Friday, September 15

OKWI MCHEZAJI BORA MWEZI AGOSTI 2017 KATIKA LIGI KUU BARA



Kutokana na kutwaa tuzo hiyo, Okwi ambaye pia ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) atazawadiwa kitita cha Sh. 1,000,000
Mshambuliaji wa Simba ya Dar es Salaam, Emmanuel Okwi amechaguliwa kuwa Mchezaji Bora wa Agosti wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2017/2018.
Okwi alitwaa tuzo hiyo baada ya kuwashinda wenzake wawili katika uchambuzi uliofanywa Dar es Salaam jana (Jumatano) na Kamati ya Tuzo ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), kutokana na mapendekezo kutoka kwa makocha wa viwanja mbalimbali ambavyo ligi hiyo inachezwa. Wachezaji wote hao timu zao zilishinda.
Walioshindana na Okwi katika hatua hiyo ya mwisho ni kiungo wa Mtibwa Sugar, Mohammed Issa ambaye alisaidia timu yake kupata pointi tatu kwa ushindi wa bao 1-0 katika mchezo dhidi ya Stand United uliofanyika Uwanja wa Manungu, Turiani, ambapo alikuwa nyota wa mchezo huo. Mwingine aliyeshindana na Okwi ni Boniface Maganga wa Mbao FC.
Maganga alitoa mchango mkubwa katika ushindi wa ugenini wa bao 1-0, ambao timu yake iliupata dhidi ya Kagera Sugar kwenye Uwanja wa Kaitaba, Bukoba ikiwa  ni pamoja na kufunga bao hilo. 
Ushindi wa Okwi unatokana na kutoa mchango mkubwa katika mchezo wa Simba dhidi ya Ruvu Shooting uliofanyika Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam na timu yake kuibuka na ushindi wa mabao 7-0, huku Okwi akifunga mabao manne. 
Pia Okwi amekuwa mchezaji wa kwanza msimu huu kufunga hattrick  (mabao matatu katika mchezo mmoja) katika Ligi Kuu ya Vodacom inayoshirikisha timu 16, ambapo hat trick hiyo alifunga ndani ya dakika 45 za kipindi cha kwanza.Mwezi huo ulikuwa na raundi moja tu iliyochezwa Agosti 26 na 27 mwaka huu ambapo kila timu ilicheza mechi moja. 
Kutokana na kutwaa tuzo hiyo, Okwi ambaye pia ni mchezaji wa timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) atazawadiwa kitita cha Sh. 1,000,000

Mwanafunzi wa sekondari apatikana akiwa na bunduki shuleni Kenya

Mwanafunzi wa sekondari apatikana akiwa na bunduki shuleni KenyaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMwanafunzi wa sekondari apatikana akiwa na bunduki shuleni Kenya
Mwanafunzi mmoja wa shule ya sekondari katika kaunti ya Homabay nchini Kenya, anashikiliwa na polisi akitarajiwa kufikishwa mahakamani baada ya kupatikana akiwa na bunduki, kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation.
Mwanafunzi huyo wa umri wa miaka 17 alikamatwa siku ya Jumanne baada ya wanafunzi wawili kuripoti kuwa amekuwa akiwatisha kwa bunduki hiyo.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo Dickens Bula, alisema kuwa usimamizi wa shule ulijulishwa na wanafunzi waliodai kuwa mwenzao amekuwa akiwatisha kuwa angewapiga risasi.
Gezeti hilo linasema kuwa baada ya mwanafunzi huyo kukamatwa na kuhojiwa, aliwapeleka polisi kwa kichaka kilichokuwa karibu ambapo alikuwa ameificha bunduki hiyo.
Daily Nation linasema kuwa bunduki hiyo ni ya kimarekani na hajaruhusiwa kutumiwa nchini Kenya.
Linasema kuwa licha ya uchunguzi kugundua kuwa bunduki hiyo haikuwa na risasi, usimamizi wa shule na wanafunzi walishikwa na hofu, na kusababsisha wanafunzi zaidi kuhojiwa kuhusu silaha hiyo.
Mkuu wa polisi eneo hilo Esau Ochorokodi, alisema mwanafunzi huyo aliwaambia wachunguzi kuwa alipata bunduki hiyo kutoka kwa jamaa wake anayeishi nchini Marekani.
Sasa mwanafunzi huyo anasubiri kushtakiwa kwa kumiliki bunduki bila kibali katika hakama ya Homa Bay.

