Saturday, November 18

TRA yapeleka elimu ya kodi kwa wachimbaji

Mkurugenzi wa huduma na elimu ya mlipa kodi
Mkurugenzi wa huduma na elimu ya mlipa kodi (TRA) Richard Kayombo 

Geita. Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) wametoa elimu ya mlipa kodi kwa wachimbaji wadogo mkoani Geita ili watekeleze agizo la Serikali la kulipa asilimia tano wanapouza madini kwa mujibu wa sheria.
Mkuu wa idara ya huduma na elimu wa TRA mikoa ya Kanda ya Ziwa, Lutufyo Mtafya alisema wameamua kuwafuata wachimbaji hao maeneo yao ili kuwaelimisha watimize matakwa ya kisheria ya kulipa kodi.
Baadhi ya wachimbaji hao eneo la Rwamgasa wilayani Geita, walisema uelewa duni kuhusu sheria ya ulipaji kodi ndiyo sababu inayowafanya kutolipa kodi.
Emmanuel Samson alisema ni vyema elimu ikatolewa zaidi kwa kuwa sasa wanashindwa kuelewa, kwani awali walijua kodi ya halmashauri na ya mmiliki wa kiwanja lakini nyongeza ya asilimia tano nyingine ni mzigo kwa wachimbaji.

No comments:

Post a Comment