Monday, August 14

Takriban watu 10 wazama baharini Lamu, Kenya

Takriban watu 10 wazama baharini Lamu, KenyaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionTakriban watu 10 wazama baharini Lamu, Kenya
Mgombeaji mmoja wa kiti cha Ubunge wa upinzani nchini Kenya ameokolewa kutoka bara hindi baada ya mashua alimokuwa akisafiria kuzama katika bara hindi maeneo ya Lamu.
Bwana Shekue Kahae alikuwa na familia yake , ambao bado hawajapatikana.
Kwa mujibu wa Kamishna wa Kaunti ya Lamu Joseph Kanyiri, mashua hiyo ilizama baada ya kukumbwa ma mawimbi makali ambayo kwa sasa yanakumba bahari hindi, maeneo ya lamu na viunga vyake. Aidha mawimbi hayo pia yametatiza shughuli za uokoaji .
Maafisa wa Polisi pamoja na wenyeji wa Lamu wenye uzoefu wa kuogelea wanasaidiana katika shughuli hiyo.
Ndio walimwokoa Bw Kahae, ambaye aligombea kiti cha Ubunge katika sehemu hiyo kwa chama cha Upinzani cha ODM na kushindwa katika uchaguzi mkuu uliofanyika Jumanne iliyopita.
Lakini familia yake ya watu 10 aliokuwa nao kwenye mashua hiyo iliyokumbwa na mkasa bado hawajapatikana, ila mwili mmoja tu. Shughuli za kuwatafuta wahanga wengine wa mkasa huo bado zinaendelea.
Hii ni ajali ya pili ya mashua kutokea kwenye sehemu hiyo kutokana na mawimbi makalia. Mnamo mwezi Juni, watu wanane waliaga dunia mashua yao ilipopinda na kuzama.

Wakenya waanza kurejea kazini baada ya uchaguzi

Mji wa Kisumu ulikumbwa na vurugu wiki iliyopita lakini leo watu wengi wameanza kurejea kazini
Image captionMji wa Kisumu ulikumbwa na vurugu wiki iliyopita lakini leo watu wengi wameanza kurejea kazini
Hali ya kawaida imeanza kurejea katika miji mingi nchini Kenya baada ya matokeo ya uchaguzi kutangazwa Ijumaa.
Watu wanaonekana kupuuza wito kwa kiongozi wa upinzani Raila Odinga wa kususia kazi leo kuomboleza watu waliouawa katika makabiliano kati ya polisi na waandamanaji waliokuwa wanapinga matokeo ya uchaguzi wa urais.
Wiki iliyopita, biashara nyingi zilifungwa watu wakihofia kuzuka kwa fujo kutokana na uchaguzi uliofanyika Jumanne.
Baadhi ya maeneo yakiwemo mitaa ya Mathare na Kibera jijini Nairobi na maeneo ya magharibi mwa Kenya yakiwemo Kisumu, Homa Bay na Migori.
Tofauti na hali ilivyokwa Ijumaa, biashara zimeanza kufunguliwa na magari ya uchukuzi wa abiria yameanza kufanya kazi katika barabara nyingi.
Baadhi ya wakazi mtaani Kibera wameambia BBC kwamba wanahitaji kufanya kazi kujipatia chakula na mahitaji mengine ya kimsingi.
Lakini wengine wameamua kutekeleza ushauri wa Bw Odinga na kususia kazi.
Bw Odinga, aliyewania urais kupitia muungano wa upinzani National Super Alliance (Nasa) amekataa kukubali matokeo ya uchaguzi yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (IEBC).
Rais Kenyatta alipata kura 8, 203, 290 ambayo ni asilimia 54.27 naye Bw Odinga akapata kura milioni 6,762,224 ambayo ni asilimia 44.74.
Muungano wa Nasa umedai mitambo ya tume ya uchaguzi ilidukuliwa na matokeo kuchakachuliwa kuhakikisha Bw Kenyatta anashinda.
Msimamo wa muungano huo unaenda kinyume na waangalizi wa kimataifa kutoka Umoja wa Afrika, Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Madola, miongoni mwa wengine, ambao walisema uchaguzi huo ulikuwa huru na wa haki.
Viongozi hao wa upinzani wamesema hawataenda kortini kupinga matokeo hayo.
Akiongea Jumapili katika mitaa ya Kibera na Mathare, Bw Odinga aliahidi kutangaza hatua zitakazochukuliwa na muungano huo Jumanne.
Nairobi
Image captionJijini Nairobi, wafanyakazi wengi wameanza kufungua biashara zao
Mjini Mombasa, biashara nyingi zimefunguliwa
Image captionMjini Mombasa, biashara nyingi zimefunguliwa

