Saturday, May 12

ELIMU YA MADRASA TANZANIA:

BISMILLAHIR RAHMANIR RAHIIM
Historia, Matatizo na Taaluma za Walimu
MUHTASARI:
- Madrasa na Kazi zinazonasibishwa nazo.
- Historia ya Elimu ya Madrasa Tanzania.
- Sahihisho kwa madrasah zetu.
- Taaluma muhimu kwa walimu na madrasah.
· Njia na mbinu zakufundishia.
· Uendeshaji wa Madrasah kwa ujumla.
· Saikolojia ya watoto na malezi.
· Maarifa katika fani wanazofundisha.

1.0 UTANGULIZI

1.1 Neno la Awali
Kwa muda mrefu sasa taasisi muhimu ya kiislam, taasisi ya “madrasa” imeachwa na kupoteza hadhi yake. Pamoja na hilo, taasisi hii imeacha pengo kubwa ambalo halizibiki kwa urahisi ila kwa kuinua hadhi ya Madrasa zetu.
Umma wa Waislam unazidi kupata kizazi kinachokosa haki za kimsingi za kuandaliwa kama madhalifa. Mwenyezi Mungu katika Qurani 51:56 ametwueleza “SIKU WAUMBA MAJINI NA WATU ILA WANIABUDU” ili kutekeleza lengo hilo, waislamu lazima waipe hadhi Madrasa. Kadhalika ili kufikia hadhi yetu wanaadam kama inavyoelezwa katika Quran 2:30 waislam lazima tuipe madrasah, hadhi yake sahihi. Kwa sababu hizo, kuna haja ya kufanya fikra juu ya kuinua hadhi ya madrasa zetu kwa ajili ya kuuendeleza umma wa kiislam utapotea na kuacha wanaoitwa Waislam lakini ummah wa kiislam haupo.

1.2 Maana ya Madrasa
Ilivyozoeleka, madrasa ni kituo cha kiislam ambapo watu hupata elimu juu ya mambo ya msingi katika uislam. Wengine wameita Shulel za Quran, wengine wamesema, vyuo vya Quran, na wengine wanaelewa kuwa madrasa ni vituo vya watoto ambapo masomo ya Quran, kusoma na kukandika hufundishwa.

1.3 Kazi zinazonasibishwa na Taasisi ya Madrasa
Madrasa zetu Tanzania, kwa muda mrefu tangu Historia ya kuingia kwa uislam nchini zimenasibishwa na kazi zinazofanywa na taasisi hii. Kwa ujumla madrasa zetu zimejikita katika taaluma zifuatazo:-
(i) Kuandika herfu za kiarabu.
(ii) Kuzisoma herfu za kiarabu.
(iii) Kutafsiri llugha ya kiarabu.
(iv) Kusoma Quran kwa ghaibu au kwa kutazamia.
(v) Jinsi ya kufanya ibada maalum na kanuni zake. Mfano, ibada, swala, swaum, hija na utoaji zakat na sadakat.

1.4 Athari za Madrasa kujikita katika shughuli hizo
Kwa kuwa Madrasa ni vituo vya elimu ya kiislam, na kwa vile madrasa zinaoa elimu hizo tu, basi elimu ya kiislam inafahamika kuwa ni ile tu inayohusiana na:
- Kusoma na kuandika Quran.
- Kukariri sura za Quran na tafsiri zake.
- Kanuni za utekelezaji wa nguzo tano.
- Kukariri hadithi kadhaa za Mtume (s.a.w).
- Kukariri visa vilivyo katikak lugha ya kiarabu.
Matokeo ya hilo, Uislam nao umeeleweka kukwa ni mambo ya kimaisha yanayohusiana na shughuli hizo tu. Nje ya shughuli hizo si vitu vya lazima katika uislam. Mfano kuksimamisha dola ya kiislam.

