Friday, November 17

USAID funded projects in Iringa voiced how keen their, in transforming people live

 The Chief of Party of the Sauti Project a Jhpiego’s lead program Dr. Albert Komba elaborating a point to the USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas when he visited projects interventions conducted to reduce HIV/Aids prevalence to the vulnerable groups in Iringa. The program is conducting Behavior Change Communication Sessions, Screening for Gender Based Violence and cancelling on usage of Alcohol and Drugs to the Vulnerable groups including young girls.
 Scholina Charles (22) a young girl from umoja groups in iringa giving her testimony to the USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas and his delegation on the risk she went through before joining the Sauti project to fight HIV/ AIDS. Looking center is the Sauti Project Chief of Party Dr. Albert Komba .
 The USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas,  Deputy Mission Director Helen Pataki (second right), Jhpiego Country Director (right) and Sauti Project Chief of Party Dr. Albert Komba (left) following a Behavior Change Communication Sessions conducted by Zera Mingo (23) to the young adolescences girls as part of HIV/ AIDS intervention to reduce HIV/Aids prevalence to the vulnerable groups in Iringa.
 The USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas and his Deputy Mission Director Helen Pataki looks at the clothes made by Mwanahamisi Mketo (23) during his field visit in Iringa to assess the implementation of USAID funded Project activities. Mwanahamisi Mketo she is a member of Behavior Change Communication group conducted by Jhpiego at kihesa ward in Iringa who are also economically empowered. 

The United State Agency for International Development (USAID) funded projects in iringa has demostrated how their bringing impacts to the lives of the people in Iringa. This expression was made by USAID funded NGO’s and local CSO’s to the newly USAID Mission Director in Tanzanian Andy Karas who conducted a field visit in Iringa to assess the implementation of USAID funded Project activities.

Andy who was accompanied by his deputy Mission Director Helen Pataki and other USAID staff expressed his appreciation to the regional administration and local authorities for the support their giving to all implementing partners funded by USAID in the region and thanks them for their work their doing for the people of Iringa.    

Explaining on how they engage the local authorities and the entire community to fight the spread of the HIV/AIDS in Iringa, the Chief of Party with Sauti Project a Jhpiego’s lead program Dr. Albert Komba said despite the fact that the project works in 14 region countrywide, in Iringa Municipal they targets all Vulnerable groups including young girls by  linking them into services like Behavior Change Communication Sessions, Economic Empowerment groups, Screening for Gender Based Violence and cancelling on usage of Alcohol and Drugs.

“we are working to ensure we reduce the spread of HIV/AIDS because the groups we are targeting like these adolescence girls and female sex workers are more vulnerable and engaging them in the fight against HIV will lead to an HIV/AIDS free generation in Iringa” said Dr. Komba

As part of their interventions to reduce HIV/Aids prevalence, the project also has mobilized girls to form WORTH+ groups which is the voluntary money saving groups for income generating activities, and train them on economic empowerment, gender issues and how to protect themselves against high risk behaviors of which most girls from these groups have managed to change their lives by living a decent life.

Reaching a testimonie delivered by Scholina Charles (22) a young girls from umoja groups on the risk she went through before joining the sauti project, she said the situation was devastating and because of her economic status from her family she got engaged into sex business as part of income generating.

“The situation was bad, I remember men used to bribe me even for two hundred shilling to have sex with them and I had no option. But now that I have joined this group, I am empowered with self-awareness on the risk of HIV/AIDS, gender violence, and through this group I have also managed to raise money and now I am engaging into agricultural activities and employ men in my maize farm”. Said Scholina.

Earlier speaking with USAID delegation and other USAID funded implementing partners, the Iringa Regional Administration Secretary Wamoja Ayubu thanks the delegation for the support they are giving to the region level by complimenting government effort in the health sector agriculture sector and other sectors especially by emphasizing the inclusion and empowerment of youth and woman. 

“The government has policy and laws which advocates for the inclusion of gender especially youth and woman in all activities, I am happy that USAID is also advocating that and we promise to collaborate with all partners to empower them especially locals so that they bring up new ideas for development and at the regional level. In our side we will chip in to address all challenges that might be faced by our implementing partners” she insisted.

Sauti is implemented by Jhpiego in partnership with Pact, Engenderhealth and NIMR/ Mwanza with support from the American people through USAID under the United States President’s Emergency Plan for AIDS Relief (PEPFAR) and DREAMS Initiatives.

MICHORO YA WATOTO KUTOKA TANZANIA WAZAWADIWA FINLAND

Michoro mitatu iliyochorwa  na watoto kutoka Tanzania hivi karibuni ilitunukiwa tuzo ya heshima ya vyeti vya stashahada ya maonesho na Taasisi ya Sanaa za watoto na vijana ya Hyvinkää, Finland.

Bryton Manyewa(10), Neev  Mistry (9) wa shule ya Academic International Primary na Mandela Mtaya (5) wa shule ya chekechea ya Upendo Montessori ndiyo waliofanikiwa kupata tuzo hiyo kwa upande wa Tanzania baada ya  kushiriki shindano la michoro liloitwa 'Pamoja' lililotayarishwa na taasisi hiyo ya nchini Finland.

