Thursday, October 5

Mshahara wa Magufuli mdogo kuliko marais wenzake

Rais wa Tanzania John Magufuli amefichua kuwa anapokea mshahara wa shilingi milioni 9 za Kitanzania kwa mwezi, sawa na dola 4000, hivyo kumfanya miongoni mwa viongozi wachache wa Afrika wanaopokea mishahara midogo.

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli (kulia) na makamu wake Samia Suluhu Hassan. (DW/Said Khamis)
Rais Magufuli yuko katika harakati za kufanikisha sera ambayo imeshutumiwa vikali ya kupunguza kwa kiasi kikubwa matumizi ya fedha za umma. Katika hotuba aliyoitoa mjini Dar Es Salam siku ya Jumanne wiki hii, Kiongozi huyo wa Tanzania alisema serikali imepunguza mishahara ya maafisa wakuu watendaji wa mashirika ya serikali hadi shilingi milioni 15 ambazo ni sawa na dola 6,700 kiasi ambacho ni cha juu kuliko mshahara wake.
Magufuli alisema kama wanahisi kiwango hicho cha fedha ni kidogo, wana uhuru wa kuziacha kazi zao akiongeza kuwa matumizi mabaya ya fedha za umma yamekithiri katika mashirika ya serikali na amekataa maombi kutoka kwa baadhi ya maafisa kuongeza marupurupu yao akihoji hawezi kuongeza mishahara ya watumishi wa umma wakati raia wa kawaida hawana huduma za maji, afya na umeme.
Tangu kuchukua madaraka mwezi Novemba mwaka 2015, Magufuli ajulikanaye kwa jina maarufu la Tinga Tinga, amepunguza matumizi ya serikali kwa kuchukua hatua kadhaa kama kudhibiti safari za nje za maafisa wa serikali, kuondolewa kwa wafanyakazi hewa kutoka kwa utumishi wa umma.
Zuma apokea Dola za Kimarekani 20,000
Baadhi ya wakosoaji wake wanamshutumu kuwa baadhi ya hatua zake zimevuka mipaka wakihoji zitaathiri ukuaji wa kiuchumi wa taifa hilo la pili kwa nguvu za kiuchumi katika kanda ya Afrika Mashariki na baadhi ya maamuzi yake yanaoekana kurudisha nyuma uwekezaji katika sekta muhimu kama madini.
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini (Reuters/M. Hutchings)
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini
Mshahara wa Magufuli ukilinganishwa na wa viongozi wengine wa Afrika ni mdogo mno. Kiongozi huyo wa Tanzania hana vyanzo vingine vya kujipatia kipato vinavyojulikana na serikali yake mwaka jana ilisema ina mipango ya kuwasilisha mswada bungeni utakaowazuia viongozii wa umma kujishughulisha na biashara ili kuepusha mgongano wa maslahi.
Rais wa nchi jirani ya Kenya Uhuru Kenyatta anapokea mshahara wa takriban dola 14,000 kwa mwezi, Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma analipwa mshahara wa dola 20,000 kwa mwezi kufuatia bunge mwaka 2015 kuidhinisha nyongeza ya mshahara wa rais.
Kiongozi mwingine wa Afrika ambaye ana mshahara wa wastani ni Rais wa Nigeria Muhamadu Buhari ambaye alikubali mshahara wake upunguzwe kwa asilimia 50 alipoingia madarakani mwezi Mei mwaka 2015. Awali mshahara wa Rais wa Nigeria ulikuwa naira milioni 14.1 ambazo zilikuwa ni sawa na dola 70,000 wakati huo.

Afrika kuinusuru Burundi na uchunguzi wa kimataifa

Mataifa ya Afrika yameanzisha mkakati kwenye Umoja wa Mataifa, ambao wakosoaji wanasema ni hatua ya dakika za mwisho mwisho ya kuinusuru Burundi kutofanyiwa uchunguzi zaidi juu ya madai ya uhalifu dhidi ya ubinadamu. 