2.0 HISTORIA YA ELIMU YA MADRASA TANZANIA KWA UFUPI
Ø Historia ya Elimu ya Madrasa Tanzania inanasibiana na Historia ya kuenea kwa uislam katika Afrika Mashariki kuanzia Pwani hadi bara.
Ø Elimu itolewayo na Madrasa zetu ilichipuka tangu wakati walivyoanza kuja Waarabu kutoka Saudia, Oman, Uajemi, Hadhramaut na Yemen.
Ø Karne ya 9 na 10 wahamiaji kutoka Saudia walianza kusihi BENADIR (Pwani ya Somalia).
Ø Karne ya 12 Waarabu wageni (Afro-arabs) walianza kufika hadi mji wa Kilwa.
Ø Karne ya 12 wageni kutoka Hadhramawt na Yemen waliingia Afrika Mashariki. Wageni hawa nao pia walitoa elimu inayohusu uislam. Lakini kufahamu uzito wa elimu waliyoitoa kunategemea ufahamu wa sababu zilizowaleta Afrika Mashariki. Hawakuja kueneza uislam na kuufundisha uislam. Bali wali kuja kutokana na:
(i) Njaa iliiyokuwapo Arabuni wakati huo.
(ii) Ukame huko Arabuni.
(iii) Ukandamizaji wa Kisiasa uliotawala huko.

2.1 Kustawi kwa Elimu ya Madrasa Afrika Mashariki
Ø Mwaka 1332, Mwarabu aitwaye IBN BATUTA alipotembelea Kilwa alikuta mji umekaliwa waliokuwa wakitumia lugha ya Kiswahili.
Ø Baadaye miji ya Tanga, Dar-es-Salaam, Mombasa, Lamu, Malindi, na Mikindani vikawa vituo vya kueneza uislam na elimu ya kiislam katika miji ya Tanzania, Kenya, Uganda, Rwandda, Zaire, Msumbiji, Malawi na Burundi.

2.2 Maarifa yaliyotolewa na njia za kufundishia
Ø Maarifa yaliyotolewa na kuonekana hayo ndiyo maarifa ya uislam ni pamoja na:
(i) Zipi ni nguzo za imani na maana yake.
(ii) Zipi nguzo za Swala na maana yake.
(iii) Namna ya kusoma Quran, lugha ya kiarabu na vira kadhaa.
(iv) Sirah ya Mtume (s.a.w)
(v) Kanuni zinazotawalal utendaji wa Ibada Maalumu.
Ø Maarifa haya yalifundishwa kwa njia kuu ya Kipurure. Mwanafunzi hakusoma kwa kuwa mdadisi sana. Wanafunzi walikasirishwa waliyofundishwa.
Ø Walimu wa kufundisha hayo, ni wale tu, walioonekana wanaweza kuyasoma hayo. Hakukuwa na mazingatio kuhusu uwezo na ujuzi wa mfundishaji kufikisha maarifa anayoyatoa.
Ø Kwa sababu hizo, pia njia kuu ya kudhibiti nidhamu, ilibaki kuwa ni viboko tu.
Ø Kwa ujumla taaluma kuu za elimu ya Madrasa zilizotawala ni KUSOMA, KUANDIKA, KUIFADHI na KUIGA ambazo zilitolewa na walioweza kuzipata taaluma hizo.

2.3 Dosari za Elimu ya Madrasa iliyotolewa wakati wa Waarabu
Utangulizi
Ø Dosari hizo zimetokana na asili ya kuenea kwa dini na elimu ya Kiislam Afrika Mashariki, hususan Tanzania.
Ø Tatizo linakuja kwa vile Uislam na elimuk ya Kiisam:-
(i) Vilenea katika taratyibu za walioeneza kkujitafutia maisha yao wala si kwa madhumini ya kufanya umisionari.
(ii) Vilienezwa na wailam ambapo hawakuwa na maandilizi ya kufanya hivyo hivyo hakukuwa na matayarisho yoyote ya malengo ya kieleimu.
Ø Matokeo yake uislam ulifundishwa ili kupata wenzi na washirika katika mas[ala ya kijamii kama vile:
o Misiba
o Harusi n.k..
· Utangulizi