Zaidi ya michoro 6800 toka katika nchi 66 duniani zilishiriki shindano hilo ambapo majaji ambao walikuwa ni wachoraji magwiji a sanaa wa nchi hiyo walichagua michoro 670 kushiriki katika maonesho yaliyoanza Oktoba mwaka huu na yatamalizika 18 Januari 2018 kwenye ukumbi wa Taasisi hiyo inayojihusisha na elimu ya Sanaa kwa watoto na vijana ukuzaji wa muingiliano wa utamaduni wa nchi mbalimbali. 

Maonesho hayo yanaweza pia kutazamwa katika mfumo wa Kidijitali kupitia tovuti ya Taasisi hiyo www.artcentre.fi

Katika miaka ya nyuma, kwa ufadhili wa ubalozi wa Finland nchini, baadhi ya watoto kutoka Tanzania waliweza kuhudhuria mafunzo ya Sanaa yanayotolewa na taasisi hiyo
 

MUHIMBILI YAADHIMISHA SIKU YA MTOTO NJITI DUNIANI


  Kaimu Mkuurugenzi wa Kinga katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Janneth Mghamba akizungumza kwenye maadhimisho ya mtoto Njiti Duniani ambayo huadhimishwa Novemba 17 kila mwaka. Kushoto ni Mkurugenzi wa Tiba Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Hedwiga Swai.
  Mkurugenzi wa Tiba Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Hedwiga Swai akizungumza na kinamama pamoja na wataalamu wengine wa afya katika siku ya mtoto njiti duniani. Kulia ni Kaimu Mkuurugenzi wa Kinga katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Janneth Mghamba, Kaimu Mkurugenzi Msaidizi wa Afya ya Uzazi na Mtoto katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dkt. Felix Bundara na Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Watoto, Dkt. Merry Charles.
 Baadhi ya kinamama wenye watoto njiti wakiwa kwenye maadhimisho hayo leo Muhimbili. 
 aktari Bingwa wa Watoto, Dkt Agustino Massawe akiweka saini kuthibitisha kuukoa maisha ya watoto njiti.

Serikali imesema imeweka mikakati endeleveu  ya kupunguza vifo vya watoto njiti kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya afya nchini.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Huduma za Kinga katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Neema Rusibamayila katika Siku ya Kimataifa ya Watoto Njiti ambayo huadhimishwa kila mwaka Novemba 17.

“Tanzania inakabiliwa na tatizo kubwa la vifo vya watoto wachanga chini ya mwezi mmoja hivyo kutokana na hali hii tunapaswa kudhibiti vifo kwa watoto wachanga,” alisema  Dkt. Rusibamayila.

Alisema takwimu zinaonyesha asilimia 13 hadi 17 ya watoto wote wanaozaliwa Tanzania ni njiti na kwamba kutokana na hali hiyo Serikali kupitia Wizara ya Afya, imekuwa ikiratibu progamu mbalimbali   za kupunguza  vifo vya watoto wachanga na wa chini ya miaka mitano.

Mkurugenzi huyo alisema moja ya program hizo ni kumsaidia mtoto kupumua baada ya kuzaliwa, kupanua huduma za watoto wachanga kwa kujenga wodi za watoto wachanga katika hospitali za manispaa na wilaya pamoja na kutoa mafunzo kwa wa hudumu wa afya jinsi ya ya kuhudumia watoto wachanga.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Profesa Lawrence Museru alisema kuwa hospitali hiyo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali inaendelea kutoa kutoa mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa wauguzi na madaktari wa kitengo cha watoto wachanga ili kuongeza ufanisi wa kazi.
“Pia tumeongeza wodi mpya ya watoto wachanga na kukarabati wodi ya za zamani ili kutoa huduma bora kwa watoto wengi zaidi. Sambamba na kuongeza wodi nyingine, pia tunatarajia kuzindua wodi maalumu ya watoto wachanga mahututi (NICU) katika maadhimisho haya. Ili kutapunguza msongamano wodini,” alisema Profesa Museru.

Profesa Museru alisema hospitali imepiga hatua kubwa katika kuboresha huduma kwa watoto wachanga kama vile kuongeza vifaa tiba katika kitengo cha watoto wachanga zikiwamo mashine za kusaidia watoto kupumua, dawa ya kukomaza mapafu kwa watoto njiti.

“Katika kuadhimisha siku hii muhimu kwa watoto, Hospitali ya Taifa Muhimbili inajivunia kuwa na wodi maalumu yenye wauguzi waliobobea kwenye kutoa huduma na mafunzo kwa kina mama wenye watoto njiti wenye uzito wa kuanzia gramu 500 kwa njia ya Kangaroo mother care. Nina imani kuwa wamama wote wanaolazwa wodi ya Kangaroo ni walimu na mabalozi wazuri kwa wa mama wenzao,” alisema Profesa Museru.

Profesa Museru Muhimbili imefanikiwa kwa asilimia kubwa kupunguza vifo vya watoto wachanga kutoka asilimia 19.8 mwaka 2015/2016 hadi asilimia 7.4 mwaka 2016/17.

