Sunday, January 13

Zitto aingia matatani

 MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameingia matatani, baada ya kutakiwa kukanusha tuhuma alizozitoa bungeni katika Mkutano wa Tisa wa Bunge, kwamba mfanyabiashara wa kigeni, Moto Mabanga, alipewa vitalu vya mafuta kinyume na taratibu.

Mfanyabiashara huyo amesema kuwa iwapo Zitto atashindwa kukanusha tuhuma hizo, atafikishwa mahakamani.

Barua iliyoandikwa kwenda kwa mbunge huyo iliyosainiwa na Mwanasheria wa Mabanga, Lawley Shein wa Kampuni ya Uwakili ya Lawley Shein Attorneys, ambayo Mwananchi Jumapili limeiona, inaeleza kuwa hoja binafsi aliyoitoa Zitto, haikuwa na ukweli wowote.

Barua hiyo ya tarehe 28 Novemba, 2012 ilisema kuwa hoja hiyo ya Zitto ni ya uongo, imemkashifu mteja wao na kumshushia hadhi yake binafsi na biashara zake.

“Katika kuthibitisha kuwa tuhuma zako siyo za kweli katika hoja uliyotoa, umemtaja mteja wetu kama raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Mteja wetu ni raia wa Afrika Kusini, lakini, umeamua kumtaja kama raia wa Kongo bila kuangalia ukweli,” alisema Shein.

Katika barua hiyo, Shein pia amesema kuwa Zitto amemtuhumu mteja wake Mabanga kuwa aliwahonga baadhi ya vigogo serikalini na kuwapa rushwa wanasiasa katika mchakato wa kufanikisha upatikanaji wa vitalu hivyo.

“Tuhuma hizo siyo za kweli, mteja wetu alifuata taratibu zote kwa uwazi na mamlaka husika nchini na hakuwahi kutoa rushwa kwa mtu yeyote,” alisema mwanasheria huyo.

“Tuhuma hizi ni za uongo, zimemharibia jina mteja wetu na kumsababishia madhara. Kama hutazifuta kauli hizo, uongo huo utamsababishia mteja wetu madhara makubwa zaidi na tutalazimika kudai fidia,” Shein alionya kupitia barua hiyo.

Shein aliongeza kuwa pamoja na Zitto kuongea hoja hiyo akiwa bungeni hivyo kuwa na kinga ya kibunge, lakini kwa mazingira aliyotolea hoja hiyo alitumia vibaya kinga ya kibunge, anayopata mbunge yeyote anapotoa hoja akiwa bungeni.

Kupitia barua hiyo, Shein alimtaka Zitto kufuta kauli yake dhidi ya mteja wao na kwamba mteja wao ana haki zote za kushtaki dhidi ya hoja hiyo.

Zitto azungumza
Alipotakiwa kuzungumzia hoja hiyo na hatua atakazochukua, Zitto alisema kuwa amemwandikia barua Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashililah, kumjulisha hatua hiyo ya kutaka kushtakiwa.
“Nimemwandikia Katibu wa Bunge kumjulisha kwamba nimeletewa kusudio la kushtakiwa, maana hili ni suala la Kinga ya Bunge,” alisema Zitto na kuongeza:

“Mbunge ana kinga kwa masuala aliyozungumza ndani ya Bunge kwa mujibu wa Ibara ya 100 ya Katiba. Kwa hiyo Katibu (Dk Kashililah), atawajibu hao wanasheria.”

Ibara hiyo ya 100 (2) inaeleza kuwa; Bila ya kuathiri Katiba au masharti ya sheria nyingine yoyote inayohusika, mbunge yeyote hatashtakiwa au kufunguliwa shauri la madai mahakamani kutokana na jambo alilosema au kulifanya ndani ya Bunge, au alilolileta bungeni kwa njia ya maombi, muswada, hoja au vinginevyo.

