Wednesday, October 11

VIJIMAMBO: Mbwa aweka rekodi mpya ya dunia

Mbwa mwenye ulimi mrefu zaidi duniani
VIJIMAMBO na BMJ Muriithi Mbwa mmoja nchini Marekani, ameweka rekodi ya kuwa na ulimi mrefu kuliko mbwa mwingine yeyote duniani. Moch Richert, ambaye anajulikana kwa jina la utani kama MO, ana umri wa miaka minane na anatokea mjini Sioux Falls, katika jimbo la South Dakota.
Kitabu cha Guiness Book of world records kimemuorodhesha mbwa huyo kama aliyeweka rekodi mpya kwa kuwa na ulimi wenye urefu wa ajabu.
Mwenye mbwa huyo, Carla Richert, amewaambia waandishi wa habari kwamba;
"Ulimi wake una urefu wa inch 7.3 ambazo ni kama centimita 18.58," alisema Richert.
Moch sasa amechukua nafasi iliyoshikiliwa na mbwa aitwaye Puggy ambaye alikuwa amemshinda mbwa aliyepata umaarufu mkubwa Zaidi duniani Brandy the Boxer takriban miaka 10 iliyopita.
Je wewe msikilizaji, iwapo una mbwa, una habari ulimi wake una urefu kiasi gani?
Tafakari hayo.
Ukitafakari hayo, hebu tuone mengine yaliyojiri katika maeneo mengine duniani.
Tunasafiri moja kwa moja hadi kaunti ya Migori nchini Kenya. Kulikoni?
Wakazi wanalalamika kuwa miili ya watu waliokufa imekuwa ikifukuliwa na wanyama kwa sababu ya kuzikwa kwenye makaburi ambayo hayana urefu wa kutosha.
Amini usiamini msikilizaji, watoto wengi wamekuwa wakilalamika kwamba awamekuwa wakipata mili barabarani ambayo imevutwa na baadhi ya wanyama katika eneo hilo. Kulikoni?

Mkosoaji mkubwa wa Rais Kagame akana mashtaka dhidi yake

Diane Rwigara
Image captionDiane Rwigara
Mwanasiasa wa upinzani nchini Rwanda Diane Rwigara mama yake na dada yake, wote wamekana mashtaka dhidi yao yanayohusu kuchochea uasi, walipofikishwa kwenye mahakama ya mjini Kigali.
Hata hivyo jaji alihairisha kesi hiyo baada ya mama yake Rwigara, Adeline Rwigara, ambaye anakabiliwa na mashtaka tofauti kusema anataka wakili wake kuweza kumuakilisha.
Diane Rwigara tayari anakabiliwa na mashtaka ya kubuni stakabadhi bandia, alizopanga kutumia kuwania urais wakati wa uchaguzi wa mwezi Agosti.
Alizuiwa kugombea uchaguzi huo ambao ulishindwa na Rais Paul Kagame.
Mwanaharakati huyo maarufu wa masuala wa wanawake na mkosoaji mkubwa wa Bw. Kagame, alisema kuwa mashtaka dhidi yao yamechochewa kisiasa.
Wote hao bado wako katika kuzuizi cha polisi.

RAIS DKT MAGUFULI AKUTANA NA KIONGOZI WA JUMUIYA YA ISMAILI DUNIANI H.H. PRICE KARIM AL-HUSSAYNI AGA KHAN IKULU JIJINI DAR ES SALAAM LEO




 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpokea kiongozi wa Jumuiya ya Ismailia H.H.Prince Karim al-Hussayni Aga Khan alipotembelea Ikulu jijini Dar es Salaam Oktoba 11, 2017.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiteta  jambo na kiongozi wa Jumuiya ya Ismailia H.H.Prince Karim al-Hussayni Aga Khan alipotembelea Ikulu jijini Dar es Salaam Oktoba 11, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo na kiongozi waJumuiya ya Ismailia H.H.Prince Karim al-Hussayni Aga Khan alipotembelea Ikulu jijini Dar es Salaam Oktoba 11, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pome Magufuli na viongozi wengine wa serikali katika picha ya pamoja na kiongozi waJumuiya ya Ismailia duniani H.H. Prince Karim al-Hussayni Aga Khan na ujumbe wake alipomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 11, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsindikiza kiongozi wa Jumuiya ya Ismailia duniani H.H. Prince Karim al-Hussayni Aga Khan alipomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 11, 2017.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Kiongozi wa Jumuiya ya Ismailia duniani H.H. Prince Karim al-Hussayni Aga Khan wakiongea na wanahabari (hawapo pichani) mgeni huyo alipomtembelea Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 11, 2017.