“Idadiya watoto waliolazwa kwenye wodi ya Kangaroo walikuwa kati ya gramu 500 na kilo 1.5 na idadi kubwa ya watoto waliotunzwa katika wodi ya Kangaroo waliofanikiwa kutoka wodini na uzito wa kilo 1.6 hadi 1.7 ambayo ni sawa na asilimia 99.5 ya watoto wote waliolazwa wodi ya kangaroo.

Alisema changamoto ni upungufu wa vifaa tiba, gharama kubwa ya kununua dawa za kukomaza mapafu na idadi ndogo ya watoa huduma.

Serikali Yawakaribisha wawekezaji kutoka China kuja kuwekeza kwenye miradi mbalimbali ya madini nchini

Waziri wa Madini, Angellah Kairuki ametoa wito huo Novemba 16, 2017 Jijini Dar es Salaam alipokutana na Balozi wa China nchini Tanzania, Mhe. Wang Ke na ujumbe alioambatana nao Wizarani hapo kutoka kwenye Ubalozi huo ili kujadiliana masuala mbalimbali ya madini ikiwemo fursa za uwekezaji.

Waziri Kairuki alisema Tanzania imebarikiwa kuwa na rasilimali nyingi za madini na hivyo zipo fursa lukuki za uwekezaji ambazo zinaweza kutumiwa na kampuni za nchini China kwa manufaa ya pande zote mbili.

“Rasilimali za madini ni nyingi na hivyo zipo fursa mbalimbali ambazo zinaweza kutumiwa na kampuni za China na wakati huo huo kuchangia katika uchumi na pato la Taifa kwa ujumla,” alisema Waziri Kairuki.

Waziri Kairuki vile vile alisema yapo maeneo ambayo wawekezaji wanaweza kushirikiana na Serikali ambapo alitaja baadhi yake kuwa ni uchimbaji wa madini kwa kushirikiana na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), tafiti za utambuzi wa maeneo yenye madini kwa kushirikiana na Wakala wa Jiolojia Tanzania (GST) na Chuo cha Madini (MRI).

Aidha, aliongeza kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha madini yanayochimbwa nchini yanaongezwa thamani kabla hayajasafirishwa ili kukuza uchumi wa Taifa na wakati huo huo, kuongeza mapato ya Serikali na kuzalisha ajira zaidi.

“Madini yakiongezwa thamani hapa nchini, faida zitakazopatikana ni nyingi na ni kubwa ikiwemo ajira lakini pia mapato nayo yataongezeka kwa kuelewa thamani halisi ya madini husika,” alisema Waziri Kairuki.
Kwa upande wake Balozi Ke alipongeza juhudi za Serikali ya Tanzania katika kuwaletea wananchi wake maendeleo endelevu.

Alisema Serikali ya China itaendeleza ushirikiano wa karibu na wa dhati na Serikali ya Tanzania hususan kwenye Sekta ya Madini ili kuhakikisha sekta hiyo inaleta tija iliyokusudiwa kwa Taifa.

Alisema kampuni mahiri nyingi kutoka China tayari zimeonyesha nia ya kuwekeza kwenye Sekta ya Madini na ziko tayari kuja kuwekeza Nchini. 
 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kulia) akizungumza na Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke na ujumbe alioambatana nao (hawapo pichani) walipomtembelea Ofisini kwake jijini Dar es Salaam.
 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (kulia) akimsikiliza Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke alipomtembelea Ofisini kwake jijini Dar es Salaam ili kujadili masuala mbalimbali.
 Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke (kulia) akiwa na ujumbe wake kutoka Ubalozi wa China nchini Tanzania walipomtembelea Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (hayupo pichani) ili kujadili masuala mbalimbali ya Sekta ya Madini.

 Waziri wa Madini, Angellah Kairuki (wa pili kutoka kulia) akijadiliana jambo na ujumbe kutoka Ubalozi wa China nchini ulioongozwa na Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke (katikati).

