Saturday, November 18

ZANU PF yamshinikiza Mugabe ajiuzulu

Chama tawala Zimbabwe ZANU PF kimemtaka Rais Robert Mugabe ajiuzulu. Gazeti la Herald limeandika kuwa matawi ya chama hicho katika majimbo yote10 yalikutana Ijumma na yamemtaka Mugabe na mke wake Grace wajiuzulu.

Simbabwe Harare Robert Mugabe (picture-alliance/AP Photo/B. Curtis)
Viongozi wa chama hicho wamesema watamshinikiza kiongozi huyo ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 1980 kuondolewa kutoka uongozi wa chama hicho ifikapo hapo kesho Jumapili, na baada ya hilo, bunge litapiga kura ya kutokuwa na imani naye.
Chama cha ZANU PF kitafanya mkutano maalamu wa kamati kuu siku ya Jumapili kujadili yanayojiri kisiasa nchini humo.
Mugabe alionekana kwa mara ya kwanza hadharani, katika mahafali ya chuo kikuu mjini Harare siku ya Ijumaa (17.11.2017) tangu jeshi lilipomuweka chini ya kifungo cha nyumbani wiki hii. Mkewe Grace hajaonekana hadharani tangu jeshi lilipochukua madaraka.
Jeshi la Zimbabwe linapata ugumu wa kuonyesha heshima kwa kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 93 kwa kumuita rais na kamanda mkuu wa jeshi.
Madaraka mikononi mwa Jeshi
Taarifa kutoka kwa jeshi hilo imesema kuwa viongozi wake wanashauriana na Kamanda Mkuu wa jeshi Rais Robert Mugabe kuhusu njia bora ya kusonga mbele na litalifahamisha taifa baadaye kuhusu matokeo hayo haraka iwezekanavyo.
President Robert Mugabe poses with General Constantino Chiwenga at State House in Harare (Reuters/Zimpapers/J. Nyadzayo)
Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe na mkuu wa majeshi Constantino Chiwenga
Kituo cha televisheni cha serikali ZBC kimeripoti kuhusu kuendelea kwa shinikizo kutoka kwa wanachama wa ZANU PF kwa Mugabe kujiuzulu. ZBC imekuwa ikitumika na serikali ya Mugabe kwa miongo kadhaa kueneza propaganda.
ZANU PF pia imeitisha maandamano Jumamosi (18.11.2017) katika mji mkuu, Harare kuliunga mkono jeshi kwa kuchukua madaraka na kumshinikiza Mugabe ajiuzulu. Gazeti la Herald limeripoti kuwa chama hicho kinataka makamu wa Rais aliyefutwa kazi Emmerson Mnangagwa arejeshwe katika wadhifa huo kwasababu alifutwa kazi bila ya ridhaa ya kamati kuu ya chama hicho.
Wazimbawe wengi wanahisi mipango ya jeshi ni kumkabidhi Mnangagwa madaraka. Huenda viongozi wa kijeshi wanasubiri Mnangagwa ambaye anajulikana kwa jina maarufu kama mamba arejeshwe katika wadhifa wa makamu wa rais kabla ya kumshinikiza Mugabe kuondoka madarakani kwa njia ya amani.
Mugabe anaheshimika sana kama kiongozi aliyepigania uhuru lakini pia wengi wanamuona kama Rais aliyeivuruga nchi yake kwa kusalia madarakani kwa muda mrefu.
Mugabe ameiongoza Zimbabwe tangu 1980
Uchumi wa nchi hiyo umeporomoka vibaya, visa vya ufisadi, usimamizi mbaya, azma ya mke wake Grace kutaka kurithi madaraka na umri wake kuwa mkubwa ni mambo yanayowafanya Wazimbabwe kuhisi hana uwezo tena wa kuliongoza taifa hilo.
Zimbabwe Mugabe Rally (picture-alliance/AP Photo/T.Mukwazhi)
Mugabe na mke wake Grace
Rais wa Botswana Ian Khama amemtaka ajiuzulu akisema hadhani kama kuna mtu yeyote anayestahili kuwa madarakani kwa muda mrefu kama Mugabe akiongeza wao ni marais na sio wafalme.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma ambaye aliongoza kikao cha viongozi wa jumuiya ya ushirikiano wa maendeleo wa nchi za Kusini mwa Afrika SADC mjini Gaberone, Botswana amesema wanafuatilia kwa wasi wasi mkubwa matukio ya kisiasa yanayojiri Zimbabwe na anatumai hayatasababisha kuingia madarakani kwa utawala usiotambulika kikatiba.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Rex Tillerson aliwaambia mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za Afrika wanaohudhuria mkutano mjini Washington kuwa anahimiza kurejea haraka kwa utawala wa kiraia Zimbabwe akisema nchi hiyo ina fursa ya kuanzisha njia mpya ambayo sharti ihusishe chaguzi zinazoendeshwa kwa njia ya kidemokrasia na kuheshimu haki za binadamu. China imesema inatumai kuwa hali ya kisiasa inayoendelea Zimbabwe itasuluhishwa kuambatana na sheria na uthabiti uterejea nchini humo.

Fedha na mgawanyiko vyakwamisha COP23

Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya tabianchi unaojulikana kama COP23, umekamilika rasmi jana mjini Bonn, Ujerumani, baada ya wajumbe kukutana kwa muda wa wiki mbili.

