Sunday, October 15

Nape afunguka kuhusu Demokrasia


Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye amesema kuzuiwa mikutano ya kisiasa si kuminya demokrasia kwa kuwa  kuna bunge ambalo linaweza kutumika kutolea maoni yao.  
Akihojiwa na kituo cha Televisheni cha  KTN kutoka nchini Kenya katika kipindi cha siasa za kanda kuhusu demokrasia katika Afrika, Nape amesema demokrasia inatakiwa kutafsiriwa kulingana na maeneo tuliyopo.
“Afrika hatuwezi kuwa na demokrasia iliyo sawa na Marekani,” amesema.
Nape alitakiwa kutoa maoni yake kuhusu viongozi wa Chadema kudai kwamba, Rais John Magufuli anaminya demokrasia hasa kuzuia mikutano ya hadhara.
Akijibu, Nape amesema nchi za Afrika hazitakiwi kutafsiri demokrasia kwa kujilinganisha na nchi zilizoendelea za Magharibi.
“Hapa kwetu baada ya uchaguzi mkuu tunaruhusiwa kufanya mikutano kwenye majimbo yetu haturuhusiwi kufanya mikutano nje ya majimbo yetu,” amesema.
Amesema uchaguzi ukishamalizika siasa zinahamia bungeni ambako wabunge wanaweza kutoa maoni yao.
“Sioni kama hapa demokrasia inaminywa au kuna udikteta kwa sababu hiyo inawahusu wabunge wote kutoka chama tawala na vyama vya upinzani,” amesema.
Nape ambaye alikuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, amesema zamani wanasiasa waliruhusiwa kufanya mikutano katika maeneo mbalimbali ya nchi.
Nape amesema wakati wa uchaguzi mkuu shughuli nyingi huwa zinasimama kwa sababu ya mikutano ya wanasiasa.
“Kwa hiyo kuna umuhimu wa viongozi wa kisiasa kwenda kutekeleza yale waliyowaahidi wananchi,” amesema.
Nape amewataka wasomi kutoa tafsiri kwa upana kuhusu dhana ya
demokrasia  ili wananchi waweze kuitekeleza kulingana na maeneo waliyopo.

LUKUVI AVUNJA NYUMBA YAKE KUPISHA UJENZI WA BARABA

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Wiliam Lukuvi ambaye pia ni Mbunge wa Ismani, ameivunja nyumba yake iliyopo Mapogoro, Ismani kama njia ya  kumuunga mkono Rais John Magufuli  katika ujenzi wa barabara ya kiwango  cha  lami  kati ya  Iringa kuelekea Hifadhi ya Taifa ya Ruaha.
Akizungumza jana mara baada ya  kushiriki zoezi la ubomoaji wa nyumba   hiyo, Waziri Lukuvi, alisema kuwa akiwa kama kiongozi ameamua kuwa  wa kwanza kuonyesha mfano kwa  kuanza  kuivunja  nyumba hiyo ambayo  kimsingi sehemu  ya  robo ilikuwa imepigwa alama ya X nyekundu na  robo  tatu  ilipigwa alama ya X ya kijani, ila kutokana na kuunga mkono jitihada za  Serikali katika ujenzi wa barabara   hiyo,  ameamua kuivunja yote na hatadai  malipo yoyote.
“Kimsingi barabara hii ya kuelekea  Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, ilianza  kabla ya sisi kuja kujenga hivyo barabara  tuliikuta hakuna hata mmoja kati yetu ambaye barabara  ilimkuta na haya  ni maendeleo yetu sote na Taifa kwa  ujumla, mimi nilijenga jirani na  barabara ili kuwapungia watu mikono  wakati wanapita sikujua kama ni  barabarani, ila  baada ya kujulishwa nimeamua kwa  mikono yangu kuja  kuvunja nyumba yangu.”
Waziri Lukuvi alisema Serikali haitalipa  fidia  yoyote  kwa  wananchi  waliojenga  nyumba  katika  hifadhi ya  barabara  akiwamo yeye mwenyewe, hivyo alitaka wananchi wote ambao walivunja sheria  kwa kutojua waanze kuvunja nyumba  zao  wenyewe kwa  hiari bila kusubiri  kuvunjiwa.
Alisema kuwa wananchi wote  waliowekewa alama ya X katika  nyumba zao, kuanza  kuvunja pasipo  kusubiri kujiuliza na maana ya alama  nyekundu ama kijani, kwani barabara   hiyo ilianza toka miaka 30 hivyo hifadhi  ya Ruaha na barabara hiyo ilianza kabla ya hapo.
  
