwekezaji kutoka nje (FDI) kwa sababu wawekezaji hawana uhakika na mwelekeo mpya wa Tanzania.
Alisema kwa sasa dhahabu imekuwa ya pili kwa kuingiza fedha nyingi za kigeni kwa Tanzania; ikizidiwa na sekta ya utalii pekee, na kwamba uwekezaji ukipungua, nchi itaanza kuumia kiuchumi.
“ Hatua zilizochukuliwa na serikali ni nzuri lakini inatakiwa iwaambie watu wajiandae na machungu yanayokuja. Makampuni ya nje yatataka kuonyesha umwamba wao kwetu kwa kupunguza uwekezaji.
“ Namna pekee ya kufanya ni kwa serikali kuongeza uuzaji nje wa mazao kama vile korosho, pamba, mawese, katani na pia kupunguza idadi ya bidhaa inazoagiza kutoka nje ili kupunguza matumizi ya fedha za kigeni.
“ Kwa maoni yangu, huu ndio wimbo ambao serikali ilitakiwa ianze kuuimba sasa kwa maana ya kuwaandaa watu na kile kinachoweza kutokea. Jambo ambalo silielewi ni kwamba serikali haiwaambii watu ukweli huu ili wajiandae na kinachokuja,” alisema Zitto ambaye alikuwa ni mmoja wa wabunge wa mwanzoni kabisa kuzungumzia suala la serikali kunyonywa mapato katika eneo la madini.
Mmoja wa wanaharakati maarufu nchini aliiyezungumza na gazeti hili kwa masharti ya kutotajwa majina yake, alifananisha kilichofanywa na serikali sawa na kitendo cha kumtishia uhai mtu ili muingie makubaliano na mtu huyo kwa kuwa katika hali hiyo  anaweza kukubali chochote kuhofia maisha yake.
“Hapa inaonekana mkakati wa serikali ulikuwa ni sawa na kutishia kuua mtu kwa kumwekea bastola kichwani. Chochote kitachotokea kumnusuru maisha yake ataona ni ushindi.
“Yaani ifanye hali ionekane ngumu kwa mpinzani wako. Akipata chochote cha afadhali atashukuru. Baada ya kibano walichopewa hawa wawekezaji, serikali inaweza kupata faida ambayo isingeipata kama isingeingia na mkwara ilioingia nao,” alisema mwanaharakati huyo aliyedai kwamba mawazo ya taasisi yaliwasilishwa kwenye semina ya wabunge na asingependa mawazo yake binafsi nayo yawe hadharani.
Hata hivyo, mwanaharakati huyo alisema upo uwezekano wa baadhi ya kampuni ambazo tayari zimefanya uwekezaji kuamua kuondoka kwa kutoridhishwa na mazingira na huenda zikaenda kudai fidia kwenye Mahakama za Kimataifa.
“ Nitakupa mfano wa Statoil ya Norway. Wao wanadai kwamba hadi sasa tayari wamewekeza kiasi cha dola bilioni mbili (shilingi trilioni nne) katika utafutaji wa gesi na mafuta hapa nchini.
“ Sasa watu kama hawa wakiamua kwenda kudai fidia na kusema wanataka kuondoka huko walikoweka bima, si ajabu ukasikia tunatakiwa kulipa fidia ya shilingi trilioni nne. Sasa hapo kama Wachina hawajaja kutuokoa unadhani tutazitoa wapi hizo,” alihoji.
Kwa mujibu wa taratibu za biashara za kimataifa, kampuni kubwa huwa na utaratibu wa kuweka bima zao kupitia taasisi iliyo chini ya Benki ya Dunia (WB) iitwayo MIGA kwa lengo la kujilinda wakati wakiwekeza katika nchi za kigeni.
Kama ikitokea kwamba nchi walikowekeza imevunja mkataba isivyo halali, MIGA huwalipa wawekezaji hao hasara waliyoipata lakini taasisi hiyo huanza kudai fedha hizo katika nchi husika; ambazo zenyewe (kama ilivyokuwa kwa Tanzania), zilikubali utaratibu wa MIGA.
Kwa maana hiyo, kama nchi itakataa kulipa, kuna uwezekano wa WB na nchi nyingine tajiri maarufu zikazuia misaada yote inayopitia nchi zao hadi pale nchi inayodaiwa itakapolipa fedha hizo. MIGA pia inaruhusiwa kukamata mali za nchi inayodaiwa na taasisi hiyo.

Je, tatizo ni mtoto wa kike?

