Sunday, September 17

MAJAJI NCHINI WAAGIZWA KUMALIZA MLUNDIKANO WA MASHAURI IFIKAPO DESEMBA 15, 2017

Majaji nchini wameagizwa kumaliza kesi zote za muda mrefu Mahakamani ifikapo Disemba 15, mwaka huu ili kuendana na azma ya Mahakama ya kutoa haki  kwa wote na kwa wakati.
Akizungumza katika Mkutano wa Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Jaji Kiongozi Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali alisema kuwa Kanda zote za Mahakama Kuu nchini tayari zimeshaainisha idadi ya kesi zote za kuanzia miaka miwili kuendelea (kesi za mlundikano) ambazo zitafanyiwa kazi.
“Nawaagiza Majaji wote nchini kuendelea na zoezi la kusikiliza kesi hususani kesi za muda mrefu Mahakamani, na zoezi hili lianze kufanyika Oktoba 16,mwaka huu na kazi hii nataka ikamilike kufikia Desemba 15,mwaka huu,” alisisitiza.
Mhe.Jaji Kiongozi amezitaja Kanda za Mahakama Kuu ambazo zinaonekana kuelemewa na mzigo wa mashauri kuandaa orodha ya mashauri ‘causelist’wanayohitaji kusaidiwa.
Mahakama hizo ni Mahakama Kuu-Kanda ya Dar es Salaam, Mahakama Kuu-Kanda ya Mwanza, Mahakama Kuu-Kanda ya Bukoba, Mahakama Kuu-Kanda ya Mbeya, Mahakama Kuu-Kanda ya Shinyanga, Mahakama Kuu-Divisheni ya Ardhi na Mahakama Kuu-Divisheni ya Kazi.
Aidha Mhe. Wambali ameagiza zoezi hilo lifanyike ndani ya wiki moja kuanzia Jumatatu, Septemba 18 ili kuwezesha kujua uhitaji wa msaada wa Majaji wengine kutoka Kanda nyingine watakaoenda kusaidia kusikiliza na kumaliza mashauri hayo katika maeneo tajwa.
Aidha Mhe. Jaji Kiongozi amewataka Majaji Wafawidhi kuitisha vikao na Wadau wa Mahakama ili waweze kujua juu ya kuwepo kwa Programu maalum ya kusikiliza na kumaliza kesi zote za muda mrefu Mahakamani.
Kwa upande wake Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahimu Hamis Juma amewataka Majaji na Watumishi wa Mahakama kwa ujumla kufanya kazi kwa kuzingatia nguzo tatu za Mpango Mkakati wa Mahakama ili kutekeleza majukumu kimkakati na hatimaye kupata matokeo chanya.
“Majaji Wafawidhi ni nguzo muhimu katika utekelezaji wa Mpango Mkakati hususani katika nguzo namba mbili ambayo ni Upatikanaji na utoaji wa Haki kwa wakati, kupitia Majaji na Mahakimu waliopo chini yao” alisema Mhe. Jaji Mkuu.
Akiongelea juu ya jukumu kuu la utoaji haki nchini, Mhe. Jaji Mkuu amesisitiza juu ya kuwa na kumbukumbu sahihi ya takwimu za mashauri zilizopo katika Mahakama husika hali ambayo itawezesha kujua ni msaada utakaohitaji, bajeti na kadhalika.
Kwa upande mwingine Mhe. Jaji Mkuu amesisitiza juu ya matumizi ya TEHAMA katika uendeshaji wa kesi ili kuendeana na kasi ya Teknolojia hali ambayo itawezesha huduma ya haki kuwafikia wananchi kwa wakati.
Mambo mengine aliyoyasisitiza Mhe. Jaji Mkuu alipokuwa akifunga Mkutano wa Majaji Wafawidhi ni pamoja na ufanyaji kazi kwa ushirikiano kwa Watumishi wote wa Mahakama na kubadili mtazamo hasi ‘change of attitude’ na kuzingatia maadili katika utendaji kazi.
Mkutano wa Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, uliofanyika kwa siku mbili (2), Septemba 15&16 ni mwendelezo wa Vikao mbalimbali ambavyo vimekuwa vikifanyika mara kwa mara vyote vikiwa na lengo la kuhakikisha kuwa azma ya Mahakama ya Tanzania ya kutoa haki kwa wakati inaonekana kutekelezeka.
 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akitoa neno alipokuwa akifunga Mkutano wa Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa-AICC jijini Arusha, Septemba, 15 na 16, 2017. 
 Sehemu ya Waheshimiwa Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu nchini wakimsikiliza kwa makini Mhe. Jaji Mkuu (hayupo pichani) 
Waheshimiwa Majaji Wafawidhi pamoja na Wasajili wakiwa katika Mkutano huo uliokamilika Septemba 16, 2017
 Waheshimiwa Majaji Wafawidhi pamoja na Wasajili wakiwa katika Mkutano huo uliokamilika Septemba 16, 2017
 Mtendaji Mkuu-Mahakama ya Tanzania,Mhe. Hussein Kattanga akitoa neno, akisisitiza juu ya ufanyaji kazi kwa malengo.
 Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali akiongea katika Mkutano wa Majaji Wafawidhi
 Mkuu wa Kitengo cha Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama,Mhe.Zahra Maruma akitoa mara ya utekelezaji wa kazi mbalimbali za Mradi mbele ya Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
Meza Kuu ikiwa katika picha ya pamoja na Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania mara baada ya kuhitimisha kikao cha siku mbili cha kujadili juu ya mikakati ya kuondosha mashauri ya muda mrefu Mahakamani. aliyeketi katikati ni Jaji Mkuu wa Tanzania,Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, wa pili kushoto ni Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali, wa kwanza kushotoni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Kanda ya Iringa pia ni Jaji namba moja wa Mahakama Kuu ya Tanzania, wa pili kulia ni Kaimu Jaji Mfawidhi,Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha, Mhe. Sekela Moshi na wa kwanza kulia ni Mtendaji Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Hussein Kattanga.Picha na Habari na Mary Gwera wa Mahakama

