Wednesday, September 20

TAARIFA KWA UMMA KUHUSU KIFO CHA ASKARI WA JWTZ ALIYEKUWA KATIKA ULINZI WA AMANI NCHINI DRC

MRISHO MPOTO KUIWAKILISHA TANZANIA KATIKA TAMASHA LA UTALII DUNIANI NCHINI CHINA


Mamia ya wadau wa sanaa wamejitokeza kwa wingi Jumanne hii jioni katika Uwanja wa ndege wa JK Nyerere jijini Dar es salaam kumuaga msanii wa muziki wa asili nchini, Mrisho Mpoto ambaye ameelekea nchini China kwaajili  ya kuiwakilisha Tanzania katika tamasha la utalii wa sanaa duniani.

Muimbaji huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo, Kitendawili alitangaza katika mitandao yake ya kijamii kwamba atasafiri Jumanne hii kuelekea nchini China hali iliyopelekea mashabiki wengi kumimika uwanjani hapo kwaajili ya kumuaga.

Akiongea na waandishi waliojitokeza uwanjani hapo, Mpoto alisema anawashukuru mamia ya watu waliojitokeza uwanjani hapo kwaajili ya kumuaga kwenda kuiwakilisha nchi katika masuala ya kiutalii nchini China.

“Sikutegemea kama watu watakuwa wengi hivi, huu ni upendo wa dhati sana na nawashukuru sana kwa moyo huo na upendo mliouonyesha, nakwenda China kwaajili ya Watanzania, sio Mpoto lakini nakwenda kuuonyesha ulimwengu kwamba Tanzania tuna utajiri wa sanaa, Tanzania tuna makabila zaidi ya mia moja na ishirini hiki ni kitu kikubwa sana, tunaenda kuwatambia usalama tuliokuwa nao,” alisema Mrisho.

Muimbaji huyo amedai haikuwa kazi rahisi kupata kazi hiyo na kuwa muakilishi pekee wa Tanzania kwenye maadhimisho hayo ya utalii duniani ambayo yanawakutanisha mataifa mbalimbali duniani.

Aliongeza, “Mungu bado anaendelea kutuona, kati ya nchi zote za Afrika ni nchi tatu tu ambazo zimepata mualiko huu ikiwemo Tanzania na Kenya. Hii ni ishara nzuri sana duniani na Afrika nzima kwa sababu wadau ambao watatembelea mahadhisho hayo washuhudia vitu vyetu vya asili, ngoma, nyimbo, ala za muziki pamoja na mitindo mbalimbali ya upigaji wa ngoma,”

Alisema safari hiyo imewezeshwa na  Ubalozi wa Tanzania China, Wizara ya Utamaduni, Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro, TANAPA, TTB, BASATA pamoja na Leopard Tours.

MILIONI MIA MOJA NA TISINI (190,000,000) ZATUMIKA KUTIBU UGONJWA WA KIPINDUPINDU HALMASHAURI YA WILAYA YA IRINGA





Afisa afya wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Samwel Nkya akizungumza na viongozi wa vijiji wa tarafa ya pawaga kuhusu uboreshaji wa vyoo bora kwa lengo la kutatua tatizo la ugonjwa wa kipindupindu ambalo limekuwa likijitokeza mara kwa mara katika tarafa hiyo walianza kutoa elimu kwa viongozi wote na baadae wakahamia kwa wananchi.

Afisa afya wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Samwel Nkya akizungumza na mama moja ambaye hana choo bora na kutundikiwa bendera ilikuwa inamuonyesha kuwa hana choo bora katika kijiji cha mboliboli tarafa ya pawaga mkoani Iringa.
Afisa afya wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Samwel Nkya akisimamia zoezi la utundikaji wa bendera kwa wasio na vyoo bora




Na Fredy Mgunda,Iringa.

Halmashauri ya wilaya ya Iringa imetumia shilingi milioni mia moja na tisini (190,000,000 ) kupambana na tatizo la milipuko ya ugonjwa wa kipindupindu katika tarafa ya pawaga na Idodi mkoani Iringa na ni miongoni mwa halmashauri 156 zinazotekeleza kampeni ya kitaifa ya usafi wa mazingira Tanzania bara.

Akizungumza wakati wa utoaji elimu ya matumizi ya vyoo bora katika tarafa ya pawaga afisa afya wa halmashauri ya wilaya ya Iringa Samwel Nkya aliwataka wananchi kuanza kutumia vyoo bora ili kumaliza tatizo la milipuko ya ugonjwa wa kipindupindu ambao umekuwa ukiwakumba mara kwa mara.

“Jamani chanzo mmoja wapo cha mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu ni matumizi ya vyoo ambavyo sio bora hivyo mnatakiwa kutumia vyoo bora na kutoa elimu kwa wananchi wenu maana nyinyi ndi wenye wananchi na leo tunawapa hii elimu nyie viongozi tunaomba muifikishe elimu kwa wananchi”alisema Nkya

Nkya alisema walitoa elimu ya uboreshaji wa miundombinu ya vyoo na kunawa mikono kwa kutumia maji tiririka kwa sabuni mara ya kutoka chooni kwa ngazi ya kaya na shule za msingi na sekondari,Vyuo,taasisi za kidini,taasisi binafsi,taasisi za kiserikali kama ofisi za serikali na vituo vya afya lengo likiwa ni kutokomeza kabisa ugonjwa wa kipindupindu.