Rais Robert Mugabe na mkewe Grace wajiandikisha upya kama wapiga kura

Rais Robert Mugabe akijiandikisha kama mpiga kura
Image captionRais Robert Mugabe akijiandikisha kama mpiga kura
Rais wa Zimabawe Robert Mugabe na mkewe Grace, wamekuwa watu wa kwanza kujiandikisha kama wapiga kura kabla ya uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwaka ujao.
Rais hata hivyo alisema kuwa shughuli hiyo ya kujiandikisha ilichukua muda mrefu.
Raia wote wa Zimbabwe wakiwemo wale waliopiga kura kwenye uchaguzi uliopita, watahitaji kujiandikisha upya kwa kutumia mfumo mpya ambao unachukua alama za vidole na picha za uso.
Grace Mugabe akijiandikisha kama mpiga kura
Image captionGrace Mugabe akijiandikisha kama mpiga kura
Ni vifaa 400 kati ya 3000 vya kuwandikisha wapiga kura vilivyowasilishwa nchini humo kutoka China kwa shughuli hiyo ambayo itakamilka mwezi Januari mwaka 2018.
Tume ya uchaguzi inasema kuwa inalenga kuwaandikisha watu milioni 7.
Bwana Mugabe ambaye ameingoza nchi tangu mwaka 1980, anatarajiwa kuwa mgombea wa chama cha Zanu-PF kwenye uchaguzi huo ambao unatarajiwa kuandaliwa kati kati mwa mwaka ujao.
Bwana Mugabe ambaye ameingoza nchi tangu mwaka 1980, anatarajiwa kuwa mgombea wa chama cha Zanu-PF kwenye uchaguzi mwaka ujaoHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionBwana Mugabe ambaye ameingoza nchi tangu mwaka 1980, anatarajiwa kuwa mgombea wa chama cha Zanu-PF kwenye uchaguzi mwaka ujao

Pacha walioshikamana wajiunga na chuo kikuu Tanzania

Maria na Consolata wakiwa darasani
Image captionMaria na Consolata wakiwa darasani
Ni ndoto iliozaa matunda kwa pacha walioshikana Maria na Consalata nchini Tanzania baada ya kuanza masomo yao katika chuo kikuu ili kujifunza kuwa walimu.
Kulingana na gazeti la The Citizen, waliwashukuru walimu wao wapya kwa mapokezi mema waliopata mbali na mazingira mazuri ya kusoma waliopata yalioandaliwa na chuo kikuu cha Ruaha Catholic University.
Waliwasili katika chuo hicho mbele ya wanafunzi wengine ili kuweza kujiandaa na mazingira yaliyopo.
Walianza masomo yao ya Kompyuta siku ya Jumatano .Waliwashukuru Wamishenari wa Consalata kwamba wamefikia kiwango hicho cha maisha yao.
Wamishenari hao waliwalea na kuwashawishi kuendelea na masomo.
Pacha walioshikana Tanzania walio na ndoto kuu
Wasichana mapacha walioshikana Tanzania
Mtawa mmoja katika Chuo hicho amesema kuwa kuwasili kwa pacha hao mbele ya wanafunzi wengine katika chuo hicho kutawawezesha kujiandaa ili kuweza kuwa sawa na wengine.
Vyumba vitatu vilivyopo na fanicha zote vimeandaliwa kwa pacha hao, ikiwemo jiko na sebule.
Naibu Chansela anayesimamia maswala ya fedha na usimamizi wa chuo hicho , Fr Kelvin Haule alionyesha furaha baada ya kuwapokea pacha hao.
Amesema kuwa masomo yataanza mwisho wa mwezi Oktoba lakini masomo ya kompyuta yanaanza mara moja.