COP23 in Bonn - PK Bangladesch (DW)
Wajumbe wa mkutano huo wamekuwa wakifanya vikao mbalimbali vya kutunga sheria zitakazotumiwa katika utekelezwaji wa Mkataba wa Paris, unaonuia kupunguza ongezeko la joto duniani.
Mazungumzo hayo yaliyotakiwa kumalizika jana mchana, yaliendelea hadi saa sita usiku kwa saa za Afrika Mashariki, huku mjumbe mkuu wa China, Xie Zhenhua akisema kwamba kuna masuala mengi ambayo bado yanapaswa kujadiliwa. Wajumbe wa mkutano huo wamesema mazungumzo yamekwama hasa katika masuala makuu mawili likiwemo kuhusu fedha pamoja na kuibuka tena mgawanyiko kati ya mataifa tajiri na yale yanayoendelea.
Mataifa maskini duniani ambayo ndiyo yanayokumbwa zaidi na madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi, yanahitaji fedha ili kujiimarisha zaidi katika kujiandaa na kujilinda na athari mbaya za mabadiliko ya tabianchi.
COP23 | Kaliforniens Governeur Jerry Brown (Getty Images/Lukas Schulze)
Gavana wa Marekani, Jerry Brown
Mataifa hayo yanataka uhakika na uwazi zaidi kutoka katika mataifa tajiri kuhusu maendeleo yaliyopatikana ili kutimiza ahadi yao ya kuchangia hadi Dola bilioni 100 kwa mwaka ifikapo mwaka 2020, kama sehemu ya mkataba wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchini.
Marekani chini ya Utawala wa Rais Donald Trump ambayo pia imepunguza ufadhili katika taasisi na miradi inayohusiana na mabadiliko ya tabianchi, imekuwa na misimamo mkali kawenye majadiliano ya kifedha, hatua iliyowakasirisha wajumbe wengi. Mjumbe wa ngazi ya juu wa Ulaya, Jens Mattias Clausen amesema serikali ya Trump ilishindwa kuzuia mazungumzo hayo yasifanyike, lakini hatua hiyo inaweza ikawa imechelewesha mambo. Amesema dunia inahitaji kuchukua hatua haraka.
Mazungumzo yamepiga hatua
Muda mchache kabla ya kumalizika kwa mkutano huo, Waziri Mkuu wa Fiji, Frank Bainimarama amewaambia wanadiplomasia kwamba wanapiga hatua nzuri kuhusu mkataba wa Paris na wataikamilisha kazi hiyo kwa wakati. Bainimarama ambaye aliongoza mazungumzo hayo, alikabiliwa na changamoto ngumu ya kuzipatanisha pande zinazopingana za nchi tajiri na maskini, hasa linapokuja suala la kila upande kufanya juhudi katika kuzuia mabadiliko ya tabianchi.
Wajumbe kutoka karibu nchi 200, wakiwemo wa Marekani, walikusanyika kuandaa sheria muhimu zitakazoidhinishwa mwaka ujao wa 2018 mjini Katowice, Poland kwa ajili ya kuutekeleza Mkataba wa mabadiliko ya tabianchi uliofikiwa mjini Paris, Ufaransa mwaka 2015 na ambao unatarajiwa kuanza rasmi katika muda wa miaka mitatu ijayo.
UN-Klimakonferenz 2017 in Bonn | Angela Merkel, Bundeskanzlerin (Reuters/W. Rattay)
Kansela Angela Merkel akihutubia mkutano wa COP23
Nchi zilizosaini mkataba wa Paris zinataka kupunguza ongezeko la joto duniani hadi chini ya nyuzi joto 2 za Celsius ifikapo mwishoni mwa karne. Lengo hilo halitafanikiwa mpaka nchi hizo zifanye juhudi zaidi katika kupunguza hewa chafu ya carbon inayosababishwa hasa na matumizi ya nishati inayotokanayo na vitu asilia.
Ujerumani kwa upande wake inalenga kupunguza matumizi ya gesi inayochafua mazingira kwa asilimia 40 ifikapo mwaka 2020. Serikali iliamua kuhusu namba hiyo miaka 10 iliyopita, lakini inaonekana kama mpango huo utashindikana. Kulingana na utabiri wa sasa uliotolewa na wizara ya Mazingira ya Ujerumani, nchi hiyo itakuwa na uwezo wa kupunguza matumizi ya gesi hiyo kwa asilimia 34.7 ifikapo mwka 2020.
Desemba 12 mwaka huu, Rais wa Ufaransa, Emmanuel Macron amewaalika zaidi ya viongozi 100 mjini Paris kuadhimisha miaka miwili tangu ulipofikiwa mkataba wa Paris. Trump anayetaka kujiondoa kwenye mkataba huo, hajaalikwa katika mkutano huo wa kilele uliopewa jina ''One Planet''.