(i) Zilifundishwa Taaluma chache tu.
Mfano: Kusoma, Kuandika, Kukariri Quran.
Taaluma hizo si pana kiasi cha kuwawezesha wanafunzi kuuhani uislam kifikra, au vyovyote Taaluma hizo hazimwezeshi mwanafunzi kumudu changamoto zinazoibuka kila kukicha; Japo uislam haushindwi na changamoto yoyote ile.
(ii) Njia za kuendeleza nidhamu, na maadili zilikuwa viboko tu, ukali tu, pasi na kuchunguza tatizo kwa lengo la kkuondoa tatizo hilo na kusaidia.
(iii) Njia za kkufundishia hazikuzingatia umuhimu wa kuendeleza na kuhusisha nyanja tatu za kujifunza.
(a) Nyanja ya ung’amuzi (Cognitive domain).
(b) Nyanja ya matendo (Psychomotoar domain)
(c) Nyanja ya kuhusisha (Affective domain)
Kila nyanza hapo inaumuhimu katikak uislam wa mtu mmoja mmoja au jamii na hatimaye Ummah.
(iv) Hakukuwapo chombo maalum cha kijamii, kinachosimamia swala zima la utoaji wa Elimu hii. Matokeo yake kila mmoja alifundisha kadiri na namna alivyodhani ni sawa.

2.4 Athari za dosari hizo
(i) Kukosekana kwa taaluma muhimu za kifiqih
Mfano:
- Taaluma inayowezesha kkuhusianisha mazingira na fatwa kadhaa za kifiqih.
- Taaluma inayofafanua hukumu kadhaa za kifiqih na yanayotokea katika maisha. Katika hili, kumekosekana taaluma ya kubainisha tofauti ya RIRA na HIBA.
(ii) Watu wachache sana ndio waliweza kwendelea na elimu ya Madrasa kwa
kiwango cha juu kwa kulinganisha na waislam wengine.
Mfano:
Ni Masheikh wachache waliweza kkufikia kiwango Fulani. Matokeo hata vitu vidogo vidogo kuweza kufahamika kwa waislam wote, vinafahamika na masheikh tu.

(iii) Kuibuka kwa Matabaka miongoni mwa waislam kutokana na dosari hizo,
kumeibuka matabaka kadhaa mingoni mwa waislam.

Mfano:
o Tabaka la wasomi wa elimu katika mfumo huu wa madrasa tu.
o Tbaka la waliosoma elimu ya madrasa kidogi na elimu ya kisekula kidogo.
o Tabaka la waliosoma kiasi elimu ya kisekula na kukosa elimu ya madrasa lakini badaye (ukubwani) wakajifunza elimu ya uislam kwa mfumo mwingine.
Mahusiano ya matabaka haya hayasaidii kuendeleza uislam na waislam wa kiislam, ni sumu kwa maendeleo ya jamii ya kiislam.

3.0 MATATIZO YANAYOIKABILI ELIMU YA MADRASA TANZANIA
i) Utangulizi
Taasisi ya Madrasah inazidi kukpoteza hata hadhi yake ndogo iliyokuwa nayo.
Mfano:
Jamii haiipi hadi na thamani stahiki licha ya kuwa madrasa ni taasisi muhimu katika kurithisha mila, na mfumo mzima wa uislam toka kizazi hadi kingine. Wazazi wa watoto wa kiislam leo hii hawana hari ya kupeleka watoto wao kwenye vituo vya madrasa. Wala wazazi hao hawana hata haja ya kujua mikati ya madrasa zinazowazunguka.

