Thursday, August 3

Kifo cha Msando:Shirika la Haki za Binadamu lataka uchunguzi huru, wazi


Mkurugenzi wa shirika hilo ukanda wa Afrika Mashariki, Pembe ya Afrika na Maziwa Makuu, Muthoni Wanyeki alitoa wito kwa serikali jana kulishughulikia suala hilo kikamilifu pamoja na masuala mengine ikiwa ni pamoja na viongozi na maofisa wa serikali kutoa taarifa fasaha.
Msando, ambaye alikuwa kaimu mkurugenzi wa kitengo cha Tehama, inaaminika aliuawa usiku wa Ijumaa kuamkia Jumamosi na mwili wake ulitupwa katika vichaka eneo la Kikuyu, Kaunti ya Kiambu. Baadaye mwili wake uliokotwa na polisi na kuwekwa katika chumba cha maiti cha Jiji ambako ulitambuliwa Jumatatu.
“Mauaji haya ya kinyama yamepeleka ubaridi hadi kwenye uti wa mgongo wa Wakenya wengi na kuzua dalili za vurugu,” alisema Wanyeki.
Mwanamama huyo alielezea mauaji ya Msando kama tukio la kutisha katika mwaka huu wa uchaguzi lakini alisema siyo tukio pekee lenye uwezekano wa kupandikiza hofu.
“Serikali lazima ichukue hatua madhubuti kutuliza watu na hali hii tete na kuwahakikishia wapigakura kwamba usalama wao ni wa kipaumbele,” alisema.
“Hii ina maana kiundwe chombo huru na madhubuti cha kufanya uchunguzi wa kifo cha Chris Msando na kuwafikisha kortini wote waliohusika.”
Shirika hilo lenye makao yake Uingereza limetoa wito wa chombo huru cha uchunguzi siku mbili baada ya mabalozi wa Marekani na Uingereza kutoa rai kwa serikali kwamba mashirika ya upelelezi ya FBI (Marekani) na Scotland Yard (Uingereza) yanaweza kusaidia katika kazi hiyo.
Aidha, viongozi wa muungano wa upinzani (Nasa) wametoa wito wa kufanyika uchunguzi huru na wameunga mkono mashirika ya FBI na Scotland Yard kuitwa.
Rais Kenyatta
Lakini Rais Uhuru Kenyatta amelitaka Jeshi la Polisi “kuharakisha uchunguzi” wa kifo cha Msando na mwanamke Carol Ngumbu ili kuhakikisha waliohusika wamefikishwa mahakamani.
Kenyatta alisema hayo alipokuwa akihutubia katika mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa 64, jijini Eldoret akiwa na makamu wake William Ruto. Rais alisema ni lazima waliohusika na mauaji hayo wapatikane na kukabiliwa na sheria.
Rais alisema serikali yake “imeshtushwa sana na imesikitishwa” na mauaji ya watu wawili hao. “Chris ni mtu aliyekuwa amejitolea kuitumikia vilivyo nchi na taasisi zake,” alisema katika taarifa ya maandishi juzi.
“Kwa hiyo ni vema kuziacha taasisi kufanya uchunguzi kwa ubora ili kuhakikisha waliohusika na uovu huo wafikishwe kwenye vyombo vya sheria.”
Kenyatta aliwataka Wakenya kujizuia kueneza uvumi unaoelezea sababu za vifo vya watu wawili hao badala yake wawaache wachunguzi kufunua ukweli.
“Uvumi wa kipuuzi kwa wakati huu wa majonzi utasababisha kazi ya wachunguzi kuwa ngumu na inawaongezea tu uchungu kwa wale waliompenda,” ilisema taarifa hiyo.
Pia, Kenyatta aliagiza makamishna wote wa IEBC wapewe ulinzi wa kutosha muda wote kwa wiki nzima hadi ufanyike Uchaguzi Mkuu. “Wagombea wote wa urais na wagombea wenza wao pia wanahitaji ulinzi ili kuzima kisingizio chochote cha uchaguzi kuahirishwa,” alisema wakati wa kampeni za Jubilee mjini Eldoret, Kaunti ya Uasin Gishu.
Rais alisema hayo huku ikiwa ni siku kadhaa tangu boma la Naibu wake, William Ruto livamiwe na kuzua vita vya risasi za masaa 18, mvamizi

