Sunday, September 10

China katika mipango ya kupiga marufuku magari yanayotumia mafuta

Heavy air pollution above cars driving in BeijingHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionChina katika mipango ya kupiga marufuku magari yanayotumia mafuta
China ambaye ni nchi yenye soko kubwa zaidi la magari ina mipango ya kupiga marufuku uundaji na uuzaji wa magari yanayotumia mafuta ya diesel na petroli
Naibu waziri wa viwanda nchini humo alisema wameanaa utafiti lakini badoo hawajaamua ni lini marufuku hiyo itaanza kutekelezwa.
"Hatua hizo bila shaka zitalea mabadiliko makubwa katika sekta yetu ya magari," alisema Xin Guobin.
China iliunda magari milioni 28 mwaka uliopita, takriban thuluthi moja ya magari yote yaliyoundwa duniani.
Volvo car, Shanghai Auto ShowHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionKampuni ya kichina ya kuunda magari ya Volvo, ilisema mwezi Julai kuwa magari yake yatatumia umeme ifikapo mwaka 2019.
Uingereza na Ufaransa tayari wametangaza mipango ya kupiga marufuku magari mapya yanayotumia mafuta ya diesel na petroli ifikapo mwaka 2040 kama sehemu ya njia za kuzuia uchafuzi wa hewa.
Kampuni ya kichina ya kuunda magari ya Volvo, ilisema mwezi Julai kuwa magari yake yatatumia umeme ifikapo mwaka 2019.
Makampuni mengine duniani yakiwemo Renault-Nissan, Ford na General Motors yote yanashughulikia mipango ya kuunda magari yanayotumia umeme.

Amnesty:Burma yatega mabomu ya ardhini kuwazuia Rohingya

Vikosi vya usalama BurmaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionVikosi vya usalama Burma vyasema vinapambana na wanamgambo
Amnesty International linasema lina ushahidi kuwa vikosi vya usalama Myanmar vimetega mabomu ya ardhini yaliopigwa marufuku katika mpaka na Bangladesh.
Hilo ni eneo ambako idadi kubwa ya waislamu wa Rohingya wanatoroka ghasia.
Shirika hilo la kimataifa la kutetea haki za binaadamu linasema raia wapatao watatu wamejeruhiwa kwa milipuko hiyo ya kutegwa ardhini katika wiki iliyopita, na inaarifiwa mwananmume mmoja aliuawa.
Watu walioshuhudia wameliambia shirika hilo kwamba waliwaona maafisa wa usalama wa Burma wakitega mabomu hayo.
Umoja wa mataifa unasema zaidi ya waislamu laki mbili na nusu wa Rohingya wametoroka Myanmar tangu jeshi lianze operesheni dhidi ya wanamgambo huko wiki mbili zilizopita.
Shirika la Umoja wa mataifa linalowashughulikia wakimbizi UNHCR linasema idadi hiyo imeongezeka baada ya ukaguzi wa kina wa maeneo ambayo awali hayakujumuishwa katika hesabu.
Waislamu wengi wa Rohingya wametembea kwa siku kadhaa wakipitia jangwani na milimani .
Baadhi wamepanda maboti wakivuka bahari ya Bengal.

Wapiganaji wa Rohingya watangaza kusitisha mapigano, Myanmar

Wa Rohingya wanaishutumu jeshi la Myanmar kwa kuteketeza vijiji vyao - Lakini utawala nchini Myanmar, unasema wanajeshi wake wanakabiliana na "magaidi"Haki miliki ya pichaEPA
Image captionWa Rohingya wanaishutumu jeshi la Myanmar kwa kuteketeza vijiji vyao - Lakini utawala nchini Myanmar, unasema wanajeshi wake wanakabiliana na "magaidi"
Katika taarifa nyingine Asubuhi hii ya leo, waasi wa kiislamu wa kabila la Rohingya nchini Myanmar wametangaza upande mmoja makubaliano ya kusitisha mapigano leo Jumapili, ili kujaribu kupunguza mgogoro wa kibinadamu magharibi mwa taifa hilo.
Mashambulio dhidi ya jeshi la taifa hilo yanayotekelezwa wapiganaji wa Arakan Rohingya Salvation Army, yalisababisha mapigano makali ya wiki mbili, ambapo zaidi ya watu laki tatu wa jamii ndogo ya Warohingya wamekimbilia nchi jirani la Bangladesh.
Image caption
Kundi hilo la waasi, yameiomba jeshi la nchi hiyo pia kuitisha wito wa kusitisha mapigano, huku likiomba mashirika ya utoaaji misaada ya kibinadamu kurejelea kazi zao za kusambaza misaada.
Waziri mmoja wa serikali ya Myanmar ameiambia BBC kuwa, wengi wa Wa-Rohingya waliokimbia nchi hiyo na kuelekea Bangladesh, hawataruhusiwa kamwe kurejea Myanmar.