Kenyatta: Tunakaribisha ushirikiano na wapinzani wetu

Rais Kenyatta alimshinda mpinzani wake Raila Odinga kwa asilimia 54
Image captionRais Kenyatta alimshinda mpinzani wake Raila Odinga kwa asilimia 54
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta ametoa wito kwa wafuasi wa upinzani ambao hadi sasa wamepinga matokeo ya urais ya wiki iliyopita.
Bwana Kenyatta alimshinda mpinzani wake Raila Odinga kwa asilimia 54 ya kura lakini upinzani umetaja matokeo hayo kuwa yasiyo ya kweli
Jana Jumamosi kinara wa muungano upinzani nchini Kenya Raila Odinga, aliwashauri wafuasi wake kususia kazi leo Jumatatu kama njia ya kupinga matokeo ya uchaguzi uliofanyika Jumanne iliyopita.
Wafuasi wengi wa Bw Odinga walihudhuria mkutano huo uwanja wa Kamukunji mtaa wa Kibera, NairobiHaki miliki ya pichaEPA
Image captionWafuasi wengi wa Bw Odinga walihudhuria mkutano huo uwanja wa Kamukunji mtaa wa Kibera, Nairobi
Akihutubia wafuasi wake mtaani Kibera, Nairobi kwa mara ya kwanza kabisa tangu kutangazwa matokeo, ambapo Rais Uhuru Kenyatta alitangazwa mshindi, Bw Odinga alidai kuwa serikali ilikiwa imepanga kuwaua wafuasi wa upinzani kabla ya kutangazwa matokeo.
Hata hivyo Rais Kenyatta amesema kuwa wakenya wamekubali matokeo hayo na wenngi wamerudi kazini.
"Kwa marafiki ambao bado hawajakubali matokeo, tunaendelea kutoa wito kwao, tunaendelea kuomba ushirikiano wao. Ikiwa kuna wale wanaendelea kupinga, kuna njia za kikakatiba.
Shughuli za kawaida zimeanaa kurejea Nairobi
Image captionShughuli za kawaida zimeanaa kurejea Nairobi
Pia Kenyatta aliwataka polisi kujizuia lakini akaongeza kuwa serikali haitaruhusu kupotea kwa maisha na kuharibiwa kwa mali.
Waandshii wa BBC sehemu tofauti za nchi wanasema kuwa hali inaendelea kurejea kawaida sehemu nyingi.
Awali katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan, ambaye alikuwa mpatanishi mkuu baada ya mzozo wa kisiasa nchini Kenya miaka kumi iliyopita, alikuwa ametoa wito kwa Bw Odinga kutumia mifumo ya kisheria kutafuta haki kuhusu matokeo ya uchaguzi wa urais.