Hariri afunguka kuhusu ziara yake Saudia

Waziri Mkuu wa Lebanon Saad Hariri akiwa na Mrithi wa Ufalme nchini Saudi Arabia Mohammed bin Salman.
Waziri Mkuu wa Lebanon Saad Hariri amesema Ijumaa amekuwa Saudi Arabia, ambako alikuwa katika mazungumzo yanayohusu mustakbali wa eneo hilo.
Vyanzo vya habari vimeripoti Hariri aliushitua ulimwengu kwa kutangaza kujiuzulu kwake akiwa nje ya nchi yake.
“Kuwepo kwangu Saudi Arabia ni kwa ajili ya kufanya mashauriano juu ya mustakbali wa Lebanon na mahusiano yake na nchi jirani za Kiarabu,” aliandika katika akaunti yake ya Twitter kabla ya kuanza safari yake kuelekea Ufaransa.
Hariri aliongeza kuwa taarifa nyingine zozote kuhusu uwepo wake Riyadh, kuondoka kwake Lebanon au kuhusu familia yake ni “uzushi”.
Hariri amekuwako nchini Saudi Arabia tangu alipotangaza kujiuzulu mapema mwezi huu, akiibua maswali kuhusu ukweli juu ya kushikiliwa kwake Saudia na kupelekea Rais wa Lebanon Michel Aoun kutangaza kuwa anazuiliwa na utawala huo.
Aoun amesema hatakubali kupokea rasmi kujiuzulu kwa Hariri mpaka atapofika Lebanon.
Waziri wa Mambo ya Nje Adel al- Jubeir Alhamisi alitupilia mbalia madai yasiyo na msingi kuwa Saudi Arabia ilikuwa inamshikilia Hariri na ni juu ya Hariri mwenye kuamua wakati gani anataka kuondoka.
Hariri amekubali mualiko wa Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kwenda Ufaransa katika siku zijazo.

Tillerson ahimiza utawala wa kiraia Zimbabwe

Rais Robert Mugabe akiwa na Jenerali Constantino Chiwenga ikulu mjini Harare, Zimbabwe, Novemba 16, 2017.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Rex Tillerson ametoa wito Ijumaa Zimbabwe kurejea katika utawala wa kiraia.
Shirika la habari la AP limeripoti kuwa Tillerson amesema Zimbabwe bado inayofursa ya kuanza "utaratibu mpya" wakati kuna dalili kuwa uongozi wa mabavu wa Robert Mugabe utalazimishwa kuachia madaraka katika mapinduzi yaliyofanyika bila ya kumwaga damu.
"Sisi sote lazima tushirikiane ili kurejesha kwa haraka utawala wa kiraia katika nchi hiyo kwa mujibu wa katiba, Tillerson aliuambia mkusanyiko wa mawaziri wa mambo ya nje na wanadiplomasia waliokusanyika Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani.
Amesema ni lazima Zimbabwe ifanye uchaguzi uliyo huru na haki. Mugabe alishinda katika chaguzi zilizopita ambazo wasimamizi waliokuwepo wakati wa uchaguzi huo waligundua kuwa ulivurugwa.
“Mwisho wa yote wananchi wa Zimbabwe ni lazima wapewe fursa ya kuchagua serikali yao,” aliongeza
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ameonekana Ijumaa hadharani kwa mara ya kwanza leo Ijumaa, tangu jeshi la nchi hiyo kumzuilia nyumbani kwake siku ya Jumatano, kuchukua udhibiti wa taasisi za serikali na kuanziisha mazungumzo yanayotarajiwa kumruhusu baba wa taifa kustahafu.
Kiongozi huyo mkongwe, akiwa amevaa kofia na mavazi ya rangi ya samawati na manjano, alihudhuria sherehe ya kuhitimu wanafunzi elfu moja katika chuo kikuu, mjini Harare, huku akishangiliwa na umati wa watu.
Wazimbabwe wanatumai kwamba mzozo wa kisiasa unaoikabili nchi hiyo utatatuliwa kwa haraka, huku viongozi wa upinzani, wanaharakati na viongozi wa kidini wakimtaka Mugabe kuondoka madarakani, baada ya jeshi kuchukua udhibiti wa serikali.
Hata hivyo, ripoti zilieleza kuwa Mugabe hajasalimu amri. Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma aliliambia bunge la nchi yake kwamba ni mapema mno kuchukua msimamo wowote kuhusiana na mzozo huo.

Sudan kukatiza mahusiano na Korea Kaskazini

Marekani imesema kwamba nchi ya Sudan itakata mahusiano yote ya kijeshi na kibiashara na Korea Kaskazini.