Pacha walioshikamana wajiunga na chuo kikuu Tanzania

Maria na Consolata wakiwa darasani
Image captionMaria na Consolata wakiwa darasani
Ni ndoto iliozaa matunda kwa pacha walioshikana Maria na Consalata nchini Tanzania baada ya kuanza masomo yao katika chuo kikuu ili kujifunza kuwa walimu.
Kulingana na gazeti la The Citizen, waliwashukuru walimu wao wapya kwa mapokezi mema waliopata mbali na mazingira mazuri ya kusoma waliopata yalioandaliwa na chuo kikuu cha Ruaha Catholic University.
Waliwasili katika chuo hicho mbele ya wanafunzi wengine ili kuweza kujiandaa na mazingira yaliyopo.
Walianza masomo yao ya Kompyuta siku ya Jumatano .Waliwashukuru Wamishenari wa Consalata kwamba wamefikia kiwango hicho cha maisha yao.
Wamishenari hao waliwalea na kuwashawishi kuendelea na masomo.
Pacha walioshikana Tanzania walio na ndoto kuu
Wasichana mapacha walioshikana Tanzania
Mtawa mmoja katika Chuo hicho amesema kuwa kuwasili kwa pacha hao mbele ya wanafunzi wengine katika chuo hicho kutawawezesha kujiandaa ili kuweza kuwa sawa na wengine.
Vyumba vitatu vilivyopo na fanicha zote vimeandaliwa kwa pacha hao, ikiwemo jiko na sebule.
Naibu Chansela anayesimamia maswala ya fedha na usimamizi wa chuo hicho , Fr Kelvin Haule alionyesha furaha baada ya kuwapokea pacha hao.
Amesema kuwa masomo yataanza mwisho wa mwezi Oktoba lakini masomo ya kompyuta yanaanza mara moja.

India kujenga treni ya kwanza ya mwendo kasi

This handout photograph released by India"s Press Information Bureau (PIB) on September 14, 2017 shows Indian Prime Minister Narendra Modi (L) and Japanese Prime Minister Shinzo Abe looking at a railway station model at a ground breaking ceremony for the Mumbai-Ahmedabad high speed rail project in Ahmedabad. India"s first bullet train project, a $19-billion initiative linking Ahmedabad to Mumbai, was launched September 14Haki miliki ya pichaAFP
Image captionMradi huo unafadhiliwa na mkopo wa dola bilioni 17 kutoka Japan na utatoa huduma kati ya miji ya Ahmedabad na Mumbai.
Waziri mkuu wa Japan shinzo Abe amezindu mradi wa kujengwa kwa treni ya kwanza ya mwendo kasi katika jimbo la nyumbani mwa waziri mkuu wa wa India Narendra Modi la Gujarat.
Mradi huo unafadhiliwa kwa mkopo wa dola bilioni 17 kutoka Japan na utatoa huduma kati ya miji ya Ahmedabad na Mumbai.
Wakati mradi huo utaanza kutoa huduma katika kipindi cha miaka mitano, safari ya kilomita 500 inatarajiwa kupunguzwa hadi masaa matatu kutoka masaa manane ya kawaida.
Bw. Abe anafanya ziara ya siku mbili nchini India ambayo ni mshirika mkuu wa Japan.
A Shinkansen bullet train moves on tracks above traffic in Tokyo on August 14, 2017.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionJapan ndiye mwanzilishi wa treni za mwendo kasi
"Rafiki yangu waziri mkuu Narendra Modi ni kiongozi mwenye kuona mbali. Alifanya uamuzi miaka miwili iliyopita kuleta treni ya mwendo kasi nchini India na kujenga India mpya," alisema baada ya kuweka jiwe la msingi leo Alhamisi.
"Nina matumani ya kufurahia mandhari mazuri ya India kupitia kw\ madirisha ya treni wakati nitarudi hapa miaka michache inayokuja".
Treni hiyo ya viti 750 inatarajiwa kuanza kuhudumua kuanzia Agosti mwaka 2022.
Mifumo ya usafiri wa treni nchini India husafirisha zaidi ya watu milioni 22 kwa siku na baadhi ya treni zimepitwa na wakati hali ambayo huchangia ajali za mara kwa mara.
An Indian Railways passenger train travels on a railway track in New Delhi on November 10, 2015.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionMifumo ya usafiri wa treni nchini India husafirisha zaidi ya watu milioni 22 kwa siku na baadhi ya treni zimepitwa na wakati hali ambayo huchangia ajali za mara kwa mara

