Friday, September 15

India kujenga treni ya kwanza ya mwendo kasi

This handout photograph released by India"s Press Information Bureau (PIB) on September 14, 2017 shows Indian Prime Minister Narendra Modi (L) and Japanese Prime Minister Shinzo Abe looking at a railway station model at a ground breaking ceremony for the Mumbai-Ahmedabad high speed rail project in Ahmedabad. India"s first bullet train project, a $19-billion initiative linking Ahmedabad to Mumbai, was launched September 14Haki miliki ya pichaAFP
Image captionMradi huo unafadhiliwa na mkopo wa dola bilioni 17 kutoka Japan na utatoa huduma kati ya miji ya Ahmedabad na Mumbai.
Waziri mkuu wa Japan shinzo Abe amezindu mradi wa kujengwa kwa treni ya kwanza ya mwendo kasi katika jimbo la nyumbani mwa waziri mkuu wa wa India Narendra Modi la Gujarat.
Mradi huo unafadhiliwa kwa mkopo wa dola bilioni 17 kutoka Japan na utatoa huduma kati ya miji ya Ahmedabad na Mumbai.
Wakati mradi huo utaanza kutoa huduma katika kipindi cha miaka mitano, safari ya kilomita 500 inatarajiwa kupunguzwa hadi masaa matatu kutoka masaa manane ya kawaida.
Bw. Abe anafanya ziara ya siku mbili nchini India ambayo ni mshirika mkuu wa Japan.
A Shinkansen bullet train moves on tracks above traffic in Tokyo on August 14, 2017.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionJapan ndiye mwanzilishi wa treni za mwendo kasi
"Rafiki yangu waziri mkuu Narendra Modi ni kiongozi mwenye kuona mbali. Alifanya uamuzi miaka miwili iliyopita kuleta treni ya mwendo kasi nchini India na kujenga India mpya," alisema baada ya kuweka jiwe la msingi leo Alhamisi.
"Nina matumani ya kufurahia mandhari mazuri ya India kupitia kw\ madirisha ya treni wakati nitarudi hapa miaka michache inayokuja".
Treni hiyo ya viti 750 inatarajiwa kuanza kuhudumua kuanzia Agosti mwaka 2022.
Mifumo ya usafiri wa treni nchini India husafirisha zaidi ya watu milioni 22 kwa siku na baadhi ya treni zimepitwa na wakati hali ambayo huchangia ajali za mara kwa mara.
An Indian Railways passenger train travels on a railway track in New Delhi on November 10, 2015.Haki miliki ya pichaAFP
Image captionMifumo ya usafiri wa treni nchini India husafirisha zaidi ya watu milioni 22 kwa siku na baadhi ya treni zimepitwa na wakati hali ambayo huchangia ajali za mara kwa mara

No comments:

Post a Comment