“Ukiangalia hadi sana tumefanikiwa kuzifikia jumla ya kaya 24 zilizotekeleza kampeni hiikupitia wadau mbalimbali kama wizara ya afya,wizara ya maji,wizara ya elimu (RWSSP),halmashauri ya wilaya ya Iringa,UNICEFU,SNV na WARID na jumla ya kata nne ambazo ni ilolompya,Mlenge,Mboliboli na Itunundu zimeanza kutekeleza rasmi kampeni hii kwa mwaka wa fedha wa 2017/2018” alisema Nkya

Mwezi wa pili hadi mwezi wan ne mwaka 2016 ndio kulitokea mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu katika halmashauri ya wilaya ya Iringa ambapo kata za Mboliboli na Mlenge zilikumbwa na ugonjwa huo huku vijiji vya Luganga,Mnadani,Idodi na Mafuruto vilikuwa na idadi ndogo ya wagonjwa wa kipindupindu.

Aidha Nkya alisema kuwa mikakati ya halmashauri ya wilaya ya Iringa kuzitambua kaya na taasisi zisizo na vyoo bora,kutambua vibarua na wamiliki wa mshamba ya mpunga,kufanya ukaguzi wa mara kwa mara wa usafi wa mazingira vijijini na kutoa elimu ya usafi wa mazingira kwa ajili ya kujikinga na ugonjwa wa kipindupindu kisitokee tena katika halmashauri hiyo.

“Tumepeana maagizo ya kutekeleza kama kuwawekea bendera nyekundu kaya na taasisi zote ambazo hazina vyoo bora,kutoa muda maalumu wa kuboresha vyoo vyao vinginevyo kuna faini ambayo itatolewa kwa kaya na taasisi ambazo zitakuwa hazijaboresha vyoo vyao” alisema Nkya

Nyamiki Kimsau ni mwananchi wa kijiji cha Usolanga pawaga alisema kuwa kuwa ugonjwa kipindupindu umekuwa sugu katika kijiji hicho kutokana na wananchi wemgi kutokuwa na vyoo bora ambavyo vinakidhi kuishi na afya bora.

“Wananchi tukiwa tunafanya usafi na kuwa na vyoo bora basi tunaweza kuepukana na milipuko ya ugonjwa wa kipindupindu hivyo naomba serikali kuwa wakali kwenye swala la kuwa na vyoo bora ili kuondokana na aibu ambayo imekuwa inatutafuna kwa muda sasa” alisema Kimsau

Naye Mwaita Bin jumbe alisema kuwa kweli wananchi wa kijiji cha mboliboli hawana vyoo bora kutokana na ugumu wa maisha hivyo wanaomba kupewa muda ili waweze kuboresha vyoo bora lakini swala la ugonjwa wa kipindupindu bado unawakumba kila mara.

“Jamani tunaomba viongozi mtoe elimu ya kutosha kwa wananchi ili wajue umuhimu wa kuwa na vyoo bora tofauti na hali iliyopo hivi sasa” alisema Bin jumbe

Hamis Matyame ni kijana wa kijiji cha mboliboli aliita serikali ya kijiji kutafuta njia mbadala ya kuwachimbia vyoo bora wazee ambao hawana uwezo wa kifedha na guvu kazi kwa sababu wasipo saidiwa ugonjwa wa kipindupindu hauta koma katika tarafa ya pawaga.

“Mimi kama kijana napenda kuwasaidia wazee kuboresha vyoo ila hapa kijijini kuna wazee wengi hivyo pekee yangu siwezi hivyo naiomba serikali kutafuta njia mbadala kuwasaidia hawa wazee” alisema Matyame

MWAKILISHI KUTOKA BENKI YA DUNIA ARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MRADI WA MABORESHO WA HUDUMA ZA KIMAHAKAMA

Na Mary Gwera, Mahakama

Mwakilishi ‘Practice Manager’ kutoka Benki ya Dunia (WB), Bw. George Larbi ameisifu Mahakama kwa utekelezaji wake wa Mradi wa Maboresho wa huduma za Kimahakama.

Bw. Larbi aliyasema hayo mapema Septemba 19, alipokutana na Mhe. Jaji Mkuu ofisini kwake Mahakama ya Rufani-Dar es Salaam ambapo alipata nafasi ya kuongea na Mhe. Jaji Mkuu na Viongozi wengine wa Mahakama akiwemo Mtendaji Mkuu na Msajili Mkuu wa Mahakama ya Tanzania.

“Mradi huu unaotekelezwa na Mahakama ni mradi wa mfano ambapo mafanikio yake yanatarajiwa kuigwa nan chi nyingine,” alisema Bw. Larli.

Bw. Larli ambaye amewasili nchini kutokea Washington D.C zilipo ofisi cha Benki ya Dunia amefanya ziara yake kwa lengo la kuangalia maendeleo ya utekelezaji wa Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama ambao unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya Mahakama ya Tanzania na Benki ya Dunia (WB).

Alisema Mradi huu unaotekelezwa na Mahakama ni Mradi wa pili kwa nchi za Afrika ambapo Benki ya Dunia inashirikiana moja kwa moja na Mahakama katika kuboresha huduma ya utoaji haki.