Mugabe aagiza usajili mpya wa wapiga kura Zimbabwe

MugabeHaki miliki ya pichaREUTERS
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameagiza usajili mpya wa wapiga kura wakati nchi hiyo inajitayarisha kwa uchaguzi mkuu mwaka ujao.
Chini ya agizo jipya la serikali, raia wote Zimbabwe watakuwana miezi minne kujisajili upya katika daftari la usajili.
Zimbabwe itafanya uchaguzi mkuu mwaka ujao kwa kutumia dafatri hiyo mpya ya usajili wa wapiga kura , ikiwa ni mojawapo tu ya mageuzi ya uchaguzi yalioitishwa na upinzani kwa muda mrefu.
Agizo hilo la rais linasema usajili unapaswa kuanza September 14 hadi Januari mwaka ujao.
Mfumo huu mpya unaidhinishwa kwa kutumia vifaa vilivyonunuliwa hivi karibuni kutoka China.
Usajili utajumuisha kunakiliwa alama za vidole na ithibati ya ukaazi.
Dafatari hilo la usajili limekumbwa na mzozo katika uchaguzi wa siku za nyuma Zimbabwe.
Mnamo 2008 vyama vya upinzani vilisema waligundua makosa ikiwemo kusajiliwa kwa wapiga kura wengi waliokuwa wanasemekana kuishi katika eneo moja, na wengine katika maenoe yasioishi watu.

Miili iliyohifadhiwa kwenye kaburi karne ya 16 yagunduliwa Misri

An Egyptian antiquities worker works on a coffin in the recently discovered tomb of Amenemhat, a goldsmith from the New Kingdom, at the Draa Abu-el Naga necropolis near the Nile city of LuxorHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMiili iliyohifadhiwa kaburini karne ya 16 yagunduliwa Misri
Wana akiolojia wamegundua kaburi lenye miili ya mwanmke na watoto wake waliokuwa wamehifadhiwa karne kadhaa zilizopita.
Kaburi hilo linaloaminika kuwa la karne ya 16 hadi 11 BC lilipatikana karibu na mji wa Luxor kilomita 70 kutoka Cairo.
Kati ya vifaa vilivyo patikana ndani ya kaburi hilo ni sanamu ya mfua viuma Amenemhat akiketi kando na mke wake.
Egyptian archaeologists work on mummies at a recently discovered tomb in the Draa Abul Nagaa necropolis, Luxor's West Bank, 700km south of Cairo, Egypt, 9 September 2017Haki miliki ya pichaEPA
Image captionKaburi lilipatikana eneo la Draa Abul Naga
Kulingana na wana akiolojia mama alifariki akiwa na miaka 50, na uchunguzi ulionyesha kuwa alifariki kutoka na ugonjwa wa mifupa.
Watoto wawili wa kiume walikuwa na umri wa kati ya miaka 20 na 30 na walikuwa wamehifadhiwa katika hali nzuri,
Skulls and hands are seen next to coffin in the recently discovered tomb of Amenemhat, a goldsmith from the New Kingdom, at the Draa Abu-el Naga necropolisHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMiili hiyo ilitajwa kuwa katika hali nzuri
A carved sandstone statue depicting the tomb's owner Amenemhat sitting on a high back chair beside his wife at a recently discovered tomb in the Draa Abul Nagaa necropolis, Luxor's West Bank, 700km south of Cairo,Haki miliki ya pichaEPA
Image captionKati ya vifaa vilivyo patikana ndani ya kaburi hilo ni sanamu ya mfua viuma Amenemhat akiketi kando na mke wake.
Egyptian antiquities worker brushes a coffin in a recently discovered tomb of Amenemhat, a goldsmith from the New Kingdom at the Draa Abu-el NagaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMiili iliyohifadhiwa kaburini karne ya 16 yagunduliwa Misri