Kinachosababisha watoto kuzaliwa wameungana hiki hapa




Kutotibu ugonjwa wa malaria wakati wa ujauzito, matumizi ya vyakula na vinywaji visivyo salama hasa vyenye gesi na tindikali, ni chanzo cha kuzaa watoto wenye maumbile tofauti ikiwamo pacha walioungana.
Vitu hivyo vimetajwa kuwa sababu ambazo huvuruga mfumo wa utengenezwaji wa viungo kipindi ambacho mtoto huanza kukua tumboni.
Hayo yalielezwa jana na daktari bingwa wa upasuaji wa watoto kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Zaituni Bokhari alipokuwa akitoa majibu ya vipimo vya pacha wa kike waliozaliwa hivi karibuni mkoani Morogoro wakiwa wameungana.
Watoto hao walizaliwa katika Hospitali ya Misheni ya Berega, Julai 21.
Dk Bokhari alisema hakuna sababu maalumu mpaka sasa, lakini kuna vitu ambavyo husababisha kujifungua mtoto ambaye si wa kawaida.
“Mama akiwa mjamzito anatakiwa kuhudhuria kliniki mapema kwani kuna maelekezo kuhusu anapaswa ale nini ambacho kitamjenga mtoto, kama vyakula vyenye calcium, protini, atapewa dawa ambazo zitakaza misuli ya mtoto, folic acid zinasaidia kumjenga mtoto akiwa bado tumboni,” alisema na kuongeza kuwa kuna dawa ambazo huzuia maambukizi ya watoto wakiwa tumboni kwani wapo wanaozaliwa wakiwa na malaria.
“Pia, kujifungua katika umri mkubwa, kula vyakula visivyo salama, vinywaji visivyo salama vyenye gesi na tindikali, vyote vinaweza kusababisha kupata shida, lakini wakati mwingine ni matatizo ya kurithi,” alisema Dk Bokhari.
Namna pacha walivyoungana
Akitoa majibu ya vipimo kuhusu pacha hao, Dk Bokhari alisema watoto hao wameungana sehemu ya kifua na tumbo na vipimo vya CT Scan vinaonyesha kuwa kuna baadhi ya viungo vimeshikana.
“Tulipenda pia kujua je, mishipa ya damu wanashirikiana? Imetusaidia kujua kwamba kila mmoja ana mfumo wake, mbali na vipimo vya X Ray, tukaangalia full blood picture bahati nzuri ikaonyesha upande wa damu hakuna shida, wingi wa damu ni mzuri wana damu zaidi ya 12 kwa wao siyo mbaya,” alisema Dk Bokhari.
Hata hivyo, alisema majibu ya CT Scan ya tumbo na kifua yalionyesha kuna baadhi ya viungo wanashirikiana ikiwamo ini na katika moyo kuna chemba nyingi za milango wanazoshirikiana, pia majibu yaliyotokana na kipimo cha ECO yameonyesha kuna muungano katika moyo.
ECO ni kipimo ambacho kinaangalia hali ya moyo kama uko sawa au una tatizo lolote.
“Kutokana na jinsi walivyokaa kuona moyo ilikuwa ngumu kwenye kipimo cha ECO. Wakashauri tufanye kipimo cha ST Scan ya moyo pekee na hivyo kipimo kwa sasa bado hakijafanywa,” alisema.
Kuhusu afya za watoto hao alisema wanaendelea kuangaliwa kwa ukaribu wodini walipo na wanapewa maziwa ya mama kupitia mpira.
Kutenganishwa miezi sita ijayo
Kuhusu kutenganishwa, Dk Bokhari alisema kutokana na majibu hayo kazi hiyo inaweza kufanywa baada ya miezi sita ijayo.
Alisema kwa sasa wanachokifanya ni kuhakikisha wanakuwa na afya njema kwa kumpa mama Rebecca Mwendi lishe zote zinazotakiwa ili aweze kutoa maziwa bora kwa watoto wake.
“Kwa sasa mama yupo na watoto anakaa katika chumba cha ndani kilichopo ICU, amepumzishwa huko karibu na watoto wake anakula vizuri na maziwa yanatoka vizuri na watoto wanakula vizuri, japokuwa aliathirika kisaikolojia lakini kwa sasa yupo vizuri baada ya tiba aliyopewa na wataalamu wa saikolojia,” alisema.
Alisema awali, watoto hao waliozaliwa na uzito wa kilo 4.270 walikutwa na maambukizi kwenye kitovu na mmoja alikuwa hapumui vizuri na kwamba walipofika walianzishiwa dawa ya antibiotic ya mishipa kwa ajili ya kusafisha kitovu chao kila siku. Alisema mwingine alikuwa ameumia paja wakati wa kuzaliwa na baada ya kipimo cha X Ray wataalamu wa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) walimtibu.
Upasuaji utakuwaje?
Kuhusu mipango ya upasuaji hapo baadaye, Dk Bokhari alisema kutakuwa na wataalamu wa upasuaji wa watoto kutoka vitengo mbalimbali kutokana na namna walivyoungana na kwamba kazi hiyo itachukua saa nyingi hivyo lazima kila kitu kiwekwe sawa hasa itakapofika kutenganisha ini na moyo, wataalamu zaidi wataongezeka.
“Ni upasuaji ambao tutashirikiana na wataalamu wengi wa aina mbalimbali, madaktari bingwa wa upasuaji wa watoto katika kifua na moyo lakini pia wakati wa kuwatenganisha kuna ngozi inayofunika viungo vya ndani iko ndogo lazima itafutwe, hivyo madaktari bingwa wa upasuaji wa kurekebisha maumbile lazima wawepo,” alisema.

