Monday, June 12

TAARIFA YA KAMATI YA PILI YA KUCHUNGUZA MAKINIKIA ILIYOTOLEWA KWA RAIS MAGUFULI 12 JUNI, 2017

RAIS DKT MAGUFULI APATA PICHA ZA PAMOJA NA VIONGOZI BAADA YA KUPOKEA RIPOTI TA MAKANIKIA IKULU DAR ES SALAAM LEO


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini na vingozi wa vikosi vya Ulinzi na Usalama baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini na vingozi wa vikosi vya Ulinzi na Usalama na baadhi ya wanahabari baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini na viongozi wa dini baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini na wakuu wa Mikoa baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini na viongozi wa vyama vya siasa baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini na wabunge baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini na wazee wa jiji baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini na wawakilishi wa Sekta binafsi baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Dar es salaam baada ya kupokea ripoti yao Ikulu leo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais Mhe Samia Suluhu Hassan, Spika Job Ndugai,  Kaimu Jaji Mkuu Profesa Ibrahim wakiwa katika picha na kamati ya Rais ya pili ya kuchunguza makinikia na mustakabali wa sekta ya madini nchini na wasanii wa Tanzania All stars baada ya kupokea ripoti yao Ikulu Dar es salaam leo.

HOTUBA YA RAIS DKT MAGUFULI BAADA YA KUPOKEA RIPOTI YA KAMATI YA PILI YA MADINI JUNE 12, 2017


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Taarifa ya Kamati ya pili ya Uchunguzi wa Madini yaliyo kwenye makontena yenye mchanga unaosafirishwa nje ya nchi kutoka kwenye machimbo ya madini sehemu mbalimbali hapa nchini kutoka kwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo Profesa Nehemiah Osoro Ikulu jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akionesha Ripoti hiyo ya Kamati ya pili ya Uchunguzi wa Madini yaliyo kwenye makontena yenye mchanga unaosafirishwa nje ya nchi kutoka kwenye machimbo ya madini sehemu mbalimbali hapa nchini mara baada ya kukabidhiwa Ikulu jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan na kulia ni Waziri Mkuu Kassim Majaliwa wakishuhudia.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza mara baada ya kukabidhiwa Ripoti hiyo ya Kamati ya Pili ya Uchunguzi wa Madini Ikulu jijini Dar es Salaam.

SERENGETI, NGORONGORO NA KILIMANJARO SI VIVUTIO PEKEE VINAVYOPATIKANA TANZANIA

kwa mujibu wa issa michuzi blog

Watalii wanaokuja Tanzania na kuelekea moja kwa moja kwenye hifadhi za taifa za Serengeti, Kilimanjaro au Ngorongoro inamaanisha nini? Ni kwamba wanakuwa wamekwishaambiwa kuwa ukifika Tanzania sehemu pekee za kutembelea ni hizo tu? Je tunawezaje kukabiliana na hali hii ambayo kwa namna moja ama nyingine inaweza kufifisha vivutio vilivyopo maeneo mengine nchini kutotembelewa?
Hakuna anayeweza kubisha kwamba sehemu ya Kaskazini mwa Tanzania imebarikiwa kwa kiasi kikubwa kuwa na vivutio visivyopatikana duniani kote. Vivutio kama hifadhi za kitaifa za Serengeti, bonge la Ngorongoro, Mlima Kilimanjaro na hivi karibuni mti mrefu zaidi barani Afrika uligunduliwa.

Tunapenda kukufahamisha kwamba tangu mwaka huu wa 2017 uanze nchi yetu imeshuhudia watu mbalimbali maarufu duniani wakifurika nyanda za Kaskazini wakiwemo Waziri Mkuu mstaafu wa Israel, Bw. Ehud Barak, muigizaji wa filamu kutokea Hollywood nchini Marekani, Will Smith na familia yake.

Kama hiyo haitoshi hazijapita hata wiki mbili tangu aliyekuwa nguli wa kusakata kabumbu nchini Uigereza, David Beckham ambaye aliwahi kuvichezea vilabu vya Manchester United, Real Madrid, LA Galaxy na PSG naye kutembelea hifadhi ya mbuga ya Serengeti akiwa na familia yake.