PICHA NA IKULU

Uchaguzi nchini DRC wahairishwa hadi 2019

Uchaguzi ulipangwa kufanyika Novemba mwaka 2016, lakini ukafutwa na tume ya uchaguzi kutokana changamoto za usafiri na za kifedha.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionUchaguzi ulipangwa kufanyika Novemba mwaka 2016, lakini ukafutwa na tume ya uchaguzi kutokana changamoto za usafiri na za kifedha.
Uchaguzi nchini Jamhuri ya Demokrasi ya Congo hautafanyika hadi mwezi Aprili mwaka 2019, kwa mujibu wa tume ya uchaguzi nchi humo.
Katika taarifa tume ilisema kuwa inahitaji takriban siku 504 kuweza kuandaa uchaguzi huo mara usajili wa wapiga kura utakapokamilika
Hii ni kinyume kabisa na makubaliano kati ya Rais Joseph Kabila na upinzani, ulioongozwa na kanisa katoliki kuwa uchaguzi ungefanyika kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Uchaguzi ulipangwa kufanyika Novemba mwaka 2016, lakini ukafutwa na tume ya uchaguzi kutokana changamoto za usafiri na za kifedha.
Hii ina maana kuwa Rais Joseph Kabila amekaa madarakani kinyume na muda unaostahili kisheria.
Watu kadhaa waliuawa wakati wa maandamano.
Kulingana na shirika la habari la Reuters, mapigano katika eneo la Kasai yamechelewesha shughuli ya usajili wa wapiga kura.

Mavazi ya naibu gavana benki kuu Nigeria yazua mjadala mkali mitandaoni

Aisha AhmadHaki miliki ya pichaAISHA AHMAD/FACEBOOK
Image captionAisha Ahmad
Uteuzi wa mwanamke muislamu kuwa naibu wa gavana wa benki kuu nchini Nigeia, umezua mjadala mkali huku baadhi ya wale wenye misimamo mikali ya dini ya kislamu wakikosoa jinsi anavyo vaa.
Aisha Ahmad, 40, anatoka eneo la kaskazini mwa Nigeria, eneo ambapo wasichana wengi hupata masomo duni ikilinganishwa na sehemu za kusini mwa nchi.
Baada ya habari kuhusu kuteuliwa kwake kufichuka, mjadala uligeuka kutoka jinsi amehitimu na kuangazia mavazi yake.
Baadhi ya viongozi wa dini walio na wafuasi wengi mitandaoni walinukuu Koran, na kusisitiza kuwa wanawake ni lazima wavae kwa njia inayostahili
Picha zake zinamuonyesha akiwa amevaa nguo ya kawaida bila ya kujifunika kichwa chake
Lakini mwandishi mmoja nchini Nigeria Gimba Kakanda, ameiambia BBC kuwa, shutuma hizo zilivuka mipaka kwa kuwa eneo la kaskazini mwa nchi lina matatizo mengi ya kushughulikiwa .