SERIKALI YADHAMIRIA KUIMARISHA KAMPUNI YA TTCL

SERIKALI ya Tanzania chini ya Rais Dk. John Pombe Magufuli, imedhamiria kuiimarisha Kampuni ya Simu nchini (TTCL) iIi iweze kuingia kwenye ushindani wa kibiashara dhidi ya makampuni mengine ya simu.
Hayo yamesemwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa shirika hilo, Waziri Kindamba alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari Makao Makuu ya TTCL jijini Dar es Salaam.
Kindamba alisema hayo kufuatia Novemba 14, mwaka huu, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kujadili na kupitisha miswada ya mapendekezo ya mabadiliko ya sheria yanayofuta sheria iliyounda Kampuni ya Simu ya TTCL (Tanzania Telecomunication Company, Incoporation Act 2002) na kutunga sheria inayounda Shirika la Mawasiliano Tanzania (Tanzania Telecommunication Corporation Act 2017).
Aliongeza kuwa, kujadiliwa na kupitishwa kwa muswada huu bungeni kunafuatia hatua za awali za miswada ya serikali ambapo maoni ya wananchi na wadau wa huduma za mawasiliano yalikusanywa na kuchambuliwa.
Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu na Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni zilichambua muswada huu na kuutolea mapendekezo yao, ambapo Kindamba alisema mambo muhimu yanayotajwa katika sheria hiyo mpya ni pamoja na; Kuweka utaratibu utakaowezesha TTCL kutekeleza majukumu yake kama shirika la Umma. Kuweka jukumu la ujenzi, usimamizi na uendeshaji wa miundombinu ya kimsingi ya Taifa, Kuweka mazingira ya kinga ya mali (Asset) na miundombinu muhimu ya mawasiliano ya shirika na Kuanzishwa kwa shirika na kuainisha uongozi wa shirika.
Mambo mengine ni pamoja na Kuanisha vyanzo vya mapato na mtaji wa shirika, Kuanisha sheria zingine zitakazoguswa, Sheria kutumika pande zote za muungano na Kufuta kampuni ya simu Tanzania na kuanzisha shirika la mwasiliano Tanzania.
Kindamba aliongeza kuwa, katika mapendekezo ya sheria mpya yaliyoridhiwa na Bunge, Shirika la Mawasiliano Tanzania linapewa jukumu la msingi la kutoa huduma za mawasiliano kwa Taifa na kuhakikisha kuwa huduma hizo zinatolewa kwa viwango vya juu vya ubora.
Aidha, Kindamba alisema sheria mpya inataja jukumu jingine kuwa ni kusimamia na kuendeleza miundombinu ya Ki-Mkakati ya Mawasiliano kama vile Mkonga wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB), Kituo Mahiri cha kutunzia kumbukumbu (National Data Centre) na miundombinu mingine itakayokuja siku za usoni.
Awali majukumu hayo yalikuwa yanafanywa na TTCL kwa niaba ya serikali bila kutajwa katika sheria. Amesema, miongoni mwa upungufu ulioonekana katika sheria ya awali ni kuwa, sheria hiyo ililenga kuwezesha mazingira ya ubia ndani ya TTCL, hitaji ambalo sasa halipo tena kutokana na TTCL kurejea mikononi mwa serikali kwa asilimia mia moja.
Kupitia utaratibu huo wa ubia, kwa kipindi cha miaka 15, TTCL ilimilikiwa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa asilimia 65 na Kampuni ya Bharti Airtel ya India kwa asilimia 35.
Kaimu ofisa mtendaji huyo mkuu wa TTC L amesema, ubia huo ulifikia ukomo Juni 2016 baada ya Bharti Airtel ya India kulipwa jumla ya Tsh 14.7 Bilioni na kuondoka ndani ya TTCL.
Kindamba amesema hoja mahususi ni kwamba Shirika la Mwasiliano ni chombo muhimu katika ustawi wa nchi na kuongeza kuwa sheria mpya itaongeza ufanisi na tija katika shirika hilo ili liweze kuchangia zaidi katika maendeleo ya Watanzania wote.
“TTCL ni taasisi yenye hazina kubwa ya watendaji wenye weledi na uzoefu mkubwa wa shughuli za mawasiliano hapa nchini,” alisema Kindamba na kuongeza; TTCL imeonesha weledi na uzoefu mkubwa katika kusimamia na kuendesha Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano wenye mtandao wa takriban kilomita elfu saba na mia nne nchi nzima.
Aidha, Kindamba amesema TTCL inasimamia na kuendesha kwa ufanisi mkubwa kituo mahiri cha kuhifadhi kumbukumbu (National Data Centre) kinachohudumia taasisi 28, taasisi 19 za serikali na taasisi 8 za sekta binafsi hadi sasa. “Makampuni yote ya mawasiliano na wadau mbalimbali wa biashara wanaotumia huduma zaTTCL wanaridhika sana na huduma inayotolewa,” alisema Kindamba na kuongeza;
“Kuhusu kuipa mtaji TTCL, serikali imeandaa mpango mkakati wa miaka mitano 2017/18-2021/2022 ambao pamoja na mambo mengine utaainisha mtaji unaohitajika na serikali ambapo serikali itatekeleza mpango huo.”
Aliongeza kuwa, kuhusu idadi ya wajumbe wa bodi kutoka Zanzibar, serikali imeridhia idadi hiyo kuongezeka kutoka mjumbe mmoja na kuwa wawili.

Kindamba amesema ieleweke kwamba mabadiliko haya ya sheria kutoka Kampuni ya Simu Tanzania kuwa Shirika la Mawasiliano Tanzania hayaathiri mikataba na makubaliano ya kibiashara yaliyofikiwa awali kati ya TTCL na wateja na wadau wa huduma zake.
Amesema madeni ambayo TTCL inadai wateja wake na ambayo TTCL inadaiwa na watoa huduma mbalimbali yapo palepale na yataendelea kufanyiwa kazi kwa mujibu wa makubaliano na mikataba ya kiabishara iliyofikiwa.