(ii) Matatizo

Matatizo yanayoikabili elimu ya madrasa ni:

3.1
Matatizo ya Kitaasisi (Institutional Problems)

(a) Hakuna mfumo wa uendeshaji elimu ya madrasa. Mfumo huo
Mfumo huo hautoi picha halisi juu ya nani hasa ndiye mratibu au msimamizi wa elimu ya Madrasa. Kwa sababu hiyo hakuna upimaji wala tathimini yoyote ili kuelewa mustak bal wa elimu hii muhimu
(b) Kukosekana kwa “usare” (uniformity) katika ufundisjaji.
Matokeo yake anapohama motto kwenda madrasa nyingine anaathirika kitaaluma.
(c) Hakuna utaratibu fasaha/muafaka wa kuwahusisha wazazi wa Kiislam katika kujadili maendeleo na kutathimini uendeshaji wa madrasa. Athari yake ni wazazi kutojihusisha na uendelezaji wa madrasa zetu na ufuatiliaji wa taaluma muhimu zipatikanazo.
(d) Kukosekana kwa utaratibu wa kubadilishana mawazo baina ya walimu tofauti tofauti, juu ya uboreshaji wa njia za ufundishaji na mafanikio katika uendeshaji madrasa.
(e) Kukosekana kwa mipango inayohusiana na madrasa, wanafunzi na walimu. Athari yake ni kupungua kwa idadi ya wanafunzi na walimu wa madrasa.
(f) Kukosekana kwa utaratibu maalumu juu ya vigezo vinavyomuwezesha mtu kuwa mwalimu. Kwa kawaida yeyote anayejua kusoma na kuandika herufi za kiarabu, kusoma Quran na mambo kadhaa katika Ibada maalumu za kifiqih, aweza kuwa mwalimu hata kama sifa za kitabia, na uwezo wa kkurithisha elimu kwake ni vikwazo.

TANBIH:
Aina za walimu zaweza kkuwa kama ifuatavyo:-
(i) Mwenye sifa (Qualified) – Anazo sifa kitabia, anaweza na ujuzi wa kkufundisha na ana elimu.
(ii) Mwenye sifa (Underqualified) – Anayo elimu ila hana mbunu bora za ufundishaji.
(iii) Asiye na sifa (Unqualified) – Hana sifa hata kidogo. Huyu ni hatari sana.

Matatizo ya Kijamii
(a) Fikra za watu juu ya elimu ya madrasa na thamani yake
- Jamii na mtu mmoja mmoja wanachukulia elimu ya msingi ya madrasa ni kusoma Quran na kujua kanuni muhimu za utekelezaji wa Ibada maalumu kama vile Swala, hija, swala ya maiti, kushona sanda na kadhalika.
- Athari yake ni kuwa, mara baada ya watoto kufikia ngazi hiyo huonekana imetosha na kwamba, wana elimu ya kutosha juu ya uislam. Elimu kuhusu uislam inapungua miongoni mwa waislam.
(b) Uchumi duni kwa wazazi na walimu
- Umaskini na kipato kidogo kwa walimu wa madrasa inakuwa tatizo kubwa kwa uendeshaji wa madrasa zetu. Hali hii husababisha walimu wa madrasa kutenga muda kidogo sana kwa ajili ya kazi ya madrasa. Kadhalika kujituma juu ya kuboresha madrasa hupungua.
- Vile vile pato la wazazi kuwa dogo huchangia tatizo. Mara nyingi watu wenyekipato cha chini ndio wanaopeleka watoto wetu madrasa na wenye uwezo na wito wa kiislam wao huwaajiri walimu wa kuwafundisha watoto nyumbani. Kwa sababu hiyo, wazazi wengi hawana uwezo wa kkuchangia fedha muhimu kwa ajili ya madrasa. Wakati mwingine mchango wao huwa kidogo na mgumu kupatikana.
- Athari ya hayo, ni kudorora kwa madrasa zetu na kupatikana kwa watoto, mabarabara, vijana wasio na elimu sahihi ya msingi kuhusu uislam na hatimaye kuporomoka kwa maadili.
(c) Mfumo wa elimu ya nchi na utaratibu wa kisekula
Mfumo wa elimu ya kisekula umembana kiasi motto anayesoma madrasa kutokana na utaratibu ulivyo. Uendeshaji wa elimu ya kisekula umezaa desturi ya “Tuition” (masomo ya ziada), desturi amabyao sit u inamfanya motto achoke bali pia inamkosesha muda wa kuhudhuria katika madrasa zetu.