Mpinzani aponda Serikali, Mahakama ya Katiba


Lusaka, Zambia. Rais wa chama cha upinzani chaUnited Party for National Development (UPND), Hakainde Hichilema ameishambulia serikali na akaiita Mahakama ya Katiba kuwa ya walarushwa.
Akizungumza na waandishi wa habari nyumbani kwake New Kasama jana, Hichilema amesema Rais Edgar Lungu anaongoza genge la wahalifu ambalo linaendesha mipango ya kifisadi nchini.
Alisema watu waliokuwa wanamsema kwamba amepunguzwa makali baada ya kukaa kwa miezi kadhaa mahabusu watajisikitikia wenyewe kwani kwa sasa ni madhubuti zaidi. Pia alisema ataheshimu kufanya majadiliano na Rais Lungu.
"Ila siku hizi wala sisemi kwa kuzunguka, nasema wazi kwamba Jaji Anne Sitali ni fisadi, Palan Mulonda ni fisadi, Mungeni Mulenga pia fisadi. Hii ndiyo sababu tunatoa wito kuwa Mahakama ya Katiba ifumuliwe," amesema.
Mahakama ya Katiba imejitengenezea wigo kwamba maamuzi yake mtu hawezi kukata rufaa lakini ndiyo ilisaidia rufa juu ya mawaziri waliobainika wakihudumu kinyume cha sheria baada ya Bunge kuvunjwa.
Hichilema amesema idara ya mahakama inapaswa kuvunjwa na kutimuliwa wote kwa kuwa imevamiwa na sura za kifisadi.
Kadhalika kiongozi huyo wa UPND amemshutumu Spika wa Bunge la Taifa Patrick Matibini akimwita kuwa ni wakala wa chama tawala cha Patriotic Front.
"Ikiwa kuna genge la wezi basi lazima awepo kiongozi wa genge hilo na sote tunamfahamu kiongozi huyo ni nani," amesema.
Hichilema amesema mjadala uliopendekezwa na Jumuiya ya Madola ulikuwa muhimu kwa ajili ya kusaidia kurejesha uhusiano mzuri kati ya serikali na upinzani. Alisema alishtushwa kusikia baadhi ya watu wakimtaka akae kimya licha ya kutopatiwa ufumbuzi masuala kadhaa kuhusiana na uchaguzi mkuu wa mwaka 2016.
Hichilema alisema watu wanaweza kumlaumu kwa kuanzisha mashambulizi dhidi ya serikali kuhusiana na matokeo ya uchaguzi lakini hatanyamaza. Alisema Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zambia, Jaji Esau Chulu lazima ajiuzulu na afuate nyayo za mkurugenzi wa ECZ Priscilla Isaacs ambaye mkataba wake haukuhuishwa.

Hospitali ya Aga Khan kupanuliwa


Dar es Salaam. Kiongozi wa Jumuiya ya Ismailia, Mtukufu Aga Khan amesema  wamedhamiria kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kupanua hospitali.
Amesema Hospitali ya Aga Khan jijini Dar es Salaam itapanuliwa na pia watajenga chuo kikuu kikubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki mkoani Arusha.
Mtukufu Aga Khan amesema hayo leo Jumatano Ikulu jijini Dar es Salaam, alipofanya mazungumzo na Rais John Magufuli.
Amesema upanuzi wa hospitali utahusisha kuongeza idadi ya vitanda vya wagonjwa kutoka 72 vya sasa hadi 172, kuimarisha matibabu ya moyo na saratani.
Taarifa ya Ikulu kwa vyombo vya habari imesema upanuzi wa hospitali pia utahusisha ufundishaji wa madaktari na wataalamu wengine wa afya.
Kuhusu chuo kikuu, Mtukufu Aga Khan amesema jumuiya imedhamiria kujenga kikubwa ambacho kitafundisha viongozi si tu wa Tanzania na Afrika Mashariki, bali Afrika nzima ili wawe chachu ya mabadiliko na maendeleo.
Rais John Magufuli katika taarifa hiyo amemshukuru Mtukufu Aga Khan kwa taasisi zake kutoa huduma za kijamii nchini Tanzania.
Ametoa wito kwa taasisi hizo kupunguza gharama za huduma ili wananchi wamudu na hasa ikizingatiwa kuwa zimekuwa zikipata msamaha wa kodi kutoka serikalini.
Rais Magufuli amesema Serikali ipo tayari kuendeleza na kuimarisha ushirikiano na Aga Khan na amemuomba kiongozi huyo wa dini kuendelea kupanua wigo wa huduma za taasisi zake ikiwa ni pamoja na kuwekeza mjini Dodoma yaliko makao makuu ya Serikali.
Kuhusu vyombo vya habari, Mtukufu Aga Khan amesema haamini kuwa ni kipaumbele kwa vyombo  hivyo kujikita katika masuala ya siasa.
Amesema anaamini kuwa vyombo vya habari vina wajibu mpana zaidi wa kujikita katika masuala ya maendeleo na hasa katika nchini zinazoendelea na kwamba, Aga Khan ipo katika mchakato wa kujikita katika wajibu huo kwa kuwa na waandishi wa habari na wachambuzi mahiri.
Soma: Rais Museveni amvika nishani ya heshima Aga Khan