Maeneo muhimu yanaotekelezwa na Mradi wa Benki ya Dunia (WB) ni pamoja na; Mapambano dhidi ya Rushwa; ni kwa jinsi gani Mahakama pamoja na wadau wengine wanaweza kushirikiana katika kupiga vita vitendo vya rushwa.Maeneo mengine ni ushirikishaji wa wadau katika masuala yote ya utoaji haki na kusogeza huduma ya utoaji haki karibu na wananchi.
Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibarhim Hamis Juma (kulia) akiongea neno na Bw. George Larbi kutoka Benki ya Dunia (katikati) wa kwanza kushoto ni Bw. Denis Biseko 'Co-Team Task Leadear' wa Mradi wa Maboresho ya Huduma za Kimahakama.
 Bw. George Larbi, kutoka Benki ya Dunia (WB) (katikati) akiongea na Mhe. Jaji Mkuu (kulia).
 Mhe. Jaji Mkuu (aliyeketi wa kwanza kulia) akiwa pamoja na Wageni kutoka Benki ya Dunia (wawili walioketi katikati) wa tatu kutoka kushoto ni Mtendaji Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Hussein Kattanga, wa pili kushoto ni Msajili Mkuu, Mahakama ya Tanzania, Mhe. Katarina Revocati na wa kwanza kushoto ni Mkuu wa Kitengo cha Mradi wa Maboresho wa Huduma za Mahakama, Mhe. Zahra Maruma.
 Ukaguzi: Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Mahakama cha Mahakama-Kisutu unaojengwa kwa fedha za Benki ya Dunia Bw. George Larbi kutoka Benki ya Dunia pia alipata fursa ya kutembelea Mradi wa ujenzi wa Kituo cha Mafunzo cha Mahakama unaofanyika katika eneo la Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kwa sasa kazi ya upakaji rangi katika jengo hilo inaendelea.
 Mafundi wakiendelea na kazi ya upakaji rangi katika jengo la Kituo cha Mafunzo linalojengwa Kisutu-Dar es Salaam (Picha na Mary Gwera, Mahakama) 

TANZANIA IMEFANIKIWA KUIMARISHA MIFUMO YA UFAMASIA KWA MSAADA WA JUMUIYA YA NCHI ZA ACP NA EU

Na Ramadhani Ali – Maelezo 

Tanzania imefaidika na imepiga hatua kubwa katika kufuata sheria na kuboresha uingizaji wa dawa na vifaa tiba sahihi kufuatia msaada mkubwa wa Jumuia ya nchi za Afrika, Caribean na Pacific (ACP) katika kudhibiti mifumo ya kifamasia kwa nchi za ukanda huo.
Akifungua mkutano wa mwisho wa Jumuiya ya nchi za ACP inayofadhiliwa na Kamisheni ya Umoja wa Ulaya, Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Bi. Asha Abdalla Ali alisema imefanikiwa kupanga mikakati kuhakikisha dawa zote zinazoingia nchini ni salama kwa matumizi ya binadamu.
Alisema Jumuiya imewajengea uwezo wafamasia kwa mafunzo mbali mbali ya kuboresha upatikanaji, usambazaji na kusajili dawa zinazoingia ili kuhakikisha zilizokuwa chini ya kiwango haziingizwi nchini.
Katibu Mkuu aliongeza kusema kuwa Jumuiya ya nchi za Ukanda wa Afrika, Carbean na Pacific imefanya juhudi ya kuimarisha Bodi ya Chakula, Dawa na Vipodozi Zanzibar na kuhakikisha inatekelezaji majukumu yake kwa ufanisi.
Aidha aligusia kuwa Jumuiya imeiwezesha Serikali kufanya mapitio ya sera yake ya dawa ili kuona inaendana na wakati wa sasa kwa mujibu wa mahitaji na kuimarisha afya za wananchi.Bi. Asha alilishukuru Shirika la Afya Duniani na Jumuiya ya nchi za ukanda wa Afrika, Caribean na Pacific kwa misaada yao mikuwa katika kuimarisha mifumo ya ufamasia nchini.
Akiwakaribisha wajumbe wa mkutano huo kwa niaba ya mwakilishi wa Shirikala Afya Duniani nchini Tanzania, mwakilishi wa Shirika hilo Zanzibar Dkt. Ghirmay Andemichael alisema jukumu la kuwa na dawa salama katika nchi linahitaji mashirikiano ya wadau mbali mbali ikiwemo taasisi za serikali, viwanda vya uzalishaji na waingizaji dawa.
Akizungumza katika mkutano huo, Mfamasia Mkuu wa Serikali ya Muungano wa Tanzania Hendry Kigunde alisema Jumuiya imetoa msukumo mkubwa katika kipindi cha miaka mitano tokea ilipoanzishwa kwa kuimarisha usambazaji wa dawa kwa njia za kisasa.
Alisema Serikali imefanikiwa kuboresha miongozo ya uingizwaji wa dawa na kuoredhesha dawa muhimu ambazo waingizaji wanashauriwa kuzipa kipaumbele kwa ajili ya matimizi ya wananchi.
Mkutano huo wa siku mbili utafanya mapitio katika kipindi cha miaka mitano cha Jumuiya ili kujua mafanikio yaliyopatika katika kutandika mifumo sahihi ya dawa kwa nchi wanachama na kufahamu changamoto zilizojitokeza katika kipindi hicho. 
Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Zanzibar Dkt. Ghirmay Andemichael akizungumza na washiriki wa mkutano wa mwisho wa Jumuia ya nchi za Afrika, Caribean na Pacific (ACP) wa kumiarisha mifumo ya kifamasia unaofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.
Mkurugenzi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) Dkt. Suzanne Hill akitoa hotuba katika ufunguzi wa mkutano wa mwisho wa kuimarisha mifumo ya upatikanaji wa dawa kwa nchi za ACP katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Wajumbe wa mkutano wa mwisho wa kuimarisha mifumo ya kifamasia wan chi za kanda ya Afrika Caribean na Pacific wakifuatilia ufunguzi wa mkutano huo unaofanyika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya nchi za ACP Balozi Emile Ognimba akizungumza na washirki wa mkutano wa mwisho wa kuimarisha mifumo ya kifamasia unaofanyika Zanzibar Beach Resort Mbweni.
Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Bi. Asha Abdalla Ali akifungua mkutano wa mwisho wa kuimarisha mifumo ya kifamasia unaoshirikisha mataifa ya Afrika Caribean na Pacific katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.Picha na MAKAME MSHENGA.

