Wednesday, October 26

Wachina Wawili Wadakwa kwa Kumteka Mwenzao

DAR ES SALAAM: JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata Wachina wawili, Wang Young Jing (37) Chen Chung Bao (35) kwa makosa ya utekaji nyara jijini Dar katika eneo la Palm Beach Hotel.


Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, CP Simon Sirro, akilionyesha gari hilo lililokuwa limeibwa kwa wanahabari (hawapo pichani).
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Kanda Maalum Dar es Salaam, CP Simon Sirro, amesema watu hao walimteka raia wa China mwanamke aitwaye  Liu Hong (48) ambaye alikuwa ni mfanyakazi wa  Le Grande Cassino waliyemteka Oktoba 23 mwaka huu ambapo  polisi walimkuta akiwa ndani ya chumba cha Hotel ya Palm Beach iliyoko Upanga jijini Dar es Salaam na walimkamata pia mtu aliyekuwa amekodi chumba hicho.

…Akizungumza na wanahabari (hawapo pichani).
Alifafanua kuwa Oktoba 24 majira ya saa kumi na moja jioni kikosi kazi cha wizi wa makosa ya kimtandao cha polisi kilifanikiwa kumtia nguvuni raia mmoja  wa China akiwa ndani ya chumba cha hoteli hiyo baada ya kuvunja mlango.


Madawa ya kulevya aina ya mirungi yaliyokamatwa na jeshi la polisi kwenye operesheni hiyo.
Sirro alisema baada ya kufungua chumba hicho walimkuta raia aliyetekwa akiwa hajitambui na akiwa na majereha usoni, pia palikutwa vipande vya taulo vyenye damu vilivyotumika kumfungia mikono ambapo alichukuliwa na kukimbizwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili kwa ajili ya matibabu.
Ameeleza kuwa sababu kubwa ya utekaji nyara huo ilikuwa kumtaka majeruhi huyo atoe YEN 100,000 ambazo ni  sawa na dola za Marekani 19,000.
…Sirro akionyesha mitambo ya kutengenezea pombe aina ya gongo iliyokamatwa wakati wa operesheni.
Katika hatua nyingine Sirro amesema kuwa wamefanikiwa kukamata wezi wa magari na kupatikana kwa gari la ofisa wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania, Mkoa wa Morogoro, Capt. Innocent  Philipo Dallu ambaye alikuwa ameegesha gari lake maeneo ya Mbezi Juu akitokea kanisani  kwa ajili ya kuingia kwenye duka la vifaa vya ofisini na mashuleni ambapo gari hilo liliporwa.
…Akionyesha baadhi ya funguo bandia zilizokamatwa katika oparesheni hiyo.
Amesema jeshi lake  limefanikiwa kulikamata gari hilo aina ya Toyota Harrier lenye namba za usajili T 400 DEH huko Kiwangwa, Bagamoyo mkoani Pwani likiwa na watu wawili ambao ni  Ezekiel David (25) na Geofrey Nkwabi (52) na upelelezi utakapokamilika watuhumiwa watafikishwa mahakamani.


Mwijage Kuzindua Maonyesho ya Magari Dar


Mratibu wa maonyesho hayo, Ally Nchahaga (wa kwanza kulia) akizungumza na wanahabari.
WAZIRI  wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Charles Mwijage, atakuwa mgeni maalum katika kuzindua tamasha la  maonyesho magari nchini lijulikanalo kama Automotive Festival (Autofest) linalotarajiwa kuonyesha magari mapya na ya kisasa katika viwanja vya Biafra, Kinondoni,  jijini Dar es Salaam kuanzia Oktoba 28 hadi 30 mwaka huu.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Mratibu wa Maonyesho hayo, Ally Nchahaga, amesema tamasha hilo litakuwa na matoleo mapya ya kila aina ya magari kama vile magari ya abiria, ya biashara, bodi za magari, mashine zinazohusiana na magari sambamba na pikipiki za kisasa na burudani mbalimbali za kusisimua zitakazofanywa katika kuyaendesha magari na kurukisha pikipiki juu kwa mbwembwe na kadhalika.
“Tukio hili linahusisha moja ya maonyesho muhimu na yenye mvuto katika ulimwengu wa vyombo vya moto na lengo letu ni kuendelea kuleta aina mbalimbali ya bidhaa za vyombo vya moto na huduma kwenye ‘Autofest’ ili wadau wapate kujifunza na  kufurahia na kukidhi tamaa yao kwani magari yatakayokuwepo yanatumia teknolojia mpya na si ya zamani,” alisema Nchahaga.
Aidha alitaja viingilio katika tamasha hilo kuwa ni 10,000/= kwa sehemu ya kawaida, 5,000/= kwa watoto,  40,000/= ni kwa tiketi za  VIP na 100,000/= kwa tiketi za musimu.
Kaulimbiu ya tamasha hilo ni “Kuendesha tunaelekea wiki ya usalama barabarani, ni muhimu madereva kutoa fursa kwa madereva wenzao hata kama una haki”.

MFALME MOHAMMED VI WA MOROCCO AWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA MSIKITI


Mfalme Mohammed VI wa Morocco akibusu Masahaf kabla ya kumkabidhi Waziri Mkuu Kasim Majaliwa katika hafla fupi ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa msikiti kwenye eneo la BAKWATA Kinondoni jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016.  Kulia ni Mufti Mkuu wa Tanzania, Abukary Zubeir. Jumla ya Masahaf 10000 zilikabidhiwa na Mfalme huyo.(Picha n Ofisi ya Waziri Mkuu)


Mfalme Mhammed  VI wa Morocco na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa  wakishuhudia wakati Mufti Mkuu wa Tanzania, Abubakary Zubeir (kulia)  akitia saini Makubaliano ya ujenzi wa Msikiti kwenye eneo la BAKWATA, Kinondoni jijini Dar es salaam Oktoba 25, 2016. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)


Mfalme   Mohammed VI wa wa Morocco,  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa , Rais Mstaafu Alhaj  Ali Hassan Mwinyi na Makamu wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohammed Bilal wakiwa katika hafla fupi ya uwekaji jiwe la msingi la ujenzi wa msiki uliofnywa na Mfalme Mohammed wa Morocco kwenye  eneo la BAKWATA, Kinondoni jijini Dar es salam Oktoba 25, 2016. (icha na Ofisi ya Waziri Mkuu)