BLOGGER TUPOKIGWE ABNERY KUZINDUA KITABU CHA RIWAYA "MAPENZI KABURINI" JIJINI ARUSHA


Tupokigwe Abnery Mwampondele amezaliwa,Seronera - Serengeti mkoani Mara.Alisomea shahada ya Isimu ya lugha ya Kiswahili Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Kwa sasa ni mwalimu wa somo la Kiswahili katika shule ya Sekondari ya Wasichana Precious blood iliyopo mkoani Arusha-Tanzania. N’je na kazi ya uwalimu Tupokigwe Abnery ni mtunzi wa vitabu vya hadithi, mbunifu wa mavazi ya kiasili, mjasiriamali na mwandishi wa gazeti tando (blogger) inayoitwa Sinyati Blog.

Tupokigwe Abnery alikuwa na kawaida ya kupenda kujibembeleza au kujifariji akiwa anatembea kwa kutengeneza hadithi katika fikra zake ili kuweza kulala au kufika anakoelekea bila kuchoka,ndipo siku moja baada ya kushiriki shindano la uandishi wa Riwaya fupi kwa wanafunzi wa shule ya msingi,sekondari na vyuo vikuu Tanzania kwa ajili ya Tuzo ya mama Salma Kikwete iliyoandaliwa na TASAKI(Tamasha la Sauti ya Kiswahili) aliibuka mshindi wa pili wa riwaya fupi kwa wanafunzi wa vyuo vikuu Tanzania.

Hivyo hiki kitabu ni muendelezo wa Riwaya aliyopatia Tuzo.Soma kitabu hiki uweze kujionea ubunifu wa hali ya juu wa fani pamoja na mshikamano wa maudhui uliyopo ndani ya kitabu hiki. 

Mapenzi Kaburini ni kitabu chenye mtazamo yakinifu,ni kitabu ambacho maudhui yake yamezitazama nchi za Afrika Mashariki na changamoto zilizopo katika nchi kwa upande wa viongozi pamoja na wananchi.Kimebeba maudhui yanayowalenga wananchi wote bila kujali utabaka.Kwa upande wa fani kimetumia majina ya halisi na kubuni hasa kwa upande wa maeneo ya miji mfano kuna miji kama Kinyonga,kupe,chatu ambayo ni majina yaliyopo katika nchi ya Simba.Nchi hii ya Simba ni nchi inayosimamia nchi zilizopo Afrika Mashariki.

Mbali na hilo pia visa na matukio vimepewa majina ya hifadhi za Taifa zilizopo katika nchi ya Tanzania.Mfano hifadhi ya Ruaha,Sanane,Manyara na kitulo kama ukisoma kitabu hiki utagundua kuwa sifa ya hifadhi inaendana na visa na matukio yaliyopo katika sehemu hiyo iliyoandikwa kwa jina la hifadhi.Mfano hifadhi ya Kitulo inasifika kwa kuwa na maua,kama tujuavyo maua huashiria sifa nyingi moja wapo hapo ni upendo,watu wengi hutumia maua katika kuwapa wapenzi wao,mfano kuomba msamaha,kumfariji mtu,hata kuonesha upendo kwa mtu unayempenda.

Utakaposoma kitabu hiki utaburudika na kufundishwa baadhi ya mambo kama Kukuza imani yako kwa Mungu,uaminifu katika ndoa,uzalendo katika nchi yako na Madhara ya kujihusisha katika mahusiano na mtu usiye mjua.
Nitakupatia kionjo kidogo katika sura ya kwanza ili kuweza kuona mwanzo tu wa hadithi hii ambayo hutapenda kuacha kuifuatilia:

Sura ya kwanza 

Hifadhi ya Sanane 
Ilikuwa siku ya Jumatatu katika ghorofa la tajiri mmoja, mmiliki wa hoteli maarufu katika nchi ya Simba. Tajiri huyo alifahamika sana kwa kuwa alikuwa akijitolea sana kwa wananchi wasiojiweza, katika miji mbalimbali ya nchi hiyo.Watu husemamfadhili punda kuliko mwanadamu vilevile tenda wema kisha nenda zako baraka utazipata kwa Mungu,usisubiri hisani za wanadamu.

Pamoja na misaada aliyoitoa kwa watu mbalimbali lakini wananchi wa Simba hawakujali misaada yake, walimteta kila kona kuwa anatumia nguvu za giza na amekwisha toa kafara ndugu, jamaa na hata watoto wake ili kujipatia utajiri mkubwa alionao. Siku hiyo ya Jumatatu katika pagala la tajiri huyo aliyefamika kwa jina la Pesa nyingi.

katika moja ya chumba cha ghorofa hilo kulikuwa na mwanamke mrembo na mzuri sana wa sura, mrefu mithili ya twiga, mwenye umbo zuri la kiafrika, chini alikuwa amevaa suruali ya chupa huku akiwa amevaa blauzi tatu juu zenye rangi tofauti na nywele timutimu zikiwa zime nakishiwa na vitu vya jaani kama vichana,visude, rasta chakavu na kufungwa kitambaa cha kitenge aina ya makenzi ,uso wake ulikuwa kama paka mwenye madoa kutokana na kujipamba kwa majivu na masizi ya mkaa wa jaani. Pembeni ya ua hilo alikuwepo mnyama mwenye maringo 

mbugani kuliko wote, sio mwingine bali ni kijana mtanashati aliyekwenda hewaani, rangi ya ngozi yake nyeusi ya kung’aa. Tabasamu la mwanaume huyo lililokuwa likimfariji mtoto mzuri, lili mvutia sana Savannah. Ghafla ilisikika sauti ya mwanamke huyo ikiita kwa sauti ya chini iliyojaaa simanzi na mateso ya muda mrefu,ilisema “John naumia mume wangu, hali yangu kila kukicha afadhali ya jana”. 