WAKULIMA WILAYANI HAI WASIFU MRADI WA N2AFRICA KWA MBEGU BORA ZA MAZAO YA MAHARAGE

Na Mathias Canal, Kilimanjaro


Wakulima wadogo katika Halmashauri ya Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro wameipongeza Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) yenye makao makuu yake nchini Nigeria kwa teknolojia walizoanzisha za kutafiti wadudu waharibifu na aina mpya ya mbegu za maharagwe aina ya Jesca, Lyamungo 90 na Uyole njano wanazozitoa kwa wakulima.

Wakulima hao wamesema kuwa mbegu hizo zimepelekea kuongezeka kwa uzalishaji wa mazao ya mbogamboga jamii ya mikunde huku katika Wilaya hiyo uzalishaji wa maharagwe ukiwa ndio ukombozi kwa wakulima kufuatia mafunzo na mbinu bora za kisasa wanazopatiwa na wataalamu wa (IITA) kupitia mradi wa N2AFRICA.

Wakizungumza kwa niaba ya wakulima wengine 30 katika Wilaya ya Hai Wanufaika wa mradi wa N2AFRICA Hashim Abdallah mkazi wa kitongoji cha Landi na Lucy David mkazi wa Kitongoji cha Madukani Kata ya weruweru wanasema kabla ya mradi huo walikuwa wanapanda kilo 60 za mbegu katika heka moja na mavuno ya gunia 3 mpaka 5 ambapo hivi sasa matarajio ya mavuno yao yataongezeka maradufu kwani wanatumia kilo 30 za mbegu kwenye heka moja na kuvuna gunia 10 mpaka 15.

Wakulima hao wameomba mafunzo ya kutengeneza mbegu bora za kilimo cha mbogamboga na mafunzo ya jinsi ya kuhifadhi mbegu hizo ili waweze kuendeleza uzalishaji wao wenyewe badala ya kuomba tena mbegu kutoka katika mradi huo wa N2AFRICA.

Pia wameiomba Taasisi ya (IITA) kupitia mradi wake wa N2AFRICA unaojihusisha na usambazaji wa teknolojia ya mazao jamii ya mikunde kuwasaidia kutafuta masoko ili kuboresha zaidi ufanisi wa mauzo yao mara baada ya mavuno.

Wakulima hao walisema kuwa Wakulima wadogo nchini Tanzania huzalisha asimia 70 ya chakula ingawa karibu nusu yao hawazalishi chakula cha kutosha kwa ajili ya mauzo.

Aidha, walisema Wamekuwa wakikabiliwa na ukosefu wa teknolojia ya kilimo cha kisasa, kukosa uwezo wa kujipatia pembejeo bora na kukosa huduma za kiufundi za ughani zinazoweza kuwasidia kukuza kilimo pamoja na ukosefu wa mafunzo jambo ambalo kwa sasa wameanza kunufaika nalo kupitia mradi wa N2AFRICA.

Kwa upande wake Afisa Kilimo (Mazao) Halmashauri ya Wilaya ya Hai Bi Matrida R. Massawe alisema kuwa upatikanaji mbegu bora za maharagwe zilizotolewa na mradi wa N2AFRICA zimekuwa na tija kubwa kwa wakulima kwani mavuno yameongezeka kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na msimu wa mavuno uliopita.

Alisema kuwa Mradi huo umetatua changamoto ya uduni wa kilimo kwa wakulima kwani walikuwa wakilima pasina kufuata mbinu bora za kilimo hivyo upatikanaji huo wa mbegu bora na mbinu za uongezaji rutuba kwenye udongo umekuwa mkombozi kwa wakulima kwani wanazalisha na kuuza mazao yao kwa faida kubwa.

Massawe aliwahimiza wakulima kuendelea kujifunza kanuni bora za kilimo na kuzingatia ushauri wa kitaalamu unaotolewa na mradi wa N2AFRICA katika uzalishaji wa mazao kwani kilimo kisichozingatia utaalamu na kanuni bora za kilimo hakiwezi kuwa na tija katika jamii.