    HIVI karibuni, Rais John Magufuli, alitoa agizo ya kuwa hakuna mwanafunzi aliyepata ujauzito atarudi kusoma katika shule za serikali kwa vile hawezi kukubali kusomesha wazazi.
Wito huu wa Rais unaweza kuwa sehemu ya suluhisho la mimba kwa wanafunzi wa kike ila sio suluhisho bora kwa ustawi wa mtoto wa kike katika nyanja ya elimu.
Kwa maoni yangu, ni vyema tukajikita katika kutazama mzizi wa tatizo na kuweza kuondoa tatizo katika mzizi ili lisiendelee kujirudia badala ya kuishia kuangalia matokeo ambayo ni mimba yenyewe na kuishia kumhukumu mwanafunzi huyu kwa kumnyima elimu.
Natambua ya kuwa watu wengi wanadhani mwanafunzi kupata mimba ni suala la mwanafunzi husika kuwa mhuni tu ama tabia ya wanafunzi wa kike kupenda ngono.
Aina ya mawazo haya yanatokana na dhana za kibepari ambazo huaminisha watu ya kuwa tatizo la mtu husika ni tatizo lake mwenyewe na si tatizo la mfumo husika. Hapa ndipo utasikia unaambiwa ya kuwa mtu ni masikini kwa kuwa hajasoma, hajajiajiri, amelogwa, sio mchapa kazi na mengine mengi.
Aina hii ya mawazo tunayasikia kila siku kwa kuwa ubepari unaamini katika dhana ya ubinafsi na si dhana nzima ya jamii. Hali hii ndio inayotukumba katika hili la mimba za wanafunzi tunafikiri ya kuwa hili ni tatizo la watoto wa kike kwa kuwa hawajiheshimu, hawapendi masomo, wana tamaa ya ngono, pesa, wakaidi, hawana maadili na mengine mengi.
Kama ingalikuwa tatizo la mimba za wanafunzi ni lao moja kwa moja ama sababu kama hizo nilizotaja hapo juu zenye mrengo wa kibepari, basi kuwafukuza shule ingekuwa suluhisho.
Kwa mtizamo wangu mimba kwa wanafunzi wa shule sio tatizo binafsi tu bali ni tatizo la kimfumo linalochangiwa kwa asilimia kubwa sana na mazingira.
Natambua dhana ya mazingira ni pana hivyo ntatumia nadharia ya Human Ecology kueleza maana ya mazingira katika muktadha huu.
Nadharia ya Human Ecology inasisitiza ya kuwa mazingira ya asili ama yale ya kutengenezwa na binadamu huchangia mabadiliko ya tabia ya mtu husika. Kwa mantiki hii, mazingira yanaweza kuwa yale yaliyotengenezwa na binadamu, mazingira ya asili na mazingira ya kijamii tamaduni ambayo mtu husika hupatikana.
Nadharia hii inatuonyesha wazi ya kuwa tabia ya mtu yeyete huchangiwa na mwingiliano alionao na mazingira yake. Kwa kusisitiza zaidi vile tunavyoona tabia za watu leo hii ndio mwingiliano alionao na mazingira yake ya asili ama yale ya kutengenezwa na mwanadamu mwenyewe.
Labda nitoe mfano kidogo. Leo hii urembo na utanashati unatafsiri tofauti kutokana na mazingira ya sasa. Kwa wanawake ili waonekane warembo lazima watinde nyusi, wapake vipodozi, waweke nywele bandia na kuvaa mavazi tunayodhani ndiyo  ya kisasa.
Kwa wanaume, lazima uvae suruali za kubana mithili ya zile za kike, ushushe suruali nusu makalio, unyoe kiduku, kujichubua kidogo, kuvaa viatu bila soksi nakadhalika.
Hiyo mifano hapo juu inatoa taswira ya namna mazingira yetu yanaweza kuwa na nguvu kubwa ya ushawishi kiasi cha kukufanya utende bila kutumia utashi kwani usipofanya utaonekana wa kale hivyo ili kuendana na mazingira binadamu aliyoyatengeneza lazima ufanye kawa wao ili ufanane nao.
Suala la mimba za wanafunzi ni tunda la mazingira wanayoishi wanafunzi wetu hawa. Na kama tunataka kutatua tatizo hili ni vyema tuanze na kurekebisha mazingira yale ambayo si rafiki kwa wanafunzi wa kike ili kuondoa ama kupunguza kabisa tatizo la mimba za wanafunzi angali wako shuleni.
Hebu tutafakari kidogo, je, watoto wa kike kwanini hupata mimba nini hasa huwa kichocheo?
Kama nilivyosema hapo awali, wanafunzi hawa wa kike huishi katika mazingira aidha yaliyo rafiki ama yasio rafiki kwao. Hapa nitapenda kuangalia mambo kama umbali kufika shuleni, aina ya elimu inayotolewa shuleni, adhabu zitolewazo shuleni, mahitaji muhimu ya wanafunzi shuleni, umasikini, kukosa mlo wawapo shuleni, ukosefu wa vyumba vya kulala kwa wanafunzi watokao mbali, malezi hafifu, talaka, malezi kutokuwa ya jamii nzima, ombwe la maadili, elimu kutokuwa na mvuto, elimu isiyoleta matumaini ya ajira, tamaduni, siasa, ufisadi na mengine mengi.
Tunapoamua kuwahukumu wanafunzi kwa kuwanyima fursa ya kusoma ni kana kwamba tunasema wanafunzi hawa wanaishi katika ulimwengu wao peke yao na hili ni kosa lao binafsi na si kosa la mfumo wala mazingira.
Suluhisho la kweli katika vita dhidi ya mimba za wanafunzi ni kupambana na mazingira yanayowakumba wanafunzi wa kike badala ya kuendelea kuwakandamiza kwa kuwanyima haki ya kukosa elimu.
Endapo wanafunzi wa kike waliojifungua watakosa elimu ni dhahiri ya kuwa mzunguko wa umasikini utaendelea na kuongeza idadi ya wanawake waliokosa elimu na hivyo kuongeza wigo za tofauti ya kielimu baina ya jinsia hizi mbili.
Nihitimishe kwa kusema, makatazo pekee si suluhisho muhimu katika vita hii dhidi ya mimba za wanafunzi, bila kuyarekebisha mazingira yote yanayopelekea kuwepo kwa mimba za wanafunzi. Ni vyema sasa wizara ya elimu na idara zake husika ikafanya utafiti wa kina kugundua changamoto za kimazingira, binafsi na za kisaikolojia ili kuweza kuja na mbinu mbadala itakayokuwa na tija zaidi kwa watoto wa kike ili mapambano yawe ya kisayansi zaidi.
Mwandishi wa Makala hii ni mtaalamu wa Sayansi ya Jamii. Anapatikana kwa baruapepe; j_mulikuza2000@yahoo.com na simu +255 786 946 931