“TTCL ipo imara na thabiti zaidi kuliko ilivyokuwa awali kwa kuwa sasa inatarajia kupata mamlaka zaidi na uwezo zaidi wa kuhudumia umma,” alisema Kindamba.
Akielezea mustakabali wa ajira za wafanyakazi wa kampuni hiyo baada ya mabadiliko hayo, Kindamba amesema ajira zao ikiwa ni pamoja na mali na miuondombinu viko salama.

Kindamba amesema huduma zinazotolewa na TTCL yaani simu za mezani, simu za kiganjani, data na TTCL PESA zinaendelea kutolewa kwa ufanisi mkubwa na kuongeza kuwa huduma za Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano (NICTBB) na Kituo mahiri cha kutunzia kumbukumbu (National Data Centre) pia zinaendelea kutolewa kama kawaida na kwa weledi wa hali ya juu.
“Kilichobadilika ni sheria ya kampuni ya simu Tanzania ambayo sasa ni shirika la mawasiliano Tanzania ambapo mapendekezo haya yanasubiri idhini ya mheshimiwa rais ili kuwa sheria kamili,” amehitimisha Kindamba.

KESI YA JALADA LA VIGOGO WA SIMBA LAREJESHWA TAKUKURU.


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Novemba 17, imeambiwa jalada la kesi inayowakabili vigogo wa Klabu ya Simba Evans Aveva na Godfrey Nyange maarufu "Kaburu" limeisharudi kutoka kwa (DPP) na limerejeshwa TAKUKURU

Hayo yameelezwa na wakili wa Takukuru, Leonard Swai mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa, wakati shauri hilo lilipokuja kwa kwa kutajwa.Wakili Swai alidai jalada hilo lilirudishwa juzi kutoka kwa DPP ambaye ametoa maelekezo ya kukamilisha zaidi upelelezi.

Upande wa jamhuri ulieleza hayo baada ya Wakili wa utetezi, Philemon Mutakyawa, kuhoji kuhusu jalada hilo la kesi ambalo lilielezwa kuwa kwa DPP, hivyo alitaka kujua lilipofikia.

Kesi hiyo imahirishwa hadi Novemba 30, mwaka huu,

Washtakiwa wanakabiliwa na mashtak uhujumu uchumi ikiwa na mashitaka matano na ya utakatishaji wa fedha

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha wa Dola za Marekani (USD) 300,000.

WANAODURUFU KAZI ZA SANAA KUFIKISHWA MAHAKAMANI.



 Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart imethibitisha kuwa Watuhumiwa wote waliokwamatwa kushiriki kufanya biashara ya kazi feki za sanaa watafikishwa Mahakamani kujibu tuhuma zinazowakabili.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Msama Auction Mart, Alex Msama amesema kuwa Watuhumiwa hao watapelekwa Mahakamani kutokana na kuwa na kesi ya kujibu.

Ameendelea kusema ni kosa kuuza Kazi za Wasanii hao ambazo hazina Stika ya TRA, kwani zinawakosesha Mapato Wasanii hao na Serikali kwa ujumla.

Amesema wataendelea na zoezi hilo kwa kupita maeneo yote kuhakikisha wanadhibiti uuzwaji wa kazi hizo feki.Kwa jana zoezi letu liliendelea maeneo ya Mbande, Mbagala, Buza Tandika na Chanika", amesema Msama.

Amesisitiza kuwa kazi za nje na ndani lazima ziwe na Stika ya TRA, pia amesema ni marufuku kuweka nyimbo za Wasanii, Kuburn CD na kuweka kwenye Flash.
 Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart inashirikiana na Jeshi la Polisi kwa ajili ya usalama, Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuendelea na kuikamisha shughuli hiyo,ambayo pia inatarajiwa kufanyika katika mikoa mbalimbali.
  Mkurugenzi wa Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart ya jijini Dar es salaam,Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari katika kituo kikuu cha Kanda Maalum Dar es salaam jana kabla ya kuanza kwa zoezi la kukamata wauzaji wa CD Feki katika maeneo mbalimbali ya ikiwemo eneo hatarishi kwa bishara hiyo la Kariakoo .
Baadhi ya watuhumiwa wakipandishwa kwenye gari na vifaa vyao.
 Mkurugenzi wa Kampuni ya Udalali ya Msama Auction Mart ya jijini Dar es salaam,Alex Msama akikagua baadhi ya CD kwenye moja ya duka.
Mmoja wa watuhumiwa akichukuliwa na na Askari baada ya kugundulika akiuza katika duka lake.
"Mfano huyu mmiliki wa duka hili, Leseni yake imeisha tangu 2014 mpaka leo na hajui taratibu zozote za kupata leseni mpya wala TIN number,bado anaendelea na biashara yake,kinyume cha sheria",alisema Alex Msama.

KWA MARA YA KWANZA UPASUAJI WA KUZIBUA MISHIPA YA MOYO KUPITIA MSHIPA WA DAMU WA MKONO (CATHETERIZATION) WAFANYIKA KATIKA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE (JKCI)

16/11/2017 Jumla ya wagonjwa 20 wamefanyiwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa upasuaji wa aina hiyo kufanyika hapa nchini.