USA Heather Nauert (picture-alliance/AA/Y. Ozturk )
Ni hatua ambayo huenda ikawa ushindi mkubwa wa juhudi za utawala wa Trump za kulitenga taifa hilo la Asia  licha ya kuzidi kwa mvutano kufuatia majaribio ya silaha za nyuklia na makombora yanayofanywa na Korea Kaskazini.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nchi za nje wa Marekani Heather Nauert alisema Sudan inachukua hatua hiyo kutokana na "tishio kubwa" linalotokana na mpango wa nyuklia wa Korea Kaskazini.
Alisema Marekani imekaribisha uamuzi huo, uliotangazwa baada ya ziara ya naibu waziri wa mambo ya nchi za kigeni John Sullivan mjini Khartoum.
Ziara hiyo ilikuja wakati Marekani na Sudan, zikihimizwa na Israeli na Saudi Arabia, wakielekea kuimarisha  mahusiano bora zaidi baada ya miongo kadhaa ya uadui.
"Kuitenga serikali ya Korea Kaskazini ni kipaumbele kwa Marekani, na ni kipengele muhimu cha kudumisha amani na utulivu duniani kote," Nauert alisema katika taarifa.
"Marekani inaishukuru Sudan kwa kutimiza ahadi ya kuchukua hatua hizi muhimu kwa sababu ya kitisho kikubwa kinachosababishwa na" Korea ya Kaskazini.”
Utawala wa Trump umekuwa ukizitia msukumo  nchi za kigeni kukata mahusiano ya kiuchumi, kidiplomasia na mengine na Korea Kaskazini katika jitihada za kuitenga nchi hiyo na kuirudisha kwenye meza ya majadiliano.
Katika wiki za hivi karibuni, utawala huo umekuwa ukiyalenga mataifa ya Kiafrika na Kusini mwa Asia na kadhaa wamekubaliana.
Sudan imekuwa mtazamo maalum wa juhudi hiyo kama sehemu ya jaribio la kuboresha uhusiano kati ya Marekani na Sudan, ambayo ilisababisha kuondolewa kwa baadhi ya vikwazo vya Marekani  dhidi ya Sudan.
Huku Korea ya Kaskazini ikiendelea kutengwa na mataifa ya magharibi, nayo imezidi kutafuta mahusiano na mataifa ya Afrika, Mashariki ya Kati na kusini mwa Asia ili kukusanya fedha zinazohitajika.
Nordkorea Kim Jong Un bei Besuch einer Fabrik für Nuklearwaffen (Reuters/KCNA)
Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un akitoa mwelekeo kwenye mpango wa silaha za nyuklia
Barani Afrika, imeimarisha uhusiano wa kijeshi na kiuchumi na nchi kadhaa, ikiwa Sudan, Uganda na Angola, kwa kutoa mipango ya mafunzo ya kijeshi, ujenzi na miradi ya viwanda na usambazaji wa wafanyakazi wageni.
Mwezi uliopita, Uganda ilitangaza kuwa imewaondoa wataalam wa kijeshi wa Korea Kaskazini na wawakilishi wa makampuni ya ya Korea Kaskazini, ikiwa ni pamoja na muuzaji wake mkuu wa silaha, kama sehemu ya jitihada za kuzingatia vikwazo vipya vya umoja wa mataifa dhidi ya Korea Kaskazini.
Korea Kaskazini kwa miaka mingi imekuwa ikiwapa mafunzo wanajeshi wa  Uganda ,ya vita vya bahari na utunzaji wa silaha.
Moussa Faki Mahamat, mwenyekiti wa Halmashauri ya Umoja wa Afrika, alijibu tangazo la Sudan kwa kusema Umoja wa Afrika umeshutumu uenezaji  wa silaha za nyuklia katika bara hilo na mahali pengine.
"Maendeleo na utengenezaji wa silaha hizi inakuwa tishio la kweli kwa amani na usalama duniani," mkuu huyo wa AU alisema katika mahojiano na shirika la habari la  AP.
Tangazo hili la Alhamisi lilikuja kabla ya uamuzi uliotarajiwa hivi karibuni kwa Marekani  kuiorodhesha tena Korea ya Kaskazini kama "serikali inayodhamini ugaidi," jina ambalo liliondolewa na utawala wa Rais George W. Bush mnamo mwaka wa 2008 kwa kuwa ulitaka makubaliano ya kidiplomasia kuzuia mpango wa silaha za atomiki wa Korea kaskazini.
Sarah Huckabee Sanders (picture alliance/AP Images/P.M. Monsivais)
Msemaji wa ikulu ya White House Sarah Huckabee Sanders aliwaambia waandishi wa habari kwamba anatarajia uamuzi juu ya hali ya Korea Kaskazini kuamuliwa mapema wiki ijayo.
Sudan ni moja ya nchi tatu tu - nyingine ni Iran na Syria - ambazo kwa sasa zimeteuliwa wafadhili wa ugaidi na wizara ya nchi ya kigeni, jina linalobeba vikwazo vya uchumi na kifedha. Tangazo la Sudan kukata mahusiano na Korea ya Kaskazini kunaweza kusaidia kesi yake kuondolewa kutoka kwenye orodha hiyo.
Hata hivyo, afisa wa wizara ya mambo za kigeni alisema uwezekano wa mabadiliko ya uteuzi ya Sudan na Korea Kaskazini hauhusiani na kwamba ukaguzi wa nchi zote mbili unaendelea.
Afisa huyo, ambaye hakuwa na mamlaka ya kuzungumza jambo hilo kwa umma na aliyezungumza katika hali ya kutojulikana, alisema uamuzi juu ya Sudan unaweza kutegemea jinsi itakavyotelekeza ahadi yake ya kukata mahusiano na Korea Kaskazini.
Taarifa ya Nauert ilisema Marekani  "itaendelea kushirikiana juu ya suala hili ili kuhakikisha kuwa ahadi hii imetekelezwa kikamilifu."