Naibu Spika
Kwa upande wake Naibu Spika, Job Ndugai alisema kuwa hana taarifa za kusudio hilo la kutaka kushtakiwa kwa Zi tto, lakini akasema kwamba mbunge ana kinga ya Bunge pindi akitoa hoja au wazo lolote, akiwa ndani ya Bunge.

Ndugai alisema kuwa kutokana na mabadiliko madogo ya sheria yaliyofanyika, mwananchi anaweza kuandika barua kwa Spika wa Bunge kutokana na tuhuma alizotoa mbunge dhidi yake bungeni.
“Mtu anaweza kuandika barua kwa Spika na Spika ataona hatua zaidi za kuchukua za kibunge,” alisema Ndugai.

Uswisi imeiumbua serikali, sasa fedha zirejeshwe

   
NILIMSIKILIZA kwa makini Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Frederick Werema, alipokuwa akijibu bungeni hoja ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe aliyoiwasilisha bungeni Novemba mwaka jana kuhusu mabilioni ya fedha yaliyotoroshewa katika mabenki mbalimbali nchini Uswisi.

Werema alisema kuwa Serikali imeanza kuzifanyia uchunguzi tuhuma hizo na kwamba Serikali haijalala bali inaendelea na uchunguzi.

Alisema vyombo vya usalama ikiwamo Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (Takukuru), wanalifanyia kazi suala hilo. Akatoa wito kwa Zitto na wananchi wengine kama wana ushahidi zaidi wauwasilishe katika vyombo hivyo ili fedha hizo ziweze kurejeshwa.

Wakati akiwasilisha hoja hizo Zitto alikwenda mbali zaidi ya kuwaelezea watu walioficha fedha hizo nje ya nchi na miaka ambayo walifanya hivyo.

Bila ya kuwataja kwa majina, Zitto aliwataja watu hao kwa nyadhifa kuwa ni watu wote walioshika nyadhifa za uwaziri mkuu katika kipindi cha 2003 hadi 2010, walioshika nyadhifa za uwaziri wa nishati na madini katika kipindi hicho na waliokuwa makatibu wakuu Wizara ya Nishati na Madini.

Wengine ni mawaziri na makatibu wakuu wa Wizara ya Ulinzi, wakuu wa majeshi, wanasheria wa Serikali, makamishna wa nishati, walioshika wadhifa wa Ukurugenzi Mkuu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC), Uenyekiti na Ujumbe wa Bodi wa TPDC katika kipindi cha mwaka 2003 hadi 2010.

Pia Zitto alitaka Serikali kuwasiliana na Benki ya Dunia kupitia kitengo cha ‘Assets Recovery Unit’ ili mabilioni ya fedha na mali ambazo zimetoroshwa nje ya nchi kwenda Uswisi, Dubai, Mauritus na maeneo mengine ziweze kurejeshwa.

Hoja hiyo ya Zitto iliungwa mkono na Wabunge mbalimbali wakiwamo wa CCM ambao walitaka serikali kuchukua hatua za haraka kurejesha fedha hizo na wahusika wachukuliwe hatua.
Wapo wabunge ambao walikwenda mbali zaidi ya kutaka watu hao waliotorosha fedha hizo wakipatikana wanyongwe kwa sababu hao ni wasaliti wan chi yetu.

Mwisho wa mjadala bunge likaazimio kuipa serikali muda hadi bunge lijalo kutoa taarifa ya utekelezaji wa azimio hilo la kurejesha fedha hizo nyumbani.

Baada ya hapo kila mmoja tukajua kweli sasa serikali huenda ikalifanyia kazi azimio la bunge la kuzirejesha fedha hizo, kwa sababu siku zote serikali imeonyesha kuwa nzito katika kuzirejesha fedha hizo.

Kauli ya serikali ya Uswisi kuwa Serikali Tanzania haijaonyesha nia ya dhati kutaka kuchunguza na kupata mabilioni ya fedha yaliyofichwa na Watanzania katika benki mbalimbali nchini humo, inashtua sana.