John alijibu “usijali Savannah nipo hapa mke wangu kwa ajili yako utapona tu tutakwenda hospitali,subiri nikuandalie chakula ule, kisha nikupeleke hospitali malikia wangu”. Basi baada ya John kumfariji Savannah aliamka na kuelekea jikoni pembeni ya sehemu aliyokuwa amelala mpenzi wake. 

Watu hawa walipendana sana ni vile tu hali yao haikuwa nzuri kifedha waliishi kwa kuhangaika, kuomba msaada na wakati mwingine walifukuzwa na walimwengu pale walipokuwa wakiomba msaada, watu waliwapita kama mbwa waliokosa matunzo. 

Wapenzi hao Walizoea maisha ya kuokota vyakula jalalani na kukimbilia magari ya taka sambamba na kusubiria mabaki ya chakula katika migahawa mbalimbali. Wakati huo John alikuwa akitimiza ahadi aliyo mhahidi malikia wake alimuandalia chakula walicho kiokota katika soko kuu la mji huo wa Chatu. John alimuinua Savannah pale alipokuwa amelala kwenye kanga chakavu akiwa amejifunika magunia yalionekana ni ya mpunga. John alimlisha Savannah chakula kile ambacho hawakujua kilipikwa lini na kutupwa na nani na lini. Savannah alisikika akisema “asante mume wangu hata 

mwanangu anafurahi sasa naona napata nafuu, nahisi ni njaa ilikuwa inaniuma”. Mwanangu nisamehe mama kakushindisha njaa, nakupenda sana najua wewe utakuwa mrembo zaidi yangu mwanangu hata baba yako anakupenda”. John alikuwa anapenda sana utani alicheka na kusema “atakuwa mrembo kama wewe kweli mke wangu lakini rangi ya ngozi yake itakuwa kama yangu, yako iko kama ya nguruwe hahahaaaa!” Savannah alikuwa mweupe kama Nguruwe, ingawa alivyokuwa anaonekana ni kama mtu mwenye ngozi ya rangi ya maji ya kunde kutokana na ugumu wa maisha. 

Wawili hao walifurahi pamoja na kusahau shida walizokuwa nazo.Walipomaliza kula wapenzi hao waliamua kutoka nje baada ya kukaa ndani ya paghala hilo kwa muda wa wiki moja, Dikidiki hao walikuwa na kaida ya kufanya hivyo wanapotafuta riziki na kujilimbikizia ndani ya paghala lao kisha wana kaa kwa muda huo bila kutoka. Usilolijua ni kama usiku wa kiza, basi Savannah na John walipotoka wakiwa n’je ya mgahawa mmoja uliokuwa unapendwa sana na wananchi wa mji huo wa Chatu zilisikika sauti za wanawake wakisema: 

“haya jamani sasa ni ule wakati wa Pesa nyingi kuingiza hela sasa wenzi wametoka fungate”. Waliamini kuwa Pesa nyingi alikuwa anawatumia Dikidiki hao kama misukule inayotoka na kurudi ndani na wanapotoka basi mzee Pesa nyingi huingiza hela nyingi sana. Kwakuwa wenzi hao walikuwa hawaelewi kinachoongelewa waliendelea kuomba msaada kwa wateja waliokuwepo hapo mgahawani. Wanapokosa waliamua kucheza baadhi ya nyimbo zilizokuwa 

zikipigwa katika mgahawa huo, wakicheza hupewa chakula na fedha ambazo hutoka katika mifuko ya wateja. John alikuwa anapenda sana kucheza,wakiwa wamekaa chini walisikia wimbo wa mwanamuziki maarufu Tanzania Diamond unaosema Je, Utanipendaga? John alimuinua Savannah aliyeonekana kachoka na mimba yake. Savannah aliamka na kucheza na mpenzi wake ,walicheza kwa miondoko ya kihindi, machozi yalisafisha uso wa Savannah huku yakiosha kifua cha John kilichokuwa kimejaa kama mlima na mikono iliyokuwa na miinuko ya kupanda na kushuka ilizunguka juu ya kifua cha Savannah na kumfanya ahisi kazungukwa na jeshi kubwa la malaika wa ulinzi.

Baada ya kumaliza kucheza savannah alikuwa amechoka sana, kitendo cha kucheza kilimsababishia kuchokoza maumivu na kupelekea kupata uchungu katika kizazi chake. Baada ya kuona hivyo John aliinama na kuchukua zawadi walizozipata kutoka kwa hadhira iliyokuwa ikiwatazama huku baadhi ya hadhira wakibubujikwa na machozi walimpelekea hela na chakula John katika kapu lake la kukusanyia riziki. Watu waliokuwa wakiwatazama Savannah na John hawakujali maumivu ya mwanamke yule na kuona kawaida. 

Wapo waliosikika wakisema hawa vichaa wana akili, wengine walisema hawa si vichaa, vichaa gani wana akili ya kutafuta hela hivi, wamekusanya umati mkubwa hivi na kuwafanya watu kutoa kile walichonacho. Mama mmoja mwenye busara anayeuza katika mgahawa huo aliyefahamika kwa jina la mama ndaga akasema“Jamani mimi nawafahamu hawa vichaa kwanza hawakuwa wakitembea hivi pamoja kama Dikidiki, huyo kaka unayemuona alikuwa..........pata mwendelezo kwa kujipatia kitabu hiki.

