Sunday, June 25

Polisi Dar mguu sawa sikukuu ya Eid


JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewahakikishia  hali ya usalama na amani wakazi, wananchi wa jiji la Dar es Salaam katika kipindi chote cha sikukuu ya Eid inayotarajiwa kuwa Jumatatu.
Lucas Mkondya, Kaimu Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam amesema kuwa askari wa jeshi hilo wamejipanga vyema kuhakikisha wananchi wa jiji la Dar es Salaam wanasherehekea sikukuu hiyo kwa kwa amani na utulivu pasipo bugudha za wahalifu.
“Uzoefu unaonesha kuwa, mara nying kipindi cha sikukuu kama hii watu wenye nia ovu hujiandaa kufanya vitendo vya kihalifu, ndiyo maana tumejipanga kukabiliana na aina yoyote  ya uhalifu kwa kuzuia au kuwatia nguvuni wote watakaoshiriki vitendo vya uvunjifu wa sheria,” amesema.
Kamanda Mkondya amesema polisi watafanya doria za masaa 24 katika maeneo yote ya jiji la Dar es Salaam hasa maeneo yenye korofi na yenye rekodi au viashiria vya uhalifu.
“Pia kutakuwa na doria katika maeneo ya misikiti, kumbi za starehe na maeneo yenye mikusanyiko mikubwa ya watu na tutatumia taarifa za kiintelijensia ili kuwabaini wahalifu wanaopanga kufanya matukio ya uhalifu.
“Tutaimarisha vikundi vya ulinzi shirikishi ili kuhakikisha maeneo yote hatarishi yanadhibitiwa,” amesema Kamanda Mkondya.

Hizi ni mbinu za ubinafsishaji




Biashara imara huanzishwa kwa ufanya upembuzi yakinifu ambao hutoa fursa kutambua mambo mengi kuhusu biashara yenyewe na mazingira ambayo biashara hiyo itawekezwa.
Biashara kubwa za kampuni hutumia fedha nyingi kufanya maandalizi ya msingi kabla ya kujiridhisha kama biashara hiyo inaweza kufanyika na kuleta matokeo chanya kwa wamiliki na wadau wengine.
Hili linaweza kufanyika kwa biashara aina zote na kiwango chochote cha mtaji ili kuziweka biashara katika maeneo salama. Uwekezaji wa biashara zote ni muhimu kuangalia mambo yafuatayo,
Upatikanaji wa malighafi au bidhaa za msingi za Biashara husika, ni muhimu sana kufungua na kuanzisha biashara eneo ambalo kutakuwa na urahisi wa upatikanaji malighafi muhimu kwa uzalishaji wa bidhaa kuu na huduma zinazotolewa na biashara husika.
Ili uimudu biashara ni lazima kujihakikishia upatikanaji wa malighafi au mizigo unayochukua kuleta kuuza iwe ndani au nje ya nchi ni muhimu kuwa na uhakika wa upatikanaji wa huduma na bidhaa zako.
Kuwafahamu wapinzani wako kwenye biashara unayokwenda kuwekeza, ili kuweza kuipata nafasi yako kwenye soko la ushindani. Wafahamu watu wanaofanya biashara kama yako au nyingine zinazofanana na yako.
Kulifahamu soko la bidhaa na mahitaji ya wateja na wadau wako, ubunifu wa bidhaa zinazokwenda na wakati ni jambo la muhimu sana kwasababu sio kila bidhaa yako inafaa kutumika kwa watu wote.
Ni muhimu kulifahamu soko lako na ulichambue vizuri ili uweze kubuni bidhaa na huduma zinazokwenda na mahitaji yao. Mfano wa kampuni ya simu kwa ubunifu wao mzuri wa vifurushi vingi kama vile vya chuo ambako huko kuna wanafunzi wengi na wanatumia sana simu na vifaa vingine kufanya mawasiliano ya mtandao na kawaida, huu ni mfano wa biashara inayotambua soko lake na mahitaji ya wadau kutokana na mazingira.
Gharama za kuendesha Biashara yako, kuna wakati unaweza kuwa na wazo zuri sana la biashara lakini katika kufanya Uchunguzi na upembuzi ukagundua kuwa gharama za uendeshaji wa biashara yako zitakuwa juu na kukufanya upate hasara au kuendesha biashara isiyokuwa na tabia ya kupanuka ni vizuri kufikiria mara mbili kuhusu biashara hiyo.
Utaratibu wa ulipaji kodi na gharama nyingine, ni muhimu na lazima kulipa kodi kwa biashara yoyote ila kama biashara yako unaona inaingia kukupa gharama kubwa na mazingira yasiyokuwa rafiki kwenye ulipaji kodi ni vizuri kujitathimini na kuangalia upya mfumo wa kuingiza au kuendesha biashara yako.
Hali ya eneo lako la biashara. Moja kati ya vitu vya muhimu sana kwenye biashara inayoanza au ile inayoendelea ni kujiuliza kuhusu eneo ambalo biashara yako unahitajika kuiweka.
Biashara nzuri inategemea sana eneo ambalo ofisi na majengo yake yatakuwepo kama yatakuwa katika maeneo sahihi kwa watu na wadau wake kufika na kupata huduma basi biashara hii itakuwa inafanya kazi nzuri lakini ukichagua eneo baya na ambalo haliendani na aina ya biashara yako unaweza kujikuta unapunguza nguvu ya biashara yako kufanya vizuri na kukupa matokeo mazuri kwenye upande wa faida kifedha.
Mazingatio haya ni muhimu kwa biashara za aina zote kuanzia viwanda, biashara za kawaida za kuuza na kununua tulizozoea au sekta za fedha huwezi kuifanya biashara yenye mafanikio bila kuzingatia vitu hivi muhimu ili kuifanya biashara yako iwe na nguvu, mbinu hizi zinatumika kwa biashara mpya na zile zilizokuwepo.
Lakini pia katika hayo machache swala la Amani ya eneo la biashara ni muhimu kwenye kutengeneza biashara yenye nguvu.

TANTRADE YAWAKARIBISHA KATIKA MAONYESHO YA 41 YA BIASHAYA YA KIMATAIFA JIJINI DAR


Mwigulu apigilia msumari agizo la JPM

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba amezionya taasisi zisizo za Serikali zinazohamasisha kudai haki ya mtoto anayepata mimba kurejeshwa shuleni kuacha mara moja na zikiendelea atazifutia usajili.
Mwigulu ameyasema hayo leo, Jumapili wakati alipomwakilisha Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa katika harambee ya kuchangia ujenzi wa Parokia ya Kisasa Mjini hapa.
Amesema Serikali haitaomba ushauri wala maoni kwa sababu maelezo yaliyotolewa na Rais, John Magufuli ni maagizo ya Serikali.
Waziri huyo amesema Serikali imetoa haki ya kila mtoto kupata elimu kwa kuifanya kuwa bure kwa hiyo atakayeikosa asitafute kisingizio.
"Rais ametoa haki hiyo sasa hivi elimu ni bure, halipi tuition wala nini, atakayeamua kuachana na haki hiyo asitafute kisingizio, asipeleke lawama kwa Serikali, "amesema.