Zaidi watu 250 wameuawa kwenye maporomoko ya ardhi Sierra Leone

A picture of the mudslide
Image captionMaporomoko ya ardhi yafukia watu wengi Sierra Leone
Idadi ya watu waliouwa kwnye maporomoko ya ardhi nchini Sierra Leone haujulikani baada ya idaia tofauti kutolewa.
Shirika la habari la AP linasema kuwa takriban watu 250 wameuawa.
Eneo moja la milima liliporomoka mapema leo Jumatatu kufuatia mvua kubwa, na kusababisha nyumba nyingi kufukiwa kwa mjibu wa mwandishi wa habari wa BBC Umaru Fofana
Makamu wa rais nchini Sierra Leone Victor Bockarie Foh, alisema kuwa kuna uwezekano kuwa mamia ya watu wameuawa akiongeza kwa idadi ya watu waliouawa huenda ikaongezeka.
Mwandishi wa habari aliye eneo hilo anasema kuwa watu wemgi walipatwa wakiwa bado wamelala wakati maporomoko yalitokea.

RAIS WA MISRI AWASILI NCHINI NA KUPOKEWA NA MWENYEJI WAKE RAIS DKT. MAGUFULI



 Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi akishuka kwenye ndege mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.




 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpokea mgeni wake Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam. 






  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na mgeni wake Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.  



 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama na mgeni wake wake Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi wakati nyimbo za mataifa mawili ya Tanzania na Misri zikipigwa uwanjani hapo.



 Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi akikagua gwaride la Heshima mara baada ya nyimbo za Taifa kupigwa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere(JNIA) jijini Dar es Salaam.



Rais wa Misri Abdel Fattah Al Sisi akiangalia vikundi vya ngoma za asili mara baada ya kuwasili nchini. PICHA NA IKULU

Mbunge atumia Sh 1.8 bilioni jimboni kwake


Mbunge wa Mbarali mkoani Mbeya, Haroon Pirmohamed ametumia Sh1.851 bilioni kutekeleza miradi minne ya maendeleo kwa wananchi wa jimbo hilo.
Mbunge huyo ambaye ni mfanyabiashara mkubwa nchini, anayetumia kauli mbiu yake ya ‘Maneno kidogo, kazi zaidi’ amesema   leo Jumatatu mjini Rujewa kuwa amedhamiria kuwasaidia wananchi wa jimbo lake wanapokwama kwenye shughuli za   maendeleo kwa kutumia rasilimali alizonazo pamoja na fedha za mfuko wa jimbo.
Alisema katika awamu ya kwanza aligawa trekta ndogo maarufu kwa jina la Powertiller   115   na kila kijiji na mtaa ilipata powertiller moja kwa ajili ya kushughulikia shughuli za maendeleo eneo husika. Wilaya ya Mbarali ina vijiji 102 na mitaa 11.
Miradi mingine aliyoitoa ni kuchimba visima 10 vya maji kwa kata saba ambavyo vimegharimu Sh129 milioni, bati 4,000  zenye thamani ya Sh84 milioni na kila kata ilipata bati 200 kwa ajili ya ujenzi  wa vyoo kwa shule za msingi na sekondari.
“Katika awamu ya nne, hivi sasa nagawa msaada wa saruji mifuko 8,475 yenye thamani ya Sh105 milioni na kila kijiji na mtaa kitapata mgawo wa mifuko 75. Hii yote kwa ajili ya kufanyia shughuli za ujenzi mbalimbali kma vile shule, zahanati  na miradi mingine inayonekana kijiji husika,”alisema mbunge huyo.
Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Reuben Mfune alipongeza juhudi anazozionesha mbunge huyo katika kuwaletea wananchi wake maendeleo, shughuli ambayo ingefanywa na Serikali.