Mfano:
Mtoto wa darasa la kwanza na pili wanaingia shule kwa zamu, mara asubuhi, mara saa tano, mara mchana. Hii inaleta ugumu kwa madrasa kuratibu jinsi ya kuwasaidia watoto.
Mtoto wa darasa la kwanza atokapo shule, anapumzika kidogi, kasha anaenda “Tuition” masomo ya zaida.
Mtoto wa darasa la tano hadi saba, anakosa muda kabisa. Muda wote, kutwa mzima anashughulishwa na elimu ya kisekula na usiku anajisomea nyumbani.
Athari ya tatizo hili ni kushuka kwa mahudhurio ya watoto katika madrasa zetu, na mara nyingine kuwapo kwa mahudhuria yasiyotabirika na kuelezeka. Mara kuna mahudhurio ya kuridhisha mara mabaya.
(d) Shughuli za Kijamii miongoni mwa Waislam
- Ndani ya jamii ya Kiislam, inapotokea shughuli kama vile harusi na kadhalika, madrasah nyingi kuhusishwa. Mfano kuandaa kaswida kwa ajili ya maulidi harusini. Hili hupunguza za muda wa ufundishaji na kujifunza katika madrasa zetu.
- Athari yake ni kuongezeka kwa tatizo katika madrasa zetu. Wazizi wengine huona kua hakuna haja ya watoto kusoma madrasa hizo.

4.0 SOLUHISHO KWA MADRASA ZETU

4.1 Utangulizi
- Ni vigumu kuliondoa tatizo hili kwa kulifanya jukumu hilo kuwa la watu Fulani tu. Mfano, kulifanya liwe jukumu la masheikh tu, au jukumu la walimu tu, au la wazazi tu. Inapaswa kuwa ni tatizo linalomgusa kihisia kila muislam.
- Kwa hakika elimu hii ni muhimu sana kwa maendeleo ya uislam na waislam kiitikadi, kitaaluma, kielimu n.k.

4.2 Mfumo
- Kunahaja ya kuudhurusi mfumo wa elimu ya madrasa na kuangalia namna ya kuuendeleza na kuuboreha kwa manufaaa ya kikazi cha kiislam.
- Mfumo wa madrasa zetu uendane kabisa na haja iliyopo katika jamii kwa lengo la kuwaendeleza watoto kitaaluma.

4.3 Walimu
- Kuwepo na mpango maalumu wa kuwaendeleza walimu kielimu, kitaaluma na kiuchumi ili kuwaongezea hari ya kujituma na kukfikiri kwa ajili ya maendeleo ya taasisi hii muhimu, “madrasati”.
Mfano:
Kuwepo kwa warsha, makongamano na semina ili kuwawezesha walimu kushirikiana ujuzi na mbinu za kufundishia na kuendeshea madrasa zetu.
- Walimu wawe wabunifu kiuchumi ili waweze kujikwamua kiuchumi na kuendeleza madrasa zetu.
- Walimu wasijione kuwa wao ni waislam au watu wa daraja la chini sana kimaisha. Bali wajione wao ni watu muhimu na kazi yao ni jukumu lao si jukumu la mtu Fulani na wala hawafanyi kazi hiyo ili tu kuwaridhisha watu Fulani bali ili kumridhisha allah (s.w).

4.4 Jamii ya Kiislam
- Ifanye fikra juu ya jinsi ya kuboresha na kuendeleza madrasa zetu na watoto wetu katika taaluma muhimu za kiislam.
- Jamii nzima ieleweshwe juu ya nafasi sahihi ya Madrasa na Elimu ya Madrasa kwa maisha yua Waislam nchini.