NKAMIA APINGWA KUSUDIO LA KUONGEZA UKOMO WA BUNGE

NA AZIZA MASOUD – DAR ES SALAAM
KITENDO cha Mbunge wa Chemba, Juma Nkamia (CCM), kuwasilisha kusudio la kutaka kuwasilisha muswada binafsi wa mabadiliko ya Katiba bungeni ili kuongeza ukomo wa Bunge, kimepingwa vikali na baadhi ya wasomi na wanasiasa, huku baadhi yao wakidai huenda akawa anatafuta umaarufu.
Nkamia aliwasilisha kusudio hilo ofisi za Bunge kwa mujibu wa kanuni ya 81(2) ya kanuni za Bunge toleo la 2016.
Katika barua yake aliyoisaini Septemba 12, mwaka huu na kuwasilishwa ofisi ya Katibu wa Bunge Dodoma, ameeleza kusudio lake la kuwasilisha muswada huo aliouita Muswada Binafsi wa Sheria ya Mabadiliko ya 15 ya Katiba.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti na gazeti hili jana, Mhadhiri wa Masuala ya Siasa wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Dk. Benson Bana, alisema pamoja na kwamba ni mawazo binafsi, lakini anapaswa kutoa sababu za msingi za marekebisho hayo yatakayokuwa kinyume na Katiba iliyopo.
“Lazima tuangalie mawazo haya kayatoa kwa muktadha gani, huenda ana lengo la kujitafutia umaarufu ili na yeye aonekane kaingiza agenda fulani katika jamii, huyu mtu aliwahi kuwa naibu waziri, isije ikawa anabembeleza nafasi ya uwaziri,” alisema Dk. Bana.
Alisema sababu zinazofanya kuwe na uongozi wa miaka mitano zilizotolewa na Watanzania bado zipo hai, hivyo kama angekuwa muungwana angepeleka hoja ya nafasi ya ubunge kutozidi miaka 10.
Pia alisema Nkamia alipaswa ajitafakari kabla ya kuwasilisha kusudio hilo kwa kuwa hoja ya kuongeza muda wa urais ilishakataliwa na Rais Dk. John Magufuli, hivyo asitafute sababu ya kuibadili.
“Maoni yake hayaakisi uhalisia hata kidogo, Watanzania tuna Katiba na bado haijabadilika, asitake ajiwekee mazingira ya kuonekana anampigia chapuo rais,” alisema Dk. Bana.
Naye mchambuzi wa masuala ya siasa, Profesa Mwesiga Baregu, alisema kauli ya Nkamia inaonyesha nchi ilivyo na wanasiasa waroho wa madaraka.
“Hizi ni kauli za wagonjwa na walevi wa madaraka, hilo suala lipo ndani ya Katiba, sasa labda kama atakuwa na sababu ya msingi ya kuhitaji mabadiliko hayo atuambie, lakini mimi sijaridhika, sioni  kama kuna sababu,” alisema Baregu.
Alisema masuala ya ukomo wa Bunge yalishazungumziwa katika Rasimu ya Mabadiliko ya Katiba mpya, kwamba ukomo wa rais ulipaswa kuwa vipindi viwili wakati Bunge vipindi vitatu.
Profesa Baregu alisema misingi ya demokrasia ni kuchochea mawazo mapya na maoni tofauti, lakini suala la ukomo wa umri na mihula ni ugonjwa katika nchi za Afrika.
Naye Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ambaye pia ni wakili wa kujitegemea, Profesa Abdallah Safari, alisema kitendo cha Nkamia kutoa kauli hiyo katika nchi za demokrasia kama Tanzania, kinamfanya kumwona wa ajabu.
“Namwona ni mtu wa ajabu, nchi zote zenye demokrasia kama Uingereza na Marekani, wana awamu nne za urais, lengo ni kumfanya kiongozi asibweteke.
“Mawazo aliyoyatoa ni uhuni wa kutaka kuwa masultani na hii si kauli yake, lazima kuna mtu atakuwa amemtuma,” alisema Profesa Safari.
Alisema Tanzania haiwezi kuiga mfano wa Rwanda kwa kuwa nchi hiyo inaendeshwa kinyume na sheria za kimataifa.
Naye Rais mstaafu wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Charles Rwechungura, alisema Nkamia anaweza kufanikisha suala hilo endapo atakuwa na sababu za msingi.
“Mimi nadhani tuone kwanza sababu zake za kutaka mabadiliko, labda ana sababu za msingi, lakini pia akiweza kuwashawishi wabunge basi sisi wananchi hatutakuwa na jinsi,” alisema.
Kwa upande wake, Nkamia, alishangazwa na kitendo cha nyaraka hiyo aliyoita ya siri kusambaa katika mitandao ya kijamii na alikiri kuwasilisha kusudio hilo na kusisitiza kuwa ataweka wazi sababu za kufanya hivyo muda utakapofika.
“Ni kweli nimewasilisha kusudio hilo na nitatoa sababu muda utakapofika, lakini mmenishangaza hiyo nyaraka ni ya siri na bado ilikuwa katika ngazi ya kiofisi, sijui imefikaje uko kwenu,” alisema Nkamia.

BLOGGER TUPOKIGWE ABNERY KUZINDUA KITABU CHA RIWAYA "MAPENZI KABURINI" JIJINI ARUSHA


Tupokigwe Abnery Mwampondele amezaliwa,Seronera - Serengeti mkoani Mara.Alisomea shahada ya Isimu ya lugha ya Kiswahili Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM). Kwa sasa ni mwalimu wa somo la Kiswahili katika shule ya Sekondari ya Wasichana Precious blood iliyopo mkoani Arusha-Tanzania. N’je na kazi ya uwalimu Tupokigwe Abnery ni mtunzi wa vitabu vya hadithi, mbunifu wa mavazi ya kiasili, mjasiriamali na mwandishi wa gazeti tando (blogger) inayoitwa Sinyati Blog.