  
  

MISHAHARA JUU WATUMISHI 59,000

RAIS Dk. John Magufuli amesema watumishi wa umma 59,967 watarekebishiwa mishahara na promosheni zao na kuanza kulipwa mwezi ujao.
Rais alitoa kauli hiyo jana ikiwa ni siku moja baada ya Serikali kupitia msemaji wake, Dk. Hassan Abbasi kukanusha tuhuma za Chama cha Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) ambazo zilidai Rais Dk. John Magufuli amekataa kupandisha mishahara ya watumishi.
Katika hotuba yake aliyoitoa jana visiwani Zanzibar wakati wa kuadhimisha Kumbukumbu ya Kifo cha Hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, Rais, Dk. Magufuli alisema Serikali baada ya kusafisha kwa kuondoa watumishi hewa na wale wenye vyeti vya kughushi, imetenga jumla ya Sh bilioni 159, 326 kwa ajili ya kulipa marekebisho ya mishahara na promosheni za watumishi hao.
Ufafanuzi huo wa Rais aliutoa wakati akielezea moja ya mifano ya kizalendo ambayo aliitenda Mwalimu Nyerere wakati wa utawala wake, ambapo  alikataa kupandisha mishahara ya watumishi ili kuboresha huduma za kijamii.
Akielezea mfano huo, Rais Magufuli alisema baada ya Tanzania kupata uhuru baadhi ya wasomi waliokabidhiwa madaraka walianza kutoa shinikizo kwa Serikali kutaka kuongezewa mishahara na marupurupu.
Alisema kutokana na mashinikizo hayo Mwalimu Nyerere hakukubaliana nao na hakusita kuikemea tabia hiyo ya ubinafsi.
Kwa mujibu wa Rais Magufuli, Mwalimu Nyerere kwa kuonyesha mfano wa kukerwa na ubinafsi aliamua kupunguza mshahara wake ili kuwakumbusha wasomi hao kwamba, haiwezekani watu wachache kuongezeana mishahara wakati wananchi wengi masikini hawapati huduma muhimu ya afya, elimu na maji.
“Tujiulize je, na sisi tupo tayari kuacha mishahara hewa. Je, mishahara tunayopata tumeifanyia kazi. Je, nasi tupo tayari kujipunguzia au kuishinikiza Serikali kuongeza mishahara na marupurupu yetu ili ituwezeshe kuboresha huduma za jamii kwa manufaa ya Watanzania?
“Ninasema hivyo simaanishi kuwa mishahara ya watumishi isiongezwe la hasha, ninachotaka kusema ni kwamba, kabla ya kudai nyongeza ya mshahara ni lazima kwanza kufahamu uwezo wa Serikali lakini pia tutambue kuwa kuna Watanzania wenzetu wengi tu wanahitaji kuboreshewa huduma…nimesema hili sina maana ya kwamba watu wasiongezewe mishahara. Tuna mifano inayoishi kwa hapa Zanzibar, Rais Shein baada ya kushika madaraka mishahara ya kima cha chini imepandishwa kutoka Sh150,000 hadi Sh 300,000. Lakini sisi kama tusingefanya ukaguzi wa kutosha tungelipa Sh bilioni 89 kwa wafanyakazi hewa,” alisema Rais Magufuli.
KUHUSU NYERERE
Akimzungumzia Mwalimu Nyerere, Rais Magufuli alisema Watanzania wanatakiwa kujikumbusha mchango wake mkubwa wa kulitumikia taifa hili.
Alisema katika kujikumbusha huko Watanzania wanatakiwa kujifunza na kutumia mafunzo yanayoelekeza kusukuma mbele maendeleo ya taifa.
Aliongeza kuwa Mwalimu Nyerere alikuwa ni kiongozi mzalendo tangu mwanzo wa uongozi wake wa kisiasa mwaka 1953 wakati alipochaguliwa kuwa Rais wa Chama cha TAA ambacho kilizaa TANU.
“Katika kipindi hicho Mwalimu Nyerere alionyesha uzalendo wa hali ya juu na kuthamini kwake utu na usawa wa binadamu. Wakati anachaguliwa kuwa Rais wa TAA na baadaye TANU, alikuwa anafundisha St. Francis College  kwa sasa inajulikana kama Shule ya  Sekondari ya Pugu na umbali wa kutoka Pugu hadi ofisi za TAA na TANU kwa maana ya kwenda na kurudi zilikuwa kilomita 46 na enzi hizo hapakuwa na usafiri wa daladala kama ilivyo sasa.
“TAA na TANU hazikuwa na usafiri wala nauli ya kumlipa, lakini Mwalimu Nyerere kwa uzalendo alitumia fedha zake kujigharamia usafiri na wakati mwingine alilazimika kutembea kwa miguu na alifanya hivyo kwa kujitolea. Tujifunze leo ni viongozi wangapi wa vyama wanaweza kujitolea kwa kiasi hicho?” alihoji.