Akiongea na Waandishi wa Habari leo jijini Dar Salaam Daktari bingwa wa magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge alisema upasuaji huo unafanyika katika kambi ya matibabu ya Moyo inayofanywa na Taasisi hiyo kwa kushirikiana na madakatari kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saudi Arabia.

Dkt. Kisenge alisema kuwa kambi hiyo inaenda sambamba na utoaji wa elimu na kubadilishana ujuzi wa kazi kati ya wafanyakazi wa Taasisi hizo mbili ikiwemo aina mpya ya upasuaji wanaoufanya kitu ambacho kinawajengea uwezo zaidi. ”

“Faida ya upasuaji huu ni kumwezesha mgonjwa kutoka chumba cha upasuaji akiwa anatembea na baada ya masaa manne kama hali yake inaendelea vizuri anaweza kuruhusiwa.“Tofauti na upasuaji wa kutumia mshipa wa paja ambao tulikuwa tunaufanya, baada ya upasuaji mgonjwa ni lazima akae Hospitali kwa zaidi ya masaa 24 ili kuangalia maendeleo ya afya yake”, alisema Dkt. Kisenge.

Kwa upande wake Daktari bingwa wa magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya IIRO Ali Al Masoud alisema kambi hiyo inaendelea vizuri kwani kwa siku wanatibu wagonjwa 10 na baada ya matibabu afya zao zinaimarika tofauti na ilivyokuwa kabla ya matibabu.Dkt. Masoud aliongeza kuwa wamekuja na utaalam mpya wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono ambapo kabla ya hapo matibabu yaliyokuwa yanafanyika ni ya kutumia mshipa wa damu wa kwenye paja.

Alifafanua, “Hivi sasa tunafanya upasuaji wa Moyo wa bila kufungua kifua kitu ambacho wenzetu hawa walikuwa wanakifanya. Sisi tumewaongeza utaalam mpya wa kutumia mshipa ya mkononi badala ya mshipa wa paja.

Naye Bader Alanezi ambaye ni Mtaalamu wa magonjwa ya Moyo na mishipa ya damu kutoka IIRO alimalizia kwa kusema kuwa wamepata muda wa kujifunza vitu vingi na kupata uzoefu mpya wa baadhi ya magonjwa na mambo ya kiteknolojia ambayo katika nchi yao hakuna.

Jumla ya wagonjwa 40 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ya siku tano ambayo imeanza tarehe 14 hadi tarehe 18 mwezi huu.

Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) na wenzao wa Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saud Arabia wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab katika kambi ya matibabu ya moyo inayoendelea kwenye Taasisi hiyo. Jumla ya wagonjwa 40 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ya siku tano.


Madaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge na mwenzake wa Taasisi ya Kimataifa ya Kiislamu ya Misaada (IIRO) ya nchini Saud Arabia Ali Al Masoud wakimfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab katika kambi ya matibabu ya moyo inayoendelea kwenye Taasisi hiyo. Jumla ya wagonjwa 40 wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji katika kambi hiyo ya siku tano.

Zoezi la kumfanyia mgonjwa upasuaji wa kuzibua mishipa ya moyo kupitia mshipa wa damu wa mkono (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab likiendelea. Picha na JKCI

