Monday, June 12

JPM: Tumepoteza zaidi ya Sh68 trilioni za kodi


Thamani ya kodi ambayo haikulipwa na kampuni za uchimbaji madini ni kati ya Sh trilioni 68 hadi 108.5.
Hayo yameelezwa na Rais John Magufuli, leo Jumatatu baada ya kukabidhiwa ripoti ya pili ya mchanga wa madini.
Pia Rais amesema anashangazwa na jinsi mawaziri wa sekta za madini na wadau wengine wa sekta hiyo ambavyo hawajawahi kufikiria kuitembelea mashine ya uchenjuaji (smelter) inayotajwa na kampuni za madini.
“Kila siku wanaomba vibali vya kusafiria lakini hawakosei wakaenda kuiangalia mashine hiyo inayochenjua mamchanga yetu,” amesema.
 Tutaendelea kuwajuza yanayojiri Ikulu leo

No comments:

Post a Comment