Alisema mwaka 1955 alipotakiwa  kuchagua kuendelea na kazi  ya kufundisha Shule ya St. Francis au kuacha kujihusisha na shughuli za kisiasa, Mwalimu Nyerere  aliamua kuacha kazi na kubaki kuwa kiongozi wa TANU kazi ambayo alikuwa halipwi mshahara wowote.
Alisema Mwalimu Nyerere aliamua kuachana na kazi ili aendelee kuongoza harakati za kudai uhuru na alikuwa na hali ngumu ya maisha.
Rais Magufuli aliongeza kuwa kitu pekee kilichomlazimu Mwalimu Nyerere kuacha kazi, ni uzalendo na upendo wake kwa Watanzania kwamba kama isingekuwa hivyo kwa elimu aliyokuwa nayo wakati huo angeamua kutafuta kazi yenye kulipwa mshahara mzuri.
“Tujiulize sisi Watanzania leo hii ni wangapi wanaweza wakafanya uamuzi wa kizalendo kama huo uliofanywa na Baba wa Taifa? Leo hii kuna Watanzania wangapi ambao kwa sababu tu  wanalipwa vizuri kwenye makampuni ya wageni wanaisaliti nchi kwa vitendo vya wizi na rushwa?
“Je, kuna viongozi wangapi waliopewa dhamana ya wananchi lakini kwa kukosa uzalendo wamekubali kusaini mikataba isiyo na tija ya nchi, je, kuna viongozi wangapi ambao hawazingatii Tanzania kwanza badala yake wanazingatia fedha kwanza?…majibu ndugu zangu Watanzania mnayo wenyewe,” alisema.
Rais Magufuli alisema Mwalimu Nyerere  hakuishi maisha ya kifahari na anasa.
“Kuna watu waliwahi kusikika wakisema kama Nyerere angekuwa mbinafsi au mpenda utajiri angeweza kuchukua fukwe yote ya Msasani lakini hakufanya hivyo. Na kweli angeweza maana kuna mifano mingi ya viongozi wengi wa zama zake na hata zama za sasa wanafanya hivyo.
“Lakini yeye hakufanya hivyo licha ya kutumikia urais kwa takribani miaka 23, Mama Maria, watoto na ndugu zake wengi ambao waliishi na wanaendelea kuishi kwa maisha ya kawaida kabisa sawa na Watanzania wengi,” alisema.
AGOMA KUFUTA MBIO ZA MWENGE
Katika hatua nyingine, Rais Magufuli alisema Serikali haitafuta mbio za Mwenge wa Uhuru kwa kuwa ni alama ya Uhuru na Utaifa wa nchi na kwamba unatoa mchango mkubwa katika kuchochea maendeleo, kuwaunganisha Watanzania na kuimarisha Muungano.
Alisema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, zitaendeleza Mbio za Mwenge wa Uhuru na kuutetea Muungano kwa nguvu zote.
Rais Magufuli ametoa kauli hiyo wakati ambao kwa miaka kadhaa sasa baadhi ya watu wamekuwa wakitamani kuona mbio hizo zikifutwa kwa kuwa hawaoni faida yake zaidi ya kutumia fedha nyingi za Serikali.
“Kaulimbiu ya Mwenge wa Uhuru mwaka huu inasema, Shiriki Kukuza Uchumi wa Viwanda kwa Maendeleo ya Nchi yetuNimefarijika zaidi kusikia kuwa katika Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka huu jumla ya viwanda 148 vimezinduliwa, viwanda hivyo vimejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 468.46 na vinatarajiwa kuzalisha ajira 13,370.
“Hii ndio sababu tumekuwa tukihimiza ujenzi wa viwanda na hizi ni baadhi ya faida za Mwenge,” alisema Rais Magufuli.
Akizungumzia vijana, Rais Magufuli amewataka kuendelea kujielimisha katika nyanja mbalimbali, kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na kujikinga dhidi ya maambukizi ya ugonjwa wa Ukimwi.
Aidha, Rais Magufuli aliwapongeza na kuwakabidhi vyeti wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa walioongozwa na Amour Hamad Amour kwa kukimbiza mwenge huo kwa siku 195 katika mikoa yote 31 na Halmashauri 195, ambapo jumla ya miradi 1,512 yenye thamani ya jumla ya shilingi trilioni 1.1 imepitiwa.
Pia ameahidi kuchukua hatua dhidi ya wote waliohusika kusababisha dosari katika miradi 19 ambayo viongozi wa mwenge wamebaini.
Maadhimisho ya Kumbukumbu ya Kifo cha Hayati Baba wa Taifa ambayo yaliambatana na sherehe za kuzima Mwenge wa Uhuru pamoja na Sikukuu ya Vijana yalihudhuriwa na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Majaliwa, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Seif Ali Idd, Mke wa Rais wa  Magufuli, Mama Janeth Magufuli, Mke wa Rais wa Zanzibar, Mama Mwanamwema Shein na viongozi wengine wa Tanzania Bara na Zanzibar.