Athari za mtoto kuchelewa kulala usiku

Athari za mtoto kuchelewa kulala usiku


Taarifa iliyotolewa na shirika la habari la Uingereza BBC, Julai 8 kuhusu utafiti uliofanyika nchini Uingereza uliowahusisha watoto 11,000 wakifuatiliwa kuhusu ratiba zao za kulala na kupima uwezo wa bongo zao.
Watafiti hao walisema ya kwamba wale watoto waliolala baada ya saa tatu usiku na waliokuwa hawana ratiba maalumu walikuwa na alama za chini kwenye hisabati na uwezo wa kusoma.
Na vilevile waliripoti kuwa ni vigumu ubongo kujifunza vitu vipya kutokana na ukosefu wa usingizi. Walichukua watoto wa kati ya miaka 3, 5 na 7 wakifuatilia uwezo wao wa kujifunza ukilinganisha na ratiba zao za kulala. Ratiba ilikuwa mbaya zaidi kwa watoto wa miaka 3. Na mpaka wanapofika miaka saba huwa na ratiba inayoeleweka kati ya saa moja na nusu usiku na saa mbili na nusu usiku.
Waliokuwa na ratiba nzuri ya kueleweka walifanya vizuri zaidi katika hisabati na kuwa na uwezo mkubwa  wa kusoma ukilinganisha na wenzao wasio na ratiba ya kueleweka na waliokuwa wanachelewa kulala .
Kuhusu kupungua uwezo wa ubongo athari zilionekana zaidi kwa wasichana ukilinganisha na wavulana. Utafiti huu uliofanywa na Prof. Amanda Sacker wa chuo kikuu cha London alisema kuwa vilevile mazingira mabaya ya familia zetu huweza kupelekea hali hii na aliijumuisha katika sababu za kupunguza uwezo wa ubongo.
Kitu Muhimu cha kuzingatia ni watoto kulala mapema na kumbuka bado hujachelewa,  ni vizuri kumuwekea ratiba nzuri ya kulala mtoto, na hakukuwa na ushahidi wa matokeo kuwa mazuri mtoto akilala kabla ya saa moja na nusu.
Kwa ujumla ili mtoto afanye  vizuri darasani ni vema apate usingizi mnono usiku.

TANZANIA YAJIPANGA KUISHAWISHI UINGEREZA, FURSA ZA UWEKEZAJI NISHATI, MADINI NCHINI: BALOZI MIGIRO, DKT. PALLANYO, WATAALAM WA WIZARA WAKUTANA