Burundi Gewalt und Proteste (Reuters/G. Tomasevic)
Septemba 25, tume hiyo ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa ilitoa mwito kwa mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC kuchunguza visa vya uhalifu dhidi ya ubinaadamu nchini Burundi. Matukio kama mauaji, utesaji, unyanyasaji wa kingono, utoroshwaji kwa nguvu na kukamwata ovyo, yamekuwa yakiendelea kutokea tangu Aprili 2015, baada ya Rais Pierre Nkrunziza kuingia madarakani kwa awamu ya tatu, hii ikiwa ni kulingana na ripoti iliyotolewa mapema mwezi huu.
Baraza la haki za binaadamu ya Umoja wa Mataifa lilikuwa likitarajiwa kuunga mkono azimio la Umoja wa Ulaya leo hii la kuongeza mamlaka ya tume ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa ambayo ilisema viongozi wa juu wa Burundi wanapaswa kuwajibika kwa uovu nchini humo.
Lakini kundi hilo la mataifa kutoka Afrika, linaloongozwa na Tunisia, liliitisha mkutano wake jana Jumatano na kuweka wazi azimio tofauti, ambalo liliisifu Burundi kwa kuonyesha nia ya kufanyika kwa mazungumzo na kushirikiana na Umoja wa Mataifa, bila ya kuzungumzia lolote kuhusu kuanzishwa upya kwa uchunguzi.
Balozi wa Burundi Renovat Tabu alidai kwamba tume hiyo ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa ilikuwa na upendeleo na ripoti zake kuhusu machafuko na uovu hazikuakisi uhalisia.
Tume yataka ICC kuingia kati iwapo Burundi haitarekebisha mfumo wa kisheria.
Kwenye mkutano wa tume hiyo ya uchunguzi uliofanyika Jumatatu mjini Brussels, rais wake Fatsah Ouguergouz, alisema iwapo serikali ya Burundi haitaweza kuzungumzia uhalifu, basi suala hilo litatakiwa kukabidhiwa kwa taasisi nyingine. Na taasisi pekee inayoweza kufanya kazi hiyo ni ICC.
Mabalozi kutoka Umoja wa Ulaya, Marekani, Norway, Uswisi, Canada na Uingereza walikataa kujadili maudhui ya azimio la kundi hilo la mataifa ya Afrika na kueleza kukasirishwa huku kukisalia saa 24 tu kabla baraza kuanza kufanya maamuzi juu ya maazimio ya Umoja huo wakati kikao kilichodumu kwa wiki tatu kinapomalizika.
Wawakilishi wa Umoja wa Ulaya walisema hali nchini Burundi bado ni tete na kuna uwezekano wa kuendelea kutokea kwa visa vya kutisha vya uvunjwaji wa haki za binaadamu. 
Mwakilishi wa Marekani alisema hatua ya ghafla ya Burundi ya kutaka kushirikiana, wakati hapo awali iligoma kufanya kazi na tume ya uchunguzi ya Umoja wa Mataifa, ilionekana kuanza si zaidi ya siku tatu zilizopita. "Nadhani mazungumzo haya yataendelea, lakini kwa upande mwingine sidhani kama tunaweza kukubali ushahidi wa chini ya asilimia moja ya mwaka kuakisi kile kinachoweza kutokea," aliuambia mkutano.
Mkakati huo wa kundi la mataifa ya Afrika kuchukua jukumu la kuichunguza Burundi unaakisi mwendelezo wa mwenendo wa viongozi wa Afrika wa kukwepa masuala mazito  kutoka Umoja wa Mataifa, na hususan mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC ya mjini The Hague.

WAGENI WOTE WANAOISHI HAPA NCHINI WATAKIWA KURIPOTI OFISI ZA UHAMIAJI WAKIWA NA VIBALI VYAO VYA UKAAZI

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA 
WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI 
IDARA YA UHAMIAJI 




WAGENI WOTE WENYE VIBALI VYA UKAAZI WANATAKIWA KURIPOTI KATIKA OFISI ZA UHAMIAJI ZILIZOPO KATIKA MAENEO WANAYOISHI NA KUFANYIA KAZI WAKIWA NA VIBALI VYAO.

Idara ya Uhamiaji inapenda kuwafahamisha Waajiri, Wakurugenzi wa Makampuni, Taasisi mbalimbali na Wageni wote wanaoishi na kufanya kazi nchini kwamba wanatakiwa kuripoti na kuwasilisha taarifa za anuani zao zikiwemo na mabadiliko katika Ofisi za Uhamiaji zilizopo katika maeneo wanayoishi na kufanya kazi katika kipindi cha siku thelathini 30 tangu kutolewa kwa taarifa hii. 