KIAMA CHAJA KWA WAGAVI VIHIYO

SERIKALI imetangaza kuwachukulia hatua wataalamu wote wa ununuzi na ugavi watakaobainika kufanyakazi bila kusajiliwa na Bodi ya Wataalamu hao (PSPTB).
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Amina Shabani kwa niaba ya Naibu Waziri wa wizara hiyo, Dk. Ashatu Kijaji kwenye mahafali ya nane ya Bodi ya Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB) katika Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam.
Alisema ni kosa kubwa kwa waajiri kuajiri wataalamu ambao hawajasajiliwa na bodi na kwamba kufanya hivyo ni ukiukwaji wa sheria.
“Napenda nitoe onyo kwa waajiri wote nchini kuacha kuajiri watu wasiosajiliwa na Bodi kwani kufanya hivyo ni kukiuka sheria namba 23 ya mwaka 2007 iliyoanzisha Bodi hiyo na kwamba Wizara yake itafuatilia suala la watu wanaofanya kazi bila usajili akianzia ngazi ya wizara.
“Hivyo yeyote atakayebainika kufanya kazi kinyume na maadili na taratibu za kazi, atatumbuliwa haraka kabla hajasababisha hasara kubwa kwa Taifa kama ambavyo imekuwa ikitokea mara kwa mara,” alisema Amina.
“Suala la maadili na uzalendo lipewe kipaumbele katika mafunzo yenu, warsha na makongamano, Serikali haitamvumilia mtu yeyote atakayetumia nafasi aliyopewa kujinufaisha na kusababisha huduma mbovu kwa wananchi, hivyo ili kudhibiti mienendo ya kimaadili kwa wataalamu wenu, ni lazima watu wote wanaofanya kazi za ununuzi na ugavi nchini wawe wamesajiliwa na Bodi kwa mujibu wa sheria,” alisema Amina.
Upande wake, Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Sista Hellen Bandiho, alisema kwa kutambua changamoto zilizopo katika ununuzi wa umma na usimamizi wa mikataba, Bodi iliboresha mtaala na kuweka masomo mahususi ili kuwajengea uwezo wataalamu wanaohitimu waweze kusimamia mikataba ya ununuzi yenye kuleta tija.
“Serikali pamoja na kazi kubwa inayofanya lakini tunaiomba iboreshe masilahi ya wataalamu wa fani hii ili angalau yalingane na walaalamu wa fani nyingine wenye viwango sawa vya elimu. Niwaase wahitimu kufanya kazi kwa kufuata maadili ya taaluma ili kulinda heshima ya fani yetu na kuleta ufanisi katika matumizi ya rasilimali za umma kwa manufaa ya Taifa na watu wake,” alisema Sista Hellen.
Jumla ya wanafunzi 1,101 wamefaulu mtihani huo kati ya wanafunzi 3,086 waliofanya mtihani.