Hata hivyo Mwaka 2017 katika msimu wa kilimo mafunzo yameendelea kutolewa na Mradi wa N2AFRICA kwa wakulima wa maharagwe ambapo wakulima 30 wamepata mafunzo ya mbegu daraja la kuazimiwa.

Aliwasihi wakulima kutumia fursa hiyo kupitia mradi wa N2AFRICA ili kuweza kuboresha kilimo cha maharagwe ambapo pia amewapongeza wadau hao wa kilimo wa N2AFRICA na kuwaomba kuendeleza kilimo hicho katika maeneo yote ya Wilaya ya Hai ili kunufaisha wakulima wengi zaidi.

Mradi wa N2AFRICA unaendeshwa na na Taasisi ya Kimataifa ya kilimo cha Kitropiki katika ukanda wa joto makao makuu yake ni nchini Nigeria chini ya ufadhili wa Bill na Melinda Gates na kuongozwa na Chuo Kikuu cha Wagenigen cha Uholanzi.


Lucy David akielezea jinsi alivyonufaika Mbegu za maharagwe zilizotolewa na Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) kupitia mradi wa N2AFRICA



Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Hashim Abdallah akiwa shambani kuendelea na shughuli zake za kusafisha majani katika shamba lake kabla ya mavuno.




Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) wakikagua shamba la Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Hashim Abdallah.



Muonekano wa mazao ya maharagwe yakiwa shambani kabla ya mavuno




Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) walipotembelea ofisi ya Afisa Kilimo, Umwagiliaji na ushiriki wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Ndg David Lekei





Afisa kilimo (Mazao) wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai Bi Matilda Massawe akielezea jinsi wakulima walivyonufaika na mradi wa N2AFRICA katika Wilaya ya Hiyo.



Muonekano wa shamba la maharagwe lililolimwa kwa kufuata mbinu bora na za kisasa za kilimo



Muonekano wa shamba la maharagwe lililolimwa bila kufuata mbinu bora za kilimo



Hashim Abdallah akielezea jinsi alivyonufaika Mbegu za maharagwe zilizotolewa na Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) kupitia mradi wa N2AFRICA

Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) wakikagua shamba la Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Hashim Abdallah.
Mkulima wa zao la maharagwe aliyenufaika na mbegu zilizotolewa na Mradi wa N2AFRICA Katika Kijiji cha Kikavu Chini, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro Mwantumu Abdillah akiwa shambani kuendelea na shughuli zake za kusafisha majani katika shamba kabla ya mavuno.
Mkulima wa zao la maharagwe Lucy David Katika Kitongoji cha Madukani, Kata ya Weruweru Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro akielezea mafanikio aliyoyapata kutokana na Mradi wa N2AFRICA, Wengine ni Wataalamu Kutoka Taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo ya (IITA) walipomtembelea shambani kwake.

WALIMU WA SAYANSI LINDI WAIOMBA SERIKALI KUWASAIDIA

Walimu wa masomo ya Sayansi mkoani Lindi wameiomba Serikali kuchukua hatua za haraka za kuandaa na kuimarisha miundombinu bora kwa shule za Sekondari zinazofundisha masomo hayo ili kuendeleza na kufufua vipaji vya wanafunzi.

Akizungumza kwa niaba ya walimu hao wakati wa ziara iliyofanywa na wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), kupitia Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara katika shule za mkoa huo,   Mwalimu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mchinga iliyopo  mkoani humo, Bw. Makopa Selemani , amesisitiza kwa Serikali kuona namna ya kujenga maabara  nyingi za sayansi ambazo zitakuwa na vifaa na kuongeza walimu wa Sayansi ambao wameonekana kuwa ni wachache katika mkoa huo.

"Tunaiomba Serikali kutazama kwa jicho la pekee shule za mkoa huu hususan zenye michepuo ya sayansi kwani si kwamba wanafunzi hawapendi masomo haya bali miundombinu hairidhishi", amesema Mwalimu Mkuu.
Aidha, Mwalimu Mkuu ameongeza kuwa ili kuwasaidia wanafunzi wa kike katika mkoa huo serikali iwajengee mabweni wanafunzi hao ili kuepusha kupata vishawishi kwani wengi wao wanaishi mbali na shule.

Mwalimu Mkuu Selemani, ameelezea baadhi ya mikakati ya shule yake katika kuhamasisha wanafunzi wa kike kusoma masomo ya sayansi ikiwemo kufanya vikao vya mara kwa mara na wanafunzi hao ili kujadili changamoto zao na kuzitatua.

Ametoa wito kwa Wizara kufanya ziara za mara kwa mara katika shule mbalimbali nchini ili kuhamasisha wanafunzi husasan wa kike kupenda na kujifunza masomo ya sayansi ambayo yameonekana kuwa ni vikwazo katika mkoa huo.

Kwa upande wake, Mhandisi  kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), kupitia Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi Liberatha  Alphonce,  amewasisitiza wanafunzi  wa kike mkoani humo kuanza kujituma na kujijengea misingi imara ya kupenda masomo ya sayansi wakiwa katika ngazi za awali ili kufikia malengo yao.