Tupokigwe Abnery alikuwa na kawaida ya kupenda kujibembeleza au kujifariji akiwa anatembea kwa kutengeneza hadithi katika fikra zake ili kuweza kulala au kufika anakoelekea bila kuchoka,ndipo siku moja baada ya kushiriki shindano la uandishi wa Riwaya fupi kwa wanafunzi wa shule ya msingi,sekondari na vyuo vikuu Tanzania kwa ajili ya Tuzo ya mama Salma Kikwete iliyoandaliwa na TASAKI(Tamasha la Sauti ya Kiswahili) aliibuka mshindi wa pili wa riwaya fupi kwa wanafunzi wa vyuo vikuu Tanzania.

Hivyo hiki kitabu ni muendelezo wa Riwaya aliyopatia Tuzo.Soma kitabu hiki uweze kujionea ubunifu wa hali ya juu wa fani pamoja na mshikamano wa maudhui uliyopo ndani ya kitabu hiki. 

Mapenzi Kaburini ni kitabu chenye mtazamo yakinifu,ni kitabu ambacho maudhui yake yamezitazama nchi za Afrika Mashariki na changamoto zilizopo katika nchi kwa upande wa viongozi pamoja na wananchi.Kimebeba maudhui yanayowalenga wananchi wote bila kujali utabaka.Kwa upande wa fani kimetumia majina ya halisi na kubuni hasa kwa upande wa maeneo ya miji mfano kuna miji kama Kinyonga,kupe,chatu ambayo ni majina yaliyopo katika nchi ya Simba.Nchi hii ya Simba ni nchi inayosimamia nchi zilizopo Afrika Mashariki.

Mbali na hilo pia visa na matukio vimepewa majina ya hifadhi za Taifa zilizopo katika nchi ya Tanzania.Mfano hifadhi ya Ruaha,Sanane,Manyara na kitulo kama ukisoma kitabu hiki utagundua kuwa sifa ya hifadhi inaendana na visa na matukio yaliyopo katika sehemu hiyo iliyoandikwa kwa jina la hifadhi.Mfano hifadhi ya Kitulo inasifika kwa kuwa na maua,kama tujuavyo maua huashiria sifa nyingi moja wapo hapo ni upendo,watu wengi hutumia maua katika kuwapa wapenzi wao,mfano kuomba msamaha,kumfariji mtu,hata kuonesha upendo kwa mtu unayempenda.

Utakaposoma kitabu hiki utaburudika na kufundishwa baadhi ya mambo kama Kukuza imani yako kwa Mungu,uaminifu katika ndoa,uzalendo katika nchi yako na Madhara ya kujihusisha katika mahusiano na mtu usiye mjua.
Nitakupatia kionjo kidogo katika sura ya kwanza ili kuweza kuona mwanzo tu wa hadithi hii ambayo hutapenda kuacha kuifuatilia:

Sura ya kwanza 

Hifadhi ya Sanane 
Ilikuwa siku ya Jumatatu katika ghorofa la tajiri mmoja, mmiliki wa hoteli maarufu katika nchi ya Simba. Tajiri huyo alifahamika sana kwa kuwa alikuwa akijitolea sana kwa wananchi wasiojiweza, katika miji mbalimbali ya nchi hiyo.Watu husemamfadhili punda kuliko mwanadamu vilevile tenda wema kisha nenda zako baraka utazipata kwa Mungu,usisubiri hisani za wanadamu.

Pamoja na misaada aliyoitoa kwa watu mbalimbali lakini wananchi wa Simba hawakujali misaada yake, walimteta kila kona kuwa anatumia nguvu za giza na amekwisha toa kafara ndugu, jamaa na hata watoto wake ili kujipatia utajiri mkubwa alionao. Siku hiyo ya Jumatatu katika pagala la tajiri huyo aliyefamika kwa jina la Pesa nyingi.

katika moja ya chumba cha ghorofa hilo kulikuwa na mwanamke mrembo na mzuri sana wa sura, mrefu mithili ya twiga, mwenye umbo zuri la kiafrika, chini alikuwa amevaa suruali ya chupa huku akiwa amevaa blauzi tatu juu zenye rangi tofauti na nywele timutimu zikiwa zime nakishiwa na vitu vya jaani kama vichana,visude, rasta chakavu na kufungwa kitambaa cha kitenge aina ya makenzi ,uso wake ulikuwa kama paka mwenye madoa kutokana na kujipamba kwa majivu na masizi ya mkaa wa jaani. Pembeni ya ua hilo alikuwepo mnyama mwenye maringo 

mbugani kuliko wote, sio mwingine bali ni kijana mtanashati aliyekwenda hewaani, rangi ya ngozi yake nyeusi ya kung’aa. Tabasamu la mwanaume huyo lililokuwa likimfariji mtoto mzuri, lili mvutia sana Savannah. Ghafla ilisikika sauti ya mwanamke huyo ikiita kwa sauti ya chini iliyojaaa simanzi na mateso ya muda mrefu,ilisema “John naumia mume wangu, hali yangu kila kukicha afadhali ya jana”. 

John alijibu “usijali Savannah nipo hapa mke wangu kwa ajili yako utapona tu tutakwenda hospitali,subiri nikuandalie chakula ule, kisha nikupeleke hospitali malikia wangu”. Basi baada ya John kumfariji Savannah aliamka na kuelekea jikoni pembeni ya sehemu aliyokuwa amelala mpenzi wake. 

Watu hawa walipendana sana ni vile tu hali yao haikuwa nzuri kifedha waliishi kwa kuhangaika, kuomba msaada na wakati mwingine walifukuzwa na walimwengu pale walipokuwa wakiomba msaada, watu waliwapita kama mbwa waliokosa matunzo. 