Na Veronica Simba – Dodoma
Kufuatia Kongamano kubwa la Uwekezaji linalotarajiwa kufanyika nchini Uingereza, mwezi Septemba mwaka huu, Balozi wa Tanzania nchini humo, Dkt. Asha-Rose Migiro amekutana na wataalam wa Wizara ya Nishati na Madini na Taasisi zake, wakiongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo na kujadili fursa za uwekezaji nchini katika sekta husika.
Katika kikao hicho kilichofanyika Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Julai 24 mwaka huu, Balozi Migiro, alisema kuwa Ubalozi wa Tanzania nchini Uingereza umejipanga kulitumia vema kongamano hilo ambapo watanadi fursa za uwekezaji katika sekta zote muhimu nchini, zikiwemo za nishati na madini.
“Ni kwa sababu hiyo, nimeona nifike hapa ili nikutane nanyi, tujadili kuhusu fursa za uwekezaji hapa nchini katika sekta za nishati na madini ili tuweze kuzinadi wakati wa kongamano hilo,” alisema Balozi Migiro.
Akifungua majadiliano baina ya wataalam hao na Balozi Migiro, Naibu Katibu Mkuu Pallangyo, alibainisha kuwa zipo fursa nyingi za uwekezaji hapa nchini, katika sekta za nishati na madini na kupongeza hatua ya Balozi Migiro kudhamiria kuzinadi fursa hizo kwa wawekezaji nchini Uingereza.
Aidha, kwa upande wa sekta ya nishati, Dkt. Pallangyo alimwomba Balozi Migiro kupeleka maombi kwa Serikali za Uingereza na Ireland kusaidia miradi ya usambazaji umeme vijijini inayoendelea nchini kote.
Akizungumzia fursa za uwekezaji zilizopo katika sekta ndogo ya umeme, Mhandisi Nishati, Christopher Bitesigirwe alibainisha kuwa mpango wa serikali ni kuzalisha umeme hadi kufikia megawati 5000 ifikapo mwaka 2020 hivyo wawekezaji makini wanaendelea kukaribishwa.
Mhandisi Bitesigirwe alieleza kuwa, vyanzo vilivyoainishwa kwenye Mpango Kabambe wa Uendelezaji wa Sekta Ndogo ya Umeme ni pamoja na gesi asilia, maji, makaa ya mawe na nishati jadidifu (jua, upepo, jotoardhi na tungamotaka).
Kwa upande wa miradi ya usafirishaji wa umeme, alitaja fursa zilizopo kuwa ni pamoja Mradi wa kusafirisha umeme kuanzia Mbeya hadi Nyakanazi (North West transmission line) wa kilovoti 400, Iringa hadi Mbeya (KV 400), Chalinze hadi Dodoma (KV 400) na SomangaFungu hadi Kinyerezi (KV 400).
Vilevile, Mhandisi Bitesigirwe alitaja fursa iliyopo katika Miradi ya Usambazaji Umeme kuwa ni uboreshaji wa miundombinu ya usambazaji umeme.
Naye Mjiolojia Mkuu kutoka Idara ya Nishati, Habass Ngulilapi, alimweleza Balozi Migiro kuwa fursa za uwekezaji zilizopo katika sekta ndogo ya Petroli ni utafiti wa gesi asilia pamoja na mafuta unaoendelea nchini.
“Hadi sasa mafuta hayajagunduliwa nchini lakini kiasi cha futi za ujazo trilioni 10 za gesi asilia, kimegunduliwa katika maeneo ya mabonde ya nchi kavu,” alisema Ngulilapi.
Aliongeza kuwa, hadi kufikia mwezi Aprili 2017 kiasi cha gesi asilia kilichogunduliwa katika maeneo ya mabonde ya nchi kavu na katika kina cha maji mafupi na marefu ni futi za ujazo trilioni 57.25.
Kwa upande wake, Kaimu Kamishna wa Madini, Mhandisi David Mulabwa, akizungumzia fursa za uwekezaji zilizopo katika sekta ya madini, aliitaja miradi ya uongezaji thamani madini ya aina mbalimbali hapa nchini.
Mhandisi Mulabwa alibainisha kuwa, Mitambo ya kuchenjulia madini ya metali inahitajika sana kwa sasa hapa nchini ili kuwezesha kuchenjua madini hayo nchini pasipo kuyasafirisha nchi za nje, kufuatia agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli.
“Tayari wapo wawekezaji mbalimbali ambao wameonesha nia kuwekeza nchini kwa kuleta mitambo hiyo lakini kulingana na uhitaji na umuhimu wake, serikali bado inakaribisha wawekezaji wengine mbalimbali wenye nia ya dhati, waje kuwekeza katika eneo hilo,” alifafanua.
Aidha, Mhandisi Mulabwa, alibainisha fursa nyingine ya uwekezaji iliyopo katika sekta ya madini kuwa ni kuongeza thamani mawe mbalimbali ya vito kwa kuyakata na kuyang’arisha.
Akifafanua zaidi, alieleza kuwa, kuanzisha viwanda vya kutengeneza mapambo mbalimbali yanayotokana na madini ya vito na metali hapa nchini, ni fursa adhimu ambapo Serikali inawakaribisha wawekezaji makini kuja kuwekeza katika sekta hiyo.
Kaimu Meneja wa Uwekezaji kutoka Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Nsalu Nzowa, alimweleza Balozi Migiro kuwa, fursa zilizopo kupitia shirika hilo ni kuendeleza Mradi wa kuchimba madini ya dhahabu wa Buhemba ambao ulikuwa ukitekelezwa kwa ubia kati ya Jeshi la Tanzania na la Afrika ya Kusini, na baadaye kusimamishwa.
Vilevile, alitaja fursa nyingine ya uwekezaji kuwa ni uchimbaji wa makaa ya mawe kwa ajili ya matumizi katika viwanda vya saruji pamoja na matumizi mengine mbalimbali.
Kwa upande wa Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST), Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Kijiolojia, Maruvuko Msechu, alimweleza Balozi Migiro kuwa Wakala huo unaendesha uchunguzi na tafiti mbalimbali za kijiolojia, ambazo zinahitaji ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali.
Naye Mkurugenzi wa Kanzidata wa GST, Yokbeth Myumbilwa, alieleza kuwa, wawekezaji wanashauriwa kutembelea Tovuti ya Wakala huo ili kujipatia maelezo kuhusu tafiti mbalimbali zilizofanywa na Wakala zitakazowasaidia kupata uelewa wa aina mbalimbali za madini yanayopatikana nchini pamoja na maeneo yanakopatikana.
 












Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia) akiwa katika kikao na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha-Rose Migiro (kushoto), Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma Julai 24, 2017. Wengine pichani ni wataalam wa Wizara na Taasisi zake walioshiriki kikao hicho.
 








Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (katikati), akiongoza kikao cha wataalam wa Wizara pamoja na Taasisi zake na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha Rose Migiro (kushoto kwa Naibu Katibu Mkuu.)
 Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha Rose Migiro (mwenye Koti la Pinki) na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini anayeshughulikia masuala ya Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia kwa Balozi), wakiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa Wizara pamoja na Taasisi zake, Makao Makuu ya Wizara, mjini Dodoma.
 















Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, anayeshughulikia Nishati, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kulia), akimkabidhi Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha-Rose Migiro, Kitabu cha Mpango Kabambe wa Uendelezaji Sekta Ndogo ya Umeme (Power System Master Plan). Wanaoshuhudia ni wataalam wa Wizara pamoja na Taasisi zake.
 
 















Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dkt. Mhandisi Juliana Pallangyo (kushoto), akiagana na Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha-Rose Migiro (kulia), baada ya kikao baina yao Makao Makuu ya Wizara mjini Dodoma, Julai 24 mwaka huu.

Chai Huongeza Uwezekano wa Kupata Ujauzito?