Viongozi - NRM wagawanyika juu ya ukomo wa umri wa urais, UGANDA

Sakata la kubadilisha ukomo wa umri wa urais lililotokea hivi karibuni katika bunge la Uganda.
Viongozi wa chama tawala cha NRM huko Buzaaya, Wilaya ya Kamuli wamepiga kura dhidi ya hatua iliyosubirishwa ya kuondoa ukomo wa umri kwa kinyang’anyiro cha urais kutoka katika Katiba ya Uganda.
Viongozi hao wamepitisha azimio wakati wa mkutano wao wa ushauri Jumamosi ulioitishwa na wabunge wa Buzaaya, Isaac Musumba katika ukumbi wa Taasisi ya Ufundi eneo la Nawanyago.
Mkutano huo wa mashauriano ulikusudia kuwahamasisha wakereketwa wa chama cha NRM wakubaliane na marekebisho ya ukomo wa urais ambayo yalisubirishwa.
Marekebisho hayo ya Katiba kwa Waganda wengi yalionekana kama ni mbinu ya kumpa mwanya Rais Yoweri Museveni, mwenye umri wa miaka 73, kuwania tena nafasi ya urais 2021,
Hata hivyo mkutano huo uligeuka kuwa ni vurugu wakati viongozi wa chama hicho katika eneo hilo Buzaaya walipowazuia baadhi ya wanachama kuingia katika eneo hilo.
Wachambuzi wa kisiasa wanakubaliana kuwa iwapo Katiba haitofanyiwa marekebisho, Museveni hatoweza kuwa na sifa za kugombea kwani ukomo wa umri wa wagombea urais hivi sasa ni miaka 75.
Vyanzo vya habari nchini Uganda vimesema kuwa watu waliozuiwa kuingia katika mkutano huo walitishia kukihama chama cha NRM na kwenda upande wa upinzani kwa sababu NRM ilikuwa imeamua kuwafanya wawe “mayatima”.
“Rais Museveni alikwenda msituni kupigana dhidi ya madikteta ambao walikuwa wananang’ania kubakia madarakani na aliahidi kuirudisha demokrasia nchini. Rais Museveni hivi leo anakubali utashi wake kumyumbisha dhidi ya mabadiliko ya msingi aliyokuwa ameyaanzisha yeye mwenyewe. Anatakiwa kuacha athari njema katika chama cha NRM," amesema Hamis Dheyongera, Diwani wa NRM eneo la Wankole.