4.5 Taasisi za Kiislam
Zishirikiane kuona jinsi ya kutatua matatizo hayo.

5.0
TAALUMA MUHIMU KWA WALIMU WA MADRASA

5.1 Utangulizi
Kila nyanja inahitaji taaluma Fulani ili kuifanya nyanja hiyo iwe makini na yenye manufaa kwamaisha na ummah kwa ujumla. Hata mitume (radhi za Allah ziwafikie) walipewa taaluma maalumu kwa kazi zao. Katika maisha yetu tunahitaji taaluma zinazowezesha watu kutekeleza majukumu yao katika mazingira wanayoishi.
Mfano:
Mwalimu wa madrasa anahitaji taaluma juu ya;
(i) Uendeshaji wa madrasa.
(ii) Ufundishaji.
(iii) Saikolojia ya watoto na malezi.
(iv) Taaluma inazofundisha kama vile Fiqih, Tareikh, Qurani, Kiarabu, Tawhiid, Sirah, Akhlaq n.k.

5.2 Njia za kkufundishia (Muhtasari)
Zipo njia kadhaa Bwana Mtume (s.a.w) amekuwa akizitumia katika kufundishia watu. Pia Quran imeeleza njia kadhaa kwa ajili ya ufundishaji na uchamasishaji. Kwa muhtasari njia hzo ni pamoja na zifuatazo.

(a) Simulizi (Narration)
- Hii ni njia ambayo mwalimu anafundisha kwa kutumia visa vya kubuni au visa halisi. Njia hii inafaa sana kutumika hususan kwa watoto wadogo.
- Katika Quran njia hii imetumika kutafundisha mara kadhaa. Kanuni na njia yenyewe katika Quran zimeelezwa katika “NJIA ZA KUFUNDISHIA KATIKA MADRASA ZETU”. Hapa ni muhtasari tu.
- Njia hii yaweza kutumika katika kufundisha Sira ya Mtume, Akhlaq, Tareikh, Fiqih hata tawhiid. Alimradi mwalimu afahamu jinsi ya kuitumia njia hiyo kwa ufanisi.
(b) Uelezeaji (Description)
- Njia hii hutumika kuelezea dhana au wazo Fulani katika uislam. Muhimu kwa mwalimu ni kuifahamu misingi ya njia hii pamoja na kuelewa mazingira yanayofaa kwa njia hii.
Mfano:
(i) Ili kutoa maf’hum nzuri kuhusu “UISLAM” kama dini njia hii yafaa kutumika.
(ii) Ili kufunldisha vizuri, mazingira ya vita vya Badr, Uhud, Khandaq n.k. kwa lengo la kkufundisha mazingatio yanayopatikana, mwalimu aweza kutumia njia ya UELEZEAJI (Description)
- Kadhalika, cha muhimu ni maarifa kuhusu njia hii.
(c) Njia ya Uoneshaji (Demonstration)
- Ni njia inayotumika kufundishia mada zinazolenga kutoa ujuzi kwa wanafunzi kutenda matendo maalum:
Mfano:
(i) Swala la mait.
(ii) Swala la Faradh na Sunnah.
(iii) Kushona Sanda.
(iv) Kuosha Maiti.
(v) Kuchukua Udhu n.k.
- Mada kama hizi zikifundishwa pasipokutumia njia hizi, ueleo wa wanafunzi unaathirika.
- Mwalimu anatakiwa kuifahamu njia hii kwa madhumuni ya kuitumia kwa ufanisi.
(d) Njia ya ugunduzi na udadisi
- Njia hii inamtaka mwalimu aoneshe tatizo kasha aongeze wanafunzi katika kugundua suluhisho. Kwa kufanya hivi, milki ya ung’amuzi (Cognitive Facult) itakuwa imeendelezwa. Quran inasisitiza matumizi ya milki ya ung’amuzi (Cognition domain).
Mfano:
(i) Baada ya kufundisha “Tawhid” – Mwalimu anaweza kutoa habari ya kweli kuhusiana na tawhiid kasha wanafunzi wakajadili kwa mnasaba wa tawhid.
(ii) Mwalimu aweza kufundisha “Tareikh” – Hijar kutoka Makka kwenda Madina, alafu wanafunzi watatakiwa kugundua wanachojifunza.
(iii) Mwalimu awezatoa tatizo liliopo katika jamii kwa mnasaba wa uislam, kasha akawataka wanafunzi waonyeshe sabbu na suluhisho.
(e) Njia ya Kuhidadhi
- Hii ni muhimu sna katika elimu na maarifa ya kiislam. Mwalimu anatakiwa kuwawezesha wanafunzi kuhifadhi katika mada kadhaa.
Mfano:
(i) Ktika Swala, mwalimu atumie njia rahisi kwa wanafunzi kuhifadhi.
(ii) Katika Wudhuu, mwalimu atumie njia hii pia ili wnafunzi waweze kuhifadhi maneno muhimu.
(iii) Katika Dua, wanafunzi wahifadhishwe dua.
(iv) Katika Tarekh, wanafunzi wahifadhishwe aya na hadithi mbalimbali zinazonasibiana na matukio katika mada. Mathalani, kufundisha Mkataba wa hudaybiya, Quran 48:1. 48:18 ni vema zikahifhadhiwa. Pia katika kufundisha AKHLAQ mwalimu awahifadhishe watoto, Sura ya 64.4 ikiwekana, kulingana na umri wa watoto, Pia wahifadhi Quran 33:21.
(f) Njia za Kufundisha Quran
Njia na mbinu pamoja na mikakati ni muhimu sana katika ufundishaji wa usomaji Quran, vinginevyo motto atosoma muda mrefu sana ili kuelewa. Baadhi ya mbinu za kufundishia ni pamoja na kusoma herufi bila irobu kwa njia ya ubao, kadi, daftari n.k.