Balozi wa Uswisi nchini, Olivier Chave alisema Ijumaa ya wiki hii kuwa mpaka sasa hakuna jitihada zozote zilizofanywa na Serikali ya Tanzania kutaka ufumbuzi wa tuhuma hizo.

Chave alisema Uswisi iko tayari kushirikiana na Tanzania kujua uhalali wa fedha hizo na endapo zikigundulika ni fedha chafu basi tutazirejesha nchini.

Alisema Serikali yao haina tatizo, kwani wameshafanya hivyo kwa nchi za Ufilipino na Nigeria hivyo watafurahi na Tanzania kama watamaliza suala hilo.

Alisema habari zinazoandikwa kuhusu mabilioni hayo kuhifadhiwa katika Benki za Uswisi, yanaharibu picha ya nchi hiyo mbele ya mataifa mengine, hivyo angependa suala hilo kumalizwa na kwamba wao wako tayari.

Kwa hakika, kauli ya balozi huyu imeimbua serikali ambayo imekuwa ikitoa visingizio vya vingi kwamba inashindwa kuzirejesha fedha hizo kutokana na kukosa ushirikiano.

Naamini kama alivyosema Zitto na watu wengine nchini kwamba fedha hizo zinamilikiwa na vigogo ndani ya serikali au waliowahi kushika nyadhifa za juu serikalini ndiyo maana inakuwa vigumu kuchukua hatua.

Kama serikali ya Uswisi inasema iko tayari kutoa ushirikiano wa kurejeshwa kwa fedha hizo nyumbani, serikali inataka msaada gani tena zaidi ya huo?

Ni kitu cha kushangaza tunapomuona Werema na mawaziri wengine wa serikali Rais Jakaya Kikwete wakisimama kuwapaka mafuta Watanzania kwa maneno matamu kwamba wameanza uchunguzi kuhusu suala hilo, wakati hata hawajawasiliana na serikali ya Uswisi.

Kuonyesha kuwa hawana nia ya dhati hata Zitto mwenyewe hadi sasa anasema Serikali haijamfuata kutaka kutoa ushirikiano wa aina yeyote kuhusu tuhuma hizo.

Zitto alikaririwa Ijumaa ya wiki hii akisema kuwa ingawa Serikali ilitaka iachiwe tuhuma hizo ili iweze kuzifanyia kazi, lakini hadi sasa ukimya umetawala.

Sasa tunaitaka serikali kuacha kutumia visingizio ili kuwazunga Watanzania, tunahitaji fedha hizo zirejeshwe na wahusika wachukuliwe hatua.
0754 304336
juliusmagodi@yahoo.com

Palestinian Leader Yasser Arafat To Be Exhumed For Toxicology Tests


The body of the former Palestinian leader, Yasser Arafat, is to be exhumed next week amidst suspicions he may have been poisoned.

Arafat, who led the Palestine Liberation Organisation for 35 years, died eight years ago after becoming the first president of the Palestinian Authority in 1996.

He fell ill in October 2004 and in spite of treatment in a French military hospital in Paris died on 11 November 2004, aged 75.

Medical records for Arafat said he died after suffering a stroke because of blood disorders. However, a French court opened a murder inquiry after high levels of radioactive polonium were found by a Swiss Institute on his clothing, which had been provided by his widow, Suha.

Arafat is buried in Ramallah on the West Bank in a tomb that was sealed off earlier this month. Once the former PLO leader's body is removed, scientists from France, Switzerland and Russia will each take samples, former Palestinian intelligence chief Tawfik Tirawi told the BBC.

No autopsy was carried out on Arafat when he died at the request of his widow, but she has since agreed to this exhumation to enable the Palestine Authority to find the truth about her husband's death, according to reports. Many Palestinians have long suspected that he was murdered by Israel, which has rejected such claims.

The exhumation is scheduled to take place on Tuesday.