NASA yaomba vyombo vya kimataifa kuchunguza mauaji Kenya

Askari wa kuzuia fujo akitupa bomu la machozi wakati wa maandamano ya Nasa yanayoendelea dhidi ya IEBC nchini Kenya.
Wabunge wa Muungano wa upinzani, Nasa, wameanza kuviomba vyombo vya kimataifa kusaidia kuchunguza vitendo vya mauaji vinavyoendelea nchini Kenya.
Kwa mujibu wa upinzani mauaji hayo yanadaiwa kufanywa na polisi kwa wafuasi wa Nasa wakati maandamano dhidi ya IEBC yakiendelea kote nchini.
Seneta wa Siaya James Orengo, ambaye aliongoza wabunge 10 wa Nasa mjini Nairobi Jumamosi, ameviomba vyombo huru vinavyoisimamia polisi, Shirika la kimataifa la haki za bindamu Amnesty International, shirika la haki za binadamu Human Rights Watch, Tume ya haki za binadamu Kenya, kikundi huru kinachotoa huduma za kisheria za afya kuingia eneo la Bondo na kuchunguza mauaji ya Wakenya yanayofanywa na polisi.
“Tunaviomba vyombo vinavyosimamia haki za binadamu kwa uadilifu kuchunguza suala zima la kuwatafuta na kuwaua wafuasi wa Nasa kinyume cha sheria.
“Wanataka kuyageuza maeneo yaliyokuwa na wafuasi wa Nasa kuwa Biafra na Kosovo ya Kenya. Rais Uhuru Kenyatta na maafisa wa serikali yake lazima wajitayarishe kukabiliana na hatma ya jambo hili,” amesema Orengo.
“Iwapo unyama huu dhidi ya watu wetu utaendelea, sisi hatutakaa na kusubiri kuuwawa. Tutachukua hatua ambayo itaweza kuhakikisha tunajihami dhidi ya serikali dhalimu inayoangamiza watu wake,” amesema, akiongeza “tunamuonya Kenyatta kuwa afahamu kwamba anaipeleka Kenya mahali pabaya ambapo ni maangamivu kwa nchi hii kama tunavyofahamu.”
The MPs, who included Junet Mohamed (Suna East), Opiyo Wandayi (Ugunja), Tim Wanyonyi (Westlands) and Busia Woman Representative Florence Mutua, accused acting Interior Cabinet Secretary Fred Matiang’i and Police Inspector-General Joseph Boinnet of unveiling and executing a policy to eliminate Nasa supporters.
Wabunge hao ni pamoja na Junet Mohamed (Suna Mashariki), Opiyo Wandayi (Ugunja), Tim Wanyonyi (Westlands) na Mwakilishi wa Mwanamke wa Busia Florence Mutua wamemtuhumu kaimu Waziri wa Mambo ya Ndani Fred Matiang’i na Inspekta Jenerali wa Polisi Joseph Boinnet kwa kuanzisha na kutekeleza sera ya kuwamaliza wafuasi wa Nasa.
Siku ya Ijumaa, watu watatu wasio na silaha waliuawawa kwa kupigwa risasi wakiwa karibu na polisi huko mji wa Bondo wakati wafuasi wa Nasa wakiandamana kuipinga IEBC nchini Kenya.
Lakini Boinnet amedai kuwa watu hao watatu walipigwa risasi walipokuwa wakijaribu kuvamia kituo cha polisi, afisa mwengine alisema watu hao walikuwa wanaiba katika duka mojawapo.

