Monday, June 12

JPM amtaja Dalaly Kafumu sakata la mchanga wa madini

Rais John Pombe Magufuli (JPM) amesema aliyekuwa Kamishna wa Madini, Dk Dalaly Kafumu alikwenda kujaribu kufanya ujanja ili ripoti ya pili ya mchanga wa madini ibadilishwe lakini hakuweza.
Kafumu kwa sasa ni Mbunge wa Igunga(CCM) ambaye alijiuzulu kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini mapema mwaka huu.
Rais Magufuli, ameyasema hayo leo Jumatatu wakati akipokea ripoti ya pili ya mchanga wa madini Ikulu na kueleza kuwa ameyasoma na kuyakubali mapendekezo yote yaliyotolewa na kamati hiyo.
“Ninawashukuru viongozi wa vyama mbalimbali ambao mmetoa ushirikiano katika hili, hizi fedha ni nyingi sana na zikienda hospitali zinawatibu wote,” amesema.
“ Haya madini hayana vyama.” Aliongeza.

No comments:

Post a Comment