Chai Huongeza Uwezekano wa Kupata Ujauzito?
  •  Utafiti uliofanywa na Chuo Kikuu cha Marekani cha Boston umesema  unywaji wa chai vikombe viwili kwa siku huongeza uwezekano wa mwanamke kupata ujauzito. Katika utafiti uliohusisha wanawake 3,600 umeonyesha ya kwamba wanawake wanaokunywa vikombe viwili vya chai kwa siku wana asilimia 27 ya kupata ujauzito ikilinganishwa na wanawake ambao hawanywi  chai. Pia utafiti huo umeonyesha ya kwamba wanawake wanotumia  vinywaji baridi  viwili kwa  siku kama coca cola, hupunguza uwezekano wao wa kushika mimba kwa asilimia 20 na haijalishi kama vinywaji hivyo  vina sukari au la. 
Mtafiti  mkuu Profesa Elizabeth Hatch amesema alifanya utafiti huu ili kutaka kujua kama kuna uhusiano wowote wa kemikali aina ya caffeine inayopatikana kwenye chai, kahawa  na uwezo wa kushika mimba kwa wanawake.Utafiti huu ulifanywa kwa kuwahusisha wanawake wa kutoka  nchi ya Denmark   kutokana na nchi hiyo kuwa na mfumo wa kuwapa raia wao namba za uraia wa kudumu wakati wa kuzaliwa na hivyo kuwa rahisi kwa Profesa Hatch kuwafuatilia kwa njia ya intaneti kwa muda wa mwaka mmoja. 
Profesa Hatch amesema “Hatujui wanawake hawa walikuwa wakinywa chai ya aina gani, hatujui kama walikunywa chai bila kuongeza kitu chengine kwenye chai, kama waliongeza maziwa au limao kwenye chai, bali inaonekana kuna uhusiano wa caffeine na uwezo wa kushika mimba au uwezo huo umetokana na mfumo wa maisha wa wanawake hao au ni kutokana na  virutubisho vya chai hiyo”. 
Pia katika utaifiti huu wanawake waliambiwa waaandike kiwango cha chai ya kijani (green tea) au chai ya  tiba (herbal tea) wanayokunywa kwa siku na hakuna uhusiano wowote ulionekana kati ya chai ya kijani au chai ya tiba na kuongeza  uwezo wa kushika mimba kwa mwanamke. 
Tafiti zaidi zinahitajika ili kuweza kujua kama chai ya kijani husaidia wanawake kupata ujauzito au la. 
Ufuatiliaji zaidi utaweza kujua afya na saizi ya watoto wataokaozaliwa  na kina mama hawa wanaokunywa chai  vikombe viwili kwa siku na kama hawa wanawake waliweza kubeba mimba hizo kwa muda mrefu/mfupi au kama mimba hizo ziliharibika. 
Maha Ragunath, bingwa wa tiba ya uzazi katika kituo cha care fertility center cha Nottingham amesema “Kuna virutubisho maalum kwenye chai vinavyosaidia katika utungaji mimba. Chai huwa na kemikali nyingi aina ya anti-oxidants ambazo ni nzuri kwa uzazi kwa wanaume na wanawake lakini nadhani kwa wanawake wanaohitaji mtoto ni vizuri kunywa chai kwa kiwango cha wastani”. 
Laurence Shaw mkurugenzi katika kituo cha uzazi cha Bridge Fertility Centre jijini London amesema “Wanawake walio na umri zaidi ya miaka 35 wanaojaribu kushika mimba ni bora watafute ushauri kutoka kwa madaktari na si kunywa vikombe 10 vya chai eti kwa sababu wanataka mtoto”.  
Ni bora tusubiri matokeo zaidi ya wanawake ambao wamepata ujauzito wakati wa utafiti huu ili tupate majibu ya uhakika kuhusu maendeleo yao baada ya kushika ujauzito huo.

Spika awavutia pumzi CUF


Spika wa Bunge, Job Ndugai

SIKU moja baada ya Mwenyekiti wa Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF), Profesa Ibrahim Lipumba kutangaza kuwavua uanachama wabunge wanane na madiwani mawili, Spika wa Bunge, Job Ndugai amekiri kupokea barua kuhusu uamuzi huo, na anatafakari kabla ya kutoa uamuzi.

Kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, Ibara ya 71 (f) chama cha siasa kina mamlaka ya kumsimamisha uanachama na hivyo anapoteza haki ya kuwa mbunge kupitia chama hicho. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Ndugai alisema ataitafakari na kuifanyia kazi barua hiyo na ataitolea taarifa baadaye.

“Suala la kuwaondoa uanachama ni la utashi wa vyama vyenyewe, na kila chama kina utaratibu wake, hivyo bado naendelea kuitafakari barua hiyo na uamuzi kuhusu wabunge waliofukuzwa uanachama nitautolea baadaye,” alisema Spika Ndugai (pichani).

Profesa Lipumba alisema Dar es Salaam jana kuwa mbali na wabunge hao, Baraza la Uongozi la chama pia limewavua uanachama madiwani wawili wa Viti Maalumu wa Mkoa wa Dar es Salaam kwa makosa ya kinidhamu tangu Julai 24, mwaka huu.

Aliwataja wabunge kuwa ni Riziki Shahali Ngwali, Saverina Mwijage, Salma Mwassa, Saumu Sakala, Riziki Lulida, Mgeni Jadi Kadika, Raisa Abdallah Mussa, Miza Bakari, Halima Ali Mohammed na Khadija Al Kassim.

Madiwani waliovuliwa nyadhifa zao ni Diwani Viti Maalumu, Leila Hussein Madibi (Ubungo) na Diwani wa Viti Maalumu, Elizabeth Magwaja (Temeke). Wabunge na madiwani hao wanatuhumiwa kutokana na kitendo cha kupewa na kupokea maelekezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na kula njama za kukihujumu CUF kwa kushiriki katika operesheni iliyoandaliwa na Chadema iliyoitwa ‘Ondoa Msaliti Buguruni’, jambo linalokiuka Katiba ya CUF ya 1992.

Pia wabunge na madiwani hao walikihujumu chama hicho katika uchaguzi wa marudio wa madiwani uliofanyika Januari 22, mwaka huu. Pia waliruhusu na kuipa fursa Chadema kuwa msemaji wa masuala ya CUF, kinyume cha matakwa ya Katiba yao na kulipia pango na kufungua ofisi ya chama Magomeni bila kufuata taratibu za kikatiba.