Wakurugenzi wawili ndugu walivyopoteza maisha ajali ya ndege Ngorongoro

Maofisa wa vyombo vya usalama wakikagua mabaki
Maofisa wa vyombo vya usalama wakikagua mabaki ya Ndege iliyoanguka juzi eneo la Empakai ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro mkoani Arusha. Picha na Mussa Juma 
Ngorongoro. Ajali ya ndege ya kampuni ya Coastal Aviation iliyotokea juzi na kuua watu 11, imepoteza maisha ya wakurugenzi wawili wa kampuni maarufu ya utalii mkoani Arusha, Masai Wandering, Nassibu Mfinanga na Shatri Mfinanga.
Ndege hiyo yenye namba 5H-EGG aina ya Cessna Grand Caravan ilianguka baada ya kugonga kingo za Kreta ya Empakai umbali wa mita 3,250 kutoka usawa wa bahari ikitoka mkoani Kilimanjaro kwenda Hifadhi ya Serengeti kutokana na ukungu uliokuwa umetanda katika eneo hilo.
Wakurugenzi hao pamoja na mkuu wa idara ya kompyuta wa kampuni hiyo, Gift Lema walikuwa wakielekea Hifadhi ya Serengeti ambapo wanamiliki kambi za watalii kwa ajili ya kupiga picha ili kuboresha mtandao intaneti wa kampuni hiyo.
Wengine waliofariki ni pamoja na Joyce Mkama mfanyakazi wa Hoteli ya Serena, Simion Kombe ambaye ni mfanyakazi wa kampuni ya Mount Kilimanjaro na Moses Maina aliyekuwa mfanyakazi wa Hoteli ya Andbeyond.
Waliofariki wengine ni Mfalala Siyabonga aliyekuwa akifanyakazi Hoteli ya Bilila Serengeti na watalii Steinert Alexis, Lickttgen Katharina, Kauser Anita na Beranek Hubert.
Walifanya sherehe kabla
Akizungumza katika eneo la ajali, mpwa wa Nassibu, Rick Thomas alisema kabla ya safari hiyo Novemba 11, wakurugenzi hao walifanya sherehe maalumu ya kila mwaka na wafanyakazi wote na wageni iliyokwenda sambamba na kuchangia vituo vya watoto yatima jijini Arusha. Thomas alisema kampuni ya Masai Wondering inavilea vituo vya watoto yatima zaidi ya 10 katika mikoa ya Arusha na Manyara ambapo katika sherehe hiyo iliyopewa jina la ‘Asante Afrika’ kila tiketi iliuzwa Sh100,000.
Mfanyakazi mwingine wa kampuni hiyo, Mubarak Mkwepu alisema katika sherehe hiyo zaidi ya Sh15 milioni zilipatikana.
Alisema kuwa Nassibu ameacha mke na watoto wawili.
Ajali ilivyotokea
Kabla ya kuanguka ndege hiyo ilizunguka juu na kumwaga mafuta.
Mashuhuda waliozungumza na gazeti hili walisema kabla ya kuanguka ilizunguka angani kwa zaidi ya nusu saa katika eneo la milima ya bonde la Empakai ndani ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Lunda Mollel na Lengio Kilembi ambao ni wakazi wa Kijiji cha Sendiu walisema wakiwa machungani waliiona ndege hiyo ikizunguka juu na baadaye kuanguka.
Hata hivyo, walisema walianza kutilia shaka baada ya kuona inachukua muda mrefu na baadaye kurejea eneo la Kreta ya Empakai kwa kasi na kisha kugonga mlima na kuanguka.
Kilembi alisema wakati ndege hiyo ikiwa juu inazunguka waliona ikimwaga mafuta, jambo ambalo liliwashangaza. “Nadhani yule rubani alishindwa kutoka katikati ya milima kutokana na ukungu na ndipo alishindwa kuidhibiti ndege na kuanguka,” alisema Mollel.
Hata hivyo, alisema washindwa kwenda katika eneo hilo kutokana na umbali, lakini majira ya saa 10 jioni ndipo walianza kuona magari yakienda na wao walikwenda na kukuta watu 11 wakiwa wamefariki dunia. Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo alisema jeshi hilo kwa kushirikiana na mamlaka nyingine ikiwamo ya anga wanaendelea na uchunguzi wa ajali hiyo.
“Uchunguzi umeanza kujua chanzo na tayari kisanduku maalumu cha mawasiliano kimechukuliwa na wataalamu waliofika mara tu baada ya ajali,” alisema.
Hiyo ni ajali ya pili kutokea ikihusisha ndege za Coastal Aviation kwani wiki mbili zilizopita ndege nyingine ya kampuni hiyo iliangika katika eneo la Lobo Serengeti na kujeruhi watu wanne.

Duce walia na deni la Sh700 milioni

Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi Duce, Profesa
Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi Duce, Profesa Rwekaza Mukandala 
Dar es Salaam. Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (Duce) kinakabiliwa na deni la Sh700 milioni, lililotokana na mkopo uliotolewa na Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) ikiwa ni gharama za kusomesha wanataaluma.
Rais wa chuo hicho, Profesa William Anangisye alisema hayo kwenye mahafali ya kumi ya Duce jijini Dar es Salaam.
Alisema ili kukabiliana na madeni kutoka bodi hiyo, chuo kimeanzisha utaratibu wa kuwachuja wanataaluma wanaoomba kusomeshwa na bodi.
“Tumeanzisha uhusiano na vyuo rafiki nje ya nchi ili vitusaidie kusomesha wanataaluma hawa,” alisema.
Anangisye alifafanua kuwa huu ni wakati wa wanataaluma kutafuta ufadhili kutoka taasisi nyingine za kimataifa zinazotoa ufadhili ili wasomeshwe.
Alisema wanatumia fedha nyingi kuwalipa wahadhiri wa muda chuoni hasa katika masomo ya Fizikia, Hisabati, na Infomatiki.
“Hii ni changamoto kwetu, hata hivyo tumeanzisha utaratibu wa kuandaa mpango wa usomeshaji wa wafanyakazi uitwao Staff Training Plan utaowezesha chuo kutathmini mahitaji ya usomeshaji,” alisema.
Pia, alifafanua kuwa chuo kinakabiliwa na uhaba wa mabweni na kwamba wanafunzi 4,888 kati ya 5,300 wamekosa nafasi za mabweni na kuishi katika vyumba vya kupanga.
Mwenyekiti wa Bodi ya Usimamizi Duce, Profesa Rwekaza Mukandala aliwataka wahitimu kuacha kujenga mazoea ya kuajiriwa na badala yake watengeneze mazingira ya kujiajiri wenyewe ili kukabiliana na changamoto ya mrundikano wa wahitimu wasio na kazi mtaani.
“Mimi nasisitiza tu kuwa ni vizuri kwa wahitimu kufikiria kuajiriwa nje ya Serikali au sekta rasmi pekee,” alisema.
Alisema tatizo la wahitimu kutegemea ajira lipo katika nchi nyingi za Afrika na dunia kwa jumla, hivyo chuo kimeona ipo haja ya kuongeza mkazo katika elimu ya ujasiriamali ili kuwajengea uwezo wa kujiajiri.
“Kwa idadi hii, leo tunategemea mtafanya kazi kwa bidii na nidhamu, na kwa wale watakaoenda kuwa wajasiriamali mna mchango pia katika jitihada za kuwezesha mikakati ya kitaifa ya kuleta maendeleo ya viwanda na uchumi wa kati,” alisema.
Mkuu wa chuo hicho, Jakaya Kikwete aliwatunuku wahitimu 1,443 shahada za fani mbalimbali.