Wapenzi hao Walizoea maisha ya kuokota vyakula jalalani na kukimbilia magari ya taka sambamba na kusubiria mabaki ya chakula katika migahawa mbalimbali. Wakati huo John alikuwa akitimiza ahadi aliyo mhahidi malikia wake alimuandalia chakula walicho kiokota katika soko kuu la mji huo wa Chatu. John alimuinua Savannah pale alipokuwa amelala kwenye kanga chakavu akiwa amejifunika magunia yalionekana ni ya mpunga. John alimlisha Savannah chakula kile ambacho hawakujua kilipikwa lini na kutupwa na nani na lini. Savannah alisikika akisema “asante mume wangu hata 

mwanangu anafurahi sasa naona napata nafuu, nahisi ni njaa ilikuwa inaniuma”. Mwanangu nisamehe mama kakushindisha njaa, nakupenda sana najua wewe utakuwa mrembo zaidi yangu mwanangu hata baba yako anakupenda”. John alikuwa anapenda sana utani alicheka na kusema “atakuwa mrembo kama wewe kweli mke wangu lakini rangi ya ngozi yake itakuwa kama yangu, yako iko kama ya nguruwe hahahaaaa!” Savannah alikuwa mweupe kama Nguruwe, ingawa alivyokuwa anaonekana ni kama mtu mwenye ngozi ya rangi ya maji ya kunde kutokana na ugumu wa maisha. 

Wawili hao walifurahi pamoja na kusahau shida walizokuwa nazo.Walipomaliza kula wapenzi hao waliamua kutoka nje baada ya kukaa ndani ya paghala hilo kwa muda wa wiki moja, Dikidiki hao walikuwa na kaida ya kufanya hivyo wanapotafuta riziki na kujilimbikizia ndani ya paghala lao kisha wana kaa kwa muda huo bila kutoka. Usilolijua ni kama usiku wa kiza, basi Savannah na John walipotoka wakiwa n’je ya mgahawa mmoja uliokuwa unapendwa sana na wananchi wa mji huo wa Chatu zilisikika sauti za wanawake wakisema: 

“haya jamani sasa ni ule wakati wa Pesa nyingi kuingiza hela sasa wenzi wametoka fungate”. Waliamini kuwa Pesa nyingi alikuwa anawatumia Dikidiki hao kama misukule inayotoka na kurudi ndani na wanapotoka basi mzee Pesa nyingi huingiza hela nyingi sana. Kwakuwa wenzi hao walikuwa hawaelewi kinachoongelewa waliendelea kuomba msaada kwa wateja waliokuwepo hapo mgahawani. Wanapokosa waliamua kucheza baadhi ya nyimbo zilizokuwa 

zikipigwa katika mgahawa huo, wakicheza hupewa chakula na fedha ambazo hutoka katika mifuko ya wateja. John alikuwa anapenda sana kucheza,wakiwa wamekaa chini walisikia wimbo wa mwanamuziki maarufu Tanzania Diamond unaosema Je, Utanipendaga? John alimuinua Savannah aliyeonekana kachoka na mimba yake. Savannah aliamka na kucheza na mpenzi wake ,walicheza kwa miondoko ya kihindi, machozi yalisafisha uso wa Savannah huku yakiosha kifua cha John kilichokuwa kimejaa kama mlima na mikono iliyokuwa na miinuko ya kupanda na kushuka ilizunguka juu ya kifua cha Savannah na kumfanya ahisi kazungukwa na jeshi kubwa la malaika wa ulinzi.

Baada ya kumaliza kucheza savannah alikuwa amechoka sana, kitendo cha kucheza kilimsababishia kuchokoza maumivu na kupelekea kupata uchungu katika kizazi chake. Baada ya kuona hivyo John aliinama na kuchukua zawadi walizozipata kutoka kwa hadhira iliyokuwa ikiwatazama huku baadhi ya hadhira wakibubujikwa na machozi walimpelekea hela na chakula John katika kapu lake la kukusanyia riziki. Watu waliokuwa wakiwatazama Savannah na John hawakujali maumivu ya mwanamke yule na kuona kawaida. 

Wapo waliosikika wakisema hawa vichaa wana akili, wengine walisema hawa si vichaa, vichaa gani wana akili ya kutafuta hela hivi, wamekusanya umati mkubwa hivi na kuwafanya watu kutoa kile walichonacho. Mama mmoja mwenye busara anayeuza katika mgahawa huo aliyefahamika kwa jina la mama ndaga akasema“Jamani mimi nawafahamu hawa vichaa kwanza hawakuwa wakitembea hivi pamoja kama Dikidiki, huyo kaka unayemuona alikuwa..........pata mwendelezo kwa kujipatia kitabu hiki.