Pia inaonesha kwamba wanatuhumiwa hao, walichangia fedha zilizotumika kukodisha mabaunsa kwa lengo la kuwadhuru viongozi watiifu wa chama upande wa Lipumba, Sakaya na Mkurugenzi wa CUF wa Mambo ya Nje na Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftaha Nachuma.

Profesa Lipumba alisema kabla ya kuvuliwa uanachama, waliitwa mbele ya Kamati ya Maadili wao waliosusia mwito huo wa kwenda kujieleza juu ya tuhuma zinazowakabili za kula njama na Chadema ili kuweza kumwondoa yeye madarakani.

Wabunge na madiwani hao walisusia mwito hata baada ya kupewa barua za kuitwa na Kamati ya Maadili, hivyo Baraza Kuu limechukua maamuzi kwa kufuata Katiba yake ya mwaka 1984 kuwafuta uanachama.

Aidha, Lipumba alisema taarifa kuhusu uamuzi huo tayari zimeshatumwa kwenda kwenda Ofisi ya Spika wa Bunge, Job Ndugai ambaye amethibitisha kuipata barua na ameahidi kuitafakari na kuitolea uamuzi baadaye na kwa Msajili wa Vyama vya Siasa kwa ajili ya hatua zaidi.

Profesa Lipumba alisema wabunge 10 hao walioitwa na kuhojiwa na Kamati ya Maadili ya CUF na kugomea mwito huo ni wale wanaomuunga mkono Katibu Mkuu, Maalim Seif.

Historia ya chama hicho inaonesha kwamba hiyo si mara ya kwanza Baraza Kuu la Uongozi la Taifa la CUF, kuwafukuza wanachama kwani Januari 4, mwaka 2012, lilimfukuza uanachama aliyekuwa Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed na wenzake watatu.

Hatua hiyo ilichukuliwa baada ya Mbunge huyo kuingia kwenye msuguano mkubwa na Katibu Mkuu ambaye pia wakati huo alikuwa Makamu wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi, Maalim Seif Sharif Hamad.

Hamad Rashidi baada ya kuondolewa wanachama, alisikika akisema tatizo kubwa hapa katika siasa za Kitanzania ni kwamba “viongozi wetu wa juu hawataki kupata changamoto kutoka kwa waandamizi wao kwani hawako tayari kuona mawazo kupingwa.”

Pamoja na Hamad Rashid ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Baraza Kuu, wengine waliofukuzwa ni Doyo Hassan Doyo, Shoka Khamis Juma, Juma Said Sanani na Yasini Mrotwa.

Mbunge huyo Hamad Rashid Januari 10, 2013, na wenzake 10 waliwasilisha maombi madogo katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, wakiiomba itamke kuwa uamuzi wa Baraza la Uongozi Taifa la chama hicho uliomvua uanachama yeye na wenzake ni batili na haikufanya hivyo.

TUNZA GARI YAKO NA KICHOCHEO CHA NANO ( NANO ENERGIZER )

Tunakitambulisha kichocheo madhubuti cha Nano  kilichothibitishwa ubora wake na shirika la 
viwango la kimataifa (ISO 9001:2015). Hii ni teknolojia ya kipekee na ya kimapinduzi kwenye tasnia ya magari na mitambo. kichocheo cha Nano kimetengenezwa na teknolojia ya kisasa duniani ya Nano (Nano technology) kwa ajili ya kuikarabati na kuipa ulinzi injini ya gari yako bila kuifungua. Kichocheo cha Nano huziba mikwaruzo yote ndani ya injini na kuirudisha nguvu ya injini kama ilivyokuwa mpya. Wasiliana nasi kupitia Namba 0715480174.



Kichocheo cha Nano kinaipa injini ganda au tabaka gumu la ceramic na platinum. Tabaka hili linafanya muunganiko wa kudumu na chuma cha injini (cylinder wall) na kina uwezo madhubuti wa kuhimili uchakavu na michubuko itokanayo na msuguano. Inarudisha uwezo wa kusukuma wa injini (compression ratio) kwa kuweka ganda gumu kwenye ukuta wa cylinder.

FAIDA ZA KICHOCHEO CHA NANO.

  1. Hupunguza matumizi ya mafuta kwa 8% - 21%.
  2. Huongeza nguvu ya injini hadi kufikia 100%.
  3. Hupunguza mlio na makelele ya injini na mtetemo hadi Mara 5 zaidi.
  4. Inatoa ulinzi wa injini hadi kufikia 40000 km.
  5. Husaidia Kuboresha uhai wa injini na vifaa vingine.
  6. Hulinda injini na kuirudisha kwenye ubora wake kama ilivyokuwa mpya.
  7. Huongeza msukumo wa injini na kuboresha uunguaji wa mafuta.
  8. Hulainisha usukani na gear box.
  9. Hupatikana kwa magari ya aina zote, generator, compressor, pikipiki, bajaji na kila aina ya mtambo.
  10. Hupunguza utoaji wa moshi kati ya mara 3 hadi 9.
  11. Ina garantii ya utendaji kazi kwa 100%.
  12. Haiharibiki kwa nanma yoyote ile.
  13. Bidhaa bora kabisa iliyothibitishwa kimataifa na kitaifa.
  14. Inakupa faida ya kutoifungua injini hivyo kuongeza thamani ya gari hata ukitaka kuiuza.
  15. Inakupa faida ya kupata mafuta bure kila unapoweka kwa mara ya 9.
  16. Faida isiyolinganishwa ya ulinzi wa gari lako hadi kufikia km 40000 kwa sh 60000 tu ukilinganisha na gharama za  mafuta na services kwa kipindi hicho.