Rais Mugabe amtunuku shahada mke wa Jenerali aliyemzuia

Rais wa Zimbabwe's Robert Mugabe amewatunuku shahada zaidi ya wanafunzi 3,300 katika chuo kikuu cha ZimbabweHaki miliki ya pichaEPA
Image captionRais wa Zimbabwe's Robert Mugabe amewatunuku shahada zaidi ya wanafunzi 3,300 katika chuo kikuu cha Zimbabwe
Rais wa Zimbabwe's Robert Mugabe amewatunuku shahada zaidi ya wanafunzi 3,300 katika chuo kikuu cha Zimbabwe, akiwemo mke wa jenerali aliyemzuia siku ya Jumatano.
Marry Chiwenga alipata shahada ya MBA kulingana na shirika la habari la Zimbabwe.
Awali Rais wa Zimbabwe Robert Mugabe ameonekana hadharani kwa mara ya kwanza tangu jeshi la nchi hiyo lichukue madaraka siku ya Jumatano.
Alihudhuria sherehe za kuhitimu kwa mahafala kwenye mji mkuu Harare.
Bwana Mugabe amekuwa chini ya kuzuizi cha nyumbani kwa siku kadhaa huku kukiwa na mvutano kuhusu ni nani atamrithi.
Jeshi lilisema Ijumaa kuwa lilikuwa kwenye mazungumzo na Mugabe na litaujulisha umma kuhusu matokeo ya mazunngumoz hayo haraka iwezekanavyo.
Mtu moja aliyeshuhudia alinukuliwa na Reuters akisema kuwa Mugabe alishangiliwa wakati wa sherehe baada ya kuzungumza.
Jeshi lilichukua madaraka baada ya Mugabe kmfuta kazi makamu wa Rais Emmerson Mnangagwa wiki iliyopita, na kuashiria kuwa alimpendelea mkewe kuweza kuchukua ungonizi wa Zanu-PF na urais.

Mwanajeshi wa Korea Kaskazini aliyetorokea K Kusini apatikana na minyoo mingi

Minyoo yapatikana ndani ya mwili wa mwanbajeshi wa Korea Kaskazini aliyetorokea Korea KusiniHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMinyoo yapatikana ndani ya mwili wa mwanbajeshi wa Korea Kaskazini aliyetorokea Korea Kusini
Mwanajeshi wa Korea Kusini aliyepigwa risasi alipokuwa akitorokea Korea Kusini katika mpaka wa mataifa hayo mawili amepatikana na vimelea vingi katika matumbo yake , kulingana na daktari wake.
Mtoro huyo alivuka eneo linalolindwa sana mpakani siku ya Jumatatu , lakini akapigwa risasi kadhaa na walinzi wa Korea Kaskazini.
Madaktari wanasema mwanajeshi huyo kwa sasa yuko katika hali nzuri , lakini idadi kubwa ya minyoo katika mwili wake unafanya hali yake kuwa mbaya.
Hali yake inaonyesha hali ya maisha yalivyo nchini Korea Kaskazini.
''Sijawahi kuona kitu kama hiki katika miaka yangu 20 kama daktari , daktari wa Korea Kusini Lee Cook-jong aliwaambia waandishi wa habari, akielezea kwamba kimelea mrefu katika tumbo lake alikuwa na urefu wa sentimita 27.
Mwanajeshi wa Korea Kaskazini akikimbizwa hospitalini Korea KusiniHaki miliki ya pichaEPA
Image captionMwanajeshi wa Korea Kaskazini akikimbizwa hospitalini Korea Kusini
Mwanadamu anaweza kupata vimelea kupitia kula chakula kichafu kwa kuumwa na wadudu ama vimela waliongia kupitia katika ngozi.
Kwa upande wa mwanajeshi huyo huenda vimelea hao waliingia kupitia chakula kichafu.
Korea Kaskazini inatumia kinyesi kama mbolea. Iwapo vinyesi hivyo havitibiwi na kutumiwa kama mbolea katika mboga ambayo haijapikwa ,vimelea hivyo vinaingia mdomoni hadi katika matumbo ya mwanadamu.

Pentagon yamtaka Trump kujiuzulu kimakosa

Ujumbe huo ambao pia uliwataka wanasiasa wengine wawili wa Marekani kujiuzulu kufuatia madai ya unyanyasaji wa kijinsia ulitumwa kutoka kwa akaunti ya @ProudResisterHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionUjumbe huo ambao pia uliwataka wanasiasa wengine wawili wa Marekani kujiuzulu kufuatia madai ya unyanyasaji wa kijinsia ulitumwa kutoka kwa akaunti ya @ProudResister
Ndio idara inayosimamia nambari za siri makombora, Idara inayosimamia usalama wa Marekani na mkuu wake ni rais wa Marekani ambaye hupendelea sana kutumia mtandao wa Twitter.
Lakini inapofikia wakati wa kusimamia akaunti yake ya mtandao huo, the Pentagon inafaa kuimarisha uwezo wake.
Siku ya Alhamisi idara hiyo ya ulinzi ilituma ujumbe kimakosa katika mtandao wake wa Twitter ukimtaka rais Trump kujiuzulu.
Ujumbe huo ambao pia uliwataka wanasiasa wengine wawili wa Marekani kujiuzulu kufuatia madai ya unyanyasaji wa kijinsia ulitumwa kutoka kwa akaunti ya @ProudResister, mwanaharakti ambaye ni mkosaji mkuu wa Trump.
Akaunti hiyo ilisema: Suluhu ni rahisi. Roy More jiuzulu katika kinyanganyiro. AI: Jiuzulu katika bunge la Congres, Donald Trump Jiuzulu katika urais. GOP: Wacha kulifanya swala la unyanyasaji wa kijinsia kuwa la kibinafsi.Ni uhalifu kama unafiki wao.
Ujumbe wa Trump uliosambazwa na akaunti ya idara ya ulinzi ya marekani kimakosaHaki miliki ya pichaTWITTER
Image captionUjumbe wa Trump uliosambazwa na akaunti ya idara ya ulinzi ya marekani kimakosa
Akaunti ya Idara hiyo ya ulinzi iliusambaza ujumbe huo kimakosa kwa takriban wafuasi wake milioni 5.2 kabla ya kuufuta.
Lakini makosa hayo yalionekana.
Picha ya ujumbe huo wa Pentagon lisambazwa na majibu yake pia yakawa ya haraka sana.