Mbunge-Tanzania aondoa pendekezo la ukomo wa umri

Jengo la Bunge la Tanzania
MBUNGE wa Chemba kwa tiketi ya chama tawala CCM, nchini Tanzania Juma Nkamia, ameondoa kwa muda kusudio lake la kutaka kuwasilisha muswada binafsi wa mabadiliko ya Katiba ya nchi ili kuongeza ukomo wa ubunge kutoka mitano hadi saba.
Nkamia aliwasilisha kusudio hilo Septemba, mwaka huu mjini Dodoma kwa mujibu wa kanuni ya 81(2) ya kanuni za Bunge toleo la 2016, kupitia barua yake aliyoisaini Septemba 12, mwaka 2017.
Kupitia ujumbe mfupi aliouandika katika mtandao wa kijamii wa WhatsApp, Nkamia alisema ameamua kuondoa kusudio hilo baada ya majadiliano na maelekezo kutoka kwa viongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
“Ndugu viongozi wenzangu, naomba kuwataarifu kuwa baada ya mashauriano na maelekezo ya viongozi wa juu wa CCM na hali ya kisiasa katika nchi kadhaa za Afrika Mashariki, nimelazimika kuondoa kwa muda hoja yangu binafsi ya ukomo wa Bunge niliyokusudia kuiwasilisha katika Bunge lijalo (linaloanza Novemba, mwaka huu,” ujumbe huo ulieleza.
Aliongeza kuwa : “Naomba ibaki hivyo hivyo kama ilivyo kwenye meseji sina cha kuongeza, kuhusu ni lini nitapeleka tena nayo subiri kwa sababu nimesema nimesitisha kwa muda, maana yake nitawasilisha tena nitakapokuwa tayari.”
Hoja ya Nkamia ilianzia Bunge lililopita lakini ilipingwa na wanasiasa wakongwe akiwamo Spika Mstaafu wa Bunge, Pius Msekwa na wasomi mbalimbali.
Akizungumza na Kituo cha Televisheni cha Azam, Alhamisi wiki iliyopita, Spika wa zamani wa Bunge la Muungano, Pius Msekwa alisema CCM haiwezi kukubaliana na maoni ya kuongeza muda wa kiongozi yeyote kutoka kipindi cha miaka mitano kilichopo kwa mujibu wa Katiba ya sasa.
Pia alisema kwa uzoefu wake bungeni anaona kuna tafakuri nyingi zilizofanywa kabla ya Taifa kuamua kipindi cha utawala kuwa miaka mitano na si vinginevyo.

Takriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu

Takriban watu 230 wauawa kwenye milipuko MogadishuHaki miliki ya pichaAFP
Image captionTakriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu
Sasa imebainika kuwa idadi ya watu waliouawa katika mashambulio mawili ya mabomu mjini Mogadishu, Somalia, imepanda na kuwa zaidi ya 230
Haijulikani nani alihusika, lakini kwa idadi ya maafa, hayo yalikuwa kati ya mashambulio makubwa kabisa nchini Somalia, tangu kundi la wapiganaji wa Kiislamu, al-Shabab, kuanza mapigano yao mwaka 2007.
Takriban watu 230 wauawa kwenye milipuko MogadishuHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionTakriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu
Katika shambulio la kwanza, bomu lilokuwa kwenye lori, lililipuka kwenye njia panda, iitwayo Kilomita-5, ambapo kuna ofiisi za serikali, mahoteli na maduka, vyote viliporomoka katika mlipuko huo.
Saa mbili baadaye, bomu jengine lilikalipuka katika mtaa wa Medina.
Mkurugenzi wa Hospitali ya Madina, Mohamed Yusuf Hassan, anasema, alishtushwa na ukubwa shambulio hilo.
Takriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu
Image captionTakriban watu 230 wauawa kwenye milipuko Mogadishu

Taliban: Hatukumuua mtoto wala kumbaka mke wa mateka wetu

Taliban: Hatukumuua mtoto wala kumbaka mke wa mateka wetuHaki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionTaliban: Hatukumuua mtoto wala kumbaka mke wa mateka wetu
Kundi la Taliban nchini Afghanistan limekana lawama kutoka kwa mwanamume raia wa Canada kuwa mmoja wa watoto aliuawa na mke wake kubakwa wakati walikuwa wakishikwa mateka na wanamgambo hao.
Msemaji wa kundi la Taliban alisema kuwa kifo cha mtoto huyo kilitokana na matatizo ya uja uzito na familia hiyo ilikuwa katika eneop la kijijini na haikuruhusiwa kumuona daktari.
Pia alisema kuwa mtu huyo na mkewe, hakutenganishwa hata dakika moja ili kulinda usalama wao.
Alitaja lawama hizo za Joshua Boyle kama propaganda za serikali za nchi za magharibi.
Wanandoa hao walitekwa nyara wakati wakiwa safarini nchini Afghanistan mwaka 2012.
Joshua Boylena mke wake walitekwa nyara mwaka 2012Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionJoshua Boylena mke wake walitekwa nyara mwaka 2012

