Tuesday, June 6

Cisco kuzikwa kesho Kisutu


Balozi Abdul Cisco Mtiro enzi za uhai wake 

By Ephrahim Bahemu, Mwananchi
Dar es Salaam. Mwili wa aliyekuwa Mkuu wa Itifaki Ikulu katika Serikali ya awamu ya tatu na nne, Balozi Abdul Mtiro ‘Cisco’ utazikwa kesho, Jumatano, katika makaburi ya Kisutu jijini hapa.
Cisco ambaye pia aliwahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Ufilipino, Cambodia na Singapore, alifariki juzi katika Hospitali ya Agha Khan alikokuwa akipatiwa matibabu.
Omar Mtiro ambaye  ni mtoto wa kwanza wa marehemu Cisco kati ya wanne, amesema mazishi  yatafanyika kesho  saa 7.00 mchana katika makaburi ya Kisutu.
Omar amesema kabla ya maziko, mwili wake utapelekwa nyumbani kwake Mikocheni B saa 5.00 asubuhi kwa ajili ya kufanyiwa kisomo na sala.
Kuhusu chanzo cha kifo chake Omar amesema, “suala la chanzo cha kifo chake nisingeependa kukizungumzia ibaki kuwa ‘privacy’ (faragha), lakini mzee aliumwa kwa wiki mbili hadi anafikwa na mauti.”
Kufuatia kifo hicho juzi Rais John Magufuli alituma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na mabalozi wengine kwa kuondokewa na mpendwa wao.


MAREHEMU NDESAMBURO AZIKWA LEO KIJIJINI KWAKE MKOANI KILIMANJARO


Gari lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo likielekea kwenye kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboriloni kwa ajili ya kuombewa. Maziko ya Marehemu Ndesamburo yanafanyika leo nyumbani kwake mtaa wa  KDC- Moshi,mkoani Kilimanjaro.
Gari lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo likiingia kwenye kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboroloni.
Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, Freeman Mbowe akiiingia katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboroloni kwa ajili ya kumuaga aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo.
Viongozi mbali mbali wa Chadema wakiingia katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboriloni.
Viongozi mbali mbali wa Chadema wakiingia katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboriloni. Waziri mkuu wa Zamani ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa akiingia kanisani.
Wabunge wa Chadema wakiwa wamejipanga kupokea mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo katika kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Kiboriloni.
Wajukuu wa Marehemu Phillemon Ndesamburo wakielekea kanisani.
Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo ukiingizwa kanisani.
Waziri mkuu wa Zamani ambaye ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chadema, Edward Lowassa akibadilishana mawazo na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi katika ibada ya kumuaga aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo.
Viongozo wa Chadema wakiwa katika ibada ya kumuombea aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo.
Mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo ukiwa kanisani tayari kwa maombezi.
Mke wa Marehemu aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo (wa pili toka kushoto) akiwa kanisani.

RAIS DKT. MAGUFULI AMUAPISHA MHE ANNA ELISHA MGHWIRA KUWA MKUU WA MKOA WA KILIMANJARO LEO



 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Anna Elisha Mghwira kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Ikulu jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi ,Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Wakuu wa Wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na viongozi wengine Ikulu jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu wa CCM-Bara Rodrick Mpogolo akimkabidhi Ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi CCM Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Elisha Mghwira huku Rais Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ,Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Salum Hapi pamoja na wakuuu wa Wilaya za Ubungo na Ilala wakipiga makofi. Picha na IKULU

VIJANA WATOA SIRI KUFICHUA MITANDAO YA UHALIFU NCHINI


TAA 2















Zaidi ya vijana wapatao  1230  wametoa siri nzito kwa  Maaskofu na Mashekhe  kutoka katika Kamati ya Kitaifa ya Maadili , Amani na Haki za Binadamu kwa Jamii ya Madhehebu ya Dini  Nchini  kufichua mtandao  haramu  wa watu  wanaoendesha mauaji na uhalifu mwingine kwenye   mikoa  13, nchini kama njia muhimu ya kumpongeza IGP mpya, Saimoni Sirro.

 Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Askofu William Mwamalanga, siri hiyo imetolewa  jana  na vijana hao katika   siku ya  tatu  mkutano wa kujenga maadili kwa vijana unao fanyika Mbagala, jijini Dar es Salaam na kuwashirikisha   vijana  wa madhehebu mbalimbali ya dini  kutoka katika  mikoa ya Pwani, Tanga, Lindi,  Morogoro,Dar es Salaam  ambapo wameyataja maeneo ya Mkuranga, Rufiji  Kigamboni, Kibiti, Msata, Tanga mjini, Pemba na Unguja kuwa maeneo hatari yanayowajengea vijana imani za  kigaidi.