Rambo akana kumnyanyasa kingono shabiki wake mwenye umri wa miaka 16

Nyota wa filamu Sylvester StalloneHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionNyota wa filamu Sylvester Stallone
Nyota wa filamu Sylvester Stallone amekana ripoti kwamba yeye na mlinzi wake walimnyanyasa kingono shabiki wake wa miaka 16 mjini Las Vegas mapema miaka ya themanini.
Gazeti la mtandao la The Mail limechapisha kile linasema ni ripoti ya polisi kutoka 1986 ambayo ilielezea madai hayo.
Mwanamke huyo hakuwasilisha mashtaka dhidi ya Stallone kwa sababu alinyanyaswa na kuaibishwa mbali na kuwa na hofu.
Hakuna hatua iliochukuliwa.
Msemaji wa nyota huyo wa filamu ya Rocky alisema kuwa taarifa hiyo ilikuwa ya uwongo.
Michelle Bega aliyaelezea madai hayo kuwa ya uwongo, akiongezea : hakuna mtu aliyekuwa akijua kuhusu habari hiyo hadi ilipochapishwa leo, akiwemo bwana Stallone.
''Bwana Stallone hakuwasiliana na mtu yeyyote ama malaka ama mtu yeyote yule kuhusu swala hilo''.

Muswada kuwabana wenye nyumba waandaliwa


Dodoma. Serikali iko katika mchakato wa maandalizi ya muswada wa sheria ambayo itasimamia sekta ya nyumba, hivyo kuondoa changamoto ya wamiliki kudai kodi ya pango ya zaidi ya mwezi mmoja.
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula amesema hayo bungeni leo Ijumaa Novemba 17,2017 akijibu swali la nyongeza la mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Halima Bulembo.
Halima katika swali lake amesema vijana ambao ni kati ya asilimia 56 na 60 nchini, wanashindwa kutimiza ndoto zao kutokana na gharama kubwa ya kodi ambayo hutakiwa kulipa kwa kipindi cha mwaka mmoja au miezi sita.
"Serikali inasemaje kuhusu kuleta sheria itakayofuta tabia ya wenye nyumba kulazimisha kulipwa kodi ya mwaka?" amehoji mbunge huyo.
Akijibu swali hilo, Mabula amesema Serikali imeliona tatizo hilo na ipo katika mchakato wa kuandaa muswada wa sheria utakaosimamia sekta hiyo.
Mabula amesema baada ya kukamilika kwa sheria ambayo itaunda chombo cha kusimamia sekta hiyo, wapangaji hawatalipa kodi ya mwaka wala miezi sita tena bali watalipa kwa mwezi na kuweka amana ya miezi mitatu.
Katika swali la msingi, Halima amesema kumekuwa na upandaji holela wa gharama za pango kwa nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).
"Je Serikali haioni kuna haja ya kudhibiti upandaji holela ambao unaathiri wananchi wengi kutokana na kipato chao?" amehoji.
Akijibu, Mabula amesema utaratibu wa urekebishaji wa viwango vya kodi za shirika hilo husimamiwa na bodi ya wakurugenzi ambayo imepewa mamlaka ya kisheria ya kusimamia kodi ya pango na kuidhinisha viwango vya kodi vinavyotozwa kwa wapangaji wa nyumba za shirika.
"Kwa mara ya mwisho bodi ya wakurugenzi ya Shirika la Nyumba la Taifa iliidhinisha viwango vipya vya kutoza kodi kwenye nyumba za shirika mwaka 2011 ambavyo ndivyo vinavyotumika mpaka sasa," amesema.

