Tuesday, June 6

Cisco kuzikwa kesho Kisutu


Balozi Abdul Cisco Mtiro enzi za uhai wake 

By Ephrahim Bahemu, Mwananchi
Dar es Salaam. Mwili wa aliyekuwa Mkuu wa Itifaki Ikulu katika Serikali ya awamu ya tatu na nne, Balozi Abdul Mtiro ‘Cisco’ utazikwa kesho, Jumatano, katika makaburi ya Kisutu jijini hapa.
Cisco ambaye pia aliwahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Ufilipino, Cambodia na Singapore, alifariki juzi katika Hospitali ya Agha Khan alikokuwa akipatiwa matibabu.
Omar Mtiro ambaye  ni mtoto wa kwanza wa marehemu Cisco kati ya wanne, amesema mazishi  yatafanyika kesho  saa 7.00 mchana katika makaburi ya Kisutu.
Omar amesema kabla ya maziko, mwili wake utapelekwa nyumbani kwake Mikocheni B saa 5.00 asubuhi kwa ajili ya kufanyiwa kisomo na sala.
Kuhusu chanzo cha kifo chake Omar amesema, “suala la chanzo cha kifo chake nisingeependa kukizungumzia ibaki kuwa ‘privacy’ (faragha), lakini mzee aliumwa kwa wiki mbili hadi anafikwa na mauti.”
Kufuatia kifo hicho juzi Rais John Magufuli alituma salamu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na mabalozi wengine kwa kuondokewa na mpendwa wao.


No comments:

Post a Comment