Walimu waliolala nje na kujikuta wamenyolewa wageuziwa kibao


Buchosa. Wananchi wa Kisiwa cha Soswa halmashauri ya Buchosa wilayani Sengerema wamewatupia mpira walimu waliojikuta wamelala nje kwa madai ya imani za kishirikina kuwa ni tukio la kutengenezwa.
Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara ulioitishwa jana Alhamisi kwa dharura kujadili suala hilo lililojitokeza usiku wa kuamkia Novemba 15, mwaka huu, katika viwanja vya shule ya msingi Soswa wananchi hao walisema tukio hilo ni la kutengenzwa ili kuishinikiza Serikali iwape uhamisho kutokana na mazingira magumu wanayokaa.
Mzee wa kisiwa hicho, Mashinga Boniphace (80) alisema hakuna ukweli juu ya tukio hilo kwani yeye pamoja na wazee wenzake waliangalia vibuyu na damu iliyokuwa imetapakaa ndani ya nyumba za walimu hao sio ya kishirikina.
“Walimu hao waliamua kuua ndege aina ya nyagenyange ili na kutapakaza damu hizo ndani ya nyumba zao pamoja na kwenye vibuyu ili kushinikiza uongozi wa juu kuwahamisha kutokana na juhudi zao za kuhama kugonga mwamba,”alisema Boniphance
Kauli ya mzee huyo wa mila ilipingwa na mkazi mwingine wa kijiji hicho, Mjula Magafu ambaye alisema suala hilo liangaliwe kwa kina kwakuwa limezua sintofahamu ndani ya kisiwa hicho na Taifa kwa ujumla.
Alisema kama walimu ndio walitengeneza tukio hilo wanapaswa kuchukuliwa hatua kwa kudanganya umma.
“Hapo awali lilipotokea tukio la nyumba zao kupondwa mawe walimu wote waliondoka na kubaki wawili ambapo hakukuwa na kitendo kama hicho, baadaye walimu waliokuwa wamesusia akiwemo mwalimu Daudi Shule na Wape Kisimu kitendo hicho kilijirudia tena na sasa wameamua kutengeneza tukio la kulazwa nje, tunapaswa kuchunguza kwa kina,” alisema Magafu
Baadhi ya wanafunzi waliozungumza na Mwananchi walisema tukio hilo limewaathiri kimasomo hivyo kushindwa kufanya vizuri kwenye mitihani yao.
Mwanafunzi wa darasa la tano, Malisela James aliiomba jamii ikubali kuwa walimu hao wamefanyiwa vitendo vya kishirikina na kwamba watafute namna ya kukukomesha ili kuwapa fursa ya kuendelea kusoma.
Mwenyekiti wa kamati ya shule, Lidia Buluba alilaani kitendo hicho ambacho kinahisishwa na imani za kishirikina huku akiwatupia lawama baadhi ya walimu waliotengeneza jambo hilo ili wapatiwe uhamisho kwa madai kuwa mazingira wanayoishi si mazuri.
Mwalimu Daudi Shule ambaye anapatiwa matibabu ya asili katika kijiji cha mwangakia yeye alidai alinyolewa sehemu za siri, mwalimu  Ernest Katunzi alithibisha kwa kumwona sehemu hizo kuwa amenyolewa pamoja na mwalimu Wape Kisumo aliyonyolewa nywele  kichwani  kwa pamoja walisema kuwa wanafanyiwa vitendo vya kishirikina  hata kipindi wanapondwa mawe jamii hiyo haikuamini.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo, Petro Lukas alisema maneno yanayosemwa na jamii hawawezi kuyaamini na haamini kama walimu wametengeneza mazingira ya tukio hilo ili wahame kwa kuwa kazi yao ni kufundisha.
Mtendaji wa Kata ya Bulyaheke, Musa Mwilomba alisema kuwa anaiomba jamii kutokutupiana mpira juu ya tukio hilo na kwamba wanatakiwa kusameheana na kusahau kilichotokea ili kuanza sura mpya na walimu waendelee kufundisha.
Mkaguzi wa shule wilayani Sengerema, Elly Msulu aliyefika katika Kisiwa cha Soswa kupata ukweli juu ya tukio hilo aliitaka uchunguzi zaidi ufanyike kujua ukweli wa tukio hilo na watakaobainika hatua kali za kisheria dhidi yao zitachukuliwa huku akiwaomba walimu kuwa wavumilivu wakati suala hilo linatafutiwa ufumbuzi.

PITIA VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO NOVEMBA 17,2017