MCT yazindua ripoti ya uhuru wa habari nchini, uvamizi Clouds


Baraza la habari Tanzania(MCT) leo Jumatatu limezindua ripoti mbili juu ya hali ya uhuru wa habari pamoja na tukio la uvamizi wa Kituo cha Clouds Media.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu wa MCT, Kajubi Mukajanga amesema tafiti hizo zinafanywa kama inavyoelekezwa na katiba ya baraza hilo.
"Ripoti hizi mbili zinalenga kuangalia hali ya vyombo vya habari kwa mwaka uliopita kwa maana ya hali ya kiuchumi, sheria, usimamizi,mafanikio pamoja na changamoto,"amesema.
Kuhusu sakata la Clouds amesema lengo la utafiti wa tukio hilo ni kutaka kujua kama lilisababisha athari juu ya uhuru wa habari pamoja na uhuru wa uhariri na si vinginevyo.
"Tafiti zimekuwa zikifanyika tangu mwaka 2001. Wakati alipouawa David Mwangosi tulituma timu ya watafiti, vilevile Serikali ilipozuia matangazo ya Bunge tulifanya tafiti. Kwa hiyo huu ni mwendelezo wa kazi za baraza hili," amesema.
Amesema tafiti hizo zimehusisha timu ya wataalamu wa sheria, vyombo vya usalama pamoja na wanahabari.

DC Kibaha acharuka, atangaza kufuta hati za viwanja 1,000


Mkuu wa Wilaya ya Kibaha, Assumpter Mshama ametanga dhamira ya kufuta hati miliki za viwanja zaidi ya 1,000 vinavyomilikiwa na taasisi mbalimbali  zikiwemo benki na Idara za Serikali pamoja na watu binafsi wilayani humo.
Mshama alisema Serikali imedhamiria kufanya hivyo kwa sababu  wamiliki wake wameshindwa kuyaendeleza maeneo yao na kufanya mji huo kuzungukwa na vichaka na mapori  hivyo kusababisha kuenea vificho na matukio ya wahalifu.
Mshama amebainisha kuwa walishawakumbusha mara nyingi wahusika lakini kwa zaidi ya miaka mitatu sasa bado hawayaendelezi na hivyo yupo tayari kwenda mahakamani kutetea maendeleo ya Kibaha.
Ametaja idadi ya viwanja vilivyotelekezwa na kuwa mapori ni 1,080 ambapo kwa Kibaha mjini pekee ni viwanja 345 na Kibaha vijijini 735 huku kati ya hizo za taasisi na kampuni pekee ni 37.
"Hawa wote wamenunua ardhi Kibaha wametelekeza wameenda kujenga mikoani, hapa sisi wanatuachia vichaka na mapori na wahalifu wamegeuza maficho  hii haikubaliki, natoa siku 30 kila mwenye eneo aje aseme ana mpango gani sasa maana baada ya muda huo kama ajajenga tunafuta hati zao tunawapa wengine wenye nia,"alisema Mshama.

Mkuranga walilia walimu


Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga imeitaka Wizara ya  Elimu, Sayansi na Teknolojia kufanya mawasiliano na halmashauri ili kujua uhitaji wa walimu katika shule wilayani humo badala ya kugawa walimu katika maeneo yalio na idadi kubwa huku kukiwa na maeneo yenye idadi ndogo.
Akizungumza mbele ya Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako,  Mbunge wa Mkuranga(CCM), Abdalah Ulega amesema licha ya kuwepo kwa uhitaji wa walimu bado idadi ya walimu wanaoletwa katika wilaya hiyo huwa  wameelekezwa katika shule zenye utoshelevu.
"Tatizo hili ni kikwazo tena si katika elimu tu pia afya ambako kuna zahanati zina muhudumu mmoja wakati kuna maeneo yanahitaji kubwa," alisema.
Alisema Wilaya ya Mkuranga ni miongoni mwa maeneo nchini ambayo yana mwamko mdogo wa elimu huku kukiwa na idadi kuwa ya wahitimu ambao hawakufanya vizuri mitihani hivyo kutoendelea na masomo.
Mbunge huyo amemuomba Profesa Ndalichako kutimiza adhma ya muda mrefu ya wananchi kwa kusaidia ujenzi wa chuo cha mafunzo ya  ufundi (VETA) ili kuzalisha wataalamu wengi katika kuelekea nchi ya viwanda.
"Kwa kipindi kirefu baraza la madiwani liliadhimia  na tukaandaa na eneo kabisa tayari kwaajili ya ujenzi, hatutapenda kuona kuwa vijana wetu wanaenda kuwa manamba katika viwanda ambavyo vinaendelea kujengwa na kuboreshwa  kila kukicha badala ya  kuendeshe mitambo," alisema.