Huyo hakuwa mchezeji pekee kutokea bara la Ulaya kufanya hivyo kwani nyota anayechezea kwa mkopo katika klabu ya Crystal Palace inayoshiriki ligi kuu ya Uingereza akitokea Liverpool, Mamadou Sakho naye pamoja na mkewe na watoto wake wa kike wawili wameonekana wakifurahi mapumziko yao katika hifadhi ya mbuga ya wanyama ya Serengeti.
Jambo la msingi la kujiuliza hapa ni kwanini watu hao wote mashuhuri pindi tu watuapo uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwl. Nyerere hubadilisha ndege na kuelekea moja kwa moja uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro ambapo kutokea pale ni rahisi kwenda hifadhi za kitaifa za Serengeti, Ngorongoro na Mlima Kilimanjaro?

Tunafahamu kwamba suala la watalii kutembelea sehemu wanazozitaka wanapofika nchini Tanzania ni maamuzi yao na pia huchangiwa na sababu kadhaa kama vile vivutio miundombinu kama vile usafiri, hoteli zenye hadhi na kuvutia lakini pia na hali ya hewa kinaweza kuwa kigezo kingine.

Kwa kuzingatia sababu za miundombinu na huduma bora za malazi na zenye viwango vya kimataifa, hakuna ubishi kwamba nyanda za Kaskazini zimejitahidi kwa kiasi kikubwa kukidhi mahitaji ya watalii. Lakini linapokuja suala la vivutio vya kitalii na hali ya hewa bado Tanzania tumejaaliwa vivutio vya kila aina na hali ya hewa nzuri karibuni kila mikoa ya nchi hii.

Kwa mfano, ukitembelea mikoa ya Magharibi utakutana hifadhi za Gombe, Katavi, Mahale, Rubondo na Saanane. Kwa ukanda wa Mashariki kuna fukwe safi za bahari ya Hindi, visiwa vya Zanzibara, hifadhi ya Saadani, kisiwa cha Kilwa, mapango ya Amboni (Tanga) na Mikindani (Mtwara). Wakati ukienda Kusini mwa Tanzania yapo mengi ya kufurahi na kuyaona katika hifadhi za Kitulo, Mikumi, Ruaha na Udzungwa.
Utajiri wa maliasili unaopatikana katika hifadhi hizo hapo juu ni Dhahiri kwamba nchi ya Tanzania haijabarikiwa sehemu chache pekee. Bali tu ni namna tunavyovitangaza, kuvitolea elimu ya kutosha na kuvipa kipaumbele kwa wageni na watalii kuvitembelea.

Yapo mambo kadhaa ya kujifunza kutokana na ugeni wa watu hao mashuhuri kupendelea kuzuru baadhi ya sehemu tu nchini.

Kwanza kabisa, kuwa na vivutio pekee haitoshi kuwashawishi watalii kuja nchini kuvitembelea bila ya kuvitangaza. Dunia kwa sasa ina takribani zaidi ya nchi 190 na zote hizo zikiwa na vivutio vya kila namna. Watalii hawawezi kutembelea sehemu kama hawajafahamishwa ina mambo gani yatakayowavutia na kushawishika kutoka huko walipo. Hivyo basi badala ya kutegemea watalii na watu mbalimbali kusikia sifa za vivutio tulivyonavyo Tanzania kutoka kwa watu wao wa karibu, serikali na wananchi tunaowajibu wa kuvitangaza vivutio vyetu.
Lakini pia, sekta ya utalii kwa kiasi kikubwa huendena na uwepo wa miundombinu ya kisasa na ya kuvutia itakayowawezesha watalii kuvifikia vivutio na kufarahia muda wao pindi wanapokuwepo huko. Hapa tunazungumzia miundombinu kama vile usafiri na huduma za malazi kitu ambacho mikoa ya Kaskazini imejitahidi kuwekeza kwa kiasi kikubwa. Uwepo wa uwanja wa ndege kimataifa wa Kilimanjaro, barabara na hoteli kadhaa zenye hadhi na viwango vya kimataifa ni vichocheo vikubwa kwa watalii kupenda kutembelea vivutio vya huko.