Amefafanua kuwa masomo ya Sayansi yanatoa fursa za kujiajiri na urahisi wa kupata mikopo kwa wanafunzi wanaochaguliwa kujiunga na elimu ya juu.Naye, mwanafunzi Shamira Salum, kutoka shule ya Sekondari ya Mchinga, ameiomba serikali kuongeza walimu na vifaa katika shule za mkoa huo ili kuweza kutimiza malengo yao ya kuwa wahandisi na madaktari wa baadae.
Ziara ya wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), kupitia Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara imelenga kutoa elimu na kuhamasisha wanafunzi wa kike nchini kusoma masomo ya sayansi ambapo pamoja na mambo mengine wahandisi hao wametembelea shule ya sekondari ya Mchinga, Lindi, Mkonge na Mingoyo ambazo zipo mkoani Lindi.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano.
 Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Liberatha Alphonce, akionesha mfano wa picha iliyochorwa kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi (hawapo pichani), ili kuhamasisha wanafunzi kupenda masomo ya sayansi.
 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi, wakimsikiliza Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Liberatha Alphonce (hayupo pichani) wakati akitoa mada kuhusu uhamasishaji wa masomo ya Sayansi kwa wasichana.
 Wahandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, wakisikiliza maoni kutoka kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi walipotembelea shule hiyo kuhamasisha usomaji wa masomo ya Sayansi kwa wasichana.
 Baadhi ya Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi, wakionesha ndoto zao kwa Wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, walipotembelea shule hiyo kuhamasisha usomaji wa masomo ya Sayansi kwa wasichana.
 Mwanafunzi kutoka Shule ya Sekondari ya Lindi, akitoa maoni yake kuhusu changamoto  zinazokabili shule  yao kwa Wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara.
Mhandisi kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, Bi. Rahma Mwinyi, akigawa zawadi ya madaftri kwa wanafunzi wa shule ya Mkonge mkoani Lindi ili  kuhamasisha wanafunzi  hao kupenda masomo ya sayansi.
 Wahandisi wa kike kutoka Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi), Kitengo maalum cha ushirikishwaji wa wanawake katika masuala ya barabara, wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya walimu pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Mchinga mkoani Lindi.

Wawekezaji wazungumzia ushindani unavyoathiri bidhaa za ndani


WAWEKEZAJI katika sekta ya kilimo na mifugo wamelalamikia ushindani unaoletwa na bidhaa kutoka nje kutokana na serikali kushindwa kuzidhibiti kwa njia ya kupunguza kodi na tozo mbalimbali katika uzalishaji.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana wawekezaji hao ambao pia ni sehemu ya wabia wa Kituo cha Kuendeleza Kilimo Kusini mwa Tanzania (SAGCOT), wakati wa ziara ya wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Kilimo, Mifugo, Maji na Umwagiliaji katika Kongani ya Ihemi mkoani Iringa na Njombe, walisema ipo haja serikali ikaangalia suala hilo kwa jicho pana ili kulinda bidhaa za ndani.

Mkurugenzi wa kiwanda cha maziwa cha ASAS Dairies Limited kilichopo mkoani hapa, Bwana Fuad Abri alisema haiwezekani Tanzania iwe nchi ya pili kwa idadi ya ng’ombe barani Afrika baada ya Ethiopia lakini bado inapitwa katika uzalishaji na uingizaji maziwa nchini.

“Wenzetu Kenya wanazalisha lita 1,500,000 za maziwa kwa siku lakini Tanzania inazalisha lita 120,000 kwa siku. Wakati huohuo sisi tunawapita kwa umbali katika idadi ya ng’ombe, kama hiyo haitoshi bidhaa za maziwa kutoka mataifa jirani zinaingia kwa wingi na kutoa ushindani mkubwa na bidhaa za ndani,” alisema Bw. Abri.

Alisisitiza kuwa zipo namna nyingi za kuzuia ushindani huu kwa sababu Serikali ya Kenya inashirikiana kwa kiasi kikubwa na wazalishaji maziwa na ndiyo maana wana uwezo wa kusafirisha nje kwa bei shindani.

“Katika biashara hii ya maziwa kitu kikubwa kinachotakiwa kuangaliwa ni namna gani unapata maziwa yako, bei utakayonunulia ikupe faida lakini faida yenyewe iwe katika soko shindani,” alisema Bw. Abri.

Wabunge hao wakiongozwa na mwenyeji wao Mkurugenzi Mtendaji wa SAGCOT, Bwana Geofrey Kirenga ambapo kwa upande wao waliongozwa na kaimu mwenyekiti wa kamati Bwana. Mashimba Ndaki, walitembelea kiwanda cha kuzalisha chakula cha mifugo na ufugaji kuku wa nyama na mayai, Silver Land kilichopo mkoani hapa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho, Bwana Jack Bennie alisema mbali ya kuwepo na utaratibu wa kulipa kiasi kidogo cha kodi kutokana na utaratibu wa kiuwekezaji lakini bado bidhaa za kuku na chakula cha mifugo vinaathiri soko kutokana na kuzalishwa chini ya kiwango lakini vingine vinaingia nchini na kuuzwa kwa bei ndogo inayovuruga ushindani.