Flynt atangaza zawadi ya dola milioni 10 kumuondoa Trump Madarakani

Mchapishaji wa jarida Hustler, Larry FlyntHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMchapishaji wa jarida Hustler, Larry Flynt
Mchapishaji wa jarida la picha chafu za utundu, Larry Flynt, amechapisha tangazo katika gazeti la Washington Post, akiahidi kulipa zawadi ya dola milioni 10, kwa mtu mwenye habari, zitazopelekea Rais Trump kushtakiwa na kuondoshwa madarakani.
Bwana Flynt, anayemiliki jarida la "Hustler", amesema ni wajibu wa kila Mmarekani, kumuondoa Bwana Trump, kabla ya kuchelewa.
Tangazo hilo, linatoa nambari ya simu ya kupiga na anuani ya barua pepe.
Larry Flynt, ambaye alikuwa mfuasi mkubwa wa Hillary Clinton katika kuania urais, ametoa matangazo kama hayo kabla, lakini hakuwahi kutoa zawadi kubwa kama hiyo.

Safari ngumu ya mapacha walioshikana kwenda kutenganishwa DRC

After surgery, the twins were flown back to VangaHaki miliki ya pichaJACKLYN REIERSON, MAF
Image captionSafari ngumu ya mapacha walioshikana kwenda kutenganishwa DRC
Mapacha waliokuwa wamezaliwa wakiwa wameshikana katika kijiji cha mbali nchini Jamhuri ya Demokrasi ya Congo, wameponea safari ya saa 15 kwa njia ya piki piki wakipelekekwa kutenganishwa.
Kisha wakasafirishwa kwa njia ya ndege hadi mji mkuu Kinshasa, ambapo walifanyiwa upasuaji na kundi la madaktari wa kujitolea
Kwa jumla watoto hao wa wiki moja, walifanya safari ya kilomita 1,400 ya barabara mbovu na kwa njia ya ndege.
Watoto hao Anick na Destin, watarudishwa kijijini wao baada ya majuma matatu. Walizaliwa baada ya uja uzito wa wiki 37 mwezi Agosti.
Twins Anick and Destin before they were separatedHaki miliki ya pichaJACKLYN REIERSON, MAF
Image captionSafari ngumu ya mapacha walioshikana kwenda kutenganishwa DRC
Karibu mmoja kati ya watoto 200,000 huzaliwa wakiwa wameshikana, na kuishi kwao huwa finye hasa sehemu za mbali ambapo hakuna huduma za kiafya.
Lakini mapacha hawa walizaliwa kawaida tu katika kijiji cha Muzombo magharibi mwa DRC.
Walipogundua kuwa watoto hao walihitaji kufanyiwa upasuaji wazazi wao Claudine Mukhena na Zaiko Munzadi, waliwafunga blanketi na kuanza safari kupitia msituni kwenda hospitali iliyokuwa karibu.
Kutokana na ukosefu wa vifaa na ujuzi wa kufanya upasuaji huo katika hospitali ndogo, madakaktari waliwahamisha kwenda mjini Kinshasa karibu umbali wa maili 480.
The twins and family after being flown back to their regionHaki miliki ya pichaJACKLYN REIERSON, MAF
Image captionSafari ngumu ya mapacha walioshikana kwenda kutenganishwa DRC
Kufika mjini Kinshasa familia hiyo ilisafirishwaa na ndege ya shirika la MAF, la kutoa huduma za kibinadamu.
"Wako salama, wanalala vizuri na kula vizuri kwa jumla, wako salama," Dr Junior Mudji alisema.
"Watakuwa hapa kwa wiki tatu zaidi kuhakikisha kuwa kila kitu kiko sawa,"
Dr Mudji anaamini upasuaji huo nduo wa kwanza wa kuwatenganisha mapacha walioshikana nchini Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.