Nuzulack Dausen apeta tuzo za mwandishi bora Afrika


Addis Ababa-Ethiopia. Mwandishi mwandamizi wa kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), Nuzulack Dausen ameshinda tuzo ya mwandishi bora Afrika wa masuala ya nishati na miundombinu katika tuzo za umahiri wa habari Afrika za Zimeo zilizotolewa jana Alhamisi usiku jijini hapa.
Zimeo ambazo zimetolewa kwa mara ya tatu sasa ni tuzo maarufu katika tasnia ya habari barani Afrika sambamba na tuzo za CNNMultichoice ambazo zimekuwa zikitolewa kila mwaka.
Tuzo hizo za Zimeo hutolewa na shirika linaloshughulikia ukuaji wa tasnia ya habari Afrika ya African Media Initiative (AMI) yenye makazi yake jijini Nairobi, Kenya na kudhaminiwa na mashirika mbalimbali ya kimataifa yakiwemo Unesco, Kamisheni ya Uchumi ya Afrika ya Umoja wa Mataifa (ECA) na Shirika la Habari la Al-Jazeera.
Katika kipengele cha nishati na mazingira, Dausen alikuwa akichuana na wanahabari Jeffrey Moyo ambaye huandikia Shirika la Habari la Thomson Reuters na The New York Times na Femi Asu wa gazeti la The Punch la nchini Nigeria.
"Kwanza namshukuru Mungu kwa tuzo hii ya heshima katika maisha yangu ya uandishi wa habari na nawashukuru viongozi na wafanyakazi wenzangu wa MCL kwa kunijenga kitaaluma na kunitia moyo kwa kila nachojaribu kukifanya.
"Pia nawashukuru familia yangu kwa kunipa moyo wa kufanya kazi kwa bidii na kukubali kunikosa kwa muda napokuwa katika majukumu ya kazi nje ya Dar es Salaam na wasomaji ambao maoni yao hunijenga zaidi," amesema Dausen.
Dausen, ambaye ni mhariri wa habari za takwimu wa MCL, amesema uhuru wa habari na uandishi mahiri wa habari unaochambua masuala kwa kina utasaidia kuchochea maendeleo Tanzania na duniani kwa ujumla kwa kuainisha fursa na kutoa majibu ya changamoto zinazoikabili jamii.
Habari iliyompa ushindi Dausen inahusu namna wakazi wa vijiji vya Namikango A na B wilayani Nachingwea mkoani Lindi Tanzania walivyotumia fursa ya umemejua kupata mwanga na kukabiliana na umaskini. Habari hiyo ilichapwa katika gazeti dada la The Citizen zaidi ya miezi miwili iliyopita.
Akizungumzia vigezo vya utoaji tuzo hizo, Jaji Mwandamizi katika tuzo hizo Dk George Nyabuga wa Chuo Kikuu cha Nairobi (UoN) amesema walizingatia vigezo vingi vya kihabari vikiwemo uhalisia wa wazo la habari, mpangilio wa hoja na umahiri wa kueleza habari hiyo ikaeleweka na wananchi wa kawaida.
Vigezo vingine ni namna mada husika inavyowagusa wananchi, matumizi ya takwimu na uzingatiaji misingi ya habari ya usawa, weledi, na ukweli.
"Haikuwa kazi rahisi kuchambua mamia ya kazi za wanahabari Afrika nzima hadi kupata washindi wetu leo, " amesema Dk Nyabuka.
Ofisa Mtendaji Mkuu wa AMI, Erick Chinje amesema ili vyombo vya habari viwe na msaada kwa watu wa Afrika ni lazima tasnia ya habari iboreshe utendaji wake kwa kuripoti na kuchambua masuala yanayogusa wananchi.
"Mchango wa AMI umekuwa katika kuandaa mipango ambayo itawasaidia wanahabari kuongeza uwezo wao kitaaluma na mbinu nyingine zitakazofanya wawe bora zaidi. Tuzo za Zimeo zitawatambua wanahabari waliofanya vyema katika kuripoti sekta muhimu katika maisha ya watu," amesema Chinje.
Baadhi ya wanahabari walioshinda tuzo hizo jana usiku ni Dorcas Wangira kutoka Kenya, Ridwan Dini-Osman kutoka Ghana na Jay Caboz wa Afrika Kusini aliyeibuka mshindi wa jumla wa tuzo hizo.

TRA yapeleka elimu ya kodi kwa wachimbaji

Mkurugenzi wa huduma na elimu ya mlipa kodi
Mkurugenzi wa huduma na elimu ya mlipa kodi (TRA) Richard Kayombo 

Geita. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wametoa elimu ya mlipa kodi kwa wachimbaji wadogo mkoani Geita ili watekeleze agizo la Serikali la kulipa asilimia tano wanapouza madini kwa mujibu wa sheria.
Mkuu wa idara ya huduma na elimu wa TRA mikoa ya Kanda ya Ziwa, Lutufyo Mtafya alisema wameamua kuwafuata wachimbaji hao maeneo yao ili kuwaelimisha watimize matakwa ya kisheria ya kulipa kodi.
Baadhi ya wachimbaji hao eneo la Rwamgasa wilayani Geita, walisema uelewa duni kuhusu sheria ya ulipaji kodi ndiyo sababu inayowafanya kutolipa kodi.
Emmanuel Samson alisema ni vyema elimu ikatolewa zaidi kwa kuwa sasa wanashindwa kuelewa, kwani awali walijua kodi ya halmashauri na ya mmiliki wa kiwanja lakini nyongeza ya asilimia tano nyingine ni mzigo kwa wachimbaji.

Serikali zatakiwa kuwajengea uwezo wataalamu wa afya


Taasisi ya magonjwa yasiyoambukizwa, usalama wa chakula na lishe kupitia Shirika la Kikanda la Afya (ECSA) limetaka Kenya, Tanzania na Uganda kuweka umuhimu wa kuwajengea uwezo wataalamu wa afya wa ngazi za chini ili waweze kutoa elimu stahiki kwa jamii.
Akizungumza leo Ijumaa Novemba 17,2017 wakati wa mkutano wa siku mbili uliohusisha nchi hizo tatu, meneja wa taasisi hiyo, Rosemary Mwaisaka amesema ili kutokomeza udumavu na magonjwa yasiyoambukizwa ni muhimu kuwekeza kwa watumishi wa afya wanaotoa huduma za kila siku kwenye vituo vya afya.
“Kwa kutambua hilo, tumetengeneza vitini kwa ajili ya watenda kazi katika ngazi ya vituo vya afya na jamii ili kutoa ujuzi katika masuala ya lishe, usalama wa chakula na kuepukana na magonjwa yasiyoambukizwa,” amesema Rosemary.
Amesema kwa muda mrefu wamekuwa wakifanya kazi peke yao lakini lishe ni suala mtambuka.
Mwakilishi wa Wizara ya Afya nchini Kenya,  Peter Cherotich amesema wamepokea vitini na kwamba, suala linalofanyiwa kazi sasa ni kuhakikisha usalama wa chakula na lishe unatiliwa mkazo.