Mmiliki wa Ngurdoto kuzikwa nje ya hoteli yake


Mfanyabiashara maarufu ambaye pia ni mmiliki wa hoteli za kitalii nchini,Maleu Mrema anatarajiwa kuzikwa katika eneo la hoteli Yake ya kitalii ya Ngurdoto iliyoko nje kidogo ya jiji la Arusha Agosti 9 .
Mrema amefariki hivi karibuni akiwa kwenye matibabu nchini Afrika Kusini katika hospitali ya City garden iliyoko katika mji wa Johannesburg .
Akizungumza na waandishi wa habari  msemaji wa familia Vincent Laswai amesema kwamba baada ya vikao mfululizo vya familia wameafikiana marehemu azikwe katika eneo la hoteli yake ya Ngurdoto 
Awali taarifa zilienea kwamba mwili wa marehemu utasafirishwa kwenda wilayani Rombo mkoani Kilimanjaro ambako alikozaliwa lakini taarifa hizo zimekanushwa na msemaji hiyo wa familia.
Laswai amesema kwamba mwili wa marehemu unatarajia kuwasili Agosti 7 mwaka huu kutoka nchini Afrika Kusini ambapo utapokelewa katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).
Amesema kwamba baadhi ya wanafamilia,ndugu ,Jamaa Na marafiki watakwenda kuupokea mwili huo katika uwanja wa ndege ambapo familia imetoa usafiri maalum kwa wale watakaoshiriki.
Naibu Waziri wa mawasiliano nchini na Mbunge mstaafu wa jimbo la Arumeru Mashariki,Goodluck Ole Medeye alifika nyumbani kwa marehemu kutoa salamu za pole.
 Medeye amesema  marehemu  alikuwa ni mbunifu ambaye alitumia uwezo wake kusaidia ajira za vijana mbalimbali nchini.

Likizo ya uzazi kwa kina baba yazua mjadala


Hatua ya Serikali kwamba inaangalia uwezekano wa kufuta likizo ya uzazi inayotolewa kwa baba, imeibua mjadala huku makundi ya haki za binadamu na wazazi wakitaka iendelee kutolewa kutokana na umuhimu wake.
Serikali imesema kuwa inafanya uchunguzi ili kujiridhisha kabla ya kuchukua hatua ya kuifuta au kuiacha baada ya kuwapo madai kuwa baadhi ya kina baba wanaitumia vibaya kwa kwenda baa au katika shughuli nyingine.
Kauli hiyo ilitolewa juzi na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati akifungua maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji duniani.
Hata hivyo, baadhi ya wananchi waliozungumza na gazeti hili jana kuhusu hilo, walisema Serikali haipaswi kuifuta na badala yake iwaelimishe kina baba umuhimu wa kushirikiana na mama kumlea mtoto mchanga.
“Sidhani kama kuna haja ya kuifuta na jambo la muhimu linalopaswa kufanywa sasa ni Serikali kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kuelezea umuhimu wa likizo ya uzazi kwa sababu familia zetu nyingi zimetoka katika makuzi yaliyotofautiana,” alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Sheria na Haki na Binadamu(LHRC), Dk Hellen Kijo- Bisimba.
Mtetezi huyo wa haki za binadamu alisema ni kweli baadhi ya kina baba hawakai na wake zao, lakini suala hilo limechangiwa na mambo mengi ikiwamo mila na utamaduni hivyo kuna umuhimu wa kutoa elimu kwa wahusika.
“Katika baadhi ya familia unaweza kukuta baba akitaka kukaa nyumbani kulea mtoto anafukuzwa kwa hisia kuwa hilo siyo jukumu lake au anataka kumtumikisha mke wake, hivyo njia pekee ya kuondokana na tatizo hilo ni kuendelea kuwapa elimu,” alisema.
Alitaka kina baba waruhusiwe kwenda wodini kushuhudia wake zao wakati wakijifungua hali ambayo itawapa picha halisi kutambua namna mtoto anavyopatikana mbali ya ilivyo sasa wamekuwa watu wa kuhisi tu.
“Hapa mimi ni mwajiri mara zote natoa likizo kwa waajiriwa wangu wakati wake zao wakijifungua na wamekuwa wakitoa msaada mkubwa na ndiyo maana nasisitiza sioni hoja ya kutaka kufuta likizo hii kwani ni ndogo,” alisema.
Hoja ya kupinga kufutwa kwa likizo hiyo pia iliungwa mkono na Hungwi Maliatabu wa mkoani Mwanza aliyejitambulisha kuwa mzazi wa watoto watatu. Mzazi huyo ambaye ni mwalimu wa sekondari alisema Serikali inapaswa kuwamulika wajanja wachache wanaotumia likizo ya uzazi kwa shughuli nyingine na siyo kuifuta.
Alisema likizo hiyo inatoa fursa kwa wazazi wote wawili kufurahia ujio wa mwanafamilia mpya, huku baba akitoa msaada wa kwenda sokoni kusaka mahitaji na kumsaidia mama katika mambo mengine muhimu.
Mama wa watoto watatu aliyejitambulisha kwa jina la Anna Maria alisema wazo la Serikali kuanza uchunguzi kuhusu matumizi mabaya ya likizo hiyo ni jema kwani litasaidia kubaini ukweli, “Iwapo Serikali itabaini kuwa likizo hiyo inatumiwa kinyume na makusudio yake napendekeza ifutwe.”
Alidai kuwa mama anapotoka kujifungua anahitaji mapenzi ya karibu kutoka kwa baba ili kuweza kuijenga afya yake, lakini kuna baadhi ya wazazi licha ya kupewa likizo hiyo hawataki kuwa karibu na wake zao.