MUHIMU:
- Mwalimu afundishe kwanza herfu bila irabu. Yaani: ALIF, BE …….
- Kisha afundishe Irabu. Yaani: FAT’HA, KISRA, ……
- Afundishe kuchanganya herufi hizo na rabu;
Mfano: BE FAT’HABA, TE FAT’HATA …….
- Mwalimu atumie michezo kadhaa kwa watoto kuzitambua herufi.
Mfano: NGAZINGAZI, KIKAPU, UPANGAJI, GURUDUMU ZA GARI, NYUMBA …. n.k.
- Mwalimu afundishe kuchanganya SILABI ili kupata neno. Ni vizuri Mwalimu akaanza na kinachoeleweka kwenda kisichoeleweka.
Mfano: Kumwezesha motto kuandika BABA kwa herufi za Kiarabu, kasha aandike neno la kiarabu kwa herfu hizo.

6.0 HITIMISHO
Mwalimu anapaswa sit u kujua anachokifundisha, bali pia kufahamu na kuweza kutumia njia na mbinu muafaka. Kwa kawaida hatupaswi kulenga kusema sana, au kueleza mengi, bali tulenge kuwezesha mengi kufahamika kwa urahisi zaidi.

7.0 MWISHO
Kwa muda mrefu MADRASA zimesahaulika na kusababisha athari mbaya. Ili kuzikuisha tunapaswa kuzingatia kazi zinazotakiwa kukfanywa na madrasa na zipi zinafanywa. Kuelewa tatizo kwa undani. Historia ya Madrasa Tanzania ni muhimu kufahamika ili kurudisha mzizi wa tatizo. Kadhalika, Matatizo yanayoikabili taasisi ya Madrasa na ufumbuzi wake ni muhimu vikajadiliwa. Aidha , kuna haja ya kukumbuka taluma muhimu kwa walimu wa Madrasah na kuona kama wengi wanazo. Kama si hivyo, basi mikakati iwepo kuwawezesha walimu wa Madrasa kuendesha madrasa zetu (Uendeshaji Madrasa) pamoja na kuwa na mbinu bora za kufundishia katika madrasah zetu.
Mbinu zilizomo humu ni muhtasari tu, hazijaelezwa zote. Na wala hazijafafanuliwa hasa.
ALLAH NDIYE MJUZI WA YOTE