Friday, April 20

TB Joshua again: Delivers man from shocking addiction!

This post and link to the video below were shared to us by Ihechukwu Njoku -- Controversial Nigerian Prophet T.B. Joshua can’t seem to stay out of the news. However, this time it’s not concerning a prophetic utterance or political visitor.

On Sunday 15th April 2012, Joshua’s popular church in Lagos was witness to a disgusting yet dramatic case of a man with a truly repulsive addiction. Mr Mukaila Malomo, a Nigerian who lived in Germany for 16 years, confessed to being addicted to regularly taking a sickening concoction of faeces, semen and urine.

According to Malomo, a graduate from the London School of Journalism, it all started one night in a prison cell in Germany. "I woke up in the middle of the night and a very wicked demon instructed me to get up from my bed,” he told the bewildered SCOAN congregation. “This strange voice said that I should go to the toilet, defecate and mix it with my sperm and urine. I mixed my urine, sperm and faeces and swallowed everything.”

Malomo, who worked in a reputable organic salad company in Munich before a drunken brawl landed him in prison, explained that an unusual anger and desire to fight immediately followed. “After I swallowed it, a very strange power came over me. I felt as if I was a small god. It overcame me and I became very strong and angry - as if there's an extra power from another world entering my body. I was ready for war. Ever since then, for over 15 years, I have been addicted to eating my faeces, urine and sperm. I can’t stop it.”

He continued his sordid tale, explaining how each indulgence in the addiction would result in further violence. “After my release from prison, I was always fighting in Germany. Sometimes, the police would have to cover the whole street to try and stop me - and I was using only a bottle. I kept on stabbing without getting tired – because of this power that entered me.”

People present in the church could scarcely contain their shock as Malomo’s revelations continued. “It is not only my own faeces; on many occasions, I visited public toilets here in Nigeria and Germany and ate from there.” He described the mixture as food to him. “I enjoy it. I don't even perceive any smell. I eat it as if I eat eba (Nigerian cuisine) or something like that.”

Malomo, married to a German Hungarian lady who gave birth to his only son while in prison, described how he had kept this addiction a total secret from the world around him. “As I am eating it, that evil spirit will be telling me that this thing is only for me, that nobody should know, otherwise the power will go.”

Joshua proceeded to tell his congregation and the viewers worldwide watching the live broadcast via Christian television station Emmanuel TV that a video clip would be shown to verify Malomo’s confession. Stating that it was too graphic for him to witness, he covered his face and advised viewers without strong stomachs to do likewise. The clip showed Malomo mixing his own urine and faeces together and then drinking the revolting contents with apparent ease and delight. People within the auditorium vomited at the sight, distressed at the level of degradation the addiction had rendered on Malomo.

Joshua then called on the congregants to join together in supplication and proceeded to pray for the ‘demon’ within Malomo to come out! Falling to the floor, Malomo’s body began vibrating uncontrollably and uncannily. Asked to explain what was happening, Malomo said he felt as if something was leaving his body.

Joshua then instructed Malomo to go to the church’s public toilet to see how his reaction towards human waste had changed following the prayer. Merely perceiving the odour of other’s defecation caused Malomo himself to vomit. He returned to the church, testifying that all desire for his former addiction had vanished as the realization of his earlier actions dawned upon him.“Apart from being irritated by the odour, I feel ashamed, in the sense that – how can a human being be eating faeces,” he told the congregation, as he joined Joshua in a joyful dance.

SCOAN has now controversially released the video on popular video-sharing site YouTube and via their Facebook account which has garnered well over 100,000 fans in just four months. Although Malomo’s case appears to be the most extreme, many with strange addictions claim to have been delivered at Joshua’s ministry over the last few months, including those addicted to drinking kerosene, eating ice cubes, sand, charcoal, mothballs and soil.

T.B. Joshua has set social networks and local media ablaze in recent months, especially with his prediction concerning the death of the late Malawian president Bingu wa Mutharika and revelations of his relationships with African leaders such as Ghana’s John Atta Mills, Zimbabwe’s Morgan Tsvangarai and Malawi’s new head Joyce Banda. His television station Emmanuel TV continues to increase in popularity, especially across Africa where he is becoming a household name.

Tafrisi ya Mjengwa kuhusu Zitto Kabwe na saini za Wabunge 70 kumg'oa Pinda


Ndugu zangu,

Leo asubuhi wakati nikifanya ' jogging' kwenye mitaa ya Dar es Salaam niliwasikia watu wa kawaida kabisa wakijiuliza na kujadili; " inakuwaje Serikali iwalipe marehemu mishahara huku sisi tulio hai hatuna hata uhakika wa milo miwili ya siku?" Wanauliza watu wa mitaani.