JPM ameiagiza JKT kurejesha ardhi kwa wanakijiji baada ya kushindwa kuiendeleza


Rais John Magufuli ameagiza Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kurejesha eneo la eka 50 walilopewa na Kijiji cha Mkata, baada ya kushindwa kuliendeleza kwa miaka saba.
Rais ameagiza hatua hiyo ichukuliwe leo Alhamisi, Agosti 3 wakati alipokuwa akizungumza na wananchi wa Mkata akiwa njiani kuelekea mkoani Tanga, ambapo alimwita Mkuu wa JKT wa eneo hilo na kumhoji kuhusu kuendeleza eneo hilo.
“Hili eneo tangu mmepewa ni miaka mingapi sasa? Mliomba ili mjenge muwekeze kwa kujenga kiwanda, lakini mmeshindwa sasa leo hii mrejeshe kwa wananchi ili waweze kumpa hata mwekezaji mwingine,” ameagiza Rais Magufuli na kushangiliwa na wananchi.
Amemweleza mkuu huyo wa JKT kwamba wakajenge kiwanda hicho kwenye kambi yao kwa kuwa wana eneo kubwa ambalo linatosha pia kwa uwekezaji huo.
Awali aliwataka wananchi hao kuwa na subira kuhusu ujenzi wa hospitali katika eneo hilo, kwa kuwa kuna shaka kwamba Sh500 milioni zilizotolewa kwa awamu ya kwanza zilitafunwa, hivyo kabla ya kuleta nyingine wanapaswa kujiridhisha na matumizi yaliyofanywa.
Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu alipopewa nafasi ya kulitolea ufafanuzi jambo hilo amesema wanaunda kamati ambayo itachunguza matumizi ya fedha hizo ndipo waweze kuruhusu fedha zingine zipelekwe ili kuendeleza mradi huo.
Rais Magufuli yupo safarini ambapo Agosti 5 atakutana na Rais Yoweri Kaguta Museveni  kwa ajili ya kuweka jiwe la msingi la Mradi wa bomba la kusafirisha mafuta Hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.

Kodi ya Acacia yapungua asilimia 45


Kodi ya huduma inayotolewa na Mgodi wa Dhahabu wa Acacia Bulyanhulu kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’wale mkoani Geita imepungua kwa zaidi ya asilimia 45 kutokana na Serikali kuzuia usafirishaji wa mchanga (makinikia) kwenda nje ya nchi.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Carlos, Gwamagobe amesema kupungua kwa mapato yatolewayo na Acacia itaathiri bajeti kwasababu  wanategemea mwaka wa fedha 2017/18 kukusanya zaidi ya Sh800 milioni kama kodi ya huduma kutoka katika mgodi huo.
“Kushuka kwa mapato haya yataathiri bajeti yetu kwakuwa kuna miradi haitatekelezwa mwaka jana tulizielekeza kwenye sekta ya elimu sasa inabidi juhudi za makusudi zifanyike fedha hizi zilikua zikitusaidia sana kwenye miradi ya maendeleo na miradi ya kijamii,”amesema Gwamagobe.

Amesema halmashauri hiyo imefanikiwa kujenga madarasa 12 ya shule ya msingi, manane ya shule za sekondari na kujenga hosteli ya Shule ya Sekondari Kakola pamoja na kujenga ghala la kuhifadhia chakula.

Mkuu wa Wilaya ya Nyang’wale, Hamimu Buyama amesema kodi ya huduma inayotolewa na Acacia imesadia kusukuma maendeleo ya halmashauri hiyo na kusema katika maendeleo lazima ziwepo changamoto kama zilivyowakuta Acacia sasa.

Amesema suala la makinikia limekua kikwazo kwa kampuni lakini pia kwa halmashauri zinazotegemea kodi ya huduma kutokana na mapato kushuka na kusema anaimani suala hilo litafika mwisho mwema na wao kuendelea kufanya kazi kama ilivyokuwa awali.

Akikabidhi hundi kwa uongozi wa Wilaya ya Nyang’wale Meneja mkuu wa mgodi wa dhahabu wa Acacia Bulyanhulu, Grahama Crew amesema kwa kipindi cha miezi sita iliyopita  kodi ya ushuru wa huduma ni zaidi ya Sh687 milion ambazo zimegawanya katika Halmashauri ya Msalala iliyopata asilimia 67 na Nyang’wale iliyopata asilimia 33.

Amesema kuanzia mwaka 2000 hadi sasa mgodi wa dhahabu wa Bulyanhulu umelipa zaidi ya Sh10.2 bilioni kama kodi ya huduma katika maeneo wanayofanya kazi ambapo amesema ni matarajio yao kuendelea kuimarisha sekta ya viwanda kwenye uchimbaji wa madini katika Wilaya ya Nyang’wale.