Upepo na mvua kali za kimbunga Irma zaipiga Cuba

Kimbunga Irma CubaHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionUpepo mkali umevunja paa za majengo Remedios, Cuba
Kiwango kamili cha uharibifu unaotokana na kimbunga Irma huko Cuba bado hakijulikani lakini hakuna shaka kuwa kimbunga hicho kimepiga miji na vijiji vilivyopo kaskazini mwa pwani ya kisiwa hicho.
Wakati mvua kubwa ilipoanza kunyesha bado kilikuwa ni kimbunga chenye uzito wa daraja la tano,ni mara ya kwanza kimbunga kikubwa kiasi hicho kupiga katika eneo hilo katika muda wa zaidi ya miaka 80.
Kumekuwa na taarifa za mawimbi makubwa yaliopiga na kuvunja kuta baharini hususan katika kijiji kunakofanyika uvuvi Caibarien.
Ukisogea zaidi katika pwani kwenye jimbo la Camaguey, watu wengi wanakabiliwana ukosefu wa umeme na usafiri umetatizika kuelekea maeneo ya nje.
Kimbunga Irma kikiandamana na upepo mkali.Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionKimbunga Irma kikiandamana na upepo mkali.
Mawasiliano pia yamekatizwa kwa ukubwa katika nchi ambayo tayari ilikuwa inakabiliwana matatizo ya miundo mbinu kwa upande wa mawasiliano kabla ya kuwasili kwa kimbunga hicho.
Baadhi ya maeneo makuu ya kitalii pia yapo katika eneo la pwani na kila jengo kuanzia hoteli za kifahari hadi vijumba vidogo vimejipata katikati ya njia inayopita kimbunga Irma.
Iwapo uharibifu unaoshuhudiwa katika maeneo mengine ya visiwa vya Caribbean ni wa kweli, raia wengi wa Cuba wanahofia hali mbaya mno.
Huenda kimbunga hicho kikaendelea katika eneo linalozunguka Cuba kwa saa kadhaa kabla ya kugeuza muelekeo kurudi baharini na kuelekea kusini mwa Marekani.

Polisi Tanzania kuwasaka waliotaka kumuua Tundu Lissu

Mkuu wa Jeshi la Tanzania
Image captionMkuu wa Jeshi la Tanzania
Mkuu wa Jeshi la Polisi Simon Sirro amesema kuwa wametuma kikosi cha ziada polisi wa upelelezi mjini Dodoma kuchunguza na kuwatafuta wahalifu.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Mkuu wa Jeshi la Polisi Simon Sirro amesema kuwa wametuma kikosi cha ziada polisi wa upelelezi mjini Dodoma kuchunguza na kuwatafuta wahalifu waliotekeleza shambulio la mwanasheria wa chama cha upinzani CHADEMA Tundu Lissu siku ya Alhamisi.
Kamanda Sirro amekanusha tetesi ya kuwa waliomshambulia mbunge huyo walikuwa wanahusika na polisi.
"Suala la sare za washukiwa kufanana na za jeshi la polisi" Kamanda Sirro amenukuliwa akisema "kinachofanya uhalifu sio sare, Kinachofanya uhalifu ni mtu anayetekeleza tukio. Nguo za jeshi la polisi Tanzania zinafanana na nguo nyingi za makampuni binafsi lakini siyo hoja kwamba polisi wetu wanahusika. Kwa hiyo jambo la msingi tunawatafuta waliotekeleza tukio hilo."
Hivi karibuni, mbunge Tundu Lissu kutoka chama cha upinzani cha CHADEMA, amekuwa akikamatwa mara kwa mara na jeshi la polisi akishutumiwa kufanya uchochezi.
Kamanda Sirro amelizungumzia suala hilo "Tunamkamata kamata Tundu Lissu kutokana na matendo yake na kutokana na sheria yenyewe."
Ikumbukwe kwamba Tundu Lissu alipigwa risasi na watu wasiojulikana Mjini Dodoma, katikati mwa Tanzania siku ya Alhamisi, na baadaye kupatiwa matibabu katika hospitali kuu ya Mkoa wa Dodoma na kisha kusafirishwa hadi mjini Nairobi, katika hospitali ya Nairobi kwa matibabu zaidi.

Takriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico

Aerial shot of damages housing reduced to rubble in Ixtaltepac, OaxacaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico
Takriban watu 90 wameuwa kufuatia tetemeko la ardhi la uzito wa 8.1 katika vipimo vya richa nchini Mexico kwa mujibu wa maafisa.
Msemaji wa serikali alisema kuwa watu 71 walikuwa wameuawa katika jimbo lililo kusini magharibi la Oaxaca.
Mamia ya familia zimeripotiwa kushinda katika mitaa, zikihofia hatari za mitetemeko midogo.
Wanajiolojia nchini Mexico wanasema kuwa mitetemeko midogo 721 imerekodiwa tangu tetemeo kubwa la Alhamisi.
Tetemeko hilo lilikuwa la nguvu nyingi zaid kuwai kushuhudiwa nchini humo kwa karne moja.
Siku ya Ijumaa, pwani ya mashariki mwa Mexico ilikumbwa na dhoruba inayojulikana kama Katia.
Watu wawili walifariki kwenye maporoko ya udongo baada ya mvua kubwa.
Mudslide with house on top of an embankmentHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico
A police tape ropes off area where people died in mudslideHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico
Rescuers and army workers search in rubble in JuchitanHaki miliki ya pichaEPA
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico
Injured people in hospital bedsHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico
Women work at stall providing aidHaki miliki ya pichaAFP
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico
Mourners crying at a funeralHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico
People search rubble for their belongings in clean-up operationHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico
Man surveys damage to collapsed housesHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico
People sort through stockpilesHaki miliki ya pichaAFP/GETTY
Image captionTakriban watu 90 wauawa kwenye tetemeko la ardhi Mexico