MATUMIZI

  1. Injini inatakiwa iwe imetumika kwa km 3000.
  2. Kichocheo cha Nano kinatumika kwa injini za aina yoyote inayotumia oili ya aina yoyote (mineral or synthetic oils).
  3. Ili kupata matokeo bora zaidi weka unapofanya service.
  4. Ipashe injini yako.
  5. Tikisa kichocheo cha Nano kabla ya kuweka kwenye injini.
  6. Fungua kifuniko cha injini oili halafu mimina kichocheo cha Nano.
  7. Funga kifuniko. Hongera, umefanikiwa.
  8. Baada ya kumimina kichocheo cha Nano usibadili oili ya injini mpaka kipindi cha matumizi yafuatayo (kilomita 400 kwa pikipiki na bajaji, kilomita 1200 - 1500 kwa magari madogo na kilomita 3000 kwa malori na mabasi).


MAPENDEKEZO.
Kichocheo cha Nano kimefanyiwa majaribio na kukubaliwa na taasisi zifuatazo.

  • Chuo kikuu cha Taifa cha Kyungpook - Korea.
  • Chuo Kikuu cha Taifa cha Seoul - Korea.
  • Taasisi ya Korea ya Mashine na Vifaa.
  • Chuo Kikuu cha Yeungnam - Korea.
  • Taasisi ya Korea ya Teknolojia ya magari.
  • Jeshi la ulinzi wa Taifa la Korea.
  • Kituo cha Jeshi la Anga la India.


UTHIBITISHO WA UBORA.
Kichocheo cha Nano kimefanyiwa majaribio maabara, kuthibitishwa, kukubalika na kutunukiwa vyeti vya ubora na taasisi zifuatazo.


  1. Shirika la Ubora la Kimataifa ISO 9001:2015.
  2. Shirika la viwango la Tanzania - TBS.
  3. Mkemia mkuu wa serikali ya Tanzania - GCLA.
  4. Maabara ya kimataifa ya SGS.
  5. Maabara ya kimataifa ya TUV SUD Industrie Service GmbH.


USHUHUDA / MAPENDEKEZO.
Kichocheo cha Nano kimefanyiwa majaribio na makampuni ya kutengeneza magari, kimethibitishwa na kupendekezwa kutumika na makampuni yafuatayo.
  • MERCEDES BENZ
  • TOYOTA
  • GM DAEWOO
  • VOLVO
  • HONDA
  • HYUNDAI
  • AUDI
kichocheo cha Nano sasa kinapatikana Tanzania na kusambazwa na POWER ENERGY ENGINEERING COMPANY LTD. Tunakaribisha mawakala kutoka wilaya zote za Tanzania. Wasiliana nasi kupitia Namba 0715480174.

Kwa wafanyabiashara: usiikose fursa hii ya kibiashara.
Kwa wamiliki wa vyombo vya moto (Magari, pikipiki, bajaji nk): Tumia Kichocheo cha Nano kwa ulinzi madhubuti wa chombo chako.


ANGALIA VIDEO HII UONE JINSI NANO INAVYOFANYA KAZI..









China kubaini watukanaji WhatsApp, Facebook Bongo

WATU wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii kama WhatsApp na Facebook, huenda wakaanza kubainika kirahisi katika siku za karibuni na kufikishwa mbele ya vyombo vya dola kwa msaada wa China, imeelezwa.

Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhandisi Edwin Ngonyani, alisema watu wanaotumia lugha za matusi, kutuma picha zisizokuwa na maadili katika mitandao ya kijamii watabainika kwa urahisi kwa kutumia mfumo wa China.

Ngonyani alisema China imefanikiwa kudhibiti suala hilo kwani kitu kibaya kinapoingizwa nchini mwao kupitia mtandao, hukizuia kabla hakijaleta madhara kwa jamii.

Sheria ya Makosa ya Mtandao ilipitishwa na Bunge Aprili Mosi, 2015 lakini ujio wa sheria hiyo haujaleta matokeo chanya kwa kuwa kumekuwa na matukio ya matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii ikiwemo Instagram pia.

Sheria hiyo ambayo tayari imeshaanza kutekelezwa ilipelekwa bungeni kwa hati ya dharura.

Ngonyani aliyekuwa akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano wa vyombo vya habari na matumizi ya mtandao uliofanyika jijini Dar es Salaam, alisema kuna idadi kubwa ya wananchi wanaotumia mitandao ya kijamii.

"Lakini baadhi yao huitumia kwa kuwatukana watu na hata kuweka vitu visivyotakiwa kwa maadili ya Kitanzania," alisema.

"Kama mtu amekutumia ujumbe mbaya, tunataka tuwe na uwezo wa kumkamata na kumchukulia hatua.

"Au (mtu) amekutumia barua pepe, au ametuma picha mbaya kwenye WhatsApp, wenzetu China wameweza kuwanasa kwa urahisi.

"Sasa na sisi tunataka kujifunza hilo ili tuanze kuwabaini."

Ngonyani alisema mgeni yoyote anayeingia China hawezi kutumia mtandao wowote wa kijamii isipokuwa wa Kichina, tofauti na hapa nchini ambako mgeni anaweza kutumia mitandao ya nje.

AANDAA MFUMO
Mhandisi Ngonyani alisema serikali inaandaa mfumo huo wa kuwabaini moja kwa moja watumiaji wabaya wa mitandao na kwamba pindi utakapokamilika utapelekwa katika Baraza la Mawaziri; kisha kupelekwa bungeni na kupitishwa kuwa sheria.