Akizungumza katika makabidhiano hayo mbunge wa Nyang’wale, Hussein Nassoro amesema wananchi wa Nyang’wale wanauhusiano mzuri na kampuni, lakini bado wanamahitaji makubwa.

Amesema wilaya hiyo bado iko nyuma katika sekta ya elimu, afya na miundombinu ya barabara na kuiomba kampuni hiyo kuendelea kuisaidia huduma za kijamii kwa wananchi ili waweze kuona faida ya uwekezaji katika maeneo yao.

Uhamiaji wamsafisha mgombea TFF

Msemaji Mkuu Idara ya Uhamiaji, Ally Mtanda

Msemaji Mkuu Idara ya Uhamiaji, Ally Mtanda akifafanua swala hilo mbele ya wanahabari mapema leo Jijini Dar es salaam 
Idara ya Uhamiaji imetoa ufafanuzi kuhusu uraia wa mgombea wa urais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia na kuthibitisha kuwa ni MTanzania.
Karia aliwekewa pingamizi na mmoja wa wagombea wa nafasi hiyo kwa hoja ya kutilia shaka uraia wake.
Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Ally Mtanda amesema ofisi yake imechunguza na kuthibitisha kuwa Karia alizaliwa nchini na mama yake ni Mtanzania.
Hata hivyo, Mtanda amesema kuwa ni kweli kuwa Karia baba yake ni msomali na alikuwa pia na uraia wa Somalia lakini alishaukana.
"Kwa msingi huo, Karia ni raia wa Tanzania kwa kuzaliwa chini ya kifungu cha 5(1) na (2) cha sheria ya uraia. Na wakati huo huo akiwa raia wa Somalia wa kurithi.
"Ni hitaji la kisheria chini ya kifungu cha 7(1), pale mtu anapokuwa na uraia wa nchi mbili kuukana uraia mmoja pale anapofikisha miaka 18, hatua ambayo Karia alitekeleza na kuthibitishwa," amesema Mtanda.

Wataka kampeni ya ‘Baki Magufuli’ ipigwe ‘stop’


Serikali imeombwa kukomesha kampeni mbalimbali zinazoanzishwa ikiwamo ya 'Baki Magufuli' ili kuondoa sintofahamu iliyopo kwamba wenye kampeni hizo wanatumwa na Rais John Magufuli.
Hayo yamesemwa leo Alhamisi Agosti 3 na Shirika Lisilo la Kiserikali la Vijana na Wanawake (Tafeyoco) wakati wakizungumza na wanahabari kuhusu  hali ya utawala bora na demokrasia inayoendelea nchini.
Mwenyekiti wa Tafeyoco, Elvice Makumbo amesema kampeni hizo siyo muda wake kwa sasa kwani zinatachochea kuzalisha kwa kampeni nyingine hali itakayoleta mvurugano nchini.
"Tukiwaacha hawa wenye kampeni ya 'Baki Magufuli' watazaliwa wengine wenye kampeni ya 'Ondoa Magufuli' madarakani na wao watataka kuisambaza kampeni yao," amesema Makumbo.
Makumbo amesema ni wakati muafaka kwa Serikali kupiga marufuku kampeni hizo, kwani Tanzania inaongozwa kwa Katiba inayoeleza awamu ya kwanza ya rais ni vipindi vitano baada ya hapo uchaguzi mkuu mwingine unaitishwa.
Amesema Rais Magufuli anafanya kazi kubwa kuiongoza nchi na kwamba haitaji ‘tochi’ kupima uwezo wake hivyo kuanzisha kampeni za yeye kubaki ni kutengeneza chuki  kati yake na Watanzania ambao wanaikubali kazi yake.
Mbali na hilo, Makumbo amewataka viongozi wa vyama siasa nchini kuacha tabia ya kuwatumia vijana kuendeleza siasa katika mitandao ya kijamii, kwani baadhi ya vijana wanatumia nafasi hiyo kuandika habari za uchochezi dhidi ya Serikali.

RAIS DKT MAGUFULI ATOA POLE KATIKA MSIBA WA MHADHIRI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM DKT STEPHEN JUMA MDACHI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapa pole wana familia wa Marehemu Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu ambaye alikuwa ni mhadhiri katikl idara ya Kemia, ameacha mjane na watoto watatu.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapa pole wana 
familia wa Marehemu Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu ambaye alikuwa ni mhadhiri katikl idara ya Kemia, ameacha mjane na watoto watatu.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapa pole wana 
familia wa Marehemu Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu ambaye alikuwa ni mhadhiri katikl idara ya Kemia, ameacha mjane na watoto watatu.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka sini katika kitabu cha maombolezi nyumbani kwa Marehemu Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu ambaye alikuwa ni mhadhiri katikl idara ya Kemia, ameacha mjane na watoto watatu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimfariji Mama Mary Mdachi, mjane wa Marehemu  Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Picha na IKULU

DC HAPI AMALIZA MGOGORO SUGU WA ARDHI NAKASANGWE


  Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Salum Hapi ametoa miezi mitatu kwa kampuni ya upimaji wa ardhi ya Afro Map kuhakikisha wanamaliza upimaji wa ardhi kwa eneo la Nakelekwe, Mtaa wa Nakasangwe Kata ya Wazo ambalo limekuwa na mgogoro wa ardhi kwa muda wa miaka 13 tangu mwaka 2004 baina ya wakazi wa eneo hilo na wamiliki wa mashamba.