Zoezi hili linafanyika kwa lengo la kuhuisha taarifa na kumbukumbu za Wageni wakaazi ambao baadhi yao wamehama maeneo yao ya awali na kuhamia sehemu nyingine na linafanyika kwa mujibu wa Kanuni ya 29 (1), (2) na 30 za Kanuni za Uhamiaji za Mwaka 1997 na Marekebisho yake ya Mwaka 2016, chini ya Sheria ya Uhamiaji Sura ya 54 Rejeo la Mwaka 2002. 

Aidha, ieleweke kwamba kutokufanya hivyo ni kosa kisheria chini ya Kanuni ya 29 (3) na 37 ya Kanuni za Uhamiaji za Mwaka 1997 na marekebisho yake ya mwaka 2016 chini ya sheria ya uhamiaji sura 54 rejeo la mwaka 2002. 

Imetolewa na 

SAMWEL RHOBBY MAGWEIGA 
KAMISHNA WA USIMAMIZI NA UDHIBITI WA MIPAKA, 
MAKAO MAKUU YA UHAMIAJI, 
04 OKTOBA, 2017.

RAIS DKT MAGUFULI AWAAPISHA MABALOZI WAPYA WA TANZANIA NCHINI MISRI NA ZAMBIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Mhe. Issa Suleim Nassor kuwa balozi wa Tanzania nchini Misri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kimkabidhi nyenzo za kazi baada ya kumuapisha Mhe. Issa Suleim Nassor kuwa balozi wa Tanzania nchini Misri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Balozi mpya wa Tanzania nchini Zambia Mhe. Abdulrahman Kaniki Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017 Abdulrhaman Kaniki kuwa balozi wa Tanzania nchini Misri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kimkabidhi nyenzo za kazi baada ya kumuapisha Mhe. Abdulrahman Kaniki kuwa balozi wa Tanzania nchini Zambia Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli balozi mpya wa Tanzania nchini Misri Mhe. Issa suleiman Nassor na Mhe. Abdulrahman Kaniki balozi mpya wa Tanzania nchini Zambia wakila viapo vya maadili ya viongozi baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017
Balozi mpya wa Tanzania nchini Misri Mhe. Issa suleiman Nassor akiongea machache baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017
Blozi mpya wa Tanzania nchini Zambia Mhe. Abdulrahman Kaniki machache baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza baada ya kumuapisha Mhe. Abdulrahman Kaniki kuwa balozi wa Tanzania nchini Zambia Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza baada ya kumuapisha Mhe. Issa Suleim Nassor kuwa balozi wa Tanzania nchini Misri Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa, Naibu Waziri wa mambo ya Nje Dkt. Suzan Kolimba, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, Katibu Mkuu wa Wizara ya mambo ya Nje Dkt. Aziz Ponary Mlima na Viongozi wa vyombo vya ulinzi na Usalama wakiwa katka picha ya pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zambia Mhe. Abdulrahman Kaniki na balozi mpya wa Tanzania nchini Misri Mhe. Issa suleiman Nassor baada ya kuapishwa Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa wakiwa katka picha ya pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Zambia Mhe. Abdulrahman Kaniki na maofisa waandamizi wa Polisi Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa pamoja na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali Venance Mabeyo wakiwa katika picha ya pamoja na Balozi mpya wa Tanzania nchini Misri Mhe. Issa suleiman Nassor Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017 

Picha na IKULU

UPASUAJI WA MOYO

WATOTO 28 WAFANYIWA UPASUAJI WA MOYO WA KUFUNGUA KIFUA NA BILA KUFUNGUA KIFUA KATIKA KAMBI MAALUM YA UPASUAJI KWA WATOTO INAYOFANYWA NA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI) KWA KUSHIRIKIANA NA SHIRIKA LA MENDING KIDS LA NCHINI MAREKANI