Lukuvi: Teknolojia changamoto upimaji wa ardhi


Morogoro.Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi ameitaja teknolojia kuwa changamoto kubwa katika mpango wa matumizi bora ya ardhi, hivyo kutoharakisha upangaji, upimaji na umilikishaji wa ardhi nchini.
Lukuvi ameyasema hayo leo Jumatatu mjini Morogoro alipokuwa akipokea rasimu ya mkakati wa kukabiliana na changamoto za matumizi bora ya ardhi nchini, iliyoainisha mapendekezo katika uandaaji, utekelezaji na usimamizi.
“Tunaweza kufikiri fedha si tatizo lakini teknolojia ni tatizo kubwa, kuna haya kwa mashirika yasiyo ya kiserikali na tushirikiane kuangalia ni teknolojia gani rahisi kupungua gharama za upimaji na upangaji wa ardhi vijijini badala ya kusubiri ndege za anga, hatuwezi ni gharama kubwa,” alisema Lukuvi.
Lukuvi aliyashauri mashirika hayo yanayounga mkono mpango huo kuangalia ni vifaa na nyenzo gani zinaweza kutumia ili kutekeleza mpango huo.
“Tunahitaji teknolojia rahisi ambayo hata ninyi mkiondoka Serikali inaweza kuhimili, hatupendi mtuambukize teknolojia ambayo itakuwa ni ngumu kwetu, kwa kuwa serikali inapopanga gharama kubwa zinajitokeza kwenye picha za anga na zile za chini,” alisema Lukuvi.
Alisema Serikali inapenda kuwa na uratibu wa haraka, ulio rahisi ambao wananchi wanaweza kupanga maeneo yao na kuongeza, lakini pia kuondokana na migogoro.
Mratibu wa Miradi ya Ardhi kutoka Oxfam, Naomi Shadrack alisema kupitia rasimu hiyo wadau wamefanya kazi kwa pamoja kuhakikisha sekta ya ardhi ambayo inatambuliwa na wengi wakiwemo  wakulima na wafugaji wadogo wadogo inafanyiwa kazi.
“Tungependa wadau mbalimbali washirikiane kuhakikisha  ardhi inapangwa na kila mtu anakuwa na uhakika wa ardhi, kupitia mpango mkakati huu tungependa  kujua Serikali imejidhatiti vipi katika bajeti, kuona ni jinsi gani inapanga kwa dhati pamoja na kukabili migogoro na changamoto mbalimbali,” alisema Naomi.

Makamba: Serikali haina nia ya kurudisha viroba


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), January Makamba amesema Serikali haina nia ya kurudisha sokoni pombe zilizotengenezwa katika mifuko ya plastiki 'viroba'na kuwataka Watanzania kupuuza uzushi unaoenezwa kwamba pombe hizo zitarudi.
Makamba alitoa kauli hiyo leo, Jumatatu Agosti 14 alipotembelea eneo la Kimara Temboni lilipo ghala la kuhifadhi pombe mbalimbali ikiwamo viroba linalomilikiwa na Kampuni Thema.
Makamba alisisitiza kwamba Serikali uamuzi wake wa kuzuia pombe hizo upo palepale na haujabadilika hivyo watu waache kupotosha wenzao.
"Baada ya kupiga marufuku kuna kampuni zilikuja ofisi kuomba kuongezewa muda, lakini tuliwakatalia na kuwaambia waheshimu uamuzi uliotolewa sasa hizi tetesi ya kwamba vinarudi sokoni sijui zinatoka wapi," alisema Makamba.
Makamba ambaye pia ni Mbunge wa Bumbuli amesema  njia ya pekee kwa wafanyabiashara hao wa viroba wanaotakiwa kuifanya ili kupunguza hasara ni kubadilisha pombe hizo na kuziweka katika chupa zenye ujazo unaotakiwa.
Amesema kamwe Serikali haiwezi kurudi nyuma na kwamba mafanikio yameanza kuonekana kutokana na hatua hiyo.