“Tumeamua kufanya uwezekazi mkubwa katika sekta hii ya mifugo, lakini kuna tatizo la ushindani usioendana na uhalisia ambapo bidhaa kutoka nje zilituathiri kwa kiasi kikubwa, tunashukuru kwa sasa serikali imezuia kuingiza vifaranga vya kuku kutoka nje, tunaomba washikilie hapohapo kwa sababu kukosekana kwa vifaranga hivyo kumesaidia wazalishaji wa ndani kupata soko,” alisema Bwana Bennie. Akizungumzia hali hiyo mmoja wa wajumbe wa kamati hiyo Dkt. Immaculate Sware alisema wawekezaji wakubwa namna hiyo ni fursa kwa watanzania hivyo serikali haina budi kuangalia namna ya kuwatengenezea mazingira mazuri ya biashara ili walipe kodi vizuri lakini pia wanufaishe jamii.

“Tumetembelea miradi mingi iliyo katika ubia na SAGCOT, mradi huu wa Silverlands ni mkubwa kwa hiyo tunapopata muda wa kusikiliza kero zao inakua jambo jema kujua namna ya kuzifikisha ili zitatuliwe na kusaidia jamii ambayo ndiyo wanufaika kwa njia nyingi ikiwemo kupata ajira na kupata huduma au bidhaa,” alisema Dkt. Sware.

SAGCOT imeamua kuwatembeza wajumbe wa kamati hiyo ya bunge ili kuona shughuli zinazofanyika katika kongani ya Ihemi ambayo ni miongoni mwa kongani sita zilizopo katika kituo hicho. Maeneo mengi waliyotembelea ni ile inayosimamia mnyororo wa ongezeko la thamani katika mazao ya nyanya, viazi mviringo, soya na maziwa.
 Mkurugenzi wa kiwanda cha maziwa cha ASAS Dairies Limited mkoani Iringa, Bwana Fuad Abri akitoa mada juu ya uendeshaji wa kiwanda chake na ubia wao na Kituo cha Kuendeleza kilimo Nyanda za juu kusini mwa Tanzania (SAGCOT) alipotembelewa na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Kilimo,Mifugo , Maji na Umwagiliaji. Lengo la ziara ya Kamati hiyo ni kujionea na kujifunza juu ya Kongani ya Ihemi na shughuli za SAGCOT.
Mkurugenzi wa kiwanda cha maziwa cha ASAS Dairies Limited, Bwana Fuad Abri (kulia)akitoa maelekezo ya uendeshaji wa kiwanda chake alipotembelewa na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Kilimo,Mifugo , maji na umwagiliaji. Ikiwa ni sehemu ya ziara ya kamati hiyo kujionea na kujifunza juu ya kongani ya Ihemi na shughuli mbalimbali za Mpango wa Kuendeleza Kilimo Nyanda za juu kusini mwa Tanzania(SAGCOT). Wapili kulia ni Kaimu Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni mbunge wa Maswa Magharibi, Bwana Mashimba Ndaki. Watatu kulia ni Mjumbe wa kamati ambaye pia Mbunge wa viti Maalum Bibi Khadija Hassan Aboud. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa SAGCOT , Bwana Geoffrey Kirenga

TANZANIA THE BEST DESTINATION FOR INVESTMENTS IN AFRICA - MWAMBE TIC.


Wabunge watwangana mjadala wa ukomo wa umri wa rais


Kampala, Uganda. Mjadala kuhusu mpango tata wa kuondoa ukomo wa umri kwa mgombea urais juzi ulipamba moto hadi baadhi ya wanasiasa wakafikia hatua ya kushambuliana.
Mbunge wa Kaunti ya Ayivu Bernard Atiku alionekana akivurumishana na mwenzake wa Manispaa ya Arua, Mr Ibrahim Abiriga, mmoja wa wabunge wanaounga mkono kuondolewa ukomo wa umri.
Alipoulizwa Atiku kuhusu ugomvi wao alisema ulitokana na Abiriga kumshutumu kuwa alikodi vijana wa kumshambulia (Abiriga) wakati wa mechi ya mpira kati ya klabu ya Onduparaka na Maroons FC iliyochezwa Luzira.
"Nilikuwa nje ya Bunge kwa ajili ya kuchukua baadhi ya nyaraka zilizokuwa kwenye gari langu ndipo nikamwona Abiriga akiwa na kikundi cha wanahabari amesimama kwenye ngazi za jingo la Bunge. Mheshimiwa (David) Abala (wa Kaunti ya Ngora) alinisimamisha kwa ajili ya kujua habari fulani. Kwa hiyo, wakati nazungumza naye, nikamsikia Abiriga akinitukana. Kisha nilipowasogelea kumuuliza alikuwa anasema nini, Abiriga alianza kunitukana kuwa mimi ni mpumbavu na mjinga," alisema.
Atiku alisema: "Yeye (Abiriga) alidai kwamba niliwakodi vijana kumtukana wakati wa mechi kati ya Onduparaka na Maroons FC, Luzira. Nilipojaribu kumweleza Abiriga kwamba mimi sikuwepo kwenye mechi hiyo ya Jumamosi, yeye alisisitiza kwamba nilikuwepo na akaanza kunishambulia. Nilimsukuma na ndipo polisi wakafika kututenganisha."
Naibu Spika, Jacob Oulanyah amesema alipokea taarifa kutoka kwa Mbunge mmoja akiomba kuwasilisha hoja bungeni akiipa serikali maoni kuhusu ukomo wa umri kwa mgombea urais.