Afisa Muuguzi wa chumba cha wagonjwa waliopo katika uangalizi maalum (ICU) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Veronica Vedastus na Arianna Minghetti wa Shirika la Mending Kids la nchini Marekani wakimnywesha maziwa mtoto aliyefanyiwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo bila ya kufungua kifua (Catheterization) katika kambi maalum ya siku tano ya upasuaji kwa watoto inayofanyika katika Taasisi hiyo. Watoto wanaofanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ni wale waliozaliwa na magonjwa ya moyo kuwa na tundu na mishipa ya damu kutopitisha damu vizuri.
Madaktari bingwa wa Upasuaji wa Magonjwa ya Moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Shirika la Mending Kids la nchini Marekani wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kufungua kifua na kuziba tundu la moyo katika kambi maalum ya siku tano ya upasuaji kwa watoto inayofanyika katika Taasisi hiyo . Jumla ya watoto 28 wamefanyiwa upasuaji kati ya hao 19 upasuaji wa bila kufungua kifua na tisa upasuaji wa kufungua kifua.
Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na Shirika la Meding Kids la nchini marekani wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa moyo wa bila kufungua kifua (Catheterization) na kuzibua mishipa ya Moyo katika kambi maalum ya siku tano ya upasuaji kwa watoto inayofanyika katika Taasisi hiyo . Jumla ya watoto 28 wamefanyiwa upasuaji kati ya hao 19 upasuaji wa bila kufungua kifua na tisa upasuaji wa kufungua kifua.
Maafisa Uuguzi wa chumba cha wagonjwa waliopo katika uangalizi maalum (ICU) wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na mwezao wa Shirika la Mending Kids la nchini Marekani wakijadiliana kuhusu maendeleo ya wagonjwa waliolazwa katika chumba hicho baada ya kufanyiwa upasuaji wa moyo katika kambi maalum ya siku tano ya upasuaji kwa watoto inayofanyika katika Taasisi hiyo. Watoto wanaofanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ni wale waliozaliwa na magonjwa ya moyo kuwa na tundu na mishipa ya damu kutopitisha damu vizuri.Picha na JKCI

RC SHIGELLA AFUNGUA MKUTANO WA BARAZA KUU LA 47 LA WAFANYAKAZI WA TANESCO NCHINI MJINI TANGA LEO


Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella akifungua Baraza kuu la 47 la Wafanyakazi wa Shirika la Umeme nchini Tanzania (Tanesco) uliofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Tanga kulia ni Katibu wa Baraza hilo,Asmaa Myale
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme la Tanzania (Tanesco) Dkt  Tito Mwinuka akitoa hutuba yake wakati wa ufunguzi huo uliofanyika mjini Tanga 
Mwenyekiti wa Tuico Taifa,Paul Sangeze akizungumza wakati wa Baraza hilo kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco,Dkt Tito Mwinukakatika mkutano huo uliofanyika mjini Tanga 
Katibu wa Baraza Kuu la Wafanyakazi,Asmaa Myale akizungumza katika mkutano huo kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco)Dkt Tito Mwinuka na Mwenyekiti wa wa Tuico Taifa,Paul Sangeze
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella kushoto akipongezwa na Mwenyekiti wa Tuico Taifa,Paul Sangeze mara baada ya kufungua mkutano wa Baraza kuu la 47 la wafanyakazi wa Shirika la Umeme nchini Tanzania (Tanesco) leo mjini Tanga anayeshughudia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo,Dkt Tito Mwinuka kushoto ni Katibu wa Baraza kuu la wafanyakazi,Asmaa Myale.
Baadhi ya wajumbe wa baraza hilo wakifuatilia kwa umakini hotuba ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martin Shigella .
Sehemu ya wajumbe wa mkutano huo wakiufuatilia kwa umakini 
Wajumbe wa mkutano huo wakifuatilia kwa umakini mkutano huo
Kaimu Meneja Uhusiano wa Tanesco Tanzania,Leila Muhaji wa pili kushoto aliyevaa koti jeusi akichukua baada ya dondoo wakati Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella alipofungua Baraza Kuu la 47 la Wafanyakazi wa Tanesco nchini mjini Tanga 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella kulia akitoa nje ya ukumbi mara baada ya kufungua baraza hilo kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco)Dkt Tito Mwinuka katikati ni Mwenyekiti wa TUICO Taifa Paul Sangeze 
Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Tanesco kulia ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo,Dkt Tito Mwinuka kushoto ni Katibu wa Baraza Kuu la Wafanyakazi,Asmaa Myale mara baada ya kufungua mkutano wa baraza kuu la 47 la wafanyakazi wa Tanesco
Picha ya pamoja na wafanyakazi wa Shirika hilo mara baada ya kufungua baraza kuu hilo
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Dkt Tito Mwinuka kushoto akiagana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella mara baada ya kufungua mkutano wa Baraza Kuu la 47 la Wafanyakazi wa Tanesco
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Tenesco,Dkt Tito Mwinuka akiuzungumza na waandishi wa habari mara baada ya kufunguliwa kwa mkutano wa baraza hilo leo na Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Martini Shigella 
Katibu wa Baraza Kuu la Wafanyakazi,Asmaa Myale akizungumza na waandishi wa habar,Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha. 