Mashamba 14 yafutwa Morogoro


Rais John Magufuli amefuta mashamba pori 14 yaliyokuwa yanamilikiwa na watu mbalimbali akiwemo mke wa waziri mkuu wa zamani Fredirick Sumaye na mfanyabiashara Jitu Patel.
Akitoa taarifa ya kufutwa kwa mashamba pori hayo kwa niaba ya Rais Magufuli, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wiliam Lukuvi alisema kuwa mashamba hayo yamefutwa kutokana na wamiliki wake kushindwa kulipa kodi ya  ardhi na kuyaendeleza.
Lukuvi aliwaonya viongozi wanaotaka kujipenyeza kuchukua maeneo kwenye mashamba hayo na hivyo kumtaka mkuu wa mkoa na wakuu wa wilaya kusimamia kikamilifu zoezi la ugawaji wa maeneo ya mashamba hayo.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Stephen Kebwe amewataka wananchi kutovamia mashamba hayo yaliyofutwa badala yake wasubiri utaratibu wa kuyagawa.

Ikulu yagoma kulipa mabilioni ya zabuni licha ya hukumu ya mahakama


Hatimaye Ikulu imesema hailitambui deni la Sh1.6 bilioni ambalo Serikali inadaiwa na kampuni ya GBL and Associates Ltd ya jijini Dar es Salaam baada ya kuinyang’anya zabuni ya kununua na kuuza meno ya tembo iliyoshinda miaka 29 iliyopita.
Uamuzi huo umetolewa licha ya kuwapo hukumu ya Mahakama Kuu inayoeleza wazi kwamba Serikali ilikosea kuifutia kampuni hiyo zabuni iliyoshinda bila sababu za msingi.
Nyaraka zinaonyesha kuwa madai ya GBL yaliwahi kufika mezani kwa marais wastaafu Ali Hassan Mwinyi na Jakaya Kikwete ambao waliagiza wasaidizi wao kutafuta ukweli juu ya suala hilo. Tawala hizo zilizopita zilikwishatoa maagizo kampuni hiyo ilipwe.
Mgogoro kati ya Serikali na GBL ulianza mwaka 1988 baada kuinyang’anya zabuni ya kununua tani 16 za meno ya tembo licha kutangazwa mshindi wa mchakato huo na Wizara ya Ardhi, Maliasili na Utalii.
Kwa mujibu wa tangazo la zabuni lilitolewa katika gazeti la Serikali la Daily News la Februari 29, 1988 kupitia Bodi ya Taifa ya Zabuni, mshindi wa zabuni hiyo alitakiwa kufanya malipo yote na kukusanya meno hayo ndani ya siku 30 tangu siku ya kukabidhiwa barua ya ushindi.
Hata hivyo, kabla siku hizo 30 hazijatimia, aliyekuwa kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyapori anayetajwa kwa jina la A. Malemaro alimwandikia mmiliki wa kampuni hiyo marehemu Gabriel Lugendo kumjulisha uamuzi wa Serikali kuifutia kampuni yake zabuni kwa kushindwa kulipa fedha ndani ya siku saba, jambo lililozua madai ya muda mrefu.
GBL iliomba zabuni hiyo ikishirikiana na Taathing Ivory Wares ya Hong Kong ambayo ilikwishakopa benki kukamilisha biashara hiyo. Baadaye Serikali ililazimika kurudisha fedha ambazo kampuni hiyo ililipa.
Jaji wa Mahakama Kuu, Yahaya Rubama aliwahi mwaka 1989 kuamua kuwa uamuzi wa kuifutia zabuni hiyo GBL haukuwa wa haki na uvunjwaji wa mkataba.