UN yafichuwa mkakati wa majeshi ya Myanmar kufuta athari za Waislam wa Rohingya

Mtoto anapewa chanjo katika kambi ya wakimbizi ya Waislam wa Rohingya
Umoja wa Mataifa imesema kuwa uvunjifu wa amani unaoendelea magharibi ya Jimbo la Rakhine, Myanmar ni sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na kuratibiwa na majeshi ya serikali ili kuhakikisha inawaondosha kabisa Waislam wa Rohingya katika eneo hilo.
Ripoti iliyotolewa Jumatano huko Geneva na ofisi ya haki za binadamu ya UNimewatuhumu wanajeshi wa Myanmar, wakisaidiwa na makundi ya wanajeshi wakibudha wenye silaha, kwamba siyo tu wameshambulia majumba ya Waislam wa Rohingya na vijiji vyao lakini pia wamekuwa wakijaribu “kuondoa kabisa alama na kumbukumbu zote za watu hao katika ardhi yao” huko eneo la Rohingya ili kufanya watu hao wasiweze kuwepo kabisa katika nchi hiyo.

Zaidi ya wakimbizi nusu milioni wamekimbia Myanmar kuelekea eneo la Bangladesh Cox Bazar tangu Agosti 25, wakati mashambulizi katika vituo vya usalama yalipofanywa na wapiganajiwa Rohingya na kusababisha majeshi ya Myanmar kutumia nguvu kupita kiasi kupambana nao. Lakini ripoti ya UN iliyokuwa imejikita katika mahojiano 65 iliyofanya na mamia ya wakimbizi, imesema kuwa operesheni ya kuwaondosha Waislam wa Rohingya huko eneo la Rakhine ilianza mapema kwa mwezi moja takriban.
Wakimbizi wamewaambia wachunguzi wa UN kwamba hata kabla ya mashambulizi na baada yake, vyombo vya usalama vilitumia vipaza sauti kuwashinikiza Waislam kukimbia eneo hilo na kutafuta hifadhi huko Bangladesh, la sivyo “tutachoma nyumba zenu na kuwaua.” Pia Waislam wa Rohingya wameeleza visa vilivyofanywa na vyombo vya usalama ikiwemo kuwapiga risasi wanavijiji na ubakaji wa makundi kwa wasichana wadogo chini ya miaka mitano yaliofanywa na askari wasio na magwanda.
Mkuu wa haki za binadamu UN Zeid Ra’ad al-Hussein siku za nyuma ameelezea vitendo viovu dhidi ya watu wa Rohingyas“ni somo la mfano wa mauaji ya halaiki.”
Maafisa wa Myanmar hawakuwa na maelezo mara moja dhidi ya ripoti hiyo mpya ya UN.
Watu wa Rohingya wasiokuwa na utaifa kwa muda mrefu wamenyimwa haki zao za msingi katika nchi ya Myanmar yenye mabudhaa walio wengi, ambao wanawachukulia kama wahamiaji kutoka Bangladesh, pamoja na kuwepo ushahidi kuwa familia nyingi za Waislam hao wameishi katika nchi hiyo kwa vizazi vingi.