DC Hapi amesema chanzo cha mgogoro wa eneo hilo ni kutokupimwa, hivyo atahakikisha maeneo yote katika wilaya yake yanapimwa ili migogoro ya ardhi iwe historia kwa wanakinondoni.

Vilevile DC Hapi ameeleza kuwa serikali haiwezi kuacha wakazi 3900 wakipoteza maeneo kisa uwepo wa mashamba, ndiyo maana ameamua kuzikutanisha pande zote mbili ili waweze kutatua migogoro hiyo, na upimaji utakapofanyika vitapatikana viwanja 6000 ambapo pande zote mbili zitanufaika bila kubagua na maeneo mengine yatatengwa kwaajili ya huduma za jamii ikiwemo zahanati, shule na miundombinu ya barabara.

DC Hapi ameongeza kuwa wananchi wa maeneo hayo wasiyauze maeneo hayo mpaka upimaji utakapo fanyika, na wale ambao maeneo yao hayo kuwa katika mgogoro wafanye hivyohivyo.

Pia DC Hapi amewataka viongozi wa kisiasa kuacha kuchochea migogoro ya ardhi kwa maslahi yao ya kisiasa na endapo wakiendelea kufanya hivyo atachukua hatua stahiki dhidi yao.

Kwa upande wao wakazi wa eneo hilo na wamiliki wa mashamba wamepongeza jitihada za serikali kwa kutatua mgogoro huo na kuhaidi kufuata utaratibu ulioelekezwa.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi leo amefanya mkutano wa hadhara na wananchi wa maeneo ya Nakasangwe, Nakalekwa na kuwapa ujumbe kuwa mgogoro wa ardhi uliodumu eneo hilo kwa miaka 13 kiasi cha kusababisha vifo sasa suluhu yake imepatikana.

Hapi amesema kuwa ikiwa ni muendelezo wa utatuzi wa migogoro ya ardhi wilayani Kinondoni ofisi yake ilizikutanisha pande mbili za wenye mashamba na wakazi ambazo kwa miaka kadhaa zimekua kwenye mgogoro mkubwa na kufanya nao mazungumzo yaliyoweka msingi mzuri wa kumaliza mgogoro huo.

Hapi amewahakikishia wananchi hao kutokuwa na wasiwasi na kwamba serikali wilayani Kinondoni imeamua kutumia falsafa ya

"pata kidogo poteza kidogo" (win win)ili kumaliza mgogoro huo baina ya pande mbili na kurejesha hali ya amani kayila eneo hilo.

"Tumeamua sasa eneo hili lote lipimwe viwanja, ili wakazi wote mliohakikiwa kila mmoja apate kipande cha ardhi cha kuishi na familia yake na viwanja vinavyobaki wapate wenye mashamba. Hii ndiyo njia pekee ya kuweza kuwafanya muishi kwa amani katika mji uliopimwa na kupangwa vizuri."Alisema DC Hapi

Aidha, Hapi aliwaeleza wananchi hao kuwa katika eneo hilo zaidi ya viwanja 6000 vitapatikana na hivyo kuwatoa shaka kuwa wakazi wote zaidi ya 3000 waliohakikiwa kila mmoja atapata ardhi iliyopimwa huku wenye mashamba nao wakipata viwanja vitakavyobakia ili waweze kuviendeleza au kuviuza vikiwa na hati miliki.

DC Hapi amesema kazi ya upimaji wa ardhi katika eneo hilo inatarajiwa kuanza haraka na kumalizika ndani ya kipindi cha miezi mitatu chini ya kampuni ya Afro Map ambayo pande mbili zimeichagua kufanye kazi hiyo.

"Nawapa kampuni hii miezi mitatu tu, kazi ya upimaji iwe imekamilika eneo hili ili wananchi wangu waishi kwa amani wakijua serikali yao ipo kuwasaidia." Alisema DC.

Mgogoro wa Nakasangwe ulianza mwaka 2004 na hivyo kudumu kwa miaka 13 kipindi ambacho kilitawaliwa na chuki, uhasama na uadui mkubwa baina ya wenye mashamba na wananchi waliovamia mashamba hayo. Watu kadhaa walipoteza maisha katika mgogoro huo.