MAJAJI NCHINI WAAGIZWA KUMALIZA MLUNDIKANO WA MASHAURI IFIKAPO DESEMBA 15, 2017

Majaji nchini wameagizwa kumaliza kesi zote za muda mrefu Mahakamani ifikapo Disemba 15, mwaka huu ili kuendana na azma ya Mahakama ya kutoa haki  kwa wote na kwa wakati.
Akizungumza katika Mkutano wa Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Jaji Kiongozi Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali alisema kuwa Kanda zote za Mahakama Kuu nchini tayari zimeshaainisha idadi ya kesi zote za kuanzia miaka miwili kuendelea (kesi za mlundikano) ambazo zitafanyiwa kazi.
“Nawaagiza Majaji wote nchini kuendelea na zoezi la kusikiliza kesi hususani kesi za muda mrefu Mahakamani, na zoezi hili lianze kufanyika Oktoba 16,mwaka huu na kazi hii nataka ikamilike kufikia Desemba 15,mwaka huu,” alisisitiza.
Mhe.Jaji Kiongozi amezitaja Kanda za Mahakama Kuu ambazo zinaonekana kuelemewa na mzigo wa mashauri kuandaa orodha ya mashauri ‘causelist’wanayohitaji kusaidiwa.
Mahakama hizo ni Mahakama Kuu-Kanda ya Dar es Salaam, Mahakama Kuu-Kanda ya Mwanza, Mahakama Kuu-Kanda ya Bukoba, Mahakama Kuu-Kanda ya Mbeya, Mahakama Kuu-Kanda ya Shinyanga, Mahakama Kuu-Divisheni ya Ardhi na Mahakama Kuu-Divisheni ya Kazi.
Aidha Mhe. Wambali ameagiza zoezi hilo lifanyike ndani ya wiki moja kuanzia Jumatatu, Septemba 18 ili kuwezesha kujua uhitaji wa msaada wa Majaji wengine kutoka Kanda nyingine watakaoenda kusaidia kusikiliza na kumaliza mashauri hayo katika maeneo tajwa.
Aidha Mhe. Jaji Kiongozi amewataka Majaji Wafawidhi kuitisha vikao na Wadau wa Mahakama ili waweze kujua juu ya kuwepo kwa Programu maalum ya kusikiliza na kumaliza kesi zote za muda mrefu Mahakamani.
Kwa upande wake Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahimu Hamis Juma amewataka Majaji na Watumishi wa Mahakama kwa ujumla kufanya kazi kwa kuzingatia nguzo tatu za Mpango Mkakati wa Mahakama ili kutekeleza majukumu kimkakati na hatimaye kupata matokeo chanya.
“Majaji Wafawidhi ni nguzo muhimu katika utekelezaji wa Mpango Mkakati hususani katika nguzo namba mbili ambayo ni Upatikanaji na utoaji wa Haki kwa wakati, kupitia Majaji na Mahakimu waliopo chini yao” alisema Mhe. Jaji Mkuu.
Akiongelea juu ya jukumu kuu la utoaji haki nchini, Mhe. Jaji Mkuu amesisitiza juu ya kuwa na kumbukumbu sahihi ya takwimu za mashauri zilizopo katika Mahakama husika hali ambayo itawezesha kujua ni msaada utakaohitaji, bajeti na kadhalika.
Kwa upande mwingine Mhe. Jaji Mkuu amesisitiza juu ya matumizi ya TEHAMA katika uendeshaji wa kesi ili kuendeana na kasi ya Teknolojia hali ambayo itawezesha huduma ya haki kuwafikia wananchi kwa wakati.
Mambo mengine aliyoyasisitiza Mhe. Jaji Mkuu alipokuwa akifunga Mkutano wa Majaji Wafawidhi ni pamoja na ufanyaji kazi kwa ushirikiano kwa Watumishi wote wa Mahakama na kubadili mtazamo hasi ‘change of attitude’ na kuzingatia maadili katika utendaji kazi.
Mkutano wa Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, uliofanyika kwa siku mbili (2), Septemba 15&16 ni mwendelezo wa Vikao mbalimbali ambavyo vimekuwa vikifanyika mara kwa mara vyote vikiwa na lengo la kuhakikisha kuwa azma ya Mahakama ya Tanzania ya kutoa haki kwa wakati inaonekana kutekelezeka.
 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma akitoa neno alipokuwa akifunga Mkutano wa Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa-AICC jijini Arusha, Septemba, 15 na 16, 2017. 
 Sehemu ya Waheshimiwa Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu nchini wakimsikiliza kwa makini Mhe. Jaji Mkuu (hayupo pichani) 
Waheshimiwa Majaji Wafawidhi pamoja na Wasajili wakiwa katika Mkutano huo uliokamilika Septemba 16, 2017
 Waheshimiwa Majaji Wafawidhi pamoja na Wasajili wakiwa katika Mkutano huo uliokamilika Septemba 16, 2017
 Mtendaji Mkuu-Mahakama ya Tanzania,Mhe. Hussein Kattanga akitoa neno, akisisitiza juu ya ufanyaji kazi kwa malengo.
 Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali akiongea katika Mkutano wa Majaji Wafawidhi
 Mkuu wa Kitengo cha Mradi wa Maboresho ya Huduma za Mahakama,Mhe.Zahra Maruma akitoa mara ya utekelezaji wa kazi mbalimbali za Mradi mbele ya Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania.
Meza Kuu ikiwa katika picha ya pamoja na Majaji Wafawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania mara baada ya kuhitimisha kikao cha siku mbili cha kujadili juu ya mikakati ya kuondosha mashauri ya muda mrefu Mahakamani. aliyeketi katikati ni Jaji Mkuu wa Tanzania,Mhe. Prof. Ibrahim Hamis Juma, wa pili kushoto ni Jaji Kiongozi, Mahakama Kuu ya Tanzania, Mhe. Ferdinand Wambali, wa kwanza kushotoni Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu-Kanda ya Iringa pia ni Jaji namba moja wa Mahakama Kuu ya Tanzania, wa pili kulia ni Kaimu Jaji Mfawidhi,Mahakama Kuu, Kanda ya Arusha, Mhe. Sekela Moshi na wa kwanza kulia ni Mtendaji Mkuu-Mahakama ya Tanzania, Mhe. Hussein Kattanga.Picha na Habari na Mary Gwera wa Mahakama

BENKI YA CRDB YAKUTANA NA WAFANYABIASHARA WADOGO NA WA KATI MWANZA

Na  Binagi Media Group.

Benki ya CRDB leo imekutana na wafanyabiashara wadogo na wa kati mkoani Mwanza na kuwahakikishia kwamba itaendelea kutoa huduma bora ikiwemo mikopo ili kukuza mitaji yao.

Akisoma hotuba ya Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Dkt.Charles Kimei, Mkurugenzi wa CRDB tawi la Mwanza, Wambura Calystus amewahakikishia wafanyabiashara hao kwamba huduma za mikopo zitatolewa kwa wakati wote katika benki hiyo kwa kuzingatia kanuni za kibenki nchini.