Dk Ndugulile azikabidhi NGO maendeleo ya jamii

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Watoto, Dk Faustine Ndugulile (kulia) akizungumza na watumishi wa Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii jijini Dar es Salaam jana. Picha na Midraji Ibrahim 
Wakati uhakiki wa mashirika yasiyo ya Serikali (NGO) ukiendelea, Naibu Waziri wa Afya, Maendelo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk Faustine Ndugulile ameripoti ofisini na kuitaka Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii kuratibu shughuli za mashirika hayo.
Dk Ndugulile alisema lengo ni kuhakikisha mashirika hayo yanafanya kazi kulingana na uanzishwaji wake.
Aliyasema hayo jijini Dar es Salaam jana alipozungumza na watumishi wa Wizara ya Afya Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, kujitambulisha kufuatia kuteuliwa hivi karibuni na Rais John Magufuli.
Alisema licha ya idara hiyo kuwa na kanzi data kwa ajili ya NGO, lazima ifuatilie utendaji wa mashirika hayo kwa kuwa baadhi yake yamekuwa yakienda kinyume na malengo.
“Ni vizuri NGO za kimataifa ziwe na sura ya kimataifa na zile za kitaifa zibaki na sura hiyo, wakati mwingine hasa kipindi cha uchaguzi baadhi ya mashirika hayo hujishughulisha na siasa na kuacha malengo yake,” alisema.
Kuhusu huduma za jamii kwa wazee, Dk Ndugulile alisema licha ya jitihada zinazofanywa, eneo hilo lina changamoto kubwa hususan katika misamaha ya huduma za afya na nyumba za kuwahifadhia.
Dk Ndugulile alisema wakati mwingine vituo vya kuhifadhia wazee vimelazimika kufungwa, au kusaidiwa na watu wengine tofauti na idara husika.
Naye Msajili wa NGO, Marcel Katemba alimweleza Dk Ndugulile kuwa idara hiyo inaendelea na uhakiki wa mashirika yasiyo ya Serikali nchini, lengo likiwa ni kuhuisha orodha na kuboresha kanzi data ili kupima utekelezaji wa majukumu yake.
Katemba alisema Tanzania ina mashirika yasiyo ya Serikali yapatayo 9,000 na kwamba, uhakiki huo utaisaidia idara hiyo kufuatilia shughuli za NGO kwa ukaribu.

Uvumi wasababisha polisi kutumia mabomu kutawanya wananchi


Mbeya. Uvumi kuhusu mwanamke mwizi wa nyanya kushindwa kutua tenga umesababisha polisi kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi mjini Mbalizi.
Hali ya taharuki imewakumba wananchi wa mji mdogo wa Mbalizi leo Jumatano baada ya mtu au watu wasiojulikana kuvumishwa kuwa mwanamke huyo baada ya kushindwa kutua tenga alikimbilia kituo cha Polisi Mbalizi kuomba msaada.
Uvumi huo ulieleza kuwa, mwanamke huyo aliimba nyanya sokoni Mbalizi.
Katika tukio hilo jana mchana Polisi walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi waliovamia kituo hicho ili kumuona mtuhumiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohammed Mpinga amesema uvumi huo ulienezwa na watu au mtu asiyejulikana kwamba kuna mwanamke aliiba tenga la nyanya sokoni Mbalizi lakini alipojaribu kulishusha kutoka kichwani ilishindikana, hivyo akaamua kwenda kituo cha polisi kuomba msaada.
“Wakati wa taharuki kama ile kila mtu anakuwa na tabia na nia yake, ndiyo maana imelazimika kutumia nguvu kidogo kuwanyamazisha watu kwa mabomu. Ule ni uvumi tu ambao hata hatujamfahamu aliyeeneza alikuwa na mlengo gani kwa kuwa hakuna tukio kama hilo,” amesema.
Kamanda Mpinga amesema sasa hali ni shwari na wananchi wameelimishwa wakaondoka kwenda sehemu zao za biashara na shughuli nyingine.
Mwenyekiti wa Soko la Mbalizi A ambako kituo cha polisi kipo, Geofrey Msigwa amesema hakuna kitu kama hicho bali naye aliona watu wengi wakielekea kituoni jambo lililosababisha polisi kuwatawanya kwa mabomu.
Amesema, “Hii ni hatari kwa mtu kusikia jambo bila kulifanyia utafiti na kuanza kulizusha bila kutambua athari inayoweza kutokea.”
Amelaani kitendo hicho akisema kinahatarisha usalama na amani.
Pia, amewaonya watu kutokimbilia vitu ambavyo ni vya kusikia bila kuvifanyia uchunguzi kwa kuwa inaweza kuwagharimu.
Msigwa amesema hawana taarifa za wizi huo na wanashangazwa na uvumi huo.