Wananchi wote wanaounda pande mbili za mgogoro wamemshukuru DC Hapi na kushikana mikono kama ishara ya mwisho wa mgogoro huo na mwanzo mpya.
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi akizungumza jana mbele ya wananchi  wa Mtaa wa Nasarangwe, Kata ya Wazo   juu   yakampuni ya Afro Map imepewa kazi upimaji wa viwanja  itakayokamilika  ndani ya miezi mitatu badala ya miezi nne iliyokuwa ikifahamika hapo awali.
 Diwani wa Kata ya Wazo Joel Mwakalebela akizungumza leo na wananchi wa juu ya kutoa ushirikiano katika kuchangia gharama za upimaji wa viwanja ili zoezi hilo lisikwame.
 Sehemu ya wananchi wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Ally Hapi

BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA-AfDB YAKUNWA NA VIWANGO VYA UJENZI WA BARABARA MTWARA



Benny Mwaipaja, WFM, Mtwara

BENKI ya Maendeleo ya Afrika (AfDB), imeelezea kuridhishwa na kasi pamoja na viwango vya miradi ya ujenzi ya barabara inayofadhiliwa na benki hiyo katika Ukanda wa Kusini, na kuahidi kuendelea kushirikiana na Serikali ya Awamu ya Tano ili kuchochea ukuaji wa uchumi wa Taifa na wananchi wake.

Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo anayesimamia Kanda wa Afrika Mashariki, Dkt. Nyamajeje Weggoro, baada ya kutembelea na kukagua barabara ya Tunduru-Nangaka-Mtambaswala, mkoani Mtwara, yenye urefu wa kilometa 202.2.

Barabara hiyo yenye vipande vitatu imejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 180 kupitia ufadhili wa benki hiyo kwa kushirikiana na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) na Serikali ya Tanzania. 

Dkt. Weggoro amesema kuwa barabara hiyo ambayo upande mmoja inaunganisha Tanzania na Msumbiji, itachochea maendeleo ya wananchi kutoka pande hizo mbili kwa kusafirisha watu na bidhaa kwa urahisi zaidi.

“Nimeona mabadiliko makubwa sana, si tu kwa barabara, lakini maisha ya watu, mabadiliko ambayo ni dhahiri yanatokana na hii miradi ya barabara ambayo imefungua fursa nyingi za maendeleo, watu wanafanyabiashara lakini pia wanatembeleana!” alisema Dkt. Weggoro.

Alitoa wito kwa Watanzania kuchangamkia fursa ya uwepo wa barabara hizo kujiletea maendeleo kwa kufanyabiashara hivyo kujikwamua kiuchumi.

Mhandisi Heldaus Jerome kutoka Wakala wa Barabara -Tanroads, Makao Makuu, alisema kuwa barabara hiyo ya Tunduru-Mangaka-Mtambaswala, ina vipande vitatu, kutoka Mangaka – Nakapanya (km 70.5), Nakapanya – Tunduru (66.5) na Mangaka – Mtambaswala (km 65.5)

Alifafanua kuwa gharama za ujenzi wa mradi huo, kiasi cha Dola milioni 210, kimetolewa na AfDB (64.79%), Shirika la Maendeleo la Japan-JICA (32.83%) na Serikali ya Tanzania (2.38%) na kwamba Wadau hao pia wanafadhili ujenzi wa barabara kutoka Dodoma-Babati yenye urefu wa kilometa 180.53.

Baadhi ya wakazi wa mji wa Mangaka wilayani Masasi mkoani Mtwara, wameishukuru Serikali kwa kufanikisha ujenzi wa barabara hiyo muhimu kwa uchumi na maisha yao kwa ujumla kwa kurahisisha usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo ndani na nje ya nchi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Kilimanihewa, Bw. Abbas Muhidin Mwira, alisema kuwa maeneo ya Mangaka yamechangamka kibiashara na vijana wengi wamejiajiri wenyewe kwa kufanyabiashara zinazowaingizia kipato huku huduma za usafiri zikiboreshwa baada ya mabasi ya abiria yaendayo mikoani pamoja na malori yanayobeba saruji kutoka Kiwanda cha Saruji cha Dangote-Mtwara kuanza kupita njia hiyo na kusisimua biashara zao.

RAIS DKT MAGUFULI ATOA POLE KATIKA MSIBA WA MHADHIRI WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM DKT STEPHEN JUMA MDACHI

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapa pole wana familia wa Marehemu Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu ambaye alikuwa ni mhadhiri katikl idara ya Kemia, ameacha mjane na watoto watatu.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapa pole wana 
familia wa Marehemu Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu ambaye alikuwa ni mhadhiri katikl idara ya Kemia, ameacha mjane na watoto watatu.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwapa pole wana 
familia wa Marehemu Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu ambaye alikuwa ni mhadhiri katikl idara ya Kemia, ameacha mjane na watoto watatu.
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiweka sini katika kitabu cha maombolezi nyumbani kwa Marehemu Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Marehemu ambaye alikuwa ni mhadhiri katikl idara ya Kemia, ameacha mjane na watoto watatu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimfariji Mama Mary Mdachi, mjane wa Marehemu  Dkt. Stephen Juma Mdachi aliyefariki Jumanne Agosti 1, 2017 katika hospitali ya Tumaini jijini Dar es salaam alikokuwa akipatiwa matibabu. Picha na IKULU

BOMBA LA MAFUTA TANGA: WANANCHI 365 KUFIDIWA CHONGOLEANI


Wananchi 365 wa kijiji cha Chongoleani watafidiwa shilingi bilioni 3,035 kwa ajili ya kutoa maeneo yao, ili kupisha ujenzi wa bomba la mafuta linalojengwa kutoka Hoima nchini Uganda mpaka Tanga.