Hivyo basi kwa kumalizia, bado serikali na wananchi kwa ujumla tunalo jukumu la kuvitangaza na kuvilinda vivutio tulivyonavyo. Kwa kuvitangaza tunaweza kulifanikisha hilo kwa kuvitembelea na kuwajulisha watu wetu wa karibu juu ya mambo yanayopatikana huko. Pongezi kwa serikali kwani siku chache zilizopita katika kuadhimisha siku ya mazingira duniani ilitoa ofa kwa watanzania wote kutembelea hifadhi za mbuga za wanyama bila ya kiingilio chochote kwa siku tatu mfululizo ili kujionea mazingira na maliasili tulizojaaliwa.

JPM: Tumepoteza zaidi ya Sh68 trilioni za kodi


Thamani ya kodi ambayo haikulipwa na kampuni za uchimbaji madini ni kati ya Sh trilioni 68 hadi 108.5.
Hayo yameelezwa na Rais John Magufuli, leo Jumatatu baada ya kukabidhiwa ripoti ya pili ya mchanga wa madini.
Pia Rais amesema anashangazwa na jinsi mawaziri wa sekta za madini na wadau wengine wa sekta hiyo ambavyo hawajawahi kufikiria kuitembelea mashine ya uchenjuaji (smelter) inayotajwa na kampuni za madini.
“Kila siku wanaomba vibali vya kusafiria lakini hawakosei wakaenda kuiangalia mashine hiyo inayochenjua mamchanga yetu,” amesema.
 Tutaendelea kuwajuza yanayojiri Ikulu leo

JPM amtaja Dalaly Kafumu sakata la mchanga wa madini

Rais John Pombe Magufuli (JPM) amesema aliyekuwa Kamishna wa Madini, Dk Dalaly Kafumu alikwenda kujaribu kufanya ujanja ili ripoti ya pili ya mchanga wa madini ibadilishwe lakini hakuweza.
Kafumu kwa sasa ni Mbunge wa Igunga(CCM) ambaye alijiuzulu kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini mapema mwaka huu.
Rais Magufuli, ameyasema hayo leo Jumatatu wakati akipokea ripoti ya pili ya mchanga wa madini Ikulu na kueleza kuwa ameyasoma na kuyakubali mapendekezo yote yaliyotolewa na kamati hiyo.
“Ninawashukuru viongozi wa vyama mbalimbali ambao mmetoa ushirikiano katika hili, hizi fedha ni nyingi sana na zikienda hospitali zinawatibu wote,” amesema.
“ Haya madini hayana vyama.” Aliongeza.

Magufuli aitaka Acacia itubu na kuanza upya


Rais John Magufuli amesema iwapo kampuni ya uchimbaji wa madini ya Acacia ikitubu na kukubali makosa yake, serikali ipo tayari kwa majadiliano lakini kwa sasa hakuna mchanga  wa madini utakaotoka nje ya nchi.
Rais Magufuli ameyasema hayo leo (Jumatatu) Ikulu baada ya kukabidhiwa ripoti ya pili ya mchanga wa madini.
Amewataka Acacia kuomba leseni upya lakini kwa makosa yaliyoonekana hawana budi kuilipa Serikali.
Pia amewataka wanasheria wa nchi hii wasimame pamoja kwani suala hili ni kwa ajili ya maslahi mapana ya taifa hili.
Amemtaka Waziri wa Sheria na Katiba, Profesa Palamagamba Kabudi, aunde timu ya wanasheria waaminifu, wasiokubali kuhongwa na kisha sheria hizo zipelekwe bungeni na zijadiliwe  
“Hata kama kipindi cha bunge kitaongezwa, lakini wanasheria wapitie sheria hizo kifungu kwa kifungu ili mradi lipatikane suluhisho,” amesema.
Ameongeza: “Tukiendelea kukaa kimya tutaliangamiza taifa, tutakuja kujibu mbele za Mungu ‘its so painful, really painful.”
Amesema ukienda maeneo mengi hapa Dar es Salaam, mikoani utaona jinsi Watanzania wanavyoishi katika mateso na hata wakati alipokuwa akipita mikoani kuomba kura za urais aliona mateso ya Watanzania. “Nilifikia wakati nikajiuliza naomba hii kazi ya nini.”