Mahakama ya juu nchini Kenya inaendelea kutoa sababu za kufutwa matokeo ya Urais

Naibu jaji mkuu Philomena MwiluHaki miliki ya pichaNTV
Image captionNaibu jaji mkuu Philomena Mwilu
Nibu jaji mkuu nchi Kenya Philomena Mwilu, amesema kuwa kushindwa kwa IEBC kufuata agizo la mahakama kuhusu madai yaliyoibuliwa na upinzani, inaonyesha kuwa madai ya udukuzi yalikuwa ni ya ukweli.
Jaji Mwilu amesema mahakama ilikubaliana madai ya upinzani kuwa matokeo yalitangazwa kabla ya matokeo yote kutoka kwa vituo 40,000 kupokelewa.
"Uchaguzi haukuwa na uwazi na hatukuwa na lingine ila kuufuta," jaji alisema.
Jaji Mwilu amesema tume ya IEBC ilitegemea ripoti za waangalizi wa uchaguzi kuamua kuwa uchaguzi ulikuwa wa haki.
Tume ya uchaguzi imelaumiwa vikaliHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionTume ya uchaguzi imelaumiwa vikali
Waangalizi walikosolewa vikali wakati uchaguzi ulifutwa kwa kuharakisha kusema kuwa uchaguzi ulikuwa huru na wenye uwazi.
Kwa upande wake jaji mkuu nchini Kenya David Maraga, amesema kuwa upinzani hakubaini madai yao kuwa kampeni za rais zilitumia fedha za umma kugharamia kampeni zao.
Jaji Maraga amesema kuwa sampuli kadha za fomu zilionyesha kuwa hazikuwa na mihuri rasmi, zingine hazikwa na sahihi na namba za usajili wala alama rasmi.
Jaji mkuu nchini Kenya David MaragaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionJaji mkuu nchini Kenya David Maraga
Amesema kuwa uchaguzi haukufutwa tu kwa sababu ulikuwa na hitilafu, lakini kile amekuwa akikichunguza ni ikiwa hitalafu hizo zilishawishi matokeo.

Hotuba ya Trump kwenye Umoja wa Mataifa yakosolewa

US President Donald Trump at the UN General Assembly in New York, 19 SeptemberHaki miliki ya pichaEPA
Image captionHotuba ya Trump kwenye Umoja wa Mataifa yakosolewa
Hotuba ya kwanza kuu ya rais wa Mareknai Donald Tump kwenye Umoja wa Mataifa imekosolewa na baadhi ya chi wanachama.
Rais Trump alizitaja nchi zikiwemo Iran akisema pia kuwa Marekani itaiharibu kabisa Korea Kaskazini ikiwa italazimika kafanya hivyo.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Iran alisema, "hotuba ya Trump ni ya wakati ya mikutano ya wanahabari wala sio kwa Umoja wa Mataifa.
Donald Trump speaks to world leaders at the UN General Assembly at UN headquarters in New York, 19 SeptemberHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionHotuba ya Trump kwenye Umoja wa Mataifa yakosolewa
Korea Kaskazini bado haujajibu tisho la Trump kuwa itaharibiwa.
Hotuba ya Trump ilizungumzia zaidi dunia yenye mataifa huru ambayo yana malengo ya kuinua maisha ya watu wao, lakini akatumia muda mwingi akilenga kile alichokija kuwa mataifa yanayoleta matatizo duniani.
Marekani mara kwa mara imeionya Korea Kaskazini kwa majaribio yake ya zana, yanayokiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa.
Kim Jong-un watches a missile launch from North Korea, 16 SeptemberHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionMarekani mara kwa mara imeionya Korea Kaskazini kwa majaribio yake ya zana, yanayokiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa
Siku ya Jumanne Trump alimkosoa Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un, akimtaja kuwa mtu wa makombora ambaye yuko katika harakati za kujitia kitanzi.
"Ikiwa Marekani italazimika kujilinda na washirika wake, hatutakuwa na cha kufanya bali tutaiharibu kabisa Korea Kaskazini," aliongeza Trump.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Sweden ambaye alikuwa ameketi katika kikao hicho, alisema kuwa ilikuwa hotuba mbaya, wakati usiofaa na kwa watu wasiostahili.
Trump speaking at the UNHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionHotuba ya Trump kwenye Umoja wa Mataifa yakosolewa
Trump pia aliishambulia nchi ya Venezuela akitaja serikali yake kuwa fisadi na ya kiimla na kuonya kuwa Marekani iko tayari kuichukulia hatua.
Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni wa Venezuela Jorge Arreaza alipinga kile alichokitaja kuwa vitisho.
"Trump sio rais wa dunia, hata hawezi kuongoza serikaii yake," alisema.
A five-part composite showing reactionHaki miliki ya pichaUN / EVN
Image captionWaakilishi kutoka Israel, Syria, Iran, na Saudi Arabia wakiisikiliza hotuba ya Trump
Akizungumza katika kikao hicho rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, aliteta mkataba wa nyuklia na Iran, akisema kuwa kuuvunja itakuwa makosa makubwa.
Lakini waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alimuunga mkono Bw. Trump. Kwenye hotuba yake aliseka mkataba wa Iran unastali kufanyiwa marekebisho au ufutwe kabisa, na kuonya dhidi ya kukua kwa ushawishi wa Iran eneo la mashariki ya kati.