UNESCO, ILO, UNICEF, UNDP NA EDUCATION INTERNATIONAL YATOA SALAMU KWA WALIMU DUNIANI

Kufundisha Kwa Uhuru, Kuwawezesha Walimu Walimu ni msingi mkuu katika ustawi wa muda mrefu wa kila jamii kwa kuwa hujishughulisha kuwapatia watoto, vijana na watu wazima elimu na ujuzi wanaohitaji ili kufikia uwezo wao. 


Lakini duniani kote, walimu wengi sana hawana uhuru na msaada wanaohitaji kufanya kazi yao iliyo muhimu sana. Ndiyo maana maudhui ya Siku ya Walimu Duniani kwa mwaka huu – ‘'Kufundisha kwa Uhuru, Kuwawezesha Walimu'’ - inathibitisha thamani ya walimu waliowezeshwa na kutambua changamoto ambazo wengi hukabiliana nazo katika maisha yao ya kitaaluma ulimwenguni kote. 

Kuwa mwalimu aliyewezeshwa ina maana ya kuwa na uwezo wa kupata mafunzo yenye ubora, malipo ya haki, na fursa zisizo na mwisho za kujiendeleza kitaaluma. Pia inamaanisha kuwa na uhuru wa kuunga mkono maendeleo ya mitaala kitaifa – na uhuru wa kitaaluma wa kuchagua njia sahihi na mbinu zinazofaa zaidi kuwezesha utoaji wa elimu yenye ufanisi, jumuishi na ya usawa. Zaidi ya hayo, inamaanisha kuwa na uwezo wa kufundisha kwa usalama wakati wa mabadiliko ya kisiasa, machafuko, na migogoro. 

Lakini katika nchi nyingi, uhuru wa kitaaluma na uhuru wa mwalimu viko chini ya shinikizo. Kwa mfano, katika ngazi za shule za msingi na za sekondari katika baadhi ya nchi, mipango ya uwajibikaji imeweka shinikizo kubwa kwa shule kutoa matokeo kwa vipimo vilivyowekwa, na kupuuza haja ya kuhakikisha mtaala wa msingi unaofaa mahitaji tofauti tofauti ya wanafunzi. 

Uhuru wa kitaaluma ni muhimu kwa walimu katika kila ngazi ya elimu, lakini ni muhimu zaidi kwa walimu wa elimu ya juu, ili uwawezeshe kutumi uwezo wao wa kuvumbua, kuchunguza, na kuendeleza utafiti kuhusiana na namnaza kisasa zaidi za kufundisha. Katika ngazi ya elimu ya juu, mara nyingi walimu hupatiwa mikataba ya ajira ya kipindi maalumu. 

Hii inaweza kusababisha hali ya kutokuwa na uhakika wa ajira kwa walimu, kupungua kwa matarajio ya kukua kitaaluma, mzigo mkubwa wa kazi na malipo duni – yote haya yanaweza kuzuia uhuru wa kitaaluma na kudhoofisha ubora wa elimu ambayo walimu wanaweza kutoa. 

Katika ngazi zote za elimu, shinikizo la kisiasa na maslahi ya kibiashara yanaweza kuzuia uwezo wa walimu kufundisha kwa uhuru. Waalimu wanaoishi na kufanya kazi katika nchi na jamii zilizoathiriwa na migogoro na machafuko mara nyingi hukabiliwa na changamoto kubwa zaidi, ikiwa ni pamoja na kupungua kwa kuvumiliana, ubaguzi, na vikwazo vinavyohusiana na utafiti na kufundisha. 

