Thursday, August 24

SERIKALI YARIDHIA MWEKEZAJI KUMILIKISHWA ARDHI MSOGA


Jonas Kamaleki- MAELEZO.
WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhe. William Lukuvi ameridhia mwekazi kupewa ardhi kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda kijijini Msoga, Wilayani Chalinze, Mkoa wa Pwani.

Waziri Lukuvi amesema kuwa wanakijiji wana uwezo wa kutoa ardhi hadi ekari hamsini tu zaidi ya hapo ni Mhe. Rais mwenye uwezo wa kutoa hati kwa mwekazaji, hivyo alikwenda Msoga kujiridhisha kabla ya kumshauri  Rais kutoa hati kwa mwekezaji.

Aliwauliza wananchi katika mkutano uliofanyika kijijini Msoga kama walikubaliana kumruhusu mwekazaji wa Region Recycling East Africa Limited kujenga kiwanda kijijini hapo, nao wananchi kwa pamoja walisema kuwa ndiyo walitoa ardhi yao kwa ajili ya uwekezezaji huo.

Kiwanda hicho kitakuwa kinatumia betri mbovu za gari na za umeme jua  (Recycling) kama malighafi ya kutengeneza betri nyingine kwa ajili ya matumizi ya magari na mitambo ya umeme jua. Mwekezaji huyo alipewa jumla ya ekari 56 na wanakijiji wa Msoga kwa ajili ya uwekezaji huo.

“Vijiji vilivyopimwa kimji vitaiingizia Serikali mapato na wananchi pia watapata fursa za kupata mikopo kwenye mabenki na kufanya biashara kubwa,”alisema Lukuvi na kuongeza kuwa anazishauri Halmashauri zote nchini kupandisha hadhi vijiji vya namna hiyo.

Kwa upande wake, Mbunge wa Chalinze, Mhe. Ridhiwan Kikwete alimshukuru Mhe. Lukuvi kwa kuridhia umilikishwaji wa ardhi kwa mwekezaji kwani kiwanda hicho kikianza kazi kitatoa fursa mbalimbali zitakazochangia kuinua uchumi wa wakazi wa Msoga na maeneo ya jirani ikiwemo ajira.

Alimwomba Mhe. Lukuvi kupitia wizara yake kuwasaidia katika upimaji wa maeneo ya Chalinze kwani wao hawana uwezo wa kujipimia au kulipia gharama za upimaji.

Hatua za umilikishwaji ardhi kwa mwekezaji huyo, zilianza mwaka 2012 na kukamilika hivi karibuni kwa jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano ambayo imekuwa karibu sana na wananchi kuwatatulia kero na changamoto mbalimbali.

Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi chini ya uongozi wa Mhe. William Lukuvi imetatua migogoro mingi ya ardhi hapa nchini na kuwafanya wananchi waishi kwa Amani katika maeneo yao.

Mwisho



Name of Ministries


Frequency
Percent
Valid Percent
Cumulative Percent
Valid
Ministry of Defence and national Service
6
1.0
1.0
1.0
Ministry of Natural Resources and Tourism
22
3.5
3.5
4.4
Ministry of Lands,Housing and Human Settlements Development
7
1.1
1.1
5.6
Ministry of Works,Transport and Communication
10
1.6
1.6
7.1
State,Prime Minister's Office,Policy,Parliament,labour Employment,Youth and Disabled
14
2.2
2.2
9.4
State,President's Office,Regional Administration and Local Government
11
1.7
1.7
11.1
Ministry of Energy and Minerals
4
.6
.6
11.7
Ministry of Healthy,Community Development,Gender,Elders and Children
4
.6
.6
12.4
ministry of Water and Irrigation
16
2.5
2.5
14.9
State,Vice President's Office,Union and Environment
1
.2
.2
15.1
Ministry of Agriculture,Livestock and Fisheries
6
1.0
1.0
16.0
Ministry of finance and planning
8
1.3
1.3
17.3
Ministry of Education,Science,Technlogy and Vocational Training
2
.3
.3
17.6
TRA
10
1.6
1.6
19.2
BOT
30
4.8
4.8
24.0
HIGH LEARNING INSITUTION
18
2.9
2.9
26.8
TPA
18
2.9
2.9
29.7
TANESCO
49
7.8
7.8
37.5
DAWASCO AND OTHER WATER AUTHORITIES
17
2.7
2.7
40.2
PROFFESIONAL BOARDS
8
1.3
1.3
41.4
TCRA
24
3.8
3.8
45.2
PENSION FUNDS
30
4.8
4.8
50.0
TANROADS
25
4.0
4.0
54.0
OTHER GOVERNMENT AGENCIES
10
1.6
1.6
55.6
TFDA
2
.3
.3
55.9
Councils and Municipals
121
19.2
19.2
75.1
NHIF
1
.2
.2
75.2
PRESIDENT'S OFFICE,PUBLIC SERVICE RECRUITMENT SECRETARIAT
12
1.9
1.9
77.1
TCAA
5
.8
.8
77.9
NECTA
6
1.0
1.0
78.9
TUME YA TAIFA YA UCHAGUZI
6
1.0
1.0
79.8
EWURA
16
2.5
2.5
82.4
TTCL
10
1.6
1.6
84.0
VETA
1
.2
.2
84.1
MSD
14
2.2
2.2
86.3
NBAA
7
1.1
1.1
87.5
TBS
5
.8
.8
88.3
COURT
4
.6
.6
88.9
SUMATRA
8
1.3
1.3
90.2
MUHIMBILI AND OTHER HEALTH RELATED INSTITUTES
6
1.0
1.0
91.1
TEA
1
.2
.2
91.3
NEMC
2
.3
.3
91.6
DART
2
.3
.3
91.9
TCU
2
.3
.3
92.2
TFS(TANZANIA FOREST SERVICE)
18
2.9
2.9
95.1
RAHCO
7
1.1
1.1
96.2
NDC
1
.2
.2
96.3
NIC
2
.3
.3
96.7
TANAPA
1
.2
.2
96.8
GPSA
3
.5
.5
97.3
TEMESA
3
.5
.5
97.8
TIC
4
.6
.6
98.4
WCF
6
1.0
1.0
99.4
PRIME MINISTER OFFICE
1
.2
.2
99.5
TANZANIA TOURIST BOARD
1
.2
.2
99.7
TMA
2
.3
.3
100.0
Total
630
99.8
100.0

Missing
System
1
.2


Total
631
100.0