Naam, nchi yetu imekumbwa na mafuriko ya habari. Kule bungeni Dodoma kuna moto unawaka. Zimeitishwa sanini 70 ili Jumatatu ipigwe kura ya kukosa imani na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda. Ndio, kuna wanaotaka Pinda ang'oke, na labda kutolewa kafara, maana, siamini kama tatizo la msingi ni Pinda, bali ni la kimfumo zaidi. Na jana kuna mbunge wa CCM kayasema makali yafuatayo;

“Mheshimiwa Naibu Spika, inashangaza na kusikitisha kuwa nchi inatafunwa. Wanaofanya haya ni mawaziri wetu. Nchi inakufa na tuelewe kuwa Tanzania sio mali ya CCM, ni ya Watanzania wote.“Mawaziri wetu wamekuwa mchwa, wanaangamiza nchi na leo nitamtaja waziri anayeongoza kwa kutafuta fedha za Watanzania. Ni Waziri wetu wa Fedha, Mustafa Mkulo. Ameuza viwanja, amelidanganya Bunge baada ya kuivunja CHC,”- Deo Filikunjombe ( CCM) Bungeni jana.

Lakini ya jana yalitanguliwa na ya juzi; Mbunge mwanadamizi wa CCM Godfrey Zambi aliyasema makali haya;

" CCM inaweza kung'olewa madarakani katika uchaguzi wa mwaka 2015 endapo kasi ya ufisadi na ubadhirifu wa fedha za umma itaendelea kama ilivyo sasa"- Godfrey Zambi ( CCM, Mbozi Mashariki).

Kauli za wabunge hao wawili wa CCM zinatoa tafsiri ya kilio cha wabunge wa CCM kuomba msaada kwa anayeweza kuwasaidia. Inatoa tafsiri pia kuwa hicho ni kilio cha wabunge wengi wa CCM. Kwamba hayo ndiyo wanayaongea hata chini chini.

Ndio, wananung'unika na wameanza kuiona adhabu wanayokwenda kuipata kutoka kwa wananchi ifikapo 2015. Wanaona pia, kuwa ' kisungura' hiki kidogo kinachopatikana kila mwaka kinavyoliwa na wajanja na wengine kuachiwa mifupa.

Wabunge wa CCM na wengine wanaona jinsi baadhi ya mawaziri wa kutoka chama chao wanavyojiangalia wenyewe kwa kujikatia zaidi kasungura hako kadogo na hata minofu mingine kuikimbizia kwenye majimbo yao badala ya kuangalia majimbo mengine pia. Hakika, Wabunge wa CCM sasa wanatoa kilio cha kuomba msaada na kilichochanganyika na hasira na hofu ya kupoteza mamlaka ya kuongoza dola ifikapo mwaka 2015. Ndio, kuna wanaokiona chama chao kikielekea kwenye kuzama 2015. Kelele wanazopiga bungeni zimegeuka kama kelele za nyikani, hazisikiki. Wameanza sasa kuwa na ujasiri wa kuzomeana wazi wazi kwenye vikao vyao badala ya kusubiri kuzomewa na wananchi hadharani. Naam, CCM ya sasa inapata tabu hata kwenye kujua namna ya kuitumia misamiati mipya ya kisiasa, maana, kuna wanaojivua gamba, wanaovuliwa magamba na sasa kuna ' wanaojinyambua' magamba wakiwa ndani ya chama- 'Political evolution' ya namna fulani.

Na Mtego wa Zitto Kabwe kwa CCM?

Jana Mbunge Zitto Kabwe ameitega CCM. Ni mtego wa hatari. Saini zile 70 zina maana hii;
- Kama wabunge wa CCM hawatachangamkia kutia sahihi zao zikavuka hata mia na hamsini, basi, kuna ujumbe unaopelekwa kwa umma. Kuwa wabunge wa CCM ni maneno tu, hawana dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi. Wabunge wengi wa CCM hawataiepuka adhabu ya umma inaweza kuwa inawasubiri 2015.
- Kwa wabunge wa CCM kutia sahihi zao na hata Pinda kupigiwa kura ya wabunge kukosa imani nae ina maana pia kuwa wabunge hawana imani na bwana mkubwa aliyemteua Pinda. Busara haiwataki wabunge wa CCM kufikia hapo. Hilo halina maslahi kwa taifa.

Nini kitakachotokea?