KUPATA ZUIO LA MAHAKAMA.

Image result for ZUIO LA MAHAKAMA
NA   BASHIR   YAKUB - 

1.ZUIO  LA  MAHAKAMA  NININI.

Ni  amri  inayotolewa  na  mahakama  kumzuia  mtu  kutofanya  jambo  fulani  kwa  muda. Kampuni  nayo  ni  mtu  ambapo  yaweza  kuomba  zuio  au  kuzuiwa. Aidha yeyote  ana  haki ya  kuomba  amri  hii  ikiwa  anaona  kuna  jambo  fulani  linafanyika  na  ikiwa  litaendelea  kufanyika  basi  litaharibu  au  kupoteza  kabisa  kitu  fulani.

Kwahiyo  zuio   ni  amri inayobeba  maagizo  maalum  kwa  mtu  au  watu  maalum kuwaamrisha  kutoendelea  na  kitu  fulani  kama  tulivyoona  hapo  juu.Sheria  ya  Mwenendo  wa Madai,  Sura  ya  33 na Sheria  nyingine  mtambuka zimeongelea  kuhusu  zuio.

2.   KATIKA   MATUKIO   GANI  UNAWEZA  KUOMBA  ZUIO.

( a ) Kwa  mfano, umeshindwa  kulipa  mkopo  na  tayari  una  taarifa  kuwa  benki au  taasisi  yoyote  ya  fedha  inataka kwenda  kuuza  na  unahisi  kuna  pahala   hapaendi  sawa katika  mikataba yenu.
 Basi  unaomba  zuio  ili  hiyo  mali  yako  uliyoweka  rehani  isiuzwe  mpaka  hapo  hilo eneo  ambalo  mmeshindwa  kuelewana  litakapopatiwa  majibu.

( b ) Kwa mfano, umemuuzia  mtu  gari, pikipiki,  au  mashine  yoyote.  Mtu  huyo  hajalipa  kiasi  cha  pesa  iliyobaki kama  mlivyokubaliana. Lakini  anaendelea  kutumia  kifaa  hicho. Unaweza  kuomba   kumzuia  kuendelea  kutumia  mpaka  atakapolipa  kiasi  kilichobaki  ili  asiendelee  kuharibu  au  kuzeesha  kifaa  hicho.

( c ) Kwa  mfano, we  ni  mpangaji  katika nyumba ya kuishi  au  biashara.  Mwenye  nyumba,eneo anataka  kukutoa  kwenye  pango  hilo  bila  kufuata  utaratibu  au  kwa  kukiuka baadhi  ya  makubaliano  kwenye  mkataba  wenu. Unaweza  kuomba  zuio asiendelee  kukutoa.

Pia  mazingira  mengine  yoyote  ambayo  unahisi  kuna  kitu, jambo  linataka  kuharibiwa  au  kuingiliwa, kuuzwa, kupotezwa,kufichwa  kinyume  na  utaratibu  unaweza  kuomba  zuio  hilo.

3.   SHARTI  KUU  .

Ili  uweze  kuomba  zuio  ni  lazima  pia  kuwepo  na  shauri  la  msingi.  Kwa  maana  utafungua  shauri  la  msingi  kulalamikia  jambo  fulani  halafu utaomba  zuio  ndani  ya  shauri hilo.  Kwa  mfano  unafungua  shauri  kulalamikia  mwenye nyumba  kusitisha  mkataba  wa  pango  bila  kufuata  utaratibu.

Hilo  ni  shauri  kuu.  Halafu  ndani  mwake  unafungua  shauri  dogo  la  kuomba  zuio ili  asikuondoe  katika  nyumba  mpaka  kwanza  shauri  kuu  la  kukiuka  utaratibu  litatuliwe.        