Amesema benki hiyo imeendelea kutanua na kuboresha huduma zake ikiwemo uwepo wa Matawi 20, vituo vya kutolea huduma 50, ATM 135, mawakala wa Fahari huduma zaidi ya 649 katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.

Aidha amesema kwa mkoa wa Mwanza benki ya CRDB ina matawi manne, vituo vya huduma 13 pamoja na Mawakala wa Fahari Huduma zaidi ya 105 na hivyo kusaidia kuwafikia wateja wake kwa urahisi.

Baadhi ya wafanyabiashara waliohudhuria mkutano huo, Agapiti Malya pamoja na Doroth Baltazari wameipongeza benki hiyo kwa namna ilivyowawezesha kwa njia ya mikopo na kuinua biashara zao ambapo wameomba benki hiyo kuendelea kuboresha zaidi huduma zake ili kuwanufaisha wafanyabiashara wengi zaidi.

Baadhi ya wafanyabiashara (wajasiriamali) wadogo na wa kati walioshiriki mkutano ulioandaliwa na benki ya CRDB mkoani Mwanza kwa ajili ya kujadili pamoja masuala mbalimbali ya kibenki ili kusaidia kuboresha huduma zinazotolewa na benki hiyo. 
Mkurugenzi wa Benki ya CRDB Mkoani Mwanza, Wambura Calystus akizungumza kwenye ufunguzi wa mkutano huu, hii leo Jijini Mwanza
Meneja Mwandamizi wa benki ya CRDB, kwa wateja wadogo na wa kati, Elibariki Masuka akizungumza kwenye mkutano huo Jijini Mwanza
Meneja Biashara benki ya CRDB, Danford Muyango akizungumza kwenye mkutano huo
Mmoja wa watoa mada kutoka benki ya CRDB akiwasilisha mada kwenye mkutano huo
Mmoja wa watoa mada kutoka benki ya CRDB akiwasilisha mada kwenye mkutano huo
Mmoja wa watoa mada kutoka benki ya CRDB akiwasilisha mada kwenye mkutano huo
Washiriki wa mkutano huo wakifuatilia mada kwenye mkutano huo
Benki ya CRDB imeendelea kuwahakikishia wajasiriamali kwamba itaendelea kushirikiana nao kwa kuwapatia mikono yenye riba nafuu ili kukuza biashara zao
Mjasiriamali Doroth Baltazari ambaye ni mmiliki wa kampuni ya Chabati Pop Food, akiwaonyesha baadhi ya wanahabari bidhaa anazotengeneza.

WAFANYAKAZI 17 WA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA WA NCHINI UGANDA WAHITIMU MAFUNZO CHUO CHA MAMLAKA YA USAFIRI WA ANGA NCHINI (CATC).

Na Chalila Kibuda, Globu yaJamii

WAFANYAKAZI 17 wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga wa Nchini Uganda wamehitimu mafunzo ya kozi mbalimbali katika Chuo cha Mamlaka ya Usafiri wa Anga  nchini (CATC).

Akizungumza katika mahafali ya 270 ya Chuo hicho ,Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini (TCAA) , Hamza Johari amesema kuwa waliohitimu mafunzo katika chuo hicho wakatumie elimu ambayo italeta mabadiliko katika usafiri wa anga.

Amesema chuo cha CATC kinatambulika na Shirika la Usafiri wa Anga Duniani (ICAO) hivyo mafunzo yanayotolewa ni bora kutokana nakutambulika kwa nchi mbalimbali kuleta watalaamu wao kuja kujifunza masuala ya usafiri anga nchini Tanzania.

Hamza amesema tofauti kinachofanya kwa watalaam hao kuwa wameiva ni kuonyesha mikakati yauekelezaji kwa kile walichojifunza katika maendeleo ya nchi yao pamoja na Afrika Mashariki katika utoaji wa huduma ya usafiri wa anga.

Amesema mikakati iliyopo kwa chuo hicho ni kuingia ubia na Chuo cha Nchini Singapore kwa ajili ya kutoa mafunzo ya usafiri wa anga kwa nchi za Afrika hali ambayo itafanya Chuo kuongeza idadi ya wanafunzi wanakuja kusoma na kuifanya Tanzania kutambulika zaidi katika utoaji wamafunzo ya usafiri wa anga.

Nae Mkuu wa Chuo CATC, Dk. Daniel Karenge amesema kuwa wahitimu waliohitimu chuo hicho tangu kilipoanzishwa mwaka 2000 niwahitimu 3056 katoka nchi mbalimbali zaAfrika .

Amesema kuwa wanaopata mafunzo hayo kwa asilimia kubwa ni watu wa nje ya nchi hivyo amewasaa watanzania kutumia fursa ya kupata mafunzo ya usafiri wa anga katika chuo chao.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini (TCAA) , Hamza Johari akizungum za katika mahafali 270 ya Chuo cha Usafiri wa Anga CATC yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA),jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo cha Usafri wa Anga (CATC), Dk. Daniel Karenge akitoa taarifa ya Chuo hicho katika mahafali ya 270 yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga(TCAA), jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA), Hamza Johari akitoa cheti kwa Mhitimu wa Kozi ya Watoa Taarifa za Usafiri wa Anga, Stella Kabagenyi katika mahafali ya Mahafali ya 270 ya Chuo cha UsafiriwaAnga Tanzania(CATC) yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA, Jijini , Dar es Salaam.
Sehemu ya wahitimu wakionesha vyeti vyao katika mahafali ya 270 ya Chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA, Jijini , Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini (TCAA) , Hamza Johari akiwa katika picha pamoja na wahitimu wa Chuo cha Usafiri wa Anga Tanzania (CATC) katika mahafali ya 270 ya chuo hicho yaliyofanyika katika Ukumbi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga (TCAA, Jijini , Dar es Salaam.