Mwaka huu unaadhimisha kumbukumbu ya miaka 20 ya Mapendekezo ya UNESCO ya 1997 kuhusu Hali ya Wakufunzi wa Elimu ya Juu, ambayo inakamilisha Mapendekezo ya UNESCO / ILO ya 1966 kuhusu Hali ya Walimu. Kwa pamoja, vyombo hivi hufanya mfumo mkuu wa rejea juu ya haki na wajibu wa walimu na waelimishaji. Yote yanasisitiza umuhimu wa uhuru wa mwalimu na uhuru wa kitaaluma katika kujenga ulimwengu ambapo elimu na kujifunza ni kwa ajili ya wote. 

Wakati dunia inapofanya kazi pamoja ili kufikia maono ya Malengo ya Maendeleo Endelevu, tunawaomba washirika wetu katika serikali, sekta ya elimu na sekta binafsi kujitolea kubeba jukumu la kuwaandaa waelimishaji wenye ujuzi ulio bora zaidi, wenye thamani na waliowezeshwa.

 Hii ni njia muhimu katika kuyafikia maono ya Malengo ya Maendeleo Endelevu hasa lengo namba 4 lenye nia ya kuwa na ulimwengu ambapo kila msichana, mvulana, mwanamke na mwanaume wanapata elimu bora na fursa za kujifunza katika maisha yao yote. 

Hii inamaanisha kuwapatia walimu mazingira mazuri ya kazi na mishahara iliyo bora, ikiwa ni pamoja na walimu wa ngazi ya juu. Inamaanisha kuwapa walimu mafunzo na fursa ya kujiendeleza. Inamaanisha kuongeza idadi ya walimu wenye ubora, hasa katika nchi zenye idadi kubwa ya walimu na waelimishaji wasio na elimu ya kutosha. 

Inamaanisha ya kuondoa vikwazo visivyo vya lazima katika utafiti na kufundisha na kulinda uhuru wa kitaaluma katika ngazi zote za elimu. Na mwisho, inamaanisha kuinua hadhiya walimu duniani kote kwa namna ambayo inaheshimu na inayoonyesha matokeo waliyonayo walimu katika jamii. 

Katika Siku hii ya Walimu Duniani, ungana nasi katika kuwawezesha walimu kufundisha kwa uhuru ili kwamba, kila mtoto na kila mtu mzima awe huru kujifunza – kwa manufaa ya dunia iliyo bora zaidi. Imetolewa na Irina Bokova, Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO; Guy Ryder, Mkurugenzi Mkuu wa ILO; Anthony Lake, UNICEF Executive Director; Achim Steiner, UNDP Administrator; pamoja na Fred van Leeuwen, General Secretary of Education International.

Homa Ini Bado Waendelea Kuwa Tishio

  Mkurugenzi wa Huduma za Tiba katika hospitali hiyo, Dk. Hedwiga Swai akisisitiza watu kujitokeza kupima afya ili kuthibiti homa ya ini pamoja na magonjwa mengine.
 Baadhi ya watumishi wa hospitali hiyo wakiwamo madaktari na wauguzi wakifuatilia kongamano hilo.
 Daktari Bingwa wa Magomjwa ya Mfumo wa Chakula na Ini, John Rwegasha wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) akizungumza katika kongamano jinsi ya kudhibiti na kutibu magonjwa ya mfumo wa chakula na ini.
Baadhi ya madaktari, wauguzi wa hospitali hiyo na watumishi wengine wakiwa kwenye kongamano hilo leo.
 Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Mfumo wa Chakula na Ini, Priumus Saidia akizungumza kwenye kongamano hilo leo.


Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) imetoa ripoti ya robo mwaka tangu ianze kufanya uchunguzi wa Virusi vya Homa ya Ini ( Hepatitis B) na kutoa tiba ya ugonjwa huo kwa kutumia dawa ya Tenofovir .

Akitoa taathimini hiyo leo jijini Dar es salaam,  Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Ini na Matumbo John Rwegasha amesema  muamko ni mkubwa  ambapo katika kipindi cha robo mwaka , Hospitali ya Taifa Muhimbili imesajili wagonjwa  950 .