Kwahiyo  ni  sharti  kuwapo  shauri  kuu  ukilalamikia jambo  fulani  halafu ndani  mwake  ndio  uombe  zuio.

4.  UMUHIMU  WA  ZUIO.

( a ) Linasaidia  mali yako  kutouzwa  au  kutoondolewa  kwenye  nyumba  kama  mgogoro  unahusu  nyumba.

( b ) Linalinda  mali  yako  isiharibiwe ,isifichwe, isihamishwe,isiingiliwe  kwa  namna  yoyote  ile  kama  ipo  katika  mazingira  hayo.

( c ) Linakupa  nafasi  ya  kutafakari  na  kujipanga  ikiwa  upo  katika  presha  ya  kukimbizana  na  jambo ama  mgogoro.

( d ) Linatoa  mwanya  wa  mazungumzo  kati  ya  mlalamkaji  na  mlalamikiwa.

5.  WAPI   UKAOMBE  ZUIO.

Zuio  linaombwa  mahakamani.  Na  linaweza  kuombwa  mahakama yoyote   katika  shauri  lolote. Linaweza  kuombwa  kwenye  mashauri  ya  ndoa, mirathi,  ardhi,  biashara,  mikataba, madai   ya  kawaida ya  pesa au  mali, makampuni n.k.

Na  linaombwa  katika  mahakama  zote  yaani  ya  mwanzo,  ya  wilaya,  ya  hakimu  mkazi  mahakama  kuu  na  ya  rufaa  pia.  Lakini  pia  linaombwa  kwenye  mabaraza    ya  ardhi  ya  kata  na  wilaya.

6.  KUKIUKA  AMRI  YA  ZUIO.

Ikiwa  utaomba  zuio  na  kupata  halafu  aliyezuiwa  akakiuka  na  kuendelea  na  kile  alichozuiwa  basi   kosa linabadilika  na  kuwa  la   jinai. Inakuwa jinai  ya   kuingilia  amri   na   shughuli  za  mahakama.  Ni  kosa  ambalo   aliyekiuka  amri  hiyo akithibitika   ni  kweli  kakiuka  basi  atatakiwa  kwenda  jela  miezi  sita  ama  vinginevyo.

Kinachotakiwa kwako  ni  kuripoti  tu  kuwa  amri  iliyotolewa  sasa  haitekelezwi   na  yule  aliyeamrishwa  kutekeleza.  Utaripoti  mahakama  hiyo  hiyo  iliyotoa  zuio  hilo.

MSIMAMIZI WA MIRATHI ANATAKIWA KUGAWA MALI BAADA YA MUDA GANI ?.

Image result for MSIBANI
NA  BASHIR  YAKUB - 

1.UKOROFI  WA  WASIMAMIZI  WA  MIRATHI.

Baadhi  ya wasimamizi  wa  mirathi  ni  wakorofi.  Baada   ya  kuteuliwa  kwa  jukumu  hilo   hawapendi  kugawa  mali  ili  kila  mtu  achukue  chake. Inapaswa  kufahamika  kuwa  mali  si  za  msimamizi  wa  mirathi .  Mali  ni  za  warithi  halali  isipokuwa  msimamizi  ni  kiongozi  tu.  Kwa  maana  hii  anawajibika  kusikiliza  warithi  wanasema  nini  ili  mradi  kile  wanachosema  kisipingane na  sheria.

Wakati  mwingine  warithi  wanataka  wagawiwe  mali  zao   ili  kila  mtu  endelee  na  maisha  yake lakini  msimamizi  hataki  tena  bila  sababu  za  msingi. Hili  linakuwa  si  sawa  isipokuwa  kama  kuna sababu  za  msingi  za kufanya  hivyo.

Sababu zaweza kuwa labda   anayetaka kugawiwa mali  ni  mtoto  mdogo asiyeweza  kumiliki  mali kwa wakati  huo, ni  mtu  asiye na  akili  timamu kwa  muda  huo,  kuna  shauri  mahakamani kuhusu  hiyo  mirathi  linaendelea, mali hazijakusanywa  zote, kuna  ugomvi  kwa  warithi  kuhusu  mali  ambao  utaathiri  mgao  nk.                      