Kuna matatu;
Mosi, Mawaziri wale watano wanaotuhumiwa kwa ufisadi na ubadhirifu wa mali ya umma wanaweza kuepusha aibu kwa Serikali kwa wao wenyewe kutangaza kujiuzulu. Ingawa hili ni gumu kufanyika katika nchi hii, lakini, wakati mwingine kuna lazima ya kufanyika- maana, hapo watakuwa wamemnusuru Waziri Mkuu na aliyemteua.

Pili- Likishindikana la kwanza, basi, kabla ya Jumatatu, Waziri Mkuu Pinda awe ameshajiandaa kufanya maamuzi magumu. Kujiuzulu na kulinda heshima yake na ya aliyemteua. Au kutolewe ' Tamko la Serikali' litakalobadili upepo unaovuma sasa bungeni.

Tatu: La kwanza na la pili yaweza yasifanyike, na badala yake. Rais anaweza kuyaona yanayotokea sasa bungeni kama fursa ya kufanya mabadiliko makubwa Serikalini mara akitua Dar kutoka ziara ya Brazil.

Naam, yumkini pale Diamond Jubilee, kabla ya Jumatatu, kuna watakaopewa kazi ya kusafisha ukumbi na kupanga viti tayari kwa Mkuu wa Nchi kusema jambo kubwa kwa taifa kupitia kwa ' Wazee wa Darisalama'.

Tuhuma za Ray kuhusika na kifo cha Kanumba

Baada ya taarifa kuenea kwamba mwigizaji Ray anahusika moja kwa moja na kifo cha mwigizaji marehemu Steven Kanumba, mwigizaji huyo amezungumza kwenye AMPLIFAYA ya CLOUDS FM na Millard Ayo na kusema yafuatayo:

“...nimekuqa nikizisikia sana hizi tuhuma, sio kweli kwa sababu Kanumba ni mdogo wangu wa karibu sana tumetoka mbali sana kimaisha mimi na yeye, nimekua na mazoea ya kuona vitu kila siku vinaandikwa ambapo juzi nilipigiwa simu na kuambiwa nitazame kwenye blog ya U-Turn ambayo anaimiliki huyu dada ambaye simfahamu anaitwa Mange Kimambi”

“...alikuwa ameandika kwamba amepata taarifa kutoka kwa polisi mmoja wa Oysterbay kwamba Ray ndio aliyepiga simu kwa Lulu siku ya kifo cha Kanumba kwa hiyo Lulu ametumika kufanya mauaji bila kujijua, na pia kukawa kuna swali kwamba kwa nini Ray alikua wa kwanza kufika kwa marehemu Kanumba. Mungu ndie anaejua...”

“...kwa hiyo anataka kuwadhihirishia Watanzania kwamba Ray ndiyo anahusika na hicho kifo, baada ya hilo nimeshirikiana na polisi na kushitaki na kufungua kesi ambapo hivi sasa ninapozungumza yupo polisi Oysterbay akihojiwa kwa sababu ameandika kitu ambacho bado kipo ndani ya uchunguzi, hana uhakika nacho sijui Lulu amekamatwa Coco Beach which is not true, sijui hizi habari kaipata wapi...”

“...sasa hii ni kutaka kunivunjia heshima, mimi nafanya kazi ya kuigiza ndio maisha yangu unapoandika kitu kama hicho kwenye internet inafika sehumu kubwa dunia nzima, sasa unategemea watu wanichukuliaje kama sio kunivunjia heshima, kunipotezea mashabiki wangu… nasema hili sitoweza kuliacha, nitalifanyia kazi na nitalifikisha mahakamani ili iwe fundisho, sitolichekea...”

Kwenye sentensi nyingine Ray amesema baadhi ya maoni yaliyotolewa na watu mbalimbali kwenye hiyo habari iliyoandikwa kwenye blogu hiyo, “maoni niliyoyasoma mengine yanamwambia yule dada kwamba anachokiandika kinaweza kum-cost kwenye maisha yake, na nyingine zinasema kwamba tuko tayari kumvamia Ray na kumuua, sasa hichi kitu ni hatari sana kwenye maisha yangu kwa hiyo nimemshitaki polisi na kuandika kwa kusema chochote kitakachonikuta hata nikipigwa jiwe na kuanguka mimi na-deal na huyo mwanamke kwa sababu yeye ndio mtu aliye-publish hivyo vitu watu wanichukulie mimi vinginevyo kabisa tofauti jinsi nilivyo na sihusiki kabisa na hicho kifo, kimsingi maisha yangu yapo hatarini lakini nasema haya ni maisha nitaendelea kuvumilia...”