Mbunge awasilisha ombi la kuondolewa kwa jaji Maraga Kenya

Jaji mkuu David Maraga
Image captionJaji mkuu David Maraga
Mbunge wa chama tawala cha Jubilee nchini Kenya amewasilisha ombi la kutaka kufutwa kazi kwa jaji mkuu David Maraga.
Mbunge huyo wa Nyeri, Njiri Wambugu amewasilisha ombi lake mbele ya tume ya huduma za majaji akidai kwamba jaji Maraga alihusika katika kufanya makosa.
Akihutubia vyombo vya habari, mbunge huyo anadai kwamba Jaji huyo ''aliwashinikiza'' wenzake kubatilisha matokeo ya uchaguzi wa rais Uhuu Kenyatta wakati alipotoa uamuzi wa kihistoria mnamo tarehe 1 Septemba.
Wambugu amefananisha ubatilishwaji wa matokeo hayo ya urais na mapinduzi ya majaji na sasa anataka nia ya jaji Maraga kuchunguzwa.
Wabunge wa chama cha Jubilee na rais Uhuru Kenyatta wamekuwa wakiukosoa uamuzi wa kufutilia mbali uchaguzi huo na wameendelea na kuwataja majaji hao kuwa ''wakora''.
Naibu wa rais William Ruto amesema kuwa baada ya kukamilika kwa uchaguzi wa urais wa Oktoba 17, uamuzi huo wa majaji na sababu zao utaangaziwa upya.

Wanawake waislamu nchini Tunisia waruhusiwa kuolewa na wanaume wasio waislamu

Tangazo hilo linakuja mwezi mmoja baada ya Rais Beji Caid Essebsi, kutoa wito kwa serikali kuondoa marufuku hiyo ya mwaka 1973.Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionTangazo hilo linakuja mwezi mmoja baada ya Rais Beji Caid Essebsi, kutoa wito kwa serikali kuondoa marufuku hiyo ya mwaka 1973.
Rais wa Tunisia ametanga kuwa wanawake sasa wako huru kuolewa na wanaume wasio waislamu, kwa mujibu wa shirika la habari la AFP
Tangazo hilo linakuja mwezi mmoja baada ya Rais Beji Caid Essebsi, kutoa wito kwa serikali kuondoa marufuku hiyo ya mwaka 1973.
Hadi sasa mwanamume ambaye si muislamu anayetaka kumuoa mwanamke wa Tunisia, alihitaji kubadili dini na kuwa muislamu na kutoa cheti cha kuonyesha kuwa amefanya hivyo.
Makundi ya kutetea haki za binadamu nchini Tunisia yamekuwa yakifanya kampeni ya kutaka kuondolewa marufuku hiyo wakisema kuwa inakiuka haki za binadamu za kumchagua mke au mume.
Tunisia inaonekana kuwa iliyopiga hatua mbele ya mataifa mengine katika masuala ya haki za wanawake, lakini bado kuna ubaguzi katika masuala ya urithi.