2. WAJIBU  MKUU  WA  MSIMAMIZI   WA  MIRATHI.     

Kifungu  cha 108(1)  cha  Sheria  ya  Usimamizi  na  Uendeshaji  wa  Mirathi,  Sura  ya  352  kinaeleza  wajibu  wa  jumla  wa msimamia  mirathi. Kifungu  kinasema  kuwa  kazi  kubwa  ya  msimamizi  wa  mirathi  ni  kukusanya, mali  na  madeni  ya marehemu,kutunza  mali  hizo, kusimamia  gharama  za  mazishi  na  msiba, na  kugawa  mali kwa  wanaostahili. Na  kazi  hii yote  ifanyike  kwa  uadilifu  mkubwa.

Kwahiyo  kumbe  moja  ya  kazi  ya lazima  na ya  kisheria  ya  msimamizi wa  mirathi  ni  kugawa mali  kwa  warithi.  Huu  ni  wajibu  ambao  msimamizi  anawajibika  kuutekeleza. Na  atagawa  kwa  mujibu  wa  wosia  au sheria  husika kama  hakuna  wosia. Hagawi  anavyotaka  yeye. Nani  apate  nini  halipo  katika  hiari  yake.

3.  MUDA  WA  KUGAWA  MALI  KWA  WARITHI.

Kifungu  cha  107 cha  Sheria ya  Usimamizi  na  Uendeshaji  wa  Mirathi kinasema  kuwa   ndani  ya  miezi  sita  tokea  kuteuliwa  kwa  msimamizi  wa  mirathi,  msimamizi  huyo  anatakiwa  kupeleka  taarifa(inventory&account)  mahakamani  akionesha  ni  namna  gani  amekusanya  mali  za marehemu,  madeni,  amelipa  gharama  kama  zipo  na  kwa  namna  gani  amegawa kwa  wahusika.

Kwahiyo  kazi  ya  kugawa  yafaa  ifanyike  ndani  ya  miezi  sita.  Hii  ina  maanisha  inaweza  kufanyika hata  ndani  ya  mwezi  mmoja  tokea  kuteuliwa  ikiwa  atakuwa  amekamilisha  taratibu  zote.

Kifungu  kinasema  ikiwa  ndani  ya  miezi  sita  hajapeleka  taarifa (inventory&account) mahakamani na kuna sababu za  msingi  na  za  kisheria  za  kutofanya  hivyo  basi  iwe  ndani  ya  mwaka mmoja. Ikiwa  ndani  ya  mwaka  mmoja  itashindikana kwasababu  za  msingi  na  za  kisheria   basi  anaweza  kuongezewa muda  na  mahakama  hadi miezi  mingine  sita.

Pamoja na  hayo  sheria  hiyo  imetoa  uhuru  kwa mahakama  kutoa  amri  au  agizo  la  kugawa  mirathi  kwa  warithi  halali  katika  muda  ambao  itaona  unafaa  na  kupendeza.  Kuna  muda  mahakama  inaweza kuamrisha  hata  ndani  ya  wiki  tatu  mali  iwe  imegawiwa  na  taarifa  imerejeshwa  mahakamani.
Mara  nyingi  amri  za  namna hii  hutolewa  kutegemea  na  udharula  wa  mazingira  husika  na  kinachohitajika.

4.  NINI  UFANYE  IKIWA  MSIMAMIZI  HATAKI  KUGAWA  MALI.

Ikiwa  msimamizi  hataki  kugawa  mali  na hakuna  sababu  za  kisheria  zinazomzuia kugawa basi  lipo  jambo  moja  unaweza  kufanya.

Ni kutoa  taarifa  katika mahakama ambayo imemteua/kumthibitisha.Utapeleka  malalamiko  yako  hapo  halafu  ataitwa  kwa  wito(summons) na  atatakiwa  aoneshe  sababu(show  cause)  kwanini  hagawi  mali  kama  sheria  inavyotaka. Haufungui  kesi  ila  unapeleka  tu taarifa.