Hayo yamesemwa na Meneja Mawasiliano wa Shirika la Usimamizi wa Bandari Tanzania TPATanga, Bibi Janeth Rwuzangi katika mahojiano maalum na Idara ya Habari (MAELEZO) leo.

Bi Ruzangi amesema kuwa kwa hapa Chongoleani mradi una ukubwa wa hekta 200 zikiwemo hekta 100 zitakazotumiwa kuweka miundombinu ya mafuta ghafi. Hekta 100 zilizosalia zitatumika kwa ajili ya shughuli za TPA) kuwekeza miundombinu ya kupokea mafuta yaliyosafishwa. Vile vile eneo hili limezingatia maendeleo endelevu ya biashara ya mafuta na gesi katika siku zijazo.

Aliongeza kuwa TPA itakuwa na wajibu wa kuhudumia meli, kuhakikisha usalama wa bidhaa, vyombo na watu pamoja na kusimamia masuala ya afya bandarini. Aidha, Majukumu la TPA yanatarijiwakujikita katika shughuli za uendeshaji wa majini ikiwemo kuwa na vyombo na boti maalumu kwa ajili ya kuongozea meli wakati wa kuingia na kutoka kwenye gati la mafuta ghafi.

Akitoa ufafanuzi, Bi Ruzangi amesema vile vile, TPA ina jukumu la kuhakikisha inahudumia shehena ya vifaa vyote vya ujenzi katika Bandari ya Tanga kwa kushirikiana na Bandari Kuu ya Dar es Salaam. Shughuli nyingine ni pamoja na ulinzi wa miundombinu ya majini pamoja na usalama wa eneo la Bandari ambalo limegawanyika katika sehemu kuu mbili; ardhini kwenye gati la mafuta na majini kwenye lango la kuingilia meli na nangani.

Kwa upande wa ajira za TPA Ruzangi amesemawafanyakazi ambao wataajiriwa ni pamoja na mabaharia, wahandisi, mafundi, wahasibu, wachumi, watakwimu, vibarua mbalimbali kwa ajili ya nguvu kazi n.k. Sehemu ya wafanyakazi hawa watatokana na waliopo sasa kwenye Bandari watakaopangiwa kazi hizo. Hata hivyo TPA inatarajia kuajiri wengine ambao watalazimika kufanya kazi hizo kulingana na taratibu za ajira za TPA.

Pamoja na kuwa na bomba la mafuta, kijiji cha Chongoleani kitafaidika na ujenzi wa barabara ya kilometa 8 itakayounganisha bandari na barabara kuu ya Horohoro – Tanga, ambapo kwa kiasi kikubwa itainua uchumi wa wananchi wanaoishi maeneo hayo kusafirisha mazao, samaki na bidhaa nyingine kwa urahisi.

Akifafanua uwekaji wa jiwe la msingi Ruzangi amesemakuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, John Pombe Magufuli na Mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni wanatarajia kuweka jiwe la msingi la Mradi wa Bomba la Mafuta tarehe 05 Agosti 2017.

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Chongoleani, Bw. Mbwana Nondo amesema; “Kwa moyo wa dhati kabisa, naomba nimshukuru sana sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli kwa kutujali wananchi wake na kutuletea neema ya Mradi wa Bomba la Mafuta, katika maisha yetu wanachongoleani, hatutaweza kumsahau kwa kizazi hiki kinachoshuhudia mradi huu na vizazi vijavyo”.

Nondo alisema kuwa anamuhakikishia Mhe. Rais kuwa kuwa wote watakaopata fursa kwenye mradi wa Bomba la Mafuta, watafanyakazi kwa bidii ili kujiletea maendeleo ya mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Bomba la Mafuta la kutoka Hoima Uganda mpaka Tanga Chongoleani lina urefu wa Kilometa 1445 ambapo kwa upande wa Tanzania itakuwa na jumla ya kilometa 1115 na Uganda 330. Aidha, Mradi utatarajia kusafirisha mapipa laki mbili na kumi na sita elfu (216,000) kwa siku .

Kijiji cha Chongoleani ndio kituo cha mwisho ambapo mitambo mikubwa itasimikwa katika eneo hili kwa ajili ya kusukuma mafuta eneo la baharini ili, kuweka kwenye vyombo vya usafirishaji kusafirisha maeneo mbalimbali duniani ambayo Uganda watakuwa wamepata soko.

Tanzania itafaidika na mradi huu kutokana na kodi, tozo na mrahaba wa bomba la mafuta, itakayofanywa moja kwa moja na mradi huo. Faida nyingine ambazo, sio za moja kwa moja ni ajira, fursa za kufanya biashara na uwezekano wa mikoa 8 ambayo ni Kagera, Geita, Shinyanga, Tabora, Singida, Dodoma, Morogoro na Tanga.