 Aidha, Askofu Mwamalanga alisema kuwa vijana 147  wa kiislamu wanaohudhuria mkutano huo  wamewataja  baadhi ya watu  ambao ni   hatari  na wamekuwa wakieneza elimu ya mauaji  kwenye  misikiti mbali mbali nchini kwa kuiita Serikali ya Awamu ya Tano jina la katili na kwamba elimu hiyo imesambazwa kwa kasi  katika mikoa ya  Kagera, Tanga, Mwanza, Arusha, Pemba, Unguja, Dar es Salaam, Lindi, Mtwara, Morogoro, Iringa, Singida, Dodoma, Pwani na Kigoma huku vikosi vya vijana vikiandaliwa kufanya mauaji  mara baada ya mufungo mtukufu wa Ramadhani kama yale ambayo yamekuwa yakifanywa  Mukuranga, Kibiti  na Rufiji. 

Vijana hao wanamuomba  IGP  Sirro kuwachukulia hatua kali maafisa wa jeshi hilo ambao wanatumia jeshi kupandikiza Umngiki, na  kwamba wana imani na IGP Sirro amabaye kwa mujibu wa hao vijana hatamwangusha Rais  Magufuli na watanzania kwa ujumla.

Akifunga  Mkutano huo  Askofu Mwamalanga  amemtaja IGP  Sirro kama polisi mahiri wa maadili na jemadali  mweledi wa mapambano hivyo amewataka  vijana kote nchini kumuunga mkono kwa kuwafichua polisi wote wanaoenzi uhalifu. “Tusipofanya hivyo tutakuwa  kama  pipa zuri  tunalo jaza maji wakati tukijua chini limetoboka”,alisema Askofu Mwamalanga na kuongeza kuwa raia wema ni asilimia 99.9  wahalifu ni 0.1   hii ina maana kuwa ukiondoa polisi wahalifu  ndani ya jeshi hilo wahalifu ni wachache mno  mitaani  watayeyuka wenyewe. 

Aidha,  Askofu huyo amewahimiza vijana na viongozi wa dini kushiriki kwenye mafunzo hayo kote nchini ili  wapewe ufahamu wa elimu ya maadili ya kweli  ili wawe walinzi wa taifa na kupenda amani  na kuweka uchu wa kuchukia rushwa  na kujiwekea  mitazamo ya kupenda kazi za baraka.

Kiongozi huyo wa dini amekemea vikali nyumba za ibada   kugeuzwa  eneo la mafunzo ya uhalifu kwani ni aibu kwa msikiti au kanisa kufanya  mafunzo ya kigaidi  ndani  ya  nyumba  za ibada  kufanya hivyo ni ibada ya sanamu, watu wa jinsi hiyo hawana uhusiano wowote na Mwenyenzi MUNGU ambaye kusudi lake ni kuondoa uovu kwa mwanadamu.

Hivi karibuni yametokea mauaji ya viongozi wa Chama Tawala maeneo ya Kibiti, Mukuranga na Rufiji na kufanya wakazi wa maeneo hayo kuishi kwa wasiwasi na mashaka juu ya maisha yao. Wakati akiipishwa kuwa IGP, Kamanda Simon Sirro alisema kupambana na kuondoa uhalifu kwa kushirikiana na raia wema ni moja ya vipaumbele vyake.

MZEE NDESAMBURO AKITOLEWA HESHIMA ZA MWISHO


Sanduku lenye Mwili wa Marehemu wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo,ukiandaliwa tayari kwa kuagwa katika uwanja wa Majengo,mjini Moshi mkoani Kilimanjaro mapema leo mchana.
  Gari lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo lilielekea katika viwanja vya Majengo kwa ajili ya kuagwa mwili huo.
Waziri Mkuu Mstaafu, Edward Lowassa akiwapungia mkono wananchi waliofika kwenye uwanja  huo mara baada ya kuwasili katika viwanja vya Majengo kwa ajili ya kuagwa mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo.
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe akiwasili atika viwanja vya Majengo kwa ajili ya kuagwa mwili wa  aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo.
Wabunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wakiwa wamebeba jeneza lililobeba mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo. 
Viongozi mbalimbali wa Kisiasa na dini wakiwa wamesimama mara baada ya mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Marehemu Phillemon Ndesamburo kuwasili uwanjani hapo



 Baadhi ya wakazi wa mji wa Moshi mkoani Kilimanjaro wakiwa kwenye uzuni mara baada ya mwili wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoani Kilimanjaro, Phillemon Ndesamburo ulipokuwa unaelekea katika viwanja vya Majengo kwa ajili ya kuagwa mwili huo.