Zitto ataka Serikali kununua tumbaku ya wakulima


Urambo. Kiongozi wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ametaka Serikali kununua tumbaku yote ya wakulima iliyoshindikana kununuliwa.
Akihutubia wananchi leo Ijumaa katika mkutano wa kampeni za uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kijiji cha Kalemela A, Kata ya Muungano wilayani Urambo Zitto ameishangaa Serikali kutumia fedha nyingi kununua ndege aina ya bombardier zinazopakia watu wachache badala ya kuwekeza kwenye kilimo kinachoajiri wananchi wengi.
Zitto amesema katika ziara yake amezunguka vijijini na kushuhudia nyuso za huzuni, huku wananchi wakimwambia tumbaku ya mwaka jana haijauzwa na msimu mpya umeanza.
“Serikali makini ingefanya nini kwenye kadhia hii ya tumbaku? Sisi ACT- Wazalendo tungekuwa madarakani tungenunua tumbaku yote ya ziada ya wakulima kwa kutumia kasma ya fedha za dharura kwenye Fungu la 50 Wizara ya Fedha,” amesema.
Amesema Serikali iliwahimiza wananchi kufanya kazi kwa bidii, lakini baada ya kuzalisha kwa wingi wanaadhibiwa kwa kukosa masoko.
Zitto ameshauri Serikali kutafuta soko kwa mfumo uliosema ni wa G to G (Government to Government) na kuuza tumbaku hiyo na kurejesha fedha hizo kwenye mfuko wa dharura.
Amesema wakati asilimia 65 ya Watanzania wanategemea kilimo kama ajira, kilimo kimekuwa kikishuka na kusababisha wakulima kuendelea kuwa masikini na kukosa chakula.
“Tunazalisha watu zaidi kuliko chakula, ni dhahiri tunaelekea kubaya,” amesema Zitto.
Amesema katika hali hiyo ya kudumaa kwa kilimo bado wakulima wa Tabora hawajafutwa machozi na zao lao la tumbaku wakati ndilo linaloingiza fedha za kigeni kuliko korosho.
“Serikali ipo tayari kutumia Sh1 trilioni kulipia ndege ambazo ni Watanzania asilimia tano wanapanda kuliko kuokoa wakulima 1.4 milioni wa tumbaku nchi nzima kwa Sh150 bilioni tu, tena ikiwa fedha hizo zinarudi ndani ya muda mfupi,” amesema Zitto.
Amewataka wananchi wa kijiji hicho kuchagua mgombea udiwani wa chama hicho ili apambane kuhakikisha tumbaku ya mwaka jana inanunuliwa.
Amesema Ilani ya Uchaguzi ya ACT -Wazalendo ilitangazwa na Taasisi ya Mviwata (Muungano wa vikundi vya wakulima) kuwa ilani bora zaidi kuhusu masuala ya kilimo kuliko ilani za vyama vyote katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015 kwa kuwa ilipendekeza kuwapo kwa Hifadhi ya Jamii kwa Wakulima.

Mabomu yatikisa Nairobi


Nairobi, Kenya. Umati mkubwa wa wafuasi wa muungano wa Nasa umejitokea kumpokea kiongozi wao, Raila Odinga katika sherehe zilizogeuka kuwa za vurugu, mabomu ya machozi na mapambano ya kukimbizana na polisi.
Watu wawili wanadaiwa kufariki dunia baada ya kupigwa na kinachosadikiwa kuwa ni risasi wakati polisi wakiwatawanya watu waliokuwa wanatembea kutoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) walipokuwa wakitembea sambamba na msafara wa kiongozi huyo wa Nasa aliyerejea mchana leo akitokea Marekani alikofanya ziara ya siku 10.
Mapema, polisi na wafuasi wa Raila walipambana katika barabara ya kuelekea uwanja wa ndege kabla ya Raila kuwasili.
Licha ya ulinzi huo na moshi wa mabomu ya machozi wafuasi wa Nasa wapatao 200 wakiwemo wanawake walifanikiwa kupita utepe uliowekwa na vyombo vya usalama na wakaingia hadi ndani ya uwanja.
Helikopta ya polisi ilikuwa ikizunguka juu ya uwanja huo huku magari ya maji ya kuwasha na magari ya maalumu ya kusafisha njia yalikuwepo uwanjani hapo na yalitumika kuzima moto wa matairi.
Lakini wakati Raila akiondoka katika msafara wenye makumi ya magari yakiwemo ya viongozi wa Nasa na mamia ya wafuasi, yalizuka mapambano huku polisi wakitumia magari ya kurusha maji ya kuwasha, mabomu ya machozi huku waandamanaji wakirusha mawe na fimbo.