Akifanunua amesema  hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu idadi  ya wagonjwa itaongezeka na kufika   1800  .Hata hivyo kati ya hao , wagonjwa 540 ndio wamerudi tena Hospitalini kwa ajili ya kuendelea na mchakato wa uchunguzi huku wagonjwa wengine wakishindwa kufika kutokana na sababu za mbalimbali hususani za kiuchumi , nakuongeza kwamba waliopo kwenye tiba ni  wagonjwa 40.

‘’Idadi ya wagonjwa imeongezeka mara dufu hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu watafika wagonjwa 1800  lakini pamoja na changamoto hiyo hatuwezi kusimamisha huduma tutaendelea kutoa huduma kwani kwa upande wa dawa tumejidhatiti kwa miaka mitano , wagonjwa  hawa wanatakiwa wafanyiwe uchunguzi  ili aanze kutumia dawa lakini  si wote wanaohitaji dawa’’ amesema DK. Rwegasha.

Kwa upande wake Dk. Tuzo Lyuu amesema tatizo la ugonjwa huo ni kubwa kwani tafiti ambazo zimefanyika ,  watu wanaoenda kuchangia damu asilimia nane wanatatizo hilo na kusisitiza kuwa tatizo hilo si la Tanzania pekee bali  hata kwa nchi zingine zinazoendelea.Kwa mujibu wa Dk. Lyuu kwa sasa tatizo la Homa ya Ini (Hepatitis B) ni kubwa kuliko Ukimwi .‘’ Hapa MNH watu tunaowaona ni vijana na watu wazima na wanaume ndio wengi ingawa hakuna takwimu halisi’’ amesema Dk. Lyuu.

Ugonjwa wa Homa ya Ini unasababishwa na Virusi viitwavyo Hepatitis B na maambukizi ya ugonjwa huo yanashabiana na njia ya  maambukizi ya Vrusi vya  Ukimwi kama vile kufanya ngono zisizo salama, kuchangia sindano au vikatio, kupewa damu isiyopimwa , kupitia uzazi wa mama na mtoto hasa wakati wa kujifungua.

Sudan ''yakata uhusiano wake na Korea Kaskazini''

Rais wa Sudan Omar El Bashir anasakwa na mahakama ya ICCHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais wa Sudan Omar El Bashir anasakwa na mahakama ya ICC
Sudan imekata uhusiano wake na Korea Kaskazini ili kuafikia masharti ya Marekani ya kuondolewa kwa vikwazo, kulingana na gazeti la Uingereza la Financial Times.
Washington inatarajiwa kutangaza uamuzi wake wa iwapo itaiondolea Sudan vikwazo vyote mnamo tarehe 12 mwezi Oktoba.
Afisa mwandamizi wa serikali ya Sudan alisema wameafikia masharti yote na wanatarajia vikwazo hivyo kuondolewa.
Mnamo mwezi Julai rais Donald Trump wa Marekani alichelewesha uamuzi wake wa kuiondolea Sudan vikwazo vyote kwa muda wa miezi mitatu.
Vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Sudan viliwekwa baada ya taifa hilo kudaiwa ''kufadhili ugaidi''.

Aliyechapisha habari ya ''nguo za ndani za Bi Grace Mugabe'' aachiliwa

Bi Grace MugabeHaki miliki ya pichaAFP
Image captionBi Grace Mugabe
Mwandishi wa Zimbabwe ambaye alikamatwa baada ya kuandika habari iliodai kwamba mbunge mmoja aligawanya nguo za ndani za mitumba kwa wafuasi wa chama tawala cha Zanu-PF kwa niaba ya mke wa rais bi Grace Mugabe amewachliwa kwa dhamana ya dola 200.
Kenneth Nyangani pia aliagizwa kuripoti kwa polisi katika mji wa mashariki wa Mutare mara moja kwa wiki.
Amekana mashtaka ya kuchafulia watu majina kufuatia chapisho la habari hiyo katika mtandao mpya wa kibinafsi wa NewsDay.
Maafisa wa polisi katika eneo la Mutare walimkamata bwana Nyangani Jumatatu kwa madai ya kuandika na kuchapisha habari kuhusu ufadhili wa chupi za mtumba zilizodaiwa kutolewa na mkewe rais Robert Mugabe kulingana na mawakili wa haki za kibinaadamu wa Zimbabwe katika taarifa yao.
Mbunge wa chama tawala cha Zanu-PF Esau Mupfumi alisambaza chupi hizo kwa wafuasi wa Zanu-PF mjini Mutare na kusema kuwa bi Mugabe alifadhili nguo kulingana na ripoti hiyo ya NewsDay.