"Mfumo huo ukikamilika tutaweza kujua ujumbe huu umetoka kwa nani, kwa sababu kwa sasa hivi mtu anaweza kutumia simu ya mtu mwingine kutuma ujumbe mbaya," alisema zaidi.

"Sasa ni lazima tutafute teknolojia mpya ambayo hata mtu akitumia simu (namba) ya mtu na kuitumia vibaya tunamkamata.

"Kule (ujumbe) ulikotoka lazima ujulikane."

Alisema kwa sasa serikali imefikia hatua nzuri ya udhibiti wa wezi wa fedha wa mitandao lakini bado inatatizwa na mitandao ya kimajii kutoka nje ya nchi. WhatsApp, Facebook na Instagram yote ina kanzidata Marekani.

Pamekuwa na hukumu zinazotokana na Sheria ya Makosa ya Mtandao hata hivyo.

Isaack Emily wa Arusha alihukumiwa kifungo cha miaka mitatu au kulipa faini ya Sh. milioni saba na Mahakama ya Hakimu Mkazi

Arusha katikati ya mwaka 2016, baada ya kumuona na hatia ya kumtukana Rais John Magufuli kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Aidha, Februari 21, mwaka huu wanafunzi wanne wa Chuo Kikuu cha Kampala (KIU) kampasi ya Dar es Salaam, walifikishwa katika

Mahakama ya Wilaya ya Ilala, kujibu shitaka la kusambaza picha za kumkashifu Rais Magufuli kupitia mtandao wa kijamii wa WhatsApp.

Washitakiwa hao ni Amenitha Kongo (19), Maria Tweve (20), Agnes Gabriel(21) na Anne Mwansasu(21).

Kwa pamoja walidaiwa kuchapisha picha ambazo zinaonyesha Rais Magufuli akiwa amevaa hijabu kama mwanamke wa Kiislamu na kuzisambaza kwenye mtandao huo wa WhatsApp, huku wakijua kufanya hivyo ni kinyume cha sheria.

Mabasi 11 yafungiwa kufanya safari za mikoani



Jeshi la polisi mkoa wa Arusha limefanya ukaguzi wa kushitukiza kwa mabasi ya kusafirisha abiria kwenda mikoani wilayani na maeneo ya vijijini na kugundua makosa mengi kwenye magari hayo  ambapo zaidi ya mabasi arobaini yametozwa faini huku  mabasi kumi na moja  yakifungiwa kusafirisha abiria baada ya kukutwa na makosa makubwa yanayohatarisha uhai wa wasafiri.

Katika ukaguzi huo maafisa wa jeshi la Polisi kitengo cha usalama barabarani wamegundua makosa mengi yakiwemo kukosa mikanda ya abiria uchakavu wa maumbo ya magari na kati ya zaidi ya mabasi hamsini yaliyokaguliwa madereva watano wenye makosa sugu wamefikishwa mahakamani.

Wakizungumzia operesheni hiyo wafanyakazi wa mabasi na mawakala wamekuwa na maoni tofauti wakati wengine wakidai kutopatiwa muda wa kutosha kufanya marekebisho wengine wameunga mkono  zoezi hlo  huku abiria wakieleza walivyoathirika.

Hatima ya viongozi 51 wa Chadema kujulikana leo


VIONGOZI na wafuasi 51 wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambao wameendelea kusota kwa siku 18 kwenye Gereza la Biharamulo mkoani Kagera kutokana na kunyimwa dhamana na Mahakama ya Wilaya ya Chato, hatma yao ikajulikana leo.

Ni baada ya mahakama hiyo kupokea hoja za upande wa mashtaka na utetezi ambao unaiomba mahakama kuondoa zuio la kutopewa dhamana ambalo liliwekwa na Mwendesha Mashtaka, Semen Nzigo.

Viongozi na wafuasi hao walikamatwa na Jeshi la Polisi wilayani hapa Julai 7, mwaka huu wakiwa kwenye kikao cha ndani kilichowahusisha viongozi wa Chadema mkoa, wilaya na Kata ya Muganza, ambapo walifunguliwa mashtaka ya kufanya mkusanyiko bila kuwa na kibali.

Baada ya pande hizo kuwasilisha hoja zao juzi, Hakimu wa Mahakama hiyo, Jovith Kato, alisema atatoa uamuzi wa mapingamizi hayo kesho, iwapo washtakiwa wapewe dhamana au waendelee kubaki mahabusu.

Wakizungumza nje ya mahakama, mawakili wa upande utetezi, John Edwar na Siwale Isambi, walisema wanatarajia mahakama itatenda haki kwa kuwapa dhamana kabla ya kesi ya msingi haijasikilizwa.

“Tunashukuru, mahakama imesema itatoa uamuzi wake keshokutwa (leo) iwapo wateja wetu wapewe dhamana au la...ila ni matumaini yetu makubwa kuwa zuio la upande wa mashtaka litaondolewa,” alisema Edward.

Baadhi ya viongozi walioko gerezani ni Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Geita, Phabian Mahenge, Katibu wa Chadema mkoa huo, Sudy Tuganyala, Mwenyekiti wa Baraza la Wazee mkoa, Vitus Makoye na Mwenyekiti wa Bavicha mkoa huo, Neema Chozaile.

Wengine ni Katibu wa Wilaya ya Chato, Mange Ludomya, Kaimu Mwenyekiti Wilaya ya Chato, Uhuru Selemani, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji wa wilaya hiyo, Meshark Tulasheshe na Katibu Mwenezi Kata ya Muganza, Marko Maduka.

Hata hivyo, wakati mahakama hiyo ikitoa tarehe ya uamuzi wa pingamizi hilo, washtakiwa wote hawakuwapo mahakamani.