Friday, November 17

KESI YA JALADA LA VIGOGO WA SIMBA LAREJESHWA TAKUKURU.


Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Novemba 17, imeambiwa jalada la kesi inayowakabili vigogo wa Klabu ya Simba Evans Aveva na Godfrey Nyange maarufu "Kaburu" limeisharudi kutoka kwa (DPP) na limerejeshwa TAKUKURU

Hayo yameelezwa na wakili wa Takukuru, Leonard Swai mbele ya Hakimu Mkazi, Godfrey Mwambapa, wakati shauri hilo lilipokuja kwa kwa kutajwa.Wakili Swai alidai jalada hilo lilirudishwa juzi kutoka kwa DPP ambaye ametoa maelekezo ya kukamilisha zaidi upelelezi.

Upande wa jamhuri ulieleza hayo baada ya Wakili wa utetezi, Philemon Mutakyawa, kuhoji kuhusu jalada hilo la kesi ambalo lilielezwa kuwa kwa DPP, hivyo alitaka kujua lilipofikia.

Kesi hiyo imahirishwa hadi Novemba 30, mwaka huu,

Washtakiwa wanakabiliwa na mashtak uhujumu uchumi ikiwa na mashitaka matano na ya utakatishaji wa fedha

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashitaka ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha wa Dola za Marekani (USD) 300,000.

No comments:

Post a Comment