Mkutano wa chama cha Jubilee wavamiwa na nyuki Kenya

Polisi na msamaria mwema wakijaribu kumsaidia mtu aliyevamiwa na nyuki nje ya mahakama ya juu nchini humoHaki miliki ya pichaEPA
Image captionPolisi na msamaria mwema wakijaribu kumsaidia mtu aliyevamiwa na nyuki nje ya mahakama ya juu nchini humo
Nyuki walitibua mkutano wa kisiasa wa chama tawala cha Jubilee nchini Kenya katika kaunti ya Taita-Taveta yapata kilomita 360 kutoka mji mkuu wa Nairobi kulingana na gazeti la The Standard.
Wafuasi wa chama hicho walilazimika kukimbilia usalama wao wakati nyuki hao walipowavamia , lakini wakapotea baada ya maombi kufanywa na mwanasiasa mmoja.
Wanasiasa walilaumu shetani kwa uvamizi huo wa mkutano huo uliofanyika katika mji wa Wundanyi ,ulioitishwa kumuunga mkono rais Uhuru Kenyatta kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa marudio wa Oktoba 26.
Mahakama ya juu nchini humo ilifutilia mbali ushindi wa rais Uhuru Kenyatta dhidi ya kiongozi wa upinzani Raila Odinga mnamo tarehe 8 mwezi Agosti ikisema kuwa uchaguzi huo ulikuwa na mkosa chungu nzima ikiwemo udanganyifu.
Nyuki wengine waliwavamia maafisa wa polisi na watu wengine nje ya mahakama katika mji mkuu wa Nairobi , wakati majaji walipotoa uamuzi wao kamili kuhusu kufutilia mbali matokeo ya uchaguzi huo tarehe 20 mwezi Agosti.

Familia ya Tundu Lissu wataka upelelezi wa kimataifa kuingia kati

Ndugu zake Tundu Lissu, Vincent Mughwai(kushoto) na Alute Mughwa (kulia)
Image captionNdugu zake Tundu Lissu, Vincent Mughwai(kushoto) na Alute Mughwa (kulia)
Familia ya mnadhimu mkuu wa kambi ya upinzani nchini Tanzania Tundu Lissu, imeiomba serikali ya nchi hiyo kuongeza kasi ya upelelezi wa kesi ya kushambuliwa kwa mbunge huyo wa Singida mashariki aliyepigwa risasi mnamo mwanzoni mwa mwezi jana huko mjini Dodoma.
Familia hiyo iliyowakilishwa na kaka zake wawili, wameitaka serikali kuvishirikisha vyombo vya upelelezi vya kimataifa kama vinavyoshirikishwa katika mambo mengine ili kuongeza ufanisi katika upelelezi huo.Tundu Lissu alipigwa risasi zaidi ya thelathini na watu ambao mpaka sasa hawafahamiki pindi alipokuwa mjini Dodoma akihudhuria vikao vya bunge.
Kwa upande wake, katika siku za hivi karibuni, jeshi la polisi nchini Tanzania lilisema upelelezi wa tukio hilo unasuasua kutokana na dereva wa Mbunge huyo kutofika polisi kutoa ushahidi.Hata hivyo, taarifa kutoka Chadema zinasema kuwa dereva wa mbunge huyo yuko nchini Kenya kwa ajili ya kupata matibabu ya kisaikolojia kutokana msongo wa mawazo alioupata baada ya kisa hicho.
Kufuatia kauli hiyo, familia hiyo imeliomba jeshi la polisi kufanya utaratibu wa kumfuata dereva huyo mjini Nairobi kwa ajili ya mahojiano ili uchunguzi uendelee.
Tundu Lissu yuko nchini Kenya kwa takribani wiki nne sasa ambako anapatiwa matibabu kutokana na majeraha ya risasi aliyoyapata kutokana na shambulio hilo.