Awali, kampuni hiyo ilidai Sh507 milioni ambazo ziliongezeka na kufikia Sh4 bilioni pamoja na riba. Hata hivyo, deni hilo lilipunguzwa hadi Sh1.6 bilioni baada ya makubaliano kati ya Serikali na GBL.
Aprili mwaka huu, Katibu Mkuu Kiongozi John Kijazi aliiandikia GBL akiijulisha kuwa Ikulu imepitia malalamiko yake ikiwamo viambatanisho vyake na hitoria ya suala hilo na kuridhika kwamba madai hayo hayana msingi wa sheria.
Balozi Kijazi anasema Ikulu imeridhika kuwa kampuni hiyo ilifutiwa zabuni ya mauzo ya meno ya tembo kwa kushindwa kulipa ndani ya wakati yaani ndani ya siku saba baada ya kupokea barua ya kuarifiwa ushindi wa zabuni.
Kwa mujibu wa barua ya Kijazi ya Aprili 20, kampuni hiyo haikuwa mnunuzi halisi wa meno hayo ila kampuni ya Ms Tathing Ivory Factory ya Hong Kong ambayo hatimaye ililipia meno hayo na fedha hizo baadaye kurejeshwa kwa kampuni hiyo baada ya GBL kufutiwa zabuni.
Anasema ilibainika pia kuwa kwa mujibu wa Mkataba wa Kimataifa wa Biashara ya Wanyama na Mimea iliyo Hatarini Kutoweka (Cites), kampuni ya Ms Tathing Ivory Factory haikuwa na sifa ya kufanya biashara ya meno ya tembo na nchi zilizosaini mkataba huo, ikiwamo Tanzania.
Hata hivyo, Mkurugenzi Mtendaji wa GBL Thomas Lugendo alisema katika barua yake ya Mei 24 kuwa, Ikulu haijafuata sheria, kanuni na taratibu za nchi kwa kuwataka kulipa fedha ndani ya siku saba wakati tangazo la zabuni lilitoa siku 30.
“Ikulu inasema tumeshindwa kulipa ndani ya siku saba lakini tangazo la zabuni lilitoa siku 30. Kutuambia tulipe ndani ya siku saba ni kinyume na tangazo la zabuni. Hatukuafiki na hata Rais wa Awamu ya Pili Ali Hassan Mwinyi hakuafiki,” anasema Thomas Lugendo.
Kuhusu madai kuwa kampuni hiyo haikuwa mnunuzi halisi wa meno hayo isipokiwa kampuni ya Taathing Ivory Wares Factory, Lugendo anasema: “Hili ni jambo ambalo isingekuwa vyema kulijibu kwa heshima ya Serikali,” anasema Thomas huku akirejea maneno ya Jaji Rubama.
Jaji Rubama alisema katika hukumu yake: “Katika mwenendo wa biashara za kimataifa, zinazotembea ni karatasi za mikataba. Mimi nimeshinda tenda, nauza kwa mtu mwingine, yule wa mwisho ndiye anabeba mzigo wa fedha ambaye kwa hapa ni kampuni ya Taathing.”
Kuhusu kampuni ya Taathing Ivory Factory kutokuwa katika nchi ambayo ni mwanachama wa Cites, Lugendo alimtaka Balozi Kijazi kurejea tangazo la zabuni lililosema waomba zabuni kutoka nchi wanachama na siyo kampuni zinazonunua.
“Sisi ni Watanzania, maombi yetu yametoka Tanzania kule tutakouzia Serikali haihusiki, hata kama tungechukua meno ya tembo tukayahifadhi kama mapambo yetu. Serikali ilishauza inahusika nini baada ya kuyauza?” alihoji Lugendo.